Simulizi : Nenda Na Moyo Wangu Sehemu Ya Kwanza (1)

ADMIN
0

 


IMEANDIKWA NA : STALLONE JOYFULL


*********************************************************************************


Ninachokumbuka ni mlio wa simu, ambao ulinikumbusha kuivua suruali kisha


viatu; nilivyotaka kulala navyo bila kuvua kutokana na pombe nyingi


nilizokunywa. Ulikuwa ni mlio ulioashiria ujumbe mfupi wa maneno uliingia


katika simu yangu, hata hivyo sikushuhurika nayo nikajitupa kitandani


kivivu. Siku hiyo sikuoga wala kukumbuka chakula.




Mara nikiwa katikati ya usingizi, ghafla simu ikaita kwa sauti ya juu.


Hapana!


Ilikuwa ni sauti ndogo ya kawaida ila kwa kuwa niliilalia kwa sikio langu,


ndio maana niliisikia kuwa ilikuwa ikitoa sauti kali mno. Kwa hasira


sikutazama aliyekuwa akipiga wala aliyenitumia meseji ile, nikaizima.


Usingizi mzito ukanibeba kwenye usiku ule wa manane mpaka nilipoamka


asubuhi majira ya saa 4:25 asubuhi. Niliandaa maji ya moto ya kuoga huku


simu yangu nikiwa nimeiweka chaji. Nikiwa nayasubiri maji yachemke,


nilikihisi kichwa changu kizito kutokana na pombe nilkizokunywa, nikaanza


kuikumbuka siku ya jana nikiwa nimekaa kitandani, kiunoni n'na taulo zito


jeupe kifua wazi tayari kwa kuoga.


....




NIKIIKUMBUKA SIKU YA JANA JINSI ILIVYOKUWA:- Jana ilikuwa ni jumatatu, kama


jumatatu nyingine zenye pilikapilika nyingi tofauti. Hiyo ilikuwa ni


kuanzia asubuhi mpaka ilipotimu majira ya jioni, jumatatu hiyo ikabadilika


kwetu na kuwa sawa na wikiendi. Katikati ya hoteli ya Lamada kwenye bustani


murua yenye ukijani uliokolea, tulijumuika katika tafrija ya tukio maalumu


la kuvishana pete mimi na mpenzi wangu Beatrice.


Tuliwaalika ndugu jamaa na rafiki zetu wa karibu, kushuhudia tukio hilo la


kipekee. Kila mmoja alikuwa na uso wa furaha kwa kushuhudia tukio lile


likitimia. Mimi na Beatrice tulifurahi zaidi kwa kuwa ndoto zetu


ziliendelea kutimia tangu tulipoanza uhusiano wetu tukiwa chuo.


"Nakupenda sana Beatrice"


"Hakuna mwingine zaidi yako Ramon"


Kisha tukapeana papi zetu, huku ndimi zetu zikipigana kwa furaha kwakitendo


cha badilishana lita kadhaa za mate midomoni mwetu. Sherehe iliendelea,


watu wakafurahi wakala wakashiba, walevi wakanywa wakalewa nikiwa mmoja wao


kati yao, huku Beatrice akiwa ameshika chupa yake ya tatu ya soda akinywa


taratibu.


Ilikuwa yapata saa 6:45 usiku, ndio tuliondoka baada ya Beatrice kunifuata


katikati ya meza niliyokaa na Michael pamoja na rafiki zetu wengine, mara


baada ya sherehe kuisha na watu kadhaa kuondoka akiwemo mama yangu, baba


akiwa na wazazi wa Beatrice wakinywa kwa furaha.


"Tunachelewa baby, saa saba kasorobo sa' hivi"


Aliniambia huku akitazama saa kwenye simu yake. Nikawaaga rafiki zangu


kisha tukaenda kuwaaga wazazi waliozama katika vicheko. Nikamsindikiza


Beatrice mpaka nyumbani kwake Mikocheni ambapo alishaacha kuishi na wazazi


wake waliokuwa wakiishi Bunju.


kisha mimi nilirudi nyumbani kwangu kijichi.


