“Dady ,its difficult to forget about what happened that night.Mimi ndiye niliyemuua Vero.Bila mimi Vero angekuwa hai mpaka hivi sasa.” Akasema Happy huku akilia.Mzee Raymond akapunguza mwendo wa gari na kuliegesha pembeni.
“Happy tafadhali nyamaza kulia.Hukukusudia kufanya jambo lile.Ile ni ajali kama ajali nyingine.Ulimsukuma Vero kwa ajili ya kumsaidia Patrick na hukudhamiria kumuua .Usijilaumu sana kwa kilichotokea ”akasema mzee Raymond.Happy akainua kichwa chake na kufuta machozi
“Nimekusikia baba lakini moyo wangu unauma sana.” Akasema Happy.Mzee Raymond akamtazama halafu akawasha gari na safari ikaendelea.
* * *
Eneo lote liligubikwa na sauti za vilio baada ya msafara wa magari kuwasili nyumbani kwa akina Vero ukitokea
hospitali ya taifa ya Muhimbili kuchukua mwili wa Vero.Gari maalum lililokuwa na mwili wa Vero likapewa nafasi na halafu jeneza zuri jeupe lenye nakshi za kupendeza likashushwa toka garini na kuingizwa ndani.Mahala hapa hapakuwa na masikilizano tena kutokana na vilio vingi na wengine walianguka na kupoteza fahamu.Kwa wale ambao bado walikuwa hawaamini kama ni kweli Vero alikuwa amefariki dunia sasa waliamini baada ya kuliona jeneza lile na kuzidisha vilio.Ilichukua zaidi ya nusu saa kuwatuliza waombolezaji na kisha muongoza shughuli akawasomea ratiba nzima ya mazishi.
Joel Armendo mjomba wa Vero akapanda jukwaani na kusoma historia ya marehemu halafu zikafuata nyimbo za maombolezo toka katika kwaya aliyokuwa akiimbia Vero.Baada ya kwaya kumaliza wimbo wa maombolezo ,kikafuata kipindi cha kutoa salamu za rambi rambi.Watu na vikundi mbali mbali walipanda na kutoa rambi rmbi zao na kumuelezea Vero kama binti aliyekuwa mfano wa kuigwa katika jamii.Wote walielezea namna walivyokuwa wameguswa na kifo kile.Baada ya watu na vikundi mbali mbali kumaliza kutoa salamu zao za rambi rambi,mwongoza shughuli akachukua kipaza sauti na kusema
“Tunawashukuru nyote kwa salamu zenu za rambi rambi na namna mlivyoguswa na msiba huu mzito.” Akanyamaza kidogo halafu akasemaCHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Kama mlivyosikia histora ya marehemu kwamba hadi anakutwa na mauti alikuwa na mchumba aitwaye Patrick ambaye walikuwa katika maandalizi ya mwisho ya kufunga ndoa.Kutokana na tukio hili kwa sasa Patrick anashikiliwa na vyombo vya usalama lakini pamoja na kwamba yuko gerezani ametuma salamu zake za rambi rambi kwa msiba huu mzito wa mchumba wake.Tunao hapa wawakilishi toka familia ya Patrick ambao wamekuja kuungana nasi katika mazishi ya binti yetu.Papo hapo bila kusahau ni kwamba Patrick naye amempoteza baba yake mzazi siku ya jana kwa hiyo kijana huyu amekutwa na misiba miwili hivi sasa.Kabla hatujaingia katika zoezi la kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa marehemu,naomba kwa heshima kubwa niwaite hapa jukwaani wawakilishi toka familia ya Patrick.Karibuni sana ndugu zetu” akasema muongoza shughuli na minong’ono ikaanza kusikika.
Taratibu Andrew na Savanna wakapanda jukwaani.Andrew akakabidhiwa kipaza sauti.
“Ndugu waombolezaji,tumesimama hapa mbele yenu kuwakilisha salamu nyingi za pole kwa familia hii kufuatia kifo cha mpendwa wao Veronika. Sipati neno la kusema kuelezea uchungu tulionao sisi kama familia ya Patrick kwa kifo hiki cha ghafla cha Veronika.Sote tulimpenda sana na kumjali kama ndugu yetu,shemeji yetu,mchumba wa ndugu yetu Patrick.Hakuna aliyefahamu kama yangetokea haya yaliyotoea.Naomba mfahamu kwamba tumeumizwa sana na kifo hiki.Hii ni kazi ya Mungu na siku zote haina makosa.” Akasema Andrew halafu akanyamaza kidogo akawatazama waombolezaji waliokuwa kimya wakimsikiliza.
“Wakati ,hata sisi kama familia tukiwa katika taharuki juu ya kilichotokea,hata sisi pia tumempoteza mzee wetu ,baba mzazi wa Patrick.Haya ni majonzi makubwa na familia zetu kwa sasa zinapitia kipindi kigumu sana.Hatuna cha kufanya zaidi ya kuziombea roho za wapendwa wetu zipumzike kwa amani.” Akanyamaza kwa sekunde kadhaa halafu akasema
“Baada ya tukio lile lililopelekea umauti wa Vero,Patrick anashikiliwa na vyombo vya usalama na tayari kesi yake imeanza kutajwa na tuna hakika kwamba haki itatendeka.Nawaomba ndugu zangu tuviachie vyombo vya kutoa haki vifanye kazi yake.Najua kwa tukio kama hili yataibuka mambo mengi sana,chuki,visasi,uhasama lakini nawasihi ndugu zangu tusifike huko.Sisi tayari ni ndugu kwa hiyo tusikubali hata kidogo tukio hili likatugawa na kujenga chuki miongoni mwetu.Tuendelee kushikamana katika nyakati hizi ngumu tulizonazo na tuepuke kuishi kwa hasama na kulipizana kisasi.Visasi havitaweza kuurudisha uhai wa wapendwa wetu.Binafsi nimekuwa rafiki mkubwa wa Patrick na Vero kwa muda mrefu sana na ninawafahamu kiundani.Ninayafahamu mapenzi yao pengine kuliko mtu mwingine yeyote kutokana na ukaribu wangu kwao.Kilichotokea hata mimi bado ninaona kama ndoto.” Andrew akanyamaza kisha akaendelea.
“Akiwa gerezani,Patrick ametuma salamu zake za rambi rambi kwa familia,ndugu jamaa na marafiki wa Vero.Baada ya salamu hizo za familia napenda sasa nikabidhi mchango wetu wa pole wa shilingi milioni tatu na papo hapo kuwataarifu kwamba baba mzazi wa Patrick atazikwa kesho .Kwa wale mtakaoweza kufika karibuni sana kuungana nasi katika kumpumzisha mzee wetu.” Akamaliza Andrew halafu akachukua bahasha na kumkabidhi muongoza shughuli kisha yeye na Savanna wakashuka jukwaani.Katika sehemu waliyokuwa wamekaa familia ya Vero,Loniki dada mkubwa wa Vero alikuwa amefura kwa hasira wakati Andrew akitoa salamu zile za rambi rambi.Sarah aliyekuwa amekaa pembeni yake alimtuliza na kumuomba asifanye jambo lolote la aibu mbele ya umati ule mkubwa wa watu.
Zoezi la kuuaga mwili wa marehemu likaanza na kuchukua muda mrefu zaidi ya ilivyokuwa imetazamiwa kutokana na umati mkubwa wa watu.Baada ya zoezi kukamilika ,waombolezaji wakapata chakula kisha ukaanza utaratibu wa kuelekea kanisani kwa ajili ya ibada.Magari yakapangwa vizuri na kisha jeneza lenye mwili wa Vero likatolewa ndani na kuingiza katika gari maalum na safari ya kuelekea kanisani ikaanza.Vilio viliendelea kusikika toka kwa akina mama waliokuwa wakilipungia mkono jeneza lenye mwili wa Vero wakati likiondolewa kwani ilikuwa ni mara yao ya mwisho kumuona tena mpendwa wao.Watu waliingia katika magari na safari ya kuelekea kanisani ikaanza.Ulikuwa msururu mrefu wa magari na wengine ambao hawakutaka kupanda magari walikuwa wakitembea kwa miguu kwa sababu kanisa halikuwa mbali na makazi ya akina Vero.
Hata kabla ya kuwasili kwa mwili wa marehemu kanisani,tayari kanisa lilikwisha jaa watu.Hii ilionyesha ni jinsi gani kifo cha Vero kilivyowagusa watu wengi.
Jeneza likashushwa garini na kuingizwa kanisani na kabla ya kuanza kwa ibada ikatolewa tena nafasi nyingine ya kutoa heshima za mwisho kwa wale ambao hawakuipata nafasi hiyo nyumbani.Zoezi hili lililazimika kusitishwa kutokana na idadi kubwa ya watu hivyo .Ibada ilichukua takribani saa moja halafu safari ya kuelekea makaburini kwa ajili ya kuhitimisha safari ya mwisho ya Vero ikaanza.Saa kumi za jioni waliwasili makaburini na ikafanyika ibada ya makaburini na taratibu mwili wa Vero ukashushwa kaburini.Lilikuwa ni tukio lililowafanya watu wengi wapoteze fahamu.Miongoni mwa watu waliopoteza fahamu alikuwa ni Loniki.Hii ilikuwa ni mara ya tatu katika siku hii kupoteza fahamu.Kifo hiki cha Vero kilikuwa kimemuumiza mno.
Familia na watu wa karibu wa marehemu wakatupa udongo kaburini na kisha likaanza zoezi la kulifunika kaburi.Baada ya zoezi lile lililofanywa na mafundi mahiri kukamilika ,yakawekwa mashada ya maua halafu Padre akalibariki kaburi na kisha watu wakatawanyika na kurejea msibani kwa ajili ya kuendelea na taratibu nyingine.Safari ya Vero duniani ikafikia mwisho.
“Andrew ninaondoka ,ninahitaji kuonana na Happy jioni hii” akasema Savanna muda mfupi tu baada ya kurejea nyumbani kwa akina Patrick wakitokea katika mazishi ya Vero
“Sawa Savanna.Tutaonana kesho.Patrick anafahamu kama baba yake anazikwa kesho?
“Sina hakika kama anafahamu ,lakini nitamfahamisha nitakapomtembelea kesho asubuhi.”
“Ukionana naye kesho mpe salamu zangu nyingi.Nitakwenda kumtembelea baada ya kumalizika kwa shughuli hizi za msiba wa mzee” akasema Andrew kisha Savanna akaingia garini na kuondoka kuelekea nyumbani kwa akina Happy.
“Kwa kweli hata mimi niliumia sana katika mazishi ya Vero.She was so pretty.Maskini Vero,amekufa na uzuri wake.Happy alistahili adhabu kwa kosa alilolifanya.Sielewi ni kwa nini Patrick ameamua kujitwisha yeye mzigo huu mzito ambao hakuustahili” akawaza Savanna akiwa njiani kuelekea kwa akina Happy
“Hata hivyo nitamsaidia Patrick kwa kila namna nitakavyoweza na atashinda hii kesi.Ninayafanya haya yote kwa sababu ya upendo wangu kwake.Ninampenda sana Patrick.Toka tulipoamua kusitisha mahusiano yetu baada ya mimi kumpata George ,bado sijaweza kabisa kumtoa Patrick moyoni mwangu.Hii ni nafasi yangu ya kumrudisha tena Patrick kwangu.Nitashinda hii kesi na Patrick lazima awe wangu tena.Happy hastahili kuwa na Patrick tena.” Akaendelea kuwaza Savanna.
Jua tayari lilikwisha punguza nuru yake kuashiria kwamba muda wowote litazama kulipisha giza lichukue nafasi yake.Savanna akafika nyumbani kwa akina Happy akafunguliwa geti na kuingia ndani.Akapokewa na mtumishi wa ndani
“Happy nimemkuta? Akauliza Savanna
“Ndiyo umemkuta.Karibu ndani ngoja nikamuite” akasema Yule msichana na kuelekea chumbani kwa Happy akamtaarifu kwamba Savanna amekwisha fika.Happy akatoka chumbani kwake na kuelekea sebuleni
“Karibu sana Savanna.” Akasema Happy huku akitabasamu
“Nashukuru sana Happy.Unaendeleaje?
“Ninaendelea vizuri Savanna.Namshukuru Mungu kwani ninazidi kupata nguvu kila siku”
“Nafurahi kusikia hivyo Happy.Ni jambo la faraja sana kuona hali yako inaboreka siku hadi siku” akasema Savanna.Kikapita kimya kifupi halafu Savanna akasema
“Happy ,nilisikia kwamba umelivua taji la Miss Tanzania..”
“Ndiyo Savanna.Niliamua kulivua taji lile ili kuendelea kulipa heshima yake kwa sababu kila neno baya lilikuwa linasemwa kwa kutanguliwa na miss Tanzania badala ya Happy.Nilifikiria na kuona haitakuwa busara kama taji la miss Tanzania likaendelea kuchafuliwa. Nikaona ni bora nilivue.”
“Pole Happy.Haya yalikuwa ni maamuzi magumu sana”
“Nimekwisha poa Savanna.Sikuwa na njia nyingine ya kufanya zaidi ya kulirudisha taji lile.” Akasema Happy
“Nimetoka katika mazishi ya Vero.Mimi na Andrew tuliiwakilisha familia ya Patrick katika mazishi.” Akasema Savanna.Happy hakujibu kitu akainama chini
“Happy nimepita mara moja kukuona kama ulivyokuwa umeomba.” Akasema Savanna ,Happy akainua kichwa.
“Samahani Savanna kwa kukusumbua.Ni kweli nilihitaji kuonana nawe kwa maongezi ya muhimu”
Akasema Happy
“Nakusikiliza Happy” akajibu Savanna.Happy akainama kidogo akafikiri na kusema
“Leo nimekwenda kuonana na Patrick gerezani.Tumeongea japo si kwa muda mrefu .Nilijaribu kumuuliza kuhusiana na maendeleo ya kesi na akanitoa wasi wasi na kusema kwamba mambo yote kuhusiana na kesi hii ameyaacha mikononi mwako.Amenihakikishia kwamba wewe ni wakili mahiri na kesi kama hii haiwezi kukusumbua hata kidogo.Kuna kitu aliniambia vile vile kilichonistua kidogo eti kwamba umekataa malipo yoyote na kwamba unaifanya kazi hii bure kabisa.Ni kweli?
Savanna akatabasamu kidogo na kusema
“Ni kweli Happy.Mimi ndiye ninayeisimamia kesi ya Patrick nikishirikiana na mawakili wazoefu toka katika kampuni yangu ya uwakili.Kuhusu malipo ni kweli kama alivyokwambia Patrick.Sihitaji kulipwa hata senti moja.Nimejitolea kuifanya kazi hii bure kwa sababu Patrick ni rafiki yangu mkubwa na wa siku nyingi.Kuna tatizo lolote katika suala hilo? Akauliza Savanna
“Hakuna tatizo Savanna.Nilihitaji tu kupata uhakika toka kwako kwa sababu haikuniingia akilini mtu kusitisha shughuli zake nyingine na kuisimamia kesi hii ngumu bila kuhitaji kulipwa hata shilingi moja.Labda naomba niwe wazi kwako Savanna kwamba moyo wangu hauna amani hata kidogo nikimuona Patrick gerezani.Ninataka kufanya kila linalowezekana ili Patrick ashinde kesi na atoke gerezani na ndiyo maana ninahitaji kuwa na uhakika kuhusiana na mtu anayeisimamia kesi yake.Kwa maana hiyo Savanna kama kuna kiasi chochote cha pesa ambacho ungependa kulipwa usisite kuniambia na nitakupatia.” Akasema Happy.Savanna akacheka kidogo halafu akamtazama Happy na kusema
“Happy mimi na wewe tumekutana na kufahamiana hivi karibuni baada ya kutokea tukio hili hata hivyo nadhani bado haujanifahamu vizuri.Mimi na Patrick tumekutana miaka mingi iliyopita,na tunafahamiana vyema. Sipendi kujisifu lakini mimi ni wakili mwenye uwezo mkubwa wa kusimamia kesi kubwa na karibu katika kesi zote ambazo tumewahi kusimamia mimi na kampuni yangu hatujawahi kushindwa.Ni kutokana na umahiri huo katika sheria nimeweza kukusaidia hata wewe kuondokana na kesi hii inayomkabili Patrick ambayo ulistahili uibebe wewe.Patrick ananifahamu vizuri na ndiyo maana hakusita kuiweka hatima ya kesi yake mikononi mwangu.Kuhusu malipo bado narudia tena kwamba sihitaji chochote.Ninafanya kazi hii kwa moyo kumsaidia rafiki yangu na si kwa ajili ya kutengeneza fedha.Ninazo pesa za kutosha na hata nikikwambia unilipe kama unavyotaka ,can you afford to pay me 100 millions? Akauliza Savanna akionyesha wazi kukerwa na maneno yale ya Happy.Happy akainama chini.
“Can you pay me 100 milions Happy? Akauliza tena Savanna
“Savanna samahani kama nimekuudhi ,lakini halikuwa kusudio langu kufanya hivyo.Lengo langu nilitaka niwe na uhakika kuhusu utetezi wa Patrick.” Akasema Happy
“One more thing.Who are you Happy? Akauliza Savanna huku sauti yake ikionyesha kuanza kubadilika.Happy akakaa kimya
“You are not even a member of Patrick’s family,….!!” Akasema Savanna.
“Savanna samahani kama kwa kukuuliza vile nimekukera.Niliuliza kwa lengo zuri tu” akajibu Happy
“Happy nimeshangazwa sana na namna ulivyoonyesha wasi wasi kwangu.Umesahau kwamba mimi ndiye niliyesababisha wewe uwe huru mpaka wakati huu na Patrick awe gerezani.” Akasema Savanna halafu akakaa kimya akamtazama Happy
“Kesho asubuhi,nitakwenda kumtembelea Patrick na nitamwambia kwamba najitoa katika kesi hii kwa sababu umeonyesha kutokuniamini nadhani litakuwa jambo la busara kama utaitumia nafasi hiyo kumuweka wakili unayemtaka wewe ambaye atafanya kazi hii kwa malipo tofauti na mimi ambaye sihitaji hata senti moja” akasema Savanna
“Savanna nakuomba usifanye hivyo.Usimweleze chochote Patrick.Atazidi kuumia.Nakuomba sana Savanna usimwambie Patrick chochote.” Akasema Happy
“Happy ahsante sana.Mimi naondoka.Kumbe umenipotezea muda wangu mwingi kwa kuja kunieleza mambo kama haya.!!!! Akasema Savanna huku akiinuka na kutoka mle sebuleni.Happy alikuwa ameinamisha kichwa.
“Bastard !!!..” akasema Savanna kwa hasira baada ya kuingia katika gari lake.
“Sijawahi kudharauliwa hata siku moja kuhusiana na kazi yangu na sipendi mtu aidharau taaluma yangu.Sikuwa nimetaka kukasirika lakini Happy amenikasirisha sana.Yeye ni nani hata anifanyie mahojiano na kuhoji uwezo wangu? akawaza Savanna.
“I will destroy you Happy.nitahakikisha Patrick humpati tena” Akawaza Savanna.
* * *
Baada ya kurejea nyumbani toka katika mazishi ya Vero Loniki hakutaka tena kuongea wala konana na mtu yeyote .Akajifungia chumbani kwake.
“Siyo ndoto tena kama nilivyokuwa nadhani.Ni kweli Vero amekwenda na sintamuona tena.Nilimpenda kupita kiasi na hii ni sababu inayonifaya niumie kiasi hiki.Vero amekufa , amekwenda na uzuri wake.Sintampata tena ndugu kama yeye.Patrick ameniondolea furaha ya maisha yangu na kwa hili sintamsamehe hadi siku naingia kaburini na lazima nihakikishe nimemlipia kisasi mdogo wangu.Kitendo alichofanyiwa na Yule shetani si cha kibinadamu na hakivumiliki hata kidogo na ninaapa kwa miungu yote kwamba lazima yeye na wale wote walioshiriki kumuua ndugu yangu wanalipa.Damu ya Vero haiwezi kupotea bure.They must pay ..!!!!!” akasema kwa hasira Loniki huku akigonganisha mikono yake.Akainuka kitandani akaendea kabatini akachukua pakiti la sigara akachomoa moja na kuanza kuvuta huku akipuliza moshi mwingi hewani.
“Sarah naye lazima atanieleza ni kwa nini kila mara amekuwa mtetezi mkubwa wa Patrick. Hata amediriki kuwaalika watu wake msibani.Anaonekana hana uchungu wowote na kifo cha Vero.Lazima naye nipambane naye.Zile fedha zilizotoka kwa akina Patrick nazo lazima zirudi zilikotoka .Itakuwa ni dhihaka kubwa kuzikubali pesa zilizotoka kwa watu waliomuua ndugu yetu.Sintakubali kamwe fedha zile ziendelee kukaa mikononi mwetu.Kama hawatazirejesha zilikotoka nitazirejesha mimi.” Akawaza Loniki huku akiendelea kuvuta sigara kwa fujo.
“Sintarejea London hadi nihakikishe wale wote walioshiriki katika kumuua Vero wamelipa uovu wao.Lazima walipe.Siihitaji hiyo haki ya mahakama,nitaitafuta haki kwa namna ninayojua mimi mwenyewe.” Akawaza Loniki huku akiendelea kupuliza moshi mwingi wa sigara hewani. Akafungua mlango na kutoka mle chumbani akamtafuta shangazi yake
“Shangazi naomba simu yako kuna mtu nahitaji kuwasiliana naye” akasema Loniki na shangazi yake akampa simu Loniki akarejea chumbani kwake akuchukua kitabu ambacho huandika kumbu kumbu zake mbali mbali akautafuta ukurasa ambao ameandika namba mbali mbali za simu akazipata namba alizokuwa anazitafuta akaziandika katika simu na kupiga
“Hallow Linah,Loniki hapa naongea” akasema Loniki baada ya simu kupokelewa.
“wow ! Loniki.!!....ni wewe kweli? Siamini .Umekuja lini shoga yangu.Na mbona umerudi kimya kimya? Akauliza Linah
“ Linah ina maana hujasikia matatizo yaliyonipata?
“Matatizo !!!.Linah akashangaaCHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“ Ndiyo Linah.Ina maana huna taarifa zozote?
“Mbona unanistua Lonny? Mimi sina taarifa zozote kwa sababu nimerudi mchana wa leo toka Nairobi kuna mizigo yangu ilikwama pale kwa hiyo sifahamu chochote na wala sijajua kama umerudi.Nini kimetokea Lonny?
“Linah nilipatwa na msiba mzito”
“Msiba !!! Linah akastuka
“Pole sana Lonny.Nani kafariki?
“Vero amefariki dunia !
“Vero !? ..Vero huyu mdogo wako?
“Ndiyo.”
“Acha masihara Lonny.”
“Si masihara Linah.Ni kweli Vero amefariki dunia na ni kifo ambacho kimetangazwa sana na nchi nzima wanajua kama Vero amefariki dunia na jioni ya leo tumetoka kumzika katika makaburi ya Kinondoni.”
Kimya kifupi kikapita.Linah akavuta pumzi ndefu na kusema
“Loniki umenistua sana .Bado siamini kama uliyonieleza ni ya kweli”
“Sikudanganyi Linah.Ni kweli kabisa Vero amefariki dunia.Vero hatunaye tena.”
“Ouh my Gosh !!!”
“pole sana Lonny.Kwa kweli ni msiba mzito sana na wala sina taarifa zozote.Loniki nitajitahidi nifike hapo nyumbani kesho asubuhi kwa sababu kwa sasa niko mbali kidogo ”
“Nitashukuru sana kama ukifika Linah ninahitaji sana kukuona.Nina maongezi nawe ya muhimu sana”
“Usijali Lonny nitafika hiyo kesho bila kukosa.Mpe pole sana mama na Sarah”
“Ahsante sana Linah ,tutaonana hiyo kesho” akasema Loniki na kukata simu,akachukua sigara nyingine katika pakiti na kuiwasha akaendelea kuvuta
Kumepambazuka Dare es salaam siku mpya imeanza.Pilika pilika katika jiji hili kubwa la kiuchumi nchini Tanzania ziliendelea kama kawaida.Saa tatu za asubuhi ilimkuta Savanna katika gereza la uwangwa kwa ajili ya kuonana na Patrick.Aliwahi sana kufika siku hii ya leo.Kutokana na kufahamika kwake hupewa nafasi ya kuongea na mteja wake katika chumba maalum tofauti na watu wengine ambao hukutana na mahabusu katika sehemu yenye uwazi.
Dakika nane toka aingie mle chumbani mlango ukafunguliwa na Patrick akaingia.
“Hallo Patrick “ akasema Savanna
“mambo vipi Savanna? Akajibu Patrick huku akitabasamu
“Mambo poa Patrick.Unaendeleaje?
“Ninaendelea vizuri Savanna.Ahsante sana kwa msaada wako kwani ninapata huduma nzuri hapa gerezani tofauti na mahabusu wengine.Vipi wewe unaendeleaje?
“Mimi pia niko salama Patrick.Nafurahi kama unapatiwa huduma nzuri.Unajua mkuu wa gereza ni rafiki yangu sana na hata viongozi wengi wa gereza hili ninafahamiana nao kwa hiyo ninafurahi kama ombi langu kwao la kuwaomba wakupatie huduma nzuri linatekelezwa” akasema Savanna kikapita kimya kifupi
“Patrick.Unajisikiaje leo?
“Ninajisikia vizuri sana Savanna.Nipe habari za huko duniani” akasema Patrick na kumfanya Savanna acheke kidogo
“Jana tumemzika Veronika.Amezikwa katika makaburi ya Kinondoni.Watu walikuwa wengi mno.” Akasema Savanna halafu Patrick akainama chini.Baada ya sekunde kadhaa Savanna akasema
“Mimi na Andrew tulikuwakilisha wewe na familia nzima katika mazishi hayo ikiwa ni pamoja na kupeleka salamu za rambi rambi kwa niaba ya familia.Tulipewa nafasi ya kusema machache na Andrew akaongea machache.Alitoa salamu za pole kwa niaba yako.”
“Ndugu wa Vero mlifanikiwa kuonana nao?
