Posts

Showing posts from July, 2025

Simulizi : Mama’ke Mama Sehemu Ya Nne (4)

Image
Sasa maji yale mithiri ya damu yalikuwa yamenifikia magotini ndipo yule kikongwe akazungumza. “Jitahidi sana uogelee kwa bidii zako, ukithubutu kuyameza haya maji utakuwa ni mwisho wako, utakufa kwa uchungu sana kwa sababu umeitwa kwa hiari yako unaleta ujanja ujanja....” alizungumza vile na kama kawaida yake aliendelea kunicheka. Mvua ilizidi kuongezeka, nilikuwa nimeuziba mdomo wangu ili nisije kumeza yale maji kama alivyonionya yule kikongwe. Hayawi hayawi hatimaye maji yalikuwa shingoni, sasa nikalazimika kuogelea katika lile dimbwi la maji, nilikata maji kwa kutapatapa lakini yule kikongwe yeye alikuwa amesimama tu.. yaani ni kama alikuwa anazidi kurefuka kadri maji yale yalivyokuwa yanaongezeka. Nilipiga mbizi mpaka nikaisikia mikono ikiwa imeshika ganzi na hapo nikasalimu amri nikijisemea na liwalo na liwe. Nikaacha kupiga mbizi nikasubiri kifo kama alivyokuwa ameniahidi. Kifo cha uchungu mkali. Nilipoacha kupiga mbizi maji yale yakakauka na nikajikuta katika ardhi kavu kabisa i...

Simulizi : Gari La Kukodi (SEASON 2) Sehemu Ya Tano (5) TAMATIII

Image
“Tom!” Tunu aliita kwa mshangao uliochanganyika na furaha baada ya kumwona akiwa amesimama mbele yake akimtazama kwa tabasamu. “Tunu!” Tom naye akaita kwa furaha huku akiharakisha kuelekea pale kitandani alipoketi Tunu na kumkumbatia kwa furaha. “Thanks Lord!” Tom alisema kwa sauti ya chini huku akizidi kumkumbatia Tunu. Walikumbatiana kwa kitambo fulani huku kila mmoja wao akionesha hisia za furaha kwa mwenzake. Tom alipomwachia Tunu na kumtazama usoni alikuwa amelengwa na machozi ya furaha. Tunu alimtazama kwa Tom makini. “Hivi nimefikaje hapa?” Tunu alimuuliza Tom kwa shauku kubwa ya kutaka kufahamu kile kilichokuwa kimetokea huku wakitazamana kwa furaha. “Uliokolewa na kina Bob baada ya kutekwa na watu wa Mr. Oduya na kuletwa hapa baada ya Bob kuwasiliana na mimi,” Tom alisema huku akishusha pumzi za ndani kwa ndani. Mara Tunu akakumbuka kuwa kabla hajapoteza fahamu na kulala usingizi mzito akiwa ndani ya ile taxi alikuwa ameliona gari la Bob, aina ya Nissan Patrol. “Bob yuko wapi?...