Simulizi: ndoa yangu inanitesa 13
Sijui kwa sababu wewe mwenyewe hujanionyeshea upendo wako kwangu”
“Hivi umesema unanipenda vile?”
“Ndio…najua umekuwa wimbo”
“Naomba unichagulie maisha nitakayoishi kuanzia sasa”
“Basi nitakuacha uchague unachotaka mpenzi bora usinidhalilishe.”
“Sina chaguo lingine zaidi ya kunitafutia ndugu yako yeyote”Alisema tena akionekana siriasi.
“Kuna rafiki yangu mpenzi ambaye tupo karibu .Yeye ndie mwandani wangu, siri zangu ni zake na zake ni zangu nitamueleza kilio changu. Naamini atakisikiliza na kulichukulia kama kilio chake na atanisaidia shida ndogo ndogo za unyumba wetu. Mtu huyo ni tajiri yangu anayeitwa Mzee Jophu. Itakubidi unihifadhie aibu hii moyoni mwako. Ndiye ambaye siku ile ulivyoletwa na Baba niliwaacheni nae nikiwa na maongezi ya faragha na Baba.” Nilijaribu kumueleza mke wangu kuwa pengine angekubali kutembea na rafiki yangu mkubwa badalaya ndugu , na aendelee kinitunzia heshima yangu kama mumewe. Japo roho ilikuwa inauma kumkabidhi mwenzangu boma langu. Wala sikuweza kugundua kuwa mzee Jophu ndiye aliye panga na Daktari anipige sindano ya sumu.
“Kama una matatizo ndoa ya nini?.Suluhisho ni kuivunja ndoa kwa amani sitaki kujidhalilisha kwani wanaume wameisha duniani? Isitoshe nilishakutaarifu kwamba sijawahi kuguswa, bado nina nafasi kubwa ya kuolewa, wameolewa machangudoa sembuse mimi kigoli. Siwezi kukuelewa kabisa ninachotaka ni talaka yangu. Kuishi na wewe ni sawa na kulinganisha kifo na usingizi” Mke wangu alinibadilikia ghafla, sikuweza kuamini maneno hayo yaliyotoka kinywani mwake . Hali hiyo ilininyima amani na kijikuta nikilia kama mtoto mchanga aliye hitaji ziwa la mama yake baada ya kulikosa kutwa nzima bila kunyonya.
“ Sijali kulia kwako kwani mimi ndiye niliye kumwagia tindikali? Mlaumu aliye kumwagia na sio mimi.Kweli ving’aavyo vyote si dhahabu. Najuta kuolewa na watu waliochelewa kuoa, huenda ni matatizo uliokuwa nayo toka zamani”. Getruda alizidi kuniumiza moyo.
“Sawa najua sina faida ya kuishi duniani,nitawaachia ninyi wenyewe umuhimu na hii dunia, lazima nife …….sio muda mrefu utaniita marehemu sio Sweedy tena ,” Nilijikuta shetani mbaya akiniingia kichwani na kuiteka akili yangu, nikaamua kujiua tu, sikupenda kuishi na mateso. Niliondoka na kuingia chumbani kwetu, nilijifungia kwandani na kutafuta kamba tayari kutoa uhai wangu. Nilikusudia kujiua na niliamua kufanya kama mawazo yalivyo nituma, sikupenda kuishi kwa manyanyaso, mateso ya unyumba.
Nilikuwa chumbani na tafuta kamba ya kujinyonga, Getruda, mke wangu muda mfupi tu, angeniita marehemu badala ya Sweedy. Getruda akiwa kwenye mtiririko wa mawazo alisikia sauti yangu, (LORD YOU KNOW MY TRIBLES)” “Mungu unajua mateso yangu”Wakati nasema maneno yale ,nilishafunga kitanzi juu ya paa la numba.Nilikuwa nimepanga stuli mbili zikiwa zimebebana,nikaanza kuingiza shingo kitanzini, nilihakikisha kamba haitakatika. Iliyofuatiwa sauti nyingine nikimuaga. “Getuuuuu! Kwa heri niagie ndugu wote, nimeamua kufa sipotayari kunyanyaswa na udhaifu wangu, hata mungu anajua”. Taratibu nilianza kusukuma stuli nilioikanyaga ili idondoke na nijinyonge, Muomba kifo hakosi basi stuli ilidondoka kamba ikaninyonga.