“Tulionana na Sarah ambaye ndiye amekuwa akitupa ushirikiano mkubwa na alifika hadi nyumbani kwenu kumpa mama pole kwa msiba wa baba.Dada mkubwa wa Vero amekuwa mgumu sana na juzi aliwafukuza Andrew na wazee wengine walipokwenda kushiriki msiba” akasema Savanna
“Please forgive me Vero.I didn’t mean to cause your death” akasema Patrick huku ameinamisha kichwa.
“Patrick leo tunamzika baba .Nasikitika kwamba hutaweza kuhudhuria lakini usijali kwani nitakuwepo kukuwakilisha” akasema Savanna na kukaa kimya akamtazama Patrick.
“Nashukuru sana Savanna kwa taarifa.Hakuna mtu mwingine yeyote ambaye amekuja kunitembelea na kunipa taarifa kuhusiana na na kinachoendelea huko nyumbani.Bila wewe nisingefahamu chochote kuhusu mazishi ya Vero wala baba yangu.” Akasema Patrick kwa masikitiko.
“Patrick,familia yako wala ndugu zako hawajakutenga wala kukutelekeza.Wameshindwa kufika kukutazama kwa sababu wako katika majonzi makubwa hivi sasa.Baada ya kumaliza shughuli za msiba wa baba nina imani watakuwa wakifika hapa mara kwa mara kukujulia hali.” Akasema Savanna
“Anyway,I deserve to be treated this way” akasema Patrick
“Patrick we’re here for you.I’ll always be here for you.Anytime you need a friend,or a shoulder to cry on ,I’ll be here .Maumivu yako ni yangu na ndiyo maana ninakuahidi kufanya kila ninachoweza ili kuhakikisha kwamba unashinda kesi hii.Tafadhali usijihisi mpweke Patrick”
“Nashukuru sana Savanna.Toka nimepatwa na matatizo haya umekuwa ni mtu pekee ambaye uko nami kila siku.Wewe ndiye mfariji wangu .Sina cha kukulipa Savanna kwa wema huu wote ulionitendea.Mungu atakulipa.” Akasema Patrick
“Patrick ninayafanya haya yote kwa sababu wewe ni rafiki yangu na mtu wangu wa muhimu sana.Halafu kuna kitu nimekumbuka Patrick”
“Kitu gani Savanna?
“Jana nilikwenda kuonana na Happy baada ya kutoka katika mazishi ya Vero.Alinipigia simu na kunitaka nionane naye kuna jambo anataka kunieleza.Nilishangazwa sana na Happy kuonyesha wasi wasi wa mimi kuisimamia kesi yako.Anaonekana hana uhakika kama ninaweza kuisimamia kesi hii hadi mwisho.Anyway sitaki kuliongelea sana suala hili nilitaka tu ufahamu na umwambie kwamba awe mkimya na awe mfuatiliaji mzuri wa kesi na si mtoa maamuzi.” Akasema Savanna.Patrick akamtazama na kusema
“Savanna ,samahani sana kama kuna maneno yoyote aliyoyatamka Happy yakakuudhi kiasi hicho.Ni kweli jana alifika hapa na aliniuliza kuhusu mwenendo wa kesi nikamwambia kwamba mambo yote kuhusiana na kesi nimeyaacha mikononi mwako.Sikutegemea kama angekutafuta na kukuuliza kuhusu suala hili.Savanna wewe ni zaidi ya rafiki,naomba usimsikilize Happy kwa lolote.Tafadhali nakuomba usiache kunisaidia katika kesi hii.Without you I’m finished.I need you now more than ever” akasema Patrick.Savanna akaishika mikono ya Patrick.
“Patrick hakuna binadamu yeyote katika hii dunia ambaye anaweza kunizuia mimi nisikutetee katika hii kesi.I’ll get you out of here .I’ll make sure you are free.Believe me” akasema Savanna.
“Ninakuamini Savanna.” Akajibu Patrick.
“Ahsante sana Patrick.Kilichonileta hapa siku hii ya leo ni kukujulia hali na kukupa taarifa za kinachoendelea nyumbani.Nitakuja tena kesho” akasema Savanna.
“Savanna nakushukuru kwa kuja kunitembelea na kunipa taarifa za mazishi ya baba na Vero.Naomba usiache kuja kunitembelea kwani wewe ndiye mfariji wangu mkuu kwa sasa” akasema Patrick.
“Usijali Patrick,hapa ni kama nyumbani na nitakuwa nikija kila siku kujua maendeleo yako.Sintaacha kukutembelea hadi siku nitakayohakikisha kwamba umekuwa huru” akasema Savanna akaagana na Patrick na kuondoka
“Ili kujiweka katika nafasi nzuri ya kumrejesha Patrick katika mikono yangu lazima kuifuta taswira ya Happy katika akili ya Patrick.Lazima niichafue picha nzuri ya Happy kichwani mwa Patrick na hapo ndipo nitakapokuwa na uhakika kwamba ninaweza kumpata Patrick tena.Najua si rahisi lakini ninatakiwa kufanya kitu kimoja tu.I have to make him hate her” akawaza Savanna na kutabasamu.
* * * *
Saa mbili na dakika ishirini za asubuhi , gari moja dogo la kifahari likawasili nyumbani kwa akina Vero na akashuka mwanamke mmoja aliyekuwa amevaa gauni refu jeusi na kichwani alijitanda mtandio mweusi na kuvaa miwani mikubwa myeusi kiasi kwamba ilikuwa vigumu kumtambua kwa haraka.Huyu alikuwa ni Linah rafiki mkubwa wa Loniki.Mara tu aliposhuka katika gari Loniki akatokea na kukumbatiana naye.Linah akashindwa kujizuia akaanza kuangua kilio kikubwa.na kumfanya Loniki naye aanze kulia.
Baada ya kulia kwa takribani dakika kumi,Loniki na Yule mwanadada ambaye ni rafiki yake kipenzi na wa siku nyingi wakanyamza kisha Linah akaitumia nafasi hiyo kuwapa pole ndugu jamaa na marafiki waliokusanyika hapo nyumbani wakiendelea na matanga.Kisha toa mkono wa pole,Loniki na Linah wakaelekea bustanini.Loniki akamuacha Linah pale bustanini ,akarejea chumbani kwake na kuchukua chupa ya mvinyo pamoja na glasi mbili bila kusahau pakiti yake ya sigara .Akarejea bustanini alikomuacha Linah na kumimina mvinyo katika glasi ,akawasha sigara na kupuliza moshi mwingi hewani.
“Bado hujaacha kuvuta sigara Lonny? Akauliza Linah.Loniki akapuliza tena moshi mwingi hewani na kusema.
“Siwezi kuacha kuvuta sigara Linah.Nimeanza kuvuta sigara nikiwa shule ya msingi na siwezi kuacha sasa hivi.Vipi wewe huvuti tena?
“Hapana Lonny,niliacha kuvuta sigara muda mrefu .nilipatwa na tatizo la kifua nikashauriwa kuachana na sigara.” Akasema Linah halafu kikapita kimya kifupi.Loniki bado aliendelea kunywa mvinyo na kuvuta sigara
“Lonny pole sana shoga yangu kwa msiba huu mkubwa.Bado siamini kama ni kweli Vero amefariki dunia.Usiku kucha nilikuwa nikitafakari kuhusu suala hili kama ni kweli au ulikuwa unanitania.Hapa nilipo mwili unanitetemeka sana,nimestuka mno” akasema Linah
“Ni vigumu kuamini Linah lakini ukweli ni kwamba Vero hatunaye tena.Jana tumempumzisha katika nyumba yake ya milele.Hata mimi bado inaniwia ugumu kuamini kwamba sintamuona tena Vero.Tabasamu lake ,ukarimu na ucheshi wake hatutaviona tena.Inauma sana Linah.Inauma sana” akasema Loniki huku akilengwa na machozi.Akachukua glasi yake ya mvinyo na kupiga funda kubwa halafu akawasha sigara nyingine.Linah ambaye naye alikuwa anafuta machozi akamtazama shoga yake na kusema
“Lakini Lonny hebu nieleze kifo cha Vero kimesababishwa na nini? Alikuwa anaumwa? Nakumbuka mara ya mwisho kuonana naye ni wiki tatu zilizopita.Nilimuomba afike dukani kwangu ili kuchukua mchango wa harusi kwa sababu nilikuwa na safari ya kwenda Dubai.Alifika dukani kwangu nikaonana naye na kumpatia mchango na akaniahidi kuniletea kadi ya harusi.Taarifa za kifo chake cha ghafla zimenistua sana” akasema LInah
“Linah dunia hii imejaa watu makatili hakuna mfano.Wamemkatili uhai mdogo wangu.Vero hakupaswa kufa mapema namna hii.” Akasema Loniki
“Ina maana Vero ameuawa? Nani hao wamefanya kitendo hicho cha kinyama?
“Ilikuwa ni siku ya pili toka aliporejea nchini akitokea London alikokuja kufanya manunuzi ya harusi yake.Kwa mujibu wa maelezo niliyopewa ni kwamba aliporejea toka London alikwenda kumtembelea mchumba wake na kushinda huko na baadae jioni wakaelekea nyumbani kwa wazazi wa Patrick kulikokuwa na kikao.Baada ya kufika huko kikaoni Patrick akasimama na kuanza kueleza mambo ambayo ni upuuzi mtupu na baadae akatangaza kwamba ameuvunja uchumba kati yake na Vero.” Akasema Loniki
“What .!!!! Linah akashangaa
“Usistuke Linah.Dunia hii imejaa watu makatili mno.Baada ya tangazo hilo la kuuvunja uchumba,watu wengi walianguka na kupoteza fahamu.Kwa mujibu wa mashuhuda ,baada ya kitendo kile Vero alipotea na haikujulikana alikwenda wapi.Baba mzazi wa Patrick ambaye naye amefariki dunia jana alikimbizwa hospitali kwa shinikizo la damu.Wakiwa hospitali walikompeleka baba yao,Patrick na kahaba wake ambaye inasemekana ndiye chanzo cha kuachana na Vero walishangaa kumuona Vero ametokea ghafla akiwa na bastora.Ulitokea ugomvi na Patrick akataka kumnyang’anya Vero bastora na aliposhindwa akaamua kumsukuma Vero akajigonga ukutani na kupoteza maisha.Wamemuua mdogo wangu ,wamemfanyia ukatili mkubwa” akasema Loniki.Linah akavuta pumzi ndefu
“Pole sana Lonny .Kwa kweli ni jambo la kuhuzunisha sana.Siamini kama ni kweli Patrick amemfanyia hivi Vero.Ni kwa nini amefanya hivi?
“Ni kwa sababu alimpata mwanamke mrembo ambaye ni miss Tanzania,akamuona Vero hafai tena.”
“Yaani Patrick aliamua kumuacha Vero kwa sababu ya Miss Tanzania? Akauliza Linah
“Huu ni ukatili mkubwa na hauvumiliki hata kidogo.” Akasema Linah kwa hasira
“Ni ukatili mkubwa sana Linah.Vero amekufa na uzuri wake.Hakuwa hata na mchubuko.” Akasema Loniki
“Patrick yuko wapi? Amekwisha kamatwa? Akauliza Linah
“Anashikiliwa na jeshi la polisi.Tayari kesi yake imekwisha tajwa mahakamani.” Akajibu Loniki
“Afadhali kama amekamatwa.Haki itatendeka kwani siku hizi mahamaka zimeboreshwa na mashauri yanaharakishwa sana.lazima ahukumiwe kutokana na kosa alilolitenda.Anastahili kifungo kirefu gerezani au ikiwezekana hata kifo” akasema Linah
“No Linah.!!....mimi sihitaji hiyo haki ya mahakama.Sina huo muda wa kusubiri haki itendeke baada ya miaka miwili.Isitoshe siviamini vyombo vya kutoa haki.Ni watu wangapi wametenda makosa makubwa na hata mauaji lakini bado tunawaona mtaani? Hakuna awezaye kuufahamu uchungu nilinao moyoni mwangu” akasema Lonny
“Kwa hiyo umepanga kufanya nini Lonny?
“Ndiyo maana nimekuita Linah.Kuna mambo nataka unisaidie”
“Sema chochote Lonny.Mimi niko tayari kukusaidia.” Akasema Linah.Lonny akanywa funda moja la mvinyo na kusema
“Linah nataka kutafuta haki kwa namna ninayojua mimi mwenyewe.Nataka wale wote waliohusika kwa namna yoyote ile na kifo cha mdogo wangu Vero walipe uovu wao kabla mdogo wangu hajaoza kaburini.They all must pay” akasema Loniki halafu akatoa sigara nyingine na kuiwasha akavuta na kumgeukia Linah
“Linah wewe ni rafiki yangu mkubwa toka shule ya msingi na hadi leo hii umeendelea kuwa mshirika wangu wa karibu.Nina imani utakuwa nami katika hili ninalotaka kulifanya kwani naamini hata wewe ulimpenda Vero kama mdogo wako pia” akasema LonikiCHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Lonny wewe ni zaidi ya rafiki.Niko nawe katika kila jambo.Vero alikuwa ni mdogo wetu sote na kifo chake kimeniumiza sana kama kilivyokuumiza wewe.Niambie umefikiria kufanya nini?
“kama nilivyokueleza Linah kwamba ninataka kuitafuta haki mimi mwenyewe.Nataka unisaidie kutafuta mtu ambaye ataifanya kazi ya kulipa kisasi kwa wale wote waliohusika na kifo cha Vero.Wa kwanza kushughulika naye ni huyu msichana miss Tanzania ambaye ndiye chanzo cha Patrick kumuacha mdogo wangu na ndipo nimgeukie Patrick.” Akasema Lonny
Linah akavuta pumzi ndefu,akachukua glasi ya mvinyo akanywa kidogo halafu akasema
“Unataka huyu Happy ashughulikiwe vipi?
“Ninataka kwanza ateseke sana kabla ya kumuondoa katika uso huu wa dunia.”
“Unaposema kumuondoa duniani unamaanisha kumuua ? akauliza Linah
“Exactly..!!!!!Ninataka baada ya kupatwa na mateso makali hatimaye auawe halafu Patrick afuate.wakisha uawa watu hawa ndipo roho yangu itakapotulia.Kwa vile wao pia waliutoa uhai wa Vero basi nao hawana budi kutolewa uhai wao.Je tuko pamoja katika hili? Akauliza Loniki
“Tuko pamoja Lonny.Siwezi kukuacha katika suala hili japokuwa si suala rahisi na linahitaji umakini mkubwa sana.”
“nalifahamu hilo Linah na ndiyo maana nimekuita ili tuongee na kuweka mikakati mizito.Nina hakika suala hili haliwezi kutushinda hata kidogo.Nimekwisha weka nia ya dhati ya kuhakikisha kwamba hawa wote waliohusika na kifo cha Vero wanalipa. Damu ya mdogo wangu haiwezi kupotea bure.Lazima nimlipie kisasi” akasema Loniki
“Lonny utakuwepo hapa nchini kwa muda gani? Akuliza Linah
“Sintaondoka hapa hadi nitakapohakikisha kwamba Patrick na Happy wamelipa uovu wao”
“Basi itakuwa vyema kama utaendelea kuwepo nchini kwa muda mrefu zaidi”
“Ndiyo Linah nitakuwepo hapa nchini kwa muda mrefu tu.Ninachokihitaji ni mtu wa kuweza kuifanya kazi hii kwa umakini mkubwa na ufanisi.Ni kazi ambayo haihitaji aina yoyote ya makosa.Ninajua unafahamiana na watu wengi wa hapa mjini ambao wanaweza kuifanya kazi hii.”
“Usijali Lonny kuhusu hilo.Mimi nitalifanyia kazi hilo suala na ……………….” Kabla hajendelea zaidi mara akatokea shangazi yake Loniki.Mama huyu amekuwa rafiki mkubwa wa Loniki na amekuwa akimuunga mkono katika kila jambo ambalo Lonny analifanya.Hii imepelekea awe akipokea misaada mingi toka kwa Loniki.
“Loniki kikao cha ndugu kinataka kuanza,unaombwa uwe karibu..”
“Sawa shangazi.Ninakuja sasa hivi” akasema Loniki
“Linah twende katika kikao” akasema Loniki
“Hapana Lonny.Kikao hicho kinawahusu wanandugu pekee”
“Toka lini umeacha kuwa ndugu yangu Linah ?Twende tukahudhurie kikao halafu tutaendelea na maongezi yetu”akasema Loniki halafu wakainuka na kuelekea kikaoni.
Karibu ndugu wote walikuwa wamejikusanya kwa ajili ya kikao cha kuhitimisha shughuli za msiba na kutoa ruhusa kwa watu waliotoka mbali kuondoka.Ni mtu mmoja tu ambaye alikosekana katika kikao hiki.Ni sarah.Akatumwa mtu mmoja kwenda kumtafuta nyumba nzima lakini hakuwepo na hata gari lake halikuwepo.Shangazi yake akajaribu kumpigia simu lakini simu ilikuwa inaita bila kupokelewa.
“Simu yake inaita bila kupokelewa” akasema
“hakuna haja ya kumsubiri.Tuendeleeni na kikao” akaamuru Loniki na wote wakakubaliana naye kikao kikaanza
“Najua mahali alikoelekea Sarah.Huyu naye lazima nipambane naye.Ngoja kwanza tumalize msiba nitamfundisha adabu ” akawaza Loniki wakati kikao kikiendelea.
Sarah akiwa garini simu yake iliita akaichukua na kutazama mpigaji.Alikuwa ni shangazi yake.Hakupokea akaiweka chini.
“Najua wananitafuta kwa ajili ya hicho kikao chao.Watanisamehe kwani sintahudhuria kikao hicho.Lazima nihudhurie mazishi ya baba yake Patrick.Nataka upendo na amani vidumishwe baina yatu na si kujenga chuki na hasama.Nawashangaa sana ndugu zangu kwa kumuunga mkono Loniki kwa kila atakachokisema hata kama hakina msingi wowote.Kwa sasa karibu wote wanamuunga mkono kuhusu kulipa kisasi wa Patrick .Nafikiri ni kwa sababu anaishi ulaya na misaada anayowatumia mara kwa mara imewafanya wamsikilize na kumfuata kwa kila jambo atakaloliongea na kumfanya awe ni mtu mwenye sauti katika familia na ukoo .Mimi sintakubaliana kwa namna yoyote ile na upuuzi ambao Loniki anaufanya.Vero alikuwa ni ndugu yetu sote na sote tumeguswa na kifo chake na hapo hapo yatupaswa tukumbuke kwamba hata yeye vero alikuwa na makosa tena makubwa ,na ndiyo chanzo cha haya yote yaliyotokea.Huu ni ukweli ambao hatupaswi kuona haya kuusema.Ninapenda kuona maisha yakiendelea kama awali na sipendi kuona familia zetu zikiingia katika mzozo mwingine.Patrick anashikiliwa na vyombo vya dola na vitafanya uchunguzi na endapo atathibitika kwamba ana makosa basi atapewa adhabu kwa mujibu wa sheria za nchi” akawaza Sarah akiwa njiani kuelekea nyumbani kwa akina Patrick kuhudhuria mazishi ya baba mzazi wa Patrick.
Msafara wa magari ukitokea katika hospitali ya taifa ya Muhimbili kuuchukua mwili wa baba mzazi wa Patrick ,uliwasili nyumbani kwa marehemu na kulifanya eneo lote ligubikwe na vilio.Wengi wa waombolezaji walikuwa wamevaa fulana zenye picha ya marehemu.Taratibu jeneza likashushwa toka ndani ya gari na kuingizwa ndani .
Taratibu zikafanyika na zoezi la kutoe heshima za mwisho likaanza.Watu walikuwa ni wengi sana na zoezi lilichukua muda mrefu tofauti na ilivyotazamiwa.Baada ya zoezi la kutoa heshima za mwisho kukamilika zikafuata salamu za rambi rambi toka sehemu mbali mbali,zoezi lililotanguliwa na kusomwa kwa wasifu wa marehemu.Salamu nyingi za rambi rambi zilitolewa.Toka serikalini ,watu binafsi,mashirika ya umma n,k.Wengi walionyesha kuguswa na msiba huu .Mzee huyu alikuwa ni kipenzi cha wengi na alikuwa na heshima ya kipekee katika jamii.
Salamu za rambi rambi zikamalizika na hivyo kutoa nafasi kwa ratiba nyingine kuendelea.Mwili wa marehemu ukapakiwa garini na kuelekea kanisani kwa ajili ya ibada.Kanisa lilifurika watu waliokuja kumsindikiza mzee huyu katika safari yake ya mwisho.Ibada iliyoongozwa na msaidizi wa askofu wa jimbo kuu la dare s salaam ambaye alikuwa ni rafiki mkubwa wa mzee huyu ilimalizika na msafara ukaelekea makaburini kwa ajili ya mazishi.Watu walikuwa ni wengi sana
Hatimaye ilipotimu saa kumi za jioni safari ya mwisho ya baba yake Patrick ikahitimishwa pale ambapo jeneza lililobeba mwili wake liliposhushwa kaburini.Baada ya familia,ndugu na wawakilishi wa makundi mbali mbali kutupia mchanga katika kaburi,hatimaye zoezi la kufukia likaanza.
Askofu mkuu msaidizi akalibariki kaburi na huo ukawa mwisho wa shughuli nzima ya mazishi.Waombolezaji walitawanyika na wengine wakarejea nyumbani kwa marehemu ili kuendelea na ratiba nyingine.
* * * *
Saa kumi na mbili za jioni Sarah akawasili nyumbani kwao akitokea katika mazishi ya baba mzazi wa Patrick.Mara tu alipowasili akakutana na dada yake Loniki akiwa amesimama nje ya nyumba akiwa na rafiki yake Linah.
“Linah amekuja lini? Sijamuona kitambo kirefu.Mmmhhh !!! ninaanza kupatwa na wasi wasi.Loniki akikutana na Linah.Ninamfahamu Linah ,sifa yake si nzuri hata kidogo.Imewahi kusikika kwamba anajihusisha na biashara ya madawa ya kulevya.Si mtu mzuri huyu hata kidogo na kwa namna anavyoonekana akiongea na Loniki ninahisi kuna jambo wanalipanga.Kwa jinsi ninavyomfahamu Loniki najua lazima atataka kumshirikisha Linah katika mipango yake ya kulipiza kisasi.” Akawaza Sarah halafu akashuka garini na kwenda kuwasalimu.
“Sarah …Pole sana jamani .Pole sana kwa msiba.Mimi sikuwa nafahamu chochote hadi Lonny aliponipigia simu na kunifahamisha .Nimeumizwa sana na kifo hiki cha ghafla cha vero” akasema Linah
“Ahsante Linah tumekwisha poa.Ni mapenzi ya Mungu.Habari za siku nyingi?
“Habari nzuri Sarah.Nimekuwa na safari nyingi hivi sasa ndiyo maana hatuonani .”akasema Linah.Loniki ambaye alikuwa amesimama pembeni akasema
“Sarah mbona hukuhudhuria kikao cha wana ndugu? Ulikuwa wapi?
Sarah akamtazama dada yake bila kumjibu kitu halafu akamgeukia Linah.
“Linah nashukuru sana kwa kufika kwako katika msiba huu.Nikipata wasaa nitafika dukani kwako kuangalia bidhaa mpya”
“Unakaribishwa sana Sarah tena kuna mzigo mpya umewasili.”
“Ok Linah nitafika” akasema Sarah halafu akaelekea ndani akawaacha Lonny na Linah wakiendelea na mazungumzo yao
“Kwa hiyo Linah naomba ulipe uzito unaostahili suala hili.Usijali kuhusu pesa.Ukisha wapata watu wanaoweza kuifanya kazi hii naomba unifahamishe mara moja .Yule hayawani anategemea kupandishwa tena kizimbani jumatano ijayo kwa hiyo sitaki mambo haya yachukue muda mrefu”
“Usijali Loniki.Nitajitahidi kuifanya hiyo kazi .kama nilivyokwambia awali kwamba suala hili ninalipa uzito mkubwa sana na ninakuhakikishia kwamba ndani ya muda mfupi nitakuwa nimewapata watu wanaoweza kuifanya kazi hii kwa ufanisi” akasema Linah halafu wakaagana akaondoka.Baada ya kuachana na Linah,Loniki akaelekea moja kwa moja hadi katika chumba ambacho Sarah allikuwa amekaa na mama yake pamoja na akina mama kadhaa,akamuita Sarah na kumuomba wakaongee nje
“Ile ni tabia gani uliyoionyesha mbele ya Linah? Akauliza Loniki
“Tabia gani?
“Nilikuuliza ulikuwa wapi toka asubuhi,hukunijibu kitu na badala yake ukanitazama kwa dharau.”
“Sikuwa na jibu la kukupa kutokana na swali uliloniuliza.Mimi nina masuala yangu na shughuli zangu nyingi tu na anayepaswa kuniuliza swali kama lile ni mume wangu pekee na si mtu mwingine yeyote”
“Kwa maana hiyo hukuona umuhimu wa kuwepo katika kikao cha familia leo? Akauliza Loniki
“Kwani kukosekana kwangu kumeharibu kitu? Au kuwepo kwangu kungebadili kitu? Akasema sarah.Loniki akamuangalia kwa macho makali
“Kuwa makini Sarah na hayo majibu yako yaliyojaa dharau.Mimi ni dada yako na hupaswi kunijibu namna hiyo”
“Si dharau Loniki,ninakueleza ukweli kwa sababu toka umefika hapa umekuwa ndiye mwenye kutoa amri ya kufanyika kila unachopenda.Kwa taarifa yako Loniki ,mimi siko tayari kukunyenyekea eti kutokana na fedha zako au kwa sababu unaishi nje ya nchi.Nina maisha yangu mazuri tu na mume wangu na sihitaji kumsujudu mtu.Kama utaniheshimu nami nitakuheshimu pia lakini kama hutaniheshimu basi hata mimi sintakuheshimu” akasema Sarah.
