Simulizi: Miss Tanzania Sehemu ya 09

ADMIN
0


 ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA


Namna gari lile lilivyoingia hospitali na sauti za matairi yakilalama kutokana na breki kali aliyofungwa,iliwafanya madaktari na wauguzi watoke nje na kushuhudia nini kilichotokea.Mzee Kibaho akashuka na kukimbia na kuwataarifu wauguzi kwamba kulikuwa na mgonjwa mahututi ndani ya gari.Kwa kasi ya aina yake,wauguzi wakampakia Happy katika kitanda na kumkimbiza katika chumba cha wagonjwa mahututi.Mzee Kibaho akaombwa asubiri nje.Bado mwili wake ulikuwa unamtetemeka kupita kiasi.Aliogopa sana.


ENDELEA…………


“Please my Lord,don’t let my daughter die” akazidi kuomba mzee Kibaho.na mara simu yake ikaita.Alikuwa ni Margreth.Mzee Kibaho akavuta pumzi ndefu kabla ya kuipokea simu ile halafu akabonyeza kitufe cha kupokelea.


“Hallo Margreth” akasema mzee Kibaho


“baba uko hospitali gani?


“ niko hapa Brahmaputra hospital.Uko wapi Margreth?


“Nimefika hapa nyumbani sasa hivi nikaambiwa kuhusu hali ya Happy.Dady tell me please how’s she? Akauliza Margreth


“Tayari amepokelewa hapa na ameingizwa katika chumba cha wagonjwa mahututi.Madaktari wamesimamisha shughuli zote na wanajitahidi kuokoa maisha yake.”


“Unaonaje hali yake? Akauliza Margreth


“Margreth siwezi kusema chochote kwa sasa”


“sawa baba,nakuja sasa hivi huko hospitali” akasema Margreth


“Maggie mama yako anaendeleaje?


“Mama hali yake naye si nzuri hata kidogo.Amezinduka na kuzirai tena.Dokta Salome Yule jirani yetu yuko hapa anaendelea kumuhudumia.” Akasema Margreth.Mzee Kibaho akavuta pumzi ndefu na kukata simu


“Whats happening to my family? Ee Mungu naomba unipe nguvu ya kuweza kuyakabili matatizo haya makubwa yanayoikabili familia yangu kwa sasa.Naomba umsaidie mwanangu Happy aweze kupona” Mzee Kibaho alikuwa anaomba kimoyo moyo.Hakuweza kutulia sehemu moja.Alikuwa ni kama mtu aliyechanganyikiwa.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/


Margreth aliwasili Brahmaputra hospital na moja kwa moja akaelekea mahala alikokuwa baba yake.Macho yalikuwa mekundu kwa kulia


“baba kuna taarifa yoyote tayari umepata kuhusiana na Happy? akauliza Margreth


“Hakuna taarifa yoyote mpaka hivi sasa.Bado madaktari wanaendelea kumshughulikia.” Akasema mzee Kibaho.Jibu lile likazidi kumtoa machozi Margreth.Baba yake akamsogelea na kumkumbatia


“Please Margreth be strong.We need to be strong for Happy” akasema mzee Kibaho huku naye sauti yake ikionyesha kutetemeka


“Dady why could Happy do such a thing to us? Kwa nini aamue kunywa sumu? Akasema Margreth huku akilia


“I don’t know Maggie,I don’t know”


“Inauma sana baba.Sijawahi kuumia kama nilivyoumia leo.Hapa nilipo ninahisi moyo wangu unakatwa vipande vipande.Baba ninampenda sana Happy na sijui nitafanya nini kama hataweza kupona.Sijui kama nitaweza kuishi bila yeye” Margreth akaendelea kulia


“Tunatakiwa tujikite katika maombi tumuombee.Mungu atasikia vilio vyetu na atamponya Happy.I know Happy is strong and she’s going to fight this .She’ll fight for us and for all those who love her.” Akasema mzee Kibaho huku naye macho yake yakiwa na machozi.Margreth akatoa kijikaratasi toka katika mkoba wake na kumpatia baba yake


“Kikaratasi hiki kimekutwa chumbani kwa Happy.Ni ujumbe aliouacha”akasema Margreth.Mzee Kibaho akakunjua kikaratasi kile na kuanza kukisoma


“wakati mnausoma waraka huu tayari nitakuwa nimekwisha ondokewa na uhai.Nimechukua maamuzi haya magumu kutokana na kuchoshwa na aina ya maisha ninayoishi sasa.Mambo mengi yamenitokea ndani ya kipindi kifupi sana na nimeyavumilia yote lakini kwa hili lililotokea leo limenifadhaisha mno .Kwa ufupi tu ni kwamba jana nilitekwa na watu nisiowafahamu wakanipeleka mahala na wakanilazimisha kuyafanya haya mliyoyaona katika magazeti,kwa ajili ya kuokoa uhai wa Patrick.Sitaki kuliongeala sana suala hili lakini naomba mnifikishie ujumbe kwa Patrick kwamba nimekufa na yeye akiwa ni mwanaume pekee ninayempenda na sintaacha kumpenda hata huko niendako.Nilikubali kufanya haya kwa ajili ya kumuokoa yeye asiuawe.Nawapenda wote na ninawaomba mnisamehe kwa jambo hili ambalo najua litawaumiza sana lakini sina namna nyingine ya kuniondoa katika aibu hii kubwa zaidi ya kujitoa uhai…Kwa herini nyote”


Mzee Kibaho alishindwa kuyazuia machozi kumtoka baada ya kumaliza kuusoma ujumbe ule wa Happy


“Ee Mungu najua unaweza na haushindwi na lolote,nakuomba umponye binti yangu Happy.Mimi na familia yangu bado tunamuhitaji sana.Ni wewe tu ambaye unaweza kumuokoa toka kifoni kwa sasa.Naomba usikilize maombi ya familia yangu na Happy aweze kupona” Mzee Kibaho akaomba kimya kimya huku akijifuta machozi kwa kitambaa


Taarifa za Happy kutaka kukatisha uhai wake kwa kunywa sumu zilianza kusambaa kwa kasi baina ya ndugu na marafiki wa karibu wa familia.Wengi walianza kufika pale hospitali ili kujua kilichokuwa kinaendelea.


“Nilijua tu lazima kuna sababu iliyomfanya Happy afanye kitendo kile.Sikuamini kabisa kama Happy ambaye nimemlea na kumkuza katika maadili anaweza akatenda kitendo kama hiki cha kujidhalilisha kwa hiari yake.Ni nani huyo ambaye amemfanyia mwanangu unyama na udhalilishaji huu mkubwa? Huu ni udhalilishaji uliovuka mipaka.Happy ameshindwa kuvumilia na ndiyo maana akaamua kuchukua maamuzi haya aliyoyachukua.” Akawaza mzee Kibaho


“Aliyefanya jambo hili na kumdhalilisha mwanangu lazima atakuwa na lengo la kulipiza kisasi.Ninaanza kuhisi kwamba pengine jambo hili linahusiana na kifo cha Veronika kwa sababu kwa nini jambo hili litokee sasa? Lazima uchunguzi ufanyike na wale wote waliohusika na udhalilishaji huu walipe uovu wao.Lazima watu hawa wapatikane kwa namna yoyote ile.Nitahakikisha watu hawa wanakamatwa na hata kwa kuwatumia wapelelezi binafsi nitafanya hivyo.Niko tayari kutumia kiasi chochote cha fedha ili kuwasaka watu hawa waliomfanyia mwanangu jambo hili.” Akawaza mzee Kibaho.


* * * *


Mlio wa simu ukamstua Loniki toka usingizini.Akanyoosha mkono na kuichukua .Mpigaji alikuwa ni Linah


“Hallo Linah” akasema Loniki akiwa bado na usingizi


“Lonny bado umelala?


“Simu yako ndiyo iliyonistua.Jana niliporudi nilikunywa sana mvinyo na ndiyo ulionipelekea kulala namna hii” akasema Loniki


“Lonny umepata habari?


“Habari gani tena wakati wewe ndiyo mtu wa kwanza kuongea naye leo?


“Dah ! mambo tayari yameanza”


“mambo gani tena Linah?


“Leo jiji zima limeamshwa na habari moja tu.Habari ya Happy”


“Tayari habari yake imeshatoka? Akauliza Loniki na kuinuka akakaa


“Chezea Khumalo wewe .! akasema Linah huku akicheka.


“Khumalo amekwishamaliza kila kitu na hivi nikwambiavyo gazeti la Mitikisiko limekwisha na halipatikani tena mtaani.Katika mitandao ya kijami,taarifa inayozunguka hivi sasa ni hii ya Happy.Kila mtandao zimetapakaa picha na video ya Happy”


“Dah ! nashukuru sana kama kazi imekamilika.Nadhani hivi sasa kama Happy atakuwa amezipata taarifa hizi atakuwa katika maumivu makali sana kama niliyonayo mimi .Baada ya kummaliza Happy sasa tutahamia kwa Patrick” akasema Loniki.


“Lazima nihakikishe wale wote walioudhulumu uhai wa mdogo wangu wanalipa.They all must pay.This is just the beginning…” akasema Loniki


“Lonny nina imani ushauri huu alioutoa Khumalo ni wa busara sana kwani endapo Happy ataziona picha zile ni wazi ataumia mno .Ni picha zenye kudhalilisha sana.”


“Kweli kabisa Linah.Ninaanza kukubaliana na Khumalo kwamba unaweza usimuue mtu moja kwa moja lakini ukampa mateso makali ya moyo na akateseka katika maisha yake yote.Kwa mfano Happy,kwa sasa maisha yake hayatakuwa sawa tena.Tayari ameingia katika kashfa nzito na hii itamtesa katika maisha yake yote yaliyobaki.Pamoja na hayo Linah kuna jambo nataka kukuuliza”


“Uliza Lonny”


“Khumalo ni mtu wa namna gani? Anajishughulisha na nini? Na kile chumba alichowekwa Happy kina kazi gani hadi kikafungwa kamera za kisasa namna ile?


Linah akavuta pumzi ndefu halafu akasema


“Kwa kuwa wewe ni rafiki yangu nitakueleza lakini naomba mtu mwingine yeyote asifahamu.Khumalo anajishughulisha na biashara nyingi haramu ikiwamo ya madawa ya kulevya na hata shughuli kama hii uliyompa na wakati mwingine hata ujambazi wa silaha huwa anahusika pia.Kwa sasa ameamua kujikita zaidi katika biashara ya madawa ya kulevya ambayo ndiyo inayomuingizia fedha nyingi sana.Ukiacha biashara hiyo ya dawa za kulevya,hukitumia kile chumba alichowekwa Happy kwa ajili ya kurekodi filamu za ngono ambazo huziuza katika nchi za ulaya na Amerika na kujipatia fedha nyingi.Huwatafuta mabinti wazuri wa kiafrika na kuwalipa pesa nyingi halafu huwarekodi wakifanya ngono.Hii ndiyo kazi ya chumba kile.Lonny tutaongea zaidi baadae kwa sasa kuna mahala ninawahi” akasema Linah


“Ok Linah.Nitakuja ofisini kwako baadae.Ahsante kwa taarifa” akasema Lonny na kukata simu


“Ouh gosh !!Sasa moyo wangu unaanza kupata amani.I cant imagine how painfull Happy is right now.Picha ndo kwanza linaanza.Nitahakikisha wale wote waliohusika kusababisha kifo cha Vero wanalipa.Japokuwa ni gharama kubwa lakini nitajitahidi kufanya kila niwezavyo hadi nihakikishe nimemilipia kisasi mdogo wangu.” Akawaza Loniki huku akitoka mle chumbani


* * * *CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/


Akiwa bado katika mapumziko huku akiendelea na shughuli zake za usafi asubuhi hii,Sarah hakuwa na habari juu ya kilichokuwa kinaendelea hadi pale jirani yake alipoingia akiwa na gazeti mkononi na kumstua.


“Shoga yangu huyu si miss Tanzania aliyevunja uchumba wa Vero? Akasema shoga yake Sarah huku akimpa Sarah lile gazeti.Sarah akafuta maji mkononi na kulichukua gazeti lile


“Ouh My God ..!!! “ akasema Sarah kwa mshangao.Taarifa ile ilimstua mno.Mikono yake ilikuwa inamtetemeka.


“Hakika malipo ni hapa hapa duniani.Amemzuia mwenzake asiolewe halafu kumbe huu ndio uchafu anaoufanya.Dah ! ameumbuka sana” akasema Yule shoga yake Sarah


“Hapana..!!..Hii si sahihi.Sidhani kama Happy anaweza akafanya kitendo kama hiki.Lazima hapa kuna namna iliyofanyika ili kumzalilisha .Lazima kuna mkono wa mtu hapa na kama ndiyo hivyo mtu huyo si mwingine atakuwa ni Loniki.Ni yeye peke mwenye chuki na Happy na aliweka dhamira ya kulipiza kisasi na ninadhani hii ni moja ya mipango yake.” Akawaza Sarah.


“Mbona uko kimya Sarah? Akauliza Yule shoga yake


“Nimestushwa sana na taarifa hii.” Akasema Sarah na kuingia ndani akachukua funguo za gari lake na kuondoka kwa kasi


“Nina hakika mkubwa Loniki anahusika kwa kiasi kikubwa na jambo hili la udhalilishaji.Lazima leo hii niufahamu ukweli.Kwa nini anataka kuendeleza uhasama usiokuwa na faida yoyote kwetu? Hapana siwezi kukubali jambo hili liendelee” akawaza Linah


“Ninahisi hata zile fedha ambazo mama aliniomba jana na kisha akampatia Lonny,alikuwa anazihitaji kwa ajili ya kutekeleza mipango yake hii miovu.Ninahisi hata mama naye atakuwa anahusika kwa namna fulani na jambo hili.Kuna kitu atakuwa anafahamu kuhusiana na mipango ya Lonny ya kulipiza kisasi.Kama ni kweli Lonny atakuwa amehusika katika kumdhalilisha Happy namna hii ,kamwe sintaweza kumsamehe .” akawaza Sarah


Mama yake sarah alikuwa amekaa nje ya nyumba yake na pembeni yake kulikuwa na meza ndogo iliyokuwa na chupa kubwa ya chai.Alistuka alipomuona Sarah akiingia pale ndani akiwa na uso uliojaa hasira


“Mama shikamoo” akasema Sarah


“Marahaba Sarah.Mbona hivyo? Kwema huko utokako?


“Kwema mama” akajibu Sarah halafu akalitoa gazeti lile la mitikisiko na kumpatia mama yake


“mama hebu niambie unafahamu chochote kuhusiana na jambo hili?


Mama yake akalichukua gazeti lile akalitazama na kustuka sana


“Ouh Mungu wangu..!!


“Hii ni kashfa kubwa sana”


“kweli mama ni kashfa kubwa mno.Nina hakika Loniki anahusika na jambo hili” akasema Sarah


“Loniki .!! mama yake akashangaa


“Ndiyo mama .”akasema Sarah


“Hapana Sarah.Loniki hawezi kuhusika na jambo kama hili”


“Mama humjui vizuri Loniki.Nina hakika lazima atakuwa anahusika na jambo hili.Aliapa kwamba atalipiza kisasi kwa Happy na wale wote waliohusika na kifo cha Vero.”


“Hapana Sarah.Sikubaliani nawe kwa hilo .Ni kweli Lonny ameumizwa sana na kifo cha vero lakini sidhani kama atakuwa anahusika kwa namna yoyote na jambo hili.Hii ni tabia ya Happy mwenyewe .Amemdhulumu mwanangu na haya ndiyo yanayomkuta sasa.”


“mama pesa ulizoniomba jana zilikuwa za kazi gani?


“Sarah naomba usitake kuyafahamu mambo yangu binafsi.Kama umeifuata pesa yako nitakurejeshea baadae kama nilivyokwambia” akasema mama yake kwa ukali


“mama sijaja hapa kufuata fedha.Nimekuja kutak…………….” Sarah akastuka baada ya Loniki kutokea ghafla


“Mbona kuna mabishano hapa? Akauliza Loniki huku akiangaliana na Sarah kwa macho makali


“Niambie uhusiki katika jambo hili ?” akasema Sarah huku akimpa Loniki gazeti ambaye alilichukua akalipitia kisha akaangua kicheko kikubwa.


“Haya ndiyo malipo ya udhalimu wake.Yeye na yule mshenzi wake Patrick walimdhulumu Vero uhai wake.Ona sasa alivyoumbuliwa na magazeti..” Akasema Loniki huku akicheka.Sarah akamtazama kwa hasira


“Mbona unanitazama hivyo Sarah? Hufurahi kwa kilichompata mtu aliyemuua mdogo wako?


“Kwa nini nifurahi? Happy si adui yangu na wala sintajenga uadui naye hata mara moja.Hata kama alihusika na kifo cha vero ,lazima niuheshimu utu wake.Kitendo cha kumdhalilisha namna hii hakivumiliki hata kidogo.”


“ Nilijua tu.Huna uchungu wowote kwa kifo cha Vero na ndiyo maana kila mara umekuwa upande wa Patrick na Happy.naomba nikufahamishe kwamba Happy anastahili kudhalilika namna hii.Anastahili kuumia kama tulivyoumia sisi kwa kufiwa na mdogo wetu.Huu ni mwanzo tu na bado ataumia sana.Mengi bado yatamkuta yeye na huyo shetani mwenzake Patrick”


Sarah alishindwa kumvumilia dada yake akamsogelea karibu


“Loniki wewe ni ndugu yangu wa damu lakini ninakuonya kwamba nitafanya uchunguzi wangu na endapo nitagundua kwamba unahusika kwa namna yoyote ile na jambo hili .I swear in heaven and earth I will never forgive you.”


“Utanifanya nini? Akauliza Loniki kwa ukali


“Utafahamu wakati utakapofika.”


“Go to hell sarah.Tena nakuomba uuchunge sana mdomo wako usije ukakuponza.Mimi si mtu wa kunyooshewa kidole kama unavyofanya.Kama ni mapambano niko tayari kupambana nawe na siogopi hata kama wewe ni ndugu yangu.Ninaweza nikakufanyia kitu kibaya sana na usiamini Sarah.”


Ilimlazimu mama yao kuingilia kati na kuwaamua wanae wale ambao walikuwa wanatoleana maneno makali.Sarah hakutaka tena kukaa pale nyumbani akapanda gari na kuondoka zake kwa hasira


* * * *


Savanna hakuwa mpenzi sana wa kusoma magazeti.Hii ilitokana na kuwa na kazi nyingi kiasi cha kukosa muda wa kupitia habari magazetini.Akiwa ofisini kwake akikamilisha baadhi ya kazi zake za kila siku asubuhi kabla ya kuelekea gereza la Uwangwa kuonana na Patrick,mara mmoja wa watumishi wa ofisi yake akaingia akiwa na gazeti mkononi.


“Savanna ,najua hupendi kusoma magazeti lakini naomba uchukue dakika chache upitie gazeti hili” akasema Edson mmoja wa mawakili wanaomtetea Patrick


“Edson toka lini umeniona nikipata muda wa kusoma magazeti? Ninataka kuelekea gerezani kuonanana na Patrick halafu nije niendelee na shughuli zangu nyingine” akasema Savanna


“Naomba usome Savanna.” Akasisitiza Edson na kuliweka gazeti lile mezani.Savanna akavutiwa na kichwa cha habari akalichukua ili alisome na ghafla akalitupa mezani


“Ouh My Gosh !!!... akasema Savanna kwa mstuko


“Bado siamini.Happy anaweza akafanya uchafu wa namna hii kweli? Happy huyu ninayemfahamu mimi? No..!! thats not true..!!!” akasema Savanna


“Ni kweli Savanna.Ukiacha picha hizi kuna video yake pia ambayo imesambaa mitandaoni.” Akasema Edson huku akiisogelea kompyuta ya Savanna akaifungua video ile ya Happy .Savanna akaitazama video ile na kujikuta mdomo wazi.


“Ouh gosh !! ..Ni vigumu kuamini.Happy kweli anaweza akafanya mambo ya aibu namna hii? Akasema Savanna na kujikuta akiishiwa nguvu miguuni,akakaa kitini.


“Usishangae Savanna.Siku hizi umezuka mtindo wa mabinti hasa hawa maarufu kujirekodi wakifanya ngono au kupiga picha za utupu kisha huzihifadhi kwa ajili ya kumbu kumbu zao wenyewe lakini ikitokea zikashindwa kuhifadhiwa vizuri na zikaingia katika mikono ya watu wabaya ,huziuza kwa waandishi wa habari kwa fedha nyingi ambao hutengeneza mamilioni ya fedha katika magazeti yao kwa kuichapisha habari hiyo” akasema Edson.Savanna akainama akafikiri halafu akachukua simu yake na kumpigia Margreth.


“Hallow “ akasema Margreth baada ya kupokea simu.Savanna akastushwa kidogo na sauti ya Margreth


“Margreth,sauti yako inaonyesha kama unalia.Unaumwa? akauliza Savanna .Margreth akashindwa kukizuia kilio chake akalia kwa nguvu


“Margreth nini kimetokea? Please tell me”


“Its…..it’s….” Margregth akashindwa kuongea akaangua kilio tena


‘Margreth nini kimetokea? Tafadhali naomba unieleze”


“Its Happy….!!


“Happy kafanya nini?


“Amekunywa sumu” Margreth akajibu halafu kikapita kimya cha sekunde kadhaa.Savanna akabaki mdomo wazi akashindwa aseme nini.Akameza fundo la mate na kusema


“Margreth tafadhali naomba uniambie ukweli”


“Ni kweli Savanna.Happy amekunywa sumu “


“So how’s She? Where ae you now?


“Niko hapa Brahmaputra hospital.She’s in critical condition fighting for her life “


“Ouh gosh ! ,nakuja sasa hivi” akasema Savanna na kukata simu kisha akachukua mkoba wake na kutoka kwa kasi hadi katika gari lake na kuondoka kuelekea hospitali.


“haya mambo mbona yanazidi kuchanganya? Jana nimepigiwa simu Happy haonekani lakini leo hii amekunywa sumu.Kitu gani kinaendelea hapa? Akawaza Savanna akiwa katika mwendo mkali kueleka hospitaliCHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/


“Masikini Patrick,sipati picha atakuwa katika hali gani mara atakapozipata taarifa hizi.Sifahamu atachukua maamuzi gani lakini nafahamu lazima ataumia sana.” Akawaza Savanna


Baada ya kuwasili Brahmaputra hospital Savanna akakutana na familia ya Happy


“Shikamoo baba”


“Marahaba Savanna hujambo?


“Sijambo baba. Poleni sana” akasema Savanna halafu akamuomba mzee Kibaho wakaongee pembeni


“Nini kimetokea ? Happy anaendeleaje? Akauliza Savanna.Mzee Kibaho akakohoa kidogo halafu akasema


“Unakumbuka nilikupigia simu jana usiku nikitaka kufahamu kama unaweza ukafahamu lolote kuhusu mahala aliko Happy kwani hadi wakati ule ninakupigia hakuwa amerejea na hata simu yake haikuwa inapatikana kitu ambacho si kawaida yake.” Akasema mzee Kibaho


“Nakumbuka baba.Happy nilikutana naye jana asubuhi gerezani akiwa na Patrick.Nilipoingia nikiwa nimeongozana na familia ya Patrick yeye akaondoka na hatukupata muda wa kuongea.Nini kilitokea? Alikuwa wapi? Akauliza Savanna


“Mida ya kama saa nane hivi za usiku nilisikia muungurumo wa gari nje ya nyuma.Nilipotoka nje ya nyumba nilikuta gari la Happy na yeye akiwa ndani yake lakini akiwa hoi hajitambui.Hatukujua nini kilimpata kwa sababu alionekana ni kama mtu aliyelewa.Tulimuita dokta wa familia akaja mara moja na kumpatia huduma na alipopata nafuu akatuomba tumuache akapumzike.Hakutueleza alikuwa wapi na wala nini kilimpata.Asubuhi ya leo nilisikia mtu akilia sebuleni nikaenda kutazama nini kimetokea nikamkuta mke wangu akiwa amezirai.Wakati tukimpatia huduma ili azinduke akatokea Happy na kuliokota gazeti lililokuwa limeanguka chini.Ghafla akalitupa na kuelekea chumbani kwake.Nililitazama gazeti lile nikastuka sana.Nilimfuata Happy chumbani kwake lakini mlango ulikuwa umefungwa,ikanilazimu kuchukua ufunguo wa akiba nikaufungua mlango na kumkuta Happy akiwa hana fahamu na povu jingi likimtoka mdomoni.Alikunywa sumu ya kuulia panya.Nimemkimbiza hapa hospitali na toka nilipomfikisha hapa madaktari wanaendelea kumshughulikia.Shughuli zote hapa hospitali zimesimama kwa muda madaktari wote wanaendelea kumuhudumia Happy.Vile vile Happy aliacha ujumbe huu” mzee Kibaho akampatia Savanna ujumbe ule aliouacha Happy.Savanna akaupitia ujumbe ule na kisha akatoa kitambaa mfukoni na kuyafuta machozi


“Nilijua tu ,Happy hawezi kufanya jambo kama lile kwa hiari yake mwenyewe.Nilijua tu lazima jambo hili lina mkono wa mtu.Ni nani huyo ambaye anaweza kuwa amefanya unyama wa namna hii? Akasema Savanna


“Hakuna ajuaye ni nani muhusika wa jambo hili.Anayefahamu ni Happy pekee.Tuombe Mungu apone na atufahamishe ni nani hawa waliomfanyia kitendo hiki.Lazima wafikishwe katika mkono wa sheria“ akasema mzee Kibaho


“Ni kweli baba watu hawa waliohusika na udhalilishaji huu lazima walipe uovu wao.lazima wafikishwe katika vyombo vya sheria.” Akasema Savanna halafu kikapita kimya kifupi


“Savanna wewe ni wakili”


“Ndiyo baba”


“Naomba ushauri wako wa kisheria kuhusu kitendo hiki cha Happy.Hiki kitendo alichokifanya Happy cha kutaka kujiua ni kosa kisheria?


“Ni kweli baba,hiki ni kitendo cha kijinai.Kwa mujibu wa sheria ya kanuni za adhabu sura ya ishirini na mbili kifungu cha 217 kinachosema mtu yeyote anayejaribu kujiua ana hatia ya kosa.Iwapo suala hili litafuatiliwa na vyombo husika Happy anaweza kukabiliwa na adhabu


“Ouh My Gosh ..!!! what am I going to do ? akasema kwa masikitiko mzee Kibaho.Savanna akamtazama mzee Yule kisha akasema


“Baba kuna jambo ambalo tunatakiwa kulifanya kwa sasa”


“Jambo gani hilo savan?


“Kwanza nataka kufahamu kama suala hili limekwisha ripotiwa katika vyombo vya usalama.”