....


http://deusdeditmahunda.blogspot.com/


Mlio wa kitufe kilichofyatuka kutoka katika birika la kuchemshia maji, ndio


ulinitoa katika mawazo hayo ya siku ya jana na kunirudisha tena chumbani


kwangu. Nikazima ukutani na kuyamwaga maji yale ya moto kwenye ndoo ya


kuogea, kisha nikabeba sabuni pamoja na mswaki niliouweka dawa nikaingia


bafuni nikiwa nimeshajaza maji mengine ya baridi ya kuyapooza yale ya moto.


Nilipomaliza kupiga mswaki baada ya kuvua taulo huku nikipiga mluzi


niliokuwa nikiimba wimbo fulani wa "Msondo Ngoma" nikakumbuka jambo. Jana


usiku nilipigiwa simu, na nani? Meseji pia? Atakuwa nani? Nilikumbuka


kutazama kweli? Si kwenda kuangalia mpaka nilipomaliza kuoga na dakika kumi


zilitosha kufanya hivyo.




Nikamaliza kuoga na kutoka bafuni huku nikijifuta maji kwa taulo.


Saa iliyopo juu ya meza ya chumbani kwangu ilionesha kuwa imetimu Saa 5:58


zilibaki dakika mbili itimie saa 6 mchana. Nikaiwasha simu yangu kuangalia


ni nani aliyekuwa akinipigia simu. Nikafungua sehemu ya simu ambazo


hazijapokelewa, alikuwa ni mpenzi wangu Beatrice. Nikaipiga simu yake,


haikupokelewa. Mara ya pili haikupokelewa, ya tatu vivyo hivyo.


Nikakumbuka kuwa jana usiku ilianza kuingia meseji kabla ya simu kupigwa,


nikaenda upande wa meseji, alikuwa ni Betrice pia. Nilipousoma ujumbe wake,


moyo ulinilipuka vuuup!! Kama taa ya kandili inayoanza kuishi mafuta yake,


nikaanza kuhisi joto kali licha ya upepo mkali wa feni ulioendelea kupuliza


ndani ya chumba changu.


Meseji hiyo iliandikwa "KWANINI UMENIUWA RAMON?"...


Nilijaribu tena kuipiga simu ya Beatrice lakini nilichojibiwa, kilikuwa ni


kile kile nilichoambiwa mara ya kwanza na sauti ya mwanamke wa huduma kwa


wateja "simu unayopiga haipokelewi, bonyeza..." Nikaikata na hapo nikahisi


naanza kuchanganyikiwa. Sikujua Beatrice alimaanisha nini mpaka aseme kuwa


ninamuuwa. Nikaamua nimpigie rafiki yangu Michael ambaye alimfahamu vizuri


Beatrice, Michael hakuwa akipatikana.


Nikaamua kwenda mwenyewe hadi Mikocheni anapoishi Beatrice.


Niliwasha gari yangu na kushusha kilima cha kijichi kisha nikaibukia kwa


buruda na kupita misheni nikaitafuta barabara ya kilwa road nije kuibukia


azikiwe niitafute barabara ya mwai kibaki baada ya mwendo wa speed kali


ulionichukua zaidi ya dakika 45 mpaka kukatisha katika mtaa anaoishi


Beatrice.


Nilisimamisha gari mara baada ya kufika getini kwake na kupiga honi nyingi,


lakini sikuona dalili za kufunguliwa. Nikaizima gari yangu na kushuka,


niseme ukweli kuwa nilikuwa n'na hasira kwa kuwa nilijua ni utani wa


Beatrice lakini wasiwasi ulinijia kila nilipowaza itakuwaje kama ni kweli


amepatwa na matatizo?


