Simulizi : Nenda Na Moyo Wangu Sehemu Ya Pili (2)

ADMIN
0




Aliponyanyuka Jafary Hiza, ndipo na yule mwanamke aliifikia meza tuliyokaa


na nikauona mshangao wa Jafary Hiza aliomtazama mwanamke yule kuanzia chini


mpaka juu naamini pia alivutiwa naye. Mwanamke yule akatabasamu hapo


akazidi kuvutia kutokana na lile tabasamu lake muruwa. Akasalimiana na


Jafary Hiza kisha akajitambulisha kwake.


"Naitwa Vanessa Noel" Huku tabasamu likiwa pana usoni mwake.


"Naitwa Jafary Hiza"


Kisha Jafary Hiza akamruhusu akae na yeye akaondoka. Vanessa alinitazama


kwa makini kwa sekubnde zisipongua dakika 10 kisha akaivua miwani yake


akazungumza nami.


"Siamini kama unaweza kumuuwa mpenzi wako" akatoa karatasi kadhaa na


kuziweka mezani kisha akatoa tepurekoda akaiweka pia mezani na kuongea tena


"kwanza kwanini umuuwe mwanamke uliyempenda? Pia ulikuwa hufahamu ukimuuwa


utaingia katika matatizo makubwa na mheshimiwa Oscer Valerian?" Hilo


lilikuwa ni jina la baba yake Beatrice ambaye alikuwa naibu katibu mkuu wa


umoja wa mataifa.


"Dada yangu hata nikikueleza vipi huweza kuamini ninachozungumza lakini


sina ukweli mwingine ninaoweza kukuambia zaidi ya kwamba sijamuuwa


Beatrice"


Akafanya kitu cha dharau sana na sijapenda na pia nilichukia ila kwa kuwa


nilikuwa mtuhumiwa, basi sikutaka kufanya fujo yeyote. Kisha akaniambia




"Naitwa Vanessa Noel nakufahamu unaitwa Ramon Lameck, mimi ni mpelelezi wa


kesi hii kwa upande wa mlalamikaji na ni mpelelezi binafsi. Mlalamikaji


ambaye ni mteja wangu amenilipa pesa nyingi sana za kung'amua kitendawili


hiki. Hataki tu kukufunga pia anataka kujua sababu ya wewe kumuua mtoto


wake. Hivyo mbali ya kuwa mpelelezi wa kesi nimesimama hapa kama


mwanasheria wako ambaye nitakutetea kutokana na vifungu vya sheria


vitakavyoniruhusu kufanya hivyo na ukweli utakaonieleza"http://deusdeditmahunda.blogspot.com/


Nikahisi ni mtego. Mpelelezi wa kesi ya mauaji aliyemtuma ni Mlalamikaji na


hapo hapo ananieleza kuwa yeye ameletwa na mlalamikaji ili anitetee!!


Nikamuuliza Mungu, Ulinikutanisha na Beatrice ili maisha yangu yaishie


hapa? Kwanini kile nilichokiota na kutamani kukifanya katika maisha yangu


kinayeyuka kama mshumaa? Chozi likanidondoka kisha nikameza donge zito la


mate. Nikiwa katika kulia, Vanessa Noel akaipiga meza ile ya bati na


kuniambia.


"Huna sababu ya kulia sasa nitakuuliza mambo kadhaa na ninaomba unieleze


kile nitakachokuuliza"


Nikatingisha kichwa kwa kukubali, akaiwasha tepurekoda yake akaanza kuongea


huku akiwa amebonyeza kitufe cha kuruhusu sauti zetu kuingia katika kifaa


kile kwa ajili ya kumbukumbu.


Vanessa Noel akaniuliza swali la msingi ambalo sikutarajia kuulizwa katika


mazingira kama hayo. Akaniuliza kama nimeshakula tangu nikamatwe? nikamjibu


kuwa si tangu nikamatwe tu majira ya saa sita, yaani tangu asubuhi mpaka


sasa saa 9:38 alasiri(kulingana na saa iuliyopachikwa juu ya ukuta mbele


yangu ilivyokuwa ikisema) sijapata muda wa japo kunywa maji.


