Posts

Showing posts from December, 2024

Simulizi: ndoa yangu inanitesa 15

Image
Inawezekana huyu mshenzi akamkataa mke wangu. Midomo yake imejaa dharau”nilijisemea kimoyomoyo huku nikibonyeza kitufe cha geti. Getruda Kimario alifika getini na kufungua, mtu wa kwanza kuingia akiwa Mzee Jophu.Shauku yake haikufichika ,alimtupia Getruda jicho la lilo jaa ubembe.Ni hapo ndipo nilipohisi Mzee Jophu kumkubali mke wangu. Alikuwa na shauku ya kumbusu Getruda, nikipindi kirefu toka wapoteane pale ofisini kwake, na Getruda alimkumbuka kuwa yule alikuwa yule aliyempa mama yake mzazi shilingi laki tano za kitanzania iliamuowe yeye. Walitupiana macho yaliyojaa furaha macho ya matamanio ya Getruda yalizidi kumchanganya Jophu. Aliyekuwa na shauku kuupitisha usiku mwanana na binti aliyemlipia shilingi laki tano. Aliamini alikuwa na haki yakujivinjari jasho lake. Mwanzoni nilihisi hawakumbukani,kumbe kumbukumbu alikuwa nazo na alishuhudia mama yake akipokea hizo hela. Ulifikia muda muafaka wakuweka mambo hadharani ili nitatuliwe shidayangu. Kabla sijazungumza chochote nilipandisha...

Simulizi: ndoa yangu inanitesa 14

Image
  Zikawa zimepita Siku mbili toka nilipookolewa na Mke wangu,Getruda pale nilipokuwa najiua kifo cha taabu. “Mume wangu nilikuwa nikikutania . Tafadhali usijaribu kujiua tena. Nimekubali mlete huyo rafiki yako leo nimuone kama sura yake ina tapisha au laa!” Getruda hakupenda kufanya hivyo aliamua kukubali ili kuninusuru kifo. Sauti ya Getruda ilipenyeza kwenye ngoma ya masikio yangu fundo kali la sononeko liliingia moyoni.Nikajivuia kulia kwa nguvu zote lakini nilijikuta machozi yakichuruzika taratibu bila kujua. “Sawa mke wangu utamuona nitakapomleta jioni,” Ilikuwa asubuhi na mapema, majira ya saa moja na nusu. “Mmmm! Lakini Getruda unanipenda.Isingekuwa wewe basi nilikuwa mfu”Nilimweleza Getruda. “Kumbe unalijua.Mkojo ulishaanza kukutoka” “Masihara hayo.Inamaana nilikikojolea kama mtoto” “Ndio”Getruda alinijibu akainuka kitini na kuelekea kwenye jokofu ambako alilifungua na kunipatia Juisi baridi ya machungwa. “Karibu mpenzi” “Ahsante mpenzi”Niliipokea na kumtolea tabasamu,lakin...

Simulizi: ndoa yangu inanitesa 13

Image
  Sijui kwa sababu wewe mwenyewe hujanionyeshea upendo wako kwangu” “Hivi umesema unanipenda vile?” “Ndio…najua umekuwa wimbo” “Naomba unichagulie maisha nitakayoishi kuanzia sasa” “Basi nitakuacha uchague unachotaka mpenzi bora usinidhalilishe.” “Sina chaguo lingine zaidi ya kunitafutia ndugu yako yeyote”Alisema tena akionekana siriasi. “Kuna rafiki yangu mpenzi ambaye tupo karibu .Yeye ndie mwandani wangu, siri zangu ni zake na zake ni zangu nitamueleza kilio changu. Naamini atakisikiliza na kulichukulia kama kilio chake na atanisaidia shida ndogo ndogo za unyumba wetu. Mtu huyo ni tajiri yangu anayeitwa Mzee Jophu. Itakubidi unihifadhie aibu hii moyoni mwako. Ndiye ambaye siku ile ulivyoletwa na Baba niliwaacheni nae nikiwa na maongezi ya faragha na Baba.” Nilijaribu kumueleza mke wangu kuwa pengine angekubali kutembea na rafiki yangu mkubwa badalaya ndugu , na aendelee kinitunzia heshima yangu kama mumewe. Japo roho ilikuwa inauma kumkabidhi mwenzangu boma langu. Wala sikuweza ...