Loniki akakunja uso na kumuangalia Sarah kwa hasira
“Nasikitika sana Sarah kwa namna ambavyo umeonyesha kutokuguswa na kifo cha mdogo wako.Nafahamu kabisa ulikuwa katika mazishi ya baba yake Patrick mtu ambaye alimuua mdogo wako kwa makusudi kabisa.Huna aibu hata kidogo” akafoka Loniki.
“Ni kweli nimetoka kumzika baba yake Patrick.Mimi sina roho ya kikatili kama uliyonayo wewe.Hakuna mtu anayepaswa kulaumiwa kwa kilichotokea.Hakuna mtu aliyetegemea mambo haya yangefika hapa yalipofika.nafahamu kwamba umedhamiria kulipiza kisasi kwa Patrick,nakuonya usifanye hivyo.Viachie vyombo vya dola vifanye kazi yake.” Akasema Sarah
“ Stupid !!!!!.akasema loniki kwa ukali
“Sarah wewe ni mdogo sana na huna nafasi yoyote ya kunizuia kufanya chochote.Mimi ndiye niliyeguswa na kifo cha Vero,wewe huonyeshi kuguswa hata kidogo.Kwa maana hiyo ninakuhakikishia kwamba sintafumba macho hadi nihakikishe kwamba wale wote waliohusika katika kusababisha kifo cha Vero wamelipa.Hata wewe kama utaamua kuungana na mashetani hawa,nitapambana nawe vile vile.” Akasema Loniki kwa ukali na kuondoka kwa kasi akaelekea ndani.
“Siko tayari kumtukuza Loniki na kumuacha afanye kila anachotaka kukifanya.Japokuwa ni ndugu yangu lakini niko tayari kupambana naye endapo atafanya jambo lolote lisilokuwa zuri kwa Parick,familia yake au Happy” akasema Sarah huku naye akipiga hatua kuingia ndani
* * * *
Ni saa tano za usiku bado Loniki amekaa kitandani.Juu ya meza ndogo iliyo pembeni ya kitanda kulikuwa na chupa ya mvinyo.Chumba kilikuwa kimejaa moshi wa sigara kutokana na kuvuta sigara mfululizo.
“Sarah amenichefua sana siku ya leo.Ninasema nitamuonyesha kwamba mimi ni mkubwa kwake,kiumri ,kifedha na hata kiuwezo.majibu aliyonijibu jioni ya leo yalijaa dharau kubwa sana.Hapana sintakubali kudharauliwa na mtu kama sarah.lazima nim……………………..” akakatisha mawazo yake baada ya mtu kugonga mlango wa chumba chake..Akainuka na kwenda kuufungua.Alikuwa ni shangazi yake.
“Ouh Shangazi karibu “ akasema Loniki
“Ahsante Loniki.Linah amepiga simu na anahitaji kuongea nawe.” Loniki akachukua simu na kuufunga mlango kisha akampigia Linah
“Loniki kuna habari njema nataka kukupa” akasema Linah baada ya kupokea simu.
“Habari gani hizo Linah”
“Tayari nimempata mtu ambaye unamuhitaji kwa ile kazi”
“wow !!..hizo ni habari njema sana.Hebu nipe taarifa zaidi“ akasema Loniki kwa furaha
“Mtu huyo anaitwa Khumalo.Ni mtaalamu na ana uzoefu mkubwa na shughuli hizi.Ni mtu anayeaminika kwa uwezo wake wa kufanya kazi za namna hii.Tayari nimekwisha ongea naye na amenihakikishia kwamba yuko tayari kuifanya kazi hii.Amekataa kutaja kiwango cha pesa anachokihitaji hadi hapo atakapokutana nawe na akapata maelezo ya kina toka kwako.Amenihakikishia kwamba anao uwezo wa kumshughulikia hata mtu ambaye yuko gerezani kutokana na kuwa na mtandao mpana.Kwa hiyo ametaka siku ya kesho tukutane naye ili tuweze kuangalia namna tutakavyoweza kuutekeleza mpango wenyewe” akasema Linah
“Nashukuru sana Linah kwa msaada wako huu mkubwa.Kesho tutaonana muda gani na huyo khumalo?
“Njoo saa nne ofisini kwangu halafu yeye atatuelekeza mahala pa kumkuta.Yeye si mtu wa kuonekana hovyo hovyo”
“Ok Linah.Nitakuja dukani kwako hiyo kesho saa nne” akasema Loniki halafu akaagana na Linah.
“lazima Patrick na Happy walipe damu ya ndugu yangu.Nataka wao pia wapate maumivu kama ninayoyapata mimi hivi sasa.” Akawaza Loniki huku akiuma meno kwa hasira halafu akachukua glasi ya mvinyo akapiga funda kubwa.
* * * *CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Ni saa sita na dakika kumi za usiku,siku mpya imekwisha anza.Bado Savanna yuko macho .Licha ya kuhisi macho mazito na kulemewa na usingizi lakini bado alikuwa ameinamia vitabu vyake vya sheria akiendelea kupitia mambo mbali mbali ya kisheria ambayo yangeweza kumsaidia katika kesi inayomkabili Patrick
Alizidi kulemewa na usingizi,taratibu akainuka na kuelekea jikoni akatengeneza kahawa na kurejea tena katika chumba chake cha kusomea akaendelea na kazi yake.Alipokaa tu ,simu yake ikaanza kuita.Akaichukua na kutazama mpigaji ,alikuwa ni George.Akakunja uso na kuitupa simu pembeni.
“Huyu mwanaume anatafuta kitu gani kwangu? Kwa nini hataki kuelewa kwamba mimi na yeye basi? Nimekwisha mweleza kwamba sihitaji mawasiliano yoyote naye lakini hataki kunisikia.? Akawaza Savanna.Simu ikaendelea kuita akaamua kuipokea.
“Hivi wewe ni mtu gani ambaye hutaki kuelewa? Nimekwisha kuambia kwamba sitaki mawasiliano yoyote na wewe.George naomba usinisumbue tafadhali.Stay away from me and my life” akasema Savanna kwa ukali
“Ouh Savanna yaani kutengana siku hizi chache umenichukia na hutaki hata nikusalimie? Nimeshindwa kulala bila kuisikia sauti yako.Hebu niambie mpenzi wangu unaendeleaje?” akasema George kwa sauti ya taratibu na kuzidi kuchukiza Savanna
“George tafadhali naomba usiendelee kunisumbua nina kazi nyingi za maana za kufanya.Naomba hii iwe ni mara yako ya mwisho kunipigia simu.” Akasema kwa ukali Savanna
“Oooh Savanna ,naomba tafadhali usikate simu.Najua una kazi nzito ya kufanya kwa ajili ya kumsaidia Patrick ambaye ndiye mwanaume pekee unayemuota usiku na mchana.Naomba ufahamu kwamba jitihada zote unazozifanya ili uwe na Patrick ni kazi bure.Hutaipata hiyo nafasi.Unaelewa ni kwa sababu gani huwezi kuipata hiyo nafasi. Ni kwa sababu Patrick hakupendi.He’s just using you.Pamoja na hayo naomba niweke wazi kwamba mimi ndiye mwanaume wako wa pekee na hutapata mwanaume mwingine zaidi yangu.Ninakupenda kuliko wanaume wote wa dunia hii na nitahakikisha ninakuwa nawe katika maisha yangu yote.Kwa maana hiyo nitahakikisha lengo lako la kutaka kuwa na Patrick halifanikiwi hata kidogo..Nitafany………..”
“Stupid !!!!!!!!!..” Savanna akasema na kukata simu kwa hasira.
“Huyu mwanaume ana akili zote kweli? Yeye ni nani wa kuweza kunizuia mimi nisitekeleze mipango yangu? Ni Mungu pekee ambaye anaweza kunizuia mimi kuwa na Patrick.Hakuna mwanadamu anayeweza kunizuia.Nitahakikisha Patrick anakuwa huru na anakuwa wangu .” akasema Savanna halafu akainamia vitabu vyake.
* * * *
Saa sita za mchana iliwakuta Linah na Loniki katika jumba la kifahari linalomilikiwa na Khumalo.Tayari mlinzi alikwisha pewa taarifa ya ujio wao hivyo akawaruhusu kuingia ndani bila matatizo.Muhudumu aliyekuwa amevaa suti nzuri nyeusi akawapokea na kuwaongoza hadi katika sebule moja kubwa yenye nakshi na samani za kupendeza sana
“Wow !! Inaonekana huyu jamaa ni mtu mwenye kujiweza sana” akanong’ona Loniki baada ya kuviona vitu mbali mbali vya thamani ndani ya sebule lile kubwa.Linah akatabasamu hakujibu kitu.Muhudumu akawakirimu kwa vinywaji wakati wakiendelea kumsubiri Khumalo.
Baada ya dakika zipatazo kumi toka wamefika ,kijana mmoja mwembamba ,mrefu aliyevaa suti iliyomkaa vyema akaingia mle sebuleni.Mara tu alipokutanisha macho yake na Linah,kijana yule akaachia tabasamu pana sana.Linah naye akatabasamu halafu akainuka pale sofani wakakumbatiana.
“Ouh Linah..I missed you so much” akasema Yule kijana
“Its been a long time khumalo.’ Akasema Linah.Loniki akatabasamu alipogundua kwamba Yule kijana ndiye Khumalo.
“Habari yako Linah” akasema khumalo akiwa bado ameushika mkono wa Linah.
“Habari yangu nzuri khumalo.Ni muda mrefu hatujaonana. Unaendeleaje?
“Ninaendelea vizuri Linah.Umepotea siku hizi,haupatikani kabisa.Nilipita China kama wiki tatu zilizopita,nikaonana na Frank akaniambia kwamba ulikuwepo pale na uliondoka jana yake kuelekea Port Elizabeth.Nilisikitika sana kukukosa”
“Ni kweli nilipita China nikaonana na Frank lakini sikukaa sana nilikuwa nawahi shughuli muhimu Port Elizabeth.Mambo yako yanakwendaje?
“Mambo yanakwenda vizuri sana Linah.Nimefurahi sana kukuona.Naona leo umeniletea mgeni” akasema Khumalo huku akimuangalia Loniki na kutabasamu
“yah ! Samahani kwa kutokutambulisha mapema.Huyu ndiye Yule rafiki yangu anaitwa Loniki.Kwa sasa anaishi na kufanya kazi nchini Uingereza.Amekuja nyumbani mara moja kutokana na matatizo ya kifamilia.” Akasema Linah halafu akamgeukia Loniki
“Lonny,huyu ndiye Khumalo,rafiki yangu wa siku nyingi na ambaye atatusaidia katika ile kazi yetu”
“Karibu sana Loniki.Nimefurahi kukuona.Mimi ninaitwa Khumalo kama alivyokueleza Linah.Ninajishughulisha na biashara mbali mbali.Karibu sana na ujisikie nyumbani.” Akasema Khumalo huku akiinuka na kumfuata Loniki mahala alipoketi na kumpa mkono.
“Hata mimi nimefurahi sana kukuona Khumalo.” Akasema Loniki
“Linah alinieleza kwa ufupi kwamba una matatizo na unahitaji msaada.Nilitaka nionane nawe ili tuweze kuongea suala hili kwa kina.Nataka nipate picha kamili ya nini tatizo lako na nini unataka nikufanyie.” Akasema Khumalo huku akitoa sigara katika pakiti na kuiwasha.Loniki akarekebisha koo lake na kumsimulia Khumalo mkasa mzima uliohusiana na kifo cha Vero.Khumalo alikuwa kimya akimsikiliza kwa makini.Baada ya kumaliza kusimulia mkasa ule ,kimya kifupi kikatanda mle sebuleni.Khumalo akainuka na kuelekea katika friji akachukua mapande ya barafu na kurejea akiwa na chupa ya mvinyo mkononi.Akajimiminia mvinyo katika glasi na kupiga funda moja kisha akawasha sigara nyingine akavuta na kupuliza moshi hewani.
“pole sana Loniki.Nimeguswa sana na maelezo yako.Hata kama ningekuwa ni mimi ningefanya kama unavyotaka kufanya.Watu waliosababisha kifo cha mdogo wako hawastahili kuendelea kuwa hai.Mimi niko tayari kukusaidia kufanya hivyo unavyotaka lakini kabla hatujaenda huko nina ushauri mdogo.Nimekuelewa kwamba lengo lako ni kutaka wale wote waliosababisha kifo cha mdogo wako wapate mateso makali na hatimaye kuuawa.Hilo ni jambo lililo ndani ya uwezo wangu lakini kutokana na uzoefu wangu katika shughuli kama hizi ni kwamba kwa wakati huu ambao suala hili bado bichi,tukisema tumuue mmoja wapo kati ya Happy au Patrick basi inaweza ikawa mbaya kwa upande wako kwani itaonekana kabisa kwamba mauaji hayo yamefanyika kwa lengo la kulipa kisasi na familia yako inaweza ikahusishwa moja kwa moja na mauaji hayo na hii inaweza ikatuletea shida sisi sote.” Akasema Khumalo akanyamaza akamuangalia Loniki.
“kwa hiyo unashauri tufanye nini Khumalo” akauliza Linah
“Nionavyo mimi,tunachotakiwa kufanya kwanza ni kuvuruga kabisa mipango yote ya Patrick na Happy ya kuwa pamoja .Tutaanza kwanza kumshughulikia Happy.Tutamfanyia jambo ambalo litauvuruga kabisa uhusiano wake na Patrick na hata yeye mwenyewe anaweza aamue kujitoa uhai wake.Patrick anampenda Happy na endapo wakitengana Patrick atapata mateso makubwa mno.Nadhani ndivyo unavyohitaji Patrick na Happy wapate mateso makali.” Akasema Khumalo.
“Linaonekana ni wazi zuri lakini nahitaji ufafanuzi zaidi hasa namna utakavyomshughulikia Happy hadi yeye na Patrick watengane na ikiwezekana akaamua kujitoa uhai wake yeye mwenyewe” akasema Loniki.
Khumalo akachukua glasi yake ya mvinyo akanywa kidogo halafu akasema
“Tutamteka Happy.” Akanyamaza na kupuliza moshi mwingi hewani
“Nini kitafuata akishatekwa?
“Tutampeleka katika maficho yetu na halafu tutamfanyisha ngono na kundi la wanaume huku akipigwa picha na kurekodiwa katika filamu.Baada ya hapo tutachukua picha zile na kuzisambaza katika magazeti yote ya udaku na katika mitandao yote ya kijamii.Ninaamini baada ya hapo hakutakuwa tena na mahusiano kati ya Patrick na Happy.Happy tayari ana jina kubwa nchini na kwa kitendo cha picha zake za utupu kusambaa atadhalilika sana na nina hakika kama si kuikimbia nchi basi ataamua kujitoa uhai wake.Atateseka sana na hatakuwa na sehemu ya kupita kwani filamu zake tutazisambaza hadi vijijini.Mnaonaje kuhusu mpango huu? Akauliza Khumalo
Linah akatabasamu huku akimtazama Loniki na kusema
“That’s a perfect plan.Au unasemaje Lonny?
“hata mimi nakubaliana na mpango huo kwani lengo langu hasa ni watu hawa wapate mateso makubwa.Nina imani kama mpango huo utafanikiwa basi Happy atakuwa katika wakati mgumu sana.Atateseka sana kisaikolojia na kutokana na msongo wa mawazo ataona ni bora ajitoa uhai.Nadhani tukifanikiwa mpango huu kwa Happy tutakuwa tumemgusa kwa kiasi kikubwa na Patrick ambaye anampenda Happy.Wote wawili watapata mateso makali sana ya moyo na nina hakika hawatakuwa pamoja tena.Gharama nzima ya shughuli hii yote ni kiasi gani Khumalo? Akauliza Loniki.Khumalo akapuliza moshi mwingi hewani na kusema
“Kwa sababu ni wewe na umeletwa na swahiba wangu Linah basi utanipa shilingi million hamsini tu, pesa ambayo nitawapa vijana watakaonisaidia katika kuifanya hiyo kazi.Mimi sintapata chochote katika kazi hii.Nimeamua kukusaidia tu” akasema Khumalo.Loniki alistushwa sana na kiwango kile kikubwa alichokitaja Khumalo.Akainama na kufikiri.
“Ok Khumalo,pesa si tatizo.Ninachohitaji mimi ni mpango utekelezeke.Nitakupatia hizo millioni hamsini”
“Sawa Loniki.Kitu kingine ninachokihitaji toka kwako ni picha ya huyo Happy na maelezo yake kamili,mahala anapoishi au kama huna nipe picha yake na mahala anapoishi vijana wangu watamtafuta.”
“kwa sasa sina picha ya Happy lakini jumatano ijayo kesi ya Patrick itatajwa tena.Ingekuwa vyema kama ungehudhuria mahakamani wewe na vijana wako na mkamuona huyo mtu mwenyewe.”
“Hilo ni wazo zuri.Basi tutafika mahakamani siku hiyo na kumtambua huyo Happy na Patrick.” Akasema Khumalo halafu akaagana na akina Linah kwani kuna mahala alikuwa akiwahi.
“Linah umefahamiana vipi na Khumalo? Akauliza Loniki wakiwa njiani baada ya kuondoka nyumbani kwa Khumalo
“Khumalo nilifahamiana naye katika michakato yangu ya biashara.Toka wakati huo tumekuwa marafiki wakubwa sana.”
“Amenifurahisha sana kwa namna anavyojiamini na hata mpango wake ni mzuri.Ninachotaka ni Happy na Patrick waumie na endapo mpango huu utakamilika basi najua wataumia mno na ndoto yao ya kuwa pamoja itapotea” Akasema Lonny
“Khumalo ni mtu mwenye roho ya paka.Usoni anaonekana ni kijana mpole lakini awapo kazini sura yake hubadilika na kuwa ya shetani.Wewe utaona tu namna atakavyoifanya kazi hii uliyompa.”
“Nitafurahi sana sana kuona namna huyo kahaba Happy aliyevamia mapenzi ya watu atakavyodhalilika.Nataka aumie moyoni kama sisi tulivyoumia.Damu ya Vero haiwezi kupotea bure”
“Usijali Lonny.Kwa sasa unaweza kupumua baada ya kumkabishi Khumalo jukumu zima.” Akasema Linah
Mahakama ya kisutu ilifurika watu zaidi ya siku za kawaida.Kilichovutia idadi kubwa ya watu ni kesi ya kusababisha kifo inayomkabili Patrick.Kesi hii ilivuta hisia za watu wengi hasa baada ya aliyekuwa mrembo wa Tanzania ,Happy Kibaho kutajwa kuwa na uhusiano wa kimapenzi na kijana huyu aliyesababisha kifo cha Vero. Kwa siku ya leo kesi hii ilikuwa inatajwa kwa mara ya pili.
Waandishi wa habari toka vyombo mbalimbali vya habari walikwisha wasili mahakamani toka asubuhi ili kujiandaa kupata habari kuhusiana na kesi hii iliyoandikwa sana na magazeti mengi hapa nchini.
Saa nne kasoro dakika sita za asubuhi gari aina ya Range rover Vogue lenye rangi nyeupe ikawasili pale mahakamani.Watu wengi waligeuza shingo zao kulitazama gari lile la kifahari lililokuwa likiingia taratibu pale mahamani.Baada ya kuegeshwa mlango ukafunguliwa na mwanadada mmoja mrembo sana aliyevaa suti nyeusi akashuka na kuacha minong’ono ikiendelea midomoni mwa watu waliokuwapo pale mahakamani.Mwanadada Yule ambaye alibarikiwa uzuri,alikuwa akitembea kwa madaha kuingia katika jengo la mahakama.Huyu alikuwa ni Savanna wakili mahiri anayemtetea Patrick.Wakati akielekea katika jengo la mahakama ,mara simu yake ikaita akasimama ,akaitoa simu yake na kutazama mpigaji halafu akageuza shingo yake na na kwa mbali akamuona Andrew akitabasamu.Akatembea kumwendea.
“Habari za asubuhi Andrew.Nimechelewa kidogo na ndiyo maana sikuangalia pembeni.” Akasema Savanna huku akimpa mkono Andrew
“Usijali Savanna.Unaendeleaje? hatukuonana tena toka tulipomzika mzee”
“ Ninaendelea vizuri Andrew.Ni kweli hatujaonana tena,nilikuwa na shughuli nyingi sana kuhakikisha kwamba kila kitu kinakwenda vizuri.Alois amekwisha fika?
“Ndiyo ,familia nzima imekwisha fika ila mama bado yuko garini.”
“Nipeleke nikawasalimu” akasema Savanna kisha wakaelekea lilipo gari la akina Alois
“Mama shikamoo” Savanna akamsalimu mama yake Patrick.
“ Marahaba mwanangu.Vipi hali yako?
“ Hali yangu nzuri mama.Unaendeleaje?
“ namshukuru Mungu ninaendelea vizuri.Kila siku ninazidi kupata nguvu.”
“Hilo ni jambo la kushukuru sana mama” akasema Savanna halafu wakaendelea na maongezi mafupi kisha akawaaga na kwenda kuendelea na mambo mengine.
Saa tano na dakika kumi za asubuhi,basi linalobeba mahabusu toka katika gereza la Uwangwa likawasili likiwa chini ya ulinzi wa askari kama kawaida yake.
“Nina hakika hili ndilo basi linalotumika kuwabeba mahabusu na Patrick atakuwemo ndani ya basi hili.Jitahidi umfahamu vizuri” Mwanamke mmoja aliyekuwa ndani ya gari nyeusi aina ya Noah akamwambia kijana mtanashati aliyekuwa naye mle garini.
“Usijali Loniki,macho yangu yanaona kama tai” akasema Kijana Yule mwembamba na mwenye sura angavu.
“nakuamini Khumalo” akasema Loniki ambaye alifika mahakani hapo akiwa ameongozana na rafikiye wa karibu na wa siku nyingi sana Linah pamoja na khumalo,kijana hatari ambaye amekodishwa ili kuweza kuutekeleza mpango kabambe wa Loniki wa kulipiza kisasi kwa wale wote waliosababisha kifo cha mdogo wake Vero.
“Mbona huyo Miss Tanzania hajatokea mpaka sasa? Inawezekana asifike mahakamani? Akauliza Khumalo
“Usihofu Khumalo,lazima atafika tu.Nina hakika hawezi kukosa mahakamani.Wait…!!!” Loniki akastuka baada ya kuona kitu
“Yule si Sarah ? akauliza Loniki na kumtazama Linah
“Ni yeye.Ni nani wale anaongea nao?
“Familia ya Patrick.Nimemkumbuka mmoja wao Yule mwenye shati jekundu .Alikuja kuwawakilisha katika mazishi ya Vero.Nashindwa kumuelewa huyu mdogo wangu .Haonyeshi kuguswa kabisa na kifo cha mdogo wake.Potelea mbali mimi nitaendelea na mipango yangu na nitahakikisha wale wote waliosababisha kifo cha Vero wanalipa “akasema Loniki huku akivaa miwani yake myeusi
“Lonny wafungwa wameanza kushushwa katika basi” Linah akamstua Loniki ambaye alikuwa ameinama.Loniki akavua miwani yake na kukodolea macho mahabusu waliokuwa wakishushwa garini.
“There he is !!!!Umemuona Yule mwenye shati jeusi? That’s Patrick.” Akasema Loniki akimuelekeza Khumalo.
“Ouh.!.He’s such a handsome guy..” akasema Linah na kumfanya Loniki ageuze shingo akamtazama kwa macho makali
“Unasemaje Linah ? akauliza Loniki
“Nakutania Lony” akasema Linah huku akicheka kidogo
“Tafadhali Linah si nyakati zote huwa za utani.” Akasema Loniki halafu akamgeukia Khumalo
“Tayari nimekwishamuona Patrick.bado huyo mwanamke Miss Tanzania.” Akasema Khumalo
“She must be here..she must be somewhere around here..Let’s just wait…” akasema Loniki.
Saa sita za mchana kesi ya Patrick ikatajwa tena.Chumba kilijaa watu .Wakati mabishano ya kisheria yakiendelea kati ya mawakili wa utetezi wakiongozwa na Savanna dhidi ya wale wa serikali Loniki ambaye naye alikuwemo ndani ya chumba kile cha mahakama pamoja na rafikiye Linah na Khumalo,aliendelea kupepesa macho yake kila kona ya kile chumba akimtafuta Happy.
“Kumbe huyu mwanamke ndiye anayemtetea Patrick.!! Mnafiki mkubwa huyu.Namkumbuka sana siku ya mazishi ya Vero alikuwepo na alionekana ni mwenye huzuni nyingi sana.Anaonekana kuifahamu vizuri sheria lakini pamoja na juhudi zake zote na ufundi wake wote katika sheria hataweza kushindana nami hata kidogo.” Akawaza Loniki huku akiendelea kuyazungusha macho yake mle katika chumba cha mahakama na mara katika pembe moja ya chumba akamuona msichana mmoja aliyejifunga kitambaa kichwani pamoja na miwani myeusi.
“There she is…!!..japokuwa amejaribu kujificha ili asionekane lakini hawezi kunipotea hata kidogo.Sura yake ipo kichwani kwangu na hakuna namna anavyoweza kufanya ili kunipotea” akawaza Loniki huku akiendelea kumtazama msichana Yule kwa jicho la chuki.
“Linah nimemuona Happy.Yule pale aliyejifunga kitambaa chekundu kichwani.” Akasema Loniki na kumuelekeza Linah mahala alipokaa Happy.Linah akamnong’oneza Khumalo na kumuelekeza mahala alipokaa Happy.Wote watatu kwa pamoja wakaendelea kumuangalia Happy.
Kama ilivyokuwa kwa watu wote mle katika chumba cha mahakama,Happy naye alielekeza macho na akili yake katika malumbano ya kisheria yaliyokuwa yakiendelea baina ya wanasheria.Ghafla akageuka baada ya kuguswa begani na Pendo mfanyakazi wao wa ndani aliyekuwa ameongozana naye siku hii ya leo .
“Dada Happy kuna watu nimewaona muda mrefu wamekuwa wanakuangalia sana” akasema Pendo .Happy akageuza shingo yake katika upande alioelekezwa na Pendo na mara akakutanisha macho na sura za watu watatu zilizokuwa zikimuangalia huku zikijadili jambo.Hakuwafahamu watu wale na hawakuonekana kama waandishi wa habari.