Nikaitazama kwa dakika kadhaa kamera ya ulinzi pale getini, lakini haikuwa


ikitazama tena getini kama nilivyozoea. kitu cha ajabu na kilichonitia


mashaka niliona kuwa ilinyofolewa kwa makusudi au bahati mbaya na mtu awaye


yeyote, lakini sikutambua. Nikaamua kugonga hodi mara kadhaa na kuona


kimya, nikaamua kulisukuma geti lile likafunguka bila ajizi. Mshangao


mwingine, haikuwa kawaida kwa Beatrice kuacha mlango wazi.


Nilipoingia ndani mara baada ya kuvuka geti lile, nyumba ilikuwa kimya huku


mlinzi Baraka akiwa hayupo eneo lake la lindo.


Nikapiga hatua chache mpaka kwenye nyumba kubwa ya Beatrice, moyo wangu


ukapiga pah! Ukutani mwa nyumba ya Beatrice karibu na ulipo mlango wa


kuingilia, niliona alama ya kiganja kilicholowa damu na kushika eneo hilo


la ukuta.


Miguu yangu ilianza kutetemeka na kuwa kama inayogongana huku kengele ya


hatari ikipiga kichwani mwangu. Ukweli ni kwamba sasa matumaini ya kumkuta


mpenzi wangu akiwa hai yalikuwa madogo kuliko nilivyokuwa nikitoka


nyumbani. Nilianza kuona ukweli wa meseji yake lakini wasiwasi ulisukuma


zaidi mapigo yangu ya moyo, kwanini aandike mimi ndiye ninayemuuwa? Ukimya


ule ulinitisha zaidi kuliko alama ya kiganja cha damu juu ya ukuta wa


nyumbani kwa Beatrice.


Nikaingia ndani ya nyumba hiyo, pale mlangoni nikalakiwa na mburuzo wa mtu


aliyekuwa akivuja damu kutoka mwanzo wa mlango mpaka katika moja ya mlango


wa kuingilia chumba ambacho Beatrice alifanya kama stoo.


Nilipofungua chumba hicho, nilichokikuta hakielezeki. Kichwa


kilitenganishwa na mwili wala kichwa chake hakikuonekana na hadi leo sijuhi


kiko wapi. Tumboni kulikuwa na shimo kubwa lililoacha sehemu kubwa ya


utumbo kutoka nje na kuleta picha iliyotisha zaidi.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/




"Baraka!!!" Niliita kwa hofu huku nikiziba sura yangu kwa uoga na machozi


yakanibubujika.


Nilijaribu kutaka kukimbia na kuingia chumbani kwa Beatrice huku nikimuita


Beatrice. Beatrice hakuitika bali nikapokelewa na utelezi ulionifanya


niisalimie sakafu na kuibusu ardhi ya chumbani kwa Beatrice na kunifanya


niilambe damu iliyoganda pembeni ya mwili ulio uchi huku macho yakinitazama


na mdomo kama unaonizomea wa mpenzi wangu Beatrice.


"Mamaa weee!!" Kwa wahka nilipiga kelele za kuchanganyikiwa, nilipomsogelea


Beatrice nikamsukasuka huku nikimuita "Beatrice, Beatrice amka mama. Nini


kimekukuta jamani Beatrice, amka mama"


Bisu kubwa lilizama tumboni kwake huku kwenye sehemu ya koromeo lake ikiwa


imekatwa hivyo kuweka kama mfereji fulani uliotisha kuutazama. Nilikuwa


nikitazama mwili wa Beatrice na si Beatrice mwanamke niliyekuwa naye jana


usiku.


Nikiwa katika kulia huko? Nikasikia mchakato wa nyayo za mtu zikitembea


kuja ndani ya nyumba ya Beatrice.


"Wauwaji!!"


Akili yangu ikaninong'oneza. Nilinyanyuka upesi kuelekea sebuleni,


nikajificha nyuma ya kochi ili niweze kuwaona waliokuwa wakiingia. Tulikuwa


tumepishana sekunde chache kwani mara baada ya kuzama nyuma ya kochi lile,


wale waliokuwa wakija wakawa wamesimama eneo la stoo karibu na kochi


nililojificha mimi. Nilipoinua kichwa changu kuchungulia ni watu wa aina


gani? Nikawa nimefanya kosa, walikuwa ni askari sita, wa kike wakiwa wawili


kila mmoja akiwa amevaa gloves wanne wakiwa na silaha mikononi mwao huku


wawili wakiwa hawajavaa nguo za kipolisi bali mikononi walibeba simu za


upepo.


