Patrick akafikiri kidogo kisha akasema
“ Andrew nakubali nilifanya kosa kuonyesha wazi wazi kuwa kuna suala linanisumbua.Nilishindwa kujizuia.That was a mistake.Lakini hata iweje safari hiyo ya kwenda shopping Uingereza siwezi kwenda.Leo nina miadi na Margreth na ninafikiri baada ya hapo nitaonana na Happy sasa huoni kuwa kwenda kwangu London kutaharibu kabisa mpango wangu mzima wa kuonana na Happy .Ni wazi ninahitaji kuonana na Happy .”
“lakini Patrick mimi bado kuna kitu kimoja ninakifikiria ambacho kinaniumiza kichwa sana” Andrew akasema
“Jambo gani hilo” Patrick akauliza huku akimkazia macho Andrew
“Kuhusu wazazi wako pindi watakapokuja gundua kuwa unampango wa kuonana na Happy ”
Patrick akatabasamu kidogo halafu akasema
“Andrew masuala haya yote niachie mimi”
“Siwezi kukuachia wewe peke yako Patrick kwa sababu mimi na wewe tunaonekana ni kitu kimoja.Chochote unachofanya wanajua na mimi nimeshiriki.Ukikosea wewe na mimi nimekosea pia.”
“Kwa hiyo unataka kusemaje Andrew? Patrick akauliza
“ Nafikiria kitu kimoja”
“Kitu gani hicho?
“Naona ni bora tu angali bado mapema uachane na suala hili la Happy .Kwa sasa uko katika maandalizi ya kumuoa Vero , huoni kuwa kuendelea kulipa kipaumbele suala hili la kuonana na Happy linapelekea hata masuala mengine ya msingi kuhusu ndoa yako kuanza kuharibika?.Naona ni bora ukaelekeza nguvu zako katika suala la ndoa yako.Suala la Happy bado halina uzito sana kwa sasa Isitoshe imekwisha pita miaka mingi na tayari Happy ana mchumba wake.Sioni sababu ya kutumia nguvu nyingi katika kumtafuta mtu ambaye alikutia matatizoni halafu baade akakuacha na kwenda zake Ulaya.Vero ndiye mwanamke pekee aliyekaa nawe katika kipindi chote hiki cha matatizo na ambaye amesimama na wewe hadi sasa ambapo maisha yako tayari yamekaa sawa.Hivi unavyofanya si vizuri na ninakwambia ukweli rafiki yangu unamuumiza Vero sana.” Andrew akasema na kumtazama Patrick usoni ambaye maneno yale yanamfanya abadilike uso wake.
“What the hell are you talking about Andrew?. Patrick akauliza kwa ukali.
“Andrew nimekwisha kwambia mara nyingi kwamba kama hutaki kuwa upande wangu naomba uniache.Sikulazimishi kushiriki katika masuala yangu”
“Patrick ! huo ulikuwa ni ushauri wangu tu na si lazima uufuate.Pamoja na ushauri huo niliokupa kama rafiki yako,lakini mwisho wa siku mwenye uamuzi juu ya masuala yako ni wewe mwenyewe..Ok tufanye kama unavyotaka”
************
Saa nne kamili juu ya alama ilimkuta Patrick katika maeneo ya Sean snacks.Hakutaka kupoteza hata dakika moja katika miadi hii ya muhimu.Sehemu hii ni moja kati ya sehemu tulivu sana .Ni mahali panapofaa sana hasa kwa maongezi ya faragha.
Mara tu aliposhuka garini alitumia muda wa kama dakika kumi kuzunguka maeneo hayo kwa minajili ya kuangalia kama anaweza akamuona Margreth.Mara simu yake ikalia.Zilikuwa ni namba ngeni.
“Halloo “ Patrick akaita
“Margreth hapa uko wapi Patrick?
‘Nimeshafika kitambo ,nilikuwa najaribu kuangaza angaza kama nitakuona”
“Mimi ndio nafika sasa hivi.Njoo basi huku nyuma kiunga L”
Akiwa bado amesimama alijikagua kwanza na kuhakikisha yuko katika muonekano nadhifu kisha akapiga hatua kuelekea mahala alikoelekezwa.
“Wow Patrick” Ilikuwa ni sauti ya Margreth mara tu alipomuona Patrick.Patrick hakusema kitu akamtazama Margreth kisha akamkumbatia kwa nguvu.Margreth machozi yalikuwa yakimtoka.Mtu aliyesemekana kufariki dunia leo hii wameonana.
“Patrck siamini kama leo tumekutana tena.Siamini kwa kweli” Margreth akasema huku akifuta machozi.