“Twende tutoke humu ndani” akasema Happy kisha wakainuka na kutoka nje ya chumba cha mahakama huku akipigwa picha na waandishi wa habari.Baadhi ya waandishi wa habari walimfuata na kujaribu kumuuliza maswali lakini hakuwa tayari kuongea chochote na waandishi wa habari. Moja kwa moja akaenda kusimama nje ya gari lakeCHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Watu wale kwa namna walivyokuwa wakiniangalia na kunong’onezana walinitoa kabisa hamu ya kukaa mle mahakamani.Yawezekana wakawa ni ndugu wa Patrick au wa Vero.Ni heri nikae tu hapa nje hadi mahakama itakapomalizika.Savanna atanieleza kitakachoendelea..Isitoshe sitaki kuonana na familia ya Patrick kwa sasa.Hawatanitazama kwa jicho zuri hata kidogo” akawaza Happy
* * * *
Mjadala mkali wa kisheria ulimalizika na hakimu akaiahirisha kesi ile na kuipangia tarehe nyingine ya kutajwa.Akiwa chini ya ulinzi Patrick akaongozwa na kutolewa nje ya mahakama.Alifarijika sana baada ya kumuona mama yake mzazi japokuwa sura yake ilikuwa imesawajika sana.Pamoja na msiba mzito wa kufiwa na mumewe kipenzi lakini bado alijitahidi na kufika mahakamani kufuatilia kesi ya mwanae.Pembeni yake alikuwa amekaa Alois pamoja na mke wake.Patrick akawapungia mkono.Walikuwepo pia ndugu mbali mbali na marafiki waliokuja kumpa moyo katika kesi hii.Mara akagonganisha macho na Sarah dada yake Vero aliyekuwa amekaa na Andrew.Patrick akawapungia mkono halafu akaangalia chini
Wakati akitoka mle chumbani,Loniki alikuwa akimtazama kwa jicho la chuki.
“Naisubiri kwa hamu siku nitakayokuona ukipata mateso na maumivu makali kama ninayoyapata mimi.Wewe na kahaba wako Happy lazima mtalipa kwa kitendo mlichokifanya.Its not a long time from now.You’ll pay dearly” akawaza Loniki huku akiuma meno kwa hasira
Baada ya Patrick kutolewa nje ya chumba cha mahakama,watu nao wakaanza kutoka.Nje ya mahakama katika gari moja lenye rangi nyeusi ,Happy alikuwa amesimama akisubiri kuonana na Savanna ili ajue kinachoendelea .Akiwa nje ya gari lake,kijana mmoja mtanashati aliyevalia nadhifu sana akajongea taratibu hadi mahala aliposimama Happy.
“Habari yako dada” akasema Yule kijana
“Nzuri habari yako” akaitika Happy huku akiendelea kuangaza macho yake katika mlango akimtafuta Savanna
“You must be Happy Kibaho” akasema Yule kijana aliyevalia nadhifu.Happy hakumjibu kitu bado aliyaelekeza macho yake mlangoni.
“By the way,I’m George….George Simkaya” akasema Yule kijana huku akimpa mkono Happy.Happy akamtazama Yule kijana usoni na kumwambia
“Tafadhali George ,sina muda wa kujibu au kuongea lolote na waandishi wa habari siku ya leo.” Akasema Happy
“Happy mimi si mwandishi wa habari.Ninafanya kazi ikulu” akasema George huku akitoa kitambulisho chake na kumuonyesha Happy
“Unataka nini toka kwangu George?
“Happy nimekuja kwako nina maongezi nawe ya muhimu sana”
“Maongezi na mimi? Yanahusu nini? Akauliza
“Yanakuhusu wewe,na hatima ya Patrick na kinachoendelea kuhusiana na kesi yake” akasema George na kumstua kidogo Happy
“Nini kuhusu hatima ya Patrick na kinaendelea katika kesi ya Patrick?
“Ni suala ambalo tunatakiwa tukae ili nikueleze kwa makini sana.Je una nafasi ya kutosha sasa hivi? Akauliza George
“Naomba unisubiri mara moja kuna mtu nahitaji kumuona” akasema Happy na mara simu yake ikaita
“Halo Savanna.” Akasema Happy baada ya kuipokea ile simu
“Happy habari yako? Nimeupata ujumbe wako sasa hivi baada ya kuwasha simu.Uko upande upi? Akauliza Savanna.Happy akamuelekeza mahala alikoegesha gari lake .Alipomaliza kuongea na Savanna simuni akageuza shingo yake lakini George hakuwepo.Happy hakujali sana mawazo yake yote hivi sasa yalikuwa kwa Savanna ambaye alimuona akipiga hatua kuelekea kule alikokuwa
“Habari yako Happy.Nafurahi kukuona leo umefika.” Akasema Savanna huku akitabasamu na kulifanya jino lake moja lililotengenezwa kwa madini ya thamani kuonekana.
“Nashukuru Mungu ninaendelea vizuri.Nilikuwamo ndani ya chumba cha mahakama lakini niliwahi kutoka.Sikutaka kuonana na ndugu za Patrick” akasema Happy
“Kwa sasa bado wana hasira kwa kilichotokea na hawatakuangalia kwa jicho zuri lakini nina imani itafika wakati ambao mambo haya yote yatapoa” akasema Savanna
“Savanna samahani sana najua una majukumu mengine lakini kitu nilichokuitia hapa ni kutaka kufahamu nini kinaendelea kuhusiana na kesi” akasema Happy
“Leo kulikuwa na mjadala mzito wa kisheria wa kutaka kesi hii ibadilishwe na kuwa kesi ya kuua bila kukusudia ili Patrick aweze kupatiwa dhamana.Japokuwa bado upande wa mashitaka unaendelea na uchunguzi lakini nina imani tutafanikiwa kuibadili kesi hii. Kwa sasa tumeiomba mahakama iwaamuru upande wa mashitaka kukamilisha upelelezi wao haraka ili tuweze kuwasilisha ombi letu la kubadili mashtaka.Bado tuna safari ndefu lakini nina uhakika mkubwa wa kusinda kesi hii.” Akasema Savanna bila ya kuwa na wasi wasi wowote.Maneno yale yakampa faraja sana Happy na uso wake ukajenga tabasamu pana.
“Nashukuru sana Savanna kwa kunipa moyo.”
“Happy usihofu kitu chochote.Kesi hii haina ugumu sana kwangu na nina imani siku moja Patrick atakuwa huru.Japokuwa inaweza ikachukua muda mrefu kidogo kutokana na upelelezi kuchukua muda mrefu lakini nakuhakikishia kwamba nitapambana hadi nihakikishe kwamba Patrick anakuwa huru.” Akasema Savanna halafu wakaagana.
Happy hakutaka tena kuendelea kukaa pale mahakamani,akaingia katika gari lake lakini kabla hajawasha gari,George akatokea na kugonga kioo cha mlangoni.Happy akaonekana kukerwa na kitendo kile akashusha kioo na kusema kwa ukali
“Its you again..Ulikuwa wapi? Mbona ulipotea ghafla?
“Sikutaka Yule wakili Savanna anione ninaongea na wewe ndiyo maana nikajificha”
“Do you know her?
“C’mon Happy,don’t ask so many questions. Are you ready to hear what I want to tell you? Akauliza George.Happy akafikiri kidogo na kusema
“Get in the car.” George akafungua mlango wa gari na kuingia ndani kisha Happy akaliondoa gari eneo lile la mahakama.
“Follow her..” akaamuru Khumalo aliyekuwamo katika gari aina ya Noah akiwa na Loniki na Linah wakimuangalia Happy.Baada ya Happy kutoka katika eneo la mahakama ,gari ya akina Loniki nayo ikatoka na kuanza kumfuatailia Happy bila ya yeye kufahamu kama alikuwa anafuatiliwa.Linah aliendesha gari lile kwa ustadi mkubwa
* * * *
“George jambo gani unalotaka kuniambia? Akuliza Happy wakiwa garini.George akamtazama Pendo aliyekuwa na Happy mle garini.
“Do you trust her? Akauliza George.
“Ofcourse I do trust her” akasema Happy
“George unataka kuniambia nini? akauliza tena Happy akiwa na wasi wasi
“Happy utanisamehe sana lakini ninachotaka kukwambia kitabaki kuwa kati yetu.Hapaswi mtu mwingine yeyote kujua.Pale mbele kuna baa,pinda kushoto ingia pale Masuke Bar,tutaongea kwa dakika chache halafu utaendelea na safari yako” akasema George.Happy akaonyesha wasi wasi kidogo
“Happy naomba uniamini.Mimi si mtu mbaya na wala hakuna jambo lolote baya litakalokupata” akasema George.Bila kusema lolote Happy akawasha taa ya kushoto kuashiria kwamba alikuwa anakata kona na kuingia Masuke Bar.Baada ya kuegesha gari akashuka yeye na George na kwenda kuketi chini ya mwavuli.Pendo alibaki garini.
“George naomba tusipoteze muda.Nieleze kile ambacho unataka kuniambia.I’m not too comfortable to be seen here” akasema Happy.George akanywa maji kidogo halafu akasema
“Kwanza kabisa naomba nikupe pole sana kwa masahibu yote yaliyokukuta”akasema George.
“Please George go direct to the point.Hatukuja hapa kupeana pole” akasema Happy huku akionekana kuanza kukasirika
“Usihofu Happy jambo kubwa nililotaka kukueleza ni kuhusiana na Yule mwanamke uliyekuwa unaongea naye pale mahakamani”.
“Savanna? Akauliza Happy
“Exactly !!!Huyo huyo Savanna” akasema George
“Savanna kafanya nini?
“Do you real know her? akauliza George
“Bado simfahamu vizuri.Tumefahamiana siku za hivi karibuni.Yeye ni wakili anayemtetea mpenzi wangu”
“Sawa Happy lakini inaonekana bado hujamfahamu Savanna ni nani.Naomba unisikilize kwa makini” akasema George
“Savanna ni mke wangu……alikuwa mke wangu”
“Savanna alikuwa mke wako? Happy akashangaa
“Ndiyo alikuwa mke wangu,lakini kwa sasa hatuko pamoja tena.Kilichosababisha mimi na yeye tukatengana ni Patrick”
“Patrick ..!!!..Happy akashangaa
“Patrick anahusika nini na kutengana kwenu wewe na Savanna? Akauliza Happy
“Kuna jambo ambalo bado hujalifahamu Happy .Ni kwamba Patrick na Savanna walikuwa na mahusiano ya siri ya kimapenzi kwa muda mrefu.”
“Mambo gani haya unanieleza George? Patrick na Savanna waliwahi kuwa wapenzi???..thats impossible.Patrick alikuwa na mpenzi wake ambaye alikuwa afunge naye ndoa na akafariki katika ugomvi na ndiyo sababu ya yeye kushikiliwa na vyombo vya usalama.”
“Niamini Happy.Mimi na Savanna tumekuwa pamoja kwa miaka mitano sasa.Kabla sijakutana na Savanna,tayari alikuwa katika mahusiano ya siri na Patrick ambaye kwa wakati huo tayari alikuwa katika mahusiano ya wazi na mchumba wake Veronika.Nilipata wakati mgumu sana kuweza kumshawishi Savanna akubali kuwa na mimi kwani walikuwa wakipendana sana na Patrick.Ilimlazimu Savanna amueleze ukweli Patrick na ndipo alipompa ruhusa ya kuwa na mimi.Pamoja na kuwa na mimi lakini mpaka leo hii akili ya Savanna bado iko kwa Patrick.Kwa kuwa ninampenda sana Savanna niliamua kuishi naye hivyo hivyo nikiamini kwamba siku moja atanipenda na kunikabidhi moyo wake lakini katika miaka hii yote niliyoishi naye sijaweza kufanikiwa kumuondoa Patrick katika akili yake.Kama huniamini ,siku ukikutana naye angalia mkufu wake anaopenda kuuvaa shingoni,una kidani kilichoandikwa P&S na hata pete yake ya dhahabu ambayo huwa haitoi kidoleni imeandikwa hivyo hvyo.Umewahi kumchunguza vizuri Patrick? Naye pia ana pete kama hii aliyonayo Savanna.” Akasema George .Happy akatoa kitambaa na kujifuta jasho lililoanza kumtoka.
“Ni kweli tukiwa Arusha nilimuona Patrick akiwa na pete kama hiyo anayoisema George na nilimuuliza kama pete ile ina maana yoyote akasema kwamba haina maana yoyote.” Akawaza Happy.George akaendelea
“Mimi na Savanna tumetengana hivi majuzi baada ya Patrick kukumbwa na masahibu.Kilichotutenganisha ni baada ya kugundua kwamba Savanna anataka kuitumia kesi hii ili aweze kuwa tena na Patrick na hasa baada ya Veronika mpenzi wa Patrick kufariki.Hii ni nafasi pekee aliyoipata ya kuurejesha uhusiano wake na Patrick na hasa baada ya mchumba wa Patrick kufariki dunia na hilo amekiri yeye mwenyewe kwa mdomo wake.Ninamfahamu Savanna,ni mwanamke ambaye akidhamiria kitu lazima atakipata.Dhamira yake ya kuitumia kesi hii kujitengenezea mazingira ya kurudiana na Patrick lazima itatimia kama asipodhibitiwa haraka” akasema George.Mapigo ya moyo wa Happy yalibadilika na kuanza kwenda mbio.
“Why are you telling me all these now? Akauliza Happy
“Happy nimekwambia kwa wakati huu ili mimi na wewe kwa pamoja tuweze kufanya kitu.Siwezi kukuficha Happy kwamba ninampenda sana Savanna na ndiyo maana ninajitahidi kufanya kila niwezalo ili niweze kurudiana naye.Sitaki kuona akiangukia tena katika mikono ya Patrick.Ninaamini vile vile kwamba Patrick ni mtu ambaye unampenda sana na hivyo hauko tayari kumuona akiangukia katika mikono ya Savanna.”
“Geoerge unataka tufanye nini” akauliza Happy.Uso wake ulikwisha badilika.Alikuwa na wasi wasi mwingi
“Nataka tufanye kila linalowezekana ili Savanna asiendelee kuisimamia kesi hii.” Akasema George.Happy akainama chini na kuzama katika mawazo.
“Ninakubaliana na Geroge kwani hata mimi nilikuwa nashangaa sana kwa nini Savanna aamue kumtetea Patrick bila malipo yoyote? Kumbe ana lake jambo.Nashukuru sana George amenifumbua macho.” Akawaza HappyCHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“George umenichanganya sana akili yangu na sielewi tutafanya nini ili tuweze kumuondoa Happy katika kesi ya Patrick.Kwa uwezo wangu mimi siwezi kufanya hivyo kwa sababu sina hakika kama Patrick au ndugu zake wanaweza wakakubali.Wote kwa pamoja wana imani kubwa na Savanna” akasema Happy
“We have to do something Happy.We have to stop her.There is must be a way to stop her” akasema George.
“Ugumu uliopo hapa ni kwamba Patrick anamuamini mno Savanna na ili kuweza kumtoa Savanna ni lazima Patrick na familia yake waamue.Vinginevyo sisi wawili hatuna uwezo wowote wa kumfanya Savanna atoke katika kesi hii.Sina hakika kama Patrick anaweza akakubali kumuondoa Savanna katika kesi yake.Kitu kingine ambacho kitaleta ugumu ni kamba Savanna anaifanya kazi hii bila kudai hata senti tano. Kazi hi anaifanya bure kabisa na yeye ndiye aliyejitolea kulipa gharama zozote zitakazohitajika katika kesi hii.” Akasema Happy.Kimya kikatanda pale mezani
“ Nimekuelewa Happy lakini lazima tujaribu.Jaribu kuongea na Patrick na umshawishi kwamba Savanna hafai kuisimamia kesi yake.Mimi nitatafuta mawakili wapya na hata kuwalipa niko tayari”
Happy akafikiri kidogo na kusema
“ Nitajaribu George.” Kimya kifupi kikapita Happy akasema
“George nashukuru sana kwa taarifa uliyonipa japokuwa imenistua sana lakini nashukuru kwa kunifumbua macho kuhusiana na kile kilichokuwa kinaendelea nyuma ya pazia.Naomba niende nikapumzike nitafakari kwa kina kuhusu suala hili na endapo kutakuwa na namna yoyote ambayo nitaona tunaweza kufanya basi nitawasiliana nawe mara moja” Akasema Happy na wakabadilisha namba za simu .Happy akaondoka akaelekea garini .Kichwa chake alikiona kizito sana.Akainamia usukani
“Ouh my God ! why always me? ..Happy akasema huku akiupiga usukani kwa mikono yake.
“Dada Happy kulikoni? Akauliza Pendo
“Ouh Pendo ! Samahani kichwa changu kimetingwa na mambo mengi sana.Anyway twende tuondoke hapa” akasema Happy akawasha gari wakaondoka.
“Ninaona kama dunia inaniadhibu.Wakati bado jereha la moyo linavuja damu na sijui nitalitibu vipi ,linaibuika tena suala jingine.Ee Mungu Kwanini umeamua kuniadhibu namna hii? Akawaza Happy
“Patrick amewahi kuwa na mahusiano na Savanna…?!!!.” Kila alipowaza jambo hili aliendelea kumuumia sana kichwa.
“Ninakubaliana na maneno ya George kwa sababu Patrick huwezi kumweleza chochote kuhusu Savanna akakuelewa.Anamuamini Savanna kupita kiasi.Vile vile hainiingii akilini hata kidogo katika ulimwengu wa sasa mtu akajitolea kuifanya kazi hii ngumu ya kisheria bila kulipwa chochote.Savanna amefanya hivi kwa sababu ana agenda yake ya siri.I’m so confused” akawaza Happy
“lakini pamoja na kuwa na agenda ya siri,Patrick ataendelea kuwa wangu peke yangu.Sintamruhusu Savanna amchukue Patrick toka katika mikono yangu.I’ve sacrificed a lot for Patrick and I wont loose him this time.Nitapambana naye” akawaza Happy
“Loniki,tayari nimekwisha wafahamu wahusika wakuu wanaotakiwa kushughulikiwa.Huyu mwanamke ,Happy ndiye nitakayeanza naye na siku ya kesho lazima nimpate” akasema Khumalo huku akipuliza moshi wa sigara hewani.Walikuwa katika ofisi ya Linah baada ya kutoka mahakamani.
“Nitashukuru sana kama zoezi hili litakwenda haraka kwani itanisaidia hata mimi kurejea haraka Uingereza.Nimeapa sintaondoka Tanzania hadi Patrick na Happy na wengine wote ambao wamesababaisha kifo cha Happy wawe tayari wamekwishalipa..Jioni ya leo nitakupatia kiasi cha shilingi million arobaini na zitakazobaki kumi nitakupatia baada ya kazi hii kukamilika.Kama kazi itakwenda vizuri basi ninaweza hata kukuongeza zaidi.Kwangu mimi pesa si tatizo hata kidogo.” Akasema Loniki.Khumalo akaaga na kuondoka zake kwa miadi ya kuonana jioni ili aweze kupatiwa mzigo wake wa shilingi millioni arobaini.
“Ninamuamini sana Khumalo.Anaongea taratibu lakini siku zote huwa anamaanisha anachokisema.Kama ameahidi kwamba kesho atampata Happy basi amini atafanya hivyo” akasema Linah baada ya Khumalo kuondoka
“Nitashukuru sana .Leo roho yangu imechafuka mno baada ya kumuona Patrick mahakamani tena akitabasamu kana kwamba hana hatia.Sitaki kuisubiri haki ya mahakama ambayo pengine isipatikane.Nitamlipia Vero kwa namna ninayojua mwenyewe.Natamani hata sasa hivi nisikie kamba Patrick na Happy wamefariki dunia.Sikufichi Linah ,moyo wangu utakuwa na amani pale tu Patrick na Happy watakapoacha kuivuta hewa hii safi na sintafumba macho mpaka nitakapohakikisha kwamba wameondoka duniani” akasema Loniki halafu akaagana na Linah kwa miadi ya kukutana jioni ili wamkabidhi Khumalo mzigo wake.
Baada ya kutoka ofisini kwa Linah,Loniki akarejea nyumbani na kumkuta mdogo wake Saraha tayari amekwisha fika na anaongea na mama yake.Loniki akasalimiana na mama yake bila kumsemesha lolote Sarah
“Mbona Sarah humsalimu? Mmekwisha onana? Akauliza mama yao
“Mama sijisikii hata kumpa salamu yangu huyu mwanao.Sioni kama anastahili salamu yangu.” Akasema Loniki kwa dharau
“Sihitaji salamu yako Lonny.” Akasema Sarah huku akitabasamu
“Sarah kwa nini unamjibu hivyo dada yako? Akafoka mama yao
“Mama kamwe sintakubali au kuvumilia dharau za Loniki.Siko tayari kumnyenyekea Loniki na kumsikiliza kwa kila anachokiongea kwa sababu tu anaishi Ulaya.” Akasema Sarah na kwa hasira akaelekea katika gari lake na kuondoka akiwaacha mama yake na Loniki wakishangaa
“Mama huyu mwanao amenichefua sana .Sikutegema kabisa kumuona akiwa hivi.Haonyeshi uchungu wowote ule wa kufiwa na mdogo wake na badala yake anadiriki hata kushirikiana na wauaji wa mdogo wake.Mama siko tayari kuvumilia upuuzi kama huu anaoufanya Sarah.Ngoja nimalize mambo yangu nitamfundisha adabu” akasema Loniki
“Hata mimi sijafurahishwa kabisa na tabia ya Sarah na hasa ya kuchangamana na familia ya Patrick,ambao wametupa mateso haya yote.Kwa uchungu nilionao sijui hata nifanye nini” akasema mama yake Loniki
“Usijali mama,haki lazima ipatikane.Lazima Patrick na wale wote waliosababisha kifo cha mdogo wangu walipe.Sintarejea Uingereza hadi nihakikishe kwamba wote walimuua mdogo wangu wamelipa”
“ Kwa kweli kwa uchungu ninaousikia hata mimi natamani sana waliomuua mwanangu nao walipe uovu wao.Walitenda kitendo cha kinyama sana.Wamemuua mwanangu bila kosa lolote..Ouh Vero ..!!!!” akashindwa kuendelea akaanza kulia.Loniki ambaye naye macho yake yalijaa machozi akamkumbatia mama yake
“Basi usilie mama Haki lazima ipatikane.” Akasema Loniki
“Ahsante mwanangu ,ila naomba wewe na Sarah msigombane kwani sina uwezo wa kuhimili maumivu mengine tena .”
“Hatutagombana mama .Tutarekebishana tu “akasema Loniki
* * * *
Saa kumi na moja za jioni Happy aliamka .Toka aliporejea akitokea mahakamani alikuwa amelala.Kutokana na mawazo mengi aliyokuwa nayo aliamua kumeza vidonge vya usingizi na kulala kwa muda mrefu namna hiyo.Mambo aliyoambiwa na George yalimchanganya sana na alishindwa afanye nini.Kichwa kilikuwa kinamgonga kupita kiasi. Akainuka na kukaa kitandani.
“For the first time I feel dead.Kwa mambo aliyoniambia George ninajihisi kama mfu.Siamini kama Patrick na Savanna waliwahi kuwa wapenzi.Na ninavyohisi kuna kila dalili kwamba bado wanaendelea na mahusiano yao kwa siri kwani walikuwa na mahusiano hata kipindi kile ambacho Patrick alikuwa na Vero.Hii nina maana Patrick hakuwa mwaminifu kwa mchumba wake.Alimsaliti Vero. Na kama aliweza kumsaliti Vero hatashindwa kufanya hivyo hata kwangu.Ouh My God..why always me ? akawaza Happy halafu akaanza kuzunguka zunguka mle chumbani.
“Ninampenda Patrick na nimejitolea kila kitu kwa ajili yake.Lazima nipambane nihakikishe kwamba Savanna hapati nafasi hiyo anayoitaka.Siwezi kukubali ndoto zangu nyingi na za muda mrefu za kuwa na Patrick zipotee hivi hivi.Nilipendana na Patrick kabla hajakutana na Savanna kwa hiyo Patrick ni wangu peke yangu.I’ve made so many sacrifices just to be with him,so I cant let all that be for nothing,I must fight” akawaza Happy halafu akachukua simu na kumpigia Pendo akamuomba amtengenezee juisi ya embe.Baada ya kumaliza kuongea na Pendo akazitafuta namba za simu za Savanna akataka kumpigia lakini akasita .Akavuta pumzi ndefu na kutafakari kwa sekunde kadhaa na mwishowe akakakata shauri
“Lazima nimpigie.Siwezi kumpa Savanna nafasi ya kumpata Patrick.” Akawaza Happy halafu akabonyeza kitufe cha kupigia simu na simu ikaanza kuita.
“Hallow Happy.habari yako?” akasema Savanna baada ya kupokea simu
“Habari yangu nzuri Savanna.” Akajibu Happy
“Happy mbona sauti yako inaonyesha kama vile hauko sawa? Una tatizo lolote Happy? Akauliza Savanna
“Savanna we need to talk” akasema Happy na kumstua kidogo Savanna
“To talk?
“yes Savanna”
“Talk about what?
“About what I’ve discovered today”
“Ok Happy ngoja niegeshe gari hapa pembeni tuongee vizuri.Nitakupigia baada ya muda mfupi” akasema Savanna na kukata simu
“Leo lazima nimeueleze ukweli na utakuwa mwisho wake kuisimamia kesi ya Patrick.Niko tayari hata kukodisha mawakili kumi lakini si kuwa na wakili mmoja aliyevaa ngozi ya kondoo kumbe ndani ni simba.”Akawaza Happy huku simu yake ikiwa mkononi akisubiri Savanna ampigie.Baada ya dakika tano simu yake ikaita.Alikuwa ni Savanna
“Happy tayari nimeegesha gari.Jambo gani unalotaka kunieleza?
“Savanna kuna jambo ambalo ninataka kulifahamu toka kwako.Wewe na Patrick mlifahamiana lini?
“Kwa nini unauliza hivyo Happy ?
