Kuna mzee wamakamo alikua ni tajiri sana, pesa zake haweki benk na hata akienda kufanya manunuzi hua haweki kwenye wallet kuzistiri zisionekane yeye hua anazishikilia tu kama wanafunzi wanavyoshika vitini vyao mikononi
Siku moja kuna kosi la majambazi lilijipanga kwenda kumvamia
Walimkuta yuko nyumbani kwake ameshikilia pesa akipata upepo kwenye garden yake
Wakamnyooshea bastola na kumwambia atulie kimya kisha atoe kila kitu alichonacho
Yule mzee akachukua zile pesa akazibana kwenye kwapa lake huku akitetemeka kwa woga
majambazi wakamsisitiza kua anyanyue mikono juu, mzee akatii amri kwa kunyanyua mikono juu kisha pesa alizozibana kwapani zikaanguka chini majambazi wakaziokota
Wakamwambia tena "toa kila kitu ulichonacho"
Round hii unaambiwa mzee alichomoa kichwa chake akakishika mkononi halafu kile kichwa kikiwa mkononi kikatoa sauti ikisema "sina chochote jamani nina kichwa tu hapa"
