ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“Naitwa Happy ..Happy Kibaho ,natokea Tanzania”
“Uuugh ! nafurahi sana kusikia unatoka Tanzania.I love Tanzanians.Nasikia ni watu wapole na wakarimu sana.Mama yangu amewahi kwenda Tanzania kupanda mlima Kilimanjaro na aliporudi akatuhadithia kuwa hajawahi kukutana na watu wakarimu kama watanzania.”
Happy akatabasamu .Ilikuwa ni mara ya kwanza kwa Michelle kumuona happy akitabasamu.
“Happy you are so pretty.Unajua sikuwahi kukuangalia vizuri.You are amazing” Michelle akajibu na kumfanya Happy afurahi.
“Jina lako zuri sawa kabisa na sura yako..ukitabasamu unakuwa mzuri zaidi ya malaika..” akasema Michelle na kumfanya Happy acheke kwa nguvu.
Huo ukawa ni mwanzo wa urafiki mkubwa kati ya Happy na Michelle.
ENDELEA............................
Urafiki kati ya Happy na Michelle uliendelea kuimarika siku hadi siku.Michelle alijitahidi kadiri alivyoweza kuwa karibu na Happy .Kila mwisho wa wiki walitoka na kwenda sehemu mbali mbali za starehe lengo likiwa ni kumchangamsha Happy.Pamoja na mambo hayo yote ambayo Michelle alijitahidi kufanya ili kumfanya Happy awe na furaha lakini haikuweza kumsahauliasha kuhusu Patrick hata nukta moja.Alijitahidi kila awezavyo ili asiweze kumsahahu kijana huyu mwenye upendo wa ajabu kwake.
Ili tokea siku moja chuo kikafungwa kwa muda wa wiki mbili,Michelle akamuomba Happy wazitumie wiki mbili hizo kwa kuitembelea familia yao huko California.Happy akakubaliana na mwaliko huo na kesho yake wakapanda ndege na kuelekea California.Walipewa mapokezi mazuri na familia ya akina Michelle.Ilikuwa ni furaha iliyoje kwao kumpata mgeni aliyetoka Tanzania. .
Siku mbili tu baada ya kuwasili kwao hapo nyumbani ,Mike naye akawasili akitokea jiji la New York anakofanya kazi.Tayari alikwisha taarifiwa na mdogo wake Michelle kuwa tayari Happy alikuwa hapo nyumbani kwao.Mike aliwasili mida ya mchana na kuwakuta familia nzima ikiwa imejipumzisha.Akasalimiana na wote kisha akaelekea chumbani kwake.Kijasho kilikuwa kikimtiririka hasa baada ya kulishuhudia kwa mara ya kwanza tabasamu pana la Happy .Alikaa kitandani na kujaribu kuwaza ni jinsi gani atakavyoweza kujiweka karibu na binti huyu mwenye urembo usioelezeka..Alishindwa kupata jibu akaamua kwenda kuoga kisha akaelekea bustanini ambako Michelle na Happy walikuwa wamepumzika kwa muda huo.
Mara tu baada ya Mike kuwasili hapo bustanini ,Michelle akainuka na kwenda ndani kuongeza vinywaji,akawaacha Mike na Happy .Mike moyo ulikuwa ukimdunda .Ilihitaji ujasiri wa aina yake kuanzisha maongezi na binti huyu mwenye uzuri wa kimalaika.Baada ya kimya cha sekunde kadhaa toka amefika pale Mike akajikaza kiume na kuanzisha maongezi.
“Happy unanikumbuka?”CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
:Happy akanyamaza kidogo kana kwamba anajaribu kukumbuka kitu kisha akajibu.
“hapana”
“Nilikuja siku moja chuoni kwenu nikakukuta umeiinamia kompyuta yako” akasema Mike na Happy akatabasamu
“Ouh ! nimekukumbuka.kumbe ni wewe ! Samahani siku ile sikuwa katika hali nzuri ndio maana sikukujibu vizuri.” Akasema Happy huku akitabasamu
“.hata mimi nilijua haukuwa katika hali nzuri kwa sababu siku hazifanani.” Mike akasema huku akatabasamu baada ya kumuona Happy akitabasamu
“Vipi unaionaje hali ya Marekani”Mike akauliza
“ ni nzuri,Marekani kuzuri,kila kitu kizuri ,but I miss home” akajibu Happy
“Tanzania? Mike akauliza
‘Yes ! nani kakwambia kuwa natokea Tanzania?
‘Michelle” Mike akajibu .Happy akatabasamu
“Hata mimi” Mike akaendelea “naipenda sana Tanzania.Nasikia ni nchi ya amani na watu wake ni wakarimu mno.” Happy akatabasamu baada ya kauli ile ya Mike
“Nafurahi kusikia hivyo.Umekwisha wahi tembelea nchi yoyote ya Afrika? Akauliza Happy
“Hapana bado sijatembelea nchi yoyote ya Afrika. Ila nina mpango wa kufanya ziara Afrika na nchi ya kwanza kutembelea itakuwa Tanzania.”
“Nini kinakuvutia mpaka uifanye Tanzania kuwa nchi ya kwanza kuitembelea? Happy akauliza
“Just to see pretty women” Mike akajibu na wote wakaangua kicheko.
“ Nina hakika Tanzania imebarikiwa kwa kuwa na vivutio vingi vya kiasili lakini hata hivyo kuna wasichana warembo mno” akasema Mike na wote wakaendela kucheka.
Ilikuwa ni wiki nzuri sana kwa Happy .Alifurahi kukutana na familia yenye watu wakarimu kama hii ya akina Michelle.Kwa kiasi Fulani ziara hii ya California ilisaida kumuondolea msongo wa mawazo uliokuwa ukimkabili.Mike na Michelle walijitahidi kwa kila walivyoweza kuhakikisha kuwa Happy anakuwa na furaha kwa muda wote atakaokuwa hapo kwao.
Jumapili Mike akamuomba Happy watoke kwa ajili ya matembezi.Michelle alikuwa hajisikii kutoka.Jioni ya siku hiyo wote wawili wakiwa wamependeza vilivyo walipanda gari na kutoka.Safari iliishia katika klabu moja kubwa na maarufu .Ilikuwa ni sehemu tulivu na yenye mandhari ya kuvutia mno.Waliagiza vinywaji na kuanza kunywa taratibu huku wakiendelea na maongezi ya hapa na pale.Kisha Mike akabadili maongezi na kusema.
“Happy leo ni siku ya furaha sana kwangu kuwa karibu nawe katika mahali tulivu kama hapa na ni siku muhimu vile vile kwa kuwa nimedhamiria kuutua mzigo mzito unaonikabili kwa muda mrefu sasa”
Happy akastuka kidogo kwa kauli ile ya Mike lakini akamuacha Mike aendelee.
“Happy nina furaha moyoni mwangu kukutamkia kuwa u mwanamke pekee ambaye umeweza kuuteka moyo wangu kwa kiasi ambacho siwezi elezea.Kwa ufupi Happy nakupenda sana na tafadhali ninaomba uridhie ombi langu la mimi na wewe kuwa wapenzi.Naomba unielewe Happy kuwa penzi langu kwako ni la dhati lenye lengo la kuja kuishi nawe kama mume na mke pindi utakapomaliza masomo yako.”
Happy akaiweka glasi chini ,akamuangalia Mike kana kwamba ni mara ya kwanza anamuona.Mike naye akamuangalia Happy kwa makini Happy akatabasamu ,tabasamu ambalo kwa kiasi kikubwa linamchanganya Mike.
“Mike you are very handsome” Happy akasema akainua glasi yake ya kinywaji akanywa funda moja
“Oh ! thank you Happy” mike akasema huku akitababasamu na kuirekebisha tai yake aliyokuwa amevaa.Happy akaendelea
“ Mike wewe ni kijana ambaye kila mwanamke angependa uwe naye.Una kila sifa za kijana bora.U mcheshi,mchangamfu na unayevutia.Nashukuru kwa kuwa wazi na hisia zako.Ila samahani kaka yangu mimi tayari nina mtu ambaye sijui hata nikuelezeje ili unielewe kwa jinsi ninavyompenda Kijana huyu ndiye aliyeushika moyo wangu,ameyashika maisha yangu.yeye ni kila kitu kwangu.Nampenda Patrick kuliko ninavyojipenda mimi.Kama nisingekuwa na Patrick nisingekukataa Mike.” Happy akasema kwa kujiamini.
Mike akainama chini kwa sekunde kadhaa akiwaza.tayari alikwisha uona ugumu uliopo mbele yake.katika kumshawishi Happy akubali ombi lake la kuwa naye katika mahusiano.
“Happy naheshimu mawazo yako na ninauheshimu sana uhusiano wa mtu.Si lengo langu kuvuruga uhusiano wako.Kwa kuwa tayari una mpenzi anayekupenda na wewe unampenda basi naomba kitu kimoja tu kutoka kwako.”
“Kitu gani Mike?” Happy akauliza
“ nataka tuwe marafiki wa kawaida”
“Kwa hilo hakuna shida.Mike nashukuru sana kwa kunielewa.Nitakuombea ili uweze kumpata msichana kama mimi ambaye nina imani utampenda zaidi yangu.”
“nafurahi kusikia hivyo Happy ” Mike akasema katika hali ya unyonge.
Maisha yaliendelea vizuri na baada ya wiki mbili kumalizika Michelle na Happy wakarudi chuoni Mike akarejea kazini kwake New york
****************************
Patrick aliendelea na maisha ya gerezani kama kawaida.Siku moja Patrick akaitwa na mkuu wa gereza na kuambiwa ajiandae kwa safari alikuwa akihamishwa gereza.Hii ilikuwa ni taarifa ambayo ilimvunja moyo sana kiasi cha kumfanya adondoshe machozi.Ni wafungwa watatu tu ndio waliokuwa wakihamishwa gereza.
Haikuweza kufahamika mara moja sababu ya kuhamishwa kwao Wakati wakijiandaa kuondoka ,hakukuwa na mfungwa mwingine wa karibu ambaye angeweza kumwachia ujumbe wowote.Hakujua anahamishiwa gereza gani. Alizoea kila wiki kupokea barua za Happy .Hakujua angewezaje kumfahamisha juu ya uhamisho ule wa ghafla.
Safari ilianza bila kuchelewa .Ilikuwa ni safari ndefu na yenye kuchosha.Gari walilopanda lilikuwa na madirisha madogo juu kwa ajili ya kuingiza hewa .hivyo kutokutambua ni wapi walikokuwa wakielekea.
Wakiwa wamepitiwa na usingizi walistuliwa na sauti ya kufunguliwa kwa mlango.Walifunguliwa pingu walizokuwa wamefungwa mikononi na kuamriwa kushuka.Walikuwa wamechoka kupita kiasi.Ilikuwa ni safari ndefu na njaa ilikuwa ikiwauma kupita maelezo.Tangu wapewe chakula mchana ambacho kilikuwa ni chipsi kavu na maji ya kunywa hawakula tena chochote.
Tayari giza lilikwisha tanda angani.Hawakujua ilikuwa ni saa ngapi mida hiyo.Hali ya mahala hapo ilikuwa ni ya baridi kali.Wote walikuwa wakitetemeka.Walisimamishwa hapo kwa takribani dakika ishirini kisha askari mmoja akatoka ndani akawaangalia na kuamuru wapelekwe ndani wakapumzike.Waliongozwa na askari wawili wenye silaha hadi ndani ya gereza.Kila mmoja akaonyeshwa chumba chake cha kulala.Hili lilikuwa ni gereza jipya kabisa na la kisasa lililokuwa limejengwa mjini songea kwa msaada wa watu wa Marekani.Lilikuwa ni gereza la kwanza la mfano nchini Tanzania kuwa na ubora wa hali ya juu afrika mashariki na kati.Patrick alishukuru Mungu kwa kuletwa hapa .Kutokana na uchovu wa safari aliokuwa nao akajitupa kitandani na kulala.
Saa kumi na mbili asubuhi king’ora kikalia .Patrick mwili wote ulikuwa ukimuuma kwa uchovu na alihisi njaa kali.
“Hey amka ndugu ” Akastuliwa na sauti ya mtu aliyekuwa akimtikisa.Akafumbua macho na kukutana na macho ya kijana mdogo mwenye sura ya upole.
“Vipi husikii king’ora hicho?” Akaendelea kusema yule kijana.
Kiuvivu Patrick akainuka na kukaa kitandani.baada ya kama dakika tatu hivi akaja askari akafungua geti la chumba chao na kumrushia Patrick nguo mpya kabisa za kifungwa.Hakusema kitu akazikunjua na kuvaa .
“Kwa hiyo nini kinaendelea saa hizi? Utaratibu wa hapa ukoje ?” Patrick akamuuliza yule kijana waliyekuwa wakilala wote chumba kimoja.
“huu ni muda wa kujiandaa,kunawa au kuoga kama unataka .Kitapigwa king’ora kingine tutaenda kupata mlo wa asubuhi halafu baada ya hapo tutapangiwa kazi.”
Patrick akaonyeshwa sehemu yenye mabafu akaingia na kuoga..King’ora kingine kikalia na wote wakakusanyika katika bwalo la chakula kwa ajili ya kifungua kinywa..Walikuwa wafungwa wachache kama arobaini hivi.CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Baadaye kazi zikapangwa na Patrick na wenzake wakapangiwa sehemu ya kufyeka.Miongoni mwao alikuwemo yule kijana anayelala naye chumba kimoja.Walifanya usafi huku wakisimuliana mambo mengi na kupeana moyo.taratibu wakaanza kuzoeana na kujenga urafiki.
Usiku wa siku hiyo Patrick na yule kijana ambaye alikuja kumfahamu kama Andrew waliutumia katika kusimuliana mikasa mbali mbali ya maisha yao.Andrew alimsimulia Patrick kisa cha yeye kuwapo pale gerezani.Kifungo chake kilikuwa cha miaka mitatu na kilitokana na kusababisha ajali wakati akiendesha gari akiwa amelewa.
Patrick naye alimsimulia hadithi yake na mpaka anamaliza Andrew alishindwa kujizuia kudondokwa na mchozi.
“Pole sana Patrick hayo yote ni majaribu katika maisha .Ni wazi Patrick una upendo wa dhati na wapekee sana kwa huyo Happy .Usikate tamaa Mungu atakusaidia utamaliza kifungo chako.”