“Hapana Savanna.Suala hili halijaripotiwa sehemu yoyote ile na tunaofahamu ni sisi familia yake pamoja na ndugu wachache pamoja na majirani”


“Vizuri sana.Tunachotakiwa kufanya kwa sasa ni kulifanya suala hili kuwa siri kubwa na kuhakikisha hakuna mwandishi wa habari anayezipata taarifa hizi.Ongea na uongozi wa hospitali hii ili hata kama ikitokea watahojiwa na vyombo vya habari au usalama wasiweke wazi kwamba Happy alijaribu kujiua kwa kunywa sumu.Baada ya hapo itabidi tufanye jambo la haraka sana kwa Happy”


“Jambo gani hilo? Akauliza mzee KIbaho


“Najua hautalipenda lakini hakuna jinsi ninabidi lifanyike tu”


“Niambie Savanna.Niko tayari kufanya lolote hivi sasa kwa ajili ya Happy” akasema mzee KIbaho.Savanna akamtazama kwa sekunde kadhaa halafu akasema


“I wapo Mungu atamsaidia akapona We have to take her away from here as quick as possible”


Mzee Kibaho akastuka kwa maneno yale ya Savanna




“Baba najua umestuka sana kwa maneno haya lakini naomba uniamini haya nikwambiayo kwamba endapo Mungu atamjalia Happy uzima,tunatakiwa kumuondoa Happy hapa nchini haraka sana”


“Kwa nini unashauri hivyo ? Akauliza mzee Kibaho


“Jambo hili lililotokea si jambo dogo kama unavyoliona na hadi hivi sasa tayari limemuathiri Happy kwa kiasi kikubwa.Taswira yake katika jamii imeharibiwa na habari hii ya leo.Kwa maana hiyo basi anatakiwa kupata sehemu tulivu yenye uangalizi makini ili aweze kupatiwa msaada wa kisaikolojia na akili yake iweze kutulia.Kuendelea kumweka hapa ni kumuongezea maumivu na kutaendelea kuhatarisha usalama wake.Vile vile kumuondoa hapa kutasaidia kumuepushia mashtaka ya kijinai.Najua hili si suala jepesi lakini inatubidi tushirikiane sote kwa faida ya Happy” akasema Savanna.Mzee Kibaho akavuta pumzi ndefu .Alionekana kama amechanganyikiwa


“I don’t know what I’m going to do” akaongea peke yake.Baada ya dakika mbili za tafakari akamgeukia Savanna


“Savanna mawazo yako naona yana msingi sana.Nina mdogo wangu anaishi Mtwara.Nadhani itakuwa vyema kama nitampeleka kule akakae kwa muda”


“Hapana baba.Mtwara bado ni Tanzania.Happy anatakiwa aende mahala ambako hakuna mtu anayemfahamu mahala ambako atapata msaada wa kisaikolojia na kumsaidia kurejea katika hali yake ya kawaida.Hapa nchini Happy ana jina kubwa na anafahamika kila kona”


“Savanna suala hili linahitaji muda wa kutosha kulifanyia maandalizi.Inabidi nikae na familia yangu baada ya kujua maendeleo ya Happy na kwa pamoja tujadili suala hili ndipo tufikie maamuzi “ akasema mzee Kibaho huku akionekana ni mwenye mawazo mengi sana


“Mzee wangu nakubaliana na wazo la kukaa na kufanya maamuzi kama familia .Pamoja na hilo naomba na mimi nitoe mchango wangu.Iwapo mwenyezi Mungu atamjalia Happy uzima na iwapo mtakubaliana na mawazo yangu basi ninapendekeza Happy asafirishwe kwenda Kigali Rwanda.Mimi nitagharamia gharama zote za safari.Nitakodisha ndege binafsi hadi Kigali.Pale Kigali nina rafiki yangu aitwaye Christine umuhiza ambaye ndiye atakayemuhudumia Happy kwa kipindi chote atakachokuwa pale.Vile vile ninafahamiana na mmiliki wa hoteli moja iitwayo Reonald Hotel.Ni hoteli mpya na kubwa pale Kigali yenye hadhi ya nyota tano.Nitafanya mpango ili Happy aweze kukaa hotelini hapo kwa muda wote atakaouhitaji akiwa katika chumba chenye hadhi ya rais.Christine atamtafutia daktari ambaye atamsaidia kumtibu na vile vile tutamtafutia daktari wa masuala ya kisaikolojia “ akasema Savanna.Mzee Kibaho aliyekuwa anamsikiliza kwa makini akakohoa kidogo na kusema


“Savanna mimi binafsi nimeumizwa sana na jambo hili na kwa mantiki hiyo basi niko tayari kufanya jambo lolote lile ambalo litakuwa na msaada kwa Happy.Sipingani hata kidogo na wazo lako la kumpeleka Happy nje ya nchi.Ninachotaka kufahamu ni iwapo Happy ataondoka hapa nchini kwa ajili ya kumsaidia kwanza kumuepusha na aibu hii na pili kumuepusha na mkono wa sheria kwa kosa la kujaribu kujiua, nini itakuwa hatima ya watu waliomtenda hivi? Sitakuwa na amani hadi nihakikishe kwamba watu waliomfanyia mwanangu kitendo hiki cha kinyama wamekamatwa ,wamefikishwa katika mkono wa sheria na wameadhibiwa kutokana na kitendo walichokifanya.Lakini ninajiuliza maswali mengi hilo litawezekana vipi wakati Happy akiwa nje ya nchi? Nataka jina la mwanangu lisafishwe .Nataka umma wa watanzania wafahamu nini kilitokea na kwamba mwanangu hawezi kufanya kitendo kama kile kwa ridhaa yake.” Akasema mzee Kibaho


“Baba hayo yote unayoyasema ni ya msingi sana lakini tukumbuke kwamba ni Happy pekee ambaye anawafahamu watu hao na ambaye anaweza akatusaidia kuwatambua watu hao na anaweza akafanya hivyo pale ambapo akili yake itakuwa imetulia .Mimi binafsi nakuahidi ushirikiano wangu wa dhati katika suala hili na mara tu watakapogundulika watu hawa nakuahidi kwamba kesi hiyo nitaisimamia mimi mwenyewe na kuhakikisha kwamba wanapata adhabu kali sana”


Kabla mzee Kibaho hajasema chochote,akatokea Margreth na kumtaarifu baba yake kwamba anahitajika na daktari.Kwa haraka wote watatu wakaongozana kuelekea katika ofisi ya daktari


“karibuni sana” akasema daktari mkuu wa hospitali hii ambaye ana asili ya India lakini anakifahamu vizuri sana Kiswahili


“Poleni sana kwa matatizo” akasema daktari.Wote watatu nyoyo zao zilikuwa zinawadunda wakisubiri taarifa ya daktari


“Jamani nimewaiteni hapa ili kuwapeni taarifa kuhusiana na maendeleo ya mgonjwa wenu.Kwa ujumla ni kwamba Happy alikuwa amekunywa dawa ya kuulia wadudu ambayo ni sumu katika mwili wa binadamu.Ninakushukuru sana mzee wangu kwa jitihada zako za kumfikisha mapema hapa hospitaloi kabla sumu ile haijasababisha madhara makubwa mwilini.Tulimpokea Happy akiwa katika hali mbaya na tumefanya kila jitihada ili kumuondoa katika hali ya hatari ya kupoteza maisha.Tunapaswa kumshukuru sana Mungu kwani tumefanikiwa katika hilo.Kwetu sisi tunaona ni kama muujiza kutokana na hali aliyokuwa nayo Happy.Tumefanikiwa kuiondoa sumu iliyoko mwilini mwake kwa kutumia mtambo wetu maalum ambao ni mpya kabisa wa kuondoa sumu ya aina yoyote mwilini.Kwa sasa ninaweza kutamka kwamba Happy hayuko tena katika ile hatari ya kupoteza maisha na endapo litatokea jambo kama hilo basi itakuwa ni kwa mapenzi ya Mungu lakini napenda kuwahakikishia kwamba tumemuondoa katika hatari hiyo.” Akasema daktari na wote watatu wakashusha pumzi .Mzee Kibaho akajifuta jasho lililokuwa linamtiririka kwa wingi


“Zoezi linaloendelea kwa sasa ni kuipitisha damu yake katika mtambo maalum wa kuchuja sumu ili kuweza kujiridhisha zaidi kwamba hakuna kiasi chochote cha sumu kitakachobaki mwilini mwake.Kwa hiyo nawasihi ndugu zangu,ondoeni wasi wasi mliokuwa nao.Happy yuko salama na anaendelea vizuri.Zoezi hili litakapomalizika tutamuondoa katika chumba cha wagonjwa mahututi na kumpeleka katika sehemu ya uangalizi maalum ili kuangalia maendeleo yake.”


“Ouh Thanx God” akasema mzee Kibaho huku akiinua mikono yake juu kumshukuru Mungu


“Daktari zoezi hilo la uchujaji wa sumu litachukua muda gani? Akauliza Savanna


“Ni muda wa masaa manne”


“Mzee wangu nini hasa kilichopeleka binti mdogo kama huyu kutaka kukatisha uhai wake? Nini kimemsibu ili tuone namna ya kumpatia msaada wa kisaikolojia na asiweze kurudia tena kufanya kitendo cha hatari kama hiki? akauliza daktari.Mzee Kibaho akakohoa kidogo na kusema


“Happy ni binti yangu wa kwanza.Hivi karibuni alifanikiwa kutwaa taji la Miss Tanzania.Baada ya kulinyakua taji hilo ndipo matatizo yalipoanza.Yote haya yamesababishwa na mgogoro wa kimapenzi uliopekeka msichana aliyekuwa akizozana naye kufariki dunia.Leo asubuhi katika gazeti moja la udaku kumechanpishwa picha za Happy za faragha.Ni picha zenye kuumiza sana na zote hizi ni njama za wabaya wake za kutaka kumchafua.Jambo hilo ndilo lililopelekea aamue kujaribu kukatisha uhai wake kwa kunywa sumu.” Akasema mzee Kibaho


“Poleni sana.Hii inaonyesha ni jinsi gani dunia ilivyobadilika hivi sasa.watu wamekosa huruma na wako tayari kufanya jambo lolote lile kwa manufaa yao bila kupima athari zinazoweza kujitokeza.Poleni sana ,lakini kitu ninachoweza kuwaambia ni kwamba Happy anahitaji msaada wa kisaikolojia.Hapa tunao madaktari wazuri sana wa masuala haya ya akili.Tunacho kitengo hicho hapa cha kuasadia watu wenye matatizo kama ya Happy.Ninawashauri kwamba baadaya hali yake kuwa nzuri basi tuendelee kumpatia msaada wa kisaikolojia hapa hapa hospitalini kwetu” akasema daktari


“Nakubaliana nawe daktari kwani inaonyesha wazi kwamba binti yangu ameathirika kisaikolojia na anahitaji msaada .Lakini kuna jambo ninataka kukuomba.Kwa mujibu wa sheria ,kitendo hiki alichokifanya Happy ni kosa la kijinai kwa hiyo kuna uwezekano endapo vyombo vya kisheria vikazipata taarifa hizi vikamfungulia mashitaka,kwa hiyo tunakuomba daktari ,jambo hili libaki kuwa siri na asifahamu mtu mwingine yeyote yule awe ni mwandishi wa habari au afisa wa polisi.Unaweza ukaandika ugonjwa mwingine wowote lakini si sumu.Jambo la pili ambalo tumekusudia kulifanya kwa haraka ni kumuhamishi Happy nje ya nchi haraka iwezekanavyo.mahala ambako hakuna mtu yeyote anayemfahamu.Nadhani hii itakuwa ni njia nzuri sana ya kumsaidia kumuondoa katika mazingira haya na wakati huo huo tukiendelea kumpatia msaada wa kisaikolojia.” Akasema mzee Kibaho


“Kwanza kabisa kuhusiana na kutoa taarifa kuwa vyombo vya habari na vile vya usalama,msiwe na hofu.Nitawasaidia katika hilo.Pili kuhusiana na suala la kumpeleka Happy nje ya nchi ni suala zuri sana lakini nina wasi wasi kidogo.Happy anahitaji bado kuwa katika uangalizi wa madaktari.Kama ni kumuondoa hapa nchini basi itawabidi msubiri kidogo hadi hapo hali yake itakapoboreka kabisa.”


“Inaweza kuchukua muda gani daktari? Akauliza Savanna


“Inaweza kuchukua zaidi ya wiki moja”


“Daktari tunahitaji kumuondoa Happy nchini leo hii.”


“Kwa leo haitawezekana kumsafirisha Happy” akasema Daktari


“Daktari naomba ufanye kila linalowezekana ili tuweze kumuondoa Happy hapa nchini siku ya leo” akaendelea kusisitiza Savanna


Daktari akafikiri kidogo na kusema


“Kama mkihitaji hivyo basi ni lazima pawepo makubaliano maalum”


“makubaliano gani hayo? Akauliza Savanna


“Baada ya zoezi la kuchuja sumu kukamilika mgonjwa anatakiwa apumzike kabla ya zoezi lingine lolote kufanyika.Endapo mtahitaji kumsafirisha Happy kwa siku ya leo,itawalazimu kumsafirisha na mmoja wa madaktari wetu kitu ambacho kitawaongezea gharama zaidi kwa hiyo nawashauri mngesubiri hadi hapo Happy atakapokuwa amepata nafuu ndipo mumsafirishe”


“Daktari hilo ulilolisema si tatizo kwetu hata kidogo kwani tunatumia ndege ya kukodi.Tunaelekea jijini Kigali Rwanda.Usijali kuhusu gharama.Tutakulipa pesa zote zitakazotakiwa ikiwa ni pamoja na kumuhudumia daktari huyo hadi hapo Happy atakapopata nafuu.” Akasema Savanna


“Kama mko tayari kwa hilo mimi sina shida yoyote.Kwa sasa naombeni mnipe nafasi nikakutane na jopo la madkatari wangu ili kwa pamoja tuweze kushauriana namna bora ya kuweza kulifanikisha jambo hili” akasema daktari.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/


“Usijali daktari.Sisi pia ngoja tukajiandae kwa safari.Naomba hesabu ya gharama zote unitumie kwa kupitia namba hizi hapa” akasema Savanna huku akimpatia daktari kadi yake yenye namba za simu halafu wakatoka mle ofisini.


“Baba mpango huu wa kumpeleka Happy Kigali umetoka wapi? Mbona hakuna aliyekuwa anafahamu kama kuna mpango kama huu? Akauliza Margreth baada ya kutoka ofisini kwa daktari


“Margreth samahani kwa kulisikia jambo hili kabla ya kutaarifiwa.Ni kwamba Savanna alikuja na wazo hili la kutaka kumuhamisha Happy na kumpeleka nje ya nchi ili kumuweka mbali na mazingira haya.Endapo ataendelea kukaa hapa wakati tayari jina lake limekwisha chafuka ataendelea kuumia zaidi.Ni bora ikiwa atakwenda kukaa mbali na hapa,mhala ambako hafahamiki kabisa.Hii itamsaidia sana kumsahaulisha kilichotokea”


“Ni mpango mzuri baba lakini maandalizi yanakwendaje manake nimemsikia Savanna akisema kamba Happy atapelekwa Kigali.Imekuwa ghafla sana na nina wasi wasi kama kuna maandalizi yoyote yaliyofanyika”


“Margreth,usihofu chochote kuhusiana na jambo hilo.Pale Kigali kuna hoteli moja kubwa ya nyota tano ambayo mmiliki wake tunafahamiana vyema na ndipo Happy atakapofikia na kukaa yeye na watu atakaoambatana nao hadi hapo hali yake itakapokuwa nzuri.Kuhusu usafiri nitagharamia mimi ,nitakodisha ndege hadi Kigali “


* * * *


Saa tano na dakika ishirini za usiku familia ya Happy ikaruhusiwa kuingia katika chumba alichokuwa amelazwa Happy.Tayari alikwisha amka toka saa mbili za usiku lakini madaktari hawakuruhusu aonane na mtu yeyote hadi hapo atakapokuwa amerejewa na fahamu zake kamili


Mara tu alipoiona familia yake ikiingia mle chumbani wakiongozwa na baba yake mzee Kibaho Happy alishindwa kujizuia akaanza kulia.


“Ouh Happy mwanangu” akasema mama yake huku akiinama na kumkumbatia wote wawili wakilia.


“Mungu ahsante kwa kumponya mwanangu” akasema mama yake Happy. Happy akasalimiana na baba yake mzee Kibaho na halafu mdogo wake Margreth na ghafla akastuka baada ya kugonganisha macho na Savanna


“Pole sana Happy” akasema Savanna.Happy akashindwa ajibu nini,donge kubwa likamkaba kooni.Savanna alilitambua hilo akatoka nje ya kile chumba.


“what is she doing here? Baba kwa nini umemleta Savanna hapa? Akauliza Happy


“Usijali Happy,Savanna tuko naye kutwa nzima ya leo tukishughulikia suala hili.Amekuwa ni msaada mkubwa kwetu katika wakati huu mgumu tulionao.Ametupa ushirikiano mkubwa sana.” Akasema mzee Kibaho


“Dady I don’t want to see her here.That woman is a devil.She’s a monster” akasema Happy kwa hasira juku akiendelea kulia.


“Its ok Happy It’s ok.Nyamaza usiendelee kulia mwanangu” akasema mzee Kibaho huku akimfuta Happy machozi


“Dady why you saved me? Akauliza Happy


“Happy naomba usahau kilichotokea.Kitu pekee kwa sasa ni kumshukuru Mungu kwa kukuponya .Sisi kama familia ni wajibu wetu kuhakikisha kwamba unakuwa salama.Tunakupenda sana na hakuna mtu yeyote anayeweza akakubali upoteze maisha” akasema mzee Kibaho halafu.Happy akainua mkono akafuta machozi.


“Baba ungeniacha nife.Nimechoka na maisha haya.I’m real tired with this kind of life.Nili……………….” kabla hajaendelea baba yake akamuwekea kidole mdomoni


“Shhhhhhhhh..!!!!..Happy usiseme hivyo.Sahau kilichotokea .Hii ni mitihani ya maisha na ambayo hatuna budi kuishinda.Happy tunakupenda sana zaidi ya unavyoweza kufikiri”


“Najua kwamba mnanipenda sana lakini kwa aibu hii niliyowapa najiona sistahili hata kuitwa mwanenu.Nime………………” Happy akashindwa kuendelea akaangua kilio


“Happy usilie mwanangu.Tunakupenda sana na siku zote tutakuwa pamoja nawe katika kila jambo.Tuko pamoja katika suala hili na ndiyo maana tumeamua kukuhamisha hapa nchini usiku huu na kukupeleka sehemu ambayo utaweza kupumzika na kusahau kilichotokea,sehemu ambayo hakuna mtu yeyote anayekufahamu”


“Mnataka kunipeleka wapi baba?


“Tumeamua kwanza uende ukapumzike Kigali Rwanda wakati tukiangalia sehemu nyingine ambayo itakufaa zaidi.Tayari kila kitu kimekwisha andaliwa kwa msaada mkubwa wa Savanna ambaye ndiye aliyefanikisha mipango yote ya safari ikiwa ni pamoja na kuandaa hoteli ambayo utafikia kule Kigali na hata kuwalipa madkatari wote watakaokuwa wakikuhudumia katika kipindi hiki chote utakachokuwa kIgali.Tumefikia uamuzi huu wa kukuondoa hapa nchini ili kukusaida usiweze kuumia zaidi kutokana na maneno ya watu na vyombo vya habari.Iwapo utaendelea kukaa hapa utakuwa ukiumia zaidi kila siku” akasema mzee Kibaho


“Please dady take me out of here right now” akasema Happy huku akitoa machozi.


“Usijali Happy.Kila kitu kimekwisha andaliwa na tuchosubiri ni taratibu za hapa hospitali .Lakini kabla hatujaondoka hapa kuna jambo ninataka kukuuliza” akasema mzee Kibaho halafu akamtazama mwanae na kusema


“Unawafahamu au kuwa na hisia ni nani aliyekufanyia hivi?


Happy akafumba macho kwa sekunde kadhaa halafu akasema


“Its not important anymore dady.Just take me out of here”


“Happy waliofanya unyama huu wanatakiwa wafikishwe katika vyombo vya sheria.Huu ni ukatili mkubwa sana ambao hauvumiliki.Tafadhali tusaidie tuweze kuwafahamu watu hao.Mimi na Savanna tutashirikiana na kuhakikisha kwamba wale wote waliotenda hivi wanakamatwa na kufikishwa katika vyombo vya sheria”


“Dady not now.Please take out of here” Happy akaendelea kuushikilia msimamo wake.Mzee Kibaho akatoka ndani ya kile chumba akakutana na Savanna.


“Savanna naomba usimjali Happy.Twende tukashughulikie masuala ya hapa hospitali ili tuweze kuruhusiwa kuondoka.” Akasema mzee Kibaho


“Kitu gani kinaendelea baina yako na Happy? Akauliza mzee Kibaho wakati wakishuka ngazi


“Its something stupid.Tulipishana maneno.Kuna mtu ambaye alimpelekea Happy maneno ambayo yalimfanya akasirike na kuja juu na mimi nikashindwa kudhibiti hasira zangu na tukajikuta tukitamkiana maneno makali.” Akasema Savanna


“Ninaweza kufahamu ni jambo gani hilo lililosababisha wewe na Happy mtupiane maneno? Akauliza mzee Kibaho


“Si jambo la msingi sana na sioni sababu ya kukwambia.Ni mambo ya wanawake tu na tutayamaliza” akasema savanna


Hatimaye ruhusa ya Happy kuondoka ikatolewa na akapatiwa daktari mmoja ambaye angeongozana naye kuelekea Kigali Rwanda ambaye angeendelea kumuhudumia hadi hapo hali yake itakapokuwa nzuri.Wote waliingia katika gari moja na safari ya kuelekea uwanja wa ndege ikaanza.Walikuwa makini sana kuhakikisha kwamba hawafuatiliwi na mwandishi yeyote wa habari kwani suala hili lilikuwa ni siri kubwa ya familia.Safari ilikuwa ya kimya kimya na hakuna aliyekuwa anaongea ndani ya gari.Waliwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere na ,mizigo ya Happy ikashushwa garini.Kilikuwa ni kipindi kigumu sana hasa kwa mama yake Happy.Alimkumbatia mwanae huku wote machozi yakiwatoka.


“Mom I’m going to miss you” akasema Happy


“Happy sina cha kusema zaidi ya kukuombea kwa Mungu akutangulie huko uendako.Uwe salama kila siku “ akasema mama yake Happy huku machozi yakimtoka


“Nitakuwa salama mama” akasema Happy halafu akamuacha mama yake na kumfuata Margreth.


“Be safe there and get well soon” akasema Margreth


Happy hakusema kitu ,macho yake yalikuwa yamefunikwa na machozi


“Its time to go Happy” akasema mzee Kibaho kwa sauti ndogo


“Baba Happy” akaita mama yake Happy.Mzee Kibaho akageuka


“Tafadhali hakikisha Happy anakuwa salama”


Mzee Kibaho hakujibu kitu zaidi ya kutingisha kichwa ishara ya kukubaliana na kile alichokisema mke wake halafu akamshika mkono Happy na kumuomgoza kuelekea ndani ya uwanja kwa ajili ya kukamilisha taratibu za hapo uwanjani kabla ya kuruhusiwa kuondoka




Waliwaisli salama katika uwanja a ndege wa kimataifa wa Kigali.Christine Umuhiza alikuwepo uwanjani kuwapokea wageni wake na kisha wakaelekea moja kwa moja Reonaldo hotel,moja ya hoteli mpya na kubwa jijini Kigali


Tayari kila kitu kilikwisha andaliwa na Happy akapewa chumba chenye hadhi ya rais yaani presidential suit kama alivyokuwa ameahidi Savanna.Mzee Kibaho ambaye ambaye naye alikuwa ameambatana na mwanae naye alipewa chumba kizuri sana kwa ajili ya kupumzika kwa siku zote atakazokaa hapo Kigali,daktari aliyeambatana nao pia alipewa chumba cha hadhi ya juu kabisa.


“Happy,nilipendekeza ufikie katika hoteli hii kwa sababu ni nzuri na huduma zake ni nzuri na za kimataifa.Jitahidi kupumzika kwa kadiri utakavyoweza na kwa muda wowote utakaohitaji.Mmiliki wa hoteli hii ni rafiki yangu sana na anafahamu uwepo wako hapa na gharama zote ni juu yangu .Endapo kutakuwa na tatizo lolote wasiliana nami moja kwa moja.Christine atakusaidia kumpata daktari bingwa wa magonjwa ya akili ambaye atakuwa akifika hapa kila siku na atakusaidia kisaikolojia ili uweze kurejea katika hali yako ya kawaida.”Akasema Savanna halafu akamtazama Happy aliyekuwa amejilaza kitandani.


“Happy najua tulipisha kauli na kutoleana maneno makali.Tafadhali naomba tusahau yale yote yaliyopita na tuangalie mambo ya mbele.Binafsi nimeumizwa mno na jambo hili kama walivyoumia wale wote wanaokupenda na ndiyo maana nimejitolea kufanya kila lililo ndani ya uwezo wangu ili kuhakikisha unarudi katika hali yako ya kawaida na kwa pamoja tuhakikishe wale wote waliohusika na kitendo hiki wanatafutwa kwa gharama zozote na kufikishwa mbele ya sheria” akasema Savanna.Bado Happy alikuwa anamuangalia kwa macho makali yaliyojaa machozi


“Happy mimi naenda kupumzika nyumbani kwa Christine.Nitakuja kukuaga asubuhi kabla ya kurejea Dar es salaam” akasema Savanna baada ya kugundua kwamba Happy hakuwa tayari kuongea naye kwa usiku ule .Akaufungua mlango na kutoka mle chumbani


* * * *


Kumekucha Kigali,kijua tayari kimechomoza na shughuli mbali mbali za uzalishaji mali zilikuwa zinaendelea kama ilivyo ada.Saa mbili za asubuhi Chistine na Savanna wakawasili hotelini.Wa kwanza kuonana naye alikuwa ni mzee Kibaho ambaye alikwisha amka na kufanya mazoezi ya viungo katika ukumbi mkubwa wa mazoezi uliopo katika hoteli ile.


“Happy ameamkaje? Akauliza Savanna


“Nimeongea naye kwa simu asubuhi ya leo ,amesema anaendelea vizuri ,lakini kwa mujibu wa daktari ni kwamba itamchukua siku kadhaa kurejea katika hali yake ya kawaida” akajibu mzee Kibaho


“usijali baba.Nina hakika baada ya muda hali yake itakuwa nzuri na maisha yataendelea kama kawaida.” Akasema Savanna halafu akaenda kuonana na daktari aliyemuhakikishia kwamba hali ya Happy ilikuwa inaendelea vizuri.Baada ya hapo akaelekea katika chumba cha Happy akabonyeza kengele ya mlangoni.Dakika kama mbili zilipita bila majibu yoyote .Akaanza kuingiwa na wasi wasi.Akabonyeza tena kengele na baada ya kama dakika mbili tena akasikia kitasa cha mlango kikinyongwa na mlango ukafunguliwa.Akagonganisha macho na Happy ambaye bado yalikuwa yamemvimba kutokana na kulia sana.Happy hakusema kitu akarejea kitandani kwake akaketi.Savanna naye akaingia mle chumbai na kusimama pembeni ya meza kubwa ya chakula.


“Happy unaendeleaje? Akauliza Savanna lakini Happy hakumjibu kitu.


“Happy nafahamu hukupenda kuniona hapa.Nafahamu ndani ya moyo wako mimi ni mmoja wa wale watu unaowachukia sana hivi sasa.Unapaswa kunichukia hasa baada ya maneno yale makali tuliyotoleana.Sote tulitoleana maneno makali kutokana na hasira tulizokuwa nazo.Sina mengi sana ya kusema lakini naomba utambue kwamba nimeguswa sana na jambo hili na kama rafiki na mwanamke mwenzako,niko pamoja nawe katika wakati huu mgumu” akasema Savanna halafu akanyamza kidogo akamtazama Happy na kuendelea


“Happy nimekuja kukuaga.Muda mfupi ujao ninarejea Dare s salaam.Ningependa kuwa nawe hapa kwa muda mrefu zaidi lakini bado ninakabiliwa na majukumu mengine mengi.Mzee Kibaho na daktari ,wataendelea kufuatilia hali yako kwa karibu na watatufahamisha kila hatua na endapo kutakuwa na tatizo lolote basi tutasaidiana namna ya kulitatua.Kitu pekee ambacho nitaka kukushauri ni kwamba ,japokuwa ni vigumu sana lakini naomba ujaribu kusahau kilichotokea na uruhusu maisha yaendelee.Happy nakufahamu wewe ni mwanamke jasiri sana naomba tafadhali usikubali kushindwa katika hili.Usimpe nafasi mtu,au kikundi cha watu kukufanya ukate tamaa na ushindwe kutimiza ndoto zako.” Savanna akanyamaza na kumtazama Happy ambaye macho yake yalikuwa yemejaa machozi


“Hapa hotelini utaishi kwa muda wowote utakaoutaka,utapatiwa kitu chochote utakachohitaji.Endapo kutakuwa na tatizo lolote naomba unipigie simu yangu moja kwa moja.Mwisho naomba ufahamu kwamba kuna maelfu ya watu wanaokupenda na mashabiki wako wanaokusubiri upone na siku moja urejee tena Tanzania.Get well soon Happy “ akasema Savanna huku naye akilengwa na machozi halafu akageuka na kuanza kupiga hatua kuondokaCHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/


“Savanna subiri kidogo” akasema Happy.Savanna ambaye alikuwa ameukaribia mlango akasimama na kugeuka.Happy akainuka pale kitandani akamfuata


“Savanna naomba unisamehe kwa yale yote niliyokutenda.Ni kweli siku ile tulipopishana maneno nilikuwa na hasira sana lakini naomba unisamehe.Kabla hujaondoka,naomba toka ndani ya moyo wangu niseme kwamba ahsante sana kwa yote.Wema huu ulionitendea ni mkubwa na sina hakika kama nitaweza kuurejesha.Pamoja na shukrani zangu kuna jambo moja nataka kukuweka wazi”akasema Happy akamtazama Savanna kwa makini halafu akasema


“Savanna sintarejea tena Tanzania.I’ve left Tanzania for good.Its my country but I hate Tanzania so much.Kwa sababu hiyo basi naomba nimkabidhi Patrick katika mikono yako.Ninamuacha mikononi mwako kwa sababu ninaamini unampenda na utahakikisha anakuwa mwenye furaha siku zote katika maisha yake.Please take good care of him .He’s all yours now.Kokote nitakakokuwa nitajua kwamba Patrick ana furaha kwa sababu yuko katika mikono salama.” Akasema Happy huku machozi yakimtoka


“Tafadhali Happy usiseme maneno hayo” akasema Savanna kwa mshangao


“Savanna naomba ufanye kama nilivyokuomba.Huu ni uamuzi wangu na nimeamua kuchukua maamuzi haya magumu kutokana na hali halisi ilivyo na ukweli ulio wazi kwamba mimi na Patrick hatutaweza kuwa pamoja japokuwa tunapendana kwa mioyo yetu yote.Pamoja na hayo naomba unihakikishie jambo moja.”


“Jambo gani Happy?


“Naomba unihakikishie kwamba Patrick atashinda kesi na atakuwa huru na kwamba hautamwambia mahala niliko.Can you promise me that?