"Muuwaji!" Alikuwa ni askari mmoja mweusi wa kiume, aliyeshika bastola yake


ndogo kiukakamavu akaropoka huku akinielekezea silaha ile. Mwingine


akaropoka kwa sauti yake thabiti.


"Mikono juu ya kichwa usijiguse popote ukikiuka maagizo haya tunakutoa


ubongo. Usijaribu kufanya ujanja wowote" Ilikuwa ni sauti isiyo na mzaha


hata kidogo


Niliogopa sana kuoneshwa mdomo wa bastola kama mtu mwenye makosa. Ila


kukutwa ndani ya nyumba yalipofanyika mauaji, hakika sikuwa na ujanja.


"Mimi sihusiki!?"


Nilijaribu kujitetea kwa sauti ya kitetemeshi lakini haikusaidia. Mmoja wa


askari wale akaangua kicheko cha fedheha na kunitazama katikati ya miguu


yangu. Nikaushusha uso wangu pia kutazama kilichomfanya askari yule


kucheka, nikaishusha mikono yangu haraka kuiziba sehemu ile. Kumbe ile hali


ya ubaridi uliokuwa ukipenya katikati ya miguu yangu ni mikojo


iliyonichuruzika kutokana na uoga.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/


"Mikono juu, pumbavu" askari yule aliyekuwa akicheka akabadilika ghafla na


uso wake ukawa ule wa kuudhi. Mmoja kati yao akawa amenisogelea na


kunifunga pingu kwa nyuma katika mikono yangu. Kisha nikatolewa ndani ya


nyumba ile na kuwekwa katika gari ya polisi kwa mateke huku nikiwa


nimekwidwa kwa nyuma kwa style ya tanganyika jerk(suruali kukamatwa kwa


nyuma ya makalio na kufanya miguu kuelea juu juu) kisha walikaa ndani huku


nikiachwa na askari wengine watatu wenye bunduki aina ya Ak-47 wakinilinda


zaidi ya dakika 40.


Nikiwa nimefungwa pingu zile huku nikitazama askari waliokuwa wakinilinda


huku wale wengine wakitoka na kuingia ndani ya nyumba ya Beatrice na


mwingine akipiga piga picha kiganja kile ukutani na mburuzo ule mimi nikawa


najiuliza. Nilianza kujiuliza meseji niliyoipokea kutoka kwa Beatrice


"kwanini unaniuwa Ramon?" Kisha nakuta maiti mbili katika nyumba yake!


Inawezekana Baraka ndiye aliyemuua? Sasa kwanini aseme mimi ninamuuwa?


Ilianza meseji kisha ikafuata simu, inamaana aliyekuwa akinipigia simu ni


Beatrice au aliyemuuwa? Kwanza aliyemuuwa ni nani? Na hawa polisi, nani


amewataarifu mapema hivi kuwa ndani kuna mauaji yametokea? Hiki ni


kitendawili na huu ni mtihani wa aina yake niliokutana nao. Kwa sababu kama


nitadhani ni Baraka ndiye alimuua Beatrice na je yeye ni nani alimuua? Na


mbwa wako wapi?


Baada ya askari wale kutoka ndani ya nyumba ya Beatrice walinifunga


kitambaa cheusi machoni pangu na hivyo sikuweza kuona chochote mbele yangu.


Wakawasha gari na msafara wa kwenda kusikojulikana ukaanza. Akili yangu


ikawa na hopfu na kule ninakopelekwa. Sasa kama ni askari na ninapelekwa


mahabusu kwanini nizibwe na kitambaa cheusi? Nikaogopa zaidi.