“Just answer my question Savanna” akajibu Happy huku sauti yake ikionyesha kutokuwa na masihara.Kimya cha sekunde kadhaa kikapita halafu Savanna akajibu
“Mimi na Patrick tulikutana miaka kadhaa iliyopita,sikumbuki ilikuwa katika mazingira gani”
“Mahusnao yenu baada ya kukutana yalikuwaje?
“Happy mbona unauliza maswali ya namna hiyo? Kuna matatizo gani?
“Savanna naomba unijibu maswali yangu” akasema Happy
“Patrick ni rafiki yangu wa muda mrefu.” Akajibu Savanna kwa ufupi
“Savanna usinidanganye.Tayari ninaufahamu ukweli halisi kuhusu wewe na Patrick.”
“Mimi na Patrick ..!!!!” Savanna akastuka
“Ndiyo.wewe na Patrick”
“Unafahamu ukweli gani kuhusu mimi na Patrick? Akauliza Savanna
“Ninafahamu kila kitu”
“Kila kitu gani Happy?CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Wewe na Patrick mliwahi kuwa wapenzi na bado mnaendelea na mahusiano yenu kwa siri na lengo la wewe kuamua kujitolea kumtetea Patrick mahakamani ni moja ya malengo yako ya kutaka kurudiana tena na Patrick “
“ouh My gosh …!!!!” Savanna akastuka
“Umezipata wapi hito taarifa? Akauliza Savanna
“Sina haja ya kukwambia nimezipata wapi .Ninachotaka kujua toka kwako je ni kweli ? akauliza Happy
“Happy nisikilize vizuri sana mdogo wangu.Tuko katika wakati mgumu wa kuhakikisha kwamba Patrick anashinda kesi kwa maana hiyo haya mambo unayoniuliza hayana msingi wowote kwa sasa.Naomba tuyaache hadi hapo tutakapomaliza haya mambo ya mahakamani na ndipo tutapata muda mzuri wa kuulizana maswali kama hayo” akasema Savanna
“Savanna mambo haya hayana umuhimu kwako lakini kwangu mimi ni muhimu sana.Tafadhali naomba unijibu” akasema Happy
“Happy kwa nini hutaki kunielewa? Nimekwisha kwambia siko tayari kukujibu maswali yako ya kipuuzi kwa muda huu” akasema Savanna kwa sauti ya ukali kidogo
“Savanna wewe ndiye hutaki kunielewa.Nimekuuliza swali rahisi sana Kwa nini hutaki kunipa jibu?
“Nenda kwa aliyekupa taarifa hizo yeye ndiye atakaye kuthibitishia kama ni kweli au si kweli.Mimi sina muda huo wa kupoteza.Tena Happy ninakuomba kama huna jambo la maana la kuongea nami,tafadhali naomba usinipigie simu.Nina mambo mengi ya kushughulikia kesi uliyoisababisha wewe mwenyewe” akasema Savanna
“Savanna hapo ulipo katika kidole chako unayo ile pete uliyopewa na Patrick? Akauliza Happy.Savanna akavuta pumzi ndefu na kusema
“Ninayo”
“kwa nini alikupa pete hiyo? Na kwa nini hujawahi kuivua kidoleni mwako? Kitu kingine ni kwa nini umekorofishana na mumeo George baada ya kuanza kujihusisha na kesi ya Patrick?” akauliza Happy.Kikapita kimya cha sekunde kadhaa,Savanna akatamani kukata simu lakini akaamua andelee kuongea na Happy
“Happy unahitaji nini toka kwangu?
“Umekubaliana nami kwamba kila nilichokiongea hapa ni ukweli mtupu? Akasema Happy.Savanna akakasirika sana.
“Unahitaji kuujua ukweli,sasa ngoja nikwambie ukweli” akasema Savanna kwa hasira
“Ni kweli mimi na Patrick ni wapenzi.Unataka ukweli gani zaidi ya huo? akasema Savanna na kumpandisha hasira Happy
“Malaya mkubwa wewe.Siku zote hizi umekuwa ukijifanya ni mtu mwema kumbe una lako jambo.Nyoka mkubwa we” akafoka Happy
“Happy naomba usinitukane.Wewe ni binti mdogo sana wa kutukanana na mimi.Tena naomba iwe ni mara yako ya mwanzo na mwisho kuniita mimi Malaya.Una jeuri ya kuufungua mdomo wako na kunitukana sasa hivi wakati kwa uwezo wangu umekuwa huru?.Hivi sasa ulitakiwa uwe gerezani na mimi na Parick tungekuwa huru tunajinafasi kwa raha zetu.Happy narudia tena kukuonya kwamba kuwa makini na kauli zako.Mimi ni mtu mzuri sana lakini hubadilika na kuwa mbaya pale ninapokorofishwa.” Akasema Savanna kwa ukali
“Savanna naomba usinitishe.Kwa taarifa yako sikuogopi hata kid……………!!!!” Happy akastuka baada ya kumuona Pendo akiwa amesimama mlangoni akiwa na sura yenye mshangao na mkononi akiwa na glasi ya juisi.
“Kwa muda gani umekuwepo mlangoni? Happy akamuuliza Pendo
“Nimefika muda huu” akajibu Pendo
“Ok weka hiyo Juisi hapo mezani na uondoke” akasema Happy na pendo akatoka mle chumbani.
“Savanna,narudia tena kukwambia kwamba usitubutu tena kunitolea vitisho.Sikuogopi na huwezi kunifanya lolote.Nakuonya kuanzia sasa achana na hiyo kesi ya Patrick.Mimi nitagharamia kumtafuta wakili mpya wa kumtetea Patrick” akasema Happy na kumfanya Savanna acheke kwa dharau.
“Happy huna uwezo wa kuniamrisha mimi nisimtetee Patrick.Wewe ni mtu mdogo sana kwa Patrick.Kama huamini basi nenda kamweleze Patrick kwamba hutaki nijihusishe tena na kesi yake na usikie jibu atakalokupa na hapo ndipo utakapoamini kwamba wewe ni mtu mdogo sana kwake na huna nguvu wala uwezo wa kuamua chochote kuhusiana na maisha yake” akasema Savanna na kuzidi kumpandisha hasira Happy
“Savanna kama hutajitoa katika kesi hii hadi kesho ba………………..” Kabla Happy hajamaliza kusema alichotaka kukisema Savanna akamzuia.
“Utanifanya nini?
“Nitapambana nawe.Sintakubali unichukulie mpenzi wangu.Nitapambana nawe hadi mwisho.Patrick nimetoka naye mbali sana na sintaruhusu fisadi kama wewe kuyaingilia mapenzi yetu.” Akasema Happy kwa ukali
“Huna lolote la kunifanya Happy.Nakuonea huruma sana Happy hujui unachokiongea.Kuwa makini na kauli zako.Kama unajiona una uwezo wa kupambana na mimi nakuruhusu ujaribu..” akasema Savanna na kukata simu.Happy jasho lilikuwa linamtiririka.Mishipa ilikuwa imemtoka usoni kwa hasira alizokuwa nazo.
“Aaaaaggggghhhh..!!!!!!!!!!!!!!!!!!” akasema Happy kwa hasira na kuanza kutupa tupa vitu hovyo mle chumbani
“Savanna siwezi kukupa nafasi,nitapambana nawe kwa kila namna nitakayoweza.Siko tayari kumpoteza Patrick” akasema Happy kwa hasira huku machozi yakimtoka
* * * *
Zaidi ya dakika tano zimekwishakwenda tangu Savanna amalize kuongea na Happy simuni.Alikuwa ameegemea kiti chake akiwa na hasira kali.
“Bastard ..!!!!!!!” akasema Kwa ghadhabu huku akiipiga mikono yake katika usukani wa gari.
“Happy mbona anataka kukivuruga kichwa changu? Amefahamuje kama nilikuwa na mahusiano ya kimapenzi na Patrick?Amefahamuje kama nilikorofishana na George sababu ikiwa ni Patrick?Ameitaja hadi pete hii aliyonipa Patrick” Akawaza Savanna halafu akainua mkono wake wa kushoto akaitazama pete ya dhahabu yenye kung’aa iliyokuwa na maandishi P&S,akatabasamu
“Ni kweli pete hii tulipeana na Patrick ishara ya kupendana hadi kifo.Patrick ni kila kitu kwangu na sintamuacha kamwe” akawaza Savanna halafu akaibusu ile pete
“Nimepata jibu.taarifa hizi zote atakuwa amepewa na George.Ni yeye pekee anayefahamu kila kitu kuhusiana na kinachoendelea kati yangu na Patrick.Aliahidi kufanya kila linalowezekana ili kuhakikisha kamba mimi na Patrick hatuwi pamoja tena.Hata hivyo anajidanganya na hawezi kamwe kuizuia mipango yangu.Hata kama ikitokea bahati mbaya nikashindwa kufanikisha mipango yangu ya kuwa na Patrick tena,itakuwa vyema kama nitaishi maisha yangu yaliyobakia bila ya kuwa na mwenzi kuliko kuwa na mtu kama George.Nimekwisha mtoa katika akili yangu na juhudi zake zote za kutaka kuhakikisha kwamba anavuruga mipango yangu kwa matazamio ya kurudiana naye tena ,hazitazaa matunda.Tena ngoja nimuonye asijaribu kupambana na mimi” akawaza Savanna na kuzitafuta namba za George akapiga
“Hallow mpenzi wangu.habari yako.Missing you like crazy my angel…” akasema George mara tu alipopokea simu.Savanna akasonya kwa hasira
“Savanna my love usich………………” kabla hajaendelea Savanna akamkatisha
“Sikiliza George tena naomba unisikilize kwa makini.Sijakupigia simu kutaka kuusikiliza upuuzi wako.Ninataka kukueleza jambo moja tu.Hongera sana,juhudi zako nimeziona.Yote uliyomwambia Happy nimeyasikia.Pamoja na hayo naomba nikwambie kitu kimoja,stay away from me,far away from my life,forget that I exist.Naomba unifute kabisa katika akili yako na usitegemee kwamba siku moja mimi na wewe tutakuwa wapenzi .It’s over George.Huna nafasi tena kwangu.I don’t love you and I never loved you.Ni heri nikaolewa na shetani kuliko kuwa na mtu kama wewe” akasema Savanna
“Savanna..!!!” George akataka kutamka neno lakini Savanna akamzuia.
“Subiri nimalize George.” Akasema Savanna kwa ukali
“Ninakuonya George kwamba usijaribu kushindana na mimi .Kama unahitaji kunifahamu vizuri basi endelea kufuatilia maisha yangu.” Akafoka Savanna na kukata simu.
“Si George ,Happy wala mtu yeyote anayeweza kunizuia kuwa na Patrick.I’ll do everything ,I mean everything to be with Patrick again” akawaza Savanna na kuwasha gari akaendelea na safari yake
“Hii ni vita na inanibidi kupambana.Patrick ni mwanaume ninayempenda na nitahakikisha ninashinda vita hii ya kumgombania.Najua akili yake iko kwa Happy lakini nitafanya kila linalowezekana ili kuiharibu taswira ya Happy kichwani mwake.” Akawaza Savanna .
Mara tu alipomaliza kuongea na Savanna simuni,George akampigia simu Happy.Uso wake ulikuwa umejikunja kwa hasira.
“Hallo naongea na Happy ? akauliza George baada ya simu yake kupokelewa
“Ndiyo George.Happy hapa ninaongea’
“Happy umefanya nini? Kwa nini umemueleza Savanna yale mambo niliyokueleza? Tulikubaliana iwe ni siri yetu mimi na wewe.Kwa nini umekiuka makubaliano yetu? Akasema George kwa ukali
“George nimeshindwa kuvumilia.Patrick ni mtu wangu na nimeshindwa kuvumilia kuona kuna mtu mwingine akiwa katika jitihada za kutaka kumchukua.Nimeamua kumueleza ukweli Savanna ili aachane kabisa na mipango yake.” Akasema Happy
“Happy umekosea sana.Umefanya kosa kubwa sana.Umeharibu kila kitu.Umeniharibia kabisa mimi .Savanna ndiye mwanamke ninayempenda kuliko wote na kwa maneno uliyomwambia umezidi kumuweka mbali nami zaidi.Sikutegemea kama ungeweza kufanya jambo la kijinga kama hili…Unadhani kwa kumweleza ukweli Savanna utamzuia aachane na Patrick? Unajidanganya Happy umezidi kujiweka katika sehemu mbaya na usipoangalia hata huyo Patrick utabaki unamsikia tu.Kwa nini ukakurupuka bila kuuliza Happy???Nilikuona ni mtu mwenye akili kumbe ni mjinga kiasi hiki…..”
Happy hakumpa nafasi George ya kuendelea kuongea akakata simu.
“ Stupid !!!....” akasema kwa hasira
“Its gonna take a lot to drag me away from you.
There ‘s nothing that 100 men or more could ever do
Just like the rain down in Africa
Its gonna take some time but I know you’re worth fighting for
I’d fight for you
Eh ba bam ba eh eh ba bam baeh
I’d fight for you
Eh ba bam ba eh eh ba bam ba eh
I’ d fight for you
Let’s go
Friends are coolCHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
But we both know
They don’t wanna see us together
Don’t wanna lose what I live for
I’m with willing to do whatever
Cause I don’t wanna see you cry
Give our love another chance
I bet we get it right this time
As long as youre prepared to fight,prepared to fight
I don’t wanna live another day
Without your body next to me
I’m not gonna let them break us down
Cause baby I know now,know now
If you got someone that’s worth fighting for .let no body hold you down.
Let me hear say whoa—oh – oh--oh
And if you you found someone that’s worth dying for
The one you cant live without
let me hear say whoa –oh—whoa
Wimbo huu ulioimbwa na Jason De Rulo ndio uliokuwa ukisika chumbani kwa Happy asubuhi hii..Kuonyesha ni namna gani wimbo ule ulivyokuwa umemgusa Happy alikuwa akiimba akienda sambamba na mashairi haya yenye ujumbe mzito.
Saa ya ukutani ilionyesha ni saa mbili na dakika kumi na nane za asubuhi.Happy bado alikuwa mbele ya kioo kikubwa cha meza yake iliyosheheni vipodozi vya kila aina.Siku hii ya leo alidamka mapema sana na aliutumia muda mrefu katika kujiandaa.Baada ya kuhakikisha kwamba amejipodoa vya kutosha akaenda katika kioo kikubwa cha kujitazamia mwili mzima ,akajitazama na kutabasamu
“Sipendi kujisifu lakini mimi ni mzuri.Yule Kunguru Savanna,hafikii hata robo ya uzuri wangu.” Akawaza Happy huku akiendelea kujitazama katika kioo.Siku hii ya leo alikuwa amevaa suruali ya jeans ya rangi nyeupe iliyomkaa vyema aliyoiambatanisha na shati jeupe lenye nakshi za kuvutia.Chini alivaa viatu virefu vyeupe.Hakika kama ungefanikiwa kumuona Happy siku hii ya leo ungekubali kwamba alistahili kuwa mrembo wa Taifa.
Akiwa katika harakati za kutaka kutoka mle chumbani mara mlango wa chumba chake ukafunguliwa na akaingia mama yake.
“Wow ! mama .!Shikamoo.”
“Marahaba mwanangu ,unaendeleaje?
“Ninaendelea vizuri mama”.
“Happy una haraka sana?
“Ndiyo mama..kuna tatizo lolote?
“Kuna jambo nilitaka kuongea nawe”
“Mama kuna mahala ninawahi lakini nitarejea baada ya muda mfupi. Tutakuja kuongea nikirudi mama” akasema Happy na kuchukua mkoba wake mweupe na kutoka mle chumbani akaingia katika gari lake na kuondoka.Hakutaka kumueleza mtu yeyote alikokuwa anaelekea.
“Its gonna take a lot to drag me away from you.
There‘s nothing that 100 men or more could ever do
Just like the rain down in Africa
Its gonna take some time but I know you’re worth fighting for”
Mashairi ya wimbo huu alioupenda Happy yalimfanya atikise kichwa huku akifuatilizia na kuimba taratibu.Alikuwa akiutumia mkono wake wa kushoto kuendesha gari huku mkono wake wa kulia akiwa ameuegemeza dirishani.Alikuwa analivuka daraja la kigamboni kuelekea Uwangwa prison kuonana na Patrick
“Nimewahi sana leo.Natumai muda huu Savanna bado hajafika.Naomba Mungu iwe hivyo na mimi nifike kabla yake.Nataka atakapofika akute tayari nimekwisha ongea na Patrick na kuanzia leo asimame kuisimamia kesi ya Parick.Ni Patrick pekee mwenye uwezo wa kumsimamisha Savanna asiendelee kumtetea.Nina imani atakubaliana na hoja zangu kwa sababu mimi ndiye mwanamke pekee anayenipenda na nimejaa katika akili yake.Nitakuwa tayari kulipa kiasi chochote cha pesa kwa wakili mwingine ili aendelee kumtetea Patrick mahakamani na si Savanna.” Akawaza Happy huku gari likienda kwa kasi kubwa.
Saa nne kasoro dakika saba ilimkuta Happy katika gereza la Uwangwa.Alisalimiana na askari kadhaa waliokuwepo mapokezi.Tayari walikwisha anza kumfahamu hivyo alishughulikiwa haraka haraka kukamilisha taratibu za kuonana na mahabusu wake .Siku hii ya leo alimkuta askari mmoja aliyemsaidia na kumpeleka katika sehemu ya tofauti na ile iliyozoeleka ambayo hutumiwa na kila mtu ajaye kumuona mahabusu.Sehemu hii aliyopelekwa Happy ilikuwa nzuri na ilifaa hata kwa maongezi ya faragha.Baada ya dakika kama kumi hivi Patrick akaletwa na alipogonganisha macho yake na Happy akaachia tabasamu kubwa.
“Ouh my angel..!!!” akasema Patrick
“Patrick..!!!” akasema Happy kwa furaha huku akiinuka kitini na kumkumbatia.
“Mama una dakika thelathini za kuongea na mtu wako” akasema askari aliyekuwa ameambatana na Patrick
“Ahsante sana” akasema Happy kisha akakumbatiana na Patrick.
“Nimefurahi sana kukuona malaika wangu” akasema Patrick kwa furaha halafu akaipeleka mikono yake yote miwili kichwani kwa Happy wakaangaliana kwa sekunde kadhaa halafu wakapeana busu zito na kukumbatiana tena
“Ouh my angel,I was dying to see you” akasema Patrick huku akiketi kitini.
“Patrick my love,before coming here I felt like I was dead but now I feel alive “ akasema Happy
“Ouh Happy usihofu kitu malaika wangu.Mimi ni mzima ninaendelea vizuri sana.Nitashinda hii kesi na nitakuwa huru tena” akasema Patrick
Happy akatabasamu na kuufungua mfuko aliokuwa amekuja nao uliokuwa umesheheni vitu mbali mbali alivyokuwa amemchukulia mpenzi wake.
“Ahsante sana mpenzi wangu kwa kunijali” akasema Patrick.Happy hakujibu kitu akatabasamu.Kimya kifupi kikapita wakati Patrick akiendelea kunywa juisi aliyoletewa na Happy
“Jana ulifika mahakamani? Akauliza Patrick
“Ndiyo nilifika na nilikuwamo katika chumba cha mashtaka .Usingeweza kuniona kwa sababu nilikuwa nimekaa mwisho kabisa.Hata hivyo nilitoka wakati wanasheria wakivutana baada ya kugundua kwamba kuna watu walikuwa wakinitazama vibaya sana.Nahisi watakuwa ni ndugu zako au wa Vero.Sikutaka kuwakwaza ikanilazimu kutoka nje.” Akasema Happy
“Pole sana Happy.Najua kwa wakati huu baadhi ya ndugu zangu na familia nzima hawatakuangalia kwa jicho zuri wakiamini kwamba wewe ndiye chanzo cha haya yoye.Kaza moyo na usiwajali .Elekeza akili yako katika ndoto yetu ya kuwa pamoja.Kesi hii nitashinda na nitakuwa huru na ndoto yetu ya siku nyingi ya kuwa pamoja itatimia.Ninamuamini Savanna,ana uwezo na uzoefu mkubwa katika kusimamia kesi kama hizi na amenihakikishia kwamba lazima atashinda kesi hii” akasema Patrick .Happy aliposikia jina la Savanna likitajwa na kumwagiwa sifa akabadilika ghafla na kuinama chini.Patrick akaendelea kunywa juisi .
“Patrick..!!” akaita Happy
“Yes my angel “ akaitika Patrick.Happy akamtazama usoni kwa sekunde kadhaa na kusema
“Umefahamiana lini na Savanna?
“Savanna ni rafiki yangu wa muda mrefu.Tumefahamiana miaka mingi iliyopita”
“Ouh Okk.! “ akajibu Happy.Patrick akamuangalia Happy usoni na kugundua Hakuwa sawa.
“Happy kuna kitu gani kinakusumbua leo mpenzi wangu? Nakuona kama hauko sawa.Halafu kwa nini umeniuliza kuhusiana na Savanna?
“Usihofu Patrick.Mimi niko sawa kabisa na sina tatizo lolote.Nilihitaji tu kumfahamu Savanna vizuri”
“Happy whats going on? Akauliza Patrick.Happy akainama chini kwa sekunde kadhaa na kisha akainua kichwa na kusema
“Patrick I know you love me”
“Yes I I love you so much”
“As much as you love me you’ll never lie to me” akasema Happy na kuzidi kumshangaza Patrick
“Happy una tatizo gani leo? Akauliza Patrick
“Patrick wewe na Savanna mmewahi kuwa wapenzi? Akauliza Happy.Patrick aliyekuwa ameshika boksi la juisi akastuka na kuliweka mezani akamtazama Happy
“Happy are you ok today?
“I’m ok Patrick.Just answer my question” Patrick akaendelea kumtazama Happy halafu akasema
“Hapana .Mimi na Savanna ni marafiki na hatujawahi kuwa wapenzi”.
Patrick akavuta pumzi ndefu baada ya kumpa Happy jibu lile.Kimya cha sekunde kadhaa kikapita wakabaki wanatazamana.
“Are you sure Patrick?
“Yes I’m sure.Happy kuna kitu gani kinakusumbua leo?
Happy akatoa kitambaa na kujifuta jasho.
“I know down deep in your heart you know exactly that you are lying to me.” Akasema Happy.Patrick akahisi kuchanganyikiwa.
“Happy nimekwambia ukweli mtupu na siwezi kukudanganya malaika wangu”
“Patrick muda niliopewa ni mdogo sana na si lengo langu kuanza kubishana nawe.Ninaomba tu ufahamu kwamba ninaufahamu ukweli wote kwamba wewe na Savanna mliwahi kuwa wapenzi wakati ukiwa na Veronika na mlitengana baada ya Savanna kumpata bwana aitwaye George.Is that true? Akasema Happy.Patrick midomo ilikuwa inamtetemeka.
“Unakumbuka tukiwa Arusha niliwahi kukuhoji kuhusu yale maneno P&S yaliyoko katika pete yako na ukaniambia kwamba hayana maana yoyote? Ukweli ni kwamba maneno yale yanamaanisha Patrick na Savan.Maneno haya yapo pia katika pete na mkufu wa Savanna.” Akasema Happy.Patrick jasho lilikuwa linamtoka
“Savanna bado anakupenda sana na kwa taarifa yako ana mpango wa kuitumia kesi hii kuwa chanzo cha wewe na yeye kurudiana na kuwa wapenzi tena na ndiyo maana amejitolea hata kuifanya kazi hii ya uwakili bure kabisa.Hii ni sababu iliyosababisha aachane na mumewe akiamini kwamba atarudiana na wewe”
Patrick jasho liliendelea kumtiririka.Happy akainuka ,akamfuta jasho kwa kitambaa chake.
“Happy mambo haya yote umeyatoa wapi? Nani aliy………………..” akataka kuuliza Patrick lakini Happy akamzuia
“Patrick hakuna haja ya kuanza kupoteza muda wa kuelezana mambo haya nimeyajua vipi.Kitu pekee ambacho unapaswa kukifahamu na kukizingatia ni kwamba wewe ndiye maisha yangu ,furaha yangu,pumzi yangu na kila kitu changu.Ninakupenda Patrick zaidi ya ninavyoweza kueleza.Usihofu kuhusu haya niliyokueleza,nilitaka tu ufahamu kwamba ulifanya kosa kuwa na mahusiano ya siri wakati ukiwa na Veronika.Sina hakika kama unaweza ukanifanyia mimi jambo kama hilo kwa sababu endapo nikigundua kwamba una mahusiano nje ya uhusiano wetu ,Patrick I swer I‘m gonna kill you and kill myself.You are mine alone.Anyway tuachane na hayo ni mambo yaliyopita na hayana nafasi kwa sasa.Ila kuna jambo moja ninaloliomba toka kwako”
“Jambo gani hilo Happy?
“I want Savanna out of this case.”
Patrick alihisi kama kuishiwa nguvu ,akabaki anamtazama Happy asijue aseme nini.