Savanna akamwangalia Happy usoni na kusema


“Patrick will be free.I give you my word” akasema Savanna


“Thank you Savanna.Thank you so much.You can go now” akasema Happy huku uso wake ukiwa umeloa machozi


“Thank you so much Happy.” Akasema Savanna huku naye machozi yakimtoka na kumkumbatia Happy halafu akatoka mle chumbani


* * * *


“The war is over now.Patrick is mine and he’s mine alone.” Akawaza Savanna akiwa katika ndege akirejea Dar es salaam.Uso wake ulikuwa umepambwa kwa tabasamu pana


“Sijafurahia kilichomtokea Happy japokuwa sote tulikuwa katika vita ya kumgombania Patrick lakini kufa kufaana.Namuonea huruma sana Happy japokuwa kwa upande wa pili nimejawa na furaha kwa yeye kuamua kuachana na Patrick.” Akawaza Savanna


“Lakini ni nani hawa waliomfanya udhalilishaji huu mkubwa? Ninaanza kujenga picha kwamba waliofanya kitendo hiki walikuwa na lengo moja tu la kumdhalilisha Happy.Nashawishika kuamini kwamba yeyote aliyefanya jambo kama hili alikuwa na lengo la kulipiza kisasi.Ninalazimika kuamini pia kwamba lazima tukio hili litakua na uhusiano fulani na kifo cha vero.Nasikitika kwamba hatutaweza kuwapata watu hawa kwa sababu Happy hayupo tena Tanzania na hana mpango wa kurejea tena wala wa kuwatafuta watu hawa. ”


Savanna alikuwa na furaha sana kwani aliamini ile ndoto yake ya kuwa na Patrick sasa inakwenda kutimia


*****************


Saa tatu za asubuhi gari moja dogo jeupe likaingia katika gereza la Uwangwa.Kijana mmoja mfupi mnene aliyevaa suti ya kijivu iliyomkaa vyema akashuka toka ndani ya gari lile na kuelekea sehemu ya mapokezi ambako alijitambulisha kama mgeni wa Apolinary.Moja kwa moja akapelekwa katika ofisi ya Apolinary mmoja kati ya maafisa wa gereza hili


“karibu sana kijana” akasema Apolinary ,mzee mmoja mnene mweupe


“Ahsante sana mzee.” Akajibu Yule kijana huku akiketi kitini na bila kuchelewa akaitoa bahasha ya khaki toka mfukoni na kupatia mzee Apolinary ambaye aliifungua na kukutana na bunda kubwa la noti mpya kabisa nyekundu


“Sina haja ya kuhesabu,nadhani ni millioni tatu kamili.”


“Ndiyo mzee,ni tatu kamili”


“namuamini sana Khumalo.Ahadi zake huwa za kweli.” Akasema Apolinary huku akizifungia fedha zile katika kabati lake na kuchukua fimbo yake akamuomba Yule kijana amfuate.Apolinary alienda hadi katika ofisi moja inayohusiana na masuala ya mahabusu akaongea na askari mmoja aliyekuwamo mle ofisini kisha akainua simu akapiga na muda si mrefu wakatokea askari wawili ambao akaongea nao jambo fulani halafu wakaongozana na mzee Apolinary pamoja na yule kijana wake.Waliingia katika chumba kimoja kidogo kilichokuwa na viti viwili.


“Nickson, Patrick ataletwa hapa muda si mrefu na utaongea naye” akasema Apolinary halafu akawatuma wale askari wawili wakamlete Patrick.Baada ya kama dakika saba hivi Patrick akaletwa


“Patrick kuna mtu amekuja kukutembelea.” Akasema Apolinary halafu akawafanyia ishara askari wale watoke mle chumbani na kuwaacha Patrick na yule kijana Nickson


“Nickson una dakika kumi tu za kuongea na Patrick” akasema Apolinary naye akatoka nje


“Watatumia dakika kumi tu halafu mumrudishe Patrick mahabusu” Apolinary aliwaambia wale askari waliokuwa wamesimama nje ya kile chumba


“Patrick pole sana.Nadhani ni mara ya kwanza mimi na wewe tunaonana.Bila kupoteza muda naomba nijitambulishe “ akasema Nickson na kutulia kidogo halafu akaendelea


“Ninaitwa Nickson.Ni mfanyabiashara.Nimekuja hapa kukuletea taarifa ambazo si nzuri na nina imani hautazifurahia lakini kama mwanaume nakusihi ukaze moyo.” Akasema Nickson na kumfanya Patrick apatwe na wasi wasi


“Nickson sina hakika kama tumewahi kuonana mahali.Ni taarifa gani hizo ambazo si nzuri kwangu? Akauliza Patrick


“Patrick ninafahamu mahusiano yako na Happy Kibaho.Ninafahamu kwamba ulivunja mahusiano yako ya awali kwa ajili yake.Ninasikitika kukutaarifu kwamba pamoja na mapenzi yote uliyomuonyesha Happy lakini yeye ameshindwa kuwa mwaminifu kwako na hasa katika kipindi hiki ambacho uko gerezani” akasema Nickson na kumfanya Patrick azidi kuwa na wasi wasi


“Happy amefanya nini? Akauliza Patrick kwa wasi wasi.Nickson hakuongea kitu akaingiza mkono katika koti lake na kutoa bahasha akaisogeza karibu na Patrick


“Fungua uangalie” akasema Nickson.Patrick akaichukua bahasha ile na kuifungua.Ndani ya bahasha ile kulikuwa na picha akazitoa.Picha ya kwanza ikamstua na kuzifanya picha nyingine zote alizokuwa amezishika mkononi zianguke mezani.Akaitazama picha ile aliyokuwa ameishika mkononi.Mikono ilikuwa inamtetemeka huku kijasho kikianza kumchuruzika.Akaiweka picha ile chini na kuchukua picha nyingine akaiangalia.Macho yake yakaanza kutoa machozi.Akajikaza na kuanza kuzipitia picha zile moja baada ya nyingine.Kabla hajamaliza kuzitazama akamtazama Nickson kwa macho makali sana


“Nani amekutuma uniletee picha hizi? Akauliza Patrick huku machozi yakimtoka.Akainama tena akaziangalia picha zile.


“Ouh my gosh !! Happy !!!.Siamini .Siamini kama Happy anaweza akanifanyia hivi.” Akasema Patrick na kufuta machozi.Ghafla kwa nguvu akainuka ,akaisukuma ile meza na kumkaba Nickson


“Niambie nani amekutuma uniletee picha hizi?


Patashika kubwa likaibuka mle ndani na mara askari waliokuwa nje ya kile chumba wakaingia haraka na kumkamata Patrick kisha wakamuamuru Nickson aondoke haraka sana.Kwa haraka Nickson akazikusanya zile picha akaziweka mfukoni na kutoka mle chumbani huku Patrick akiwa ameshikiliwa na askari.Ghafla Patrick akamsukuma kwa nguvu askari aliyekuwa amemshikilia na kwa kasi ya aina yake akamvaa askari aliyekuwa amesimama pembeni ya mlango na kutaka kunyang’anya bunduki.Kuliibuka kizaazaa kikubwa .Patrick na Yule askari walikuwa wananyang’anyana silaha.Yule askari aliyekuwa amesukumwa na kuanguka chini akakiona kitendo kile na kuinuka haraka akamtandika teke kali la mbavuni na kumfanya Patrick aachie bunduki ile aliyokuwa akiing’ang’ania na kutoa yowe.Bila kujali maumivu aliyoyapata kwa teke lile akainuka tena kwa kasi na kutaka kumvamia askari tena yule mwenye silaha lakini askari Yule e alikiona kitendo kile na kwa nguvu akampiga na kitako cha bunduki akaanguka na kupoteza fahamu.Kwa kutumia simu ya upepo wakatoa taarifa kwa viongozi ambao walifika mara moja kushuhudia kilichotokea na kuamuru Patrick apelekwe katika hospitali ya gereza kwa matibabu wakati uchunguzi wa tukio lile ukiendelea.Patrick akatolewa mle chumbani na kukimbizwa katika hospitali ya gereza kwa ajili ya matibabu




* * * *


Savanna aliwasili salama jijini Dar es salaam,kutoka pale uwanjani alikodisha teksi iliyompeleka hadi nyumbani kwake.


“ Kitu cha kwanza ninachotakiwa kukifanya siku ya leo ni kwenda kuonana na Alois na kumuomba wasimueleze kitu chochote Patrick kuhusiana na tukio lile la Happy.Inatakiwa itafutwe namna nzuri ya kumfahamisha Patrick juu ya tukio hili kwani endapo tukikurupuka kumweleza tunaweza kusababisha mambo mengine.” Akawaza Savanna akiwa njiani kuelekea nyumbani kwake


“Namuonea huruma sana Patrick.Matatizo aliyonayo ni makubwa sana.Amempoteza Vero,baba yake na sasa amejitumbukiza katika kesi kubwa ya mauaji na kabla haijajulikana hatima yake linaibuka tena suala hili la Happy.Ninatakiwa nifanye kila niwezalo ili kuhakikisha ninamtoa Patrick gerezani “akaendelea kuwaza Savanna


Alifika nyumbani kwake akaoga na kuvaa suruali nyeupe ya jeans na shati jekundu .Alipendeza vilivyo kama ilivyo kawaida yake.Kabla hajatoka akampigia simu Alois kaka yake Patrick na kumuomba waonane,kisha akaingia katika gari lake akaondoka .


“Nayaona maisha yangu kama yamejaa nuru na furaha hivi sasa na yote hii ni kwa sababu nina uhakika wa kuishi maisha yangu yote nikiwa na mwanaume nimpendaye kuliko wote duniani.” Akawaza Savanna akiwa njiani kuelekea nyumbani kwa wazazi wa Patrick kuonana na Alois kaka wa Patrick


Alipofika alipokelewa na Alois na baada ya maongezi machache akamkaribisha sebuleni


“Unaendeleaje Alois?


“Ninaendelea vizuri Savanna.Tumekwishaizoea hali hii.Nashukuru Mungu hata mama naye anaendelea vizuri hivi sasa” Akasema Alois


“Nashukuru kusikia hivyo”


“Vipi kuhusu wewe Savanna unaendeleaje? Kesi inakwendaje?


“Mimi ninaendelea vizuri sana Alois na kuhusu kesi hakuna haja ya kuwa na wasi wasi kila kitu kinakwenda vizuri .Nawaomba muondoe shaka kabisa kuhusu kesi hii kwani ni lazima tushinde.” Akasema Savanna na kumfanya Alois atabasamu


“Ahsante sana Savanna kwa kuzidi kutupa matumaini.Umekuwa mfariji wetu na tegemeo letu katika suala hili la Patrick.Umemsaidia sana hata mama kutokuwa na wasi wasi na mwanae.Nikupe siri moja mama anampenda sana Patrick.”akasema Alois halafu kikapita kimya kifupi


“karibu sana Savanna” akasema Alois


“Alois mimi si mkaaji sana nimepita hapa mara moja ili tujadili kwa pamoja jambo hili lililotokea.” Akasema Savanna


“Jambo gani Savanna? Hili la Patrick?


“Ni kuhusu Happy.Nadhani umeisikia kashfa iliyompata”


“Ndiyo.Alinipigia simu Andrew jana na kunifahamisha.Niliitazama video yake katika mtandao sikuamini kama ni kweli Happy ameweza kufanya kitendo cha aibu kama kile.Nimefadhaika sana kwa sababu yule msichana ndiye chanzo cha Patrick kusota gerezani hivi sasa.Ni aibu kubwa mno na hata mama nimemficha sijamweleza chochote” akasema Alois


“Nakubaliana nawe Alois.Kitendo kile ni cha aibu sana na hakivumiliki.Kikubwa kilichonileta hapa ni kukuomba kwamba Patrick asifahamishwe kwa sasa.Endapo akifahamu alichokifanya Happy itamsababishia matatizo makubwa sana kwani kchwa chake kwa sasa kimebeba mambo mengi ”


“Savanna bila hata kuomba lakini naomba nikuhakikishie kwamba si mimi wala mtu yeyote katika familia yetu angeweza kumweleza Patrick kitu chochote kuhusiana na uchafu uliofanywa na Happy.Ni kitendo cha aibu sana na kisichovumilika.Moyo wangu umeumia hasa nikimuangalia mdogo wangu anavyoteseka gerezani kwa ajili ya huyu huyu msichana”


“Ahsante sana Alois kwa busara hiyo.Basi ni hilo pekee lililonileta hapa.Naomba uniruhusu niondoke nikaendelee na majukumu mengine.” Akasema Savanna


“Nashukuru sana Savanna kwa kuja kututembelea bahati mbaya mama amelala alikuwa na hamu sana ya kukuona”


“Mpe salamu zangu.Nitakuwa nikija hapa mara kwa mara kumsalimu” akasema Savanna kisha akainuka na kuondoka.


“Kwa sasa ni safari ya moja kwa moja kueleka Uwangwa .kabla sijafanya chochote lazima niaonane kwanza na Patrick.Sijamtia machoni kwa siku nzima ya jana” akawaza Savanna


* * * *


Ilimchukua dakika arobaini kuwasili katika gereza la Uwangwa.Kijua kilikuwa kikali sana siku hii.Kisha shuka garini akaelekea moja kwa moja mapokezi kama ilivyo kawaida yake na pale alipewa taarifa kwamba akaonane na mkuu wa gereza.Alistushwa sana na taarifa ile.Alijaribu kudadisi ili kufahamu nini kilichotokea hadi ikamlazimu akaonane na mkuu wa gereza kabla ya kuonana na Patrick lakini hakuna aliyekuwa tayari kumweleza chochote.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/


Huku akiwa na uso uliojaa wasi wasi Savanna akatembea kwa kasi kuelekea katika ofisi ya mkuu wa gereza.Alijitambulisha kwa katibu muhtasi wa mkuu wa gereza ambaye alimpigia simu mkuu wake na kisha akamruhusu Savanna aingie ofisini.


“karibu Savanna” akasema mkuu wa gereza.


“Nashukuru sana mkuu” akasema Savanna.Kikapita kimya cha sekunde kadhaa


“Mkuu nimekuja kuonana na mteja wangu lakini nimestushwa kidogo kwa kuambiwa kwamba unahitaji kuniona kabla ya kuonana na mteja wangu” akasema Savanna


“Ni kweli Savanna.Nilitoa maagizo hayo.Kuna jambo limetokea leo kuhusiana na mteja wako” akasema mkuu wa gereza na kumfanya Savanna astuke


“jambo gani limetokea tena?


“Leo asubuhi kuna mtu ambaye alikuja kuonana na Patrick.Kwa mujibu wa askari waliokuwepo eneo la tukio,mtu huyo alikuwa na bahasha yenye picha ambazo alimpa Patrick azitazame.Hatujui picha hizo ni za nani na kwa nini mtu huyo alimpa Patrick lakini inasemekana baada tu ya Patrick kuziona picha hizo alibadilika na kuwa kama mtu aliyechanganyikiwa.Alimkaba mtu Yule aliyempeleka zile picha na akazua tafrani kubwa.Askari ambao walikuwa nje waliingilia kati ugomvi huo na kumdhibiti Patrick lakini alifanya kitu cha ajabu sana kwani alimvamia askari na kutaka kumnyang’anya silaha.Hatuelewi alikusudia kufanya nini na ile bunduki lakini nina hakika angefanikiwa kuipata silaha ile angeleta maafa makubwa.Askari walifanikiwa kumdhibiti na kumsababishia jereha kidogo kichwani na hivi sasa anaendelea kupatiwa matibabu katika zahanati ya gereza”


“Ouh my gosh !! akasema Savanna huku ameshika kichwa kwa mikono.


“Kuna taarifa zozote za maendeleo yake?


“Kwa taarifa nilizozipata toka kwa madaktari muda si mrefu ni kwamba Patrick anaendelea vizuri.”


“Ouh Mungu wangu ..!!” akasema Savanna.Suala lile lilikuwa limestua sana.


“Savanna suala hili la Patrick ni suala zito sana na endapo litafika katika vyombo vya sheria litakuwa na athari kubwa sana kwa Patrick na hata kwa uongozi wa gereza.Kwa heshima yako suala hili litaishia hapa hapa na halitaenda sehemu yoyote lakini hata hivyo inabidi tuchukue hatua za kuzuia jambo kama hili lisijitokeze tena.Tumeamua kudhibiti watu wanaokuja kumtembelea Patrick.Kuanzia hivi sasa watakaoruhusiwa kuonana naye ni wewe pamoja na familia yake pekee.Hakuna mtu mwingine yeyote atakayeruhusiwa kumuona.Hii ni kwa ajili ya usalama wa Patrick vile vile kwani hatujui katika watu wanaokuja kumtazama ni yupi atakuwa adui yake”


“Nashukuru sana mkuu wa msaada wako huu mkubwa.Nitaongea na Patrick na kumsihi asithubutu kufanya kitendo cha hatari namna hiyo tena.Ninaweza kuruhusiwa kuonana naye?


“Twende tuongozane na mimi nikaangalie maendeleo yake.” Akasema mkuu wa gereza huku akiinuka akatoka mle ofisini


“Nahisi mwili wote ni kama umekufa ganzi.Ni nani huyu aliyemletea Patrick picha? Najua ni lazima zitakuwa ni picha za Happy.Ninaanza kujenga hisia kwamba jambo hili si la mtu mmoja bali linahusisha kikundi cha watu na wana ajenda yao ya siri kufanya hivi na ajenda yao kubwa ni kuuharibu uhusiano wa Patrick na Happy.Kwa mujibu wa barua ile aliyoindika Happy ni kwamba alitekwa na kundi la watu waliomlazimisha kufanya ngono na kisha kumpiga picha za utupu na kuzisambaza.Kuna ulazima wa kuwafahamu watu hawa wenye roho za kikatili namna hii” akawaza Savanna wakati wakielekea katika zahanati ya gereza kumuangalia Patrick


Mkuu wa gereza na Savanna waliingia katika ofisi ya mganga mkuu wa gereza ambaye aliwapa taarifa za maendeleo ya Patrick na kisha kuwapeleka katika chumba alichokuwa amelazwa Patrick


“Tumemchoma sindano ya usingizi nadhani baada ya masaa mawili au matatu ataamka.” Akasema daktari.Patrick alikuwa amelala usingizi mzito sana pale kitandani na sehemu ya juu ya jicho lake alikuwa na jeraha.Mkono wake wa kushoto ulikuwa umefungwa pingu.Savanna akashindwa kuvumilia kumuona Patrick katika hali ile akaangusha machozi


“Tafadhali mkuu naombeni mumfungue hiyo pingu.Hatakwenda sehemu yoyote.Hawezi kukimbia”


“Hii pingu amefungwa kwa ajili ya usalama.Alipoamka mara ya kwanza alionekana ni kama mtu aliyechanganyikiwa.Alitaka kukimbia akazuiwa hivyo tumeona ni bora kama tukimfunga pingu ili asiweze kutoka hapa kitandani akasema daktari


“Savanna wewe unaweza kwenda kupumzika.Mteja wako yuko katika uangalizi makini .Endapo kutakuwa na tatizo lolote tutakutaarifu” akasema mkuu wa gereza.


“Ahsante sana mkuu ,lakini naomba niendelee kukaa hapa hadi hapo atakapoamka ili niweze kuongea naye hata maneno mawili na nimsihi atulie asifanye jambo lolote la hatari.tafadhali mkuu naomba uniruhusu kwa hilo” akaomba Savanna


Mkuu wa gereza akainama akafikiri kwa muda kisha akasema


“Sawa Savanna,kama unahitaji kujiridhisha zaidi na maendeleo ya mteja wako basi hakuna shaka.Kuna mgahawa wa gereza unaweza kwenda kukaa pale na pindi atakapoamka tutakutaarifu.” Akasema mkuu wa gereza halafu wakatoka .Savanna akakabidhiwa askari aliyempeleka hadi katika mgahawa wa maofisa wa gereza.


“Sintawataarifu familia yake kwa sasa hadi hapo nitakapohakikisha anaendelea vizuri.Nikiwaeleza sasa hivi kwamba mtoto wao amepatwa na matatizo tena ninaweza kuwasabishia matatizo mengine katika wakati huu mgumu walionao” akawaza Savanna




Ni mtu mmoja tu aliyekuwa anasubiriwa atoke ndani ili safari ya kuelekea makaburini ianze.Siku hii ya leo familia ya Vero waliamua kwenda kulitembelea kaburi la Vero ambalo tayari lilikuwa limemalizwa kutengenezwa.Kazi iliyokuwa ikifanyika ilikuwa ni kuweka vigae pamoja na marembo mengine na kulifanya lipendeze mno


Familia yote ilikwisha kusanyika na aliyekuwa anasubiriwa ni mama yao.Wote walikuwa wamepanda katika gari moja.


“She’s taking too long” akasema Loniki


“Labda anasal…….” Shangazi yao akataka kusema kitu lakini kabla hajamaliza mtu waliyekuwa wanamsubiri akatokea na safari ikaanza


Kabla hawajafunga mlango simu ya Loniki ikaita.Akaitoa mfukoni na kutazama mpigaji alikuwa ni Linah


“Hallow Linah


“Lonny umeamkaje dear?


“Nimeamka salama Linah.”


“Uko wapi mida hii? Bado umelala?


“Hapana Linah.Niko na familia tunajiandaa kwenda kutembelea kaburi la Vero.Mafundi tayari wamemaliza matengenezo”


“Lonny kama ningekuwa na muda ningekuja kuungana nanyi lakini nimebanwa sana leo”


“usijali sana Linah.Vipi kuna habari gani mpya?


“Khumalo kanipigia simu sasa hivi na kunitaarifu kwamba tayari Patrick ameziona zile picha”


“Ouh gosh ..!! what happened? Akauliza Loniki kwa furaha huku akishuka garini ili aweze kuongea vizuri na Linah bila ya mtu kusikia maongezi yao


“kwa mujibu wa taarifa ya kijana aliyezipeleka picha hizo ni kwamba mara tu Patrick alipozitama alibadilika na kuwa kama mtu aliyepandwa na uchizi.Alimvamia kijana huyo na kutaka kufahamu aliyemtuma ampelekee picha hizo kwa bahati nzuri kulikuwa na askari karibu hivyo hakuweza kumdhuru.Baada ya askari kumshikilia Patrick asiendelee kuleta fujo ,alimrukia askari aliyekuwa na bunduki na kutaka kumnyang’anya silaha jambo lililowalazimu askari kumtembezea kipigo kikali sana.Hivi sasa nasikia hali yake ni mbaya na amelazwa katika hospitali ya gereza”


“Ouh gosh ! that’s great news to hear this morning.Sipati picha ingekuaje kama angefanikiwa kuinyakua hiyo bunduki.Nadhani lengo lake lilikuwa kujiua.Hahaha haaa I think the plan is working .Patrick and Happy are both in great pain right now” akasema Loniki huku akitabasamu kwa furaha


“Si hilo tu Lonny kuna taarifa nyingine pia imevuja kwamba Happy alitaka kujiua kwa kunywa sumu baada ya kuziona picha zile.Taarifa zinaseama kwamba baada ya kunywa sumu alikimbizwa katika hospitali ya Brahmaputra lakini uongozi wa hospitali ile umekanusha taarifa hizo.Taarifa mpya iliyopatikana toka vyanzo vya karibu vya Khumalo ni kwamba mpaka muda huu Happy hajulikani alipo.Waandishi wa wa habari wamekuwa wakimtafuta kwa mahojiano lakini hawajui yuko wapi na simu yake haipatikani tena na hata familia yake haiko tayari kusema mtoto wao yuko wapi” akasema Linah


“hahaaa aahahaa haaa!! Loniki akacheka kwa furaha na mara honi ya gari ikapigwa


“Linah wananipigia honi.Tutaongea baadae.Ahsante kwa taarifa” akasema Linah akakata simu na kukimbilia garini


“mambo ndo kwanza yanaanza Patrick.I’ll make your life a living hell.You and your girl must pay for what you did to Vero” akawaza Loniki


“Natumai kwa muda huu Patrick na Happy watakuwa katika mateso makubwa sana.Niliahidi kulipiza kisasi kwa kifo cha mdogo wangu na nitafanya hivyo.Huu ni mwanzo tu” akawaza Loniki


Safari ilikuwa ya kimya kimya hadi walipofika makaburini.Wakashuka garini na kuelekea katika kaburi la Vero.Lilikuwa kaburi linalopendeza na lililojengwa kwa ustadi mkubwa.Mama yake Vero akashindwa kuyazuia machozi kumtoka tena.Akakaa juu ya kaburi la binti yake aliyempenda sana na kuanza kulia


“Masikini binti yangu,wamekukatili uhai wako.Hukustahili kuondoka na kuniacha peke yangu mapema namna hii.Ninaomba usiku na mchana wale wote waliokukatili mwanangu na kunisababishia mateso haya makali wapate adhabu kali inayowastahili” akalia mama yake Vero.Loniki akamsogelea na kukaa pembeni yake


“Usilie mama,wote waliohusika na kifo cha Vero watapata adhabu inayowastahili na tayari yamekwisha anza kuwapata makubwa.Wataumia na kuteseka kama sisi tunavyoumia na kuteseka” akasema Loniki


Sarah ambaye anaye alikuwa amesimama karibu na kaburi akastuka baada ya kusikia maneno ya Loniki.


“mama ,kitu peke kinachoweza kukupa amani ya moyo ni kumuachia Mungu suala hili na si kuwaombea mabaya wahusika wa tukio hili.Kwa kuwaombea mabaya unakwenda kinyume na maandiko yanayotukumbusha kwamba tuwapende wabaya wetu na tuwaombee neema na Baraka .Ni Mungu pekee ndiye atakayewaadhibu” akasema Sarah


“Sarah najitahidi sana kufanya hivyo lakini ninashindwa.Kila nikifikiria namna mwanangu alivyokufa najikuta nikiwa na hasira na hamu ya kutaka kuwaona wale wote waliofanya kitendo kile wakipata adhabu kali.”


“Usiseme hivyo mama.Unat……” akasem Sarah lakini Loniki akaingilia kati


“Mama usimsikilize huyu.Siku zote yeye amekuwa upande wa Patrick.Hana uchungu wowote na kifo cha mdogo wake.Mama mimi ndio niko pamoja nawe.Wote waliosababisha kifo cha Vero lazima wapate adhabu kali”


Sarah na Loniki wakaangaliana kwa macho makali sana.Ikamlazmu mama yao kuingilia kati


“Haya inatosha sasa.Tuwekeni maua tuondoke” akasema mama yao halafu akachukua maua akayaweka juu ya kaburi na kupiga magoti,akasali kimya kimya na kusogea pembeni kuwapa nafasi wengine.Kila mmoja aliyekuja hapo aliweka shada la maua na kusali sala fupi


“Vero mdogo wangu,natumai huko uliko unaniona mida hii.Niliahidi kulipa kisasi kwa wale wote waliokufanyia unyama ule mkubwa na kukukatili maisha yako .Tayari nimeanza kuitekeleza ahadi yangu na wahusika wameanza kulipa.Si kazi rahisi lakini nakuahidi nitaifanya hadi nihakikishe Patrick na mwenzake wamelipa” akasema Loniki kwa sauti ndogo akiwa amepiga magoti katika kaburi la Vero.Zoezi lilipokamilika wakaingia garini na kuondoka kuelekea nyumbani


* * * *


Mlio wa simu ukamstua Savanna toka katika mawazo mengi.Ilikuwa ni simu toka kwa mkuu wa gereza


“hallo mkuu” akasema Savanna-


“Savanna nimetaarifiwa kwamba tayari Patrick ameamka,unaweza kwenda kumuona sasa”


“Ahsante sana mkuu” akasema Savanna huku akiinuka na kuanza kupiga hatua kuelekea katika zahanati ya gereza


“Mungu msaidie Patrick katika kipindi hiki kigumu alichonacho.” Akaomba Savanna wakati akipanda ngazi kuingia zahanati.Alionana na daktari ambaye alimpeleka moja kwa moja katika chumba alicholazwa Patrick


Mara tu Patrick alipomuona Savanna akainuka na kukaa kitandani.Savanna akamuendea na kumkumbatia


“Ouh Patrick,pole sana” akasema Savanna


“Savanna nashukuru umekuja” akasema Patrick kwa sauti ndogo yenye kukwama kwama.


“Patrick unajisikiaje sasa hivi?


“I’m dead Savanna.I feel dead” akasema Patrick


“Patrick usiseme hivyo”


“Savanna I want to die.namba uwaambie wanifungue hii pingu nife.I want to die.Sioni tena sababu ya kuendelea kuishi“CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/


“Patrick tafadhali naomba unisikilize”


“Savanna believe me I’m dead.Ninahisi maumivu makali ya moyo.Nahisi kama kuna kitu kikali kinaukata moyo wangu vipande vipande..Ninasikia maumivu makali ambayo siwezi kuyaelezea” akasema Patrick


“Patrick nini kimetokea? Akauliza Savanna


“Savanna Happy yuko wapi? Happy ameniua.Ameniua bila kosa kama alivyomuua Vero.Nimemkosea nini mpaka anifanyie unyama wa namna hii? Upendo wote huu niliomuonyesha iweje leo hii anifanyie namna hii? It was all a lie.There was no us,there was no love ,it was all lies.Please let me die” akasema Patrick kwa uchungu


“Patrick tafad…………….” kabla Savanna hajamaliza alichotaka kukisema Patrick akapaaza sauti


“Waambie wanifungue.I want to die..!!!!!!!!!!!!!!!!”