Ulikuwa ni umbali mrefu ambao siwezi kukadiria tulitumia dakika ngapi au


kilometa ngapi mpaka kufika katika jumba hili kubwa lenye giza nene.


Nilitolewa ndani ya gari na kufunguliwa kitambaa na kisha taa zikawashwa,


kumbe tulikuwa tumeingia gereji nikapitishwa katika mlango mdogo wa


kuingilia katika nyumba hiyo. Ilikuwa ni nyumba kubwa sana, nyumba ambayo


haikuonesha dalili ya kuwa ni makazi ya mtu labda ni ofisi fulani. Kama ni


ofisi, kwanini niletwe ofisini na sio nipelekwe mahabusu nizijuazo?


Nikapelekwa katika chumba fulani kidogo chenye meza fulani ndogo na viti


viwili vikitazamana. Nikawekwa katika kiti kimoja huku taa yenye mwanga


mkali ikining'inia. Nikatolewa zile pingu kisha nikaachwa peke yangu.


Nilikitazama kile chumba kile pemnbe na kuziona kamera nne katika kila


pembe ya ukuta. Mbele yangu kulikuwa na kioo kipana ambacho hakikuwa na


tofauti na vile ambavyo huwa naviona kwenye picha za wazungu katika vyumba


vya mahojiano kama hiki.


Sikujua kuna siku na mimi nitakuwa katika mazingira kama haya.


Nilikaa kwa dakika kumi na tano mpaka mlango ulipofunguliwa na kuingia


kijana mrefu mwenye mwili uliokomaa kimazoezi na misuli iliyojazia. Alikuwa


ana kipara kichwani mwake na sauti nadhifu iliyombana.


"Habari yako Ramon?" Alinisalimu mtu yule. Nikajiuliza amenijuaje?


"Salama tu!" Sauti yangu ilitoka kwa shida kutokana na hofu ya hapo nilipo.


Kwanza nilianza kuhisi huenda wauaji waliomuua mpenzi wangu ndio


walionichezea mchezo huu na kujifanya wao ni askari. Sikujua ilikuwaje


walifahamu ndani ya nyumba ile kumetokea mauaji na iweje waje dakika chache


tu mara baada ya mimi kwenda katika nyumba ile na vipi huyu sasa anitaje


jina langu? Nini hiki kinaendelea?http://deusdeditmahunda.blogspot.com/


"Unavuta sigara?"


Nilimuona yule mtu ambaye bado hakuwa amejitambulisha kwangu, akitoa kasha


la sigara aina ya embassy na kuiwasha moja ya kwake baada ya kuitupia


mdomoni. Aliivuta mikupuo miwili mimi nilipokataa kisha akarudisha kete ya


maongezi mezani.


"Naitwa Jafari Hiza ningependa unifahamu hivyo kwa sasa mpaka hapo baadaye"


akanyamaza kwa tuo, kisha akavuta mkupuo mwingine wa sigara na moshi wake


ukaelea angani kisha akaizima sigara ile. "Nakufahamu wewe ni Ramon na ni


mpenzi wake Beatrice, Sivyo?"


"Ndivyo, Lakini..."


Alininyooshea kiganja chake kilichokomaa na kuinamisha uso wake kama kwamba


hakutaka kunisikiliza nilichotaka kuzungumza.


"Sihitaji uongee kitu ambacho sijakuuliza" alinyamaza kwa muda kama


anayetafakari jambo, kisha akaendelea. "Umefanya kosa kubwa sana mdogo


wangu. Kumuuwa mtoto wa kigogo wa umoja wa mataifa? Unajiamini nini?"


"Mimi...?"


Akanikatisha tena


"Mimi sijauuwa!" nikajitetea bila matumaini


"mimi sijamuuwa" Akaniigiza kwa kubana pua kisha akacheka kwa kebehi. "Na


ile meseji aliyokutumia kuwa kwanini unamuuwa, aliituma saa ngapi? Ulimuuwa


na kuondoka zako kisha wakati anakata roho ndio akapata nafasi ya kukuuliza


swali lililotia simanzi kiasi kile au meseji ile alikutumia wakati gani?"