Vanessa alisikitika sana nilipomueleza hivyo, kisha akazima ile tepurekoda


na kubonyeza kitufe kile chekunde kwenye meza na kuzungumza na mtu wa


upande wa pili.


"Nahitaji chakula kwa ajili ya mteja wangu"


"Dakika chache" sauti ile nzito ikajibu.


Dakika chache baadaye, kweli lango lile likafunguliwa na toroli


lililosheheni hotpot tatu za vyakula na jagi kubwa la kuvunjika lililobeba


maji ya matunda, lilikuwa likisukumwa na askari wa kike mrembo .


Hotpot zikafunguliwa, Vanessa akaitwaa sahani yake na glass ya kujimiminia


maji yale ya matunda ya embe na pansion, kisha akachota tambi akachanganya


na nyama roast pamoja na zile za kukaangwa wa kuku. Nikapata nafasi ya


kumuuliza Vanessa baada ya kila mmoja akiwa anashughulika katika kung'ata


minofu ile.


"Hapa ni wapi? Na kwanini nimeletwa hapa na si mahabusu kama


nilivyotarajia?"


"Hapa panaitwa Safe house watu kama wewe huletwa sehemu kama hii kutokana


na makosa yenu mliyoyatenda. Kama unamkumbuka yule kijana aliyemuua Mtoto


wa Raisi Baraka katika ule mkasa ulioibua hadithi iliyouza nakala nyingi ya


kitabu kilichoitwa NISAMEHE MWANANGU, aliletwa hapa kabla hajapelekwa


Mwanza kwa ajili ya hukumu. Hata yule aliyemuua Waziri mkuu Peter Chongola,


katika mkasa uliandikwa na mwandishi mashuhuri mwenye njaa stallone na


kuita TAKSI YA KIJIVU(MUUWAJI ANAYETAFUTWA), yeye pia aliletwa hapa. Hivyo


na wewe uliyemuua mtoto wa kigogo wa Un umelazimika kuletwa hapa kwa ajili


ya mahojiano kabla ya kesi yako kunguruma"


Hapo nikawa nimemuelewa sana Vanessa kisha tulipomaliza kula alikuja askari


yule yule akatoa vyombo tulivyolia mazungumza yakaendelea.


"Anafanana na Beatrice kwa mbali?" Vanessa akanitoa katika mawazo ya


kumtazama askari yule akaniuliza kiuchokozi. Mimi sikumjibu, bali nilicheka


kiasi na kumtazama Vanessa.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/


Vanessa ni mwanamke mrembo sana niliyewahi kukutana naye katika maisha


yangu. kwa ufupi si rahisi kumuelezea Vanessa nikamaliza. Vanessa akawa


anaweka kifaa kile cha kurekodia sawa na akaniuliza swali.


"Nataka nianze kufahamu mlikutana wapi na Beatrice"




Nikaanza kusimulia tangu siku ya kwanza nilipopelekwa na baba chuoni pale-:




CHUONI UDOM




kilikuwa ni kipindi cha kipupwe na baridi kali ilivuma kiasi cha kila


mwanafunzi pale chuoni alikuwa amevaa sweta la kumkinga na baridi. Mimi


nikiwa mtoto wa pekee katika famili yetu, baba yangu mzee Lameck alikuwa na


furaha sana kwa kuwa sikumuangusha tangu nilipomaliza kidato cha nne,


nikapata alama nzuri za kuniwezesha kuchaguliwa na serikali kwenda shule ya


Tambaza kisha baada ya hapo ndipo nikachaguliwa kwenda Udom.