“Patrick sitaki kulia tena .Tumekwisha lia vya kutosha kwa ajili yako.Tunashukuru Mungu kwamba u mzima na ametukutanisha tena.Huu ni kama muujiza ambao hakuna aliyeutegemea.” Margreth akasema
“sawa kabisa Margreth hata mimi sikutegemea kabisa kama nitakuja kuonana nanyi tena hasa kutokana na mambo yaliyotokea .Na ndio maana nilipatwa na mstuko wa moyo baada ya kumuona tena Happy katika Tv .Hebu kabla hatujaendelea naomba unipe japo kwa muhtasari maendeleo ya hali ya Happy .”
“Happy anaendelea vizuri” Margreth akasema kwa ufupi huku akimtazama Patrick usoni kwa makini.
“Really?
“Yes .She’s fine.Tuachane na hayo.tuendelee na kilichotukutanisha hapa” Margreth akasema
“Ok Margreth ,lakini naona tumejisahau hata kuagiza vinywaji.Sijui unatumia nini?
“Mimi nakunywa wine.Wewe je bado unaendelea na kunywa Juice mpaka sasa?
“Yes margreth.Patrick habadiliki.Umuonaye ndiye Patrick yule yule wa zamani..Ingawa mhh mwenzangu umebadilika sana yaani umependeza sasa hivi umekuwa msichana mrembo kama dada yako Happy .” Wote wakacheka kisha Patrick akainuka na kufuata vinywaji.
“Patick” Alianza maongezi Margreth baada ya Patrick kurejea na vinywaji.
“Ni mengi sana yametokea katika kipindi hiki tulichopotezana.Ni mambo mengi kiasi kwamba tukianza kukumbushana itachukua siku nzima.Kabla sijaendelea kwa niaba ya familia yetu nakupa pole nyingi sana kwa yote yaliyotokea.Sitaki kukumbusha mateso na machungu ya adhabu ile ya kifungo lakini kwa dhati kabisa naomba niweke wazi kuwa familia yetu haikukutupa na kukuacha peke yako gerezani.Baada ya Happy kuondoka alituachia jukumu la kukuangalia mara kwa mara gerezani.lakini baadae zikaja taarifa kuwa umehamishwa gereza na ndio wakati huo huo baba akawa amestaafu kazi tukahama Mbeya na kuhamia Dar es salaam.Toka hapo ndipo utengano ulipoanzia.Tulipofika Dar mdogo wetu akaanza kuumwa hivyo tukatumia muda mwingi kumuuguza kiasi cha kukusahau kabisa.Kitendo hiki cha kukusahau tayari kimetia doa kubwa sana baina yako na sisi.”
Akanyamaza akanywa funda kadhaa za wine kisha akaendelea.
“Patrick kitu kingine kilichotufanya tukate tama kabisa ni baada ya kupata taarifa kuwa umefariki ukiwa gerezani”
“Nimefariki nikiwa gerezani ? Patrick akauliza kwa mstuko.
“Yes Patrick Happy alipata taarifa kwamba umefariki ukiwa gerezani.”
Patrick akavuta pumzi ndefu halafu akaseam kwa sauti ndogo
“I cant believe this.Nani alimtumia taarifa hizo kwamba nimefariki dunia?
“Siwezi kufahamu Patrick taarifa za kifo chako alizipata toka kwa nani.Suala hilo atakueleza yeye mwenyewe kwa kirefu pindi mkionana uso kwa uso” Margreth akasema
Patrick akazama katika mawazo mengi ya ghafla.taarifa ile ya kwamba alikuwa amefariki dunia ilikuwa imemstua mno.
Margreth akamtazama Patrick usoni halafu akaendelea.
“ Ni vigumu mno kulezea uchungu uliotupata baada ya kupata taarifa ile.Happy alilia mno ,akawa akizimia kila siku mpaka ikabidi baba na mama wasafiri kwenda marekani kukaa naye na kumfariji.Baada ya kumaliza masomo yake Happy alirudi nyumbani na kitu cha kwanza alichokifanya ilikuwa ni kutafuta ni wapi ulikozikwa.Baada ya kufanya uchunguzi ikagundulika kuwa taarifa zile za wewe kufariki hazikuwa za kweli.Tulikaa tukimuomba Mungu kwa mapenzi yake atukutanishe siku moja.Mungu amesikia maombi yetu na hatimaye leo hii tumeonana.”
Margreth akatulia ,akachukua glasi yake ya wine na kupiga funda kadhaa.Patrick jasho lilikuwa likimtoka.Alikosa kitu cha kuongea.Kutokana na joto kali alilokuwa akilisikia akavua koti kisha akatoa kitambaa na kujifuta jasho lililokuwa likimtiririka kwa wingi.Machozi yalimlenga lenga.
