Posts

Showing posts from November, 2024

Riwaya:penzi la mfungwa 05

Image
  Zabroni alirudi nyumbani baada kutoka kumsindikiza mzee Maboso,akiwa njiani aliwaza kipi afanye nini sasa baada kumtambua mbaya wake. Je, aendelea kuchoma nyumba ama adili na mbaya wake? Akili ya fasta ikamjia kwamba bora aendelea kuchoma nyumba ikiamini kuwa maumivu aliyonayo moyoni mwake huwenda yakatulia kama sio kupotea kabisa. Yote hayo kijana Zabroni alikuwa akiyawaza huku akirejea nyumbani mikono nyuma kichwa chini,alipo fika nyumbani alikuta karatasi ndogo kwenye meza iliyokuwepo sebuleni. Zabroni alionekana kustuka huku moyo wake ukihitaji kufahamu kilicho andikwa kwenye karatasi hiyo,hatimaye aliichukuwa akakuta maneno yaliyoandikwa "Kijana Zabroni, mjukuu wangu mwanangu pia.  Nimekupa dawa hii ili uweze kulipa kisasi juu ya kile ulicho fanyiwa,hakuna ubishi mzee Fungafunga ndio muhusika mkuu wa vifo vya wazazi wako. Alifanya kitendo kile baada kuona baba yako anamzungusha kumlipa deni lake alilokuwa akimdai. Zabroni Zabroni lipa kisasi kijana unyama huo kamwe huwe...

Riwaya:penzi la mfungwa 04.

Image
  Usiku ulipo fika,mzee Maboso alimkumbusha Zabroni kuhusu mzizi ambao utamfanya Zabroni kupotea popote pindi atakapo nuia na kisha kugusa kitu chochote. "Hapa kila kitu kitakuwa sawa kijana wangu", aliongea mzee Maboso huku akiutoa mzizi huo kwenye kitambaa alichotumia kuhifadhia. Akaketi kwenye kigoda, akamtazama Zabroni kwenye mwanga hafifu wa kibatali, akaendelea kumueleza uwezo wa mzizi huo na maneno anayotakiwa kuyaongea pindi atakapo hitaji kupotea kwenye mazingira husika. "Kwahiyo unataka kuniambia kwamba nikishaongea maneno hayo halafu nikagusa kitu chochote iwe nyasi au ukuta napotea?..", aliuliza Zabroni kwa umakini zaidi. "Naam! Hii dawa sio ya mchezo", alijibu mzee Maboso halafu akamkabidhi. Zabroni aliupokea mzizi huo, akautafuna. Alionekana kukunja uso wake, kwa namna gani mzizi huo ulivyokuwa mchungu. Baada kukamilika suala hilo, sasa akahitaji kufanya jaribio usiku huo huo. Alichomo moto nyumba nyumba tano, katika nyumba hizo hakubahatika ...

Riwaya: penzi la mfungwa 03

Image
Mkutano wa kijiji ulifanyika siku hiyo,waliopata taarifa ya msiba huo walifika na ambao hawakupata hawakufika. Mazishi yalifanywa na wanakijiji wachache sana, hakuna aliyekuwa na taarifa kuhusu msiba huo, mjumbe wala mwenyekiti hawakufika pia. Jambo hilo lilimuumiza sana mzee Maboso akajiaminisha kuwa huwenda vifo hivyo ukawepo mkono wa mtu. Wakati mzee Maboso akiwaza suala hilo upande wa Zabro naye aliamini kama mzee Maboso alivyokuwa akiamini. Baada ya msiba, mzee Maboso akamtaka Zabroni aishi nyumbani kwake, lilikuwa pigo baya sana katika maisha yake. Jambo hilo liliweza kumfanya asitishe zoezi la kuendelea kuiba, kwani aliyekuwa akimfanya aibe ameshapoteza maisha. Lakini licha ya kuamua kuacha zoezi hilo, ndani ya moyo wake kuna kitu alipania kukifanya mbadala. Roho ilimuuma sana, aliona hatolizika endapo kama kitu hicho hatokitekeleza  "Nitahakikisha kila siku iendayo kwa Mungu nyumba moja inateketea kwa moto", alijisemea kwa uchungu ndani ya nafsi yake Zabroni, chozi ha...