“Ahsante sana Andrew kwa kulitambua hilo na kunipa moyo.Lakini kitu ambacho bado kinaniumiza sana kichwa ni jinsi nitakavyoweza tena kuwasiliana na Happy .Katika gereza lile nilikotoka ,mkuu wa gereza alikuwa amejitolea kunisaidia kwa kutuma barua zangu kwenda kwa Happy na kupokea zitokazo kwa happy na kuniletea..Ningeweza kuwatumia wazazi wangu lakini bado hawajui kama nimehamishwa gereza “ akasema Patrick kwa masikitiko
Siku moja Patrick akapangiwa kwenda kufanya usafi katika nyumba ya mkuu wa gereza.Huko alipangiwa kufyeka na kurekebisha viunga vya maua .
Katika dirisha lililoelekea upande wa mbele ya nyumba dada mmoja mrembo alikuwa amekaa mkono shavuni kwa takribani dakika kumi na tano akimuangalia Patrick bila yeye kujua kama alikuwa akiangaliwa.Alistaajabu kwa kumuona kijana kama yule ambaye kwa mbali tu alionekana ni kijana mpole,mtaratibu na mwenye kuvutia ,akiwa gerezani.
“ama kweli jela haina mwenyewe.How such a handsome guy be in prison?.Alifanya nini kijana yule i? Mhh ! hebu mwangalie vizuri halafu anaonekana ana mawazo mengi.Namuonea huruma ..jamani !! ..” Akawaza mwanadada yule.
Haraka haraka dada yule akaenda jikoni na kutengeneza chai akaweka katika sinia akabeba na kuelekea mahali alipokuwa akifanya kazi Patrick.
“kaka habari za kazi? Patrick akastushwa na sauti tamu,laini ya mwanadada.Akageuka na ghafla akajikuta akiangusha fyekeo.Macho yake yakakutana na binti ambaye uzuri wake wa asili ulikuwa unasisimua.Hakuamini kama angeweza kukutana na binti mrembo vile maeneo yale.
“Pole na kazi “ Akasema tena binti yule baada ya kuona Patrick akimuangalia tu bila kusema kitu.
‘Nzu…r..rii tu dadangu” Akajibu.Patrick kwa sauti yenye kigugumizi.
“Kaka unaweza ukapumzika walau upate kikombe cha chai kwani toka asubuhi nakuona unachapa kazi bila hata kupumzika ”Akasema yule dada akamkaribia Patrick na kuweka lile sinia chini.
“Nashukuru sana dadangu lakini naogopa mkuu akinikuta hapa patakuwa hapatoshi”
“Usihofu kaka yangu ,mjomba hayupo amekwenda Dar leo asubuhi na hata mkewe naye hayupo atarudi kesho”akajibu yule dada
Patrick anamkazia macho yule dada baada ya kusikia kauli ile.
”Ina maana binti huyu ni mjomba wake na mkuu wa gereza? Du ! mtoto ameumbika vilivyo.Ananikumbusha sana mpenzi wangu Happy .”
Patrick hakujivunga tena akaenda katika bomba na kunawa mikono
“Karibu” yule dada akamkaribisha Patrick
“Ahsante lakini mbona kikombe chenyewe ni kimoja? Patrick akauliza
“Usijali kaka yangu hii ni kwa ajili yako”
Patrick akanywa chai ile nzuri .Kwa muda mrefu hakuwahi kuipata chai nzito kama ile.Akamaliza kikombe cha kwanza na kuongeza tena cha pili na hatimaye cha tatu.Kimoyo moyo alimshukuru sana yule dada mrembo kwa chai ile kwani alihisi njaa kali asubuhi hiyo.
Wakati Patrick akinywa chai ile,yule dada aliingia ndani na kwenda kukaa katika lile dirisha akiendelea kumwangalia
“Anateseka huyu kaka .Namuonea huruma kweli.Halafu mpole.Sijui alifanya kosa gani huyu kaka manake haonekani kama mhalifu “ Akawaza yule dada
Patrick akamaliza kunywa chai akakusanya vyombo na kwenda kugonga mlango.Yule dada akafungua mlango na kuvipokea.
“Ahsante sana dada Mungu akubariki” Akasema Patrickkisha akaendelea na kazi yake yake ya usafi .Kila dakika taswira ya yule dada mpole mwenye roho ya huruma ilikuwa ikimjia na kumfanya atabasamu
.”Kumbe duniani bado kuna watu wenye upendo “ Akasema taratibu huku akiendelea na kazi yake ya kurekebisha bustani ya maua.
“Imezoeleka katika jamii yetu kila mfungwa ni mnyang’anyi,hali ambayo kufanya wafungwa kutokuthaminiwa,kutokuhurumiwa,na hata kutokusaidiwa lakini bado wako watu wachache wenye huruma na upendo kwa wafungwa kama huyu dada alivyofanya leo.Aliwaza Patrick.Wakati akiendelea na usafi dada yule akatoka tena na kisinia kilichokuwa na glasi mbili za juice.
“Kaka karibu upumzike upate juice” akasema yule dada
Patrick aliingiwa na wasiwasi iwapo wakuu wake wangekuja na kumkuta amekaa .
“ahsante sana dadangu ila naogopa iwapo hawa wakuu wetu watakuja na kunikuta nimekaa nakunywa hiyo juice itakuwa ni habari nyingine” Patrick akasema huku akiwa na wasi wasi lakini moyoni alitamani sana juice ile.Huku akitabasamu dada yule akasema
“Usihofu kaka nimekwambia mjomba wangu hayupo na hata mkewe hayupo kaenda Iringa .Hapa nipo mimi tu .Kaa upumzike kaka yangu unajua upatapo nafasi ya kufanya usafi katika nyumba hizi za wakuu ni nafasi yako ya kupumzika.Kazi zenu ni ngumu sana” Akasema dada yule
“Ni kweli usemayo dada yangu lakini inategemea na mahali penyewe.Unajua kwa sisi wafungwa jamii inatuchukulia kama wote ni wanyang’anyi kumbe sivyo.Nimekuwa nikifanya usafi katika baadhi ya nyumba za maafisa wakubwa na wadogo lakini hakuna hata siku moja niliyowahi kupewa hata glasi ya maji.Lakini kumbe kuna watu wana roho za utofauti sana na mmoja wao ni wewe.U mkarimu sana dada yangu.”akasema Patrick
Taratibu Patrick akajikuta akikaa chini kwenye bustani huku ameikamata glasi ya juice.Juice kama hii alizowea kuipata wakati Happy hajaondoka.Siku hii ya leo inamkumbusha mbali sana.Alishindwa kuyazuia machozi kudondoka mara alipomkumbuka Happy
“Vipi kaka yangu mbona unalia?
“ Juice hii imenikumbusha mbali sana” akajibu Patrick
“Basi usilie kaka yangu Mungu yupo na atakusaidia uweze kumaliza kifungo chako”
Kilipita kimya cha sekunde kadhaa Patrick akauliza
“lakini dada yangu inaonyesha wewe si mwenyeji kabisa wa maeneo haya”
Huku akitabasamu dada yule akajibu
“kwa nini unasema hivyo”
“Inaonyesha tu.Mwonekano wako haufanani kabisa na mazingira haya”
Dada yule akacheka kicheko kikubwa kisha akajibu.
“Una uwezo mkubwa wa kuweza kumsoma mtu na kumwelewa kwa haraka.Ni kweli mimi si mwenyeji wa hapa .Mimi naishi Dar es salaam.Mzee Joel mkuu wenu wa gereza ni mjomba wangu na nimekuja mara moja kumletea mizigo yake iliyotumwa na dada toka Ulaya.Ingawa sintakuwa na muda mrefu hapa lakini nimetokea kupapenda sana.Pana hewa nzuri na nimazingira tulivu sana.” Akasema yule dada
Yule dada akatulia kidogo akanywa mafunda mawili ya Juice kisha akasema
“ Kwa jina naitwa Veronika .Veronika Rugi sijui kaka wewe unaitwa nani?
Patrick akanyamaza na kutafakari iwapo amweleze jina lake au vipi.Mwishowe akaamua kumtajia jina lake
“Naitwa Patrick “CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“ nafurahi sana kukufahamu Patrick.Unajua toka nimekuona asubuhi ukifanya usafi moyo wangu haukutulia kabisa.Nilikuwa na hamu sana ya kutaka kukufahamu.U mpole sana na haufanani na wafungwa wengine”
Patrick akacheka baada ya kauli ile ya Veronika.
“Kweli kabisa patrick,haufanani na wafungwa tuliozoea kuwaona.Mtu yeyite akikuona mara moja atahisi kuwa uliingizwa gerezani kimakosa.Sura yako haionyeshi kuwa unaweza ukafanya kosa katika jamii ambalo lingepelekea wewe kufungwa gerezani”
Patrick akacheka tena na safari hii kicheko kikubwa zaidi,Vero akatabasamu.
“Patrick nitafurahi sana kama utaungana nami kwa chakula cha mchana leo hii.Niko mwenyewe hapa nyumbani na kama ujuavyo chakula cha peke yako katu hakina utamu”Akasema Vero
“Hamna shida Veronika “Patrick akajibu .Alikwisha anza kumzoea binti yule mrembo.Veronika akamkaribisha Patrick ndani sebuleni na kumuwashia luninga kisha yeye akaelekea jikoni kuandaa chakula.Patrick alijisikia faraja kubwa kwa kukalia tena sofa nzuri kama zile baada ya muda mrefu.
“ Veronika ni binti mzuri ,mrembo mwenye kila sifa inayohitajika kwa binti mrembo .Ni mwelewa na ana huruma sana.Nafurahi kukutana na binti huyu japo kwa muda mfupi.Nina imani vile vile anaweza kunisaidia kurejesha mawasiliano kati yangu na Happy “ akawaza Patrick mara akastuliwa toka katika mawazo na sauti ya Vero
“Hello Patrick ,mbona unaonekana mnyonge hivyo?Usihofu kitu .Unaonekana umezama kwenye dimbwi la mawazo.Just relax.Hakuna mtu atakaye kuja kukusumbua.Pumzika mpaka muda wa kurudi ndani utakapofika.” Akasema Verokwa sautiya upole
“Ahsante Vero,nashukuru sana dada yangu”
Waliongea mambo mengi na kujikuta wakifahamiana na kuzoeana zaidi.Patrick alimsimulia Vero hadithi nzima ya maisha yake iliyomfanya Veronika atokwe na machozi.
Hatimaye muda ukafika kwa wafungwa kurejea gerezani wakaagana huku Vero akiahidi kufanya kila njia ili waonane kabla hajaondoka kurudi Dar.
* * * *
Ulikuwa ni usiku mgumu sana kwa Vero.Hakujua ni kwa nini Patrick alikuwa ameingia moyoni mwake kwa kasi ya ajabu namna ile.
“Sielewi ni kwa nini Patrick amenigusa ghafla hivi .Ni kijana mpole ,mtaratibu na mwenye kuvutia hata akiwa katika mavazi ya kifungwa.Namuonea huruma sana .Ameugusa sana moyo wangu.Nitajitahidi niweze kumsaidia katika kipindi chote atakachokuwepo gerezani.Toka nimezaliwa sijawahi kuguswa moyo wangu na kijana yeyote kama alivyonigusa leo Patrick na hadithi ya maisha yake.Ni mapenzi mazito aliyonayo kwa Happy ndiyo yaliyopelekea mpaka kijana wa watu anasota gerezani.Namuonea wivu huyo Happy kwa kumpata kijana mwenye upendo wa dhati kama Patrick.Natamani kama angekuwa ni mpenzi wangu.Ningejitahidi kwa kadiri niwezavyo kuweza kumfanya mwenye furaha daima.I’m dreaming for a man like Patrick.Ana karibu kila kitu ninachokihitaji kwa mwanaume wa ndoto zangu.Lakini mhh!!!… Mbona naanza tena kuwaza mambo ya ajabu ajabu?Ni kwa nini siwezi kupitisha hata dakika moja sijamuwaza Patrick ? Mhh !! nahisi tayari ameanza kuingia moyoni mwangu taratibu.Ouh My God help me with these feelings.” Veronika akajikuta akiwa katika mawazo mazito
“Ingekuwa ni mimi ndiye niliyepelekea Patrick akafungwa nisingekubali kabisa kwenda Ulaya na kumwacha akiteseka gerezani peke yake.Stupid girl Happy . Nitafanya kila niwezalo ili kuifanya sura ya Patrick iwe na tabasamu tena.Nitahakikisha anakuwa msafi,anakula vizuri na kupata raha zote.Mkuu wa gereza ni mjomba wangu.Nitamweleza ukweli ili aweze kunisaidia.Nitamuomba kila siku Patrick awe akipangiwa kufanya kazi kwa mkuu wa gereza ili aweze kupata nafasi ya kula vizuri na kupumzika." akawaza Veronika huku akiendelea kujigeuza geuza pale kitandani akijaribu kuutafuta usingizi.
Wakati Veronika akiwa katika wakati mgumu kwa mawazo usiku huo hali haikuwa nzuri sana kwa upande wa patrick .Mchana wa siku hiyo ulimkumbusha mbali sana.Ulimkumbusha kipindi alichokuwa katika mapenzi mazito na Happy . Alizikumbuka nyakati zile za furaha alizokuwa nazo .Alihisi kuihitaji furaha ile tena.
Ghafla ikaja picha ya Veronika akiwa na sinia lenye chupa ya chai .Akakumbuka toka wakati akinywa chai ile na jinsi alivyokula chakula kitamu siku hiyo .
“Mhh haya ni majaribu makubwa sana” Akawaza
“Bado nampenda sana Happy lakini mbona Veronika naye anakuja kwa kasi sana katika mawazo yangu.Mhh ! hapana labda ni kwa ajili ya ule ukarimu wake.Tangu nimefungwa sijawahi kukutana na binadamu ambaye si mtu wangu wa karibu mwenye roho ya huruma na upendo kama Veronika.Veronika hatofautiani sana na Happy .Nahisi hii ni sababu inayonifanya niwe nikimuwaza sana kwa sababu kila nikimkumbuka Vero ananifanya nimkumbuke Happy " akawaza Patrick .