Savanna akaogopa na kuwaita madaktari ambao walimkamata na kumchoma sindano ya usingizi


“Savanna unaweza kwenda nyumbani saas.Patrick bado akili yake haijatulia.Tutaendelea kumuangalia na kama kutakuwa na tatizo lolote tutakufahamisha” daktari akamshauri Savanna ambaye alikubali na kuondoka kuelekea nyumbani kwake.Hakutaka tena kufanya kazi yoyote kwa siku ile.kili yake yote ilikuwa inamuwaza Patrick.


* * * *


Ni siku ya pili sasa toka Parick alpolazwa katika hospitali ya gereza.Hali yake ilikuwa imeimarika tofauti na siku zilizotangulia


“Halloo Patrick “ akasema Savanna aliyekuja kumsalimu asubuhi hii


“Savanna.Karibu sana” akasema Patrick huku akijilazimisha kutabasamu


“Ahsante Patrick,unaendeleaje?


“Namshukuru Mungu leo sijambo.Naendelea vizuri sana.Madaktari wamenisaidia sana kunirejesha katika hali ya kawaida” Akajibu Patrick ambaye siku hii hakuwa amefungwa pingu kama siku zilizotangulia.


“Nashukuru sana kama unaendelea vizuri” akasema Savanna huku akiifungua chupa ya chai aliyokuja nayo na kummiminia Patrick chai katika kikombe


“mama na ndugu zangu wote hawajambo? Akauliza Patrick


“wote wazima na wanaendelea vizuri .Ninapita kila siku kuwasalimu na kumpa mama maneno ya matumaini.Mama anafarijika sana kila anionapo.Utanisamehe kwa kuwa sijawaambia chochote kuhusiana na wewe kulazwa hapa hospitali.Niliogopa kumuongezea mama matatizo hasa katika wakati huu ambao hali yake imeanza kuimarika.”


“Ulifanya vizuri sana Savanna kutokuwaeleza chochote.Wamekwisha umia vya kutoka kwa sababu yangu na sitaki waendelee kuumia zaidi.Nataka niendelee kuteseka mimi mwenyewe.” Akasema Patrick


“Savanna nakushukuru sana .Sipati nena la kuelezea shukrani zangu .You are my true friend.Umekuwa na mimi toka dakika ya kwanza na hadi leo hii haujaniacha hata siku moja.Savanna you have a special place in my heart.Sikujua kama siku moja wewe ndiye ungekuja kuwa mkombozi wangu.Watu niliowaamini na kuyatoa maisha yangu kwa ajili yao leo hii hawako tena na mimi,wamenisaliti na kuniacha peke yangu.Rafiki yangu Andrew,Happy…” Patrick akainama akazama katikam awazo halafu akainua kichwa na kusema


“Savanna naomba unisaidie ili niweze kutoka humu gerezani kwani sioni tena sababu ya mimi kuendelea kukaa humu gerezani.Nimempoteza Vero msichana aliyenipenda kwa moyo wake wote kwa ajili ya mtu ambaye haoni thamani yangu kwake.I was so wrong” Akasema Patrick kwa uchungu.


“Patrick usijilaumu sana kwani hukutegemea kama yangetokea haya yaliyotokea.Pamoja na kuondoka kwa Vero lakini kaa ukijua kwamba bado kuna watu wengi wanaokupenda na kukuombea usiku na mchana ili uweze kutoka salama gerezani na kuendelea na maisha yako.Familia yako,Happy na m………” kabla hajamaliza sentensi yake Patrick akasema kwa ukali


“Savanna tafadhali naomba usilitamke jina la huyo Malaya mbele yangu tena.Hilo ni jina ambalo sitaki kulisikia tena katika masikio yangu.Nilimpenda sana nikampa mwili na moyo wangu,nilikuwa tayari kuachana na kila kitu kwa ajili yake lakini kwa alichonifanyia sidhani kama nitakuja kumsamehe Happy.Savanna nimeumia sana.Sikuona sababu ya kuendelea tena kuishi siku ile niliponyeshwa picha za uchafu wake.” Akasema kwa uchungu Patrick


“Sijui nimweleze ukweli kuhusu suala hili? Lakini hapana,siwezi kufanya hivyo.Tayari amekwisha mtoa Happy akilini mwake na hii ni nafasi yangu sasa.Nataka Patrick awe wangu na inanibidi kuitumia vyema nafasi hii niliyoipata.Sintamweleza lolote kuhusiana na Happy” Akawaza Savanna


“Patrick pole sana.Hata mimi nilistuka sana nilipoziona picha za Happy katika gazeti na mitandao.Niliogopa sana hata kukwambia kwani nilijua ungeumia mno.” Akasema Savanna


“Usijali Savanna.Kuna watu walioguswa sana na kitendo kile na wakaniletea picha zile ili niangalie uchafu alioufanya mtu niliyemkabidhi moyo wangu.Siwafahamu watu hawa lakini nawashukuru sana kwa kunisaidia kutambua kwamba mtu niliyedhani ni kondoo ,alikuwa ni chui.Sikutegemea kama Happy angeweza kutenda kitendo kichafu na cha kujidhalilisha kama kile.Ninachoweza kukuomba kwa sasa ,nisaidie niweze kutoka humu gerezani na nianze upya maisha yangu.tafadhali Savanna usiniache nikafungwa kwa sababu ya mtu ambaye haioni thamani yangu kwake.”


“Patrick usijali kuhusu hilo.Kama nilivyokwisha kuahidi na ninavyoendelea kukuahidi ni kwamba nitafanya kila niwezalo ili uweze kushinda kesi hii.Bado hujachelewa kuyaanza upya ,maisha yako.Siku zote fahamu kwamba umezungukwa na watu wanaokupenda na kukujali kwa hiyo usijione mpweke.I’m right here for you any time you need a friend” akasema Savanna..


**********************




Dr Consolata bugama bingwa wa magonjwa ya akili,aliagana na mgonjwa wake akapanda gari lake na kuondoka pale Reonaldo hoteli.Happy alilitazama gari lile hadi lilipotoka kabisa katika lango la hoteli ile ya kifahari jijini Kigali.Akatabasamu na kuelekea katika sehemu ya kupumzikia


Ni siku ya tisa sasa toka alipokuja katika jiji hili la Kigali.Hali yake ilikuwa inaimarika siku hadi siku.Kwa msaada mkubwa anaoupata toka kwa daktari aliyeambatana naye toka Dar es salaam pamoja na Dr Consolata bingwa wa magonjwa ya akili katika hospitali kuu ya Kigali hali yake ilikuwa ya kuridhisha sana.


“Namshukuru sana Mungu kwa huruma yake hivi sasa ninaendelea vizuri.Sikutegema kama hali yangu ingekuwa namna hii.Mungu ni mwema sana na bado ananipenda na ndiyo maana hakuruhusu nife kwa sumu.Nawashukuru sana madkatari wangu kwa jitihada zao za kuhakikisha kwamba ninarejea katika hali yangu ya kawaida.Dr Consolata amejitahidi sana kuhakikisha kwamba akili yangu inarejea katika hali yake ya kawaida.Namshukuru sana pia Christine.Huyu dada amekuwa ni mtu wangu wa karibu na kila mara ninapohitaji mtu wa kuongea naye yeye amekuwa tayari kufanya hivyo.Siwezi kuusahau uongozi na wafanyakazi wa hoteli hii .They are all wonderfull people.Ni wakarimu na wote wananipenda sana.Ninahudumiwa kama mtoto wa rais.Ninapenda sana kuendelea kuishi hapa.Nimepapenda Kigali.I feel so Happy and safe around here” akawaza Happy huku akitabasamu


“Ouh gosh ! siwezi kumsahau Savanna.Japokuwa moyo wangu unastuka kila ninapoikumbuka sura yake lakini sina budi kumshukru kwa msaada mkubwa alionipatia.Najua hata wazo la kuondoka Tanzania na kuja Kigakli ni yeye ndiye aliyelitoa na kulisimamia kwa nguvu zote na likafanikiwa.Amenisaidia mno kuniondoa katika aibu na fedheha niliyoipata.Niko nje ya Tanzania sasa,ninashukru sana kwa sababu aibu niliyoipata ni kubwa na ambayo inanifanya nisitake tena kurudi Tanzania.Inaniuma sana kuiacha nchi yangu na kumuacha Patrick mwanaume wa maisha yangu niliyempigania kwa kila namna niliyoweza lakini kwa hili lililotokea nimeinua mikono.Sina namna nyingine zaidi ya kukubali kushindwa na kumuacha Patrick mikononi mwa Savanna.Najua atakuwa katika mikono salama.Mimi na Patrick hatuwezi kuwa pamoja tena.Huu ni ukweli ambao hatuwezi kuukwepa.” Akawaza Happy na sura yake ikaanza kubadilika na kuwa ya huzuni kidogo


“ Najaribu kumuhusisha Savanna na tukio lile la kutekwa kwangu lakini sioni kama ana uhusika wowote katika jambo lile.Kama si yeye nani basi anaweza kuwa nyuma ya tukio lile? Picha niliyoipata ni kwamba watu walionitenda vile lengo lao lilikuwa ni kunidhalilisha na kuhakikisha kwamba kwa namna yoyote ile ninaachana na Patrick.Laiti ningejua kwamba lengo lao ni hilo nisingekubali kufanyiwa udhalilishaji ule mkubwa.Anyway namuachia Mungu yeye ndiye atakayenilipia kwa mambo yote niliyofanyiwa.” Akaendelea kuwaza Happy


“Najua maisha yangu hayatakuwa na furaha tena na ninajua kwamba sintampata mwanaume kama Patrick katika maisha yangu yaliyobaki lakini ni vyema endapo nitakwenda kuishi mbali kabisa naye,mbali na Tanzania .Sitaki kukaa karibu naye kwani itanifanya niendelee kulipigania penzi letu na kadiri ninavyoendela kuupigania uhusiano wetu ndivyo mambo mabaya yanavyozidi kunitokea.Nimekwisha msababishia Patrick maumivu mengi ya moyo na sitaki aendelee kuumia zaidi.Nadhani uamuzi huu wa kutorejea tena Tanzania ni uamuzi wa busara sana ingawa najua Patrick ataumia mno na kunichukia.Ataniona kama ni msaliti na nilifanya kitendo kile kwa makusudi.Hakuna siri siku hizi hata kama yuko gerezani lazima atazipata taarifa zangu na nina hakika ataamini kwamba hii ndiyo tabia yangu.Ouh gosh ! ni mateso makali sana ya moyo atakayoyapata..” Akawaza Happy halafu akainuka na kuanza kuzunguka bustanini


“Dr Consolata amekuwa akijitahidi sana kuhakikisha ninasahau yaliyopita .Sipaswi kuendelea kuyafikiria yaliyopita.Ninachotakiwa kufanya kwa sasa ni kufikiri kuhusu maisha yangu ya mbele yatakuwaje.” akawaza Happy huku akiendelea kuzunguka zunguka mle bustanini


“Nimeipenda sana Rwanda .Ni nchi nzuri na ningefurahi mno kama ningeishi katika nchi hii kwa maisha yangu yote yaliyobakia.Lakini siwezi kufanya hivyo.Lazima niondoke Rwanda.Natakiwa kwenda kuishi mbali kabisa na Tanzania ikiwezekana nje kabisa ya Afrika.Nataka nikaishi mahala ambako nitaishi bila kuonana na mtu yeyote wa kutoka Tanzania.Kuna mtu mmoja tu ambaye anaweza akanisaidia katika hili. Ni Mike pekee.Najua niliutia moyo wake jeraha kubwa ambalo si rahisi kupona haraka ,niliuvunja vunja moyo wake pale nilipoamua kuachana naye na kurudiana na Patrick.Najutia nafsini kwangu kwa kitendo kile.It needs more than a man to forgive me for what I did.Japokuwa kabla hajaondoka Tanzania alinihakikishia kwamba amenisamehe lakini sina hakika kama ataweza kukisahau kitendo kile nilichomfanyia.”


Happy akasimama baada ya picha ya Mike akiondoka Tanzania chini ya ulinzi mkali kumjia kichwani.


“Ouh Gosh ! forgive me Mike” akasema Happy huku akisikia uchungu mwingi moyoni


“Sina hakika kama Mike anaweza kuwa tayari kunisaidia au hata kunisikiliza lakini sitakiwi kukata tamaa.Natakiwa kujaribu kumuomba anisaidie.Endapo atakataa kunipa msaada ninaoutaka nitatafuta namna nyingine ya kufanya.Nitamuomba hata Savanna anisaidie.Kitu pekee ninachokiami na kinachonipa msukumo wa kutaka kuwasiliana na Mike ni kwamba Mike ananipenda kwa moyo wake wote.” Akawaza Happy na kuupeleka mkono sehemu ulipo moyo wake ambao ulikuwa unadunda kwa kasi kubwa.


“lazima niwasiliane naye na nimuombe anisadie.Lazima niondoke hapa Kigali na kwenda mbali.Namuonea huruma sana baba yangu .Amekuwa nami kwa kipindi kirefu toka matatizo haya yalipoanza na yeye ndiye amekuwa msaada mkubwa kwangu.Ni wakati sasa wa yeye kupumzika na kuendelea kufanya shughuli zake za kimaendeleo.Ninajisikia furaha sana kuwa na baba kama huyu.He’s the best father in the world.” Akawaza Happy na kutabasamu


“Ngoja sasa nikampigie simu Mike.” Akawaza Happy na kuelekea chumbani kwake.Alipoingia chumbani kwake akasimama mbele ya meza iliyokuwa na simu akaitazama simu ile na kuvuta pumzi ndefu.


“I’m so scared” akasema kwa sauti ndogo.Kwa takribani dakika tatu alisimama akiitazama simu ile.Alihisi kama mikono yake ikimtetemeka kila alipojaribu kutaka kuichukua simu ile na kupiga


“Mungu wangu tafadhali naomba unisaidie.Nahitaji kufanya hivi.Nahitaji kuongea na Mike” akasema Happy kwa sauti ndogo.Baada ya tafakari akaamua kupiga.Alizifahamu namba za simu ya mkononi ya Mike na akaziandika huku mapigo ya moyo wake yakienda kwa kasi kubwa.Akauweka mkono wa simu sikioni na simu ikaanza kuita.Baada ya sekunde kadhaa akasikia sauti ikimwambia


“Mike hayuko katika nafasi ya kupokea simu kwa sasa tafadhali acha ujumbe wako baada ya mlio.” Happy akavuta pumzi ndefu na mara baada ya mlio kusikika akasema


“Hallow Mike,ni mimi Happy.Naomba upatapo uumbe huu,unipigie simu.Kwa sasa niko Kigali Rwanda,Reonaldo hoteli presidential suit number two.Please call me back Mike.I real need to talk to you” Happy aliyasema maneno haya huku machozi yakimtoka.Akauweka mkono wa simu chini ,akapangusa machozi na kwenda kuketi sofani


“Please Help me Mike” akasema kwa sauti ndogo


Baada ya dakika tano kupita simu ikaita.Akainuka na kwenda mezani akasimama na kusita kuipokea.Simu ikaendela kuita na mwishowe akaamua kuipokea.


“hallo “ akasema Happy


“Hallow Happy.Mike hapa nongea” Ikajibu sauti ya upande wa pili.Mikono ya Happy ikaloa jasho.Kwa sekunde kadhaa alihisi kama sauti yake ikigoma kutoka


“Hallow Mike” akasema Happy kwa sauti yenye kitetemeshi


“Hallow Happy.Unaendeleaje? Nimeupata ujumbe wako muda si mrefu.Habari ya Tanzania?


“habari ya Tanzania nzuri ila kwa sasa niko Kigali Rwanda”


“Sawa Happy.Nashukuru sana kwa kunikumbuka .Patrick anaendeleaje?


Swali lile likamchoma sana Happy akahisi kama miguu inaisha nguvu


“ Anaendelea vizuri” akajibu kwa ufupi


“Happy una tatizo gani? Naisikia sauti yako kama haiko sawa.Ninakufahamu vyema wakati una tatizo”


Happy akakaa kimya akahisi kama midomo yake inashindwa kufunguka


“ Happy una tatizo gani? Akauliza tena Mike


Happy akakohoa kidogo na kusema


“Mike ni kweli nina tatizo na ninahitaji msaada wako” kimya kifupi kikapita Mike akasema


“Una tatizo gani Happy?


“Mike siwezi kukueleza katika simu ni tatizo kubwa.Najua kwa sasa mimi ni mtu ambaye hupendi kuniona na hata kuisikia sauti yangu kutok…………”


“No ! No ! Happy.Usifikiri hivyo” mike akamkatisha Happy


“Ni kweli Mike.Hata mimi mwenyewe nafsi yangu inanisuta sana kwa kitendo nilichokufanyia lakini pamoja na hayo yote yaliyotokea sina mtu mwingine ninayeweza kumkimbilia kuomba msaada kwa sasa.Mike najua ndani kabisa mwa moyo wako bado nina nafasi japokuwa ndogo sana.Ninakuomba kama rafiki unisaidie” akasema Happy huku machozi yakimtoka.Kupitia spika za simu Happy akamsikia Mike akivuta pumzi ndefu na kusemaCHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/


“Happy,napenda niwe wazi kwako kwamba kilichotokea baina yetu kiliniumiza sana.Nilipata jeraha ambalo halitaweza kutibika.Ulipoamua kuniacha niliumia sana.hadi hivi sasa bado ninaamini kilichotokea ni kama ndoto na ndiyo maana nilipoupata ujumbe wako nimekupigia simu mara moja.” Akasema Mike na kunyamaza .Maneno yale yakamuumiza sana Happy na kuzidi kumtoa machozi.Mike akaendelea


“Happy kama nilivyosema siku ile nilipokuja kukuaga kwamba mimi tayari nimekusamehe na wala sina kinyogo chochote nawe.Kwangu mimi ,wewe bado ni mtu muhimu sana na rafiki wa pekee kabisa. Niko tayari kukupa msaada wowote na kwa wakati wowote.Naomba unieleze unahitaji msaada gani Happy? Akasema Mike .Happy ambaye kifua chake kilikuwa kimeloa machozi akasema


“Mike kwa sasa nimekwama hapa Kigali na lengo langu kubwa ni kuondoka hapa. Nataka kuja Marekani lakini sina namna ya kuondoka hapa.Naomba unisaidie ili niondoke hapa kuja Marekani.Nahitaji kuwa mbali na Tanzania.Tafadhali Mike nahitaji sana msaada wako sasa kuliko wakati wowote katika maisha yangu.Tafadhali naomba unisaidie Mike” Happy akaomba.Sauti yake ilitia huruma sana na ilionyesha dhahiri ni jinsi gani alivyokuwa akihitaji msaada wa Mike


Mike akavuta pumzi ndefu ,kikapita kimya cha dakika moja halafu akasema


“Nimekuelewa Happy.Nitakusaidia.Siwezi kukuacha wakati wa matatizo.Nitakusaidia Happy.Ninachohitaji kufahamu ni kama nyaraka zako zote za kusafiria unazo?


“Ndiyo Mike.Nyaraka zote ninazo hapa”


“Sawa Happy.Usijali nitakusaidia .Nitakupigia simu jioni ya leo kukufahamisha mchakato mzima ulivyo”


“Ouh Mike nakushukuru sana kwa kukubali kunisaidia” akasema Happy huku uso wake ukichanua kwa tabasamu


“Ni wajibu wangu kukusaidia Happy na nitafanya hivyo.Nitaongea nawe tena jioni ya leo kwa kirefu zaidi”


“Ahsante Mike” akasema Happy na kukata simu


“Ouh Gosh ! Siamini kabisa kama Mike amekubali knisaidia. Nasikia aibu sana kumuomba msaada Mike lakini kwa wakati huu nimekwama na ni yeye pekee anayeweza kunisaidia.Ninaamini Marekani nitaweza kuishi kwa amani bila bughudha.Ouh Mungu wangu naomba unisaidie ili Mike asiweze kubadili mawazo yake.” Akawaza Happy


Wakati Happy akiwa katika lindi la mawazo lililochanganyika na furaha mara kengele ya mlangoni ikalia. Haraka akajipangusa machozi na kuelekea mlangoni.Alikuwa ni baba yake mzee Kibaho aliyetoka kuvinjari mitaa ya jiji hili la Kigali


“Ouh Dady..!!” akasema Happy na kumkumbatia baba yake.


“I missed you dady” akasema Happy.Baba yake akamtazama kwa makini usoni


“Ulikuwa unalia? akauliza mzee Kibaho .Happy akakaa kimya


“Happy una tatizo gani? Siku zote nimekuwa nikikwambia kwamba kama una tatizo lolote usisite kuniambia”


“Ni kweli baba nilikuwa nalia lakini machozi ya furaha.


“Machozi ya furaha?


“Ndiyo baba”


“Umefurahi nini leo?


“Dady kwanza kabisa napenda sana nikushukuru kwa upendo wako mkubwa kwangu.Dady umekuwa nami katika matatizo yangu.Hujawahi kuniacha hata sekunde moja toka nilipoanza kuandamwa na matatizo.You are the best dady in the whole world.I’m proud to be your daughter.” Akasema Happy na kumfanya mzee Kibaho atabasamu


“dady umekuwa nami hata katika nyakati zile ambazo hakuna mwingine aliyethubutu.Kazi uliyoifanya ni kubwa na ninadhani ni wakati wako sasa wa kupumzika”


“Happy unazidi kunichanganya.Hata siku moja sijawahi kuchoka wala sintachoka kuwa nawe kwani ni jukumu langu kuhakikisha kwamba siku zote binti zangu wanakuwa na furaha.”


“Nafahamu hilo dady na ndiyo maana nasema kwamba wewe ni baba wa kutiliwa mfano duniani.Nimesema kwamba ni wakati wako wa kupumzika kwa sababu nimeamua kuondoka Kigali


“Unaondoka Kigali? Mzee Kibaho akashangaa


“Ndiyo dady.Kigali ni mji mzuri na ninapapenda sana na ningependa kama maisha yangu yote yaliyobaki ningeishi hapa lakini kuwepo kwangu hapa kutaendelea kunikumbusha tukio lile.Baada ya kufikiri sana nimeamua ili niweze kulisahau kabisa tukio lile basi niende kuishi mbali na nyumbani,mahala ambako sifahamiki na sintaweza kukutana na mtu yeyote anayenifahamu.Nataka niyaanze maisha yangu mapya.Nataka nisahau yale yote yaliyonipata japokuwa najua si kazi rahisi lakini nitajilazimisha kufanya hivyo .Maisha yangu mapya nataka kwenda kuyaanza mbali kabisa mahala ambako ni familia yangu pekee watapafahamu”


“Happy nashukuru sana kwa maamuzi hayo.Siku zote hilo limekuwa ni wazo langu kwamba ukaanze maisha mbali kabisa na nyumbani ikiwezekana nje ya afrika.Ni wapi umefikiria kwenda ili tuanze mchakato wa Safari.?


“Ouh dady.Huna haja ya kusumbuka.Tayari nimekwisha pata msaada .Nitakwenda kuishi Marekani”


“marekani?


“Ndiyo baba”


“marekani yuko Mike na ukumbuke bado atakuwa na hasira kwa mambo yaliyomtokea Tanzania.Nina wasi wasi anaweza akakufanyia kitu kibaya cha kulipiza kisasi”


“hapana baba.Huwezi kuamini kwamba Mike ndiye anayenisaidia mimi katika mchakato huu wa kurejea Marekani”


“Happy…!!!!” akastuka mzee Kibaho


“Usiogope baba.Tayari nimekwisha ongea naye na ameniahidi kunisaidia.”


Mzee Kibaho akamtazama mwanae kwa makini na kusema


“Do you trust him?


“Yes dady ! I trust him.Mike ananipenda sana na hawezi kukataa kunisaidia”


“Najua Mike bado anakupenda na anaweza kuwa amekubali kukusaidia kwa matumaini kwamba mtarejesha mahusiano yenu.Naomba nisikie toka kwako je bado unampenda Mike na uko tayari kurudana naye?Vipi kuhusu Patrick?..akauliza mzee Kibaho.Haoppy akafikiri kidogo na kusema


“I don’t know dady… I real don’t know what going to happen there.Kuhusu Patrick I think its right time now that I let him go.Matatizo niliyoyapata katika kipindi hiki kifupi nilichokutana naye yametosha na sintaweza kuvumilia zaidi.Dady nimekuwa ni mtu wa kulia kila siku kutokana na majanga yasiyokwisha.Inauma kusema lakini ni ukweli ulio wazi kwamba mimi na Patrick hatuwezi kuwa pamoja tena.NI vyema kama tutatengana kwa sasa.Ninaumia sana kwa kuamua kuondoka na kumuacha Patrick gerezani kwa kosa nililolisababisha mimi lakini sina namna ya kufanya siwezi tena kurejea Tanzania.Nina hakika Savanna atahakikisha kamba hafungwi gerezani.Savanna amenihakikishia kwamba Patrick atakuwa huru na ataendelea na maisha yake.Patrick told me to put a trust in her and I trust her. It hurt so much dady.All these years I’ve been dreaming that some day I’ll be married to Patrick but now I have to forget him.”” akasema Happy huku machozi yakimtoka.Kikapita kimya kirefu mzee Kibaho akasema


“Nakubaliana nawe Happy ni kweli yawezekana wewe na Patrick haikupangwa muwe pamoja.Ni vyema kama utakwenda kuishi mbali naye na kujitahidi kumsahau.Vipi kuhusu wale wanaharamu waliokufanyia udhalilishaji ule? Uko tayari kuliongelea suala hilo kwa sasa?


“No dady .I’m not ready.Thats the part of my life I’m trying to forget”


“Ok Happy usijali.Utaliongelea suala hilo pale utakapokuwa tayari”


Happy akainuka pale alipokuwa amekaa akaenda dirishani akatazama nje kisha akasema


“I’ll never be ok without Patrick.But then I have to live my life without him.It hurt so much dady……” Happy akashindwa kujizuia akazidi kulia






Tayari kiza kimetanda jijini Dar es salaam,ndani ya mkahawa mmoja maarufu sana jijini Dar es salaam,watu watatu,wanawake wawili na mwanaume mmoja walikuwa wameizunguka meza iliyokuwa imesheni vinywaji vikali


Mwanamke mmoja aliyekuwa na sigara mkononi akapuliza moshi mwingi hewani na kusema


“Khumalo tumekuja kama ulivyotutaka tuonane jioni ya leo” akasema Yule mwananmke na kuchukua glasi yake ya mvingo akapiga funda kubwa.Khumalo akawatazama wanawake wale kisha akasema


“Loniki na Linah ,nimewaiteni hapa ili kuwapeni taarifa ya maendeleo kuhusiana na kazi mliyonikabidhi.Kama mnavyokumbuka ,makubaliano yetu yalikuwa ni kuwashughulikia watu wawili waliohusika katika kifo cha ndugu yenu,.Watu hawa ni Patrick na Happy.Kwa mujibu wa Loniki ulitaka watu hawa wauawe lakini nilikushauri kwamba suala la kuua mmoja wao kati ya Hapy au Patrick kwa wakati huu lingeweza kuleta utata mkubwa na lingeonekana kabisa ni tukio la kulipiza kisasi.Nashukuru mlikubaliana na ushauri wangu na na kazi ya kwanza ikafanyika. Happy alishughulikiwa na nyote mkishuhudia.Ninathubutu kusema kwamba tulifanikiwa sana lengo letu kwa Happy kwani toka picha zile na video kutolewa Happy amepotea na hajulikani alipo.Vijana wangu wamekuwa wakimtafuta lakini hakuna anayefahamu mahala alipo.Kuna tetesi vile vile kwamba alijaribu kujiua kwa kunywa sumu lakini hakuna aliyepatikana kulithibitisha hilo kwani hospitali ile aliyotibiwa wamegoma kata kata kuthibitisha taarifa hizo.Kuhusu Patrick tulifanikiwa kumpekekea picha za Happy na alipoziona nusura apandwe na uchizi.Nina hakika kwamba tumefanikiwa kuyavunja mahusiano ya watu hawa na hivi sasa watu hawa wote wawili watakuwa katika mateso makubwa sana.Happy akiteseka kwa picha zile na Patrick akiteseka kwa kumuona mpenzi wake akifanya jambo kama lile. Jana usiku nilipokea simu toka kwa Linah akiniambia kwamba Loniki bado hajaridhishwa na jambo tulilolifanya na anataka Patrick na Happy wauawe.” Khumalo akanyamaza kidogo akanywa mvinyo na kuendelea


“Loniki naomba niwe wazi kwako kwamba suala la kumuua Patrick kwa sasa limekuwa gumu kidogo kwa sababu ulinzi umeimarishwa sana pale gerezani toka alipopelekewa picha zile za Happy na akazua tafrani kubwa.Kwa sasa wanaoruhusiwa kuonana naye ni mawakili na familia yake tu.Ninashauri kwamba suala hili la kumuua Patrick au tulivutie subira kwanza ili tuweze kutafuta namna bora kabisa ya kuweza kuutekeleza mpango huu.Endapo tutataka kulazimisha jambo hili linaweza kutuletea matatizo”


Kauli ile ya Khumalo haikuonekena kumfurahisha Loniki


“Ouh gosh..!!” akasema Loniki na kukaa kimya


“Mbona umestuka Lonny? Akauliza Khumalo


“Damn you Khumalo ! laiti ungejua ni namna gani ninavyosubiri usiku na mchana kuona watu hawa wakifutika toka katika uso wa dunia usingetamka maneno hayo uliyoyatamka”


“Nahafahamu Loniki,lakini naomba ufahamu kwamba mimi ndiye uliyenikabidhi kazi na ndiye ninayefahamu ugumu wa kazi yenyewe.Hii si kazi ya kuiendea haraka.”