“Patrick” Margreth akamstuaCHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Haikuwa dhamira yangu kuongea mambo haya ila ni katika kuweka mambo na kumbukumbu sawa. kikubwa kilichonifanya nikutafute kwa hali na mali ni suala hili lililoko mbele yetu.Patrick suala hili ni suala gumu sana.kwa taarifa yako ni kwamba Happy alipatwa na mstuko mkubwa mpaka akapoteza fahamu mara tu alipokuona.Leo hii umeniambia kuwa hata wewe ulipatwa na mstuko baada ya kumuona Happy katika Tv na wewe ukapoteza fahamu.Happy kwa sasa yuko katika wakati mgumu sana akitafuta jinsi ya kuonana na wewe na nina imani hata wewe pamoja na yote yaliyotokea utakuwa na shauku ya kutaka kuonana na Happy .”
Margreth akanyamaza na kimya kikapita.
“Patrick hali ya Happy si nzuri.Nasema si nzuri kimwili na hata kiakili.Tangu amekuona Diamond Jubilee Happy anashindwa hata kula.anashinda analia.Hakuna mwingine anayetaka kuongea naye zaidi yangu.Mimi peke yangu ndiye inayeweza kuongea naye tukaelewana.Ni kutokana na hali yake hii imenibidi nichukue jukumu la kukutafuta ili tuone ni jinsi gani tunaweza kulitatua tatizo hii lililoko mbele yetu.Pamoja na kwamba mmepotezana miaka mingi sasa lakini nina imani wakati mnapotezana kila mmoja alikuwa bado akimhitaji mwenzake na ndio maana baada ya kuonana kila mmoja amepatwa na mstuko wa ajabu.Kitu ninachohitaji kukifanya ni ninyi kukutana .”
Margreth akakaa kimya na kuyaacha maneno yale yazame kabisa ndani mwa Patrick.
“Yes ni lazima mkutane tena.Kinachomuumiza Happy kwa sasa ni jinsi gani atakavyoweza kuonana na wewe.Nina imani hata wewe utakuwa na hamu ya kuonana na Happy japokuwa miaka imeenda na kila mmoja kwa sasa ameendlea na maisha yake.Nina imani mtakapoonana mtaongea na yatakwisha.najua kila mmoja analo la kumweleza au kumuuliza mwenzake kwa hiyo mtakapokutana utakuwa ni mwanzo mpya wenye amani.Hata kama hamtarudiana tena lakini litakuwa jambo jema kama mtamaliza tofauti na kuendelea kuishi kwa amani.”
Patrick alikuwa kimya kabisa jasho likiendelea kumtiririka.Akarekebisha koo na kusema
“margreth uko sahihi.Ni lazima nionane na Happy .”
Margreth akatabasamu kisha akasema.
‘Ok Patrick nashukuru sana kama umeridhia kuonana na Happy .Nimefurahi sana.Nina imani ni fursa hiyo ambayo hata Happy alikuwa akiingojea kwa hamu kubwa.Sasa basi kama unavyojua Happy kwa sasa ni mrembo wa Tanzania.Tayari ana jina kubwa.Kila analolifanya yeye kwa sasa linakuwa ni habari.Vyombo vya habari na hasa haya magazeti ya udaku yanamfuatilia usiku na mchana.Kwa hiyo basi hatutaki kutengeneza story na kuwafaidisha watu.Makutano haya yawe ni ya siri kubwa kiasi kwamba iwe ni siri baina ya mimi wewe na Happy .makutano yenu yafanyike nje ya dare s salaam ambako hamjulikani kabisa.Mimi napendekeza makutano yenu yawe morogoro au we unasemaje?
Patrick akafikiri kisha akasema
“Hapana margreth Morogoro bado ni karibu sana na Dar es salaam.Morogoro hapawazuii watu kufunga safari na kuwafuatilia hasa wakijua kuwa wanatengeneza story ambayo itawaingizia fedha.Mimi napendekeza tukakutanie Arusha.Tena nje kabisa ya mji.Pale tunaweza kukaa tukaongea na kuweka mambo sawa bila kuingiliwa na mtu yeyote yule.Au we unaonaje margreth?
“Hilo ni wazo zuri .Tena zuri sana.Nina imani hata Happy mwenyewe hawezi kulipinga kwa sababu akili yake yote kwa sasa ni kuonana na wewe tu hata kama makutano ni Ulaya.Ok hebu nipe dakika tano hivi niongee naye nisikie anasemaje.”
“Ok Margreth.”
Margreth akatoa simu yake na kwenda mbali kidogo na mahali walipokuwa wamekaa akapiga simu.
Baada ya kama dakika kumi hivi akarejea.
“Enhee anasemaje Happy ? Patrick akauliza kwa shauku.