Urafiki kati ya Patrick na Veronika ulikua kwa kasi sana.Vero kwa kupitia mjomba wake ambaye ndiye aliyekuwa mkuu wa gereza alihakikisha kuwa patrick anapangiwa kufanya kazi mbali mbali nyumbani kwa mkuu wa gereza.Bila uoga Veronika akamueleza ukweli mjomba wake Joel armendo mkuu wa gereza hilo kuhusu urafiki wake na Patrick.Alimueleza kila kitu kuhusiana na hisia zake kwa kijana huyu.Mjomba wake alimwelewa na akaahidi kumsaidia Vero lakini Ili kujiridhisha na maelezo ya Veronika mara moja akaanza kufanya uchunguzi juu ya kijana huyu ambaye jarada lake linaonyesha kuwa alihukumiwa kifungo kutokana na kesi ya kuua bila kukusudia.Hakuridhika sana na maelezo yale.Hakutaka Veronika awe na mahusiano na kijana mwenye rekodi ya uhalifu.Siku moja akamwita Patrick ofisini kwake na kuanza kumuhoji mambo kadhaa ikiwa ni pamoja na kutaka kufahamu historia kamili ya Patrick.Hadithi ya Patrick ilimkuna sana Joel na kumfanya aridhike na kuoa kuna umuhimu wa kumsaidia Patrick katika maisha ya pale gerezani.Joel akajikuta akimpenda sana Patrick hasa kutokana na tabia yake nzuri na kujituma.Familia nzima ya Joel Armando ilitokea kumpenda Patrick na kadiri siku zilivyozidi kwenda taratibu wakaanza kumhesabu kama mmoja wa wanafamilia.Kila siku alipangiwa kufanya kazi nyumbani kwa mkuu wa gereza na kusaidia kazi mbali mbali mpaka muda wa kurudi gerezani ulipowadia.Hakuhitaji tena kusimamiwa .Alikuwa ni mfungwa ambaye alitokea kuaminiwa mno siyo tu na wakuu bali hata wafungwa wenzake na askari magereza wote.
Urafiki na ukaribu baina ya Patrick na Veronika ukaongezeka maradufu.Veronika alifurahi mno kwa ukaribu ule kiasi kwamba hakuwa na hamu hata ya kurudi nyumbani kwao Dar es salaam..Mama yake akashangaa sana kwa binti yake kuchukua muda mrefu namna ile kurudi nyumbani wakati makubaliano yalikuwa atumie wiki mbili tu kwa mjomba wake lakini sasa ni wiki ya tatu hajarejea . Mama yake akaamua kumpigia simu kaka yake Joel ambaye ndiye mjomba wa Vero na kumwomba amwambie Vero arudi haraka sana Dare s salaam kwani shughuli nyingi zilikuwa zikimsubiri.Veronika alikuwa ndiye msimamizi mkuu wa miradi na shughuli zote za familia yao.Veronika alilia sana usiku huo kwa kuachana na Patrick kijana ambaye tayari alikwisha mzoea kwa kiasi kikubwa na urafiki mzito ulikwisha anza kujengeka baina yao.Alikuwa na matumaini makubwa ya kuwa urafiki ule ni lazima ungekuwa ni wa manufaa kwake..
Siku iliyofuata alimweleza Patrick kuwa mama yake anamwitaji arudi Dar mara moja.Taarifa hii ilikuwa ni ya mstuko kwa Patrick pia kwa sababu tayari alikwisha mzoea sana Veronika.
“Usihofu Patrick pamoja na kwamba ninaondoka lakini nitajitahidi walau kila mwisho wa mwezi niwe nakuja hapa kukutazama.Niambie kitu kimoja Patrick..”
“kitu gani hicho Veronika ?” Patrick akauliza
“Will u miss me ?! “
Patrick akatabasamu ,akamshika mkono Vero na kusema.
“ Very much.I’ll miss you very much Vero”
Veronika akatoa tabasamu pana sana baada ya kusikia kauli ile.
“Lakini usijali kama nilivyokwambia nitajitahidi kuja mara kwa mara kukuangalia.Isitoshe familia ya mjomba ipo nawe hivyo hutajisikia mkiwa hata kidogo na hapa kuna simu nitakuwa nakupigia kila siku tunaongea .Nadhani hutanimiss sana” akasema Veronika.
“Vero usijali sana .Unajua toka siku ya kwanza tumeanza urafiki nilijua tu iko siku utaondoka.Tayari nilikuwa nimekwisha jiweka tayari kwa hilo.Usihofu chochote juu yangu,mimi nimekwisha zoea kuumia.Siyo siri Vero kuondoka kwako ni jeraha jingine kubwa katika moyo wangu.Umekuwa mtu wangu wa karibu sana na kunifanya nisahau mateso na mchungu yote ya gereza japo kwa muda mfupi...”Patrick akasema
“Patrick najua una uchungu sana kwa mimi kuondoka.Hata mimi ninaumia vile vile kwa kukuacha peke yako hasa katika kipindi kama hiki ambacho ni wazi unahitaji sana mtu wa kukufariji na kukupa moyo.Lakini usijali nitarudi .”
“Nimekuelewa Vero.Ila naomba unisaidie kitu kimoja”
“Kitu gani hicho Patrick niambie niko tayari kukusaidia kitu chochote” akasema Vero
“Kama unavyofahamu kuhusu kinachoendelea baina yangu na Happy .Nina imani Happy hajui kama nimehamishwa gereza na anaendelea kunitumia barua kwa kutumia anuani ya gereza la awali .Wazazi wangu pamoja na mkuu wa gereza nilikotoka ndio waliokuwa na kazi ya kuniunganisha na Happy lakini mpaka sasa hivi hawajaja kunitazama.Kwa hiyo sifahamu nini kinachoendelea.Ninachohitaji toka kwako ni msaada wako ili niweze tena kuwasiliana na Happy .Nitaandika barua na kumweleza Happy kila kitu na nitaomba ukanisaidie kuiposti kwa haraka.” Akasema Patrick.
Akionyesha uso wa furaha Veronika akajibuCHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Usihofu Patrick .Nimekwisha kueleza toka awali kuwa nipo kwa ajili yako,hivyo usisite kunituma jambo lolote lile na nitakusaidia kwa uwezo wangu wote”
Siku hiyo Patrick akaandika barua ndefu na kumfahamisha Happy juu ya uhamisho wake na kuzidi kumsisitiza juu ya ahadi zao walizowekeana..
“Kazi kubwa bado ninayo” Aliwaza vero usiku kabla ya siku ya kuondoka kwake.
“Ninampenda Patrick lakini bado inaonyesha mapenzi yake yako kwa Happy .Mapenzi yao ni ya dhati kabisa.Ni ndoto yangu ya siku nyingi ya kumpata kijana mwenye mapenzi ya kweli kama Patrick.Hata hivyo bado sikati tamaa.Happy yuko mbali na mimi niko karibu na Patrick nani alisema fimbo ya mbali inaua nyoka? Kwa kuwa ninampenda Patrick nitapambana .Kwanza ni lazima niuvuruge uhusiano huu wa Patrick na Happy baada ya hapo utazaliwa uhusiano mpya kati ya Patrick na veronica.” Akawaza Veronika na kwa hasira akaifungua barua ile aliyopewa na Patrick ili akaiposti kwenda kwa Happy akaanza kuisoma.alipomaliza akairudia tena na tena.Ilikuwa ni moja kati ya barua zenye msisimko wa hali ya juu.
“Siwezi kuituma barua hii.Maneno aliyoyaandika humu yanaweza kumfanya mgonjwa aliye mahututi kupona ghafla.Ni maneno yenye mahaba mazito.I deserve a guy like him.He must be mine.” Vero akasema mwenyewe kwa hasira huku akiichana katikati ile barua aliyopewa na patrick.
" Nitakuwa mjinga kama nitaituma barua hii iende kwa Happy na kuzidi kuliimarisha penzi la Patrick na Happy wakati hata mimi ninamtaka Patrick..Natakiwa niuvuruge kabisa uhusiano wao ili niweze kuipata nafasi ya kuwa na Patrick..Penzi lao ni zito na kuwatenganisha si kazi rahisi lakini I will have to do something.Lazima nifanye kila linalowezekana niwatenganishe Patrick na Happy..I'll do anything I mean anything to separate them..." akazidi kuwaza Veronika.
* * * *
Ni siku moja tu tangu Veronika aondoke ,Patrick akatembelewa na wazazi wake.Ilikuwa ni siku ya furaha kubwa mno kuwaona tena wazazi wake .Aliruka na kufurahi,alitamani kama Vero ngekuwepo ili awafahamu wazazi wake.
Kitu kikubwa ambacho alikitarajia na kukisubiri kwa hamu ni iwapo kulikuwa na barua yoyote toka kwa Happy .Aliamini wazazi wake watakuwa wamekuja na barua kwa sababu kimepita kipindi kirefu sasa toka alipopokea barua ya happy kabla hajahamishwa gereza..Patrick hakupoteza muda akauliza iwapo wamekuja na barua yoyote toka kwa Happy .Baba yake akajibu kwa masikitiko
“Patrick ninasikitika kuna mambo mengi yametokea hapa kati kati na hukuwa ukifahamu..Kwa ufupi tu ni kwamba nilipata uhamisho wa ghafla kwenda Dar es salaam na ndiko tunakoishi kwa sasa.Toka tumehama hatujapata mawasiliano yoyote toka kwa Happy .Tulitaarafiwa na mkuu wa gereza ulilokuwa awali kwamba umehamishiwahuku hivyo hatukupita tena katika gereza la Iringa.Kama atakuwa ametuma barua basi zitakuwa zimetua katika mikono ya watu wengine.Nasikitika vile vile kwa kutomfahamisha juu ya kuhama kwetu ili asiendelee kutumia anwani ile tuliyokuwa tukiitumia awali “.akasema baba yake Patrick
Patrick akainama kwa sekunde kadhaa akitafakari.
“Oh My God” Akajikuta akitamka kwa nguvu.Kukosa mawasiliano na Happy kulimtesa sana.
“Patrick mwanangu “Akasema mama yake baada ya kumuona mwanae amezama katika mawazo ghafla.
“Nadhani ni wakati sasa wa kusahau yote yaliyopita na kuanza maisha mapya.Nakuomba jitahidi toka moyoni mwako uweze kumsahau Happy .Nakuomba umsahau na uuvunjilie mbali urafiki kati yako na huyo Happy .Bila Happy usingepatwa na matatizo haya mwanagu. ,Happy kakusababishia matatizo mpaka umefungwa gerezani lakini yuko wapi leo ? yuko Ulaya anasoma ! Wewe unasota gerezani,umepoteza masomo na mwelekeo mzima wa maisha .Angalia mateso unayoyapata mwanangu.Mimi na baba yako hatulali tunakuwaza wewe mwanetu.Kama ni kweli angekuwa anakupenda na kukuthamini basi asingekubali kwenda Ulaya na kukuacha peke yako hapa gerezani ukiteseka.Sisi wazazi wako tunasema hatutaki tena kuusikia urafiki kati yako na Happy .yaliyotokea yametokea tunashukuru. na tunamwachia Mungu lakini hatutaki tena kusikia wala kumwona Happy mtoto asiye na fadhila hata kidogo.’ Akasema mama yake Happy.Patrick akastuka sana.Akamtazama mama yake na kusema
“ Hapana mama kamwe sintathubutu kufanya kitu kama hicho maishani mwangu.Siwezi kumuacha Happy hata iweje.Nilipambana kwa ajili yake na kwa ajili ya kuulinda utu na heshima yake na yote hii ni kwa sababu nampenda.Nikumuacha leo haya yote niliyoyafanya kwa ajili ya upendo wangu kwake yatakuwa ni bureWazazi wangu siwezi hata kwa sekunde moja kumsahau au kuachana na Happy..”Akasema Patrick huku machozi yakimtoka. Baba yake akamuangalia na kusema
“Patrick sisi ni wazazi wako na ndio wenye tamko la mwisho.Kauli yetu ni hii hatutaki kumsikia Happy masikioni mwetu.Narudia tena hatutaki kabisa kumsikia binti huyo wala kusikia eti una mahusiano naye..You and her its over...” Akasema baba yake kwa hasira kisha akatoka nje.
Hili likawa ni jaribu lingine kwa Patrick la kutenganishwa na mtu aliyempenda kupita maelezo.Alikuwa njia panda je achague kuwa na Happy au wanavyotaka wazazi wake ? Mama yake akaendelea kumbembeleza mwanae ausikie ushauri wao ili amani iweze kudumu kwani ndugu wote walikuwa wamepitisha azimio hilo kuwa hawataki kuusikia urafiki wa Happy na Patrick.Patrick hakuwa na jibu la kutoa kuhusiana na amri ile ya wazazi wake ya kumtaka atengane na Happy.Wazazi wake wakaondoka na kumuacha Patrick akiwa katika mawazo mengi mno
Veronika alifika nyumani kwao Dar na kulakiwa na mama yake.Ilikuwa ni furaha sana kwa mama huyu kumuona tena mwanae ampendaye.Wakiwa katika mlo wa jioni mama yake Vero akaanzisha mazungumzo.
“ Vero hebu niambie kisa cha kukaa kwa mjomba wako siku zote hizi hali makubalianao yetu yalikuwa ni wiki mbili tu.Unafahamu fika kuwa hapa niko peke yangu sina mtu mwingine wa kunisaidia katika biashara Msaidizi wangu pekee ni wewe.”
Vero akatabasamu na kusema
“mama samahani sana kwa kukaa siku zote hizi kwa mjomba na kukuacha peke yako.Sikuwa nimetarajia kufanya hivyo ila ilitokea dharura ikanibidi nikae.Nashukuru hata ulivyonipigia simu kwani bila hivyo nadhani ningeendelea kukaa zaidi.” Akasema Vero huku akicheka kichini chini
“Dharura gani hizo we mtoto hebu niambie.” Akasema mama yake.Happy akala vijiko viwili vya chakula kisha akasema
“mama wewe ni mzazi wangu lakini umekuwa ndiye mshauri wangu na zaidi ya yote umekuwa ni rafiki yangu wa karibu sana.Ni kutokana na juhudi zako wewe za kunifundisha maadili mema ndio maana leo hii nimekuwa ni binti mwenye mafanikio na kukuletea heshima kubwa.Katika mambo ambayo umekuwa ukiniusia kila siku na kunionya ni kujikita katika mahusiano ya kimapenzi.Nimekuwa nikilifuatilia hilo na ndio maana mpaka umri huu najivunia usichana wangu.Kweli mama simjui mwanaume mpaka leo hii.Lakini mama mapenzi ni kitu ambacho hakikwepeki.Mapenzi yapo na kila mtu kwa wakati wake anajikuta yu mapenzini kama nilivyojikuta mimi.”
