Chombezo: Sharaboro wa Tandale 02
.jpeg)
Kufuatia sharobaro Dullah kuitwa, aliivaa chupi yake chapchap’ Doreen naye alisimama pale sofani na kuchukua nguo zake na kukimbilia chumbani. Zakayo aliendelea kuita ndipo Dullah alitoka haraka pale sebuleni na kwenda jikoni kwa akina Doreen, Zakayo alipoona kijana huyo haitiki alijua alitoka nje ya geti akarudi kumfahamisha fundi Yassin kwamba hakuwepo.CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/ Dullah alipoona Zakayo kaondoka alivuta pumzi na kuzishusha akafurahi kwani alijua atakapokuwa akitoka mle ndani asingeonekana, wakati akiwaza hivyo Doreen ambaye tayari alivaa nguo alikwenda na kumshika Dullah begani. “Vipi, amejua kama upo humu ndani?” Doree ambaye macho bado yalikuwa yamemlegea alimwuliza. “Hajaniona na kaingia ndani,” Dullah ambaye alimlaani sana Zakayo kumkatishia starehe yake alimwambia Doreen. “Kama hajakuona vizuri, ili kuwapoteza maboya itabidi nikutoe nje kabisa kwa kutumia mlango huu wa uani, baadaye ugonge geti ujifanye ulikwenda kununua soda,” Doreen alimwambi...