Huku akitabasamu Margreth akajibu
“Amekubali bila wasi wasi na tena amefurahi sana yaani bado haamini kama ni kweli”
“wow ! nipe basi niongee naye mimi mwenyewe”Patrick akasema
“No huwezi ongea naye kwa sasa.Mtaongea mkionana uso kwa uso.Kinachotakiwa kwa sasa tupange kabisa utaratibu wa safari ni lini na ni wapi mtakwenda kukutana,nina maana ni hoteli gani mtafikia.”
Huku akichezesha mguu wake kwa furaha Patrick akasema
“ Kuna hoteli moja mpya kabisa imefunguliwa nje kidogo ya Usa river.Ni sehemu ya kisasa na yenye utulivu wa pekee.Ninadhani inafaa sana kwani hakuna mtu atakayekuja kufuata umbea kule.Kuhusu usafiri gharama zote zitakuwa juu yangu.Wala usihofu.Community airlines wana ndege ya kwenda kaskazini kila siku saa saba na saa kumi na moja jioni.Mimi nitatangulia na ndege ya saa saba mchana na Happy itambidi aje na ndege ya saa kumi na moja jioni.Kwa hali ilivyo hatuwezi kusafiri na ndege moja.Ngoja nimpigie simu rafiki yangu Andrew afanye mpango wa tiketi hizo haraka sana.Usihofu huyu ni zaidi ya rafiki ninamwamini sana.”
Patrick akaitoa simu yake na kumpigia Andrew.
“Haloo Andrew”
“Patrick vipi? Mambo yanakwendaje?
“mambo shwari tu Andrew”
“Sasa Andrew ni hivi,natakiwa niende Arusha leo.hapa niko na Margreth .Nimeongea naye na mwisho wa yote natakiwa nikutane na Happy Arusha.Naomba basi ufanye hima uende pale katika ofisi za community airlines na unifanyie mpango wa tiketi mbili .Ya kwangu mimi ni ya ndege ya saa saba mchana huu na nyingine ni ya Happy Kibaho ndege ya saa kumi na moja.Please Andrew its urgent.”
“Ok Patrick tena imekuwa vizuri kwa sababu hapa nilipo sasa si mbali na ofisi zao ngoja niwahi basi.Nipe kama dakika ishirini hivi nitakupigia simu.
“Ok Andrew”
Patrick akakata simu na kupumua kwa nguvu
“Everything is going to be fine.Hatimaye baada ya muda mrefu ninaenda tena kuonana tena na lulu ya thamani kubwa maishani .” Patrick alikuwa akiongea mwenyewe na kumfanya margreth atabasamu .
Waliendelea kuongea maongezi ya hapa na pale mara simu ya Patrick inalia.
“Ni Andtrew huyu”Patrick akasema
“Haloo Andrew hebu nipe habari”
“Patrick kila kitu tayari.Kuna rafiki yangu yule bwana Kimaro anafanya kazi pale pale amenisaidia sana kufanikisha zoezi hili kwa haraka.Kwa hiyo unaweza kupita ofisini kwangu kwani ndiko naelekea kwa sasa”
“Ok Ahsante sana Andrew nitafika hapo muda si mrefu”
Patrick akakata simu halafu akamwangalia Margreth kwa tabasamu pana sana kisha akasema
“margreth kila kitu tayari tunaweza kwenda sasa ofisini kwa Andrew”
“You are so fast Patrick”
“Kwa miadi kama hii ya kukutana na Happy kila kitu lazima kiende haraka” Patrick akasema huku akitabasamu
Walitoka hapo Sean snacks na kuelekea moja kwa moja ofisini kwa Andrew.
Iliwachukua kama dakika arobaini hivi kuwasili zilipo ofisi za Andrew.Haraka haraka wakafululiza hadi ofisini.
“Wow Comrade “Akasema Andrew mara tu Patrick alipoingia ofisini kwake.Wakakumbatiana kwa furaha.
“Andrew kutana na Margreth kibaho mdogo wake Happy .Margreth kutana na Andrew,rafiki yangu mkubwa na wa pekee kabisa”
llikuwa ni mara ya kwanza kwa Andrew kumtia machoni Margreth.Macho yake yalijikuta yameganda yakiustaajabia uzuri wa kimwana huyu.
“Mhhhhhh !! mtoto mrembo kama malaika.Ama kweli familia hii imebarikiwa kwa kuwa na watoto warembo .Hapana I have to do something.Hii ni nafasi yangu na mimi” Andrew akawaza.
“Hello Margreth nashukuru sana kukufahamu.Karibu sana”Andrew akasema huku akitoa rabasamu pana sana .