“Happy…..!!” Patrick akataka kusema kitu lakini Happy akamzuia
“Patrick you are my angel,my everything.Uko hapa ndani kwa sababu yangu,kwa sababu ya upendo wako kwangu.Patrick hicho ni kitu pekee ninachokuomba mpenzi wangu.Nataka Savanna aachane kabisa na kesi hii .Mimi niko tayari kumtafuta wakili mwingine mahiri ambaye ataendelea kukutetea mahakamani lakini si Savanna.Siko tayari kukupoteza Patrick.” akasema Happy.Patrick akainama akatafakari na kusema
“Happy napenda nichukue nafasi hii kwanza kukuomba msamaha kwanza kwa kusema uongo pale uliponiuliza kama niliwahi kuwa na mahusiano na Savanna.Ni kweli niliwahi kuwa na mahusiano na Savanna lakini tulisitisha mahusiano yetu pale yeye alipompata George.Toka wakati huo tumeendelea kuwa marafiki wa kawaida.Tumekuwa tukisaidiana katika mambo mengi na ndiyo maana hata katika kesi hii Savanna ananisimamia kama rafiki na mtu wake wa karibu na si kama mpenzi wake.Savanna ni mwanasheria aliyebobea na mzoefu katika kesi kubwa kama hizi.Amekuwa akisimamamia kesi kubwa kubwa na hajawahi kushindwa.Tafadhali nakuomba uniamini Happy kwamba hakuna kinachoendelea kati yangu na Savanna kwa sasa zaidi ya urafiki wa kawaida.Nakuomba Savanna uniamini kwamba ni Savanna pekee ambaye anaweza kuniweka huru.Naomba tusimuondoe katika kesi hii” akasema Patrick kwa sauti ndogo
“Patrick nakuelewa na sina tatizo na uwezo wa Savanna..Najua unamuamini sana na ni wakili mzoefu na mbobezi wa sheria.Ninachotaka kukiepuka mimi ni kupigana vita ya pili kati yangu na Savanna.Wewe ni mwanaume wangu wa pekee na niko tayari kufanya jambo lolote lile kwa ajili yako na ndiyo maana nimeamua kuachana na kila kitu kwa ajili yako kwa hiyo atakapotokea mwanamke ambaye atatishia usalama wa penzi langu nawe lazima nipambane naye.Sitaki kupambana na Savanna na ndiyo maana ninataka umuondoe katika kesi hii.Mimi niko tayari kulipa gharama za wakili hata zaidi ya mmoja.Najua Savanna anakupenda na yeye atafanya kila linalowezekana ili aweze kunitenganisha nawe.tafadhali Patrick naomba unikubalie jambo hili moja tu.” Akasema Happy
“ Happy nimekuelewa unachokisema na mimi niko radhi kufanya chochote kile kwa ajili yako na ndiyo maana niko hapa gerezani muda huu.Pamoja na yote uliyonieleza bado sijaona sababu ya msingi yakumuondoa Savanna katika kesi yangu.Naomba Happy muache Savanna aendelee kunisimamia mahakamani”
“Patrick umejitolea kuibeba adhabu yangu kwa sababu ya upendo wako mkubwa kwangu.Sina cha kuweza kukulipa kulingana na thamani ya upendo wako kwangu.Please Patrick allow me to do at least one thing for you.Allow me to hire another lawyer for you to replace Savanna.” Happy akaendelea kusisitiza
“Happy najitahidi sana kupingana na nafsi yangu kuhusiana na suala hilo unalolitaka.Najitahidi kutaka kukubaliana nawe lakini bado moyo wangu unakataa kabisa.Najua una lengo zuri la kutaka kunisaidia lakini sina hakika kama uamuzi wa kumuondoa Savanna ni uamuzi unaofaa kwa sasa.Nahitaji kutoka humu gerezani,nahitaji kushinda kesi ili niwezi kuitimiza ndoto yangu ya kuwa nawe na hilo litawezekana tu kama Savanna ataendelea kuisimamia kesi hii.Endapo tutaamua vinginevyo basi ndoto zangu zote za kuwa nawe zitapotea kwa sababu nitapotelea gerezani”
“Patrick huwezi kupotelea gerezani.I give you my word.Nitamtafuta wakili mahiri kabisa na hata zaidi ya mmoja kama itahitajika.” Happy akaendelea kuusimamia msimamo wake bila kutetereka.Patrick akainama akafikiri kidogo na kusema
“Happy hilo ni jambo lisilowezekana hata kidogo.” Happy machozi yakamlenga
“You are still in love with her,right? Akauliza Happy
“Si hivyo unavyofikiri Happy “
“Nijibu Patrick.Bado unampenda Savanna? Kwa sababu yake hauko tayari hata kunisikiliza mimi mpenzi wako” akasema Happy huku machozi yakimtoka na mara mlango ukafunguliwa na wote wakapigwa na butwaa baada ya kumuona mtu aliyesimama mlangoni.Alikuwa ni Savanna.Nyuma yake alikuwepo Andrew ,rafiki mkubwa wa Patrick ,Alois kaka wa Patrick aliyeongozana na mke wake na pamoja nao alikuwepo mama yake Patrick.
Happy akahisi mwili wote unamtetemeka.Akakosa neno la kusema.Savanna akawaongoza watu aliokuja nao wakaingia mle chumbani.Mama yake Patrick nusura aanguke kwa mstuko baada ya kuingia mle chumbani na kugonganisha macho yake na Happy
“Wewe ..!!!” akasema kwa sauti yenye mshangao.Hakuwa ametegemea kama angekutana na Happy mahala pale.Happy alikuwa anatetemeka kwa woga namna alivyokuwa anaangaliwa kwa jicho la chuki.
“Shikam…….” Happy akataka kumsalimu mama yake Patrick lakini kabla hajamaliza salamu yake akazuiwa.CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Haraka sana toka nje” akasema kwa ukali mama yake Patrick.
“Mama ..!!! Patrick akataka kusema jambo lakini naye akazuiwa
Kwa Haraka Happy akauchukua mkoba wake uliokuwa kitini .Machozi yalikuwa yanamtoka akaanza kupiga hatua kuondoka.
“Na iwe ni mara ya mwanzo na ya mwisho kufika hapa.Sitaki kukuona tena karibu na mwanangu shetani wewe.Kila mara unapokaa karibu na mwanangu lazima jambo baya limfike.Una laana wewe mtoto na ndiyo maana mambo mabaya yanakukuta kila wakati.” Akasema kwa ukali mama yake Patrick
“Basi mama imetosha.Usiongee sana utasababisha matatizo mengine” akasema Alois
“Na wewe Patrick naomba ukae mbali kabisa na huyu mwanamke.Sitaki kuona ukiwa karibu naye.Yeye ndiye chanzo cha haya matatizo yote” Akaendelea kufoka mama yake Patrick.
“Patrick nimekuletea wageni” akasema Savanna baada ya hali kutulia mle chumbani
Patrick akasalimiana na mama yake pamoja na ndugu zake.Waliongea mambo mengi na kumpa moyo kuhusiana na kesi inayomkabili.Baada ya maongezi yao yaliyochukua zaidi ya nusu saa wakaaga na kuondoka.Ni Savanna pekee aliyebaki.
“Patrick unajisikiaje leo kwa kuonana tena na ndugu zako na hasa mama? Akauliza Savanna
“Nimefurahi sana kuonana nao tena,nimefarijika sana.Ahsante Savanna kwa kuwaleta.Pamoja na ujio wao lakini bado kichwa changu hakiko sawa” akasema Patrick.Savanna akamuangalia kwa makini na kusema
“Its because of her,right? Amekwambia nini Happy?
Patrick akafikiri kidogo na kusema
“Tayari anafahamu kwamba mimi na wewe tuliwahi kuwa na mahusiano ya kimapenzi.”
“Hata mimi alinipigia simu jana na kunieleza kuhusu suala hilo na sikuweza kukataa kwa sababu alikwisha elezwa kila kitu na George.Happy alinitukana sana na kusema kwamba atahakikisha ninaondolewa katika kesi yako.Nadhani hilo ni jambo mojawapo lililomleta kwako asubuhi hii.She wanted me out,right?
“Ni kweli Savanna.Happy alinitaka nikuondoe katika kesi yangu na nitafute mawakili wengine”
“wewe umemjibu nini?
“Siwezi kufanya jambo la kipuuzi kama hilo.” Akasema Patrick
“Kwa nini hujamsikiliza mpenzi wako Patrick.Kwa nini hujamtimizia alichokuomba? Akauliza Savanna
“kwa sababu nakuamini Savanna.Umejitolea kunitetea na ninaamini kwamba nitashinda kesi.Hakuna mtu anayeweza kunishauri nikutoe katika kesi hii.”
Savanna akatabasamu baada ya kauli ile ya Patrick.
“Nilikwambia Happy,mipango yako kamwe haitaweza kufanikiwa.Nilikuonya kwamba Patrick hawezi akakusikiliza .Na huu ni mwanzo tu.Ulitaka mapambano na mimi na sasa utaiona nguvu yangu “ akawaza Savanna
“So is that true? akauliza Patrick
“Is what true?
“kwamba umeachana na George.
“Yah..its true.” Savanna akajibu
“Samahani Patrick kwa kutokufahamisha kuhusu jambo hili kwa sababu halikuwa na umuhimu wowote”
“Sababu gani iliyopelekea mkaachana? Akauliza Patrick
“George alinitaka niachane na kesi yako.Aliogopa kwamba kesi hii ingeweza kutuweka karibu muda mwingi kwa hiyo akahofu kwamba pengine tunaweza kujikuta tukirejesha mahusiano yetu ya zamani.Sikuwa tayari kuachana na kesi yako kama alivyotaka George kwa hiyo tukaachana.Patrick niko tayari hata kutengana na dunia nzima lakini si kukuacha katika kipindi hiki kigumu.Hakuna mtu yeyote chini ya jua zaidi yako wewe mwenyewe anayeweza kunizuia nisikutetee.” Akasema Savanna
“Ahsante sana Savanna kwa kunithamini namna hii.Sina kitu cha kukulipa kwa wema wako huu mkubwa.Tafadhali fanya kila linalowezekana ili uweze kuniondoa katika kesi hii”
“Patrick usihofu.Nitafanya kila linalowezekana na kukuweka huru.naomba uniamini.I’ll fight till you get free.I give you my word” akasema Savanna na kumfanya Patrick atabasamu
“Ahsante sana Savanna” akasema Patrick
Ilimchukua Happy zaidi ya dakika kumi kutulia na kuwasha gari.Mikono yake ilikuwa inamtetemeka. Kitambaa chake cha mkononi kilikuwa kimeloa machozi.Hatimaye akawasha gari na kuondoka maeneo yale ya mahakamani.
“Na iwe ni mara ya mwanzo na ya mwisho kufika hapa.Sitaki kukuona tena karibu na mwanangu shetani wewe.Kila mara unapokaa karibu na mwanangu lazima jambo baya limfike.Una laana wewe mtoto na ndiyo maana mambo mabaya yanakukuta kila wakati”
Maneno haya ya mama yake Patrick,yalikuwa yanajirudia kichwani kwa Happy na kumfanya aangushe machozi huku akiendesha gari.
“Kwa mara ya kwanza ninajuta ni kwa nini nilionana tena na Patrick.Nadhani ingekuwa vyema kama Patrick asingejitokeza tena katika maisha yangu.Nilikuwa na maisha yangu mazuri na yenye furaha na Mike.Sikutegema hata siku moja kama siku moja ningekuja kuwa na wakati mgumu namna hii.Toka nilipoonana na Patrick maisha yangu yamebadilika ghafla.Ndoto zangu zote za maisha nilizokuwa nazo zimepotea.Mateso na maumivu ya moyo hayaishi.Nimekuwa ni mtu wa kulia kila siku.maisha yangu yamepoteza mwelekeo” akawaza Happy huku akipunguza mwendo wa gari na kufuta machozi
“Una laana wewe mtoto na ndiyo maana mambo mabaya yanakukuta kila wakati.”
Maneno ya mama yake Patrick yakazidi kujirudia kichwani mwa Happy
“Inawezekana ni kweli nina laana na ndiyo maana mambo yangu hayafanikiwa.lakini ni kwa nini hunikuta nikiwa na Patrick pekee? Miaka hii yote niliyokuwa na Mike sijawahi kuangusha hata chozi”.Happy akajiuliza na kushindwa kupata jibu.Sura ya mama yake Patrick akimtazama kwa macho makali yaliyojaa chuki ikamjia kichwani.
“Kila nikiikumbuka sura ya Yule mama mwili unatetemeka.Macho yake yalionyesha dhahiri ni namna gani anavyonichukia.Nimeogopa sana na sijui nitawezaje tena kuonana na Patrick .Kwa sasa itanibidi nijitahidi kwa kila namna nitakavyoweza kuikwepa familia ya Patrick kwani kwao mimi ni adui wao namba moja” Happy alikuwa amezama katika mawazo mazito.Alikuwa analivuka daraja la Kigamboni.
Wakati akiendelea na safari yake huku kichwa chake kikiwa kizito kwa mawazo mengi aliyokuwa nayo,mita kama mia moja hivi nyuma yake gari mbili zilikuwa zinakuja kwa kasi.Gari zile zilionekana kana kwamba zilikuwa zinafukuzana.Happy aliziangalia kupitia kioo cha pembeni lakini hakuzitilia maanani.Gari zile zikafika usawa wa gari la Happy na zote mbili zikawa kama zinataka kupishana kwa wakati mmoja.Gari lililotaka kupitwa likasogea karibu sana na gari la Happy kitendo kilichomstua na kabla hajafanya chochote gari lake likakwaruzwa ubavuni.Happy akataharuki na kufunga breki ya ghafla .Kwa bahati nzuri hakuwa katika mwendo mkali.Gari lililomkwaruza ubavuni nalo likasimama mbele yake.Happy akashuka kwa hasira na kutazama gari lake lilivyokwaruzwa.Kwa hasira akaelekea katika gari lililomkwaruza ambalo lilisimama mita chache toka aliposimamisha gari lake.Milango ya gari lile ikafunguliwa na wakashuka watu watatu mwanadada mmoja na wanaume wawili.
“You people don’t you know how to drive?? !!....” akafoka Happy
“Samahani sana dada.Hatukutegemea kama tungeweza kukukwaruza.Nilikuwa najaribu kumkwepa Yule jamaa” akasema mmoja wa wale jamaa huku akimuelekezea jamaa mmoja aliyevaa suruali nyeusi na fulana nyeupe aliyekuwa akiwaelekea
“Nasema hivi,sitaki kesi wala mjadala wowote.Nahitaji gari langu likatengenezwe.” Akaendelea kufoka Happy
“Usihofu madam,wenye makosa ni sisi na tunaomba tugharamie matengenezo ya gari lako na hata kukupatia gari lingine la kutembelea wakati gari lako linatengezwa mahala lilipokwaruzwa”
“Nimesema sihitaji kitu chochote ninachotaka ni gari langu litengenezwe haraka sana” akaendelea kufoka Happy Muda huo huo jamaa mmoja mnene akiongozana na vijana wawili akafika eneo la tukio”
“Dada samahani sana kwa tatizo lililotokea,naomba tusipoteze wakati,tuelekee gereji gari lako likatengenezwe” akasema yula jamaa mnene.Happy akaanza kupiga hatua kurejea katika gari lake lakini Yule jamaa akamzuia
“Hapana panda gari hili” Happy akageuka kwa hasira .Hakuamini macho yake kwa alichokiona.Alikuwa anatazamana na midomo miwili ya bastora.Kijasho kikamtoka,mwili mzima ukamtetemeka.
“Taratibu bila ubishi ingia ndani ya gari hili.Usitulazimishe tutumie nguvu” akaamuru Yule jamaa.Huku akitetemeka Happy akajikaza na kuuliza
“What’s going on here? What’s the meaning of this?
“Get in the car ,now !! akafoka Yule jamaa mnene.Bado miguu ya Happy ilikuwa mizito sana kunyanyuka.Hakuamini kilichotokea aliona ni kama njozi.
Kwa haraka mwanadada aliyekuwa ameongozana na watu wale akamfuata Happy na kumnong’oneza kitu sikioni halafu akamshika mkono na kumuingiza katika gari lile aliloamriwa kupanda.Haraka haraka wakarejea katika magari yao na kijana mmoja akaenda katika gari la Happy.Magari yakawashwa na kuondoka eneo lile.Kitendo kile hakikuchukua zaidi ya dakika kumi.
* * * *
Ilikuwa ni mara yake ya kwanza kuwaona watu wale waliokuwamo garini.Hakuwafahamu na wala hakufahamu lengo la wao kumtaka aongozane nao.Mapigo ya moyo wake yalikuwa yanaenda kwa kasi ya ajabu na jasho jingi lilimtiririka na kuloanisha shati lake jepesi.
“Mungu wangu mambo gani haya yananitokea tena ? Watu hawa ni akina nani na wanataka nini kwangu? Happy akawaza huku machozi yakimtoka.
“Jamani mnanipeleka wapi? Naombeni msinidhuru tafadhali.Nitawapa kiasi chochote cha pesa mtakachokihitaji” Akalia Happy
“Shut up !!! akafoka jamaa aliyekuwa amekaa pembeni yake.Happy alikuwa amewekwa kati kati ,mikononi alifungwa pingu.Gari lilikuwa linakwenda kwa kasi kubwa na kabla ya kulimaliza daraja la kigamboni jamaa mmoja aliyekuwa amekaa mbele pembeni ya dereva akapokea simu na kuongea kwa takribani dakika mbili halafu akawageukia wale waliokuwa wamekaa kiti cha nyuma ,akawafanyia ishara Fulani na kwa haraka wale jamaa wakamfunga Happy kitamba cheusi usoni na hakuweza kuona chochote tena.Bado aliendelea kulia akiomba aachiwe huru lakini hakuna mtu hata mmoja aliyemjali na kumsikiliza.gari lilianza kukata mitaa ya jiji .Happy hakuweza kutambua ni wapi walikokuwa wanaelekea .
Katika gari iliyokuwa imetangulia mbele,kijana mmoja mwembamba mrefu alikuwa anatabasamu kwa furaha wakati akiongea na simu.Alipomaliza kuzungumza na simu akamgeukia dereva wake
“Sasa ngoja nimpigie simu Loniki nimtaarifu kwamba mtu wake tayari tumekwisha mtia mikononi.” Akasema na kuzitafuta namba za simu la Loniki na kumpigia
“Hallow Khumalo” akasema Loniki baada ya kupokea simu
“Hallo Loniki ,habari yako.Uko wapi mida hii?
“Kwa sasa niko saluni natengeneza kucha”
“Lonny nimekupigia simu kukutaarifu kwamba Happy tayari tumemtia mikononi mwetu na hivi sasa tunaelekea mahala kazi itakapofanyikia.Nitakutaarifu baadae ni wapi tumempeleka ili ushuhudie namna atakavyofanyiwa”
“Wow !! that’s wonderful.Thats good news” akasema Loniki kwa furaha
“One more thing lonny,hatutakiwi kumuweka mafichoni kwa muda mrefu sana.Kila kitu kinatakiwa kifanyike usiku wa leo na halafu tumuache huru.Ukumbuke vile vile kuja na kiasi cha pesa kilichobakia.Jambo la mwisho vijana wanataka uwaongeze shilingi million ishirini ili waweze kuendelea kutoa ushirikiano katika kazi iliyobaki.Kwa kweli vijana wamefanya kazi kubwa na ya kitaalamu sana kiasi kwamba tumemchukua Happy bila ya rabsha wala mtu yeyote kugundua kwa maana hiyo basi vijana wanahitaji motisha ili waendelee kuwa na ari ya kazi.”
“Twenty million more …!!!!???. Loniki akastuka
“yes Lonny vijana wanataka uwaongeze kiasi hicho”
“Khumalo hatukupatana hivyo na wala hatukukubaliana kuongeza kiasi chochote cha pesa zaidi ya kile cha million hamsini tulichopatana.Hizo million ishirini unazozisema nitazipata wapi sasa hivi? Its a lot of money” akasema Loniki
“Sikiliza Lonny.tusiendelee kubishana kuhusu suala hilo.Ulitupa kazi ya kufanya tumekwisha ifanya tayari lakini kutokana na ugumu wa kazi yenyewe vijana wanataka uwaongeze kiasi hicho cha pesa ili kazi yako ikamilike.Najua hauko tayari kuona kazi hii kubwa ikiharibika,kwa hiyo jitahidi upate kiasi hicho cha pesa na tutakapoonana jioni ya leo utukabidhi.”
“Khumalo that’s unfair” akasema Loniki
“Lonny find that money.Mpaka jioni ya leo kama hutakuwa umezipata ,nitamuachia Happy” akasema Khumalo na kukata simu.Uso wake ukapambwa na tabasamu kubwa.Bado akiwa na simu yake mkononi akazitafuta namba za Linah na kumpigia
“Hallow Linah” akasema Khumalo
“Khumalo vipi maendeleo?
“Kila kitu kinakwenda vizuri.Tayari Happy tunaye na kwa sasa tunampeleka mafichoni.Nimempigia simu Lonny na kumwambia kwamba aongeze milioni ishirini na kama akishindwa kuzipata fedha hizo hadi jioni ya leo basi nitamuachia Happy.Nina uhakika atakupigia simu , na kama akifanya hivyo na wewe endelea kumsisititiza ili aweze kuzitafuta hizo fedha.”
“Good job Khumalo.Its time now to make easy money.Kama nilivyokwambia kwamba Lonny ana pesa na nina hakika mpaka jioni ya leo atakuwa amezipata hizo fedha.Hakukuwa na tatizo lolote wakati wa kumkamata Happy?
“Hapana Linah.Tulimchukua kirahisi mno na ni tukio ambalo lilichukua chini ya dakika kumi na hakuna nguvu iliyotumika zaidi ya gari lake kupata mikwaruzo kidogo”
“Vizuri sana khumalo.Nitakuja jioni na Lonny”
“Sawa Linah .Nitamtuma kijana ambaye atakuja kuwachukua jioni na kuwaleta mahala tutakapompeleka Happy”
“Ok Khumalo.Lakini naomba msimuumize Happy.Namuonea huruma sana huyo binti hana kosa lolote”
“Usijali kuhusu hilo.Hakuna mtu atakayempiga hata kofi moja.Atapatiwa kila kitu na hata mimi mwenywe sijisikii vizuri kwa kitendo hiki lakini kwa kuwa kazi hii ina hela nzuri imenilazimu kuifanya tu.See you later Linah.” Akasema Khumalo na kukata simu
“hahahaaaaa..!!! thats why I love Dar es salaam.Its easy to make money in here” akasema Khumalo nakuendelea kucheka halafu akatoa sigara yake akaiwasha na kuvuta.
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
* * * *
Mara tu alipomaliza kuongea na Khumalo simuni ,Loniki alihisi kuchanganyikiwa.Haraka haraka akapanda gari na kurejea nyumbani.Alipofika nyumbani akamvuta pembeni mama yake aliyekuwa amekaa na kundi la akina mama waliokuja kumpa pole.
“ Loniki vipi,mbona uko hivyo? Akauliza mama yake
“Mama nina shida”
“Shida gani Lonny?
“Mama nina shida ya pesa”
“Pesa !! mama yake akaonyesha mshangao.Hakuwahi kumsikia hata siku moja Loniki akiwa na shida ya pesa
“Unahitaji kiasi gani cha pesa? Akauliza mama yake
“Nahitaji million ishirini”
“Millioni shirini !!!! mama yake akastuka
“Ndiyo mama”
“Pesa zote hizo za nini Loniki?
“Nina shida nazo kubwa na ya haraka kwa leo.Nimeongea na mume wangu na ameniahidi kunitumia pesa hizo kesho toka London.Kama una kiasi hicho cha pesa naomba uniazime na kesho nitakurejeshea.”
Mama yake akabaki anamuangalia loniki kwa mshangao.
“Mama mbona unanitazama hivyo?
“Nimestushwa na kiasi hicho kikubwa cha pesa.lakini hebu niambie Loniki unataka kuzipeleka wapi fedha zote hizo?
“Mama nina shida nazo sana kwa leo.” Akasema Loniki.Mama yake akafikiri kidogo na kusema
“Kwa sasa bado sijajua nina kiasi gani cha pesa ndani kwani Vero ndiye aliyekuwa meneja wangu.Twende ndani nikaangalie nina kiasi gani “ akasema mama yake na wakaelekea chumbani kwake ,akafungua kabati na kutoa vitita vya pesa wakaanza kuhesabu.
“Millioni kumi na tatu” akasema mama yake wakatazamana
“Bado million saba” akasema Loniki
“Tutatoa wapi hizo zilizobaki? Akauliza mama yake
“Mimi sijui mama.Jaribu kufanya maarifa.” Akasema Loniki
“Jaribu kuongea na mdogo wako Sarah anaweza akakupatia kiasi hicho cha pesa”
“Hapana mama siwezi kufanya hivyo.Tena ninaomba usimweleze chochote kile kuhusiana na pesa hizi.Kama unataka kuazima kwa Sarah,azima kama wewe na asifahamu kama unanipa mimi.” Akasema Lonny.mama yake akachukua simu na kumpigia Sarah.
“Hallow mama” akasema sarah
“Sarah nina shida kidogo mwanangu”
“Shida gani mama?
“Nina shida ya pesa “
Sarah akacheka kidogo aliposikia mama yake anashida ya pesa.
“Mbona unacheka Sarah?
“Ni mara yangu ya kwanza kukusikia ukisema una shida ya pesa”
“Kweli Sarah nina shida ya pesa lakini nitakurejeshea kesho”
“Unahitaji shilingi ngapi mama?
“nahitaji million saba”
“Millioni Saba? !!!!..Sarah akastuka
“Ndiyo sarah.Ninahitaji pesa hizo kwa haraka.Kama unazo naomba uniazime na kesho nitakurejeshea.”
Sarah akavuta pumzi ndefu na kimya kifupi kikapita
“Sarah unaweza ukanisaidia kiasi hicho cha pesa?
“Mama unataka kutumia kwa kazi gani fedha zote hizo?
“Nina mizigo yangu imekwama nataka nikaikomboe.Kesho nitakwenda benki na kukurejeshea pesa zako”
Sarah akafikiri kidogo na kusema
“mama naomba unipe masaa mawili,nitakuletea fedha hizo nyumbani”
“Ahsante sana Sarah” akajibu mama yake na kukata simu
“Sarah atatupatia fedha hizo.Lakini hakikisha kwamba kesho tumepata fedha za kumrudishia ndugu yako”
“Usijali mama kesho nitatumiwa fedha na tutazirejesha fedha za Sarah,ila nakuomba sana Sarah asifahamu lolote kama fedha hizo unanipa mimi.”
“Usihofu Loniki sintamwambia kitu”
“Haya ahsante mama.Niko chumbani kwangu” akasema Loniki na kuinuka akaelekea chumbani kwake.