Naweza kusema kuwa baba yangu ni rafiki yangu wa karibu sana katika maisha


yangu. Alifurahia mafanikio yangu na kuhuzunika kwa shida zangu hakika


najivunia sana kuwa na baba kama yeye. Siku hiyo ya kwanza akaniacha niende


kuripoti ofisini na kupewa chumba changu akaniambia kuwa


"Soma kwa bidii sana mwanangu, wewe ni mtoto wa kiume wa kike ataolewa wewe


utaowa hakikisha unaposoma ukitazama daftari unamuona mke na watoto wako


pale" akawasha gari na kuondoka.


Mimi nilienda kwa Den of student kisha akanikabidhi kwa warden ambaye


atanipa ufunguo wa chumba changu pale hostel za chuo. Nikakaa katika hostel


za watu wa social huku mimi nikiwa nasomea Public administration. Huko


nikakutana na vijana wawili Steven Ngonyani pamoja na Michael Stambuli.


Hapo ndipo nilianza kumfahamu Beatrice.


Tukiwa tumetoka dinner na wale vijana wenzangu yaani steve na michael,


tulienda katika Carteen ambayo Michael alituelekeza kwa kuwa yeye alikuwa


ni mwenyeji pale chuoni kabla yetu. Huyu Michael alikuwa mwaka wa pili huku


mimi na Steve tukiwa mwaka wa kwanza steve akiwa amenitangulia wiki moja


kabla mimi sijawasili pale chuoni.


"Huku kuna watoto balaa" Michael akaendelee kutudokeza kama alivyoanza


kutushawishi mpaka tukaja katika mgahawa huu. "Nyinyi rukeni kote ila kuna


mtoto anaitwa Beatrice huyo niachieni, chombo changu hicho"


Nikapatwa na hamu sana ya kumuona huyo Beatrice ambaye Michael alikuwa


haachi kumtaja. Niliagiza wali samaki huku wenzangu wakila ugali na samaki


mkavu. Ghafla Michael akatushitua wote tutazame kule alipokuwa akitazama


yeye.


Alipokuwa akitazama Michael, kulikuwa na wasichana watatu waliokuwa


wakiingia pale katika ule mgahawa tulipo sisi. Kutokana na mgahawa ule kuwa


mrefu sana, japo walikuwa mbali niliweza kuuona urembo wao sawia.


Mmoja alikuwa chotara bila shaka, kutokana na nywele zake za singa zilizo


ndefu kiasi zilifika mgongoni zilipeperuka peperuka; alikuwa akicheka na


mmoja aliye kuwa upande wake wa kushoto huyu alikuwa mweusi wa kawaida


mwenye shepu ya kibantu kwa mbali nilifanikiwa kuuona mwanya wake yeye


alivaa sketi fupi hivyo miguu yake minene niliweza kuiona kwa ukaribu


zaidi. Msichana huyo mwingine ndiye ambaye Michael alitaka tumuone bila


shaka. Maana alipoona tu tumegeuka, akaropoka kama aliyewehuka.


"Huyo anakuja, huyo hapo anayeongea na simu"


Kwa mara ya kwanza nikawa nimemuona Beatrice, ilikuwa ni siku ya kwanza ya


mimi kuingia hapo chuoni na ndiyo siku ya kwanza kukutana na Beatrice.


Itachukua kitabu kizima endapo nikitaka kuelezea uzuri wa msichana huyu.


Niliacha kula nikimtazama. Alikuwa ni mrembo kweli, mrembo haswa. Sasa


nikagundua kilichokua kikimchanganya Michael.


Kwa ufupi tu ni kwamba Beatrice alivaa sketi kama yule mbantu, yeye hakuwa


mweusi wala mweupe rangi yake wala haikuwa maji ya kunde, ila alikuwa


anaukaribia weupe. Siwezi kuelezea kwa ufasaha rangi hiyo ukanielewa. Sura


yake ilikuwa ya mviringo lakini alikuwa ana asili ya nywele kwa sababu


alijaa vinyweleo juu ya ngozi yake kiasi cha kunivutia zaidi kwa kuwa mimi


ni mmoja kati ya wanaopenda aina ile ya ngozi. Vinyweleo laini vilivyolala


juu ya ngozi. Kifuani alikuwa amebeba embe sindano ambazo ziliendelea


kusimama wala hazikutaka kulala hivi karibuni. Kiuno kilikatika kikike huku


hipsi zikijichora sambamba na makalio yaliyovimba na kuinua sketi ile na


kuifanya iwe ndogo zaidi. Alikuwa akiongea na simu mpaka alipovuta kiti


akakaa na mara nikashituka nikishikwa.