Simulizi: ndoa yangu inanitesa 12

Image
Mume wangu amka basi tufanye.” Getruda alinihimiza huku akiwa amenishika mkono wangu kidogo akininyanyua . “Subiri kidogo naumwa na homa” “Imekuwa homa leo” kwa kweli mke wangu alichoka na idadi ya magonjwa niliokuwa nikimtajia kila leo. “Eti homa, utashaa leo, sikusikilizi ninachotaka ni penzi tu, usiniletee hadithi za riwaya, zile hadithi ndefu za kubuni, sizihitaji kabisa!, wewe mwanaume gani? Hivyooo!” Getruda mke wangu alianza kunidharau baada ya kuona sina lolote. Nilianza kulia nikilaumu ugonjwa ulioniingia nikiwa na ndoa yangu, niliulaani ugonjwa huo nilitamani nikatwe vidole kuliko kuwa na udhaifu wa nguvu za kiume. Kilio changu kilikuwa chungu mwenye na roho yangu. Pamoja na kunywa dawa za mitishamba kutoka kwa wamasai aina ya mchuma mbele bado nizidi kupata mateso ya unyumba. “Mke wangu unadiriki kunikashifu. Kunitukana mtusi ya nguoni!, kweli umenichoka” nilijaribu kumlaumu mke wangu, lakini haikusaidia kitu. “Ndio, nimekuchoka, naomba talaka yangu asubuhi hii hii, longolon...

Simulizi: ndoa yangu inanitesa 11

Image
 Naomba unipe muda wa wiki nzima” “Sitaki, ninacholilia ni haki yangu.Kwani kanisani uliapa kwamba utanitendea hivi. Ulinioa wanini kama hukunipenda, naomba talaka yangu haraka…” “Umeenda mbali sana mke wangu…” “Mimi sio mkeo kuanzia sasa. Naomba uelewe. We mwanaume gani?”Getruda alionekana mwenye hasira ,nikaamua kutulia kama niliyenyeshewa na mvua. Akrabu za saa zilionyesha saa tisa na robo usiku, mke wangu alijawa na fukutiko la moyo lililokuwa zito, japo alikuwa na hasira lakini alijitahidi kuiondoa ili kunitamanisha. Muda mfupi aliingia chumbani na kufuata kabati lake lenye makorokoro yote ambayo yanampendezesha mwanamke kuwa kivutio mumewe au mchumba au mwanaume rijali. Alichukua muda kidogo akijipodoa na kujipara, mafuta sijui lotion, cream, manukato, wanjaa lipshine nk. Hakuishia hapo alivaa sketi fupo, ambayo wanaita kimini kilichoonyesha mapaja yaliyonona, na kibilauzi kifupi, wengi huita “kitopu” chenye kuonyesha kitovu kilichoumbika sawia, usoni alipaka poda kwa mbali n...

Simulizi: ndoa yangu inanitesa 10

Image
  Getruda alisema kwa hasira baada ya kunitengea chai mezani. Nilishindwa hata kuokota kikombe nikabaki nimeduwaa. Nikanyamaza kimya, nilishindwa niongee uwongo gani,kwani kila siku nilikuwa muongo wa kupindukia,mara naumwa, mara nimechoka kazini, mara sijisikii,zote hizo zilikuwa njia za kukwepa aibu. “Sema”Mke wangu alifoka kwa kunihimiza. “Kwani baada ya ndoa ni haki kunitendea hivi?Kila siku hupandi kitandani mpaka mimi nishikwe na usingizi………” Nilinyamaza kwa muda dakika tatu, kichwa nikiwa nimekiinamisha kama kondoo, kisha nikameza mate na kulamba mdomo, kila nilipotaka kuongea nilijikuta machozi yakitiririka kwa kasi,nilihisi labda nililogwa na walimwengu,kweli imani ya kishirikina ilitawala ndani ya ubongo.Niliamua kujikaza na kuanza kuongoa uwongo. “Mke wangu shughuli zangu nzito sana, halafu ni za usiku mno!huwa nachoka nashindwa kufanya tendo la ndoa na wewe”. “Eti nini? kwa hiyo kuna wengine unaofanya nao?. Si ndio, hao machangu wa shule ndio wanakusababishia unione kam...