“ Hata mimi nimefurahi sana kukufahamu Andrew”
*********************
“Patrick “ Akasema Andrew
“Kwa kuwa muda uliopo mpaka saa saba ni mfupi sana na nina imani hautaweza kuonana na mama kama ulivyomuahidi ,unaonaje kama ukimpigia simu na kumweleza kuwa hutaweza kuonana naye leo ili asije akadhani umemdharau.”
Patrick akatabasamu na kusema
“Andrew una akili sana”Akasema Patrick huku akiitoa simu yake na kumpigia mama yake
“Halloo mama”
”Enhe!! Unasemaje?Mbona huji we mtoto?Mwenzio yuko hapa toka asubuhi ,tunakusubiri wewe” Mama yake akasema kwa ukali
Patrick akastuka akafikiri kidogo kisha akasema
“Ina maana mpaka muda huu Vero yupo hapo nyumbani?
“Vero yuko hapa akikusubiri wewe.Mbona unamtesa mwenzio namna hii Patrick”
“mama samahani sintaweza kufika tena hapo nyumbani leo hii kama nilivyokuwa nimekuahidi.Nimepata dharura moja ya muhimu mno.Nafikiri labda kesho kutwa tutaonana”
“Unasemaje wewe???? Mama yake akahamaki.
“Mama nimepata udhuru wa ghafla hivyo sintaweza kufika leo mpaka kesho kutwa.”
“Hivi Patrick una akili zote kweli?Hivi hayo masuala yako unayaona ya muhimu kuzidi ninalokuitia mimi mama yako?
“Mama”Patrick akadakia
“Nafahamu unaniitia jambo la msingi kabisa na siku zote siwezi kukudharau wewe mama yangu.Lakini kwa hili naomba unisamehe mama.Ni muhimu mno kwangu”
Patrick akakata simu na kuizima kabisa.Akashusha pumzi ndefu
“Oh My God help me.”Akasema Patrick huku akitoa kitambaa na kujifuta jasho usoni.
Andrew na Margreth wakamuangalia usoni
“mama anasemaje?” Andrew akauliza.
“Hakuna muafaka .Bado ananitaka niende nyumbani kwani bado Vero yuko kule wananisubiri.Anyway ni mambo ya kawaida nimeyazoea.Ila andrew nakuomba sana rafiki yangu niko chini ya miguu yako usije ukamweleza mtu yeyote nimekwenda wapi.Najua watakusumbua sana wakiamini kuwa ni lazima utakuwa ukifahamu nimekwenda wapi.Kuonana na Happy ndilo jambo la muhimu mno kwa sasa”
Kabla hajaendelea mbele simu ya Andrew ikaita.alikuwa ni mama yake Patrick.
“Ni mama” Andrew akasema kwa wasi wasi
“Ongea naye mwambie hujaniona kabisa tangu tulivyoonana asubuhi”
”Haloo mama “Andrew akasema baada ya kuipokea simu ile
“Samahani Andrew ,hivi huyu mwenzio yuko wapi?Uko naye hapo?
“Hapana mama kwani bado hajafika huko nyumbani?
“hapana baba bado hajafika.”
“Mimi nilimfuata nyumbani kwake asubuhi na kumweleza vile ulivyonituma nikamwacha hapo akijiandaa sasa nashangaa unaposema hajaonekana mpaka saa hizi”
“Mimi sielewi andrew huyu mwenzio ana matatizo gani kwa sasa.Tangu apatwe na huu mstuko amebadilika sana.Mwenzake bado yuko hapa akimsubiri yeye bado haonekani.Kanipigia simu muda si mrefu na kunitaarifu kuwa ana dharura .Dharura gani hiyo ya kuushinda wito wangu mimi mama yake? Kibaya zaidi amekata simu na kuizima kabisa.Hivi kweli Patrick amefikia hatu ya kunizimia simu hata mimi?Sasa ukimuona mweleze kwamba sitaki tena aje nyumbani na hao waliompa hizo dharura ndio watakuwa wazazi wake,Ha…..”
“Hapana Mama”Andrew akadakia
“Samahani kwa kukukatisha mama ila huko unakofika mama ni mbali sana.Kwa jinsi ninavyoelewa mimi Patrick hawezi kukata simu na kuizima kabisa.Ni kwamba leo nilivyokwenda kwake asubuhi nimemkuta akihangaika kuikausha simu yake iliyomwagikiwa maji.Hivyo basi simu yake inatatizo hilo kwa sasa la kuwaka na kuzima.Hata mimi nimekuwa nikimtafuta kwenye simu bila mafanikio.” Andrew akadanganya huku Patrick akitabasamu.
“Unamtetea mwenzio siyo? Haya anayoyafanya unaona ni mazuri?