"Hoya brother, ndio ushachanganyikiwa?" Alikuwa ni Michael huku Steven


akinicheka "Haya ulikuwa ukimtazama nani? Yule Alisia, Prisca ama Beatrice?"


"Duh! Kaka! Mtoto Beatrice namba nyingine" nikaishia hapo nikachota kijiko


cha wali nikakitupia mdomoni, nikavuta mrija wa juisi nikautia mdomoni


nikawa nanyonya juisi taratibu nikimtazama Michael.


Chuki!! Nikaiona hasira katika uso wa Michael iliyozaa chuki. Ndita


zikaharibu paji lake la uso kisha akasonya na kufinya kidogo macho yake


kama atiaye mkazo kwa jambo alilotaka kuzungumza, hakuongea bali midomo


iliishia hewani akatupa kidole chake cha shahada kama akinionya jambo.


Steve akawa anatazama hali hiyo kwa mshangao sanjari na ilivyokuwa kwangu.


Sikuwa na shaka kwa kuwa moyoni mwangu sikumaanisha kumpenda Beatrice kwa


wakati ule ila kama ujuavyoa wavulana tumuonapo mwanamke mzuri lazima nafsi


zetu ziwake tamaa. Wao waliumbwa kwa ajili yetu.


Tuliendelea kula huku mimi nikiibia ibia kutupa jicho katika meza ya sita


aliyokaa Beatrice na wenzake. Mara ya kwanza, ya pili na ile ya tatu


niligongana macho kwa maho na Beatrice halafu kama waliyekuwa wakiniteta na


yule chotara ambaye baadaye nilikuja kufahamu kuwa ndiye Alisia. Sikujua


walichozungumza lakini walikuwa wakitazama meza yetu. Nikazuga kumtazama


Michael nikamkuta yeye akiachia tabasamu pana huku akiwapungia mkono


akiwasalimia. Nilitamani kucheka ila nilijizuia kwa kujifanya nakunywa


juisi.


Nikanyanyuka kwenda kunawa mikono kwenye ndoo itiririshayo maji kama


bombani, ghafla nikagongana na mtu, mtu yule hakuwa mwingine bali ni


Beatrice. Akanimwagia juisi iliyobaki kidogo kwenye glass yake na kuchafua


shati langu nililovaa.




http://deusdeditmahunda.blogspot.com/


MAHOJIANO NA VANESSA SAFE HOUSE


Kabla sijamaliza kueleza kila kilichokuwa kikiendelea, Vanessa


akanikatisha.




"Sasa ni saa 11 jioni naomba tuishie hapa kwa leo kesho tena nitakuja


kukutembelea ili niweze kujua kilichoendelea. Naomba usiache hata moja


unalolijua niweze kujua jinsi ya kukusaidia"


"Sawa" nikamkubalia, kisha tukaagana na Vanessa.


Vanessa alipoondoka askari wawili waliingia katika kile chumba na mnyororo


fulani uliunganisha pingu za miguu na mikono ambao nilifungwa mimi kisha


nikavalishwa kitambaa cheusi mfano wa kofia ya mzula kisha nikatemnbezwa


taratibu kutoka katika chumba kile.


Nilipokuja kuvuliwa kile kitambaa, nilikuwa ndani ya selo ya peke yangu


lakini ni chumba chenye hadhi ya kulaliwa na mtu mzito. Chumba hicho


kilikuwa na hewa ya pekee na utofauti wa chumba hiki hakikuwa na dirisha


wala mlango.