Simulizi:ndoa yangu inanitesa 09

Image
Kwanini usingenieleza kabla, umenitesa naunaendelea kunitesa. Utafanya nini ilikunisaidia, najisikia vibaya sana mwenzio” aliongea kwa sauti ya chini akiwa anadondosha machozi, mwili wake ulikuwa umelegea, macho mekundu na ya kurembua, hakuweza kuvumilia zaidi ya kulia kwa kwikwi, alitamani niondoe hali ya ubikira na kumpeleka kwenye utu uzima. Maneno ya Getruda yaliniumiza moyo wangu, nilimuonea huruma alivyokuwa akijigaragaza kitandani. Machozi yalichuruzika kwa kasi nilizidi kuwaza. “Au ni kwa vile ndio mara ya kwanza kukutana naye nini?. Lakini hapana sijapaniki” labda ni uzuri wake unanichanganya nini? . Au ni chango la tumbo limesababisha nini?.Sasa tatizo hili litaniumbua” Nilijiuliza bila kupata muafaka wala sikuweza kuhisi kitu chochote zaidi ya ugonjwa wa kawaida. Tuliupitisha usiku huo usio na ladha ya mapenzi, si mimi wala Getruda wote tulihuzunika. ************ Kwa ujumla maisha ya ndoa niliyaona machungu kama shubiri na pengine machungu kama mitishamba. Nilishindwa kuelew...

Simulizi: ndoa yangu inanitesa 08

Image
  Wiki tatu zilitimia na siku ile ya harusi iliwadia. Kila mtu aliisubiri kwa hamu sana siku hiyo hasa wazazi wangu kwani walijisikia furaha kwa mtoto wao wa kiume pekee kufunga pingu za maisha. Nadhani moyoni mwao walijisemea, sasa ule wakati wa kuwaona wajukuu toka kwa mtoto wetu Sweedy umewadia. Mzee Jophu ndiye alikuwa mtu wa kwanza kwa watu walionichangia mchango mkubwa katika kuifanikisha harusi yangu. Sherehe ilipendeza sana, watu walikula na kunywa hadi wakasaza. Namshukuru Mungu sikupata lawama yoyote ya kuhusu sherehe yangu. Getruda ambaye ndiye ubavu wangu sasa aligubikwa na furaha isiyo kifani. Sherehe iliyopendeza kwa shamrashamra na vifijo, DJ alitumbuiza kwa muziki wa taratibu wa wapendanao hasa kibao kilichopigwa na mwanamuziki Bob rudala nadhani msomaji unaupatapata ule wimbo vilivyo . Utajisikia vipi ukipigwa siku ya harusi yako? “NIMEKUCHAGUA WEWE” nakumbuka baadhi ya maneno yake, “Nimekuchagua wewe uwe wangu, wangu wa maisha wa kufa na kuzikana”msomaji sitaki ni...

Simulizi: ndoa yangu inanitesa 07

Image
Kesho yake ilikuwa siku ya mimi kupimwa afya ikiwemo na kupimwa virusi vya Ukimwi, sikuwa na wasiwasi nilisubiri waje kunipima kwani nilijiamini sikuwa na virusi, japo nilifanya mapenzi na Jennifer kule Thailand bila kutumia kinga yoyote.Na hata mapenzi niliyofanya yenyewe yalimfurahisha na kumridhisha Jennifer na kukiri mimi ni miongoni mwa wanaume wanaojua mapenzi. Sikupenda Jennifer anidharau kwa upande wa kutomridhisha kimapenzi. Waliingia Daktari waliovaa magwanda meupe wakiwa na vipimo vyao. Waliongozana moja kwa moja ofisini kwangu, cha ajabu baada ya kusalimiana nao walitaka nivue nguo nibaki na kaptula, jambo hilo nilipinga. “Kama kunipima damu ninatolewa damu kwenye mkono sio karibu na uume wangu. Nyie ni daktari kweli?” “Ndio sisi ni daktari unataka vitambulisho?”. “Sina shida na vitambulisho vyenu. Nyie chukueni damu mkaipime, mkileta majibu mabaya nitarudia hospitali nyingine niliwaeleza waziwazi bila kuwaficha kitu.”Nikiwa nimeketi kitini,wao walikuwa wamesimama. Haraka h...