“Hapana si hivyo mama usinielewe vibaya.Wewe ni mama yetu na kamwe hatuwezi kukudanganya.Naomba mama unipe jukumu la kumtafuta Patrick na kumleta hapo nyumbani haraka iwezekanavyo.”
“Sawa baba.Jitahidi basi umtafute umlete hapa haraka Kesho wana safari na mwenzake ya kwenda London.Atake asitake ni lazima aende na mwenzake Uingereza””
“sawa mama” Andrew akajibu na kukata simu.CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Wote wakajikuta wakiangaliana baada ya simu kukatwa.
“Good.Umemjibu vizuri kiasi ambacho hata sikutegemea.Sasa hatua hiyo imekwisha.Kifuatacho sasa naona tumruhusu margreth yeye aondoke na mimi nikajiandae.Au unasemaje?
“sawa tu Patrick .Mimi ngoja nimsindikize Margreth mpaka hapo nje nakuja sasa hivi andrew akasema Patrick akatabasamu.
“Ok kwa heri Patrick nawatakia kila la heri.Ila please sitaki dada yangu aendelee kulia tena.Promise?
“Happy hatalia tena ,nakuahidi ” Akasema Patrick
Margreth na Andrew wakashuka ngazi na kumwacha Patrick katika tabasamu pana sana
“Mhh kwa jinsi ninavyomuelewa Andrew tayari keshapenda pale”
Baada ya dakika kama kumi hivi andrew akarejea.
“Vipi niambie Andrew naona mzee eenh” Wote wakacheka.
“Mhh ! Patrick hii familia ina vifaa bwana.Unajua Margreth nilikuwa namsikia tu.sasa leo ndio nimemwona Live.Wallah mtoto huyu anawapeleka puta watu wengi..Tuachane na hayo.Patrick unajua tuko matatizoni ndugu yangu.Yaani Mama kwa jinsi alivyokuwa akiongea halafu aje agundue kuwa Happy ndiye sababu ya kuifanya safari ya London isifanikiwe sijui kama patatosha.Kwa hivi sasa hata mimi haniamini tena.anajua letu moja.”
“Andrew nilikutahadharisha kuwa mpango huu wa kuonana na Happy ni mgumu na ambao ni lazima utatufanya tukumbane na vikwazo vingi.Nina imani siku itakuja ndugu zangu wote watanichukia na kunitenga kabisa.Jipe moyo andrew haya ni mambo madogo tu yatakwisha”
“Ok Patrick kwa sasa tuelekeze macho na akili zetu katika makutano yako na Happy huko Arusha ambako ndiko kutatoa jibu la uelekeo mzima wa suala hili.Ya hapa Dar niachie mimi nitayamaliza.Muda unakwenda sana .Sasa hautatakiwa uende nyumbani kwako.Itabidi tuende kwangu kila kitu kuhusu safari utakipanga pale.Unaweza kwenda kwako ukakutana na Vero na kila kitu kikaharibika.”
‘Hapo umenena ndugu yangu.Twende haraka”
Wakaingia garini moja kwa moja hadi nyumbani kwa Andrew.Baada ya kupakia nguo na vitu kadhaa vya safari wakaingia garini na safari kuelekea airport ikaanza.
***************
Baada tu ya kushuka ndani ya gari iliyomleta toka ofisini kwa Andrew,Margreth akakimbia kuelekea ndani.Wote waliokuwa sebuleni walishangaa jinsi Margreth alivyoingia kwa kasi na bila kuongea au kumsalimu mtu yeyote.Moja kwa moja alikwenda kugonga mlango wa dada yake.
“Happy fungua I’m back”
Mlango ukafunguliwa na kitu cha kwanza ikawa ni kukumbatiana kwa nguvu.
Sebuleni ndugu kadhaa walikuwa wamekaa wakijadili juu ya mwenendo mzima wa hali ya Happy .Ujio wa Margreth uliwafaya wote wastuke .Mama yao ambaye naye alikuwapo sebuleni akainuka na taratibu akaelekea chumbani kwa Happy ili kujua kumetokea nini.Akakinyonga kitasa taratibu lakini kilikuwa kimefungwa kwa ndani.Akajaribu kutega sikio ili asikie ni kitu gani walikuwa wakiongea binti zake wale wawili akashindwa kusikia lolote kutokana na sauti kubwa ya muziki waliyokuwa wameifungua.Akasimama pale mlangoni kwa sekunde kadhaa ,akatikisa kichwa na kurudi tena sebuleni.
“Watoto hawa bwana mbona nakuwa siwaelewi elewi? Lakini najua ni lazima Margreth akawa anajua kila kitu kinachoendelea kwa dada yake.Ngoja tuwaache tuone “Aliwaza mama yao huku akipiga hatua kuelekea sebuleni.