Baada ya kuingia chumbani kwake akampigia simu Linah na kumuomba amfahamishe Khumalo kwamba tayari amekwisha pata kiasi cha pesa alichokuwa anakihitaji na atampelekea jioni ya siku hiyo kama alivyokuwa ameagiza
* * * *
Bado kitambaa kilikuwa machoni kwa Happy na hakuweza kuona chochote.Hakutambua walikuwa wapi lakini alichojua ni kwamba alikuwa wamefika mahala fulani na gari likasimama.Milango ya gari ikafunguliwa na wale watu wakashuka na kumshusha naye pia.Hakujua alikokuwa anaelekea lakini alihisi kama vile alikuwa anashushwa ngazi.Mara wakafika mahala wakasimama na watu wale wakajadili jambo halafu akasikia milango inafungwa na kitambaa kikatolewa machoni.Happy akajikuta katika chumba kikubwa chenye samani za kuvutia.Kulikuwa na kitanda kikubwa kizuri chenye nakshi,kilichotandikwa mashuka mazuri,.Kulikuwa pia na kabati kubwa la nguo na meza kubwa iliyosheheni vipodozi.Kulikuwa vile vile na runinga kubwa na sofa nzuri za kupendeza..hali ya hewa ilikuwa ni ya ubaridi uliotokana na kiyoyozi.
Happy alikitazama chumba kile halafu akageuza shingo yake na kumgeukia mwanadada aliyesimama mbele yake.
“Mmenileta wapi? Mnataka nini toka kwangu? Nani kawatuma mnilete huku? Happy akauliza maswali mfululizo.Mwanadada yule akatabasamu na kusema
“Usihofu Happy.Hapa uko salama na hakuna tatizo lolote.Jisikie huru na wala usiogope chochote.”
“mnataka nini kwangu? Nani kawatuma mnikamate na kuja kunifungia humu? Niambieni mnataka kiasi gani cha pesa? Familia yangu itatoa” akasema Happy huku machozi yakimtoka
“Relax Happy.Huna haja ya kutoa machozi.Sisi hatuna haja na pesa zako na wala hatujakuleta hapa kukudhuru au kuitaka familia yako itupe pesa” akasema Yule mwanadada
“Kama hamna shida na pesa,kwa nini basi mmeniteka nyara?
“Tumekuleta hapa ,kuna mtu anataka kuongea na wewe”
“Mtu anataka kuongea na mimi? Thats crazy.!!!! Kwa nini mtu huyo asinitafute nikaongea naye hadi awatumie ninyi mniteke na kunileta hapa?
“Happy darling,why don’t you take some rest first? Tumekuandalia kitanda kizuri.Feel at home.Anything you need let me know” akasema Yule mwanadada halafu akainuka sofani na kuufungua mlango mmoja
“Kuna bafu hapa.Ingia uoge ujisikie vizuri.Katika kabati kuna nguo nzuri utabadilisha baada ya kuoga”
“Nimesema sitaki kitu chochote,nataka mniache huru niende zangu.” Akasema Happy kwa ukali
“Huna haja ya kukasirika Happy.Mara tu mtu anayetaka kuongea nawe akifika tutakuacha huru.By the way ninaitwa Rosa” akasema Yule mwanadada.Happy akamtazama kwa hasira halafu akajitupa kitandani
“Mambo gani haya yananitokea mimi? Mbona mikosi inaniandama namna hii? Kabla ya suala moja kumalizika linaibuka lingine.why always me?” akawaza Happy huku machozi yakimtoka
“Watu hawa walionileta hapa ni akina nani ? Huyo mtu anayetaka kuongea na mimi ni nani? Anataka nini kwangu? Ouh Mungu wangu tafadhali naomba unisaidie” akawaza Happy na mara mlango ukafunguliwa na jamaa mmoja mnene akaingia akiwa na sinia la chakula.Happy akamkumbuka alikuwa ni mmoja wa watu waliomteka.Taratibu mtu yule akamsogelea Happy pale kitandani
“How do you feel Happy? Akasema Yule jamaa huku akiliweka sinia lile juu ya meza ndogo
“what do you want from me? Who are you people? Akauliza Happy kwa ukali
“Usihofu Happy.Sisi si watu wabaya na wala hatuna lengo baya nawe.Just relax and eat”
“Sintakula chochote hadi huyo mtu aliyewatuma mniteke na kunileta hapa aje anieleze sababu ya kunileta na kunifungia humu.”Yule jamaa akamtazama Happy usoni halafu akatoka nje.
Sarah aliwasili nyumbani kwako baada ya masaa mawili kama alivyokuwa ameahidi.Katika mkoba wake kulikuwa na kiasi cha shilingi millioni saba alizokuwa ameomba mama yake.Ilikuwa ni mara ya kwanza kwa mama yake kumuomba msaada wa kiasi kikubwa cha pesa kwa hiyo alifanya kila aliloweza hadi akazipata fedha hizo.
Baada ya kushuka garini moja kwa moja akaelekea sehemu alikokuwa mama yake halafu wakaelekea chumbani akamkabidhi fedha zile
“Mama mzigo huu hapa.Nimelazimika kuzichukua katika akaunti ya mume wangu kwa hiyo kama ulivyoahidi kuzirejesha kesho naomba iwe hivyo” akasema Sarah
“Ahsante sana Sarah.Kesho nitakurejeshea fedha zote”
“Sawa mama,lakini mbona hujaniambia fedha hizo ni kwa ajili ya nini? Umepatwa na tatizo gani?
“Usijali sarah.Ni suala la kawaida katika biashasra zangu” akasema mama yake.Sarah hakutaka maongezi mengi akatoka mle chumbani lakini wakati akitoka akagongana na Loniki ambaye naye alikuwa anaelekea chumbani kwa mama yake.Sarah akapatwa na wasi wasi.
“Whats going on here? kuna kitu gani kinaendelea kati ya mama na Loniki.? Sarah akajiuliza maswali lakini hakutaka kuwafuatilia akaendelea na shughuli zake.Baada ya kama dakika ishirini toka Loniki aingie mle chumbani mwa mama yake mlango ukafunguliwa na wote wawili wakatoka.Sarah akamfuata mama yake
“mama kitu gani kinaendelea kati yako na Loniki?Mna mipango gani ya siri?
“Hakuna kitu chochte kibaya Sara.Kuna masuala Fulani yanayohusiana na biashara zangu ambayo Loniki anakwenda kuyashughulikia.”
“Ni masuala gani hayo mama? Naomba unieleze.”
“Ni masuala yangu ya kibiashara. Mbona maswali yanakuwa mengi Sarah?
“mama nina haki ya kufahamu tatizo lako kama mwanao.Kinachonishangaza ni kwamba miaka hii yote Loniki hakuwepo na tuliokuwa tukikusaidia katika masuala yako mbali mbali ya kibiashara ni mimi na Vero sasa iweje leo uniache mimi na umtumie Lonny?
“Sarah si kila kitu kuhusiana na biashara zangu unapaswa kukifahamu.” Akasema mama yake
“Mama nimetoa pesa zangu nyingi katika tatizo hilo kwa hiyo nina haki ya kujua zinakwenda wapi”
“Sarah inatosha sasa.Nimechoshwa na maswali yako.Umenipa pesa subiri kesho nitakurejeshea pesa zako” Akasema kwa ukali mama yake na kuanza kuondoka lakini Sarah akamuita
“Samahani mama kama nimekuudhi lakini nimekuuliza kwa nia njema tu ya kutaka kufahamu kama una tatizo lolote.Siku zote nimekuwa rafiki yako na hujawahi hata siku moja kunificha tatizo linalokusumbua.Vile vile hata siku moja hujawahi kuniomba pesa na ninafahamu unazo pesa za kutosha toka katika miradi yako .Kitendo hicho kimenistua sana na ndiyo maana nahitaji kufahamu endapo kuna matatizo katika biashara ili kwa pamoja tuone namna ya kuweza kuyaondoa”
“Sarah ahsante sana kwa msaada wako.Kwa sasa tatizo lenyewe limekwisha na endapo nitahitaji msaada zaidi nitakueleza.” Akasema mama yake na kuondoka.Hakutaka tena maongezi na Sarah
“lazima nifahamu Lonny anazipeleka wapi zile pesa.Sina hakika kama mama ana shida ya pesa.Biashara zake zinamuingizia mamilioni ya pesa na hawezi kuwa na shida na millioni saba.Lazima kuna kitu kinaendelea hapa ambacho mama hataki kukiweka wazi.Hata macho yake yanaonyesha kabisa kuna jambo analificha.Taa ya tahadhali inaanza kuwaka kichwani,inaonekana Lonny ameanza kutekeleza mpango wake wa kulipiza kisasi.” Akawaza Sarah
* * * *
Saa kumina mbili za jioni gari aina ya Toyota Surf lenye rangi nyeusi likawasili katika jumba moja la kifahari lenye rangi nyeupe lilizungukwa na miti na maua mazuri
Linah na Loniki wakashuka katika ile gari .Wakiongozwa na kijana aliyetumwa kwenda kuwachukua wakaingia ndani ya jumba lile kubwa la kifahari.Walikaribishwa katika sebule kubwa na nzuri sana na baada ya dakika tano akajitokeza Khumalo.
“Karibuni sana” akasema khumalo huku akiwapa mikono
“Hii ni moja ya makazi yangu pia na mara nyingi hupenda kuja kupumzika huku.Ni watu wachache sana wanaopafahamu mahala hapa? Akasema Khumalo huku akitabasamu na kupuliza moshi wa sigara hewani
“Hongera ,umejitahidi sana Khumalo” akasema Linah
“Ahsante sana” akajibu Khumalo halafu kikapita kimya kifupi ,Khumalo akasema
“Miss Tanzania tuko naye hapa na anaendelea vizuri”
“Kazi nzuri sana Khumalo.Hakukuwa na rabsha zozote wakati wa kumchukua? Akauliza Loniki
“Hapana Loniki.Hakukuwa na tatizo lolote.Tukio hilo limefanywa kitaalamu sana.Natumai umekuja na ule mzigo kamili kama tulivyoongea” akasema Khumalo
“Ndiyo Khumalo.Nimekuja kamili” akasema Loniki na kuufungua mkoba wake akatoa mabunda ya noti akayaweka mezani.CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“million thelathini.” Akasema Loniki.Khumalo akayashika mabunda yake akatabasamu
“Mtu wangu yuko wapi? Akauliza Loniki
“Usihofu Loniki.Utamuona tu” akasema Khumalo halafu akayakusanya mabunda yale ya noti akaondoka nayo na baada ya dakika tano akarejea na kuwaomba Linah na Loniki wamfuate.Waliongozana hadi katika chumba kimoja kikubwa kilichokuwa na mitambo mingi.Kilionekana ni kama studio.Kulikuwa na kompyuta nyingi na runinga kubwa ukutani.
“Nipatie namba nane” Khumalo akamwambia kijana aliyekuwamo mle ndani na baada ya sekunde kadhaa kupitia ile runinga kubwa Happy akaonekana akiwa amekaa kitandani.Loniki akasonya na kukunja uso kwa hasira
“Unaweza kuniruhusu nikaonana naye ana kwa ana?
“Hapana Lonny.Hutakiwi kuonana naye ana kwa ana.si vizuri kwa usalama wetu.Nadhani tusiendelee kupoteza muda ni wakati wa kuianza kazi sasa”.Akasema Khumalo,Loniki akatikisa kichwa kuitikia lakini ilionyesha dhahiri kamba alikubali kwa shingo upande.Lengo lake lilikuwa ni kuonana ana kwa ana na Happy
“Ninyi mtashuhudia kila kinachoendelea kupitia hii runinga ambayo imeunganishwa na kamera zilizoko katika chumba alimo Happy.Mtashuhudia kila kitu” akasema Khumalo halafu akatoka mle chumbani.Bado Loniki aliendelea kumtazama Happy kwa hasira
Mlango wa chumba alimowekwa Happy ukafunguliwa na Khumalo akaingia.Happy ambaye alikuwa amejiinamia akainua uso wake baada ya kusikia mlango unafunguliwa.Akakutana na sura iliyomstua na kumfanya aismame
“Its you ..!!!” akasema Happy kwa mshangao
“Hallo Happy..!! akasema Khumalo huku akitabasamu.
“Kumbe ni wewe !!!.Nakukumbuka sana.Ulikuwepo mahakamani juzi na ulikuwa unaniangalia kwa jicho baya.Who are you? ..Happy akasema kwa hasira
Khumalo akatabasamu na kuizima sigara aliyokuwa anaivuta
“Calm down my love.Huna haja ya kuhamaki namna hiyo.Unajisikiaje Happy? Mbona hujala chakula? Akasema Khumalo na kuketi sofani.Happy bado aliendelea kumuangalia kwa hasira
“Niambie ni kwa nini umewatuma watu wako waniteke na kunifungia humu? Unataka nini toka kwangu?
“Happy naomba ukae,kuwa na amani na wala usiwe na hasira.Nimekuleta hapa nina maongezi nawe mafupi lakini ya muhimu sana.Baada ya kumaliza maongezi nawe nitakuruhusu uende zako” akasema Khumalo kwa upole
“Unataka kuongea nami nini na kwa nini usinitafute katika njia za kawaida hadi uniteke nyara? Akauliza Happy
“Happy ni saa moja za jioni sasa na nina imani familia yako tayari imeanza kuwa na wasi wasi juu yako kwa hiyo naomba tusipotee muda .Nisikilize kile kilichonifanya nikulete hapa halafu nitakuacha uende zako” akasema Khumalo na kauli ile ikamfanya Happy atulie.
“Naitwa Job.Mimi ni mfanya biashara wa kimataifa.Nafikiri ni mara yako ya pili kuniona.Baada ya kujitambulisha kwako ,napenda nichukue nafasi hii kukuomba samahani kwa usumbufu wote ulioupata.Nafahamu ulikuwa na shughuli zako nyingi tu na zote zimevurugika kwa kukuleta hapa.Kuna mtu ambaye alitaka uwepo hapa kwa sababu anazojua yeye mwenyewe lakini kwa bahati mbaya hutaweza kumuona mtu huyo kwani jukumu zima la kuongea nawe amenikabidhi mimi.” Akasema Khumalo na kukaa kimya akamuangalia Happy
“ Ni nani huyo aliyekutuma unikamate? Ni Savanna? Akauliza Happy kwa hasira.Khumalo hakujibu kitu akamuangalia Happy kwa makini usoni na kusema
“Happy nafahanmu uko katika wakati mgumu hivi sasa kutokana na mfululizo wa matukio lakini kuna swali moja tu ninalotaka kukuuliza.” Khumalo akatulia halafu kwa sauti ndogo akauliza
“Do you love Patrick?
Happy akamtazama Khumalo kwa mshangao na kusema
“yes I do love him”
“How much do you love him?
“More than my life” akajibu Happy kwa ufupi
“Good.Nafurahi kusikia hivyo” akasema Khumalo
“Jibu lako ninanifanya niamini kwamba uko radhi kufanya jambo lolote kwa ajili yake?
Happy akamuangalia Khumalo machoni halafu akasema
“Ndiyo .”
“nafurahi sana kusikia hivyo.Ni watu wachache sana ambao wanaweza kuyatoa maisha yao kwa ajili ya wale wawapendao.” Akasema Khumalo akakaa kimya kwa muda halafu akasema
“Patrick alikuwa na mpenzi wake aitwaye Veronika.walipendana sana na walikuwa katika hatua za mwishoni ili wafunge pingu za maisha na kuishi maisha yenye raha,lakini ulipojitokeza wewe mipango yao yote ikavurugika. Patrick alibadilika na kusitisha kila kitu kuhusiana na ndoa yake na Vero.Watu wengi sana waliumia.Vero alipatwa na uchungu mwingi na hatimaye alifariki dunia.Ni pigo kubwa kwa ndugu zake,rafiki zake na wale wote waliompenda.Matukio haya yote yaliyotokea yanadhihirisha wazi ni namna gani wewe na Patrick mnavyopendana.Ninadiriki kusema kwamba wewe na Patrick mmeumbwa ili muwe pamoja.Penzi lenu ni zito na la kweli na hakuna wa kuwatenganisha katika hii dunia” akasema Khumalo .Happy bado aliendelea kumshangaa asielewe alikuwa anamaanisha nini kwa maneno yale.Kumalo akaendelea
“Awali ulinihakikishia kwamba uko tayari kufanya jambo lolote kwa ajili ya Patrick.Vizuri sana Happy.Nitapenda nilitibitishe hilo siku ya leo” akasema Khumalo
“Sijakuelewa unamaanisha nini.Naona unaongea maneno mengi sana na sikuelewi unahitaji nini toka kwangu.Kama unahitaji pesa niambie unahitaji kiasi gani nikupatie ili niondoke zangu” akasema Happy
“Happy naomba unisikilize tena unisikilize kwa makini sana.Hatuna haja na pesa zako ,mtu aliyetutuma tukulete hapa ametupa pesa nyingi sana ,a lot of money .Kwa hiyo hatuna shida na senti yako hata moja.” Akasema Khumalo
“Hivi tunavyoongea “ akaendelea Khumalo
“Kuna mtu ambaye ni mfanyakazi wa idara ya magereza anayefanya kazi katika gereza alimo Patrick,yuko tayari na chakula chenye sumu ambacho anasubiri kumpa Patrick na baada ya dakika kumi tu atakuwa amekufa.Anachosubiri ni maelekezo yangu tu.Just one call and Patrick dies” akasema Khumalo
“whaaattt…!!!!!!!!!!.Happy akastuka na kusimama akamuangalia Khumalo kwa hasira
“Najua umestuka sana kusikia kwamba Patrick yuko hatarini kuuawa.Najua Patrick ndiye mwanaume wa maisha yako na endapo atafariki basi ndoto zako zote za kuwa na maisha yenye furaha pamoja naye zitayeyuka.Maisha yako yataharibika na juhudi zako zote ulizozifanya katika kulijenga penzi lako na Patrick zitakuwa ni kazi bure.Maisha ya Patrick ,mwanaume umpendaye yako mikononi mwako hivi sasa.Wewe ndiye utakayeamua hatima ya maisha yake kwa sasa endapo aendelee kuishi au afariki dunia kwa sumu.” Akasema Khumalo.Happy akatetetemeka .Khumalo hakuonyesha kama anafanya masihara
“Please Job,don’t ever hurt Patrick.Hakuna anayefahamu umuhimu wake kwangu.Patrick ndiye maisha yangu,ndiye furaha yangu,ndiye kila kitu kwangu.Siwezi kuishi bila yeye.Tafadhali naomba msimfanye jambo lolote la kumdhuru.Nambieni mtu aliyewatuma amewapa shilingi ngapi? Nitawapa mara mbili yake” akasema Happy huku akilia
“Happy sisi kwa maelekezo tuliyopewa na mtu aliyetutuma tukulete hapa ,hatutamgusa Patrick na wewe utaachiwa huru endapo utakubali kufanya anavyotaka yeye.”
“Huyo mtu anataka nini toka kwangu? Nimemkosea nini? Naomba niongee naye mimi mwenyewe anieleze nilichomkosea” akasema Happy
“Hapana Happy.Huwezi kuongea naye.You’ll talk to me” akasema Khumalo
“Ok Niambie unataka nini? Huyo mtu wenu anataka nini toka kwangu kama malipo ya kutomdhuru Patrick?
“Ni kitu kidogo sana ambacho kiko ndani ya uwezo wako.Kabla sijakwambia nini unatakiwa kufanya hebu kwanza angali picha hizi namna mtu aliyekula sumu hii tunayotaka kumpa Patrick anavyokufa” akasema Khumalo na kwenda katika runinga akachomeka kifaa kidogo cha kuhifadhi kumbu kumbu na kukiwasha.Picha zikaanza kuonekana
“Ukimaliza kuangalia kama utakuwa tayari kumuokoa Patrick utabonyeza kitufe hiki chekundu.Hii ni kengele ambayo itaniashiria kwamba uko tayari na mimi nitakuja mara moja.You have twenty minutes to decide” akasema Khumalo na kutoka.Happy akabaki peke yake mle chumbani akitazama picha zile za kutisha
* * * *
Baada ya kutoka katika chumba alichokuwamo Happy ,chumba ambacho kilijengwa chini ya ardhi,Khumalo akapanda moja kwa moja hadi katika chumba walimo Linah na Loniki walikokuwa wakifuatilia kila kilichokuwa kinaendelea kule chini kupitia runinga kubwa.
“Nimemuacha aangalie picha zile na nina hakika baada ya kumaliza kuzitazama lazima ataniita.Anampenda Patrick sana na hawezi kukubali Patrick adhurike.” Akasema Khumalo
“Bado roho yangu haina amani kabisa Khumalo.Nilichokuwa nakitaka ni kuona mida hii Happy akiwa katika mateso makali sana.” Akasema Loniki
“Relax Lonny.Hii ni mbinu ya kumfanya Happy akubali kufanya mapenzi yeye mwenywe kwa hiari yake na vijana wetu na ili filamu zitakapotoka isionekane kwamba kuna nguvu ilitumika.Ninakuhakikishia Lonny ,kama lengo lako ni kutaka Happy ateseke basi ndani ya muda mfupi ujao atapata mateso makali sana na kwa namna jina lale litakavyochafuka nina hakika lazima atachukua jukumu la kujimaliza .Filamu hiyo tutaisambaza katika mitandao ya ngono duniani,katika mitandano ya kijamii,katika simu na kila sehemu ambayo tutaweza kuitumia kumchafua Happy.Atateseka kwa maisha yake yote yaliyobaki hapa duniani.” Akasema Khumalo
Lonny bado aliendelea kumtazama Happy kwa hasira kupitia runinga ile.
“Usisahau vile vile kwamba picha zitakazopigwa ,Happy akifanya mapenzi na vijana wetu atafikishiwa pia Patrick gerezani.I swear to you Lonny,kwa namna Patrick anavyompenda Happy I’m sure he will drop dead” akasema Khumalo huku akicheka
“Kwa mtu mwenye jina kubwa kama la Happy kuingia katika kashfa kubwa ya ngono ni habari ambayo haitaweza kufutika kwa urahisi katika vinywa vya watanzania.Ni historia ambayo itadumu kwa vizazi hadi vizazi na atakayeteseka si Happy pekee bali hata familia yake ka ujumla na zaidi sana Patrick” Akasema Khumalo huku akipuliza moshi mwingi hewani
“Damn you Happy !!.Laiti ningekuwa na uwezo wa kufika katika chumba ulimo ,ningekuua mimi mwenyewe kwa mikono yangu.Natamani hata niutafune moyo wako.Wewe ni sababu ya mdogo wangu kufariki dunia.I swear I’ll make your life a living hell before you die” akawaza Lonny huku akiendelea kumtazama Happy kwa hasira kupitia Runinga
* * * *
Familia yote ya mzee Kibaho ilikwisha rejea nyumbani na walikuwa wanajiandaa kupata mlo wa usiku.Ni Happy pekee ambaye hakuwa ameonekana .Toka amerejea nyumbani,mzee Kibaho hakuwa ameonana na mwanae kipenzi Happy.
“Happy ameshindaje? Yuko wapi? Akauliza mzee Kibaho
“Bado hajarejea toka alipoondoka asubuhi.” Akajibu mama yake Happy
“Toka alipoondoka asubuhi?? Akashangaa mzee Kibaho
“Ndiyo.Aliondoka hapa nyumbani asubuhi na alisema kwamba hatakawia kurudi lakini nashangaa mpaka mida hii hajarajea”
“Alikuaga anakwenda wapi?
“Hakusema anakwenda wapi lakini ilionekana alikuwa na haraka na mahala alikokuwa anakwenda”
Mzee Kibaho akainuka na kwenda chumbani kwa Happy kuhakikisha kama ni kweli Happy hayupo.Akarudi sebuleni na kuchukua simu yake akapiga namba za simu za Happy lakini simu haikuwa inapatikana.
“Si kawaida ya Happy kuzima simu.” Akasema kwa wasi wasi mzee Kibaho huku akijaribu tena na tena kupiga simu ya Happy lakini jibu likawa ni lile lile namba anayopiga haipatikani.
“Margreth,Happy hakukueleza mahala anakoelekea leo? Akauliza mzee Kibaho baada ya Margreth kuingia pale sebuleni
“Hapana baba .Jana nilichelewa sana kurudi na sikuweza kuonana naye na leo asubuhi nimeondoka mapema mno na yeye akiwa bado amelala.Nilimtafuta katika simu yake mchana lakini simu yake haikuwa ikipatikana”
Mzee Kibaho akamuita Pendo mfanyakazi wa ndani
“Pendo wewe ndiye uliyekuwa na Happy jana mahakamani.Kuna jambo lolote alikueleza kuhusu mahala alikokusudia kwenda leo?
“Hapana baba hakunieleza chochote.Ninachokumbuka ni kwamba kabla hatujaondoka pale mahakamani alitokea kijana mmoja akaongea kitu na dada halafu tukaondoka naye hadi katika baa Fulani wao wakashuka mimi nikabaki ndani ya gari.Walikuwa na maongezi muhimu lakini sikujua walikuwa wanaongea nini.Baada ya muda mfupi dada akarejea garini kwa kasi akauinamia usukani akaanza kulia.Nilimuuliza alikuwa analia nini lakini hakunijibu kitu,akawasha gari tukaondoka.Jioni mida ya saa kumi na moja akanipigia simu akaniomba nimtengenezee juisi ya maembe.Nilipompelekea chumbani kwake nilimkuta akiongea na simu na kuna mtu alikuwa kama anajibizana naye.Walikuwa ni kama wanazozana.Nakumbuka nilimsikia akitaja jina la Savanna katika maongezi yao”
“ Savanna !!..akastuka mzee KibahoCHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Ninayo namba ya simu ya Savanna ngoja tumpigie pengine anaweza kufahamu mahala alipo Happy” akasema Margreth
“Nipe niongee naye” akasema mzee Kibaho
“hallo Margreth” akasema Savanna baada ya kupokea simu
“Hallow Savanna.Mimi ni mzee Kibaho baba yake na Happy”
“Ouh shikamoo mzee.”
“marahaba Savanna.Samahani kwa kukusumbua usiku huu.Tumekuwa na wasi wasi kuhusu Happy.Hajaonekana toka alipoondoka nyumbani asubuhi ya leo na hata katika simu hapatikani.Umeonana naye kwa siku ya leo?