“Khumalo naomba usianze kuniletea hadithi zako.I’ve paid you a lot of money for this job ,so do your job..I want Patrick and Savanna dead !! ..” akasema Loniki kwa ukali.Khumalo akamtazama,akainua glasi na kupiga funda moja na kusema


“Lonny,naomba ufahamu kwamba nilikubali kuifanya kazi hii kwa heshima ya Linah.Naomba vile vile ufahamu kwamba kazi hii nimeifanya kama msaada tu kwa sababu kazi kama hii mimi huifanya kwa milioni mia mbili na zaidi.Nimekwambia haya yote ili ufahamu kwamba sijaifanya kazi hii kwa pesa. Na endapo ukihitaji fedha zako unaweza ukaniambia nikakurejeshea na ukatafuta watu wengine wa kukufanyia kazi yako” akasema Khumalo.


“Jamani naomba tusifike huko.Loniki naomba umsikilize Khumalo anavyosema.Ushauri wake mimi binafsi naona ni mzuri tu.Tujipe muda ili tuweze kujipanga vizuri zaidi kwani hata kazi iliyofanyika ni kubwa na inatia matumaini.Patrick na Happy wote kwa pamoja wameumia sana na nina hakika hawatakuwa pamoja tena “ akasema Linah


“ Linah hujui ni namna gani nilivyokuwa nahitaji kuona Patrick na Happy wameuawa kabla sijarejea London.Kamwe moyo wangu hautakuwa na amani kumuona Patrick akiendelea kuvuta hewa hii safi wakati mdogo wangu akioza kaburini”


“Usihofu Lonny.Hata kama hautakuwepo mimi nitakuwepo kuusimamia mpango huu.Unaweza ukawa Uingereza lakini tukafanya kila kitu sisi tuliobaki huku.Ninakuahidi mimi binafsi nitashirikiana na Khumalo kwamba nitahakikisha lazima Patrick na Happy wanauwa na tunalipa kisasi kwa kifo cha Vero “ akasema Linah na kauli ile ikampa moyo Loniki na kumfanya akubaliane naye japo kwa shingo upande.


MIEZI SITACHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/


Ni siku iliyotawaliwa na kijua kikali kama ilivyo kawaida ya jiji la Dar.Pilika pilika katika jiji hili lenye shughuli nyingi ziliendelea kama kawaida.Katika mahakama ya kisutu kulikuwa na idadi kubwa ya watu tofauti na ilivyozoeleka.Ongezeko hili wa watu lilitokana na minong’ono iliyokuwa imeanza kusambaa kwamba huenda Patrick ambaye anakabiliwa na kesi ya kuua bila kukusudia,angepatiwa dhamana siku ya leo baada ya taratibu zote kukamilika.Kwa muda wa miezi sita sasa toka Patrick alipoanza kushikiliwa na polisi kwa tuhuma za kusababisha mauaji,kesi hii imekuwa ikipewa umuhimu mkubwa sana na vyombo vya habari na hasa kutokana na miss Tanzania Happy Kibaho kutajwa kuhusika katika ugomvi uliosababisha kifo cha Vero.Kutokana na kutangazwa sana na vyombo vya habari watu wengi walikuwa wanaifuatilia ili kujua nini hatima yake.


Wengi wa watu waliofika walitegemea kumuona miss Tanzania aliyevua taji lake Happy Kibaho akiwa mahakamani.Toka picha na video yake ya utupu kuchapishwa na kusambaa mtandaoni Happy alipotea ghafla na hakuna aliyefahamu mahala alipo hivyo wengi walitegemea pengine angeweza kuonekana mahakamani siku ya leo.


Hatimaye kama ilivyokuwa imetegemewa na wengi,saa saba za mchana Patrick alipatiwa dhamana baada ya masharti yote yanayohitajika kutimizwa.Kilikuwa ni kipindi cha furaha sana hasa kwa familia yake,ndugu jamaa na marafiki.Ilikuwa ni kama ndoto pale Patrick aliposhikwa mkono na Savanna na kuthibitishiwa kwamba yuko huru kuondoka.Hakuamini macho yake.


“Savanna thank you very much.” Hilo ndilo neno pekee aliloweza kulitamka Patrick kwa wakili huyu mahiri ambaye amekuwa akimtetea katika kesi hii.Patrick akasalimiana pia na mawakili wengine ambao kwa pamoja wanaunda jopo la mawakili wanaomtetea na kisha taratibu huku akiwa ameongozana na Savanna wakatoka nje ya jengo la mahakama ambako aliendelea kusalimiana na watu mbali mbali mbali waliofika mahakamani.Wakati akiendelea kusalimiana na watu mbali mbali ,ghafla akastuka baada ya kuiona sura yenye tabasamu ya mwanadada mrembo na kuufanya moyo wake kuanza kudunda kwa kasi.Alikuwa anatazamana na Sarah dada yake Vero.Kwa sura Sarah na Vero walikuwa wanafanana sana kiasi kwamba ungeweza kudhani ni mapacha


Sarah ambaye alikuwa anatabasamu na kumkumbusha Patrick lile tabasamu alilolizoea la Vero akamsogelea na kumkumbatia.


“Pole sana Patrick.Usijali Mungu atakusaidia na mambo haya yatakwisha.” Akasema Sarah na kumshangaza sana Patrick ambaye alikosa neno la kusema midomo yake ilikuwa inamtetemeka.Hakutegema kama Sarah angeweza kuongea naye kistaarabu namna ile hasa baada ya kusababisha kifo cha mdogo wake.


“Sarah nashukuru sana” Patrick akasema.Sarah akatabasamu na kusema


“Patrick tutaongea siku nyingine kwa sasa unahitaji mapumziko.” Akasema Sarah halafu wakaagana akaondoka zake.Baada ya Patrick kusalimiana na watu wengi waliokuja kumpa pole siku hii ya leo,Savanna akamshika mkono na kumuongoza hadi katika gari lake na ndugu wengine nao wakaingia katika magari yao na kuondoka pale mahakamani.Patrick alikuwa amegeuza shingo yake akiangalia nje na mara akavuta pumzi ndefu


“Ouh my gosh ..!!! “ akasema Patrick akionekana kustushwa na kitu Fulani


“Patrick whats wrong? Akauliza Savanna


“Bado naona ni kama muujiza vile leo nimerejea tena uraiani.Sipati neno la kukushukuru Savanna.Ni Mungu pekee ndiye atakayekulipa” akasema Patrick


“Ouh Patrick plase don’t say anything.Ni wajibu wangu kufanya hivi na huna sababu ya kunishukuru” akasema Savanna huku akitabasamu


“Unanipeleka wapi,nyumbani kwangu au kwa mama? Akauliza Parick


“Patrick ,haitakua vizuri kama ukienda nyumbani kwako kwa sasa.Nyumba ile ina kumbukumbu nyingi ambazo zitakukumbusha historia ya wewe na Vero ambayo unajitahidi kuisahau.Nyumbani kwa mama nako kuna kumbukumbu nyingi ambazo zitakukumbusha kuhusu baba.Unatakiwa kwanza kuwa tayari kukabiliana na hayo yote.Nashauri kwanza upate mapumziko halafu tutakwenda nyumbani kwa mama lakini kwa sasa utakwenda kuishi kwangu .Nimekuandalia chumba maalum.Pale utapata kila kitu unachokihitaji hadi hapo utakapojisikia kuwa tayari kurejea kwako” akasema Savanna.Patrick akatabasamu


“Nilipenda sana kufika nyumbani kwa mama siku ya leo.Najua hata yeye pia ana hamu kubwa ya kuniona”


“Nyumbani kwa mama utakwenda lakini kwanza unatakiwa ukaoge,upate chakula,upumzike kidogo halafu ndipo uwe tayari kuonana na mama”


“Ok Savanna.Wewe ndiye kiongozi wangu kwa sasa.Siwezi kukupinga kwa lolote” akasema Patrick huku akicheka na kumfanya Savanna naye acheke


“Simu hii hapa mpigie Alois na umtaarifu kwamba utakwenda nyumbani kwa mama jioni ya leo” akasema Savanna.Patrick akaichukua simu ile na kumpigia Alois akamtaarifu kwamba atakwenda kuonana nao jioni.


* * * *


Geti la rangi nyeupe likafunguliwa na gari aina ya Range rover vogue likaingia katika jumba la kifahari lenye rangi nyeupe.Milango ikafunguliwa akashuka Savanna na Patrick


“Karibu nyumbani Patrick” akasema Savanna


“Ahsante sana Savanna.Una nyumba nzuri sana” akasema Patrick huku akitabasamu.Waliingia ndani ya sebule kubwa


“Jisikie nyumbani Patrick” akasema Savanna


“Nashukuru sana Savanna.Nyumba yako nzuri mno” akasema Patrick huku akitabasamu.Mtumishi wa ndani akafika na kuwahudumia vinywaji.


Baada ya maongezi kidogo,Savanna akampeleka Patrick katika chumba maalum kilichoandaliwa kwa ajili yake


“Patrick, hiki ndicho chumba chako.Nimekiandaa maalum kwa ajili yako..Utaishi hapa hadi hapo utakapojisikia kurejea katika makazi yako.Nimejaribu kuweka karibu kila kitu unachokipenda.Katika kabati kuna nguo nilizokuandalia na sina hakika kama nimekosea vipimo” akasema Savanna na wote wakacheka halafu Savanna akamuacha Patrick na kwenda chumbani kwake .


Patrick aliingia bafuni na kabla ya kuoga akasimama kwanza na kuzama katika mawazo


“Hatimaye nimekuwa huru tena.Naona ni kama ndoto lakini huu ndio ukweli nimerudi tena nyumbani baada ya kusota gerezani kwa muda wa miezi sita.Ama kweli maisha yanaweza kubadilika ndani ya sekunde moja kama yalivyobadilika kwangu.Sikuwahi kuota kma maisha yangu yangebadilika namna hii” akawaza Patrick na mara sura ya Vero ikamjia kichwani


“Sura hii ya Vero itaendela kuniandama kwa muda mrefu sana na kuifuta sura hii kichwani kwangu itanichukau muda pia” akawaza Patrick


Baada ya kuoga akajumuika na Savanna wakapata chakula pamoja halafu akarejea chumbani kwake kupumzika.


“Ni muda mrefu sijalala katika sehemu nzuri kama hii.I missed this life a lot.Shukrani za pekee zimwendee Savanna ambaye amepambana na kuhakikisha ninapata dhamana.Savanna ni mwanamke wa shoka.Nina deni kubwa kwake.Amenionyesha kwamba yeye ni rafiki wa kweli kuliko hata wale niliowaamini kwa moyo wangu wote.Ni Mungu peke atakaye mlipa Savanna kwa wema wake huu mkubwa” akawaza Patrick


“Kwa sasa natakiwa kujipanga kwa ajili ya kuanza upya maisha yangu.Nimepoteza kila kitu.Nimepoteza kazi,nimewapoteza wapendwa wangu Vero na Happy , hata Andrew rafiki yangu mkubwa naye ameniacha na sina taarifa zake tena. Sijilaumu sana kwa kilichotokea bali napaswa kutuliza akili na kujipanga upya.Bado sijachelewa kuyapanga na kuyajenga upya maisha yangu bila ya wale niliowapenda .Tukio lililotokea limenifundisha mambo mengi sana na safari hii sitaki kurudia makosa.Nakiri nilifanya kosa kubwa kuachana na Vero.Sikupaswa kufanya vile.Vero alikuwa ni mwanamke aliyenipenda kwa moyo wake wote na siku zote alikuwa tayari kwa lolote kwa ajili yangu.Nilimpuuza,nikaupuuza upendo wake kwangu na kuamini kwamba Happy ndiye mwanamke ambaye nimepangiwa niwe naye katika maisha.Nilijidanganya sana.Mimi na Happy katu hatuwezi kuwa pamoja.Tumekwisha jaribu na imeshindikana na tayari nimemfahamu Happy ni nani.Nashukuru nimeweza kumuondoa moyoni mwangu na amebaki ni katika historia ya maisha yangu lakini moyo wangu haudundi tena kwa ajili yake.Alichokifanya kimenifanya nimvue thamani kabisa na hana nafasi tena moyoni mwangu” Akawaza Patrick halafu akafumba macho na kulala


Saa moja za jioni akiwa ameongozana na Savanna akawasili nyumbani kwa wazazi wake ambako baadhi ya ndugu walikuwa wamekusanyika ili kumpa pole kwa masahibu yaliyomkuta.Wote walijawa na furaha kubwa kwa Patrick kurejea tena nyumbani.Chakula kizuri kiliandaliwa,wakala na kunywa na ilipofika saa tano za usiku Patrick na Savanna wakaondoka kurejea nyumbani kwa Savanna ambako Patrick aliwekewa makazi yake ya muda


* * * *


Saa nne za asubuhi siku iliyofuata iliwakuta Patrick na familia yake katika kaburi la baba yao.Alois ndiye aliyeongoza sala fupi ya kumuombea marehemu baba yao halafu ukafuata wakati wa kuweka shada za maua.Patrick aliyekuwa amevalia suti nyeusi ndiye aliyekuwa wa kwanza kuweka shada la maua juu ya kaburi la baba yake.Akaliweka karibu kabisa na msalaba halafu akapiga magoti na kuliinamia kaburi


“Baba kokote uliko hivi sasa naomba unisamehe sana kwa mambo niliyoyafanya na kusababisha kifo chako.Sikutegemea kama maamuzi yangu yangetufikisha hapa.Ninasikia uchungu mkubwa sana ambao si rahisi kuuelezea.Baba nahitaji msamaha wako ili niweze kuondokana na mateso haya makubwa niliyonayo na nianze maisha mapya.Siku zote nitakuombea kwa Mungu ili aipumzishe roho yako mahala pema peponi Amina”


Baada ya kumaliza maombi yale mafupi ya kimya kimya akainuka na kuwapa nafasi ndugu zake wengine nao waweke shada zao za maua.Zoezi lile lilipokamilika Patrick na Savanna wakaingia garini na kuondoka kuendelea na ratiba nyingine ya siku hiyo.


“Kinachofuata sasa hivi kwa mujibu ratiba yetu tunaelekea katika kaburi la Vero” akasema Savanna


Walifika makaburini na Savanna akamuongoza Patrick hadi katika kaburi la Vero.


Hapa ndipo alipozikwa Vero” akasema Savanna.Patrick akaweka shada lake la maua na kuliinamia kaburi na machozi mengi yakamtoka.Savanna akasogea mbali kidogo na kumpa Patrick nafasi ya kuwa peke yake katika kaburi la aliyewahi kuwa mchumba wake.


“Anatia huruma sana Parick lakini hii ndiyo hali halisi ambayo lazima akabiliane nayo.” Akawaza Savanna


Baada ya dakika kumi za Parick kuliinamia kaburi la Vero akainuka.Macho yake yalikuwa mekundu na uso wake ulijaa machozi.Savanna akamsogelea na kumpa kitambaa


“its ok Patrick,Don’t cry anymore” akasema Savanna Patrick akafuta machozi.Akaendelea kulitazama kaburi lile kwa uchungu


“rest in peace Vero.You’ll always be in my heart” akasema Patrick halafu wakaondoka .


Toka makaburini ,Patrck na Savanna wakaendelea na safari yao hadi nyumbani kwa Patrick.Walinzi toka katika kampuni binafsi ya ulinzi ya Chem Chem security waliendelea kuilinda nyumba ya Patrick kwa kipindi chote ambacho Patrick alikuwa gerezani


“Welcome home Patrick” akasema Savanna huku akitabasamu.Patrick alishindwa kuzuia furaha yake alipoishuhudia nyumba yake namna ilivyokuwa imependeza.Ilikuwa imepakwa rangi nzuri nyeupe na kupandwa maua mengi kuizunguka.


“wow !! its incredible…!!!” akasema Patrick kwa furaha


“Nyumba yote ni salama.Imeendelea kulindwa na kampuni hii ya ulinzi kwa kipindi chote ulichokuwa gerezani.Niliingia nao mkataba wa mwaka mmoja wa kuendelea kuilinda nyumba yako na tayari fedha zote nimekwisha zilipa.Vile vile nyumba yote imepakwa rangi kwa nje.It looks beautiful,isn’t it?


“Savanna sijui hata niseme nini.Sijui nikushukuruje.The house looks so beautiful.Sikutegemea kama ningeikuta nyumba yangu katika hali hii.Ahsante sana Savanna kwa kunitunzia nyumba yangu.” Akasema kwa furaha Patrick na kuufungua mlango mkubwa akaingia ndani.Patrick alionekana kama anaiogopa nyumba yake.Hakutaka kugusa kitu chochote mle sebuleni.Walitoka sebuleni wakazunguka katika baadhi ya vyumba na hatimaye wakaingia katika chumba cha kulala cha Patrick.Mara tu walipoingia Patrick akastuka sana baada ya kuziona picha mbili kubwa zilizowekwa ukutani.Ilikuwa ni picha yake na Veronika.Alisimama kwa sekunde kadhaa akizikodolea macho picha zile kubwa


Juu ya kitanda kulikuwa na nguo za vero ambazo alizivua na kuziweka kitandani mchana wa siku ile ya kufariki kwake.Patrick akakumbuka dakika za mwisho akiwa na Vero mle chumbani.Vero alikuwa akimkumbatia kwa mahaba mazito.Alikumbuka namna walivyofanya mapenzi kwa mara ya mwisho na walipanga kuendelea tena jioni yake lakini Vero hakurejea tena katika chumba kile


“That’s the day I’ll never forget in my life.It’s the day that I made the biggest mistake of my life.Niliipoteza dhahabu ya thamani kubwa kwa mng’ao wa jiwe” akawaza Patrick huku machozi yakimlenga


“Savanna I need to be alone for a while” akasema Patrick na Savanna akatoka mle chumbani,Patrick akaufunga mlango halafu akapanda kitandani na kuzikumbatia nguo za Vero huku akilia


“Please forgive me Vero,forgive me“ akasema Patrick huku machozi yakimtoka.Alilia sana kisha akainuka na kwenda katika meza ya vipodozi iliyokuwa imesheni vipodozi vya kila aina alivyokuwa anatumia Vero.Akalifungua kabati kubwa na kuzikuta nguo nyingi za Vero ,akaanza kuitoa nguo moja baada ya nyingine na kuziweka kitandani.Kila nguo aliyoishika ilimkumbusha nyakati zile za furaha alizokuwa nazo akiwa na Vero.Alivikusanya vitu vyote vya Vero na kuviweka katika masanduku mawili makubwa


“Natakiwa kuvirudisha vitu hivi kwa ndugu zake.Kuendelea kuviweka hapa vitanifanya nishindwe kumsahau Vero na kuendelea na maisha yangu.Nitamtafuta Sarah na kumpatia vitu hivi vya mdogo wake” akawaza PatrickCHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/


“Itanichukua muda mrefu kurejea tena katika nyumba hii.Kwa sasa itanilazimu kuendelea kuishi nyumbani kwa Savanna.Ninahisi furaha na amini nikiwa pale.Savanna ananijali sana na anajitahidi kwa kila namna niweze kurejea katika maisha yangu ya kawaida.She’s a wonderfull woman” Patrick akatabasamu halafu akatoka na kuelekea sebuleni aliko Savanna.


“Savanna itanichukua muda sana kuweza kumsahau Vero .Kuna kumbu kumbu nyingi humu ndani zinazonikumbusha mbali na hasa dakika za mwisho nilizokuwa na Vero.Laiti ningejua kama ile ilikuwa ni siku ya mwisho ya Vero basi nisingefanya vile nilivyofanya.” Akasema Patrick


“Pole Patrick.Mambo haya yote yatakwisha japokuwa ni ngumu na itachukua muda kumsahau Vero lakini naomba ujitahidi kwa kila namna kuizoea hali hii na kuiona ya kawaida”


“Nitajitahidi Savanna.I’ll be ok” akasema Patrick halafu wakazungukia nyumba yake yote na walipomaliza wakaingia garini na kuondoka kurejea katika makazi ya Savanna




Siku zilizidi kusonga huku Patrick akijitahidi kujaribu kusahau mambo yote ya nyuma na kuanza maisha mapya.Bado aliendelea kuishi nyumbani kwa Savanna.Maisha ndani ya nyumba hii yalikuwa mazuri,aliishi yeye,Savanna pamoja na mtumishi wa ndani,.


Siku moja mwishoni mwa wiki Savanna alimuomba Patrick watoke kwa ajili ya matembezi.Walikwenda katika hoteli moja kubwa na tulivu iliyokuwa na ufukwe mzuri na msafi.Savanna alikuwa amejitahidi sana kwa kila namna alivyoweza ili kumsahaulisha Patrick yaliyopita na kumfanya awe na furaha lakini bado alionekana kuna jambo linamnyima raha.


“Patrick ni jambo gani hasa linalokunyima raha? Tafadhani naomba unieleze .Mimi ni rafiki yako na kama kuna jambo lolote ambalio linakufanya usie na furaha naomba unieleze mimi nitakusaidia.” Akasema Savanna wakiwa ufukweni.


“Savanna wewe ni zaidi ya rafiki yangu kwa hiyo siwezi kukuficha kitu.Kitu kinachoninyima raha ni pale ninapowaza kuhusu maisha yangu.Kama unavyojua nimepoteza kila kitu pamoja na mwelekeo mzima wa maisha yangu.Nimepoteza kazi yangu na mpaka sasa hakuna hata kampuni moja iliyoonyesha dalili za kuniajiri tena.Ninajiona kama nina laana vile lakini hata hivyo nahitaji kusahau kilichotokea na kuanza maisha mapya lakini kadiri siku zinavyozidi kwenda najikuta nikishindwa namna ya kuweza kuanza tena maisha yangu na kujitegemea mimi mwenyewe.Sijisikii vizuri ninapokutegemea wewe katika kila jambo”


Savanna akatabasamu na kusema


“Pole Patrick lakini hukupaswa kuumiza kichwa chako namna hiyo.Ulipaswa kunieleza kuhusu jambo hilo kwani tayari ninalifahamu hilo na nina mipango mizuri kwa ajili yako ila sikuweza kukueleza mapema kwa sababu nilikuwa nataka nikwambie wakati kila kitu kimekamilika.Kwa ufupi tu ni kwamba nimeanzisha kiwanda cha kusindika nyama na muda wowote kuanzia sasa kitaanza kazi.Wewe ndiye utakayekuwa meneja wa kiwanda hicho.


.majukumu yote ya uendeshaji wa kiwanda hiki yako juu yako kwa hiyo usiumize kichwa chako kuhusiana na ajira,you are a manager now.” Akasema Savanna huku akicheka.Patrick akashindwa kujizuia akasimama akamkumbatia Savanna kwa furaha.


“Savanna ni kitu gani nimekufanyia hadi ukanifanyia mambo yote haya? Nitakulipa kitu gani? Patrick akasema huku akimtazama Savanna


“Ni wajibu wangu kufanya hivi nifanyavyo Patrick na hutakiwi kunilipa chochote .Nina imani hata mimi ningekuwa katika hali kama yako ungefanya kama nifanyavyo mimi.Isnt it Patrick?


“Ndiyo Savanna .Ningefanya kama ufanyavyo.Nisingethubutu kukuona ukiwa katika hali kama yangu.Naomba nikiri kwamba ni hali ngumu sana lakini nimeweza kuvumilia na kufika hapa kutokana na jitihada za watu wachache wanaonuipenda na kunijali wakiongozwa na wewe Savanna ,watu ambao wamesimama nami toka dakika ya kwanza ya matatizo yangu na hadi leo bado wako nami.Nina deni kubwa kwako Savanna na sijui nitalilipaje.” akasema Patrick halafu akainamisha kichwa chini akazama katika mawazo ghafla.


“Patrick unawaza nini? Akauliza Savanna baada ya kumuona Patrick amebadilika ghafla


“Savanna nimekumbuka kesi yangu.Kila mara niwazapo kuhusu kesi hii ninashindwa kujizuia kuogopa.Ninafikiria itakuwaje endapo nitahukumiwa kifungo gerezani na kushindwa kutimiza malengo yangu.Sitaki kufungwa jela kwa sababu ya mtu asiyekuwa na thamani kwangu hata kidogo.”


“Patrick siku zote nimekuwa nikikwambia kwamba usiwaze chochote kuhusiana na kesi hii. Mambo yote niachie mimi na nitalishughulikia suala hili na litakwisha.I give you my word Patrick” akasema Savanna huku akitabasamu .Kikapita kimya cha dakika mbili kila mmoja akiwaza lake


“Patrick ..!! akaita Savanna.Patrick akamtazama usoni


“Kuna jambo ambalo nataka kukueleza”


“Jambo gani Savanna?


“Patrick najua ni namna gani unavyoumia kila siku moyoni kwa haya yaliyotokea.Ninayaona maumivu yako na kuyahisi na kunifanya na mimi pia niumwe kwa kukuona ukiwa katika hali hii ya mateso makubwa ya moyo.Patrick nafahamu kwamba si rahisi kuyasahau yaliyotokea na kuanza maisha mapya kwa haraka.Itachukua muda kuwasahau wapendwa wako,vero,Happy na baba yako.Hawa ni watu uliowazoea na kuwapenda lakini leo hii hawako tena nawe.Pamoja na kwamba kumbu kumbu zao bado zinakujia ,lakini ni wakati sasa wa kuwaacha waende na wewe uuruhusu moyo wako uanze maisha mapya.Its time now to let them go.Kuondoka kwao si mwisho wa maisha yako wala ndoto zako .Bado unayo maisha marefu na yenye furaha lakini pale tu utakapoufungua moyo wako na kuuruhusu uanze maisha mapya.Ufungue moyo wako sasa kwa wale wanaokupenda na kukujali na kuwa tayari kusimama nawe katika nyakati zote za shida au raha.Pamoja na yaliyotokea lakini bado unahitaji kuwa na marafiki na hata mtu ambaye unaweza tena kumwamini na kumkabidhi moyo wako.” Akasema Savanna.Patrick akamuangalia kwa makini halafu akatabasamu na kusema


“Unamaanisha nini Savanna unaposema mtu ambaye ninaweza kumwamini na kumkabidhi moyo wangu?


“Ninamaanisha kwamba you have to learn to love again.Only love can help you forget the past” Akasema Savanna na kumfanya Patrick atabasamu na kucheka kidogo


“Mbona unacheka Patrick? Ni kosa la jinai kupenda? Akauliza Savanna


“Si kosa la jinai lakini…………………………”


“ Lakini ……………? Akauliza Savanna


“Sina hakaika kama moyo wangu uko tayari kupenda tena Savanna.Kidonda nilichonacho moyoni kilichosababishwa na mapenzi kitachukua muda mrefu kupona..Nimeumizwa sana na pengine sintaweza kupenda tena.Pengine nitaishi maisha yangu yote yaliyobakia nikiwa mwenyewe.Sintavumilia tena maumivu yoyote ya kuumizwa.Kuna watu katika dunia hii hawajaumbwa ili kupenda na ninaamini mimi ni mmoja wao” akasema Patrick katika hali ya kukata tamaa kabisa


“Patrick nafahamu ni namna gani ulivyoumizwa. Sisi sote tunaumizwa na mapenzi .Lakini mimi bado nasisitiza kwamba kuuruhus moyo wako kupenda tena kutakusaidia sana katika kusahau mambo yaliyopita.Find yourself someone who truly loves you and I swear you’ll be Happy again” akasema Savanna


“Hata kama nikiamua kupenda tena ni nani nitakayempenda? Nani ambaye nitamuamini katika ulimwengu huu wa sasa na kumkabidhi moyo wangu tena? Savanna naomba niwe wazi kwako kwamba sioni sababu ya kupenda tena kwani kila mara nilipojaribu kupenda nimeishia kuumizwa moyo wangu tu.Nilimpenda mno Happy na nilikuwa tayari kufanya lolote kwa ajili yake,niliwahi hadi kuua kwa ajili yake lakini ona jeraha alilonitia moyoni..I’m hurt Savanna..’m deeply hurt.”Akasema Patrick.Savanna akamshika mikono na kumuangalia usoni.


