INATOSHA - 5

Ilipoishia jana.. Nilishangaa kwa mara nyingine tena Gervas akimfuata Jammy nakumkumbatia kisha bada ya pale Gervas alinifuata na mi nakunikumbatia, "Levina...? Nakupenda na Jammy nawapenda sana" "hata sisi Gervas tunakupenda...!" Songa nayo sasa… Maisha yaliendelea kupendeza zaidi kwani kwa sasa tulikuwa tukiishi kama wanandugu tena wale wa damu na siyo wachumba tena,niliishi mi Gervas na Jammy huku mfanyakazi wa ndani alitusaidia kwa kupika chakula,hata inapofka muda wa kulala huwa kila mmoja anachumba chake, Nakumbuka siku moja ambayo ilikuwa ni sikukuu tulitengeneza chakula kizuri nakuwaalika marafiki,hivyo tulisherekea vizuri kwa kunywa nakucheza muziki na hata ilipofika muda wakulala kila mmoja alilala kwake,kwa upande wangu nilikuwa nimelewa sana kiasi chakuamua niwahi kulala,lakini mkojo ndio tatizo kubwa nilikuwa nalo hivyo kila baada ya muda nilikuwa ni mtu wa kwenda chooni kukojoa na kwa kipindi hiki nikasahau njia ya kuingia chumbani kwangu nakujikuta ...