Kisa kingine nilikisikia kilitokea maeneo ya sumbawanga

ADMIN
0

 



Kuna mzee wamakamo alikua ni tajiri sana, pesa zake haweki benk na hata akienda kufanya manunuzi hua haweki kwenye wallet kuzistiri zisionekane yeye hua anazishikilia tu kama wanafunzi wanavyoshika vitini vyao mikononi

Siku moja kuna kosi la majambazi lilijipanga kwenda kumvamia


Walimkuta yuko nyumbani kwake ameshikilia pesa akipata upepo kwenye garden yake


Wakamnyooshea bastola na kumwambia atulie kimya kisha atoe kila kitu alichonacho


Yule mzee akachukua zile pesa akazibana kwenye kwapa lake huku akitetemeka kwa woga


majambazi wakamsisitiza kua anyanyue mikono juu, mzee akatii amri kwa kunyanyua mikono juu kisha pesa alizozibana kwapani zikaanguka chini majambazi wakaziokota


Wakamwambia tena "toa kila kitu ulichonacho"


Round hii unaambiwa mzee alichomoa kichwa chake akakishika mkononi halafu kile kichwa kikiwa mkononi kikatoa sauti ikisema "sina chochote jamani nina kichwa tu hapa"

Tags

Post a Comment

0 Comments
Post a Comment (0)

Made with Love by

Pixy Newspaper 11 Template is Designed Theme for Giving Enhanced look Various Features are availabl…
To Top