“Happy kila kitu tayari kama nilivyokueleza katika simu.”margreth akatoa tiketi ya ndege na kumwonyesha dada yake ambaye aliruka kwa nguvu na kumkumbatia mdogo wake.
“Margreth thank you so much.ahsante sana mdogo wangu” Happy akasema huku machozi yakimtoka
Happy akainuka na kuikumbatia picha ya Patrick ambayo walipiga wote toka kipindi wako shuleni.
“Ooh Patrick nuru ya maisha yangu siamini kama nimefanikiwa kukuona tena” Akasema Happy.Margreth akatabasamu na kusema
“ Happy kama nilivyokueleza nimekutana na Patrick.Imekuwa ni siku yenye msisimko mkubwa sana hasa kwa Patrick.Sikuongea naye mambo mengi kutokana na muda na vile vile sikutaka kuingia kwa undani sana katika masuala yanayowahusu wewe na yeye.Lengo kuu lilikuwa ni kuwakutanisha nyie wawili na hapo ndipo mtakapokuwa na nafasi ya kutosha kwa kila mmoja wenu kuongea na kuweka wazi hisia zenu.Patrick alilikubali wazo la kuonana na wewe kwa furaha.Nilitaka mkakutanie Morogoro lakini Patrick akakataa na kupendekeza Arusha.Nje kidogo ya mji wa Usa river kuna hoteli mpya kabisa iitwayo Kobe village.Pale ni mahala palipotulia na hakuna bugudha yoyote.Unajua kwa sasa wewe umekwisha kuwa na jina kubwa hapa nchni.Kwa hiyo wanaokufuatilia ni wengi.Yaani haya matatizo tu ya siku mbili tayari kila siku yanazipamba kurasa za magazeti.Itakuwaje iwapo utakutwa faragha na Patrick?Kwa kuliogopa hilo ndio maana tukaona ni bora mkakutanie mbali na hawa wadaku.Kila kitu tayari kimekamilika na hiyo hapo ndiyo tiketi yako ya ndege.safari ni leo saa kumi na moja jioni.Patrick yeye anatangulia na ndege ya saa saba mchana huu.”
Happy akamkumbatia tena mdogo wake kwa nguvu.
“Sasa kazi inabaki jinsi ya kumkoroga mama mpaka akubali kuniachia.Hivi atanielewa kweli? Happy akauliza.
“Fanya hivi , mwambie kwamba unaomba uende mahala ukapumzike ila usimwambie ni wapi.Mwambie unahitaji kuwa sehemu ya peke yako kwa siku kadhaa.Mama anakupenda sana na hataweza kukukatalia”
“Ok ngoja nikamjaribu” Happy akasema huku akiinuka.
“Wakati unaenda kuonana naye nenda na uso wa furaha ulojaa tabasamu ili asiwe na mashaka na wasi wasi wowote.” Margreth akasema
Happy akajiweka safi akatoka chumbani na kuelekea sebuleni akiwa katika tabasamu.
Mama yake akastuka baada ya kumuona mwanaye ghafla pale sebuleni tena akiwa katika hali ambayo hakuna aliyeitarajia.Happy alionekana mwingi wa furaha na uso mwangavu wenye nuru.
“Ouh Happy mwanangu”mama yake akashindwa kujizuia na akainuka na kumkumbatia mwanae kwa nguvu.Watu wote pale sebuleni wakasimama na kumwangalia Happy kwa mshangao.
“Unaendeleaje mwanangu?mama yako sili silali nakuhofia wewe”Mama yake Happy akasema.Huku akitabasamu Happy akasema
“Naendelea vizuri sana mama.”
“Nashukuru sana mwanangu kama unaendelea vizuri.Hapa unapotuona tuko familia nzima tukijadili juu ya hali yako na isitoshe tumekuwa katika maombi ya sala ili Mwenyezi Mungu akujalie afya njema na upone haraka.Nashukuru Mungu kwa sasa u mzima.”
Akamwangalia tena usoni mwanae na kumpiga piga bega huku akisema
“Mwanangu u mrembo sana”
“Mremo kama mama yangu” Happy akajibu na wote mle sebuleni wakacheka.
Furaha ikatawala ndani.Chakula kikaletwa watu wakala na kufurahi.Baada ya kumaliza kula Happy akamuomba mama yake waende bustanini kwa maongezi kidogo.
