Riwaya: penzi la mfungwa 18



Baada ya siku nne Zabloni tayari alionekana kuwa sawa kiafya kimwili na akili pia,siku hiyo anarudi jela ilikuwa shagwe na vifijo kutoka kwa wafungwa wenzake. Pole kwa wingi zilimfikia Zabroni kwa yaliyomkumba huku wengine wakimsifu kwa kuamua kujitosa kupigana na nyampala Bluyner kijana ambaye ni tishio kwa kila mfungwa. 


Kitendo alichokifanya Zabroni kilikuwa cha kishujaa sababu tangu jamaa huyo ahukumiwe jela hakuna mfungwa hata mmoja aliyejaribu kukabiliana naye lakini Zabro alithubutu japo alichezea kichapo. "Zabro...Zabro..Zablo..Zabrooooni",Ni shangwe zilizokuwa zikitoka kwa wafungwa ambao walionyesha kufurahishwa na ujio wa Zabroni. 


Zabroni alibaki kusimama huku akiachia tabasamu pana,alipogusa upande bega lake alipofunga hirizi yake mkono wa kulia akagundua hirizi ipo. Haraka sana akatazama upande wa kushoto umbao walionekana Askari magereza wanne akiwemo na yule aliyemsaidia kumpatia hirizi,Askari huyo akamnyooshea Zabroni dole gumba akimanisha ishara kuwa mambo ni safi. 


Naye Zabroni akajibu kwa kuitikia kwa kichwa kisha akajiunga na wafungwa wenzake,wakati huo moyoni akijisemea "Veronica Veronica Zabroni nakuja kuifanyia upasuaji sehemu hiyo iliyopoteza nguvu zangu sababu hicho ndio chanzo cha haya yote "


ITAENDELEA

Comments

Popular posts from this blog

Chombezo : Huruma Ya Dudu Sehemu Ya : Pili (2)

Leyla binti bikra -01

SEHEMU YA 06---10