Alisita kidogo baada ya kumuona mama yake akimtazama kwa macho yenye udadisi .
“Mama nikiwa kule kwa mjomba Songea nilifanikiwa kukutana na mwanaume ambaye ninaamini ndiye mwanaume wa ndoto zangu.”
Akatulia tena na kuyaacha yale aliyoyasema yazame kabisa kwa mama yake.
Kisha akamsimulia kisa kizima,jinsi alivyokutana na Patrick na hadithi nzima ya maisha ya Patrick .
Mambo yalikuwa tofauti na jinsi Veronika alivyowaza.Yeye alitegemea labda mama yake angemgombeza na kumkanya juu ya jambo lile lakini ikawa tofauti.
“Vero mwanangu nimefurahi sana kwa kuwa wazi na hisia zako.Ni wazi mapenzi hayakwepeki.Yapo na kila mtu anapenda.Mimi nafurahi kusikia kuwa kijana huyo unampenda kwa dhati.Anaonekana ni kijana mtaratibu sana na mwenye mapenzi ya kweli.Mimi nakuunga mkono na niko tayari kukusaidia kwa lolote lile ili uweze kufanikiwa kumpata kijana huyo umtakaye.Kwani lengo langu ni wewe uishi maisha ya furaha na si karaha.” Waliongea mambo mengi kisha wakaagana na kila mmoja akaenda zake kulala.
Hakuweza kupata usingizi usiku huo.alikuwa na furaha kubwa sana baada ya mama yake kukubali kubariki harakati zake za kumpata Patrick.
“Sasa kinachofuata ni kuharibu kabisa kila kitu baina ya Happy na Patrick.” Akasema kimoyomoyo halafu akachukua kalamu na karatasi akakaa mezani na kuanza kuandika barua ambayo alipanga aitume kwa Happy .
Kwako dada Happy
Ni matumaini yangu kuwa unaendelea vizuri na masomo huko uliko.
Naomba kabla yote nijitambulishe kuwa mimi ni jirani wa akina Patrick hapa Sumbawanga.Tumeishi vizuri na familia yao na baadaye nikahamia mkoani Mbeya.Kwa jina naitwa Grace.Nilisikia matatizo yaliyomkumba Patrick.Nikasikitika sana.
Si lengo langu kusema haya yote lakini dhumuni kuu la barua hii ni kukufahamisha kuwa Patrick mpenzio Amefariki dunia kwa ugonjwa wa kuhara akiwa gerezani.
Kaka yake ndiye aliyenipa anwani yako na kunitaka niwasiliane nawe na kukufahamisha juu ya kifo hicho.Anadai kuwa hawawezi kukufahamisha kwa sababu familia yao haitaki kukusikia kabisa hasa baada ya kumsababishia matatizo mtoto wao na kumwacha akiteseka gerezani hali wewe ukipata maisha mazuri i na kuendelea na masomo yako huko Marekani.
Pole sana dada ,haya ndiyo mambo ya dunia.Ulimpenda sana Patrick lakini Mungu kampenda zaidi.Jipe moyo na utampata kijana mwingine kama Patrick
Pole sana
Grace
Vero Aliipitia tena na tena barua ile na kuhakikisha iko safi na siku iliyofuata akadamka na kwenda kuiposti.
* * * *
Akiwa katika mawazpo mengi akimuwaza mpenzi wake Patrick na maisha anayoyaishi gerezani mara mlango waq chumba chake ukagongwa .Kwa uvivu Happy akainuka na kwenda kuufungua .Alikuwa ni mtumishi wa chuo aliyekuwa na bahasha mkononi.Akamkabidhi Happy barua ile kisha akaondoka.
Happy aliitazama barua ile kwa wasi wasi .Alitazama muhuri ulikuwa wa Tanzania.Mwandiko juu ya bahasha hakuufahamu ulikuwa ni wa nani.
Kwa muda wa miezi miwili sasa amekuwa akiandika barua mfululizo kwa Patrick kupitia wazazi wake bila kupata majibu.Hii ilimpa wasiwasi mkubwa .aliumia sana kila alipofikiria Patrick atakuwa katika hali gani.aliujutia uamuzi wake wa kwenda Marekani na kumwacha Patrick peke yake.Alijiuliza maswali mengi juu ya ukimya huo uliotokea ghafla.
Taratibu akakaa kitandani na kuifungua barua ile na kuanza kuisoma kwa makini.Kabla hajamaliza akapiga ukelele mkubwa sana,akaanguka chini na kupoteza fahamu.
Ukelele ule ulikuwa mkubwa kiasi cha kuwastua wenzake waliokuwa katika vyumba vya jirani.Watu walifika hapo chumbani na kumkuta Happy amezimia.haraka haraka wakamchukua na kumkimbiza katika hospitali ya hapo chuoni kwa ajili ya huduma ya kwanza.
Hakuna aliyeweza kufahamu mara moja sababu ya Happy kupiga ukelele ule na kupoteza fahamu.
Saa saba za usiku Happy akazinduka na kujikuta akiwa hospitali.Michelle pamoja na wanafunzi wengine walikuwa pembeni ya kitanda.Alifumbua macho akatazama pande zote kisha akalala tena.Baada ya kama nusu saa akaamka tena na kukaa kitandani.Daktari akafika ,akampima na kumwomba aendelee kupumzika.
Alijilaza kitandani na kuanza kukumbuka mambo yaliyotokea .Alikumbuka barua ile aliyotumiwa na kuanza kulia.Michelle ambaye kwa sasa ni rafiki mkubwa wa Happy alifanya kazi ya ziada kumbembeleza
“ Nyamaza kulia Happy..tafadhali usilie tena..” akasema Michelle
“siwezi kunyamaza Michelle,kilio hiki hakiishi leo,ni kilio cha milele.Nimempoteza mtu muhimu sana maishani mwangu.”akasema Happy kisha akaendelea kulia.
“ Umempoteza nani,baba,mama au ndugu? Akauliza Michelle
“Michelle its Patrick.Patrick is dead”
“Whaat? Michelle naye akastuka.Aliufahamu uhusiano wa Patrick na Happy kwani kila siku Happy alikuwa akimuhadithia namna anavyompenda Patrick
” Yes Patrick is dead” Happy akazimia tena.
Baada ya muda akazinduka.Safari hii aliweza kutazama lakini hakuweza kuongea .Alijaribu kufungua mdomo lakini maneno hayatoki.Ni machozi tu ndiyo yaliyokuwa yakitiririka..Iliubidi uongozi wa chuo kuwataarifu wazazi wake juu ya ugonjwa wa mtoto wao na kwa haraka ikawalazimu waende kumtazama.Ilikuwa ni siku ya sita tangu amelazwa hospitalini hapo wazazi wake walipowasili.Aliwaeleza kilichotokea wote wakastuka sana.Hawakuwa na taarifa kwamba Patrick amefariki kwa sababu toka Happy alipoondoka na kwenda Marekani kusoma hawakuwahi kumtembelea tena Patrick gerezani kwa hiyo hawakuwa na taarifa zozote juu yake.Wazazi wake wakajitahidi kwa kila namna walivyoweza kujaribu kumliwaza binti yao ili aweze kurejea katika maishaya kawaida kwani alionekana kukata kabisa tamaa ya maisha.
* * * *
Wiki ya kwanza ikakatika bila ya Veronika kutokea.Patrick akaanza kupatwa na wasiwasi kwani Vero alimuahidi kuwa atakuwa akimtembelea karibu kila wiki.Alikuwa na hamu sana ya kutaka kupata walau ujumbe wowote toka kwa Happy kwani Vero aliahidi kufanya kila analoweza ili kurejesha mawasiliano kati yake na .Patrick alijipa moyo na kuendelea kusubiri.Wiki ya pili ikakatika hatimaye ya tatu na ya nne Vero akarudi Songea kwenda kumjulia hali Patrick.
Patrick alifurahi mno kumuona tena Vero.Vero naye alifurahi sana kumuona Patrick kijana ambaye amekuwa akimkosesha usingizi.Bila ya kupoteza muda Patrick akataka kufahamu kama kuna habari yoyote kutoka kwa Happy .
Veronika akamwangalia kwa sekunde kadhaa akakohoa kidogo kisha akasema
“Patrick nimekuja na habari Fulani ambazo si nzuri “
Patrick akastuka na kuuliza.
“habari gani hiyo Vero”
Vero akatulia kidogo kisha akaendelea
“Patrick nimechelewa kuja kukuona kama nilivyokuwa nimekuahidi lakini kilichonichelewesha ni suala hili hili la Happy .”CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Happy ? Kafanya nini tena? Patrick akauliza kwa hamaki
“Patrick you are strong I know but you need to be more stronger to hear this” Vero akasema
“Vero sikuelewi .Mbona unanichanganya?Go straight to the point” akasema Patrick
Vero akajiweka sawa akakaza sura ili asije onekana anadanganya
“Patrick ! Nilipiga simu chuoni kwa Happy kama tulivyokuwa tumekubaliana na nikaambiwa kuwa Happy alikuwa amehama chuoni hapo muda mrefu.Sikuchoka nikaomba nielekezwe alihamia chuo gani nikasaidiwa nikakipata chuo alichokuwa anasoma nikapiga simu na kweli nikampata lakini nilipojitambulisha tu kuwa nina ujumbe muhimu toka kwa Patrick akakata simu.Nilistuka sana lakini sikukata tamaa.Kwa muda wa siku mbili mfululizo nikawa napiga simu lakini haipokelewi.basi nikaamua kumtumia binamu yangu mmoja ambaye naye anasoma huko huko lakini chuo kingine tofauti na hiki cha Happy .Yeye akafanya uchunguzi wake na baada ya siku kama tano hivi akaniambia kuwa amefanikiwa kumfahamu Happy lakini kwa bahati mbaya Happy amepata bwana ambaye anaishi naye na inavyosemekana tayari ana ujauzito wa mzungu huyo.Niliumia mno nikapiga tena simu kwa hasira nikaongea naye bila aibu akanijibu hivi “ sitaki kusikia habari yoyote juu ya Patrick .Kama ni gerezani alitaka kwenda mwenyewe.mwacheni akae atatoka atatafuta maisha yake.Mimi nina mtu wangu kwa sasa na sitaki usumbufu hata kidogo na wala huko Tanzania sitegemei kurudi tena ..Halafu akakata simu.Nikaj………………..” Hakumalizia sentensi yake Patrick akaanguka chini na kupoteza fahamu.Vero akapiga kelele kuomba msaada na mara wakaja askari magereza na kumbeba Patrick na kumkimbiza katika zahanati ya hapo gerezani kwa ajili ya kumpatia huduma ya kwanza.
Veronika akachanganyikiwa na kijasho kikamtoka.Alijilaumu sana moyoni kwa kutunga uongo ule mkubwa kiasi cha kuhatarisha maisha ya wawili hawa waliopendana.Hakutegemea kama hali ingekuwa vile
Hatimaye miezi ikatika bila ya mawasiliano yoyote baina ya Patrick na Happy .Wakati Happy akiamini kuwa Patrick ni marehemu ,Patrick kwa upande wake yeye alikuwa bado ana hasira moyoni kwa kusalitiwa na Happy .Alijiona mjinga sana kwa kuyatoa maisha yake kwa mtu asiyekuwa na thamani kwake hata chembe.Alilia usiku na mchana kwa kitendo hiki cha Happy .Happy yeye alikuwa akimlilia Patrick kila siku.Kila alipoiona picha yake machozi hayakukauka.
Taratibu kila mmoja kwa upande wake akaanza kukubaliana na matokeo kuwa hayakuwa mapenzi ya Mungu wao kuwa pamoja.Kila mmoja akamweka mwenzie kama kumbukumbu ya pekee maishani.Pamoja na kukubali huko kuwa Patrick alikuwa amekufa lakini Happy alikuwa na dhamira moyoni ya kuja kulitafuta kaburi la Patrick na kutoa heshima zake kwa mtu pekee aliyempenda na kumthamini.
Wakati Happy akiwa na wazo la kuja kutembelea kaburi la Patrick pindi atakaporejea nyumbani Patrick yeye aliamua kumsamehe kwa maamuzi aliyoyafanya na kuamua kusonga mbele na maisha yake.Ingawa ni kitu ambacho kilimuumiza akili kila siku lakini alijitahidi aweze kumsahanu Happy na kuanza maisha yake mapya bila ya kiumbe huyu aliyempenda zaidi .
Ni katika wakati huu mgumu aliokuwa nao Patrick ndipo Veronika alipozidisha ukaribu wake kwa Patrick.Patrick kwa kiasi Fulani alishukuru sana kwa kufahamiana na Vero kwani yeye ndiye mfariji mkuu wake mkuu katika kipindi hiki kigumu alichokuwa nacho.Ni vero pekee ambaye anaonyesha kumuelewa na kumjali.Ukaribu wao ukaongezeka mara dufu na tayari kukaanza kuwa na kila dalili za kuibuka kwa uhusiano mzito baina yao.
“Vero ni msichana mrembo ,ambaye ni wazi anaonyesha ana mapenzi ya kweli.Vero amekuwa ndiye mtu wangu wa karibu.Ni yeye tu ambaye anaonyesha kunielewa na kunisaidia.Ni kwa sababu ya Vero leo hii maisha yangu hapa gerezani yamekuwa mazuri kwani ninaishi kama niko nyumbani.Mjomba wake Vero mkuu wa gereza ananijali mno na kunithamini.Yote hii ni kwa sababu ya Vero.Amenifanya nisijione mkiwa tena,ameniondolea lindi la mawazo mazito niliyokuwa nayo juu ya Happy .Vero amenisaidia kurudisha tena matumaini ya ndoto zangu ambazo tayari zilikuwa zimeanza kufutika,kwa haya yote aliyoyafanya Kwa nini basi nisimpe nafasi aliyokuwa nayo Happy ? Nilitambua toka awali kuwa Vero ananipenda lakini ikawa vigumu kuipata nafasi ndani ya moyo wangu kwa sababu wakati huo funguo ya moyo wangu alikuwa nayo Happy .Ninakubaliana na hisia zangu kuwa Vero ndiye msichana pekee ambaye anaweza kuliziba pengo la Happy “
.Patrick akawaza kwa kina sana juu ya suala hilo na akadhamiria kumtamkia wazi wazi Vero juu ya adhma yake ya kutaka wawe wapenzi.