"Mimi sijauuwa"


"Hujauwa? Jana usiku wa manane haukuwa naye? Mlisimama getini ukiwa na gari


yako aina ya Funcargo ukiwa umevaa shati nyeusi ya polo iliyokubana? Labda


nikuulize, ulirudi saa ngapi tena kufanya mauaji yale?"


Nikapatwa na ubaridi wa unyevunyevu fulani wa uchungu ulionitiririsha


machozi kama chemchem kutoka juu ya maporomoko na kwenda chini ya ardhi.


Nikalia sana kwa kuwa sifahamu chochote kuhusu mauaji ya Beatrice lakini


kila anachozungumza kilikuwa ni kweli na kuweza kunitia hatiani katika


mauaji hayo. Nilimuona akisimama na kuweka cd kwenye deki na kuiwasha tv


iliyopo pembeni yetu. Nikatumbua macho kushuhudia nini alikuwa anaenda


kunionesha.


Cd iliyowekwa ilikuwa ikionesha giza, lakini kwa msaada kidogo wa taa


niliweza kujiona mimi pamoja na Beatrice. Wajihi alioutaja huyu mtu


aliyejitambulisha kwangu kama Jafary Hiza ndio ule niliouona kwenye cd ile.


Hapo nikagundua kuwa waliitazama kwanza kabla hawajanihoji chochote.


Nikajiuliza sana hawa ni watu gani? Kwanini nisipelekwe polisi basi kama


n'natuhumiwa kwa mauaji na niletwe katika chumba hiki ? Hakika niliumia


sana nafsi. Jafary Hiza alinitazama na kuniambia


"Nimekuonesha cd hii kukuambia kuwa vithibitisho vyote vya wewe kuwa umeuwa


tunavyo sasa sielewi utakataa nini? Na pia labda nikuulize swali"


akanyamaza kiasi kisha akaendelea "hivi nyinyi vijana kwanini unapomchoka


mwenzio unamfanyia jambo la kinyama kiasi kile? Na yule mlinzi wa watu


amekukosea nini? Ndio kupoteza ushahidi? Wale mbwa uliowapa sumu je! Ndio


walianza au ni Baraka alianza kufa? Kwanini umeamua kufanya mauaji ya


kutisha kiasi hiki Ramon?"


Nikanyanyua mdomo wangu kwa mshangao wa ajabu baada ya kusikia kuwa mbwa


wale waliokuwa wakimlinda Beatrice kuwa wameuwawa kwa sumu "Mimi sihusiki


na mauaji hayo Jafary sihusiki chochote na sifahamu chochote kuhusu mauaji


hayo"http://deusdeditmahunda.blogspot.com/


Kabla Jafary Hiza hajazungumza alichotaka kuzungumza, kuna sauti ilitoka


kutoka katika chombo fulani pale mezani.


"Namba 3 kuna mwanasheria anahitaji kuzungumza na mtuhumiwa"


Jafary Hiza akajibu "Sawa nimekuelewa namba 1 mfungulie mlango niwaache


wazungumze"


Kisha niliuona mlango ambao aliingilia Jafary Hiza ukifunguka na kuingia


mwanamke mmoja mrembo sana. Kiukweli mwanamke yule alikuwa ni mrembo


kuanzia alivyovaa hata sura pamoja na umbo lake. Alivaa suruali ya kitambaa


iliyonyooshwa vyema na kutiwa upanga mkali kisha na koti lake la kitambaa


kinachofanana na suruali ile aina ya linen ya kahawia, usoni akiwa


amebandika miwani nyeupe. Hata mwendo wake mwanamke huyu, ulikuwa ni ule wa


kujitupa tupa kama wa walimbwende waoneshao mavazi au kugombania taji la


umisi.



ITAENDELEA 

Tags

Post a Comment

0 Comments
Post a Comment (0)

Made with Love by

Pixy Newspaper 11 Template is Designed Theme for Giving Enhanced look Various Features are availabl…
To Top