Simulizi: ndoa yangu inanitesa 06

Image
Hakuna shida boss mimi nitapima virusi najiamini sina kitu, mimi sio mkware” Nilimjibu. Furaha yangu nikutaka kwenda nchini Thailand nikaonane na Jennifer . “Kesho asubuhi watakuja Daktari kukutoa damu. Hutaenda huko hospitalini, cheo chako kinakulinda na sitaki uhangaike. Watakuja na kukupima na wiki ya tatu utaenda Nchini Thailand kama hutakuwa na virusi. Sio sheria yangu hapana ni serikali”Akasema Boss akizunguka zunguka pale ofisini.Alionekana mwenye furahabaada yakukubali kuopimwa. “Nitakuongezea mshaharaasilimia hamsini wa mwanzoni”Alizidi kunipa motisha. “Nitafurahi Bossi” . Tukiwa kwenye maongezi nilisikia simu ikiita. Nilipoitoa mfukoni niliona namba za baba juu ya kio cha simu. Niliipokea na kuanza kuongea . “Shikamoo baba.Mama hajambo?” “Marahaba!. Wote wazima wanakusalimu. Jiandae kwa harusi yule mama amekubali umuoe mwanae. Ni baada ya kwenda kwenye mila na desturi, amepewa faini ya kutaka kurudisha mahari. Umenielewa mwanangu?” “Ndio baba. Kweli amekubali nimuoe mwanae?. ...

Simulizi: ndoa yangu inanitesa : 05

Image
  Jennifer alikuwa ni mchanganyiko wa Mzungu na mwafrika (chotara) na ni msichana aliyetoka Bara la Africa kama mimi, tofauti ni kwamba yeye alitokea Africa ya kusini, na mimi nilitokea Tanzania. Wala hakujali Nchi niliyotoka kuwa ilikuwa ya kimaskini, inamaana alinipenda na umasikini wangu. Tuliongea na kujikuta mawazo yetu yakiwa sawa, kwa kutaka kunionyesha upendo alikubali ombi langu la kutaka anisindikize kuupitisha usiku uliojaa raha za kila aina. Alidiriki kuacha chumba chake na kuja kulala na mimi, nilimgusia suala la ndoa nalo alilikubali alikuwa tayari kubadili uraia kuwa Mtanzania. Lakini kama angekuwa Mtanzania aliyekuwa Afrika ya Kusini umwambie arudi aolewe Tanzania, angeruka hata futi mia. Kwa upande wa mapenzi nilikoga na penzi motomoto, hakuwa mvivu wa kujishughulisha, tulisaidiana kupitisha usiku huo mwanana uliojaa mahaba ya kila aina, si mlimani tulipanda vichochoroni tulipita kwa nia imara ya kumridhisha Jeniffer aliyeonekana mgeni kwenye ulimwengu huo. Asubuhi...

Simulizi:ndoa yangu inanitesa :04

Image
  Halo.kutoka hapa hadi Care lodge ni kiasi gani cha pesa?” “Dola tano.Karibu” “Sikuweza kubishana sana kwani niliamini kauli ya ‘nipunguzie bwana’ ni huku kwetu.Alinifungulia mlango wa mbele, nilivuta mguu wangu wa kulia na kuingia ndani mlango wa mbele kulia mwa dereva.Gari hilo lilikuwa ‘Left hand’.Nilienda moja kwa moja kwenye hoteli iliyoitwa CARE LODRGE .Dereva alitumia kama dakika nne kuingia lango la hoteli hiyo.Nilipofika, nilimlipa ujira wake, nikaelekea ofisi za kupokelea wageni(Mapokezi). Sikutaka kwenda kufanya biashara kwa wakati huo. Niliamua kujipumzisha kutokana na uchovu wa safari, jambo la kushangaza nilichokiona mbele ya macho yangu sikuweza kuamini macho yangu kama yalikuwa sawa sawa ama vipi, nilijaribu kupikicha macho pengine ni ule ukungu wa kutokuwahi kupenda. Lakini cha ajabu moyo wangu ulisimama kama sekunde kadhaa, kisha ukaendelea mapigo yake yakawa ya taratibu mno, ambayo sikuweza hata kuyasikia. Nilihisi jasho jepesi likitiririka, kwanza nilijitazama ...