* * * *
Ingawa alihuzunika sana kwa kusikia kuwa Patrick mpenzi wa Happy amefariki dunia kwa upande mwingine Mike Cambell alikuwa na furaha isiyo kifani kwani aliamini kuwa sasa ni nafasi yake ya pekee ya kuwa na Happy.Aliamini kuwa kwa sasa Happy hatakuwa tena na kisingizio cha kumkataa .Alihama toka New york city hadi Washington DC ambako Happy alikuwa akisoma.Lengo likiwa ni kujaribu kujenga ukaribu kati yake na Happy .
Taratibu akaanza kujenga mazoea na kuwa karibu na Happy na kumfariji kwa kumnunulia maua n.k.Yeye na dada yake Michelle wakajitahidi kwa kadiri walivyoweza katika kumfariji na kumuondolea Happy majonzi yasiyokwisha.Walitoka kila mwisho wa wiki na kwenda sehemu mbali mbali za kuvutia na burudani lengo likiwa ni kujaribu kumsahaulisha juu ya msiba wa Patrick.Baada ya miezi minne kupita tayari Happy alikwisha anza kurudia hali yake ya kawaida.Tayari ukaribu mkubwa ulikwisha jengeka kati yake na Mike kiasi kwamba hakusikia raha kupitisha siku bila kumuona kijana huyu ambaye ametokea kuwa mfariji wake mkubwa hasa katika kipindi hiki cha msiba mkubwa uliompata.
Pamoja na ukaribu huo uliojengeka baina yao bado ilikuwa ngumu kwa Happy kuitoa nafasi ya Patrick kwa mtu mwingine.Kwa mapenzi mazito aliyokuwa nayo kwa Patrick alikuwa radhi aishi peke yake kwa heshima ya kijana huyu.Suala hili liliendelea kumuumiza kichwa Mike kwa muda mrefu lakini hakukata tamaa.Alizidi kuonyesha mapenzi ya wazi na nia dhahiri ya kutaka kuwa na Happy .
Siku moja wakiwa katika klabu ya usiku Mike akaamua tena kumkumbushia Happy juu ya ombi lake la kutaka wawe wapenzi.
“Happy naomba kwanza nitangulize samahani kwa jambo ninalotaka kukueleza kwa sababu najua unaweza usilipende.” Akanyamaza kidogo huku Happy akimtazama kwa macho maangavu.
“Najua bado uko katika kipindi kigumu cha kufiwa na mpenzi wako.Kusema kweli ni kipindi kigumu kwetu sote kwa sababu wewe ni rafiki yetu wa karibu na hivyo huzuni yako ni yetu pia.Pamoja na yote yaliyotokea ambayo ni kazi ya Mungu,lakini maisha hayana budi kuendelea.Ninachokusihi ni kuyasahau yote yaliyotokea na kuanza maisha mapya” Akanyamaza akamtazama Happy usoni halafu akaendelea.
“Happy nimeona nikueleze tena kile nilichokueleza muda mrefu uliopita.Happy napenda kwa mara nyingine tena kukuhakikishia kuwa wewe ni mwanamke pekee ambaye umeweza kutua katika moyo wangu na kukataa kutoka kama vile nyuki anavyong’ang’ania ua lenye asali tamu..Toka mara ya kwanza nilipokutia machoni sura yako imejichora moyoni mwangu kiasi ambacho haitaweza kufutika kamwe.Happy nakupenda kupita ninavyojipenda mwenyewe.Naomba kwa mara nyingine tena unipe nafasi ndani ya moyo wako ya kuwa nawe.Ninaomba unipatie nafasi ya Patrick .Wewe ni mwanamke mrembo ambaye unahitaji mtu mwenye mapenzi ya dhati na ya kweli kama alivyokuwa Patrick.Siwezi kuwa kama Patrick lakini ninakuhakikishia kuwa upendo wangu kwako ni wa kweli na wa dhati .Niko tayari kufanya lolote lile katika dunia hii ilimradi tu niwe na wewe.Tafadhali Happy naomba unielewe ninaposema kuwa moyo wangu unateketea kwa penzi lako.Naomba unipe nafasi ndani ya moyo wako “
Mike akasema na kumtazama Happy ambaye alikuwa amenyamaza huku machozi yakimtoka kwa mbali.Akatoa kitambaa katika pochi yake akajifuta uso halafu akakaa vizuri na kusema
“Mike kwanza napenda kuchukua nafasi hii kukushukuru wewe na Michelle kwa kuwa watu wangu wa karibu.Sio siri mmenisaidia sana na hasa katika kipindi hiki kigumu nilichokuwa nacho.Bila uwepo wenu sijui ningekuwa katika hali gani.Mmekuwa na mimi katika kila hali,kila dakika.Mmefanya kila mliloweza kunifariji na mpaka leo hii ninaendelea vizuri.Sioni kitu cha kuwalipa zaidi ya maneno haya machache Ahsanteni sana.Kuhusu suala ulilonieleza ,naomba unipe muda wa kutosha wa kutafakari na kufanya maamuzi.Nitakapokuwa tayari nitakujibu”akasema Happy na Mike akamuelewa na hakutaka tena kuendelea kulionglea suala hilo.
BAADA YA MIAKA MITANO
Hatimaye siku iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu ikawadia.Ni siku ambayo Patrick alihitimisha adhabu yake ya kutumikia miaka mitano gerezani.Tangu asubuhi ya siku hiyo Patrick alikuwa ni mtu mwenye furaha sana.Aliwaaga wafungwa wenzake wote huku akiwa mwingi wa tabasamu.Wakati Patrick akiwa mwingi wa furaha kwa upande mwingine ilikuwa ni simanzi gerezani kwa kuondokewa na kijana kama huyu ambaye alipendwa karibu na kila mtu.Alikuwa mstari wa mbele katika kuwapa moyo na kuwafariji wale wenzake waliokata tamaa,vile vile alikuwa ni kiungo kikubwa katika kuwasaidia wenzake kupata vitu kama sigara,sabuni n.k kwa sababu yeye muda mwingi alikuwa akishinda nyumbani kwa mkuu wa gereza hivyo kuvipata vitu hivyo kwake ilikuwa rahisi..Kuondoka kwake lilikuwa ni pigo kubwa kwa wale wafungwa waliokuwa wakimtegemea .
Saa tatu na nusu juu ya alama Patrick aliitwa katika ofisi ya mkuu wa gereza ambako alitaarifiwa rasmi kuwa kuanzia muda huo alikuwa huru.Aliombwa awe raia mwema huko aendako ili asije rudishwa tena gerezani.Hii ilikuwa ni kama ndoto.Hakuamini hadi pale mkuu wa gereza alipompa mkono na kumwambia kuwa yuko huru na kumtakia kila la heri katika maisha yake .
Katika lango la kuingilia gerezani kundi kubwa la watu likongozwa na wazazi wa Patrick lilikuwa likimsubiria kwa hamu kubwa.Walikuwepo ndugu na baadhi ya rafiki zake akiwemo rafiki yake Andrew ambaye walikutana hapo hapo gerezani lakini yeye aliwahi kutoka.Alikuwepo pia binti mrembo ambaye urembo wake leo hii ulizidi mara dufu.Alikuwa amependeza zaidi ya maelezo.Huyu ni Veronika ambaye yeye pamoja na ndugu zake na mama yake waliungana na familia ya akina Patrick katika kusherehekea tukio hili kubwa .Tayari Patrick na Vero walikwisha kuwa wapenzi na urafiki wao ulikuwa na baraka ya pande zote mbili yaani upande wa akina Patrick hali kadhalika mama na ndugu zake Veronika hawakuwa na kipingamizi chochote juu ya urafiki huu.
Taratibu lango likafunguliwa na Patrick akaruhusiwa kutoka nje akiwa huru.Alitumia sekunde kadhaa kulitazama gereza hilo ambalo amekaa takribani miaka mitatu.
Huku akitiririkwa na machozi mama yake alikuwa mtu wa kwanza kumkumbatia mwanae,kisha wakafuata wengine wote waliokuwapo hapo .Zilikuwa ni dakika chache zenye furaha kubwa .Wote wakapanda katika magari yaliyoandaliwa na kuanza safari ya kuelekea Dar .Patrick alipanda katika gari maalum lililokuwa likiendeshwa na Andrew rafikiye mkuu pamoja na mfariji wake na hatimaye mpenzi wake ,Veronika.ambaye kwa sasa alikuwa ni kila kitu kwake .
Ndani ya gari Patrick na Vero walikuwa wamekumbatiana wote wawili machozi yakiwatoka.Patrick alikumbuka toka alivyoonana na Vero siku ya kwanza,wakazoeana na kuwa marafiki na hatimaye kwa sasa ni wapenzi.Alimshukuru sana Mungu kwa kumrudishia furaha iliyokuwa imepotea baada ya kumpoteza Happy .Mwanzoni aliamini kuwa Happy ndiye ilikuwa furaha yake lakini baada ya Happy kuondoka akatokea Vero na kuirudisha tena furaha hiyo.Veronika alionyesha mapenzi ya kweli na uvumilivu mkubwa katika kipindi chote walichofahamiana mpaka leo.
“Veronika nashukuru sana kwa yote uliyonifanyia.Nashukuru kwa upendo wa ajabu ulionionyesha”Akasema Patrick kwa kunong’ona.
“ahsante pia Patrick kwa kuufungua moyo wako na kunikubali .Najiona ni mwenye bahati sana kuwa na mtu kama wewe.” Akasema Veronika.
* * * *
Hatimaye Happy naye baada ya kumaliza masomo yake akarejea nyumbani Tanzania.Toka akiwa safarini alikuwa na shauku moja tu ya kutaka kufahamu mahala alipozikwa Patrick .Tayari alikwisha kuwa na mahusiano ya kimapenzi na Mike cambell.Alikubali kumpa nafasi Mike baada ya kuamini kwamba Patrick hatarejea tena.
Familia yake yote ilikuwepo uwanja wa ndege kumlaki.Tayari baba yake alikwisha staafu kazi na sasa familia yote inaishi jijini Dar es salaam.Happy alipata mapokezi makubwa sana toka kwa familia yake.
Siku tatu tu baada ya kuwasili nchini Happy akafunga safari hadi mjini Sumbawanga ambako ndiko Patrick alikuwa akiishi mwanzo.Kule alitaarifiwa kuwa familia ya akina Patrick ilikwisha hama muda mrefu na walihamia jijini Dar es salaam. Hakukata tamaa akaondoka na kuelekea Iringa katika gereza ambalo Patrick alikuwa amefungwa mwanzo.Lengo lilikuwa ni kupata ukweli juu ya kifo cha Patrick.Pale gerezani alitaarifiwa kuwa Patrick alihamishwa na kupelekwa katika gereza jipya huko Songea.Pale gerezani hawakuwa na kumbukumbu naye zozote.
Happy hakukata tamaa akafunga safari tena hadi Songea katika gereza jipya ambako ndiko Patrick alihamishiwa.Pale akaonana na mkuu wa gereza na kumweleza kilichompeleka.Mzee Joel ambaye ni mjomba wa Veronika akamwangalia kwa mstuko .
“wewe ndiye Happy kibaho? Akauliza baada ya kuikumbuka historia ya Patrick
“Ndiye mimi mzee “Happy akajibu
Mzee Joel akamtazama kwa makini na kuuliza
“Happy nimefurahi kukuona.Niliwahi kusikia habari zako toka kwa Patrick.Nimeshangaa kwa wewe kuja kumuulizia Patrick hapa gerezani ina maana hamkuwa mkiwasiliana wakati ukiwa masomoni?
“Tulikuwa tukiwasiliana lakini mawasiliano yakakata ghafla sana na siku moja nikapokea taarifa kuwa Patrick alifariki kwa ugonjwa wa kuhara akiwa gerezani.Baada ya kurejea nyumbani nimeona nitafute kwanza taarifa sahihi za kifo chake na nifahamu mahala alikozikwa.Nimeelekezwa kwamba alihamishiwa katika gereza hili”
Mkuu wa gereza akstuka sana alipopata taarifa ile inayohusiana na kifo cha Patrick .Kwa kiasi fulani taarfa ile ikamchanganya kwa sababu kwa mujibu wa taarifa aliyoipata toka kwa Vero ni kwamba Happy akiwa masomoni nchini Marekani alipata bwana mwingine na kuolewa naye na kumsahau Patrick kitu kilichopelekea Patrick ampe nafasi Veronika.
Mzee Joel akakaa kimya akitafakari kisha akasema
“Happy kwanza nakupa pole sana kwa yote yaliyotokea kati yako na Patrick.Ni kweli Patrick alihamishiwa katika gereza hili akitokea Iringa.Patrick alikuwa ni mmoja kati ya wafungwa bora kabisa ambaye hajawahi kutokea katika gereza hili.Alipendwa na kila mtu hapa gerezani.Alikaa hapa gerezani hadi alipomaliza kifungo chake na kuachiwa huru.Hapa gerezani alitoka salama salimini .Kama ni kufariki basi atakuwa amefariki baada ya kutoka hapa kwa sababu mimi ndiye niliyeidhinisha kuachiwa huru baada ya kumaliza kifungo chake.”
Maneno yale yakamfanya Happy atetemeke mwili .Aliinama chini akashindwa kuyazuia machozi kumtoka.Hakuyaamini maneno yale ikambidi aulize tena.
‘Mzee sijakuelewa vizuri.Umesema nini?
“Nimesema kuwa Patrick alimaliza kuitumikia adhabu yake akiwa mzima wa afya na mimi kama mkuu wa gereza hili ndiye niliyemuachia huru baada ya kumaliza kifungo chake.Kama ni kufariki basi alifariki baada ya kutoka hapa gerezani.Nasikitika sana kwa kumpoteza kijana kama yule.” Akasema mkuu wa gereza.
