Simulizi : Chozi La Mwisho Sehemu Ya Pili (2)

ADMIN
0


Jinsi mke wangu alivyokuwa akimpenda mama yake sikujua


itakuwaje. Nikiwa katika ya lindi la mawazo nilikatishwa na sauti ya Minza:


"Baba Shikilwa hubadili nguo utanisindikiza hiyohiyo bukta yako?"

Songa nayo sasa...

"Ooh! Nilichanganyikiwa mke wangu," nilinyanyuka na kuingia


ndani kubadili, kisha nilichukua pesa za kutosha na kutoka sebuleni


na kumpatia mke wangu.


"Yaani baba Shikilwa ningefurahi kama tungkwenda wote."


"Hata mimi nilitaka iwe hivyo, si unakumbuka kuwa ile kesi yetu ya


kiwanja leo jioni. Kama nilivyo kueleza ukikuta tatizo kubwa


nijulishe mara moja."CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/


"Sawa mume wangu."


Nilimsindikiza mpaka kamanga feli, baada ya kuingia kwenye boti ya


Karumo, nilisubiri mpaka boti iondoke ndipo niliporudi nyumbani nikiwa na mawazo tele juu ya ujumbe aliopewa mke wangu. Siku zote jambo lolote lililo mnyima raha mke wangu liliniumiza sana na kunikosesha raha.


Baada ya kufika nyumbani sikuwa na nyendo zozote niliingia ndani na kujitupia juu ya kochi na kuchukua limoti na kuwasha redio upande wa CD na


kusikiliza muziki laini ambao mara nyingi ninapokuwa na mawazo


hupenda kusikiliza na kuwa tiba ya matatizo ya akili yangu.


Nikiwa nimetulia nikisikiliza muziki laini huku kijiusingizi


kikinichukua kwa mbali. Nilishtushwa na sauti ya mtu akibisha hodi


ilikuwa sauti ya kike, nilimwambia apite ndani kwa kuwa mlango ulikuwa


wazi. Mara aliingia mke wa jirani yangu nilipomuona nilimkaribisha:


"Karibu jirani."


"Asante kwema hapa?"


"Kwa nini unauliuza hivyo?"


"Nimeshangaaa kuona mizigo asubuhi asubuhi pia nilisikia kama


mama Shikilwa analia sijui ni masikio yangu. Nina wasiwasi labda


mmepata msiba."


"Mmh! Ni kweli kuna tatizo la kawaida si msiba, tatizo ninyi wanawake


jambo dogo tu kilio."


"Kwani kuna tatizo gani?"


"Kaletewa taarifa mama yake mgonjwa."


"Ooh! Poleni sana, vipi hali yake?"


"Hatujajua yote nitayajua akifika."


"Mbona wewe hukwenda?"


"Mimi nitakwenda kesho, ugojwa sio lazima twende wote labda


ungekuwa msiba."


"Najua leo utapata shida kuwa peke yako?"


"Umejuaje kwa kweli Minza anapokuwa mbali na mimi ninakuwa


kama kinda la ndege lililonyonyolewa manyoya."


"Lakini shemu mimi si nipo kwa ajili ya kukuliwaza kwa leo."


"Utani huo shemeji na mumeo je?" Nilimuuliza kwa utani kutokana


jinsi tulivyozoeana, hupenda kutaniana ni mmoja wa majirani zetu


tunaye elewana naye sana.


"Huna habari mume wangu amesafiri, leo ni siku ya nne tangu


aondoke."


"Amekwenda wapi?"


"Amekwenda kwenye semina ya wiki mbili."


"Ooh pole, kumbe upo kama mimi?"


"Ndio maana nikasema mimi nipo kwa aili ya kukuliwaza kwa siku


ya leo."


"Kazi kwako uwanja ni wako," nilimjibu kwa utani,wakati huo mke


wa jirani yangu ambaye alikuwa wameoana mwaka mmoja ulio


pita, lakini walikuwa hawajabahatika kupata mtoto wala ujauzito. Sabina ndio jina lake aligeuka na kuondoka huku akisema:


"Basi badaye jirani."


"Sawa," nilijibu huku nikimsindikiza kwa macho baada ya kuondoka


nilikumbuka njiani wakati natoka kumsindikiza mke wangu


nilinunua gazeti la michezo la Risasi. Nililichukua gazeti na kusoma.


Majira ya saa tisa alasiri nilipata taarifa kuhusu safari ya mke wangu juu ya ujumbe wa simu juu ya hali ya mgonjwa. Habari zilikuwa tofauti na ujumbe uliotufikia kuwa hali ya mama mkwe ni buheri wa afya njema, wala hakuna aliye piga simu yoyote hata wao walishangaa kusikia habari zile.


Safari hii mke wangu aliongea kwa furaha lakini nilijiuliza ni nani


aliyetuchezea akili kwa kutaka kumuua mke wangu kwa presha. Lakini nilishukuru kukuta mama mkwe mzima wa afya njema. Nilimuuliza kama siku ya pili atarudi alisema kuwa kwa vile ameishafika mama mkwe aliomba akae hata wiki.


Kwa upande wangu wiki sawa na miaka kumi nilimpa ruhusa ya


siku mbili. Baada ya kuachana na mazungumzo na mke wangu nilirudiwa na furaha ya kujua hali ya mama mkwe kuwa mzima wa afya njema. Iakini niliingiwa na simanzi ya kuwa mbali na kipenzi changu Minza mwanamke niliyempenda na yeye alinipenda mpaka nikajua napendwa.


Nikiwa na nusu ya furaha nilijiandaa kwenda kwenye kesi yetu


ya mpaka wa nyumba na jirani ambaye analitaka eneo langu. Japo


kila mmoja alilijua, hata ramani ya nyumba inaonyesha kuwa eneo


lile ni langu.