“Patrick si wanawake wote ni wabaya na wanaweza kukuumiza kama ulivyoumizwa.Usiuamini ule msemo usemao samaki mmoja akioza na wote wameoza.Bado kuna wnawake wazuri ,wenye kukupenda ,kukujali na kukuthamini,wanawake ambao kwao una maana kubwa sana.Tafadhali usiufunge moyo wako kwa mwanamke kama huyu”


“Savanna hata wale niliokuwa nao Happy na Vero walinipenda kwa mioyo yao yote.Walinijali na kunithamini.Kwa ufupi ni kwamba sina tatizo na wanawake hata kidogo lakini sina uhakika wa kupenda tena kwa sababu niliwapenda kwa moyo wangu wote.Kuna nyakati ninahisi kama dunia inaniadhibu.The world has been so cruel to me so even if I’ll start a new relationship it wont work out and I’ll get hurt again.Sitaki kuumia tena” akaendelea kusisitiza Patrick


“Patrick,Mungu ametuleta hapa duniani tuyafurahie maisha na ndiyo maana akaumba mwanamke na mwanaume kwa hiyo si sahihi kusema au kuamini kwamba kuna watu ambao wameshushwa katika hii dunia kwa ajili ya kuishi wao wenyewe bila kuwa na mahusiano.Kama kuna watu wa namna hiyo basi Mungu angewaumba bila kuwa na jinsia” akasema Savanna halafu wote wawili wakacheka sana.Savanna akaendelea


“Ninavyoamini mimi ni kwamba kila mtu ana haki ya kuwa katika mahusiano labda upende mwenyewe kutokujihusisha na mahusiano kama vile watawa na makasisi lakini hata hao watawa wanaishi chini ya uangalizi maalum tena mkali ili kuwasaida wasiweze kuingia katika vishawishi vya kimahusiano.Tukirudi katika swala lako lingine,si kweli kwamba dunia imekuwa katili sana kwako ,dunia si mbaya hata kidogo ,dunia inatupenda wote na ndiyo maana wote tunavuta hewa sawa,inatupa mazao na kila kitu.Binadamu waishio juu ya dunia ndiyo wabaya na kwa upande wako ni kwamba you fell I love with wrong people.People whom you’re not meant to be with” akasema Savanna,Patrick akatabasamu halafu akasema


“Maneno yako yanaweza kuwa na ukweli Savanna kwa sababu kuna usemi usemao kwamba kila jambo linafanyika kwa sababu maalum.Inawezekana ni kweli nilipenda watu ambao hawakuwa sahihi kwangu.Hata hivyo nahitaji kulifikiri tena suala hili kabla ya kuamua kuingia katika mahusiano mengine na nina hakika inaweza ikanichukua muda mrefu sana.Kwa sasa nataka nielekeze nguv na akili yangu katika kazi yangu mpya” akasema Patrick


“Hilo ni jambo la msingi sana Patrick.Hutakiwi kuidhulumu nafsi yako.You need to be Happy and to be be Happy you need to love and be loved ” Akasema Savanna .Patrick hakujibu kitu


“It’s getting late Patrick.Twende tuondoke .Leo nataka tukaandae pamoja chakula cha usiku.Unakumbuka ni muda mrefu sana umepita toka tulipoandaa kwa pamoja chakula cha usiku?” Akasema Savanna


“Wow ! That’s great Idea.Ni siku nyingi sana sijaingia jikoni kupika .Nakumbuka sana nyakati zile tulizokuwa tukiandaa chakula pamoja. “ akasema Patrick huku akicheka kidogo


“Unapenda tupike nini kwa ajili ya usiku wa leo? Akauliza Savanna


“Kitu chochote utakachopenda tupike Savanna mimi niko tayari.” Akajibu Patrick na kumfanya Savanna atabasamu


“Today we’re going to have a very special dinner just for two of us.Lets make this night a wonderful and memorable one.” Akasema Savanna kisha wakaondoka.


Kabla ya kuelekea nyumbani walipita kwanza kununua vitu mbali mbali ambavyo wangependa kuvitumia kwa ajili ya usku huo.Walipofika nyumbani,waliingia jikoni na kuanza maandalizi kwa pamoja.Kitendo cha kushirikiana kuandaa chakula kile kilimpa Patrick furaha ya ajabu sana na kumkumbusha nyakati zile wakati bado alikuwa katika mahusiano ya sirina Savanna


Mpaka kufika saa mbili za usiku,chakula kilikuwa tayari.Savanna akamuomba Patrick amuachie yeye kazi zilizobakia na yeye aende akajiandae kabla ya kupata mlo huo wa usiku wazo ambalo Patrick alilikubali na kwenda kujiandaa


“Tonight is the night .I’ve been waiting for this night for so long.Leo hii Patrick lazima awe wangu tena” akawaza Savanna huku akitabasamu baada ya Patrick kuondoka mle jikoni


“Baada ya usiku wa leo nitaamka nikiwa mikononi mwa mwanaume ninayempenda sana kuliko wote.After tonight I’ll be complete and no one than death can separate us again.Patrick will be mine forever” akawaza Savanna wakati akiandaa meza


Kwa upande wake Patrick baada ya kuingia chumbani kwake,moja kwa moja aliingia bafuni akajimwagia maji


“Namshukuru sana Savanna kwani kwa sasa najisikia vizuri na nina nguvu ya kuendelea na maisha yangu mapya. Bila yeye sijui ningekuwa katika hali gani hivi sasa” akawaza Patrick halafu akaendelea kujimwagia maji .Wakati akiendelea kuoga akakumbuka kitu halafu akatabasamu


“ Katika siku zote ambazo nimekuwa na Savanna ,siku ya leo nimejikuta nikiwa na furaha sana na hasa zoezi la kupika pamoja,zoezi ambalo limenikumbusha nyakati zile nilizokuwa naye katika mahusiano ya siri .Niliwahi kuwa katika mapenzi mazito na Savanna,nakumbuka wakati ule nilikuwa na furaha sana japokuwa nilikuwa tayari katika mahusiano na Vero.Savanna alinionyesha mapenzi ya dhati na moyo wangu ulifurahi .Nilikubali kuachana naye kwa shingo upande pale alipompata George.Kama nisingekuwa katika mahusiano na Vero kwa wakati ule basi tayari ningekuwa nimekwisha funga ndoa na Savanna kwani ni mwanamke mwenye kila sifa ya kuwa mke bora .Zaidi ya yote bado ananipenda kwa dhati ya moyo wake na ndiyo maana amejitolea kwa hali na mali katika kuhakikisha kwamba suala la kesi yangu linakwisha na ninakuwa huru tena.” Akawaza Patrick na kisha akaendelea kuoga


“Hata mimi toka ndani kabisa ya moyo wangu ninakiri kwamba bado ninampenda Savanna.Ninahisi yeye anaweza kuwa ndiye mwanamke anayenifaa,lakini kutokana na msaada mkubwa alionisaidia ninasita kuziamsha tena hisia za mapenzi kati yetu” akawaza Patrick halafu akaendelea kuoga.Sura ya Savanna wakiwa jikoni wakipika pamoja ikamjia kichwani akatabasamu


“She have a pretty face,macho mazuri,shepu nzuri na sauti kama malaika.Savanna ni mwanamke bora na mzuri kupita kiasi” akawaza Patrick kisha akatoka mle bafuni


Savanna aliendelea na zoezi la kuandaa meza kwa ajili ya chakula cha usiku.Alizima taa na kuwasha mishumaa na kupafanya mahala pale pawe pa kuvutia sana.Alipohakikisha kila kitu kiko sawa akaenda chumbani kwake kujiandaa kwa ajili ya usiku huo ambao aliupanga uwe maalum kwake


* * * *


“Huu ni usiku wangu wa pekee kabisa ni usiku ambao nimekuwa nikiuota kwa muda mrefu.Ni usiku ambao nitalala nikiwa kifuani kwa Patrick.” Mawazo hayakumkauka Savanna wakati akimalizia kujipaka rangi ya mdomo halafu akajitazama katika kioo na kutabasamu.Alikuwa amependeza sana.Alivaa gauni refu jepesi la rangi jeupe ambalo lilionyesha hadi nguo ya ndani.Akageuka akajitazama na kutabasamu halafu akachukua uturi wa gharama kubwa na kujipulizia kisha akatoka mle chumbani.Patrick alikuwa bado chumbani kwake wakati Savanna alipowasili sebuleni.Savanna akampigia simu na kumtaarifu kwamba muda wa kupata chakula cha usiku umewadia.


Patrick akatoka chumbani na kuelekea sebuleni.Mara tu alipoingia ,akapigwa na mshangao kwa alichokikuta.Sebule ilikuwa imebadilika na kuwa na mandhari ya kuvutia mno.Taa zote zilikuwa zimezimwa na kilichokuwa kinawaka ni mishumaa iliyopapendezesha mahala pale na kupafanya pa pekee kabisa.


“Wow ! amazing “ akasema Patrick huku akitabasamu


“karibu Patrick” akasema Savanna kwa sauti laini huku akiinuka pale sofani alipokuwa amekaa na kwenda kumshika Patrick mkono akaumuongoza kuelekea katika meza ya chakula.Japokuwa mwanga ulikuwa hafifu lakini Patrick aliweza kulishuhudia vyema vazi la Savanna na kusisimka mwili kwani aliweza kuiona hadi nguo ya ndani aliyokuwa amevaa .Mapigo ya moyo wake yakaanza kumuenda kasi.Ni muda mrefu sasa umepita hajawahi kusisimkwa mwili.Savanna na Patrick wakaangaliana kwa sekunde kadhaa Savanna akauliza


“Mbona unaniangalia hivyo Patrick?


“You are so amazing tonight” akajibu Patrick


“Thank you” akajibu Savanna kisha wakaelekea katika meza iliyokuwa imesheheni vyakula vya aina mbali mbali walivyoviandaa


“Karibu chakula Patrick,chakula ambacho ni maalum kwetu.Just for tonight let us forget the world and enjoy the night.Let us make our own world ” Akasema Savanna.


Waliendelea kula taratibu huku wakisindikizwa na muziki laini.Kila Patrick alipomtazama Savanna alisisimka mwili wake kutokana na kuzishuhuhudia chuchu za kuvutia za Savanna ambazo zilikuwa zinaonekana kwa urahisi kutokana na vazi lile alilokuwa amevaa lililoonyesha kila kitu.Taratibu akahisi mtafaruku katika sehemu za ikulu ambazo zilikuwa zimechachamaa kupita maelezo.


“Gosh ! haya ni majaribu makubwa sana.Savanna ananiweka katika wakati mgumu mno.Ouh jamani nitafanya nini mimi? Akawaza Patrick huku akiendelea kumtazama Savanna ambaye alikuwa ameinamisha kichwa.Ghafla akainua kichwa na kugundua kwamba Patrick alikuwa anamuangalia akatabasamu


Baada ya kumaliza kula Savanna akamuomba Patrick waelekee katika sofa lililokuwa na meza ndogo pembeni iliyokuwa na chupa tatu za mvinyo pamoja na glasi mbili.


“Na tunywe kwa furaha huku tukitakiana maisha marefu” akasema Savanna huku akiisogelea glasi yake iliyokuwa na mvinyo karibu na Patrick wakagonganisha glasi.Waliendelea kunywa na kadiri muda ulivyozidi kusonga ndivyo maongezi na vicheko vilivyozidi.Walikumbushana mambo mengi na hasa nyakati zile walizokuwa wapenzi,Ulikuwa ni wakati wa furaha mno kwa wote.Maongezi yalikolea na kulikuwa na kila dalili kwamba walianza kulemewa na kilevi.Savanna akainuka pale alipokuwa amekaa na kuelekea katika redio akaweka muziki laini sana halafu akamfuata Patrick


“Patrick can we dance?


Bila ubishi Patrick akainuka akakumbatiana na Savanna wakaanza kucheza.Patrick akahisi kama chaji za umeme zinapita mwilini mwake pale kifua cha Savanna kilichobeba chuchu laini kilipokigusana na kifua chake.Kadiri muziki ulivyokuwa ukienda ndivyo walivyojikuta wakikumbatiana kwa nguvu zaidi.Muziki ulimalizika lakini bado waliendelea kukumbatiana kwa nguvu .Taratibu Savanna akaupeleka mkono wake wa kulia chini kidogo ya kiuno cha Patrick na kukutana na kitu kigumu kilichotuna.Taratibu na kwa ufundi Savanna akakishika kitu kile kilichotuna na kumfanya Patrick atoe mguno na kuhema kwa nguvu kisha akampiga Savanna busu zito lililomfanya aweweseke.Taratibu Patrick akausogeza mdomo wake karibu na Savanna na kuutoa ulimi wake na zoezi la kunyonyana ndimi likaanza huku wakishikana na kutomasana sehemu mbali mbali za mwili.Wote wawili walikuwa wakihema kwa nguvu na kila mmoja akiongea maneno ambayo mwenzie hakuweza kuyaelewa.


“Ouh,Ouh,ouh Patrick take ..m.me..to ..parr….r..paradise” akasema Savanna kwa sauti yenye kukwama kwama.Alikuwa hajiwezi tena kwa raha alizozisikia.Patrick akamuinua na kwenda naye chumbani.Kilichoendelea huko ni miguno na vilio vya utamu uliopitiliza


* * * *


CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/


Mlio wa saa ya ukutani ndio uliomstua Patrick akafumbua macho na kutazama ukutani kulikokuwa na saa kubwa.Ilikuwa ni saa mbili za asubuhi.Pembeni yake alikuwa amelala Savanna akiwa katika usingizi mzito.Patrick akamtazama na kutabasamu


“Gosh ! Usiku wa jana kamwe sintausahau katika maisha yangu.Sijawahi kuwa na usiku wa kipekee kama ule.Nilijihisi kama nimetoka kabisa katika ulimwengu huu.Ouh Savanna I didn’t know how much I still love you.Umenirudishia tena furaha yangu iliyopotea.” akawaza Patrick halafu akainama na kumbusu Savanna shavuni na mara Savanna akafumbua macho.


“Ouh Patrick thank you so much.You are so sweet” akasema Savanna


“Thank you for the wonderfull night.Sijawahi kuwa na usiku mzuri kama wa jana.Nimekuwa nikiuota usiku kama ule kwa miaka mingi.Ahsante sana Patrick..Ahsante sana” akasema Savanna akamvuta tena Patrick kwake na kumpa busu zito.Patrick akatabasamu na kusema


“Savanna you are wonderfull,you are amazing.Baada ya usiku wa jana,najiona mtu mpya.Savanna naomba nitamke kwamba najiona ni kama mfalme mwenye nguvu mwenye uwezo wa kufanya chochote nikiwa nawe.Umenipa nguvu na matumaini.Siku zote nitaendelea kumshukuru Mungu kwa kunikutanisha nawe.Nina uhakika mkubwa kwamba kukutana kwetu haikuwa kwa bahati mbaya.Mungu alikuwa na makusudi yake na ndiyo maana leo hii ninathubutu kutamka kwamba pamoja na kwamba tuliachana na kila mmoja akaendelea na maisha yake ,lakini bado moyoni mwangu una nafasi ya kipekee kabisa.Bado ninakupenda Savanna na hata siku moja upendo wangu kwako haujapungua.Sitaki kubishana na moyo wangu kwamba wewe ndiye mwanamke ambaye umeumbwa kwa ajili yangu.Savanna ninaombi moja kwako” Patrick akanyamaza akamtazama Savanna ambaye machozi yalikuwa yanamtoka


“Omba chochote Patrick nitakupatia” akasema Savanna huku akifuta machozi yale ya furaha


“Savanna pengine ombi langu kwako linaweza kuwa gumu hasa kutokana na matukio ambayo yamekuwa yananitokea lakini napenda kuwa wazi kwako kwamba ninaomba nafasi nyingine katika moyo wangu.Ninakubaliana na maneno uliyoniambia jana kwamba natakiwa kuufungua moyo wangu tena.Nimeufungua moyo wangu kwako na nina imani wewe ndiye pekee ambaye utaweza kunisahaulisha mambo yote yaliyopita na kunifanya niwe na maisha yenye furaha sana hapa duniani.Naomba uwe malkia wangu Savanna.” Patrick aliyasema maneno haya taratibu na kwa hisia kubwa.Mara tu alipomaliza kusema ya moyoni mwake,Savanna aliinuka kwa kasi na kulitupa shuka pembeni kisha akamkumbatia Patrick kwa nguvu.Alikuwa akiweweseka huku akimpiga Patrick mabusu mfululizo


“Patrick unataka kunipa uchizi.Kwa muda mrefu sana nimekuwa nikiota kuusikia mdomo wako ukitamka meneo haya mazito uliyonitamkia sasa hivi.Patrick nashukuru sana na sina cha kusema zaidi ya kukuhakikishia kwamba siku zote moyo wangu ulikuwa na nafasi kwa ajili yako pekee.Niliamini siku moja mimi na wewe tutakuwa pamoja hata kama si katika maisha haya basi katika maisha mengine baada ya kufa.Nimekuwa nikimuomba sana Mungu kwa jambo hili lakini hatimaye leo hii limekuwa kweli.Huu ni kama muujiza kwangu.Patrick nakukabidhi moyo wangu na kila kilicho changu.Naomba unitawale ee mfalme wangu.Niamuru chochote nitakutii” akasema Savanna kwa hisia kali huku akitokwa na machozi ya furaha.Ilikuwa ni kama ndoto.Hakuamini kama ile ndoto yake ya siku nyingi ya kuwa na Patrick leo hii imekuwa kweli.Walikumbatiana kwa furaha huku wakiepeana mabusu mfululizo na taratibu wakajikuta wakianza kuhama katika ulimwengu huu na kwenda katika ulimwengu uliojaa mahaba mazito.Migumo na mihemo ya kimahaba ndivyo vilitawala chumba hiki.Patrick akaufungua mpya wa mapenzi na Savanna.




Ukurasa mpya wa maisha ya Patrick umefunguliwa na tayari ni meneja wa kiwanda cha kusindika nyama.Maisha yake yanakwenda vizuri kwa sasa.Alinawiri na kupendeza sana.Alikiongoza kiwanda hiki cha kusindika nyama kwa ufanisi mkubwa na ndani ya kipindi kifupi kiwanda hiki kilikuwa ni moja kati ya viwanda bora kabisa nchini


Mizizi ya penzi imara kati yake na Savanna ilichomoza kwa kasi na kwa sasa penzi lao halikuwa la siri tena.Lilikuwa kwa ndugu jamaa na marafiki.Alimtambulisha rasmi Savanna kama mpenzi wake na kwa pamoja walikuwa na mipango mingi na ndoto nyingi za kutimiza katika maisha yao yajayo na kubwa likiwa ni kufunga ndoa mara tu kesi ya Patrick itakapomalizika.Bado kesi ya kuua bila kukusudia inayomkabili Patrick iliendelea kuunguruma mahakamani.Tayari upande wa mashitaka ulikwisha funga funga ushahidi wao hivyo kutoa nafasi kwa upande wa utetezi nao kuwaleta mahakamni mashahidi wanaomtetea Patrick.Upande wa utetezi ukiongozwa na Savanna uliitaka Mahakama kumuachia huru mteja wao kwa sababu alisababisha kifo wakati akijaribu kunyang’anya silaha mtu aliyekuwa ameishika silaha hiyo na aliyekuwa na dhamira ya kufanya mauaji.Baada ya Patrick kutoa ushahidi wake mahakamani ilifuata nafasi ya mashahidi kuanza kutoa ushahidi wao mbele ya mahakama.


Siku moja jioni Savanna alichelewa kurudi nyumbani na kukuta tayari Patrick amekwisha rejea toka kazini.Siku hii Savanna alionekana mchovu na mwenye mawazo mengi.Patrick aliligundua hilo na kumuuliza ni jambo gani lililokuwa limemsibu.Savanna hakujbu kitu akainuka pale sofani akajimiminia mvinyo katika glasi akanywa funda kubwa halafu akamtazama Patrick


“Savanna una tatizo gani leo mpenzi wangu? Si kawaida yako kuwa katika hali hii.Tafadhali niambie kama una tatizo lolote.” Akasema Patrick.Savanna akainama akafikiri kwa sekunde kadhaa na kusema


“Patrick nina tatizo mpenzi wangu.Kuna jambo linaniumiza kichwa changu sana.Nimekuwa nikilifikiria suala hili kwa muda mrefu sasa lakini nimeshindwa kulipatia ufumbuzi”


“Jambo gani hilo linakusumbua Savanna? Tafadhali niambie.Hakuna jambo lolote linaloweza kutushinda kulipatia ufumbuzi” akasema Patrick.Savanna akainamisha kichwa akafikiri kidogo na kusema


“Kuna tatizo kidogo katika kesi”


“Katika kesi? Patrick akastuka


“Ndiyo Patrick kuna tatizo dogo”


“Tatizo gani” akauliza Patrick ambaye tayari moyo wake ulianza kumwenda mbio


“Patrick nilishindwa kukutaarifu mapema kuhusu jambo hili kwa kuwa naamini ni jambo ambalo hutapenda kulisikia lakini naomba nikutaarifu kwamba katika orodha ya watu wanaotakiwa kutoa ushahidi wao mahakamani lipo pia jina la Happy”


Patrick kijasho kikamtoka .Alistushwa sana kwa taarifa ile


“Ou my God “ akasema kwa sauti ndogo huku akimkazia macho Savanna


“Happy kibaho? Akauliza Patrick


“Ndiyo.Happy Kibaho”


“Ouh my Gosh.! How could you do that Savanna?Tulikubaliana kwamba Happy hatahusika na chochote katika kesi hii,aliniacha nikisota gerezani kwa kosa ambalo sikulifanya,hakuona umuhimu wangu,kwake yeye hata kama nikifungwa gerezani hatajali,kwa nini basi tumtumie mtu kama huyu? Savanna Happy kibaho ni jina ambalo sitaki kulisikia tena katika masikio yangu.” Patrick akasimama


“Patrick hii ndiyo sababu sikutaka kukueleza mapema.Nilijua lazima ungeshtushwa sana na taarifa hiyo”


“Savanna tafadhali niko chini ya miguu yako naomba kama kuna uwezekano liondoe jina la Happy katika orodha ya mashahidi.Tunao mashahidi wengi ambao tutawatumia katika kesi hii.” Akasema Patrick.Savanna akamshika mabegani na kusema


“Patrick mpenzi wangu ninafahamu ni namna gani Happy alivyokuumiza na jinsi gani unavyomchukia.Nafahamu pia uhusika wa Happy katika kesi hii unavyokuumiza kwani utairudisha tena taswira ya mtu ambaye hutaki tena kumuona au kumsikia katika maisha yako.Hata mimi suala hili ni gumu sana kwangu lakini naomba niwe wazi kwako kwamba Happy ni mtu muhimu sana katika hatua hii tuliyofikia.Ushahidi wake una nguvu sana”


“Savanna mashahidi hawa wote tulionao hawatoshi hadi Happy naye ashirikishwe katika kutoa ushahidi? To be honest I hate her.Sitaki kuiona tena sura yake kutokana na mambo aliyonifanyia.” Akasema Patrick


“Ushahidi mzito tuliouwasilisha mahakamani pamoja na ule unaoendelea kutolewa na mashahidi unajitosheleza sana lakini katika ushahidi wote huo Happy ametajwa sana kwani yeye ndiye aliyekoswa na risasi iliyotoka katika bastora aliyokuwa ameishika Vero.Happy anatakiwa aieleze mahakama kila kitu kilichotokea jioni ile.Ni ushahidi muhimu mno ambao ninaamini ndio utakaoisaidia mahakama kuamua hatima ya kesi hii.Patrick nakuomba mpenzi wangu tumtafute Happy na kumuomba atoe ushahidi wake .Nafahamu kwamba unamchukia na hutaki kumuona tena lakini kwa hatua hii Happy ni mtu muhimu sana kwetu.Patrick we’re almost to the end now so we need to do everything we can to win.Ninamuomba sana Mungu atusaidie ili tuweze kulimaliza suala hii haraka na tuitimize ndoto yetu ya kufunga ndoa.Naomba uniruhusu mpenzi wangu nimtafute Happy ili aweze kuja kutoa ushahidi wake “ akasema Savanna.


Patrick akashika kichwa kwa mikono yake akainama na kuzama katika mawazo.Akainuka pale alipokuwa amekaa akaenda dirishani,akasimama na kuelekeza macho yake nje kana kwamba kuna kitu alikuwa anakiangalia


“Happy Kibaho !” akasema taratibu halafu akainama tena


“Nilimpenda kiasi ambacho siwezi kuelezea.Nilimpa kila kitu na kuamini kwamba yeye ndiye mwanamke pekee ambaye nimepangiwa niwe naye katika maisha yangu.Pamoja na kumuonyesha kila aina ya upendo lakini Happy bado alidiriki kufanya kitendo kichafu ambacho sikuwahi kutegemea au hata kuota kama msichana kama Happy anaweza akafanya.Aligundua kosa alilolitenda na akapotea moja kwa moja akiniacha nikiozea gerezani kwa kosa ambalo alilisababisha yeye mwenyewe.Je mtu wa namna hii aliyenisababishia majeraha makubwa ya moyo ninastahili kuonana naye tena ana kwa ana? Moyo wangu hautaki kabisa na hauko tayari kuonana tena na Happy lakini kwa kuwa hili ni ombi la Savanna itanibidi nikaze moyo na kukubali aje atoe ushahidi wake.” Akawaza Patrick halafu akamgeukia Savanna


“Unafahamu mahala aliko Happy kwa sasa? Savanna akainuka na kumfuata Patrick pale alipokuwa amesimama.


“Patrick kuna jambo lingine ambalo naomba ulifahamu”


“Jambo gani hilo Savanna?


“Happy hayupo hapa nchini”


“Hayupo hapa nchini?.How do you know that she’s not here? Akauliza Patrick kwa wasi wasi


“Samahani Patrick kwa kutokufahamisha suala hili toka mwanzo lakini naomba nikufahamishe kwamba mimi ndiye niliyemsaidia Happy kuondoka hapa nchini” akasema Savanna.Patrick akazidi kuchanganyikiwa


“Savanna unazidi kunichanganya akili yangu.Ulimsaidia Happy kuondoka hapa nchini? Kwa nini hukuniambia muda wote huu? Do you know where she is now?


“Patrick ni hadithi ndefu sana na sikutaka kukwambia mapema kwa sababu nilijua utaumia na mimi sitaki kukuona ukiumia.”


“Ok niambie nini kilitokea? Happy yuko wapi? Akauliza Patrick.Savanna akainama akafikiri kidogo halafu akasema


“Nilipigiwa simu usiku na mzee Kibaho baba mzazi wa Happy akaniuliza kama nina taarifa zozote kuhusiana na Happy kwani hakuwa ameonekana nyumbani kwao toka alipoondoka asubuhi.Sikujua mahala alipokuwa Happy na mara ya mwisho kuonana naye ilikuwa ni gerezani asubuhi.Hii ilikuwa ni siku ile nilipokuja gerezani na mama na tukamkuta Happy pale mama akamfokea sana.” Savanna akasema halafu akamtazama Patrick kisha akaendelea


“Asubuhi ya siku iliyofuata nikiwa najiandaa kuja gerezani ,alikuja mmoja wa wafanyakazi wangu akiwa na gazeti lililokuwa na picha chafu za Happy katika ukurasa wa mbele.Nilistuka sana baada ya kuziona picha zile na kama haitoshi mtumishi yule akainionyesha pia na video iliyokuwa mtandaoni.Ilinibidi nimpigie simu Margreth naye akanifahamisha kwamba Happy alikuwa amekunywa sumu kwa lengo la kujiua.Nilikwenda hadi katika hospitali ya Brahmaputra ambako Happy alikuwa amekimbizwa na kupatiwa huduma ya kuondolewa sumu mwilini.Nilishauriana na familia yake na tukakubaliana kwamba ili kumuepusha Happy na aibu kubwa aliyoipata itabidi kumpeleka mafichoni nje ya nchi sehemu ambako hakuna mtu anayemfahamu .Kama mchango wangu kwao nilijitolea usafiri wa kwenda Kigali Rwanda ambako tayari nilikwisha fanya mawasiliano na meneja wa hoteli moja kubwa mjini Kigali ambaye ni rafiki yangu na kumuomba Happy akae katika hoteli yake hadi hapo atakapopona kabisa .Mimi baba yake,mzee Kibaho pamoja na daktari mmoja tulielekea Kigali Rwanda na nilimuacha Happy kule akiwa na baba yake pamoja na daktari “ akasema Savanna.