“mzee mbona taarifa niliyoipata mimi inasema kwamba Patrick alifariki akiwa gerezani? Tena inasema kuwa alifariki kwa maradhi ya kuhara? Happy akasema huku machozi yakimdondoka
“Taarifa hiyo ulipewa na nani? Mkuu wa gereza akauliza
“Taarifa hiyo nilitumiwa na mtu nisiyemfahamu akidai kuwa yeye anamfahamu Patrick kwa sababu aliishi jirani na wazazi wake kule Sumbawanga.Dada huyo alisema kwamba familia ya Patrick haikuweza kunifahamisha juu ya msiba wa mtoto wao kwa madai kwamba nilimtelekeza mtoto wao gerezani nikaenda kusoma ulaya,wakati yalikuwa ni makubaliano yetu mimi na yeye.Sikutaka kumwacha Patrick peke yake na mimi nikaenda kusoma Marekani,lakini ni Patrick huyo huyo ndiye aliyenishawishi nikubaliane na uamuzi wa baba wa kunipeleka Marekani kusoma.”akasema Happy
“Pole sana Happy.Jipe moyo.Haya ni mambo ya kawaida Jitahidi sana uyaruhusu maisha yako yaendelee.”Mkuu wa gereza akasemaCHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Nashukuru sana mzee kwa msaada ulionipa.Japokuwa bado kuna utata mkubwa juu ya kifo hicho lakini namuachia Mungu.Kama amekufa kweli nitamuombea kwa Mungu apumzike kwa amani lakini kama hajafa kweli huko aliko atambue kuwa maumivu anayonisababishia ni makubwa kiasi ambacho siwezi kuelezea.”
Happy akaagana na mkuu wa gereza ,akapanda gari lake na kuondoka huku machozi yakiendelea kumtoka.Akashindwa kuendesha gari akaegesha pembeni akainamia usukani.
“ Nina kila sababu ya kuamini kuwa Patrick hajafa.Kutokana na maelezo ya mkuu wa gereza ni kwamba Patrick alimaliza kifungo chake na kutoka gerezani salama.Na katika ile barua niliyoandikiwa ilisema kwamba Patrick alifariki akiwa gerezani.Mbona mambo haya yananichanganya? Je Patrick alinifanyia hila nijue kuwa amekufa? Kama ni kweli hajafa kwa nini basi amenifanyia hivi??”Happy akajiuliza huku akiupiga usukani kwa hasira. .
“Nilimkosea nini Patrick hadi akaamua kunidanganya na kuniacha niteseke miaka yote hii?Moyo wangu hauna furaha hata kidogo yote hii ni kwa ajili yake .Au labda kitendo cha mimi kuondoka kwenda kusoma Marekani hakikumfurahisha?Anyway nitakutafuta Patrick hata kama itanigharimu maisha yangu I promise I’ll find you because you left me at the time I needed you most “
Miaka sita sasa imekwisha pita toka Patrick toke gerezani na tayari Patrick amekwisha maliza shahada yake ya kwanza ya uandishi wa habari na tayari ni mwajiriwa katika kituo kimoja kikubwa cha Televisheni nchini.
Pamoja na kwamba ni muda mrefu umepita lakini picha ya Happy bado haijafutika kabisa moyoni mwake.Huja na kufutika na wakati mwingine humuacha katika huzuni kubwa.
Uhusiano kati yake na Vero umekomaa ukakubaliwa na ndugu wa pande zote mbili na hatimaye ukafikia hatua ya uchumba .Aliamua kumvisha pete ya uchumba Vero baada ya kuamini kuwa tayari Happy hakuwa na nafasi tena katika maisha yake.Aliamini Vero ndiye mwanamke pekee aliyepewa na Mungu ili awe mke wake.Vero ndiye aliyekuwa naye katika kipindi kirefu cha mahangaiko,Vero amemsaidia kufuta majeraha ya moyo na kuanza maisha mapya,Vero amekuw ani kila kitu kwake.
Kwa upande mwingine baada ya Happy kugundua kuwa Patrick hakufa gerezani na kuamini kuwa bado yu hai alikumbana na shinikizo kubwa toka kwa wazazi na ndugu zake la kutaka amsahau kabisa kijana huyu na kuolewa na Mike cambell ,kijana mmarekani mweusi ambaye mapenzi yake kwa Happy hayana kifani.Mike amekuwa ndiye mfariji mkubwa wa Happy toka alipopata taarifa kuwa Patrick amefariki dunia.Ni yeye na dada yake Michelle ndio walioweza kumfuta Happy machozi aliyokuwa akilia kila uchao akimlilia Patrick.Ni Mike ndiye aliyejitolea kila alichoweza kukifanya kuhakikisha binti huyu mwenye uzuri uliotukuka anarejea katika maisha ya kawaida.Pamoja na ugumu uliokuwepo wa Happy kumsahau Patrick lakini Mike alivumilia na kuamini kuwa iko siku Happy atamsahau Patrick na yeye kupewa nafasi ndani ya moyo wa binti huyu mwenye sura ya kimalaika..Hatimaye baada ya kujishauri kwa muda mrefu akaamua kumkubali Mike awe mpenzi wake na bila kupoteza muda akakubali kuvishwa pete ya uchumba na Mike Cambell katika sherehe kubwa iliyohudhuriwa na umati wa watu.
Pamoja na kuamini kuwa Patrick hakuwa ridhiki yake,kitu kilichompelekea akubali kuvishwa pete ya uchumba na Mike lakini bado Happy alikuwa na kitu moyoni juu ya Patrick.Kuna kitu ambacho hakuweza kukifuta moyoni mwake.Na hiki kilizidi kumtesa siku hadi siku licha ya kujitahidi kwa kadiri alivyoweza kumsahau Patrick.
********************
Veronika akamtazama Patrick kwa macho makali na tayari akagundua kuna kitu kinachomsumbua mpenzi wake.Kilichomuumiza roho zaidi ni kwa nini kama Patrick ana tatizo asimwambie?
Akapanda kitandani na kukaa karibu ya Patrick akamkumbatia .
“Patrick mpenzi kwa siku chache sasa nimegundua mabadiliko Fulani kwako.Hauko kawaida.Kuna jambo gani linalokusumbua hebu niambie mpenzi wangu.Unajua ninapokuona katika hali hiyo hata mimi ninapata wasiwasi mwingi.Nimezoea kuiona sura yako iliyojaa tabasamu kila wakati lakini kwa sasa unajilazimisha kutabasamu na unaonekana u mwingi wa mawazo.Au kuna kitu nimekuudhi Patrick?
Aliongea maneno haya taratibu machozi yakimlenga hali kichwa chake amekilaza kifuani kwa Patrick
“Vero mpenzi hakuna jambo lolote linalonisumbua.Nahisi ni hizi dawa ninazotumia ndiyo zinanifanya niwe katika hali hii lakini usijali si muda mrefu nitarudia hali yangu ya kawaida.”Akasema Patrick huku akimsugua Veronika mgongoni.
“Patrick mimi ni mchumba wako na nimekuwa karibu nawe kwa muda mrefu sasa.Sidhani kama kuna mtu mwingine anayekufahamu kiundani zaidi yangu.Nina imani kabisa kuna kitu kinakusumbua akili yako .Nina jua kabisa ni wakati gani unakuwa na furaha na ni wakati gani unakuwa na matatizo.lakini sikulazimishi kuniambia.Kama unaona tatizo hilo halina ulazima wa mimi kulijua basi hakuna neno.Ila kumbuka muda wowote utakapohitaji msaada wangu nipo tayari kukusaidia.”
Vero akambusu Patrick kisha akatoka nje.
Saa saba za usiku Patrick akastuka toka usingizini .Vero alikuwa pembeni yake amelala .Akamwangalia mpenzi wake kwa dakika kadhaa.akapatwa na uchungu mwingi baada ya kuyaona mapenzi makubwa aliyokuwa nayo binti huyu kwake.
“Ni wazi vero amekuwa ni msichana wa pekee maishani mwangu ambaye ameweza kunionyesha mapenzi ya kweli na kunisaidia kupata uelekeo mpya wa maisha yangu.Nampenda Vero na nina imani ndiye mwanamke atakayenifaa maishani.lakini huyu Happy ……………mhhh …naye kajitokeza tena katika hatua za mwisho kabisa za kukamilisha ndoa yangu na Veronika.Yes ! nilimpenda Happy kuliko kitu chochote kile lakini alinitenda kitu kibaya nikamwondoa katika moyo wangu.Lakini ni kwa nini siachi kumuwaza ?Kila dakika sura yake inanijia akilini….ooh Mungu wangu nisaidie katika mtihani huu mguu nilionao.Lakini pamoja na yote yaliyotokea baina yetu lazima nimtafute Happy .Ni lazima nionane naye .Lazima nifahamu ni kwa nini alinitenda vile?
Patrick akamtazama tena vero akamkumbatia kwa nguvu.
Asubuhi na mapema aliamka akaoga kisha akamuaga Happy kuwa anakwenda kumuona Andrew.Vero hakuwa mbishi akamwacha aende
Akiwa ndani ya gari Patrick alijaribu tena kupiga ile namba ya simu ambayo aliamini kabisa itakuwa na uhusiano Fulani na Happy lakini bado ikawa haipatikani.
“Yawezekana labda alipopiga simu jana mchana ikapokelewa na Vero ,walitoleana lugha chafu .Pengine labda walitukanana ,kitendo kilichomfanya akasirike na kuizima kabisa simu yake.”
Akawasili nyumbani kwa Andrew mishale ya saa moja na dakika ishirini hivi
“ooh Patrick mbona asubuhi hivi.Kuna usalama kweli? Akauliza andrew kwa shauku ya kutaka kufahamu kama kulikuwa na tatizo lolote.
“Si kwema andrew” akasema Patrick huku akiketi sofani.
“Enhe ! kulikoni ? Akauliza tena Andrew
Patrick akatulia kidogo akavuta pumzi kisha akasema
“mambo katu si mazuriAndrew.Jana mchana mimi nikiwa nimelala mtu ambaye nahisi atakuwa ni Happy akalipiga simu ,basi si ikapokelewa na Vero?
“Mhh usiniambie Patrick.Enhee ikawaje? Andrew akauliza huku akionyesha hali Fulani ya mstuko
‘Sasa sielewi waliongea nini kwa sababu kwa mujibu wa maelezo ya Vero ni kwamba mtu huyo hakuongea chochote.Nikajaribu kupiga mimi mwenyewe simu ikapokelewa na sauti niliyoisikia ni dhahiri ni ya Happy .Sidhani kama ninaweza kuipotea sauti yake japokuwa hatujaonana kwa kipindi kirefu.Baada tu ya kuitikia akakata simu na kuizima kabisa na hadi muda huu tunapoongea simu yake haipatikani.Nimechanganyikiwa Andrew sijui hata nifanye nini ndio maana nimekuja hapa kwako asubuhi hii ili tuone tufanye kitu gani.”
Andrew akavuta pumzi ndefu akasimama na kuzunguka zunguka humo sebuleni kisha akasema.
“Patrick hata mimi naanza kuhisi kuwa kuna kitu waliongea na Vero ambacho kimemfanya awe na hasira na asitake tena hata kuiwasha simu yake.lakini bado hatuna haja ya kukata tamaa,kitu tunachotakiwa kukifanya kwa sasa ni kutafuta mahala anapoishi Happy .kazi hiyo niachie mimi nitaifanya kikamilifu.Baada ya kupafahamu anapoishi itakuwa rahisi kwetu kumpata”
‘Ahsante sana Andrew kwa kunisaida.” Baada
ya dakika chache za maongezi Patrick akaaga na kiondoka.
***************
Happy alistuliwa toka katika usingizi mzito na hodi iliyogongwa mlangoni.Alijiinua kiuchovu na kuangalia saa.Ilikuwa ni saa nne asubuhi.
“Mhh ! dada mbona umelala hivyo? Mi nimepatwa na wasiwasi pengine unaumwa.” Akasema Margreth.Happy hakujibu kitu akageuka na kukaa tena kitandani huku akiyafikicha macho yake ambayo kwa sasa yalionyesha hali ya kuvimba kutokana na kulia kwa muda mrefu.
“Happy hebu niambie kitu gani tena kinakufanya uwe katika hali hiyo? Na Patrick vipi ulimpigia simu?
“Ah ! acha tu Margreth.Nilimpigia simu lakini ikapokelewa na mwanamke.Nilishindwa kuongea jambo lolote nikakata simu.nahisi Patrick tayari atakuwa ameoa”
Happy akashindwa kuvumilia machozi yakamtoka.
“Hebu nisikilize dada.Hupaswi kulia.Ninaimani hizo ni hisia zako tu kwamba Patrick tayari ana mke.Huwezi jua pengine labda ni ndugu yake ,dada yake au hata katibu muhtasi wake.hata hivyo ni muda mrefu sasa umepita toka mlipopotezana na mlipotezana katika mazingira yenye kutatanisha sana huku kila mmoja akiwa bado anampenda mwenzake,nina imani kabisa kuwa pendo lile bado liko hai.Najua ndio maana unahisi kuumizwa na hisia kuwa Patrick tayari ana mke kwa sababu bado unampenda.Yawezekana labda atakuwa ameoa au pengine ana mchumba lakini hilo lisikupe shaka.Tutalifahamu muda si mrefu.”
Maneno yale ya Margreth yanampa moyo sana Happy .
“nashukuru sana mdogo wangu kwa kunifariji.Pamoja na hayo naomba tafadhali hii iwe ni siri yako na asijue mtu mwingine yeyote yule.”
“Usijali Happy Hakuna mtu yeyote atakayefahamu juu ya Patrick.leo nataka nimfuate Patrick ofisini kwake kama hii kadi yake ya biashara inavyoonyesha.”
***************
Saa tano na nusu ilimkuta Margreth katika jengo lenye ofisi anakofanyia kazi Patrick .Akashuka garini na na kupanda lifti kuelekea ghorofa ya saba ziliko ofisi hizo alizokuwa akizitafuta.
Aliposhuka tu katika lifti akakutana na bango kubwa linaloelekeza zilipo ofisi hizo.Taratibu na kwa mwendo wa madaha kama ilivyokawaida yake alifika mpaka katika chumba cha mapokezi akakutana na akina dada wawili warembo,Akajitambulisha na kuoma kuonana na Patrick.