Hapana! Sasa mimi nilipita wapi? Sikushuka ngazi wala kupanda ila kuna


mlango ulifunguliwa, uko wapi sasa? Mauzauza!!!


Nilijaribu kugusa kuta za pande zote nne za chumba kile baada ya kufanikiwa


kufunguliwa kile kitambaa cheusi, sikufanikiwa kuona chochote kinachofanana


na mlango. Hapo nikakumbuka kile chumba nilichowahi kukiona katika


tamthilia moja pendwa inayoitwa 'The legend of the seeker' sasa nikajiona


mimi nikiwa ni muhanga mmoja wapo kama wale wasichana wawili ndani ya


tamthilia ile.


Nilijaribu kupiga kelele lakini chumba kile kikameza sauti yangu hata


mwangwi haukurudi kama nilivyotaraji. Niligusa hapa na pale sikufanikiwa


kupata chochote ninachokitafuta. Nikaamua kukaa pembeni mwa kitanda kipana


chenye godoro zito pana kutoka chini kwenda juu na kulia kwenda kushoto


lenye mashuka meupe pee! Kisha usingizi ukanipitia. Nikiwa hapo hapo bila


kujitambua.


Niliamka mara baada ya kuamshwa na askari wa kike ambaye alibeba sahani ya


chakula pamoja na glass ya juisi. akaniambia


"Kesho kuna ndugu zako watakuja kukuona"


Nikamshika mkono, nikamuuliza mara alipotaka kuondoka.


"Mlango wa hiki chumba uko wapi? Kwanini nipo hapa na si mahabusu yeyote


chafu kama wafanyiwavyo wavunjaji wa sheria kama mimi?"


Msichana yule alitabasamu kisha akauputa mkono wangu na kunieleza.


"Hapa ni Safe house, wewe ni mtu katili sana na inabidi ulindwe kwa


uangalifu sana kabla hatujajua chanzo cha wewe kufanya mauaji yale.


Unalindwa kwa kuwa inaaminika kama umeweza kumuuwa mwanamke ambaye usiku


uliopita uliweza kudanganya wazazi wake kwa kumvisha pete ya uchumba na


mbele za watu wengi ukakiri unampenda yeye tu huku ukitabasamu kinafki, je


tutajuaje kama umetumwa kumuangamiza mheshimiwa Oscer? Nimekusaidia


kukueleza siri nyingi ila sijilaumu kwa kuwa huoneshi kuwa katili kama


inavyotangazwa huko nje" akatoa gazeti na kunitupia katika mapaja yangu


"Nilipoitazama sura yako katika gazeti hili, sikukubaliana na kichwa hicho


cha habari"


Mara, mara!! Nini hiki? Nasinzia jamani, mara nikalala wala sikumuona yule


askari wa kike wakati anatoka.


Nilipokuja kuamka nililikuta gazeti lile pale pale mapajani mwangu pembeni


kukiwa na sinia la chakula. Nilitazama huku na kule sikumuona yule mwanamke


wala sikuona chochote kilichobadilika katika kuta zile. Nilipotazama katika


sinia lile la chakula, sikukitamani chakula kwanza kabla sijasoma


kilichoandikwa katika gazeti hilo.




"MUUWAJI WA MTOTO WA KIGOGO WA UMOJA WA MATAIFA AKAMATWA NDANI YA NYUMBA YA


MAREHEMU"http://deusdeditmahunda.blogspot.com/


Kisha picha kubwa ikinionesha nikiwa ndani ya nyumba ya mpenzi wangu


Beatrice. Picha hiyo alinipiga yule askari ambaye hakuvaa sare za kipolisi


kisha akanicheka mara nilipokuwa nimejikojolea. Niliitazama picha ile kwa


uchungu na kuisoma habari ile kwa hasira kisha nikameza donge zito la mate


lililonikaba kwa uchungu. Nikakunja kunja lile gazeti na kulitupa kisha


nikapiga kelele za maumivu kutokea ndani ya moyo wangu kutokana na kesi


hiyo mbaya ya kusingiziwa.