“So she’s in Kigali now? Akauliza Patrick


“Alikuwa Kigali lakini kwa taarifa nilizozipata toka kwa rafiki yangu Christine ni kwamba Happy alitoweka pale hotelini na hakuna anayefahamu alikwenda wapi.” Akasema Savanna


“Ouh my God.Tumekwama tena” akasema Patrick


“Tukitaka kumpata Happy hatuna budi kuwasiliana na familia yake.Nina imani lazima watakuwa wanafahamu mahala alipo”


“Hilo nalo ni tatizo lingine.Sina hakika kama familia yake inaweza kutupa ushirikiano na kutuambia mahala aliko Happy” akasema Patrick


“Mimi ndiye nitakayekwenda kuonana nao.Nina imani msaada wangu hawataweza kuusahau kwa hiyo watanisaidia”


“Hata kama familia yake itakubali kushirikiana nasi ,vipi kuhusu Happy mwenyewe atakuwa tayari kurudi tena hapa Tanzania kutoa ushahidi wake baada ya mambo ya aibu kubwa aliyoyafanya? Sina hakika kama anaweza akakanyaga tena Tanzania hasa kutokana na aibu kubwa aliyoipata kutokana na uchafu mkubwa alioufanya.Sina hakika kama suala hili litafanikiwa Savanna,Naomba tusiumize vichwa vyetu kuhusu huyu mwanamke.Tutafute njia nyingine ya kutusaidia na si kumtegemea Happy” akasema Patrick akionyeaha kukata tamaa kabisa ya kumpata Happy


“Patrick mpenzi wangu laiti kama kungekuwa na njia nyingine ya kufanya nisingethubutu kukutajia jina la Happy lakini kwa hatua tuliyofikia ni lazima tumpate Happy.We’re almost to the end.Patrick naomba uniruhusu mimi nikaonane na familia ya Happy nitawalilia na kuwaomba wanisaidie.Mzee Kibaho ni mtu mwelewa sana na nina hakika atakuwa tayari kutusaidia”


Patrick akainama akafikiri kidogo na kusema


“Do what you have to do Savanna lakini moyo wangu haujapenda kuonana na Happy kabisa”


“Ahsante sana mpenzi wangu.Umefanya jambo la maana sana kwa kukubali.Najua si maamuzi mepesi lakini its for the best of us.I promise you that we’re going to finish this once and for all” akasema Savanna,Patrick hakujibu kitu


* * * *


Saa nne za asubuhi siku iliyofuata ilimkuta Savanna nje ya geti la nyumba ya akina Happy.Ni muda mrefu umepita toka alipokuja katika nyumba hii.Akiwa ndani ya gari lake ,alilitazama geti la nyumba ile na kuvuta pumzi ndefu


“Help me God.Laiti ningekuwa na namna nyingine ya kufanya katu nisingethubutu kuja tena katika nyumba hii.Sikutaka Happy aonane tena na Patrick hasa katika wakati ambao penzi letu limekwisha weka mizizi imara,lakini kwa hali halisi ilivyo ninalazimika kurejea tena katika nyumba hii kutafuta msaada” akawaza Savanna halafu akashuka na kwenda kubonyeza kengele ya getini


Baada ya dakika moja geti likafunguliwa.Alikuwa ni mama yake Happy.Savanna akaingiwa na woga kidogo lakini akakaza moyo akasalimiana na mama yake Happy na kukaribishwa ndani


“Savanna umepotea sana mwanangu.Habari za siku nyingi?


“Kazi zimekuwa nyingi mama na ndiyo maana sijafika hapa muda mrefu sijafika kuwatembelea.Habari za hapa?


“Habari za hapa nzuri Savanna.Karibu sana” akasema mama Happy kisha mtumishi wa ndani akawahudumia vinywaji


“Mama mna mawasiliano yoyote na Happy? Nilipigiwa simu na Christine yule rafiki yangu niliyemkabidhi amuhudumie kule Kigali kwamba Happy aliondoka katika hoteli ile aliyokuwa anakaa na mpaka sasa hajui alipo.Nimepata wasi wasi sana na nikaona ni bora nije kuuliza kama mnalifahamu jambo hili” akasema Savanna na mama yake Happy akaonyesha mstuko Fulani


“Savanna suala hili tumelisikia na hata sisi limetustua sana.Mpaka hivi sasa hatujui Happy yuko wapi na hatuna mawaliano naye yoyote.Tumeamua kumuachia Mungu na kumuomba amlinde na kumpa uzima kokote kule aliko.Tunaamini siku moja lazima atarejea nyumbani” akasema mama Happy


Savanna kijasho kikamtoka.Akavuta pumzi ndefu na kusema


“Ouh my gosh !


Kimya kikatanda mle sebuleni halafu Savanna akauliza


“Margreth naye yuko wapi?


“Margreth yuko kazini “


Savanna akainama na kufikiri kwa muda kisha akasema


“Mama mimi nakwenda.Tutaonana tena siku nyingine.Endapo mtapata mawasiliano yoyote ya Happy naomba mtanitaarifu “akasema Savanna huku akiinuka.Mama yake Happy akastuka


“Savanna kulikoni? Mbona ghafla hivyo?


“Utanisamehe mama nimekumbuka kwamba nina miadi na mtu wa muhimu sana muda mfupi ujao.Nitakuja tena kukusalimu siku nyingine” Akasema Savanna na kuonyesha kwamba hakutaka tena maongezi akaingia katika gari lake na kuondoka


“Kuna kitu nimekigundua toka kwa mama yake Happy. Alikuwa na wasi wasi mwingi.Inaonekana kuna jambo analifahamu kuhusu Happy na hakutaka kunieleza.Margreth au mzee Kibaho wanaweza wakanipa ukweli halisi.Ngoja kwanza nikaonane na Margreth” akawaza Savanna halafu akaegesha gari pembeni ya barabara akachukua simu yake na kumpigia Margreth


“Hallo Savanna.Habari za siku nyingi? Akasema Margreth baada ya kupokea simu


“Habari nzuri Margreth.Hatujaonana muda mrefu sana”


“Ni kweli Savanna.Mbona umekuwa kimya hivyo?


“Ni mihangaiko tu Margreth.Uko wapi sasa hivi?


“Sasa hivi niko kazini lakini niko mbioni kutoka nataka kwenda kuhudhuria mazishi ya rafiki yangu”


“Margreth,ninahitaji sana kuonana nawe.Kuna jambo muhimu nahitaji kuongea nawe.Tunaweza kuonana kabla hujaenda msibani?


“Hakuna tatizo Savanna.Tukutane wapi?


“Tuonane pale Lemina Café.Ninaelekea huko sasa hivi.Utanikuta pale”


“Sawa Savanna.Nakuja hapa muda si mrefu” akajibu Margreth na kukata simu.


* * * *


Habari za siku nyingi Margreth? Alianzisha mazungumzo Savanna baada ya kuonana na Margreth


“Habari nzuri Savanna.Umepotea sana dada yangu”


“Ni kweli Margreth ni muda mrefu sana hatujaonana.Hii inachangiwa na majukumu mengi ya kazi”


“Ni kweli kabisa Savanna” akajibu Margreth.


“ Patrick anaendeleaje? Kesi yake imefikia wapi?


“ Patrick anaendelea vizuri na kesi yake naendelea vizuri pia.Kwa hivi sasa kinachoendelea na kusikilizwa kwa mashahidi wa utetezi.Tutalimaliza suala hili” akasema Savanna


“ namuombea Mungu Patrick suala hili liishe na aendelee na maisha yake” akasema Margreth kisha kikapita kimya kifupi.Savanna akasema


“Margreth nimekuita hapa nina tatizo ambalo nahitaji sana msaada wako” akasema Savanna


“Usijali Savanna niko tayari kukusaidia kwa lolote”


“Ahsante sana.Tatizo langu ni kutaka kufahamu mahala aliko Happy.Nahitaji kuzungumza naye”


Margreth akastuka na kumuangalia Savanna


“Happy ..?!! akauliza Margreth.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/


“Ndiyo.Nina shida kubwa ya kuongea na Happy.”


“Happy yuko Kigali mahala ulikomuacha” akajibu Margreth na kumfanya Savanna acheke kidogo


“Happy hayuko Kigali.Aliondoka kule muda mrefu sana .Tafadhali naomba Margreth unisaidie nizungumze na Happy.” Akasema Savanna.Margreth akaona aibu kidogo na kutabasamu


“Samahani Savanna kwa kutaka kukudanganya lakini ukweli ni kwamba taarifa hiyo uliyonayo ndiyo hata sisi tunayo.Tulitaarifiwa kwamba Happy ameondoka katika hoteli aliyokuwa akikaa na haijulikani alielekea wapi.Tumejaribu sana kumtafuta bila mafanikio.Kwani kuna tatizo gani Savanna?


“Nina tatizo kubwa sana kumuona Happy.Tatizo ninalomtafutia Happy ni kwa sababu ya Patrick.”


“Patrick !!..” Margreth akashangaa


“Patrick anamtafutia nini Happy?


“Nadhani ulisikia kwamba Patrick alipata dhamana akatoka gerezani”


“Dada Savanna kwa kweli sihitaji kusikia au kufuatilia lolote linalohusiana na Patrick.Yeye ndiye chanzo cha dada yangu kuteseka na kupoteza mwelekeo mzima wa maisha yake.Kila anapokuwa karibu na Happy basi lazima kuna jambo baya linatokea.Kabla hajaonana na Patrick maisha ya Happy yalikuwa mazuri na yenye furaha lakini mara tu alipokutana na Patrick basi maisha yake yamebadilika ghafla na kupoteza kabisa mwelekeo mzima wa maisha yake.To be honest I hate that dude” akasema Margreth


“Nakuelewa sana Margreth lakini naomba nikukumbushe kwamba mara ya kwanza Patrick aliua bila kukusudia wakati akimuokoa dada yako asidhalilishwe na kundi la wahuni waliokuwa na lengo la kumbaka.Alifungwa gerezani na yakatokea yaliyotokea hadi walipokuja kukutana tena siku chache kabla ya kufunga ndoa.Kwa mapenzi makubwa waliyokuwa nayo na kwa ridhaa yao wenyewe waliamua kuachana na wapenzi wao ili waweze kutimiza ndoto yao ya kuwa pamoja.Katika ugomvi ule uliotokea na kupelekea kifo cha Vero na ni Happy ndiye aliyemsukuma Vero akajigonga ukutani na kufariki dunia.Kwa mapenzi makubwa aliyokuwa nayo Patrick wa Happy aliamua kuubeba mzigo wote wa kesi hii.Na kwa taarifa yako ni kwamba mimi ndiye niliyepambana na kumtoa Happy katika kesi ile kwa ombi la Patrick.Kwa maana hiyo hakuna sababu ya kumlaumu Patrick” akasema Savanna.Margreth hakusema kitu na kwa mbali macho yake yalionyesha kulengwa na machozi


“Kesi ya Patrick inaendeleaje? Akauliza Margreth


“Mashahidi wanaendelea kutoa ushahidi wao na wiki hii shahidi aliyebaki atatoa ushahidi wake na baada ya hapo atabaki shahidi mmoja tu katika orodha ya mashahidi upande wa uetetezi.Ni Happy.Yeye ndiye mtu wa mwisho kutoa ushahidi wake .Ushahidi wake una nguvu sana kwa sababu yeye ndiye anayeifahamu vyema historia yake na Patrick na kila kitu kilichotokea usiku ule.Kwa hiyo namuhitaji sana Happy.Nakuomba kama unafahamu mahala alipo niambie tafadhali”akasema Savanna.


“Sifahamu aliko Happy” akajibu Margreth.Savanna akamtazama kwa macho makali na kusema


“Margreth nafahamu kuna kitu ambacho unanificha”


“I don’t know anything Savanna” akasema Margreth


“Margreth mimi ni rafiki wa familia yenu.Nilimsaidia Happy kama ndugu yangu wakati alipokutwa na matatizo.Na mimi nimepatwa na tatizo na ninaomba mnisaidie kama ndugu yenu.Sina maana ya kwamba nataka Patrick na Happy warudiane tena la hasha.Ninachotaka mimi ni ushahidi tu tena teknolojia imeimarika sana siku hizi anaweza akatoa ushahidi wake huko huko mahala aliko na si lazima aje Tanzania” akasema Savanna


“Savanna nimekwisha kwambia kwamba sifahamu mahala aliko Happy,mbona hutaki kunielewa? Akafoka Savanna


“Ok! Ok! nimekuelewa Margreth.Hakuna yeyote kati yenu anayeiona thamani ya Patrick tena.Natumai nyote mnatamani kusikia Patrick amefungwa gerezani.I cant let Patrick go to jail after all that has sacrificed.He’s my friend and I’ll do anything to set him free.Nitakwenda kumtafuta Happy mimi mwenyewe kwa gharama zangu na kwa njia ninayoijua mimi.Kama bado yuko hai nakuhakikishia kwamba nitampata tu.Kesho nitakwenda Kigali na nitaanza kumtafuta Happy tokea pale.Nina marafiki wengi pale na watanisaidia kujua Happy alipo.Ahsante kwa kuitika mwito wangu.Tutazidi kuonana” akasema Savanna halafu akainuka akachukua mkoba wake na kuanza kuondoka.


“Savanna wait…!! akasema Margreth.Savanna akageuka ,akamtazama Margreth na kurejea pale mezani


“Unasemaje Margreth? akauliza Savanna


“Naomba ukae chini Savanna” akasema Margreth


“Savanna umenipa wakati mgumu sana.Nashindwa nifanye nini lakini naomba nikufahamishe kwamba ninafahamu mahala alipo Happy” akasema Margreth.Uso wa Savanna ukaonyesha tabasamu .


“Ahsante sana Margreth kwa kuwa muwazi.Happy yuko wapi?


“Happy aliondoka Kigali na kuelekea Marekani .Kwa sasa anashi Los angeles .Yeye binafsi hataki mtu yeyote zaidi ya familia yake afahamu mahala aliko.Hivi sasa maisha yake ni mazuri na yenye amani.Nimeamua kukueleza ukweli wa mahala alipo Happy kutokana na uzito wa suala unalomtafutia japo najua kutakuwa na mtafaruku kwa sababu nimevunja makubaliano yetu ya kutomweleza mtu yeyote mahala aliko” akasema Margreth


“Usihofu Margreth.Hakuna mwingine zaidi yangu atakayejua kuhusu jambo hili.Sasa nieleze nitampata vipi? Unaweza kunipatia mawasiliano yake?


“Its not that simple Savanna.Nitakachofanya mimi ndiye nitakayeongea naye kwanza ili tuone atatoa jibu gani.Naomba niwe wazi kwako kwamba Happy hataki mawasiliano na mtu yeyote sasa na hasa hasa wewe.Sijui ulimfanya kitu gani kwani aliweka wazi kwamba katika watu anaowachukia basi wewe ni mmoja wao.Naomba uniachie mimi hiyo kazi nitaongea naye halafu nitakwambia jibu atakalonipa” akasema Margreth


“Ahsante sana Margreth.Nakuomba ujitahidi kwa kadiri utakavyoweza umshawishi akubali.Mkumbushe kwamba hatima ya Patrick iko mikononi mwake.”


“Ni kazi ngumu Savanna lakini nitajitahidi” akajibu Margreth.


“Jitahidi Margreth.Hata kama italazimika kumtumia tiketi ya ndege ya kuja na kurudi mimi niko tayari kugharamia.Kitu kingine ambacho unapaswa kumkumbusha ni kwamba hakuna mtu mwenye lengo la kumshawishi arejeshe uhusiano wake na Patrick kwani najua tayari ana maisha yake yenye furaha halikadhalika Patrick naye ana maisha yake yenye furaha pia.Tunachohitaji sisi ni ushahidi tu ambao utamuweka huru Patrick “ akasema Savanna halafu akafungua pochi lake na kutoa bunda la noti akahesabu noti kumi na tano za elfu kumi kumi na kumkabidhi Margreth.


“Hizi ni kwa ajili ya mawasiliano na Happy” akasema Savanna.Margreth akazichukua fedha zile na kumrudishia


“Nashukuru sana Savanna lakini naomba uziweke pesa hizo utazitumia kwa kitu kingine.Nitafanya mawasiliano kwa gharama zangu.” Akasema Margreth .Savanna akazichukua fedha zile na kuweka mkobani wakaagana akaondoka


Baada ya Savanna kuondoka,bado Margreth aliendelea kubaki pale mezani akiwa na mawazo mengi


“Nimefanya kosa kubwa sana kuvunja makubaliano yangu na Happy . Kwa mdomo wake mwenyewe alitamka kwamba hataki tena kurudi Tanzania.Nitaanzaje kumwelezea kuhusiana na suala hili? Ouh my gosh ! nimekoroga mambo.Happy atanilaumu sana kwa jambo hili lakini kwa upande mwingine ana haki ya kufahamu kinachoendelea huku nyumbani.Ana kila sababu ya kuja kutoa ushahidi mahakamani na kumuepusha Patrick na adhabu yoyote anayoweza kuipata kwa kosa ambalo hakulitenda.” Akawaza Margreth halafu akainuka akachukua mkoba wake na kuondoka


Margreth alifika nyumbani kwao lakini kabla hajaingia chumbani kwake mama yake akatokea


“Margreth mbona umewahi kurudi leo?


“Ninakwenda kuhudhuria mazishi ya yule rafiki yangu aliyefariki juzi” akasema Margreth


“Maggie ,Savanna alifika hapa “


“Alikuwa anataka nini? Akauliza Margreth


“Kikubwa alichoniuliza ni kama tuna mawasiliano na Happy au kama tufahamu mahala aliko hivi sasa.”


“Ulimjibu nini?


“Nilimjibu kwamba hata sisi hatufahamu mahala aliko Happy.Baada ya jibu hilo akaondoka zake.Nina wasi wasi sana kwa kuamua kumtafuta Happy hivi sasa.Sitaki kabisa wafahamu mahala Happy alipo” akasema mama yake


“Mama nimeonana na Savanna.Alinipigia simu wakati nikitoka kazini na nikaonana naye.Ni kweli ana tatizo na ndiyo maana anamtafuta Happy.” Akasema Margreth


“Ana tatizo gani? Sitaki wamuhusishe tena mwanangu katika masuala yao.”


“Mama Savanna ana matatizo makubwa na ni lazima aonane au awasiliane naye”


“Ana tatizo gani?


“Ni kuhusiana na ile kesi ya Patrick”


“Kesi ya Patrick ?!!..mama yake akashangaa


“Ndiyo mama.Happy anatakiwa atoe ushahidi wake.”


“Margreth ..!!!! akasema mama yake


“Hapana Margreth.Mwanangu Happy kamwe sintaruhusu aje tena huku na kuonana tena na Yule kijana.Mambo aliyokumbana nayo yanatosha sitaki tena mwanangu aumie.Maisha yake ni mazuri kwa sasa na tayari amekwisha msahau Patrick.Sitaki aonane tena na yule kijana aliyejaa mabalaa mwili mzima”




“mama..!!! “ akasema Margreth


“Hapana Margreth.Siruhusu mwanangu kushiriki kwa namna yoyote katika kesi hii.Tayari maisha yake yametulia hivi sasa na sitaki apate tena matatizo mengine.”


“Mama kama Happy asipofanya hivyo kuna uwezekano Patrick akafungwa gerezani.”


“Itakuwa vyema kama akifungwa.Ninamchukia sana yule kijana na kama ningekuwa na uwezo ningemuondoa kabisa katika uso wa dunia” mama yake Happy akasema kwa ukali


“mama si sahihi kusema hivyo.Kumbuka Patrick alikubali kuubeba mzigo mzito wa kesi kwa kosa ambalo hakulitenda.Happy ndiye aliyeua na ndiye anayestahili kusimama mahakamani hivi sasa lakini Patrick ameliepusha hilo na amejitolea yeye mwenyewe kuubeba mzigo huu.Mama huoni kwamba Happy analazimika kuwa mstari wa mbele kumtetea Patrick? Ninajua kwa sasa amekwisha anza maisha mapya na hana mpango tena na Patrick wala kurejea nyumbani lakini pamoja na hayo bado ana wajibu wa kuja kumtolea ushahidi mwenzake.” Margreth akajitahidi kumuelewesha mama yake ambaye bado alionekana kutokubaliana kwa namna yoyote ile na hoja ile ya kumtaka Hapy atoe ushahidi kwa Patrick


“Pamoja na hayo,bado sitaki mwanangu arejee.Sitaki aumie tena.Margreth wewe mwenyewe unafahamu fika kwamba yule kijana sijui amempa nini Happy.Kitendo cha Happy kumuona tu basi huwa anasahu kila kitu na kumkimbilia yeye.Kwa sasa Happy amekwisha rudiana tena na Mike na maisha yake yana furaha sitaki aonane tena na yule kijana.“ mama Happy bado aliendelea kuushikilia msimamo wake


“Mama natambua Happy tayari ameamua kuendelea na maisha yake na hana tena mpango wa kuendelea na Patrick kwa hiyo usiogope hata kama wataonana hakuna kitakachotokea.Anachotakiwa kufanya yeye ni kutoa tu ushahidi wake halafu aondoke zake akaendelee na maisha yake.Isitoshe hata Patrick naye amekwisha endelea na maisha yake na hana tena mpango na Happy”


“Margreth nimekwisha kueleza kwamba hata unishawishi vipi Happy hatakuja tena na kuonana na Patrick.Neno langu mimi ni la mwisho na sitaki tena mjadala huu uendelee.” Akasema mama yake Happy huku akiondoka akiwa amekasirika sana.Margreth naye akaelekea chumbani kwake na kujitupa kitandani


“Sikubaliani na mama hata kidogo.Hatutatenda haki kama Happy hatatoa ushahidi wake mahakamani kumtetea Patrick mtu aliyeubeba mzigo wa mashtaka yaliyokuwa yanamkabili yeye.Lazima niwasiliane na Happy nisikie naye ana maoni gani kuhusu suala hili.Tukifanya mchezo Patrick anaweza akafungwa” Akawaza Margreth halafu akaichukua simu yake na kuzitafuta namba za Happy akapiga huku moyo wake ukimwenda mbio.Simu iliita na kukata.Akaangalia saa ya ukutani ilionyesha ni saa sita za mchana


“Yawezekana yuko katika usingizi mzito kwani mida hii huko kwao bado ni usiku.Ngoja nimpigie tena” Margreth akapiga tena


“Hallow “ simu ikapokelewa na sauti nzito ya kiume.Margreth akastuka na kudhani labda amekosea namba


“Halow naitwa Margreth,napiga simu toka Tanz…..” kabla hajamaliza,yule mwanaume aliyepokea simu akasema


“Margreth,Mike hapa naongea.Habari za Tanzania?Umekwisha isahau sauti yangu mara hii?


Margreth akavuta pumzi ndefu na kusema


“Mike !! nafurahi kuongea nawe tena.Ni muda mrefu umepita.Samahani kwa kukusumbua na kukuamsha usingizini.Nilikuwa Nahitaji kuongea na Happy”


“Happy niko naye hapa.Subiri kidogo nimuamshe” akasema Mike na baada ya muda sauti yenye usingizi ya Happy ikasikika


“Hallow Margreth”


“Happy.!! Samahani nimekuamsha”


“Usijali Margreth hata hivyo nimelala muda si mrefu sana.Mike amekuja leo hivyo tukaenda club,Habari za huko?


“Huku kwema Happy,tunaendelea vizuri isipokuwa yule rafiki yangu Salama amefariki dunia wakati akijifungua na leo tunamzika”


“Salama yule aliyeolewa na mzungu?


“Ndiyo huyo”


“Dah ! poleni sana.Habari nyingine?


“Habari nzuri Happy.” Akasema Margreth


“Maggie nilikuahidi kukutumia ile hela ya kununua gari,sijasau nitakutumia wiki ijayo,wiki hii nilikuwa nimetingwa sana na kazi”


“Ahsante sana Happy lakini sijakupigia kwa ajili ya suala hilo.Kuna suala linguine”


“Suala gani Maggie?


“Happy kuna tatizo limejitokeza”:


“Tatizo gani? akauliza Happy.Margreth akashusha pumzi na kusema


“Its about Patrick”


“Patrick ..!!!! “ Happy akastuka


“Ndiyo Happy.Nimeoanana na Savanna muda si mrefu na amenifahamisha kwamba Patrick alifanikiwa kupata dhamana na yuko huru lakini kesi yake inaendelea kusikilizwa na kinachoendelea hivi sasa ni mashahidi wa upande wa utetezi kutoa ushahidi wao.Savanna alitaka kufahamu mahala ulipo” akasema Margreth


“Ananitafuta mimi? Kwa nini? Akauliza Happy kwa wasi wasi


“Jina lako liko katika orodha ya watu wanaotakiwa kutoa ushahidi wao mahakamani kumtetea Patrick”


“No ! No ! no !!!..Thats impossible.Margreth no body should know where I am.” Akasema Happy


“Its too late Happy.Nimelazimika kumweleza ukweli Savanna kutokana na uzito wa suala lenyewe.”


“Ouh Margreth how on earth could you do such a thing? Tulikubaliana kwamba asiambiwe mtu mwingine yeyote mahala nilipo.Kwa nini lakini umefanaya hivyo? How could you betray me? Akalalama Happy


“Naomba unisamehe sana Happy kwa kilichotokea.Najua yalikuwa ni makubalianao yetu kwamba asifahamu mtu mwingine yeyote mahala ulipo lakini nimelazimika kumweleza Savanna na hakuna mtu mwingine yeyote anayelifahamu hilo zaidi yake.”


“Margreth siwezi kukuamini tena.Umeyafanya maisha yangu yawe magumu tena.Umenifanya nirudi tena katika kile ambacho nimekuwa nikikimbia kwa muda huu wote” akasema Happy


“Happy naomba unisikilize kwa makini.Nililazimika kumweleza Savanna mahala ulipo baada ya kuniweka wazi kwamba ushahidi wako una nguvu sana ya kumsaidia Patrick asihukumiwe kifungo.Happy hata mimi inaniuma sana kukukumbusha mambo ambayo unajitahidi kuyasahau lakini naomba niwe muwazi kwako kwamba you have to save Patrick.He saved you from going to jail and its your turn now to save him” akasema Margreth.Baada ya ukimya mfupi Happy akasema


“Margerth nimekuelewa lakini sina hakika kama nitaweza kufanya hivyo.Ninapambana hivi sasa kumsahau Patrick na kuendelea na maisha yangu mapya yenye furaha na siko tayari kuonana tena na Patrick ana kwa ana.” Akasema Happy


“Happy sina maana ya kwamba ukitoa ushahidi utarudiana tena na Patrick na wala sikushauri ufanye hivyo lakini nakukumbusha tu kwamba Patrick ameubeba mzigo mkubwa sana na endapo atafungwa kwa sababu tu ya kukosekana ushahidi wenye nguvu,nakuapia Happy hautakuwa na furaha hata siku moja katika maisha yako.Patrick’s shadow will haunt you forever” Akasema Margreth


“What can I do Margreth? Let it be.Look Margreth ,there is nothing I can do now to help him.I’m trying to pick up the pieces and arrange my life again so I cant go back to square one.Nilimtenda vibaya Mike na kumsababisia maumivu makali ya moyo lakini hivi sasa ndiye amekuwa msaada wangu mkubwa na ndiye anayenisaidia kusahau mambo yote yaliyopita.Ninaishi hapa Marekani kwa sababu yake.Amenitafutia nyumba,kazi na kila kitu.He loves me and I’m learning to love him so how could I tell him that I’m going back to Tanzania? Please Margreth,this conversation is over.” Akasema Happy


“Happy kabla hujakata simu naomba nikukumbushe kitu kimoja.Ulinitamkia wewe mwenyewe kwa mdomo wako kwamba Patrick hakusababisha kifo cha Vero bali ni wewe uliyemsukuma akajigonga ukutani na kufariki.Patrick kwa mapenzi makubwa aliyokuwa nayo kwako aliamua kujitwisha yeye mzigo wote .Ameteseka gerezani kwa kipindi kirefu na bado anaendelea na kesi.Nomba leo unitamkie neno moja tu kwa mdomo wako kwamba uko tayari Patrick afungwe gerezani kwa kosa ambalo hakulitenda? Nipe jibu moja tu na nitakuelewa” akasema Margreth.Happy machozi yakamtoka


“I don’t know Margreth.’ll call you later” akasema Happy na kukata simu.Machozi yalianza kumtoka na akaanza kulia kwa kwikwi.Mike aliyekuwa chumbani akatoka haraka aliposikia Happy akilia kwa kwikwi.


“Happy kuna nini? Mbona unalia? Kuna taarifa ambayo si nzuri? Akauliza Mike


Happy akamkumbatia Mike kwa nguvu huku akiendelea kulia


“Nyamaza kulia mpenzi wangu na uniambie nini kinakuliza.Kuna tatizo gani nyumbani? Akauliza Mike.Happy hakujibu kitu aliendelea kulia kwa kwikwi.Mike akamletea glasi ya maji akanywa


“Tafadhali niambie Happy una tatizo gani?


“Mike kuna tatizo limetokea”


“Niambie Happy ni tatizo gani ? Niko hapa kukusaidia”


“Si tatizo kubwa lakini linahusiana na kesi ya Patrick” akasema Happy na kumstua Mike


“Nini kimetokea katika hiyo kesi?


“Savanna wakili anayemtetea Patrick amefika nyumbani leo hii na kuulizia taarifa zangu na kuomba apatiwe mawasiliano yangu lakini kwa bahati mbaya amekutana na Margreth na akamueleza kila kitu kuhusu mimi”


“Ouh my gosh ! Kwa nini lakini amefanya hivyo wakati mlikwishakubaliana kwamba mtu yeyote asifahamu mahala ulipo?


“Kwa madai ya Margreth ni kwamba aliamua kumweleza ukweli Savanna kutokana na uzito wa suala hilo alilokuwa ananitafutia”


“Ni suala gani alilokuwa anakutafutia?