“Patrick kwa sasa yuko mapumzikoni nyumbani kwake.Alipatwa na matatizo ya moyo hivi karibuni hivyo amepewa muda wa kupumzika .Labda tukuelekeze nyumbani kwake kama kuna ulazima wa kumuona yeye mwenyewe ”
Margreth akaelekezwa nyumbani kwa Patrick kisha akaaga na kuondoka.
Ilimchukua kama masaa mawili hivi kuipata nyumba ya Patrick.Kwa mujibu wa ramani aliyopewa alitumaini pale palikuwa ni penyewe kabisa.Taratibu akalisogelea geti kubwa la mbele na kubonyeza kitufe cha kengele.Baada ya kama dakika nne hivi dada mmoja mrembo ,aliyevalia nadhifu akafungua mlango.
“Karibu dada” Yule dada akasema
“ahsante sana” Margreth akajibu
“sijui nikusaidie nini?
“Samahani dada ,sijui hapa ndio nyumbani kwa Patrick?
“Yes ndio hapa.Una shida naye ?
“Yes nina shida naye ya kiofisi.Kuna mzigo wake ulipitia katika ofisi zetu.Baada ya kuona kimya kingi tukaona tumtafute.Nimekwenda ofisini kwake wakanieleza kuwa Patrick ni mgonjwa na wakanielekeza hapa nyumbani kwake.”
“Kweli dada ,Patrick ni mgonjwa ana wiki ya pili sasa anamumwa.Ana matatizo ya moyo kwa hiyo amepewa muda mwingi wa kupumzika.Hivi tunavyoongea amelala lakini ninaweza kumwamsha kama kuna ulazima wa kuonana naye sasa hivi.”
“Usijali dada ni masuala madogo tu ya kiofisi hivyo sioni kama kuna haja yoyote ya kumsumbua mgonjwa.Ila atakapoamka mwambie kuwa Margreth Kibaho alifika hapa.”
“Sawa dada Margreth karibu sana.Mimi naitwa Veronika.karibu basi hata ndani upate walau glasi ya maji.”
“Nashukuru sana dada Vero siku nyingine nitaingia ndani.Haya kwa heri”
Margreth akaondoka maeneo hayo huku kichwa chake kikiwa kizito mno kwa mawazo aliyokuwa nayo.
“Je yawezekana kweli Patrick akawa na mke?Inawezekana Vero akawa ndiye mke wa Patrick?Sasa nimepata picha kamili.Naona siku ile Happy alipopiga simu ya Patrick ikapokelewa na Vero na ndio maana akashindwa kupata kitu cha kuongea.Ok nitamshauri tujaribu tena kumpigia Patrick leo jioni.Aliwaza Margreth akiwa katika kurudi nyumbani.
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Saa kumi na moja jioni Margreth akarejea nyumbani kwao na mtu wa kwanza kukutana naye alikuwa ni mama yake ambaye akamwita na kumuuliza
“margreth ,naomba unieleze kwa undani bila kunificha ni kitu gani kinachomsumbua dada yako?Nina imani ni lazima utakuwa unafahamu kinachomsumbua dada yako.Kutwa nzima amejifungia ndani,hajala kitu na wala hataki kuonana na mtu yeyote.wakuu wake wa Miss Tanzania wamekuja kuonana naye leo hii mchana lakini ameshindwa kuonana nao.na hata waandishi wa habari wamekuja kutaka kumuhoji lakini hao ndio kabisaaa hataki hata kuwasikia.Sasa hebu niambie kitu gani kinachomsumbua mwenzio?
“Mama hakuna jambo lolote alilonieleza mimi.Nimekuwa nikijaribu toka jana kumshawishi ili anieleze ni kitu gani kinachomsumbua lakini amekuwa mgumu kunieleza.Ni wazi hata mimi naona kuna kitu kinamtatiza .naomba uniachie kazi hiyo mama nitajitahidi kumdadisi.”
“sawa Margreth jitahidi mwanangu.hali ya dada yako si nzuri na inatia shaka.”
“tena mama nipeni chakula nimpelekee nitamkoroga mpaka atakula tu.”
Haraka haraka akapewa sinia la chakula na kwenda hadi mlangoni kwa Happy .Akasimama hapo mlangoni kwa takribani dakika moja akatega sikio na kwa mbali akaisikia sauti ya Happy akilia.Aliumia sana moyoni mwake kuona jinsi dada yake anavyoteseka namna ile kwa sababu ya mapenzi.
Akagonga mlango kisha taratibu mlango ukafunguliwa akaingia ndani.Ni wazi Happy alionyesha hali ya kukata tamaa kwa jinsi alivyosawajika.Macho yalikuwa yamemvimba kwa kulia.
“Happy jaribu kuwa jasiri dada yangu.Unajua mambo yanaweza kuwa magumu zaidi iwapo hautaonyesha ujasiri .Hebu kwanza nyamaza kulia ule chakula.Mama anawasiwasi sana juu yako.”
Happy akamtazama mdogo wake usoni kisha akasema
“Najua ni rahisi kutamka hivyo kwa sababu wewe hayajakukuta.Ungekuwa katika mahala pangu , sijui ungefanya nini.Huwezi jua ni maumivu kiasi gani niliyonayo moyoni .Naumia sana Margreth.Patrick amekitonesha tena kidonda kilichokuwa kimeanza kupona.”
“Ok Dada Happy tulia basi ule halafu nikwambie habari za leo”
“Hebu nieleze kuna habari gani huko utokako? Akauliza Happy
Margreth akavuta pumzi ndefu akajiweka sawa na kusema.
“Nilipotoka hapa nikaelekea moja kwa moja katika zilizo ofisi za Patrick kwa mujibu wa wa hii businesscard inavyoonyesha.Nilifika katika ofisi hizo na nikaambiwa kuwa Patrick hayupo anaumwa .amepatwa na mstuko wa moyo na hivyo yuko nyumbani kwake anapumzika.Wakanielekeza nyumbani kwake nikaenda nikamkuta dada mmoja anaitwa Veronika .Akanikaribisha ndani na kutaka kwenda kumwamsha Patrick lakini sikuingia ndani nikamuachia ujumbe kuwa akiamka amwambie kuwa nilifika pale.Kwa ufupi ndiyo hivyo.” Akasema Margreth.
Happy alibaki ameshika tama asiamini alichokisikia kutoka kwa Margreth.Kilichomfanya anyong’onyee ni kusikia kuwa Margreth alikuta msichana pale nyumbani kwa Patrick.
“Najua kabisa huyu ndiye aliyeipokea simu siku ile nilipopiga.Yawezekana akawa ni mke wake? Au mchumba wake? Ni lazima nimpate Patrick ili nipate ukweli toka kwake.Yes ni muda mrefu umepita lakini…….”Alikuwa katika mawazo mazito wakati simu ya Margreth ilipolia.Alikuwa ni Mike Camble mchumba wa Happy .
“Ni mike” Akasema Margreth huku akimtazama Happy.
“Mwambie sipo “ Akasema Happy huku amejishika kichwa.
Alichanganyikiwa ghafla.Tayari alikuwa amekwishaanza kukubali matokeo kuwa Mike ndiye mtu wa maisha yake lakini Ghafla sana ametokea Patrick na kumfanya Happy achanganyikiwe.Margreth akaweka sauti kubwa ili Happy asikie watakachoongea.
“hallow Mike”
“hallow margreth mambo vipi?
“safi tu Mike habari ya huko?
“Huku kwema vipi huko?
“Huku nako kwema tu”
“Hebu niambie Margreth mbona Happy simpati katika simu?Nimejaribu sana kuitafuta simu yake lakini haipatikani kabisa.nilipata taarifa kuwa amefanikiwa kulitwaa taji la Miss Tanzania lakini akapatwa na mstuko akaanguka na kupoteza fahamu.Mara ya mwisho alinipigia simu kabla hawajaanza mashindano toka hapo sijapata mawasiliano yoyote toka kwake.Hebu nieleze margreth nini kimetokea?
Margreth akamtazama Happy kisha akasema
“Happy alipatwa na mstuko kidogo baada ya kutangazwa mshindi.Lakini kwa sasa anaendelea vizuri.Kuhusu mawasiliano ni kwamba simu yake bado hata hakumbuki aliiweka wapi ngoja kwanza atulie kabisa atakupigia Mike”
“Ok nimekuelewa margreth upo karibu naye hapo walau niongee naye kidogo?
“Hapana niko mbali naye kwa sasa.Labda ujaribu kupiga tena baadae”
“Ok margreth nimeomba wiki mbili za dharura ili niweze kuja Tanzania kukaa naye katika kipindi hiki kigumu alichonacho.Kesho nitaanza safari.Lakini usimwambie chochote .Nataka nimshangaze kidogo.Nitakujulisha kabla sijaanza safari yangu.
“Ok Mike bye”Margreth akajibu na kukata simu.
Happy alijilaza kitandani mikono ikiwa kichwani.
“why me ?Nampenda Mike .Yes nimeshakubali kuvishwa pete ya uchumba na Mike sasa ni kwa nini Patrick ametokea na kufanya akili yangu iyumbe namna hii?
Happy alijikuta tena katika mtihani mgumu.Ni wazi alimpenda Mike lakini baada ya kutokea Patrick taratibu ameanza kuonyesha dalili za kuanza kumsahau Mike..
*************
Saa kumi na moja jioni Patrick akaamka na kumkuta Veronika amekaa pembeni ya kitanda.
“Unajisikiaje mpenzi? Vero akauliza
“najisikia vizuri dear”
Vero akasogeza karibu meza ndogo iliyokuwemo humo chumbani na kumuandalia Patrick kinywaji.
“My dear wakati umelala kuna dada mmoja alikuja kukutafuta.Lakini nilimwambia kuwa umelala na hakutaka kukusumbua.Akasema kwamba nikikutajia jina lake utakuwa umemfahamu.”
“ Alisema anaitwa nani?Patrick akauliza kwa shauku
“Margreth kibaho”Vero akajibu
“whaaat !!!!!!!!!!!!!....”
“Margreth Kibaho” Vero akarudia tena
Patrick akasimama na kujishika kiuno
“Veronika una uhakika na unachokisema? Patrick akauliza
“Kwani vipi Patrick mpenzi wangu kuna tatizo gani?hayo ndiyo maagizo aliyoyaacha yeye mwenyewe.” Vero akajibu kwa wasiwasi
“Oh My god ! Margreth came here ? Alikuwa na nani? Patrick akauliza huku akiwa bado amepatwa na mshangaoCHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“alikuwa peke yake”
Patrick akakaa tena kitandani .Vero akastushwa na hali ile aliyoipata Patrick ghafla akamsogelea na kumkumbatia.
“My dear Patrick tafadhali niambie kuna kitu gani kinachokusumbua”
“Hakuna kitu Veronika.”Patrick akajibu
Patrick akainuka na kumwacha Vero pale kitandani.
“Vero naenda kwa andrew.Yeyote atakayekuja kunitafuta anisubiri sintakawia sana” Akasema Patrick huku akivaa shati lake.
‘Patrick ngoja basi nikusindikize kwa hali hiyo huwezi endesha mwenyewe.”Vero akasema hali machozi yakimlenga lenga
“Vero hakuna matatizo ninaweza kuendesha”
Haraka haraka aktoka ndani akaingia garini na kuondoka kwa kasi akimwacha Veronika amesimama mlangoni akimwangalia kwa uchungu.
************
“Patrick kuna tatizo gani best? Aliuliza Andrew baada ya kumuona Patrick jinsi alivyosawajika
“Uuuuuph ……………” Patrick akapumua kwa nguvu na kujitupa sofani
“Mambo yanazidi kuwa magumu Andrew”
“Kwani kumetokea nini Patrick?
“Margreth alikuja nyumbani”Patrick akasema
Andrew akamtazama Patrick kwa makini sana.
“margreth amekuja nyumbani kwako? Alikuja kukueleza nini?Andrew akauliza
“ Nilikuwa nimelala hivyo sikuweza kuonana naye.Alionana na Vero na kumwachia maagizo kuwa nikiamka aniambie kuwa alifika pale.Nahisi atakuwa alikuja na ujumbe wa muhimu sana.I’m confused”
Kimya kizito kikatanda hapo sebuleni kila mmoja alikuwa akiwaza lake.Ghafla wote wakastushwa na mlio wa simu ya Patrick.Akaitoa mfukoni na kuangalai namba za mpigaji.Zilikuwa ni namba ngeni kabisa katika simu ya Patrick.
“ Hallooo” Akaita Patrick.
“Halloo naongea na nani? Ikauliza sauti ya upande wa pili ambayo ilikuwa ni sauti tamu ya kike.
“ Patrick hapa”
“Uuuh Patrick .margreth hapa.”
“margreth??? Patrick akauliza kwa mstuko
“Yes margreth Kibaho”
“I cant believe it.magreth ni wewe kweli??
“Yeah its me margreth”
“ sikiliza Patrick ni hivi ,nilikuja nyumbani kwako leo mchana ulikuwa umelala nikamkuta dada mmoja anaitwa Veronika.Pole sana kwa muumwa”
“Yah vero aliniambia kwamba ulifika nyumbani kwangu”Patrick akasema
“Kwa ufupi shida yangu iliyonileta ni kuongea na wewe.nahitaji sana kuonana na wewe mapema iwezekanavyo.Kwa hiyo kama upo tayari nijulishe ili nikutaarifu tuonane lini na wapi”
“Yes margreth nipo tayari,nipo tayari hata sasa hivi,we se…,” hakumaliza sentensi yake Margreth akadakia
“Ok Patrick nitakutumia ujumbe kukufahamisha ni wapi tutaonana”
“Sawa Margreth lakini hebu nipe habari za Hap……”Kabla hajamalizia sentensi yake margreth akasema
“Patrick I have to go.See you ” akakata simu
Zilipita dakika mbili toka margreth akate simu ,lakini Patrick bado alikuwa ameishikilia simu yake sikioni.
“Hebu niambie Patrick ni nani uliyekuwa ukiongea naye?
Sauti hiyo ya Andrew ndiyo iliyomfanya astuke
“ni Margreth “
“Anasemaje?
“Anasema kuwa anahitaji sana kuonana na mimi.hakutaka maongezi mengi amesema atanitumia ujumbe kunitaarifu kuwa tonane lini na wapi.”