Majira ya saa tatu na nusu usiku wakati najiandaa kwenda


kulala. Baada ya kurudi kwenye kikao cha usuruhishi ambako bado


mimi nilionekana nina haki. Jirani yangu hakuridhika alisema


atakwenda mbele zaidi japo kila mtu alikuwa upande wangu na


kusema wao wote watakuwa mashahidi yangu.


Nikiwa ndiyo najiandaa kupanga vitu vizuri tayari kwenda


chumbani kulala, huwezi amini kuondoka kwa mke wangu chumba nilikiona kipana, niliamua niende zangu chumbani kulala. Kabla ya kuingia chumbani kulala nilihakikisha kila kitu kipo sawa, baada ya kuridhika nilikwenda hadi mlangoni na kufunga mlango makomeo yote ikiwa pamoja na kushusha mapazia yote.


Nilirudi hadi kwenye swichi ya taa ya sebuleni na kuzima, Wakati


nageuka niende chumbani nilisikia mlango ukigongwa, nilijiuliza


nani tena usiku ule.


"Nani mwenzangu?" Niliuliza kwa sauti ya juu.


"Ni mimi Sabina."


"Aah! Jirani mbona usiku, unasemaje?"


"Maswali gani jirani bila kufungua mlango je, nikikabwa mlangoni mwako utasemaje?"


Sikuongeza neno nilirudi hadi mlangoni na kufungua mlango, aliingia mke wa jirani yangu akiwa amejitanda kanga ambayo ilimficha mwili na ilikuwa vigumu mtu kumjua.


"Vipi jirani mbona usiku?"


"Nimekuja."CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/


"Umekuja kufanya nini?" Jibu la jirani nilinishangaza.


"Aah! Jirani umesahau asubuhi tuliongea nini?"


"Ni mengi hebu nikumbushe."


"Nikukumbushe?" Aliniuliza swali huku akiwa amelegeza sauti


"Ndiyo."


Ha! mke wa jirani yangu nilishangaa kumuona akitoa ile kanga ya


juu na kubakia na kanga ya chini ilionyesha alikuwa amejifunga


kanga moja tu chini na kujitanda ingine juu. Baada ya kutoa ile kanga na


kubakia mabega nje aliniuliza tena.


"Bado hujakumbuka?"


Nilishindwa kumuelewa alikuwa na maana gani ilibidi nimuulize


kutokana na tabia yetu ya kutaniana, lakini hatukufikia utani kama ule.


"Mbona sikuelewi jirani una maana gain?"


"Yaani jirani bado hujanielewa?" Aliniuliza huku akilegeza sauti na macho.


"Kwa kweli bado sijakuelewa."


Ooh! makubwa sikuamini alichokifanya jirani yangu mbele ya macho yangu bila aibu kutokana na jinsi tunavyoheshimiana familia zetu pia ndiye


shoga wa karibu wa mke wangu. Mke wa jirani yangu aliiondoa na


ile kanga aliyokuwa amejifunga chini na kubakia mtupu kama


alivyozaliwa.


Nilijikuta napigwa butwaa na kujiuliza ana maana gani kufanya


kitendo kile cha kukosa haya cha kusimama mbele yangu mtupu kama


alivyozaliwa bila aibu. Nilikiwa sijui nifanye nini mke wa jirani yangu alinisogelea na kuanza kunipapasa. Japo joto la mwili wake liliusisimua mwili wangu, lakini sikuwa tayari kutenda dhambi ya uzinzi wakati tayari nina mke wangu anaye nipenda mapenzi ya dhati.



Kibaya kingine kilikuwa kufanya mapenzi na mke wa mtu ni dhambi kubwa, sikuwa tayari kutenda dhambi pia kuvunja uaminifu katika ndoa yangu ambayo sijui kwa mwenzangu. Lakini kwa upande wangu toka nimuoe Minza sikuwahi


kutembea nje kwa kuwa kila alichonacho mwanamke wa nje Minza anacho na kuwazidi.


Alivyozidi kunipapasa nikimsukuma na kuangukia kwenye kochi akiwa bado


mtupu kama alivyozaliwa. Hakukubali alinyanyuka haraka haraka na


kunifuata tena, nilimuuliza kwa sauti ya chini:


"Jirani unataka nini?"


"Hujui kama ulikuwa hutaki ya nini kunikubalia nimeacha shughuli


zangu kwa upuuzi huu wa kunidhalilisha," alisema huku akimwaga machozi.


"Mimi nilijua ni utani kama wa siku zote," nilijitetea baada ya kuona jirani hafanyi utani.


"Kuna utani na mambo ya watu wazima? Kwa hiyo ili tumalize yote


nipe nilichokifuata bila hivyo leo siondoki."


"Jirani unajua nakuheshimu sana hata mumeo ni rafiki yangu


mkubwa, unafikiri akijua mimi na wewe tumemuibia itakuwaje?"


"Utakuja kumwambia wewe?"


"Dunia haina siri, lazima itajulikana," nilizidi kujitetea.


"Huo ni uongo ni vingapi vimefanyika kwa siri mpaka leo


havijajulikana."


"Pamoja na hayo, kwa mimi sipo tayari."


"Utani huo baba Shikilwa...huwezi kuuona mwili wangu kisha


uniache hivi hivi, nitatembeaje nitakuwa sawa na kutembea uji kila


nikutanapo na wewe...nipe japo kwa leo tu, " jirani yangu alionesha amedhamilia.

CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

ITAENDELEA

Tags

Post a Comment

0 Comments
Post a Comment (0)

Made with Love by

Pixy Newspaper 11 Template is Designed Theme for Giving Enhanced look Various Features are availabl…
To Top