Happy akafikiri kidogo na kusema


“Natakiwa kutoa ushahidi wangu mahakamani kumtetea Patrick.”


Kimya kikatanda mle ndani.Kila mmoja alikuwa anawaza lake.Mike alionekana kuishiwa nguvu.


“Happy my angel tell me its not true and if true you wont do it” akasema Mike


“Its true Mike.Natakiwa mahakamani nikatoe ushahidi wangu.


“That’s impossible.You cant go back there” akasema Mike.Alistushwa sana na taarifa ile ya Happy


“Happy mpenzi naomba unihakikishie kwamba hutakwenda tena Tanzania.Hutakwenda kuonana tena na Patrick.Kama ingekuwa ni kesi inayomkabili mtu mwingine nisingekuwa na wasi wasi wowote lakini kukuacha ukaonane tena na Patrick hilo ni jambo ambalo siwezi kulifanya” akasema Mike huku amemshika Happy mabeganiCHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/


“Mike kuna jambo ambalo ningependa ulifahamu” akasema Happy


“Jambo gani Happy ? Mbona unanipa wasi wasi mpenzi wangu? Akauliza Mike.Happy akavuta punzi ndefu na kusema


“Patrick hakumuua Vero”


Mike akastuka na kumtumbulia Happy macho.


“Sikuelewi unamaanisha nini Happy.Patrick anatuhumiwa kwa kusababisha kifo cha Vero.Kwa nini unasema kwamba si yeye aliyesababisha kifo cha Vero? Akauliza Mike.Happy akamtazama usoni na kusema


“Mimi ndiye nilisababisha kifo cha Vero.” Akasema Happy


Mike akastuka na kumuachia Happy mikono halafu akasimama na kumuangalia Happy kana kwamba ni mara ya kwanza anamuona


“That’s not true .Its not true…” akasema Mike


“Its true Mike.I killed her.Samahani kwa kutokwambia kuhusu suala hili kwa sababu hii ni sehemu moja ya maisha yangu ambayo ninapambana ili niisahau.”akasema Happy


“Sikuelewi mpenzi wangu.Kwa nini unifiche kitu kikubwa kama hiki?


“Nisamehe mpenzi wangu.Naomba unisamehe Mike na unielewe kwamba sikufanya makusudi kutokwambia kitu kama hiki.Naamini hata wewe ungekuwa katika nafasi yangu ungefanya kama nilivyofaya mimi yaani kuliweka jambo hili kuwa ni siri ya moyoni.Ni jambo ambalo kila nikilifikiria huwa linanipa wakati mgumu sana.I’ve been trying to forget that night but I cant..” akasema Happy huku akishindwa kujizuia na kutoa machozi.Mike akamsogelea na kumkumbatia


“Nyamaza mepnzi wangu.Nyamaza Happy.Naomba unieleze ni kitu gani kilitokea usiku huo na kwa nini Patrick ndiye anayetuhuiwa kwa kusababisha mauaji hayo? Akasema Mike.Happy akafuta machozi akafikri kidogio na kusema


“Tulikuwa hotelini mimi na wewe tukipata chakula nilipopigiwa simu na Patrick kwamba kuna matatizo yametokea na baba yake amelazwa katika hospitali kuu ya magonjwa ya moyo .Kama utakumbuka nilikuomba unirudishe nyumbani ambako nilichukua gari langu na kukimbia hospitali.Nilimkuta Patrick halafu tukapanda katika ghorofa ya juu ambayo bado ujenzi wake ulikuwa unaendelea na Patrick akaanza kunisimuilia kilichotokea.Ghafla akatokea Vero akiwa na bastora mkononi.Alikuwa amekasirika na sura yake ilionyesha kwamba alikuwa amedhamiria kufanya kitu kibaya.Nadhani nilikueleza kuhusiana na kitendo alichokifanya Patrick cha kuvunja uchumba na Vero kitendo ambacho kilimuumiza sana.Alituelekezea bastora ile huku akitoa vitisho vingi sana na kutishai kututoa uhai mimi na Patricki.Patrick alimsihi aache utani na silaha za moto na ndipo alipoonyesha kwamba hakuwa akitania pale alipoachia risasi iliyonikosa na kupiga nguzo.Nilihisi kama nimekufa nikaanguka chini.Kitendo kile kilimkasirisha Patrick ambaye bila kujali hatari iliyokuwepo akamfuata Vero na kuanza kumnyang’anya Vero ile silaha.Kitendo kile kiliniogopesha sana na nikajua Vero angeweza kumdhuru Patrick hivyo nikainuka na kwenda kumsukuma Vero ambaye alijigonga ukutani na kufariki dunia.Patrick hakutaka nihusishwe katika kesi ile kwa kuamua kuubeba mzigo wote wa kesi ya mauaji .Kila mtu anajua kwamba Patrick ndiye aliyesababisah kifo cha Vero.Alikubali kuubeba mzigo huu mzito wa kesi kubwa kama hii kwa ajili yangu kwa ajili yua kunikinga na kesi hii.”akasema Happy.Mike akamtazama kwa makini na kusema


“Ahsante Happy kwa kunieleza ukweli lakini pamoja na hayo ninataka kukuuliza jambo moja ”


“Uliza Mike”


“Do you still love him? Akauliza Mike


“Mike !! ..akasema Happy


“Just answer my question Happy.Do you have any feeling for him?


“Mike I’m with you now.Its you that I love now.Nimekuwa nikijitahidi kuifuta picha ya Patrick moyoni mwangu na hiyo inamaanisha kwamba sina hisia zozote kwake”


“Are you sure? Akauliza Mike


“Yes Mike I’m sure”


“Kama ni kweli hayo unayoniambia kwa nini ulikuwa unalia baada ya kuzipata taarifa hizi?


“Mike hata kama ungekuwa ni wewe lazima ungetoa machozi.Patrick naye ni binadamu na anakabiliwa na kesi kwa kosa ambalo hakulitenda .Nilishindwa namna ya kufanya hasa katika wakati huu ninaojitahidi kumsahau ndiyo maana nikashindwa kujizuia kulia” akasema Happy


“Its ok Happy.Forget about that.Umeshaamua kuyasahau yote ya nyuma kwa hiyo songa mbele.Mimi niko hapa na niko tayari kukusaida kwa kila namna nitakavyoweza ili uweze kusahau historia na matukio yote yaliyopita.Let him go”


“Mike ! How could you say that? Ingekuwa ni wewe uko katika nafasi yangu ungefanya nini? Ungemuacha mtu kama huyu afungwe gerezani? He saved me.He saved a woman you love.So that’s how you repay him? Akauliza Happy


“So what’s your decision? Akauliza Mike


“Nitakwenda Tanzania.Nitakwenda kutoa ushahidi wangu mahakamani.Siko tayari Patrick afungwe gerezani.Tafadhali Mike naomba uniruhusu niende Tanzania nikamtolee Patrick ushahidi.Lengo langu ni ili Patrick awe huru na aendelee na maisha yake.Najua unaogopa nini kitatokea endapo nitaonana naye lakini nakuhakikishia kwamba kitakachonipeleka huko ni kutoa tu huo ushahidi wangu na jambo lingine lolote.Me and him its over.” akasema Happy.Mike akazunguka zunguka mle ndani na kusema


“Laiti nisingekuwa na marufuku ya kukanyaga ardhi ya Tanzania nisingekubali uende peke yako.Ningekupeleka ukatoe ushahidi wako halafu turudi wote marekani.Sijui ni kwa nini ninakosa imani na Patrick.” Akasema Mike kwa masikitiko


“Kwa maana hiyo unaniruhusu niende Tanzania? Akaulza Happy


“Sina haja ya kukuruhusi kwani tayari umekwisha fanya maamuzi na siwezi kukukatalia.Ni kweli Patrick anastahili kutendewa wema kama alioutenda kwako.Lakini sijui kwa nini roho yangu bado inasita sana”


“Huniamni Mike?


“Nakuamini sana mpenzi wangu lakini nashindwa kujizuia kuwa na wasi wasi kuja kwamba unakwenda kuonana na Patrick tena.Patrick alifanya kitendo cha kijasiri sana ambacho hata mimi kimenigusa ,lakini naomba nikiri kwako mpenzi wangu kwamba siwezi kushindana na Patrick katika vita ya kukugombania .Nafahamu Patrick amekuwa moyoni mwako kwa miaka mingi sana .Nenda Tanzania mpenzi lakini ujue kwamba ninakuamini na kwamba hutafanya kitendo kama ulichonifanyia kipindi kile kwani sijui kama nitaweza kuyavumilia maumivu na mateso ya moyo kama niliyoyapata wakati ule.” Akasema Mike


“Mike naomba uniamini haya nikwambiayo kwamba kilichobaki kati yangu na Patrick ni historia tu.Kinachonisukuma kutaka kwenda kutoa ushahidi wangu ni kumsaidia ili kama ikiwezekana aweze kuachiwa huru.Alionyesha ubinadamu mkubwa kwangu kwa hiyo na mimi sina budi kumsaidia.After this I’m done with him.Patrick atakuwa huru na maisha yake na mimi nawe tutakuwa huru” akasema Happy


* * * *


Margreth akiwa msibani pamoja na waombolezaji wengine mara simu yake ikaita.Alikuwa ni Happy aliyempigia


“Hallo Happy” akasema Margreth baada ya kupokea simu


“Tayari umefika msibani?


“Ndiyo Happy.Tunajiandaa kwenda kuzika”


“Sawa Magreth,nimekupigia kukutaarifu kwamba ninakuja Tanzania kutoa ushahidi wangu halafu nitarejea tena marekani. Najua nitakabiliana na matatizo mengi lakini sina namna lazima nikabiliane na kila kitu.Naomba uongee na Savanna na akwambie ni lini ninahitajika mahakamani.”


“Ouh god thank you so much.Ahsante sana Happy kwa uamuzi huu.Nitamtaarifu Savanna halafu nitakufahamisha jibu atakalonipa” akasema Margreth na kukata simu halafu akamtafuta Savanna na kumtaarifu kuhusiana na jibu la Happy” .Hizi zilikuwa ni habari njema sana kwa Savanna japokuwa alishindwa kujizuia kuwa na wasi wasi nini kitatokea pale Patrick na Happy watakapokutana tena


“Sijui ni kwa nini ninakuwa na wasi wasi mwingi kuhusu Patrick kuonana na Happy.Labda ni kutokana na historia yao kwamba kila wakutanapo hushindwa kuzizuia furaha zao basi mapenzi yao huanza upya.Lakini sipaswi kuwa na wasi wasi wowote.Patrick ni wangu na hakuna yeyote mwenye uwezo wa kumnasua toka katika mikono yangu.Ni Happy pekee ndiye mwenye kunipa wasi wasi “akawaza Savanna akiwa ofisini kwake




Ndege ya shirika la ndege la afrika kusini iliwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam saa mbili za usiku.Miongoni mwa abiria waliokuwemo katika ndege hii ni Happy Kibaho ambaye monekano wake ulikuwa umebadilika sana na alionekana mrembo zaidi ya alivyokuwa alipoondoka Tanzania miezi zaidi ya kumi iliyopita.Kama ungekutana naye ghafla ingekuwia ugumu kidogo kumtambua.


Baada ya kukamilisha taratibu alitoka nje na kulakiwa na familia yake yote.Kilikuwa ni kipindi cha furaha kubwa kwa familia hii kukutana tena na mtoto wao ambaye hawakuwa wametegemea kama wangeonana naye tena hivi karibuni.Wote waliustaajabia uzuri wa Happy na namna alivyokuwa amebadilika.Hakukuwa na mwandishi yeyote wa habari aliyekuapo pale uwanjani kwani ujio wa Happy ulikuwa ni wa siri kubwa


“Wow Happy umebadilika sana” akasema mzee Kibaho na kumkumbatia mwanae kwa mara ya pili


“Ouh Dady ! nililazimika kufanya mabadiliko kidogo katika muonekano wangu wa zamani.Nilitaka nibadilike na kuwa Happy wa tofauti na zamani”


“You look so wonderfull and amazing as always.You look more than an angel” akasema mzee Kibaho kisha wote wakaelekea katika gari lao na kurejea nyumbani.Waliwasili nyumbani ambako kuliandaliwa tafrija ndogo ya kumkaribisha tena nyumbani Happy.Baada ya chakula na maongezi Happy akapelekwa chumbani kwake kulala.


“Margreth naomba nikalale chumbani kwako.Sitaki kulala katika chumba change cha zamani.Kuna kumbukumbu nyingi za nyuma ambazo nimekwisha anza kuzisahau.” Akasema Happy na kuelekea katika chumba cha Margreth.Kabla ya kulala,Happy akamkumbusha Margreth amtaarifu Savanna kwamba tayari amekwisha wasili na kama ana nafasi waonane kesho .Margreth akazitafuta namba za simu za Savanna akapiga.


Kwa muda wa dakika kadhaa sasa Savanna alikuwa anamkodolea macho Patrick bila kuongea lolote


“C’mon my angel ! Mbona unanitazama namna hiyo? Akauliza Patrick


“Sijui ni kwa nini nimejikuta nikiwa hivi siku ya leo.Natamani niendelee kukuangalia usiku kucha.Patrick nakupenda sana.Nakupenda zaidi ya unavyoweza kufikiri.Naomba niwe wazi kwako kwamba sintaweza kuishi maisha yangu bila ya kuwa nawe.” Akasema Savanna kwa sauti laini yenye mahaba mazito.Patrick akamvuta kwake na kumbusu kisha akasema


“Savanna wewe ni malaika wangu.Naomba ufahamu kwamba nakupenda na nitakupenda daima.Nakuahidi mara tu mambo haya yatakapokwisha basi tutafunga ndoa na tutaishi sote hadi kifo kitakapotutenganisha.” Akasema Patrck


“Patrick my love kwa nini tusifunge ndoa hata kabla ya kesi hii kumalizika? Binafsi sioni kipingamizi chochote cha kutuzuia tusifunge ndoa mapema” akasema Savanna


“Hakuna kipingamizi chochote Savanna cha kutufanya mimi nawe tushindwe kufunga ndoa.Kitu pekee kinachonisukuma na kunifanya niamni kwamba ni vyema kama tutafunga ndoa baada ya kesi kumalizika ni kuogopa kuchanganya mambo.Ninafikiria ni bora kama tukaelekeza nguvu katika jambo moja kwanza na baada ya kulimaliza basi tuelekeze nguvu katika jambo lingine ambalo ni ndoa yetu”


“Nakubaliana nawe Patrick japokuwa nilipenda sana jambo hili tulifanye mapema.Hata hivyo wazo lako zuri ni la msingi sana.Hatuna budi kuelekeza nguvu zetu zote kwa sasa katika kesi na baadae tushughulike na ndoa.” Savanna akastushwa na mlio wa simu yake.Akausogeza mkono na kuichukua


“Ni Margreth” akasema Savanna


“Anataka nini usiku huu? Akauliza Patrick


“sijui ngoja nimsikilize” akasema Savanna na kubonyeza kitufe cha kupokelea


“Hallo Margreth”


“Hallo Savanna.Samahani kwa kukusumbua usiku huu”


“Bila samahani Margreth.Jisikie huru kunipigia wakati wowote”


“Ahsante sana.Savanna nimekupigia kukutaarifu kwamba Happy amekwisha wasili.Amefika usiku huu.Ameomba kesho muonane hapa nyumbani”


“Ouh ok.Thats good news.Mwambie nashukuru sana kwa kufika kwake .Amefanya jambo kubwa na la maana sana na kesho nitakuja kuonana naye” akasema Savanna


“Kitu kingine Savanna,utakapokuja kuonana na Happy please don’t bring Patrick with you.Make sure Patrick and Happy they wont see each other.”


“Usijali Margreth.Siwezi kuambatana na Patrick. “


“Thank you Savanna.Good night”


“Good night Margreth” akajibu Savanna na kukata simu halafu akamgeukia Patrick


“Happy amekwisha wasili”


Patrick akavuta pumzi ndefu kisha akasema


“Hizo ni habari njema sana.”


“Yah.Amefanya jambo la maana ” akasema Savanna kisha akamkazia macho Patrick


“Nini Savanna? Mbona unaniangalia hivyo?


“Kuna kitu ambacho nahitaji uhakika toka kwako”


“Kitu gani Savanna?


“Are you sure there will be no problem when you see Happy again?


Patrick akamtazama Savanna akavuta pumzi ndefu na kusema


“Usihofu Savanna,nakuhakikishia kwamba hakutakuwa na tatizo lolote.Siwezi kukuficha kwamba tayari nimekwisha mtoa Happy moyoni mwangu lakini bado nina donge kubwa limenikaa kooni la kutaka kufahamu ni kwa nini alitenda vile ? Kwa nini alifanya kitendo kile cha kupiga picha na video za utupu na kuzivujisha? Zaidi ya yote kwa nini aliamua kunitelekeza gerezani wakati akifahamu fika kwamba nilikuwa nimeubeba mzigo ambao ulimuhusu yeye? Ningefurahi sana kama ningepata nafasi ya kumuuliza na kupata majibu ya maswali yangu lakini sintaweza kufanya hivyo kwani sitaki kukumbuka mambo ya nyuma.Kitu cha msingi ninachoshukuru ni kwa kukubali kwake kuja kutoa ushahidi.Baada ya kumaliza kutoa ushahidi sintahitaji kumuona tena.Nataka niendelee na maisha yangu nikiwa na wewe mpenzi wangu ambaye unanipenda,unanijali na kunithamini.” Akasema Patrick na uso wa Savanna ukajenga tabasamu pana,akainama na kumbusu halafu wakakumbatiana.


* * * *


Ni Happy ndiye aliyemuamsha mdogo wake Margreth asubuhi ili ajiandae awahi kazini.Usiku wa kuamkia siku hiyo ulikuwa mrefu sana kwa Happy na hakuweza kupata kabisa usingizi.Picha za matukio yaliyotokea miezi zaidi ya kumi iliyopita zilikuwa zkimjia kila alipojaribu kufumba macho.Alikumbuka toka kipindi alichokutana na Patrick shuleni Malangali Iringa hadi muda huu.


“Happy leo hujalala kabisa” akasema Margreth kwa sauti iliyojaa usingizi.Happy akatabasamu


“Mimi ni kawaida yangu.Huwa nina muda mchache sana wa kulala,muda mwingi ninafanya kazi.Amka ujiandae uende kazini” akasema Happy


Margreth akaamka akajindaa na kuondoa zake kuelekea kazini.Happy naye akatoka na kuanza kuizunguka nyumba yao.


Saa nne za asubuhi ilimkuta Savanna katika geti la akina Happy.Akapiga honi na Pendo mfanyakazi wa ndani akamfungulia geti na kumkaribisha ndani


Mtu wa kwanza kusalimiana naye alikuwa ni mzee Kibaho.Kwa kuwa mzee KIbaho alikuwa na haraka ya kuwahi katika shughuli zake hakuongea sana na Savanna akaondoka na kumuacha Savanna akiongea na mama yake Happy hadi pale Happy alipojitokeza.Savanna alishindwa kujizuia kutoa tabasamu pana sana baada kumuona tena Happy na namna alivyobadilika na kuwa mzuri


“My gosh ! huyu ni Happy au ni mzimu wake? Gosh ! she’s so pretty.She’s amazing.Dah ! binti huyu amejaaliwa uzuri wa aina yake” akawaza Savanna


“Hallow Savanna” akasalimu Happy


“Hallow Happy” akajibu Savanna na kuinuka kisha wakakumbatiana


“karibu tena nyumbani Happy” akasema Savanna


“Ahsante Savanna,nimefurahi sana kurejea tena nyumbani.Poleni na matatizo ya kila siku”


“Tumekwisha poa Happy.” Akasema Savanna halafu mama yake Happy akainuka na kuwaacha peke yao pale sebuleni ili kuwapa nafasi nzuri ya kuongea mambo yao kwa uhuru.


“Savanna twende bustanini ,naona hapa sebuleni hapatufai kwa maongezi yetu” akasema Happy kisha wakainuka na kuelekea bustanini


“Karibu sana Savanna.Habari za siku? Akaanzisha mazungumzo Happy baada ya kufika bustanini


“Habari nzuri Happy.Nimefurahi tena kukuona.Umebadilika sana.Ouh my gosh you are so beautiful.You are mazing” akasema Savanna na Happy akatabasamu


“Thank you Savanna” akajibu Happy


“Vipi maisha yako kwa ujumla? Akauliza Savanna


“Namshukuru Mungu .Kwa kweli Mungu anaweza.Ukimuomba kwa dhati Mungu anajibu.Nilikwisha kata tamaa kabisa na maisha yangu.Nilimuomba Mungu nikamlilia anisaidie na kweli amenisaidia na hali yangu imebadilika kama unavyoniona” akasema Happy na kucheka kidogo


“Nilipatwa na wasi wasi mkubwa Christine aliponipigia simu na kunitaarifu kwamba umetoweka pale hotelini Kigali na hawajui mahala ulipo.” Akasema Savanna na kumfanya Happy acheke kidogo


“Savanna kwanza kabisa napenda nikushukuru wewe binafsi kwani msaada wako ulikuwa mkubwa mno na ambao siwezi kuulipa.Ulinisaidia sana kujitambua na kunifanya niamue kuishi tena.Baada ya kukaa kwa muda pale Kigali nilipata wazo la kuondoka .Niliamua niende Marekani .Nilijua ile ndiyo sehemu salama kwa mimi kuishi tofauti na pale Rwanda ambako ni karibu sana na Tanzania.Vile vile tayari taarifa zangu zilikwisha fika kule na tayari nilianza kufahamika.Mtu pekee aliyenisaidia nikarejea tena Marekani ni Mike.Ninamshukuru sana kwa msaada wake mkubwa.Kwa sasa ninaishi na kufanya kazi Los Angeles na maisha yangu yanakwenda vizuri.” Akasema HappyCHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/


“So you are back together,you and Mike” akauliza Savanna


“I’m sorry to say this Savanna but yes ! we’re back together and deeply in love na tunategemea kufunga ndoa” akasema Happy huku akitabasamu kuona aibu kwa mbali


“Ouh ! Congraturations” akasema Savanna


“Thank you” akajibu Happy kisha kimya kifupi kikapita


“What a stupid woman..Yaani anadiriki kusema wazi wazi kwamba amerudiana na Mike na wanatarajia kufunga ndoa huku akisahau kwamba alimuacha Patrick akisota gerezani kwa kosa ambalo hakulitenda.” Akawaza Savanna.Happy akasema


“Savanna haikuwa rahisi kwangu kuamua kuja tena Tanzania.Niliapa kutokurudi tena Tanzania lakini kutokana na uzito wa suala lenyewe nimevunja kiapo changu ili na mimi niweze kutoa msaada wangu japo mdogo kwa Patrick ambaye alifanya jambo la kijasiri sana kuniokoa mimi nisikae gerezani kwa hiyo isingekuwa vyema kama ningekataa kuja kumtolea ushahidi .Nimekuita hapa ili unipe mwongozo wa kinachoendelea na ninachotakiwa kukisema mahakamani” akasema Happy


“Happy nimefurahi sana kusikia maendeleo yako na kukuona ukiwa ni mwenye furaha.Lakini kabla hatujaendelea na maongezi yetu aren’t you gonna ask?


“Ask what? Happy akashangaa


“How he’s doing”


“Savanna,Patrick ni mtu ambaye nilimpenda kwa moyo wangu wote.Sijawahi kupenda mtu kama nilivyompenda yeye.Amenifanyia mambo mengi ambayo hakuna mtu yeyote anaweza akanifanyia.Patrick made me a woman.Kuna mengi ambayo naweza kueleza kwa siku nzima kuhusu Patrick lakini naweza kusema kwamba maisha ni kitu cha ajabu sana.Pamoja na upendo wote na kila kitu alichonifanyia Patrick lakini hivi sasa I’m fighting to forget him.Its difficult but I thank God I’m doing fine without him.Ninaamini mimi na Patrick hatukupangwa tuwe pamoja.” Akasema Happy akanyamaza akameza mate na kuendelea


“Sijataka kumuulizia kwa sababu ninajua mimi ni mtu ambaye hataki kuniona tena katika maisha yake na ana hasira kubwa na mimi kwanza kwa kuziona picha zile na pili kwa kuondoka na kumuacha gerezani.Savanna moyo wangu unaniuma sana japokuwa hakuna anayeweza kulifahamu hilo.Bado kitendo kile cha kudhalilishwa kwa zile picha chafu hakijapona na kurudi kwangu tena Tanzania kumekitonesha kidonda change.Sina hakika kama ulimueleza Patrick ukweli halisi wa kilichotokea.Japo kwa ufupi unaweza ukanieleza anaendeleaje?


“Patrick is fine.He’s doing ok.Tuliibadili kesi na kuwa kesi ya kuua bila kukusudia na akapatiwa dhamana.Anaendelea vizuri na maisha yake mapya na kwa sasa ni meneja wa kiwanda cha kusindika nyama.” akasema Savanna


“Ouh that’s great.Is he married ? akauliza Happy huku akitabasamu.Savanna naye akatabasamu


“Not yet”


“Ouh Gosh ! what he’s waiting for? Is he still waiting for me?


“Tunasubiri mambo haya yamalizike ndipo tuanze taratibu za ndoa yetu” akasema Savanna huku akitabasamu


“We? are you two together? Akauliza Happy kwa mshangao.


“Yes ! we’re together now.We live together though not yet married” akasema Savanna


Happy akavuta pumzi ndefu na kumeza fundo la mate.Akapatwa na kigugumizi akakohoa kidogo na kusema


“Congraturations guys” akasema Happy na sura yake ilionyesha mabadiliko kidogo.


“Thank you “ akasema Savanna.Ni wazi maneno yale ya Savanna yalimchoma Happy.Savanna aliligundua hilo na hakutaka kuendeleza maongezi kuhusu mahusiano yake na Patrick na badala yake akaendelea kumweleza Happy kuhusiana na mwenendo wa kesi na namna atakavyotoa ushahidi wake.Baada ya maongezi marefu Savanna akaondoka zake.


* * * *


Ni alhamisi siku ambayo Happy alitakiwa kusimama kizimbani na kutoa ushahidi wake.Siku hii aliamka mapema sana asubuhi akaanza kujiandaa.Alikuwa mkimya na mwenye wasi wasi.Mpaka ilipotimu saa tatu za asubuhi tayari alikwisha jiandaa tayari kabisa kuelekea mahakamani .Familia nzima ilikuwa imejiandaa kuandamana naye mahakamani.


“Are you ready Happy? akauliza mzee Kibaho


“I’m ready dady though I’m a bit nervous” akajibu Happy


“Be strong .You can do it” akasema mzee Kibaho


“Yes Dady.I’ll be strong.I need to finish this”


“Tuko pamoja Happy usiogope” akasema Margreth kisha kwa pamoja wakaingia garini na safari ya kuelekea mahakamani ikaanza.


Mahakama ilifurika watu tofauti na siku za kawaida.Tetesi za Happy kuwepo mahakamani siku hii zilisambaa na kuwafanya watu wafurike mahakamani ili kumuona mrembo huyu ambaye aliviteka vyombo vya habari miezi zaidi ya kumi iliyopita kutokana na skendo zake mbali mbali na hasa ile ya mwisho ambapo picha na video zake za utupu vilisambaa katika magazeti na mitandao na kisha akatoweka ghafla bila kujulikana alielekea wapi.Wengi walikuwa na hamu ya kumuona tena.


Saa tano na dakika ishirini,Happy aliwasili mahakamani akiwa ameongozana na familia yake.Pale mahakamani alipokewa na Savanna na kuongozwa kuelekea ndani ya jengo la mahakama.Wengi hawakuweza kumtambua kwa haraka kutokana na namna alivyokuwa amebadilika.


“Nashukuru sana umekuja Happy.Naomba ondoa wasi wasi” akasema Savanna


“Usijali Savanna.I’ll do my best” akajibu Happy huku uso wake ukijilazimisha kutabasamu


Savanna aliingia ndani ya mahakama na Happy akaufungua mlango wa chumba kimoja mle mahakamani akaingia ndani na kumuomba Happy naye aingie.Mara tu alipoingia ndani ya chumba kile Happy akapatwa na mstuko mkubwa.Alitumbua macho kana kwamba ameona mzuka au kitu cha kushangaza.Alibaki amesimama huku akihisi mwili wake kuingiwa na baridi.Alikuwa anatazamana na Patrick ambaye naye alipatwa na mstuko .Chumba kikagubikwa na ukimya mzito.Savanna ambaye alisimama katikati yao akawaangalia wote na kisha akasema


“I’ll be outside.I’ll leave you guys alone so that you can great each other” akasema Savanna na kutoka mle chumbani.Patrick na Happy waliendelea kutazamana huku wote wakiwa bado wamesimama.Baada ya kama dakika mbili Patrick akakohoa kidogo na kusema


“Hallow …Ha..Happy”

INAENDELEA

Tags

Post a Comment

0 Comments
Post a Comment (0)

Made with Love by

Pixy Newspaper 11 Template is Designed Theme for Giving Enhanced look Various Features are availabl…
To Top