Andrew akainama chini kwa sekunde kadhaa na kisha akasema
“Mambo yanazidi kupamba moto.Inavyoonyesha kuna jambo zito anataka mkaliongee hususani kizungumkuti hiki kilichopo mbele yetu”
“Sawa Kabisa Andrew hata mimi nadhani hivyo.”
Andrew akaiendea friji na kujimiminia mvinyo katika glasi .mara simu ya Patrick inalia tena.Akaichukua na kuiangalia.Ilikuwa ni simu toka kwa shemeji yake yaani dada yake Veronika aishiye Uingereza.Kijasho kikaanza kumtoka.
“Hallo shemeji” Akasema Patrick
“ouh Shemeji habari za jioni?
“Nzuri shemeji vipi huko wazima?
‘Huku wote tu wazima,Pole sana shemeji yangu nasikia ulipatwa na matatizo kidogo ya mstuko.Ilikuwa tuje kukuangalia lakini kutokana na kutingwa sana na shughuli tukashindwa”
“Kweli shemeji nilipatwa na tatizo kidogo la mstuko lakini kwa sasa naendelea vizuri Hivi sasa niko katika mapumziko mafupi na hali yangu inaendelea vizuri.”
‘nafurahi sana shemeji kusikia unaendelea vizuri.Nimepiga simu kwa vero sasa hivi akaniambia umetoka kidogo hivyo nikaona ni bora nikupigie katika simu yako.sasa ni hivi pamoja na kukujulia hali nilikuwa nataka kuwataarifu kuwa zile tiketi zenu za ndege za kuja na kurudi Uingereza kwa ajili ya kufanya shopping ya harusi yenu tayari zimekwisha tumwa katika ofisi za british airways hapo dare s salaam na kwa kuwa kila kitu kuhusiana na safari hii kimekwisha tayarishwa basi safari itakuwa kesho kutwa.Mkiwa huku tutaangalia pia uwezekano wa kukupeleka katika hospitali kubwa zaidi kwa ajili ya uchunguzi wa afya yako.Msihofu shemeji hizi zote ni gharama zetu.”
Ilimchukua Patrick sekunde kadhaa kurudisha akili na kukumbuka kuwa alikuwa akiongea na simu.Alikuwa amechanganyikiwa.
“hallo shemeji” Aliita shemeji yake baada ya kuona muda unapita hapati jibu
“Ouh shemeji.”Patrick akajibu
“Vipi mbona kimya shemeji?
“mhh shemeji nashukuru sana kwa msaada wenu shemeji yangu.Nimefurahi sana.Kesho tutafanya maandalizi ya mwisho na kesho kutwa tutaanza safari ya kuja hapo uingereza kwa ajili ya shopping ya harusi yetu.”
“Ok shemeji tunawatakia safari njema”
“haya shemeji bye” Akakata simu
Kijasho chembamba kilimtiririka Patrick .Akaitupia simu yake sofani na kujishika kichwa.
“Patrick kuna nini” Akauliza Andrew
“Andrew I’m confused”
“Kwa nini Patrick”
“Si unakumbuka niliwahi kukwambia kuwa dada yake Vero yule anayekaa Uingereza alikuwa akitushughulikia safari yetu ya kwenda uingereza kufanya shopping ya harusi sasa zile tiketi za ndege za kwenda London tayari zimetumwa na safari wanataka iwe kesho kutwa.”
“Ooh My God” Andrew akasema huku akizunguka zunguka humo sebuleni
“Patrick” Akaita Andrew
“Yes Andrew”
“hata mimi nahisi kuchanganyikiwa lakini hebu amua kitu kimoja.Nini kifanyike kati ya mpango wa kumtafuta Happy au kushughulikia harusi yako na Vero?Suala la ndoa yako limepiga hatua kubwa sana kwa sasa na vile vile suala la kuonana na Happy nalo liko katika hatua nzuri.sasa chagua moja ili tushughulike nalo kwa ukamilifu”
Patrick hakujibu kitu akaendelea kujiinamia pale sofani .Baada ya dakika kama mbili hivi akainua kichwa akasema
“Andrew siendi London “
“Patrick!!!!!!!! “ Andrew akahamaki
Patrick akainuka akaichukua simu yake na kuuendea mlango
“Tutaonana Andrew”
“Patrick !!! Andrew akapaza sauti lakini tayari Patrick alikwisha ingia garini na kuondoka zake.
Patrick alifika nyumbani na kumkuta Vero amekaa sofani akimsubiri.Aliinuka akamkumbatia na kumbusu.
“Welcome back darling.” Patrick hakujibu kitu akambusu shavuni na kwenda kuketi sofani
“Patrick mpenzi naomba kabla ya yote ule kwanza chakula.Nimekuandalia chakula kizuri sana ili ule na urejee katika hali yako ya kawaida.”
“ahsante sana vero lakini sijisikii kula kitu chochote leo.Naomba juice baridi”
“No Patrick lazima ule chakula “ Vero aliongea kwa msisitizo.
Ni kweli Patrick hakuwa na hamu ya kula lakini hakutaka kumpa Vero mawazo mengi akainuka na kuelekea mezani.Vero alijitahidi kumlisha chakula na kumwonyesha mapenzi ya hali ya juu.
Baada ya kumaliza kula wakaketi sofani wakiangalia Tv .
“Patrick darl ,kuna habari nzuri sana nataka nikwambie “ Alisema Vero.
Patrick akamwangalia Vero usoni kwa kituo kwani alikwishagundua kitu gani Vero alitaka kumwambia.Alitabasamu na kusema
“jambo gani hilo Vero”
Vero akakohoa kidogo akaendelea
“Dada kapiga simu jioni hii na kunitaarifu kuwa tiketi zetu za kwenda na kurudi London kwa ajili ya ile shopping ya harusi zimekwisha tumwa katika ofisi za British airways na safari ni kesho kutwa.”
Vero aliongea maneno haya huku akimsugua sugua Patrick kifuani.Patrick hakusema kitu alikaa kimya na ni wazi alionekana yuko katika mawazo mazito sana.
“Vipi dear unawaza kitu gani?
Patrick akamwangalia Vero usoni kwa muda mrefu kisha akasema
“Vero dear I’m sorry .Itakubidi uende peke yako.Hali yangu kwa sasa bado si nzuri kusafiri safari ndefu kama hii.Nasikitika sana Vero”
Vero akasimama wima akashika kiuno huku akimwangalia Patrick
“Whaat !!!!!!!! “
“I’m sorry Vero itakubidi uende tu mwenyewe mimi nitabaki niendelee kupumzika .Hali yangu bado si nzuri kusafiri safari ndefu kama hii”
“No Patrick inatubidi tumuone daktari kwanza ili athibitishe kama kweli itakuwa ngumu kwa wewe kusafiri .Halafu isitoshe dada amesema kuwa watagharamia uchunguzi wa afya yako huko huko Uingereza sasa tatizo liko wapi mpenzi?
“Veronika nimeshasema hali yangu si nzuri sasa huyo daktari wa nini tena? Ni yeye anaumwa au mimi? Tafadhali Vero hakuna mjadala katika hili” Patrick akasema kwa hali Fulani ya ukali
Vero akaondoka sebuleni hapo kwa kasi huku akilia
Patrick akaogopa akamfuata.Vero alikaa kitandani huku akilia kwa kwikwi.Patrick akamsogelea na kumkumbatia.
“Vero mpenzi najua ni kwa kiasi gani kauli yangu hii imekuumiza moyo.Samahani sana kwa hilo mpenzi wangu.Wewe ndiwe kila kitu kwangu na wala sina sababu yoyote ya kukuliza.Nisamehe Vero mpenzi wangu.”
Patrick aliingia katika kazi nzito ya kumbembeleza Vero
“Patrick why ur doing this to me?Nimekukosea nini Patrick mbona unanifanyia hivi lakini?Patrick umebadilika ghafla.Mbona nakuwa sikuelewi ?.Hebu niambie kama kuna jambo nimelikosa niombe msamaha na nijirekebishe.”
Maneno yale yanamwingia vilivyo Patrick anamfuta Veronika machozi
“Veronika nyamaza mpenzi wangu.Nakupenda sana kuliko kitu chochote.Sikuwa na lengo au nia mbaya kukwambia vile ni kutokana tu na hali yangu kutokuwa nzuri bado .Hata mimi mwenyewe inaniuma sana .Lakini hakijaharibika kitu tunaweza tukapanga ukaondoka hata na Andrew akakusaidia katika shopping”
“Shame on you Patrick.Nafunga ndoa na wewe au Andrew?Andrew ndiye mpenzi wangu au wewe?Hebu jaribu kukaa chini na kufikiri kwa makini.Dada amejitolea kugharamia uchunguzi wa afya yako katika hospitali kubwa ili kabla ya harusi yetu uwe katika hali nzuri sasa unadhani atanielewaje akisikia huendi?
Patrick hakujibu kitu.Maneno yale ni wazi yalitoka ndani kabisa mwa moyo wa wa Vero.Alimwonea Huruma Vero kwa hali ile aliyokuwa nayo lakini ghafla sura ya Happy inamjia akilini akajikuta akitamka.
“Vero I love you soo much.Sioni kama kuna ubaya wowote kama ukienda peke yako?Huna haja ya kuwa na wasiwasi Vero wewe ni wangu na muda si mrefu Mungu akijaalia tutafunga ndoa sasa wasiwasi wa nini mpenzi?Wewe u wangu Vero na popote nisipokuwepo wewe ni badala yangu kwa hiyo sioni bado tatizo lolote katika hili”CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Vero hakujibu kitu akaendelea kulia.
Mara ujumbe mfupi ukaingia katika simu ya Patrick .Akaufungua na kuusoma huku moyo wake ukienda kwa kasi sana..Ujumbe ule ulitoka kwa Margreth Kibaho
‘Kesho saa nne asubuhi Sean snacks Mbezi.margreth”
baada ya kuusoma ujumbe ule akaufuta kabisa katika simu yake.
************
Saa kumi na moja alfajiri Vero ndiye aliyekuwa wa kwanza kuamka .Hakutaka kumwamsha Patrick.Taratibu akaingia bafuni akaoga kisha akavaa nguo na kumwamsha Patrick.
“Patrick naondoka”
Patrick akafikicha macho yaliyojaa usingizi akasema
“Mbona mapema hivyo kuna nini?
“Nothing.Tutaonana”
Ni wazi Veronika aliondoka akiwa bado na hasira na haikuhitaji akili ya ziada kung’amua kuwa dada huyu mrembo alikuwa amekasirika.Patrick hakutaka kujibizana naye ingawa aliumia sana moyoni kwa hali ile waliyoifikia katika uhusiano wao.
Akiwa hapo kitandani Patrick akajaribu kurudisha kumbukumbu nyuma toka walivyoanza kufahamiana na Happy ,urafiki wao ulivyoanza hadi walivyokuja kutengana.Kumbukumbu zikamjia siku alipoiona suya ya Happy katika Luninga na akapoteza fahamu.Kumbukumbu zikamrudisha tena Diamond Jubilee ambako Happy alitwaa taji la miss Tanzania.
“Ni lazima nionane na Happy .”Alitamka maneno haya kwa sauti.
Taratibu akajiinua kitandani na kuingia bafuni kujimwagia maji.Akiwa chumbani kwake akijiandaa mara simu yake inaita.Ilikuwa ni simu toka kwa mama yake.
“Sikamoo mama ‘
“marahaba.Hivi wewe mtoto una matatizo gani jamani?Umepatwa na nini Patrick?Hivi ni kitu gani kinakusumbua we mtoto? Mama yake alisema kwa ukali.mama huyu ni mmoja kati ya akina mama wakali na asiyependa mchezo
“mama kwani kuna nini mbona hivyo? Aliuliza Patrick makusudi hali akijua kuwa amekwisha likoroga.Alijua tu tayari Vero atakuwa amekwenda kushtaki nyumbani .
“Umemfanya nini mwenzio?
“nani Vero?
“sasa kwani una wenzio wangapi?
“hakuna chochote kibaya mama nilichokifanya .Ni tatizo la kupishana kauli tu”
“sasa sikiliza Patrick nataka ufike hapa nyumbani haraka sana asubuhi hii.Mbona unaanza kutuumiza vichwa we mtoto?Alifoka mama yake
Patrick hakujibu kitu akakaa kimya kwa sekunde kadhaa kisha akastuliwa tena
“Umenisikia lakini?Nataka uje hapa nyumbani haraka iwezekanavyo.Na ukae ukijua kuwa kesho ni lazima usafiri vinginevyo umtafute mama yako.”
Patrick kijasho kikamtoka.Akajikaza na kusema
“mama huko unakofika sasa ni mbali mama yangu.Nitakuja nyumbani tuongee ila si kwa asubuhi hii.Kuna mahala natakiwa niende Nina miadi ya muhimu sana “
“Hiyo miadi ni muhimu kushinda wito wangu mimi mama yako?
“Nothing is important than you mother”Akajibu Patrick
“Ah! Ah! Ah!!! Sitaki kabisa kusikia hivyo vingereza vyako.Kama unaona mimi ni muhimu njoo nyumbani haraka sana.”
“mama samahani siwezi kuja nyumbani sasa hivi .Tayari nina miadi na mtu na ananisubiri asubuhi hii .Nitakuja baada ya kutoka huko.M…..
Kabla hajaendelea akasikia simu ikikatwa.Patrick akabaki njia panda.Je aende kwa mama yake au aende katika miadi yake na Margreth?
Akiwa amezama katika fikra nzito hajui nini cha kufanya mara mlango unagongwa na Andrew akaingia.
“Hi Patrick” Andrew akasema
“Hi” Patrick akajibu
“Hebu niambie ndugu yangu mambo yanakwendaje kwa sababu nimepokea simu toka kwa mama asubuhi hii akilalamika sana juu yako.Anasema kuwa Vero ameenda pale alfajiri na kumweleza kuwa umebadilika mno kwa siku hizi za karibuni.Na kikubwa zaidi ni kukataa safari ya kwenda London.Hilo ndilo linawafanya wawe na hasira juu yako.Sikiliza Patrick kuna kitu kimoja ulichokosea nacho ni kuonyesha wazi wazi kuwa kuna jambo zito linakusumbua.Tayari Vero amekwisha ng’amua hilo .Na hili la kukataa kwenda safari ndio limedhihirisha wazi kuwa kuna kitu unakificha.Chonde chonde Patrick jaribu kuwa makini ili tusije haribu mambo.”
.jpeg)