Nikalipiga teke sinia lile la chakula nikapiga magoti kwenye kitanda changu


cha kulalia kisha nikalia kwa uchungu. Hakika hakuna kipindi kigumu


nilichokuwa nikipitia zaidi ya hiki katika maisha yangu. Wakati nikiwa


nimejiinamia pale, askari watatu wakaingia.


"Wewe muuwaji! Una nini?"


Ilikuwa ni sauti ya askari mmoja mnene mrefu kiasi, kidevu chake kilikuwa


chakavu kutokana na ndevu na mapele yake yaliyokomaa. Nilipoinuka na


kumtazama ila sikumjibu kitu.


"Mtoeni humu labda hapendi Ac mpelekeni mahabusu za kawaida kule napo kuna


ulinzi mkali"


Wale askari wawili ambao walisimama pembeni yangu wakanibeba msobemsobe kwa


kunishika makwapani kwangu huku mimi nisisimame, hivyo walikuwa


wakiniburuza. Hapo nikawa nimeuona mlango ulivyokuwa wazi na jinsi ya


kuufungua na kuufunga ilinishangaza teknolojia ya namna hii. Sikutegemea


kama hapa hapa Tanzania nilipoishi zaidi ya miaka 26 kungekuwa na sehemu ya


namna hii.


Nikaburuzwa mpaka katika sehemu yenye selo nyingi ambazo zilikuwa tupu na


kutupwa katika moja ya mahabusu hizo bila huruma, kisha wakaniacha hapo


bila kusema lolote. Baada ya dakika chache baadaye, alikuja yule askari wa


kike aliyeniletea chakula mwanzo akaniambia.


"Nimekuletea chakula ule ukikimwaga na hiki shauri yako sintakuonea huruma


tena"


Uso wake haukuwa na mzaha, akakisukumiza kile kibakuli kilichojaa wali,


paja la kuku na ndizi mbivu kwa mguu wake kisha yeye akaondoka.


Nilikula kile chakula mpaka nilipomaliza kisha nikaenda kujitupa katika


kitanda kidogo kipatacho futi 4 kwa 6 cha chuma, nikasinzia.


Ilikuwa asubuhi, alikuja yule askari wa kike na kuniamsha kwa kirungu.


"Wewe, wewe!!"


Nikaamka.


"Embu njoo! Una mgeni wako"


Niliamka haraka haraka kwenda kukutana na mgeni huyo. Sikujua ni nani,


lakini nilitamani sana kukutana na ninayemfahamu ili niweze kupata faraja


ya moyo japo kujua ni vipi watu wanachukulia kesi yangu. Yule askari


akanifunga pingu mikono yangu kwa nyuma kisha akaniongoza mpaka ilipo


sebule ya nyumba ile.


Hapo mwanzo sikuweza kufahamu kabisa kama nilikuwa ndani ya nyumba ya


kifahari namna hii. Samani za gharama zilisheni katika sebule ile. Kila


kona kulikuwa na vitu vya thamani sana. Sikuvalishwa tena kile kitambaa


cheusi ila ulinzi wa kuvalishwa pingu mfano wa minyororo haukukoma.


Nilipotokeza nikiwa katika mshangao wa nyumba ile, niliweza kuwaona walinzi


lukuki wakitembea tembea huko nje na nilipoyatupa macho yangu kwenye


makochi ya pale ukumbini, mgeni aliyekuwa akinisubiri ni Michael rafiki


yangu. Yule askari akazungumza


"Dakika mlizopewa ni 30 tu za kuzungumza"


Nikatazama ukutani kulipokuwa na saa ilikuwa ni saa 3:14 asubuhi siku ya


pili tangu Beatrice auwawe. Nasema auwawe kwa kuwa si mimi muhusika wa


mauaji hayo licha ya kuwa kila mtu anaamini ni mimi ndiye niliyeua.