“Ndiyo baba.Happy nilionana naye asubuhi .Tulikutana gerezani alikuja kumtembelea Patrick.Mimi nilimkuta tayari amekwisha fika na inaonekana aliwahi mapema sana.Hatukupata wasaa wa kuongea zaidi ya kusalimiana kwa sababu nilikuwa nimeongozana na familia ya Patrick.” Akasema Savanna.Mzee Kibaho akavuta pumzi ndefu
“Ahsante sana Savanna,.Endapo ikitokea ukawasiliana naye basi tutaarifu mara moja”
“Sawa baba nitafanya hivyo.” Akajibu Savanna na kukata simu
“Kwa mujibu wa maelezo ya Savanna,Happy alikwenda gerezani asubuhi ya leo kuonana na Patrick.” Akasema mzee Kibaho baada ya kumaliza kuongea na Savanna simuni
“Atakuwa ameelekea wapi? Akauliza mama yake
“Alipoondoka asubuhi alinihakikishia kamba hatakawia kurudi.Na hata mavazi yake hayakuonyesha kama alikuwa na safari ya kuelekea mbali.Alivaa mavazi ya kawaida”
“Kama ni hivyo atakuwa wapi? Akauliza Magreth na kisha wakaanza kupiga simu kwa watu mbalimbali kumuulizia Happy lakini hakuna hata mmoja aliyekuwa amemuona Happy
“Msiwe na wasi wasi.Happy ni mtu mzima na anafahamu kitu anachokifanya.Inawezekana amepatwa na dharura kama mnavyofahamu kwa siku za hivi karibuni amakuwa na mambo mengi .Tuendeleeni kumsubiri na nina hakika atarejea muda si mrefu” mzee Kibaho akawapa moyo familia yake lakini hata yeye alikuwa na wasi wasi mwingi moyoni kutokana na mfululizo wa matukio yaliyomuandama binti yake
Mlio wa kengele ukasikika katika chumba walichokuwamo akina Khumalo.
“kazi imeanza.” Akasema Khumalo na kuondoka kuelekea katika chumba alichokuwamo Happy
“Hallo Happy” akasema Khumalo
“Stop it..Please stop it” akalia Happy huku akiyafunika macho yake kwa viganja vya mikono ili asiendelee kuzitazama picha zile za kutisha
“Umeona Happy? Umeona namna sumu hii inavyowatesa watu kabla hawajafa?
“ Please Job ,dont do that to Patrick.I beg you don’t hurt Patrick” akalia Happy
“Kwa hiyo umeamua nini? Uko tayari kufanya kile tunachotaka kwa ajili ya kuokoa uhai wa Patrick? Akauliza Khumalo
“I’m ready.Please don’t hurt Patrick.I’m ready to do anything to save him”
“Vizuri sana.Watu kama wewe ni wachache sana.Hata mimi namuonea wivu Patrick kwani amempata mwanamke anayempenda kwa dhati.”
“Tafadhali sema mnataka niwafanyie nini? Akasema Happy huku akifuta machozi.Khumalo akainuka pale sofani alipokuwa amekaa akamsogelea Happy
“Stop crying Happy.Usilie tena.” Akasema Khumalo halafu akanyamaza kidogo akamtazama Happy usoni na kusema
“ Aliyenituma nikulete hapa alitoa sharti moja tu ambalo ukilitekeleza utaokoa maisha ya Patrick na wewe utakuwa huru.Anao vijana wake wawili wanaokupenda sana na anataka ufanye nao mapenzi.”
“ What !!!!????...Happy akastuka na kumtazama Khumalo kama ameona mzuka
“Hilo ndilo sharti pekee alilolitoa mtu aliyekuleta hapa.Ni juu yako kukubali au kukataa.Kama hautakuwa tayari sisi tutakuacha uende zako lakini nakuhakikishia kwamba wakati wewe ukitoka ndani ya jumba hili,mtu umpendaye kuliko wote duniani atakuwa atakuwa tayari amelala usingizi wa milele.” Akasema Khumalo na kuzidi kumtisha Happy.
“ Ni nani huyo shetani ambaye amenileta hapa? Ni nani huyo asiyekuwa na hata chembe ya ubinadamu? Nimemkosea kitu gani hadi aamue kunitenda namna hii ? akasema Happy huku akilia kwa uchungu
“Happy ni juu yako kuamua .Kilio na matusi kamwe havitakusaidia na muda wetu unazidi kwenda.Ninakupa tena dakika kumi nyingine za kuamua “ akasema Khumalo na kupiga hatua kutoka mle chumbani
“Ouh My God !!!! akalia Happy.Alihisi kuchanganyikiwa
“whats happening to me? Ni kweli nina laana? Kwa nini ninaandamwa na mikosi kama hii kila siku? Huyu mtu aliyenileta hapa ni nani na kwa nini atake kunidhalilisha namna hii? Happy akazidi kulia
“Huyu mtu aliyenileta hapa lengo lake ni moja tu ,kunidhalilisha. Nini kitatokea kama nitakataa kufanya anavyotaka? Je ni kweli Patrick yuko katika hatari ya kuuawa? Sina hakika kama suala hili ni la kweli.Huyu mtu lengo lake ni kuudhalilisha utu wangu.Ninaanza kuhisi mtu huyu atakuwa ni Savanna kwani ndiye mtu niliyelumbana naye jana na tukatoleana vitisho.Pengine ameamua kunionyesha uwezo wake kwa kuniteka na kunileta hapa ili nidhalilike.Siwezi kukubali hata kidogo kuwapa nafasi ya kuuchezea mwili wangu.Ni bora waniue kuliko kuwapa nafasi ya kunichezea.” Akawaza Happy lakini mara akastuka
“What if its true and Patrick is going to die? Inawezekana pengine watu hawa wakawa wanasema kweli ..Am I ready to let Patrick die? I’m confused..!!! Happy akahisi kuchanganyikiwa
“Patrick amejitolea mengi kwa ajili yangu na hata hivi sasa anasota gerezani kwa ajili yangu.Kwa nini na mimi nishindwe kusimama imara kuutetea uhai wake? Kwa maana hiyo itanilazimu kukubaliana na matakwa yao ya kufanya mapenzi na watu wawili? Ouh Jamani akili yangu naona haifanyi kazi tena.Sijui nifanye nini” akawaza Happy na mara mlango ukafunguliwa Khumalo akaingia.Safari hii macho yake yalionekana mekundu na yasiyo na masihara hata kidogo.Happy akaingiwa na woga.Mwili ukamtetemeka
Happy dakika kumi zimekwisha na ninadhani tayari umekwisha fanya maamuzi” Akasema Khumalo huku akimuangalia Happy kwa macho makali sana.
Happy mwili ulimtetemeka na hakujua aseme nini
“Inaoneka bado hujaamua lolote.I’m so sorry Happy.” Khumalo akasema kwa masikitiko halafu akatoa simu yake na akabonyeza namba na kupiga
“Hallow Josh,amekataa kutoa ushirikiano endelea na mpango wetu,mpe Patrick chakula” akasema Kumalo halafu akamuangalia Happy kwa masikitiko
“I’m so sorry Happy.Muda mfupi toka sasa Patrick hatakuwa nasi tena.”
“Stop it !!!!!..Please stop it !!!!...” akapiga kelele Happy
“Please stop it.Dont kill Patrick.Niko tayari kufanya mnavyotaka.” Akasema Happy.Khumalo akamtazama kwa makini machoni halafu akatoa simu yake na kupiga
“Hallow Josh,subiri kwanza.Sitisha kwanza hilo zoezi” akasema Khumalo na kukata simu
“Happy nadhani sasa umeamua kumuokoa Patrick”
“Niko tayari kufanya lolote ili msimdhuru Patrick”
“Vizuri sana” akasema Khumalo huku akitabasamu
“Please don’t hurt Patrick.Hastshili mateso yoyote.Kama ni mateso naomba mnitese mimi”
“Hatukutesi Happy.Fanya kama ulivyoamriwa na utakuwa huru na hakuna mtu atakayemgusa Patrick” akasema Khumalo
“Niko tayari kufanya mnavyotaka lakini kwa sharti moja tu.Mtu huyo ambaye mnataka afanye mapenzi na mimi lazima atumia kinga”
“Usihofu kuhusu hilo Happy.Tunazingatia sana usalama wa afya yako.Jiandae Happy,baada ya muda watakuja vijana wawili unachotakiwa ni kuonyesha ushirikiano na jitahidi kuwaridhisha vijana hao.Baada ya hapo tutakuruhusu uende zako” akasema Khumalo halafu akatoka mle chumbani akimuacha Happy ameinama akilia
“Mpango mzima umekamilika .Mtashuhudia kila kitu muda si mrefu.Ninawahakikishia kwamba hili ni pigo kubwa kwa Happy” akasema Khumalo baada ya kurejea katika chumba walichokuwamo akina Linah
Baada ya dakika zipatazo kumi hivi,Khumalo akiwa ameongozana na vijana wawili waliojazia miili yao na wenye vifua vipana,wakaingia katika chumba alichokuwamo Happy.Vijana wale walikuwa wamezificha nyuso zao ili wasitambulike. Happy alipowaona akaogopa na kuanza kulia.
“Naombeni mnihurumie jamani.Nimewakosea nini hadi mnifanyie hivyo? Akalia Happy lakini Khumalo wala vijana wake hawakumsikiliza
“Happy nyamaza kulia.Futa machozi yako na tukamilishe zoezi letu ili tukurejeshe nyumbani kwenu.Nina imani familia yako ina wasi wasi mwingi sana sasa hivi” akasema Khumalo huku akiwasha taa kubwa iliyokuwamo mle chumbani na kukifanya chumba kiwe na mwanga mkali
“Happy kumbuka makubaliano yetu kwamba unatakiwa uonyeshe ushirikiano na uwaridhishe vijana wangu .Tumeelewana Happy? akasema Khumalo
“Ndiyo “ akajibu Happy
“Vizuri sana” akasema Khumalo na kutoka mle chumbani .Jamaa mmoja kati ya wale vijana walioletwa na Khumalo akamfuata Happy akaketi karibu yake na kumfuta machozi
“Fanya kama alivyokuamuru mkuu wetu.Endapo utaenda kinyume na matakwa yake anaweza akabadilika na akibadilika huwa ni mtu mbaya sana” akasema yule jamaa huku akianza kumtomasa Happy
“Please don’t hurt me “ akasema Happy
“Hautaumia mrembo.You’ll feel like you are in heaven” akasema jamaa mwingine
“Ninafanya hivi kwa ajili ya Patrick, kwa ajili ya kumlinda yeye “akawaza Happy halafu kijana mmoja akaanza kufungua vifungo vya lile shati lake dogo alilokuwa amevaa
“Leave me alone…Nitafanya mwenyewe” akafoka Happy na kumsukuma Yule jamaa halafu akasimama na kuanza kufungua vifungo vya shati lake huku machozi yakimtoka
“Mtu anayenifanyia kitendo hiki ni nani? Nimemkosea kitugani? akawaza Happy
Khumalo,Linah na Loniki walikuwa wameyaelekeza macho yao katika runinga ile kubwa mbele yao wakiangalia namna zoezi linavyoendelea.Baada ya kama dakika tano za mabishano kati ya Happy na wale vijana hatimaye vijana wale wenye nguvu walifanikiwa kumuangusha Happy kitandani na kuanza kumuingilia kwa zamu.Happy alilia sana wakati vijana wale wakiendelea na udhalimu wao juu ya mwili wake.Zoezi liliendelea huku likiendelea kurekodiwa pamoja na kupigwa picha.
Zoezi lilichukua zaidi ya dakika ishirini .Vijana wale walimaliza kazi waliyopewa huku wakihema kwa nguvu sana.Taratibu waliondoka mle chumbani na kumuacha Happy akiwa analia.
“kazi tayari” akasema Khumalo huku akitabasamu
“Ina maana kazi ndo imeishia hapa? Akauliza Loniki kwa mshangao
“Pesa zote hizi nilizotoa ni kwa ajili ya kazi hii ?
“Ndiyo Loniki.Lengo lako ni kumuadhibu Happy,? Akasema Khumalo
“Ndiyo” akajibu Happy
“Kama lengo lilikuwa hilo basi kazi imekwisha kwa leo na subiri kwa hatua itakayofuata.Kesho asubuhi nchi nzima itatikisika kwa taarifa hii.Ni skendo ambayo haijawahi kutokea hapa nchini” akasema Khumalo
“Kwa hiyo nini kitafuata baada ya hapa? Akauliza Loniki
“Niachie mimi kila kitu.Kesho asubuhi usiache kufuatilia vyombo vya habari,magazeti ya udaku na mitandao ya kijamii.Taarifa itakayokuwa inatawala ni ya picha za ngono za Happy” akajibu Khumalo.
Baada ya maongezi kadhaa na Khumalo Linah akamshika mkono rafiki yake Loniki wakaelekea katika gari ambalo liliwarudisha hadi ofisini kwa Linah ambako Loniki alichukua gari lake na kurejea nyumbani
Baada ya Loniki na Linah kuondoka ,Khumalo akaelekea katika chumba alimo Happy,akaufungua mlango na kuingia ndani.Happy alikuwa amelala kitandani akilia.Khumalo akamtazama kwa sekunde kadhaa halafu akapuliza dawa ya usingizi na kutoka mle chumbani
Baada ya dakika kumi na tano kupita toka Khumalo aipulize dawa ile katika chumba alichokuwamo Happy,Khumalo akarejea akiwa na vijana wake na kumkuta tayari Happy amelala fofofo hajitambui.Wakamuinua na kumpakia katika gari lake na kuondoka naye
“Kazi ya kwanza imekwisha.Kazi iliyobaki ni kuzisambaza picha na video.Naamini hadi kesho asubuhi zoezi hili litakuwa limekamilika na hatutakuwa na deni tena kwa Loniki“ akawaza Khumalo akiwa na vijana wake wakimrejesha Happy nyumbani kwao.Khumalo ndiye aliyekuwa ametangulia mbele na gari lake halafu gari la Happy lililokuwa linaendeshwa na kijana mwingine likafuata nyuma.Tayari Khumalo alikuwa anafahamu mahala anakoishi Happy kwani alikwisha mfanyia uchunguzi wa kutosha.
Saa saba kasoro za usiku waliwasili nyumbani kwa akina Happy.Kwa haraka haraka vijana wale wa Khumalo wakashuka katika gari la Happy.Kabla ya kushuka walimuwekea kitu fulani puani na kumzindua toka usingizini .Akapiga chafya mfululizo.Kwa haraka vijana wale wakaingia katika gari la Khumalo na kuondoka kwa kasi maeneo yale.
Mlio wa magari nje ya nyumba yake,ulimstua mzee Kibaho ambaye alikuwa macho mpaka mida hii akimsubiri mwanae arejee.Akatoka chumbani kwake na kwenda getini.Mbwa walikuwa wanabweka.Akachungulia nje kupitia uwazi mdogo na kuliona gari la Happy.Haraka haraka akafungua geti na kuliendea gari.Akachungulia ndani ya gari na kumuona Happy akiwa amelala kitini.Akapigwa na butwaa kwa hali aliyokuwa nayo .Happy alikuwa amelegea na mwili wake haukuwa na nguvu hata kidogo.Kwa haraka akamtoa mwanae garini na kumpeleka ndani na familia nzima ikaamka .Kila mtu alistushwa na hali aliyokuwa nayo Happy.Haraka haraka akaanza kupatiwa huduma ya kwanza.Hakuna aliyefahamu nini kimemsibu hata akawa katika hali ile.Ilikuwa ni hali ya kusikitisha sana.Daktari wa familia aliitwa akafika kwa haraka kuja kumuangalia Happy,akampima na kisha akampatia dawa na kumtaka akapumzike hadi asubuhi atakapopata majibu ya vipimo alivyochukua.
*******************
Kumekucha Tanzania.Ni saa moja za asubuhi, jijini Dar es salaam barabara zimesheheni watu na magari wote walikuwa wanaelekea katika shughuli mbalimbali za kila siku za uzalishaji mali.Katika vibanda na katika sehemu mbali mbali za kuuzia magazeti,kulikuwa na makundi ya watu waliokuwa wakihitaji magazeti ili kufahamu kulichoandikwamo asubuhi hii.Katika baadhi ya vituo vya kuuzia magazeti kulitokea ugomvi wa watu wakigombea magazeti kitu ambacho ni nadra sana kushuhudiwa.
Gazeti lililozusha mjadala asubuhi hii na kuwafanya watu wajazane katika vibanda vya kuuzia magazeti na wengine kufikia hata hatua ya kurushiana makonde ni gazeti la Mitikisiko,gazeti maarufu kwa kuandika habari za udaku na hasa zile zinazowahusu watu maarufu ndani na nje ya nchi.Siku hii ya leo gazeti hili lilipambwa na kichwa cha habari kilichobeba habari iliyozua gumzo nchini.
“HAIJAWAHI KUTOKEA” hiki kilikuwa ni kichwa cha habari kilichoandikwa kwa maandishi makubwa na chini yake kulikuwa na vichwa vingine vidogo vidogo.
“NI VIGUMU KUAMINI LAKINI KWELI”
“HUU NDIO UCHAFU WA MISS TANZANIA”CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Vichwa hivi vya habari vilisindikizwa na picha kubwa ya Happy Kibaho,akiwa mtupu huku sehemu ya kifuani na chini ya kiuno zikiwa zimezibwa kwa rangi nyeusi.Picha nyingine ilimuonyesha Happy akiwa amelala kitandani akiwa na wanaume wawili waliozifunika nyuso zao ambao ilionyesha wazi walikuwa katika harakati za kufanya mapenzi.
“Mlimbwende aliyenyakua taji kubwa la urembo hapa nchini la miss Tanzania ambaye siku chache zilizopita amelivua taji hilo kutokana na kashfa ya kujihusisha katika ugomvi wa kumgombania mwanaume,na kusababisha kifo cha msichana aitwaye Veronika ,ameingia katika aibu kubwa baada ya picha na video yake ya ngono kuvuja” Haya yalikuwa ni maelezo ya utangulizi ya habari hii kubwa na kulifanya gazeti la Mitikisiko kuongoza katika mauzo kwa siku hii.Taarifa ile iliendelea katika ukurusa wa tatu huku ikipambwa na picha zinazomuonyesha Happy akiwa mtupu huku akifanya mapenzi na wanaume wawili waliozifunika nyuso zao katika mitindo tofauti tofauti..Ilikuwa ni aibu nzito isiyoelezeka .
Katika tovuti mbali mbali na mitandao ya kijamii,tayari video na picha za Happy vilianza kusambaa kwa kasi kubwa na kuwa gumzo mtandaoni.Watu walikuwa wanatumiana video na picha hizo za Happy akifanya ngono na wanaume wawili hadi katika simu za mikononi.Kutokana na kukua kwa teknolojia ya upashanaji habari ndani ya masaa machache tayari habari kuhusu Happy ilikwisha sambaa karibu nchi nzima.
Mlango mdogo katika geti la kuingilia nyumbani kwa akina Happy ulikuwa wazi,hivyo kumfanya mama Joseph jirani wa akina Happy,apite kama mshale na kuingia ndani huku akihema akiwa na gazeti mkononi
“Mama Happy ..!!! akaita mama Joseph .Alikuwa anahema huku jasho likimtoka.Mama yake Happy ambaye alikuwa katika kazi za usafi wa nyumba asubuhi hii,akaja kwa kasi baada ya kusikia sauti ya mama Joseph.
“Mama Joseph kuna tatizo gani? akauliza mama Happy kwa mshangao
“Mama Happy njoo huku” akasema mama Joseph huku akimvuta mama Happy kuelekea sebuleni.
“Mama Happy umeshapata taarifa?
“Taarifa gani mama Joseph? Mama yake Happy akazidi kushangaa
“Ina maana hakuna hata mtu mmoja aliyekupigia simu kukueleza nini kimetokea leo?
“mama Joseph mbona unanichanganya? Nini kimetokea?
“Soma gazeti hili” akasema mama Joseph huku akimpa mama Happy gazeti lile alilokuwa amelishika mkononi.Mara tu mama Happy alipolitupia macho akaanguka na kupoteza fahamu
Mama joseph akapiga ukulele mkubwa uliomstua mzee Kibaho aliyekuwa chumbani na kumfanya atoke haraka na kuelekea sebuleni kuangalia kumetokea nini.Alistuka baada ya kumkuta mkewe akiwa ameanguka chini akiwa hana fahamu
“Nini kimetokea? Akauliza mzee Kibaho huku akimuinamia mkewe.Mama Joseph hakuweza kujibu chochote alikuwa anatetemeka huku machozi yakimtoka.Haraka haraka mzee KIbaho akaanza kumpatia mke wake huduma ya kwanza.
Kelele zile za mama Joseph,zilimstua pia Happy .Alizisikia kelele zile akiwa usingizini na mwanzoni alidhani labda alikuwa ndotoni lakini alipofumbua macho aliendelea kuzisikia.Akaogopa pengine kuna jambo baya limetokea pale nyumbani kwao. Kichwa kilikuwa kizito na mwili wake ulimuuma sana.Alisikia maumivu makali sana sehemu za kinenani lakini akajikaza na kuinuka na kukaa kitandani.Akafikiri kidogo halafu akavaa nguo na kutoka mle chumbani na kuelekea sebuleni ambako ndiko kelele zilikokuwa zinatokea.Alistuka baada ya kumuona mama yake akiwa amelala chini hana fahamu.Baba yake alikuwa anahangaika kumsaidia ili aweze kurejewa na fahamu.
Mama Joseph na mfanyakzi wa ndani Pendo walikuwa wanalia kwa uchungu.Mara tu mama Joseph alipomuona Happy ameingia pale sebuleni akazidi kulia.Happy akatamani ajue kilichokuwa kimetokea na kumpelekea mama yake apoteze fahamu,akamfuata mama Joseph na kumuomba anyamaze ili aweze kumueleza nini kilichotokea
“Mama mdogo kuna nini? Nini kimetokea hapa? ..akauliza Happy kwa sauti dhaifu lakini mama Joseph hakujibu kitu na badala yake akamuonyeshea ishara alichukue lile gazeti lilikokuwa limeanguka chini.Taratibu Happy akainama na kuliokota ,akalikodolea macho.Mwili wote ukamtetemeka alipokuwa analisoma.Alikuwa ni kama mtu aliyeliona jitu la kutisha.Mara gazeti lile likaanguka chini na uso wa Happy ukajaa machozi .Taratibu bila kuongea na mtu yeyote akageuka na kutembea kwa kasi kuelekea chumbani kwake.
Mama Joseph aliyekuwa anamuangalia Happy kwa makini ,akaogopa sana kutokana na mstuko alioupata Happy.Akamfuata mzee Kibaho na kumuomba amfuate Happy
“Kuna nini? Happy amefanya nini? Akauliza mzee Kibaho huku akiendelea na jitihada zake za kumpatia huduma ya kwanza mke wake ili aweze kurejewa na fahamu
Mama joseph akaliokota gazeti lililoanguka chini na kumpatia mzee Kibaho
“Hili ndilo chanzo cha haya yote” akasema mama Joseph
Mzee Kibaho akaanza kulipitia lile gazeti na mara akahisi mikono yake ikimtetemeka.
“Ouh My God !!!” akasema mzee Kibaho na kwa haraka akainuka na akaelekea chumbani kwa Happy.Mlango wa Chumba cha Happy ulikuwa umefungwa.Akagonga lakini hakukuwa na dalili zozote za kuwepo mtu ndani.Akachungulia katika tundu la funguo na kuiona funguo ikiwa ndani.
“Happy fungua mlango..Fungua mlango mwanangu …” akasema mzee Kibaho lakini hakusikia dalili zozote za kuwepo mtu mle chumbani.Kwa kasi akakimbia kuelekea chumbani kwake akachukua ufunguo wa akiba na kuja kuufungua mlango akaingia ndani
“Ouh Mungu wangu ..!!!!!..Mzee Kibaho nusura aanguke kwa alichokiona mle ndani.Happy alikuwa amelala kitandani huku mapovu yakimtoka mdomoni.
“Happy..!! Happy.!!! Happy.!!!!!...akapiga ukelele mzee Kibaho huku akimtikisa Happy lakini hakuwa na fahamu hata kidogo,alikuwa anakoroma.
“Ouh Mungu wangu !!” akasema mzee Kibaho baada ya kuiona chupa ndogo yenye dawa ya kuulia panya ikiwa mezani.Haraka haraka akamuinua Happy na kukimbia naye hadi garini.Mama Joseph na Pendo wakapiga ukeleel mkubwa baada ya kuishuhudia hali ile ya Happy.Mzee Kibaho hakuwajali akawasha gari lake na kwa kasi ya aina yake akaondoka pale nyumbani huku akipishana na majirani waliokuwa wakiingia kwa kasi mle ndani baada ya kusikia kilio cha mama Joseph na Pendo.
“Please God.dont let my daughter die, Please save her” mzee Kibaho ambaye kwa mbali macho yake yalilengwa na machozi ,alikuwa akiyarudia maneno haya mara kwa mara wakati akiendesha gari kwa kasi kuelekea hospitali.Kila sekunde zilivyozidi kusonga mbele ndivyo hali ya Happy ilivyozidi kubadilika na kupoteza matumaini.Alikuwa anakoroma na povu jingi likiendelea kumtoka
Geti la hospitali ya Brahmaputra inayomilikiwa na daktari bingwa Makhresh Patel lilikuwa wazi .Gari la mzee Kibaho lilikuwa likija kwa kwendo wa kazi huku likiwa limewasha taa zote.Watu waliokuwa wamesimama karibu na geti walikimbia baada ya kuliona gari lile namba lilivyokuwa likija.
Namna gari lile lilivyoingia hospitali na sauti za matairi yakilalama kutokana na breki kali aliyofungwa,iliwafanya madaktari na wauguzi watoke nje na kushuhudia nini kilichotokea.Mzee Kibaho akashuka na kukimbia na kuwataarifu wauguzi kwamba kulikuwa na mgonjwa mahututi ndani ya gari.Kwa kasi ya aina yake,wauguzi wakampakia Happy katika kitanda na kumkimbiza katika chumba cha wagonjwa mahututi.Mzee Kibaho akaombwa asubiri nje.Bado mwili wake ulikuwa unamtetemeka kupita kiasi.Aliogopa sana.
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
ITAENDELEA
.jpeg)