“Ahiiiii”nilitoa sauti moja kwa shida sana.Kutoa neno la zaidi,nilijijigeuza na nikawa natapatapa kama mfa maji.
“Haraka Getu aliamka na kuekekea sauti ilipotoka, aliamini nilikuwa nianajiua akajuta na kujilaumu kwanini alinipa maneno ya ukali badala ya kunifariji.
“Dhambi zote ni mimi, isingekuwa mimi asingejiua, yanipasa nijitahidi kumnusuru na kifo,” Getu alianza kuniita kwa sauti ya huruma, “Sweedy…Sweedy… naomba unisikilize mkeo naongea. Niwie radhi nilikuwa na kutania nimekubali kuwa na rafiki yako. Naomba unielewe mpenzi nitalitunza penzi lako na siri yako. Kama nikujiua basi nisubiri tuongee nitakuacha uendelee kujiua.” Getu aliendelea kuniita bila ya kupata kujibiwa. Kilikuwa kitendo cha haraka alichukua uamuzi wa kuvunja mlango na kuingia ndani, alinikuta nikiwa nimeningia mapovu ya kitoka puani.Aliona kisu kilichokuwa mezani,Hakupendakupoteza muda ,kwa mwendo wa umeme alikata kamba na nikadondoka chini kama gunia la maharage, aliponigusa alipeleka mkono kifuani kuona kama nilikuwa hai. Ajabu ni kwamba hakusikia mapigo ya moyo ya kienda. Miguu ndio ilikuwa nikiitupatupa huku na kule, ulimi ukiwa nje kama wa kenge. Hali iliyomfanya asijidanganye kuwepo hai tena na kuamini zisingepita dakika kumi ningepoteza uhai.
Uzito wangu haukuwa kigezo kikubwa cha kumfanya Getruda ashindwe kunibeba, alijitahidi alivyo weza kunitoa nje ambako alipiga simu kwa dereva teksi aliyemfahamu. Dakika takribani mbili ,alisikia gari likiegeshwa nje ya jengo letu.
“Vipi shem. Imekuwa je?”Dereva teksi aliuliza.
“Wee achatu.Hebu tumuwahishe hospitali mazungumzo baadaye”
Walinibeba juu juu hadi kwenye gari, dereva akafungua mlango wa nyuma ambako walinilaza chali na kufunga mlango.Hawakukawia kufika hospitali ya rufaa Mount meru kwa matibabu zaidi.Getruda aliniingiza ofisi ya dakitari wa zamu.
“Anasumbuliwa hasa na nini?”
“Amevamiwa na majambazi ambao walimnyonga kwa kutumia kamba”Getruda alidanganya wazi wazi.Huku akiuma mdomo wa chini kana kwamba alijawa na dhahabu kali.
“Sasa umeripoti polisi?”
“Daktari mbona unaniuliza maswali ya sio na msingi kabisa.Wewe unataka ripoti ama kumtibu mgonjwa?”
“Hatuwezi kutibu bila kupokea karatasi ya PF3 kutoka polisi”
“Dokta kipi bora .Kuokoa maisha ya mgonjwa ama kumwacha afe kwa sababu ya PF3?”
“Kuokoa maisha yake”Dokta akajibu akichukua vipimo vyake.
“Basi kumbe unajua. PF3 baadae, nisamehe kama nimekuudhi”Getruda alimwomba radhi Dokta.
Dokta alinishughulikia kwa haraka.Nilitibiwa kwa makini na baada ya saa nzima nilipata ahuen.Ila kooni nilihisi maumivu kwa ndani.
**********
ITAENDELEA
Comments
Post a Comment