Nikamtazama Michael nikiwa na furaha lakini Michael alionesha wasiwasi mara


aliponiona. Wasi wasi ule wa Michael ukanitisha sana. Hakuzungumza wala


mimi sikuzungumza kama kwa sekunde kumi hivi, kisha akaniuliza.


"Ramon" kama aliyekuwa akiniita lakini hakumaanisha kuniita, akaendelea


"Umekuaje rafiki yangu?"


Sikujibu haraka, nilimtazama Michael moja kwa moja katika macho yake kama


niliyekuwa nikimsoma jambo kisha nikamuuliza "Michael wewe una amini


nimeua?"http://deusdeditmahunda.blogspot.com/


"Unadhani mimi nitaamini vipi Ramon?" Alinijibu huku akiitupa mikono yake


miwili hewani na uso wake ukiwa katika hali ya msisitizo.


Hapana! Kuna kitu nakiona katika macho ya Michael si kizuri. Kwanini


Michael anayenifahamu mimi kwa miaka 4 zaidi leo anaamini mimi nimeua? Mimi


nina sura ya kuua? Michael anaigiza na kuna kitu anafahamu. Nikapatwa na


wasiwasi na Michael juu ya kifo cha Beatrice.


"Kiukweli habari hizi zimenishangaza sana Ramon. Sikutegemea mtu kama wewe


unaweza kufanya jambo la kikatili namna ile"


Sikumjibu kitu ila kuna kitu kikawa kimenikaba ndani ya koo yangu na


machozi yakinilenga kwa uchungu.


"Sina cha kukusaidia au kukushauri katika hili kwa kuwa unafahamu fika mzee


Oscer(baba yake Beatrice) ana nyadhifa gani hapa Tanzania. Cha ajabu na


kinachonishangaza wakati umeua na bado ukaendelea kubaki eneo la tukio.


Ramon pombe ulizokunywa, pombe mbaya rafiki yangu nilikuwa nikikuambia kila


siku"


"Unasema nini wewe Michael? Kwanini unanituhumu moja kwa moja bila kuwa na


uhakika Michael? Mimi wa kuuwa?" Uvumilivu ukanishinda sasa nikawa naropoka


kwa hasira huku sauti yangu ikipaa juu hata niipoinyanyuka ikaongezeka


zaidi "nakuuliza, mimi naonekana muuwaji kwako leo? Au kwa kuwa msichana


yule ulikuwa unampenda? Ina maana nilidhani huna chuki tena nami kumbe


ulikuwa mnafki? Michael.." Nikamuinamia mpaka ulipo uso wake na kunyoosha


kidole katika kifua changu nikamwambiwa kwa dhati na hisia kali kwa sauti


ya chini "Mimi sijamuuwa Beatrice lakini muuwaji atapatikana"


http://deusdeditmahunda.blogspot.com/


Walinzi waliovalia sare nyeusi ambazo si za askari niliowazoea wa hapa


Tanzania, walikuja na silaha nzito na mmoja wao alituuliza


"Kuna nini? Ustaarabu umewashinda?"


Michael alinyanyuka huku akinitazama, akacheka kwa dharau na kutingisha


kichwa. Akaniambia


"Pole rafiki yangu nitakuja kukuona siku nyingine"


Michael akaondoka.


Nilibaki pale sebuleni wale walinzi nao wakaondoka. Machozi sasa


yakadondoka kwa uchungu. Rafiki yangu amenisaliti. Vipi kuhusu wazazi


wangu? Mama yangu ataniamini?Sina shaka na baba kwa kuwa yeye hunijua vyema


mimi. Nikatupa jicho pembeni nikakutana na gazeti la udaku.



ITAENDELEA 

Tags

Post a Comment

0 Comments
Post a Comment (0)

Made with Love by

Pixy Newspaper 11 Template is Designed Theme for Giving Enhanced look Various Features are availabl…
To Top