Riwaya: penzi la mfungwa 02

Image
  mwandishi alex wamilazo king Moshi mzito ulioambatana na kipupwe cha aina yake ulipaa angani kwa kasi huku Zabroni naye akizidi kupiga hatua kurudi nyumbani ilihali ndani ya hiyo nyumba inayoteketea kwa moto ilisikika sauti ya mama Zabroni akipiga mayowe kuomba msaada,lakini kulingana na kuugua kwa kipindi kirefu,ilimfanya sauti yake isikike kwa mbali sana kiasi kwamba mtu aliyepo hatua kumi na tano mbele asingeweze kusikia mayowe hayo.  Nyumba ilizidi kupamba moto,mama Zabroni akakosa msaada akafa namna hiyo hali ya kuwa mwili wa mzee Ndalo ambaye naye alikuwa ameshajinyonga nao uliungua,kamba ikakatika mwili wake ukazidi kuteketea ukiwa chini.  Zabroni alistuka kuona moshi mkali ukitanda angani,moshi huo ukitokea nyumbani kwao. Hali hiyo ilimfanya kohofia usalama wa nyumbani kwao haraka sana alitimua mbio ili ajue kipi kinachoendelea. "Lahaula" alipigwa na butwaa baada kukuta moto ukiishia huku fito zilizoungua nazo zikidondoka chini.  Alipagawa,alipasa sauti kum...

Riwaya: Penzi la mfungwa 01

Image
Ilikuwa muda wa saa nane usiku zilisikika sauti za wanakijiji wakipiga mayowe.."mwizi mwizii mwizii..", sauti hizo zilitambaa kwa kasi ya ajabu usiku ule kitendo ambacho kiliwafanya wanakijiji waliokuwa wamelala wakaamka ili kumkimbiza mwizi huyo ambaye kimuonekano alionekana kuwa shapu na kasi ya ajabu,alifanikiwa kuruka vigingi mbali mbali akatoka kijijini akakimbilia nje ya kijiji akatokomea kunako mashamba yaliyokuwa kando ya kijiji hicho.  Hapo mwizi huyo akawa amefanikiwa kuwatoka hao wanakijiji walioonekana kuwa na hasira kali kwani baada kutokemea nje ya kijiji,walibaki kujilaumu huku kila mmoja akiwa na hamu ya kumkata ili wamuadabishe jambo ambalo lilienda kinyume na malengo yao. Mwizi aliwapotea. Baada mwizi kufanikiwa kuwatoka,wanakijiji waliamua kurudi majumbani kwao.  Kesho yake asubuhi palipo pambazuka mwenyekiti wa kijiji alimtaka mjumbe wake apige mbiyu kuitisha mkutano wa kijiji kwa maana siku hiyo palikuwa na agenda mbali mbali alizotaka kusema na wanakijij...

Chombezo: wapangaji 05 MWISHOO

Image
Kuna wakati mwanaume unapofikwa na jambo ni lazima ufanye maamuzi ya kiume,... Kiukweli Swalehe alimpenda sana Zahra lakini kwa nyodo zake akahisi Swalehe sio mtu sahihi kua kama mume wake, Swalehe hakukata tamaa alisota na kusota juu ya Zahra, mpaka ikafikia wakati anapewa ushauri na baadhi ya kaka zake ambao ni mafundi wake, hivyo kuanzia siku hio akaacha kumfuatilia Zahra..... Zahra baada ya kufanyiwa uhuni ndipo akajua kuna umuhimu wa kumpenda mwanaume aliekupenda na haijalishi ana kazi gani... Kwasababu mpaka mwanaume kukutaamkia anataka kukuoa, tayari keshajijua anaweza kukuachia pesa ya kula kila siku,... Zahra alipigana sana juu ya kumrudia Swalehe mpaka akafanikiwa kumpata, lakini Swalehe hakua na upendo kama ule wa zamani hivyo hata kumkubalia kwake ni kama kishingo upande tu,.... Na ilifikia hatua mpaka akataka kulala nae, sema kuna vikwazo vilijitokeza mpaka akaamua kumuacha, lakini ilibaki kiduchu tu Zahra aliwe na Swalehe,.. Na Swalehe akamuahidi Zahra kuwa akirudi watafa...