“mama ninashida sana na ni wewe tu ambaye unaweza kunisaidia.”Happy akasema wakiwa bustanini yeye na mama yake
“Kitu gani hicho mwanangu unakitaka?Sema tu kama ninacho nitakupa”
“mama nadhani unafahamu matatizo yaliyonipata.Ni wazi yameniletea athari kubwa kisaikolojia na ndiyo maana kila siku zinavyokwenda mbele ninazidi kudhoofika.Daktari wangu ameongea na Margreth na kumwambia kwamba nina tatizo la kisaikolojia.Sikuwa nimejiandaa kulitwaa taji kubwa kama hili na hivyo akashauri nipate muda mwingi wa kupumzika bila kubugudhiwa na kitu chochote.Nimekubaliana na ushauri wake ambao nina imani kwamba utanisaidia sana.Mama nahitaji kusafiri,kuwa nje na nyumbani,nje na Dar es salaam kwa siku mbili au tatu.Nahitaji kuwa peke yangu kwa siku hizo kadhaa ili niweze kuyasahau yote yaliyotokea na niweze kujiandaa vyema jinsi ya kuweza kuishi maisha mapya nikiwa kama mrembo wa Tanzania.Mama najua siwezi kuongea na baba juu ya suala hili kwani baba hatanielewa.Please mama naomba unisaidie sana kwa hilo.Nahitaji kuwa sawa kiakili mama.taji nililonalo ni kubwa sana kwa hiyo nahitaji mandalizi ya kutosha”
Maneno haya yanamfanya mama yake Happy akae kimya kwa sekunde kadhaa kisha akamwangalia mwanae usoni na kusema
“Happy mwanangu,mimi mama yako kwanza nafurahi sana na kumshukuru Mungu kwa kukujalia afya njema.Huwezi kujua ni jinsi gani mimi mama yako nilivyokuwa naumia kila nikikuona ukiwa na hali ile ya majonzi mengi.Namshukuru sana Mungu kwa muujiza huu mkubwa alioitendea familia yetu.Siku zote yeye ndiye amekuwa ngao na kinga yetu.Happy nakubaliana na mawazo yako ya kwamba unataka kwenda mbali na hapa ukapumzike.Kwa jinsi ninavyokupenda mwanangu siwezi kukukatalia kwani ninataka siku zote uwe ni mwenye furaha na afya tele.Lakini kuna kitu kimoja kinanipa wasi wasi,mwanangu hauna tatizo lolote linalokusumbua akili ?naomba kama una tatizo nieleze mimi mama yako nitakusaidia.Usiponieleza mimi mama yako nani mwingine utakayemweleza akakusaidia?
Happy akacheka kidogo kisha akasema
“Mama nadhani unanielewa vizuri siku zote niwapo na tatizo mtu wa kwanza kumkimbilia ni wewe.Zaidi ya kupata ule mstuko na kupoteza fahamu sina tena tatizo lingine.Naomba uniamini mama ni tatizo hili la kisaikolojia ndilo inanibidi nipambane nalo kwa sasa.Ninaamini nitakaporejea nitakuwa mzima wa afya tele.”
“Vizuri kama hayo uyasemayo ni ya kweli.Lakini Happy umenipa mtihani mgumu sana kwa baba yako.Unamfahamu baba yako alivyo mkali.Iwapo nitakupa ruhusa bila ya yeye kujua nitakuwa na wakati mgumu sana kumpa majibu yenye kueleweka.Sasa sijui nifanye nini mwanangu?
“mama usiwe na wasi wasi wowote.naomba unipe ruhusa halafu mimi mwenyewe nitaongea naye na kumuelewesha.”CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Mama yake happy akainama akafikiri kidogo kisha akasema
“Unataka kwenda wapi?
“Nje ya Dar es salaam.Sijajua bado kama niende Morogoro,Tanga .Moshi au kokote kule ili mradi iwe nje ya Dar es salaam.”
“ Unakwenda na Mike?
Happy anastuka kidogo kwa swali lile.
“Mike? Happy akauliza
“Ndiyo Mike” mama yake akajibu
“Kwa nini umeuliza mama?Mi nitakuwa mwenyewe tu.Sintakuwa na mtu yeyote”Happy akajibu.Mama yake akamuangalia usoni halafu akasema
“Jana Mike alipiga simu na kuniambia kuwa leo saa mbili usiku atawasili lakini alisema nisikwambie kwa sababu anataka akushangaze,ndio maana nikahisi pengine mlipanga muende wote hiyo safari”
“Hapana mama mimi nitakuwa peke yangu.Yeye kama akija atanisubiri hapa hadi nitakaporudi.”
“Kwa hiyo una maana unaondoka leo hii kabla mwenizo hajafika?
“ndiyo mama.Nimekwishafanya booking ya ndege ya leo jioni inayokwenda Mwanza kupitia Morogoro na Kilimanjaro.Nitashukia Morogoro halafu toka pale nitaangalia kama nitabaki Morogoro au nitakwenda sehemu nyingine.Nianweza kwenda Iringa au Mbeya au sehemu yoyote ile.”Happy akasema huku mama yake akimkazia macho
“Happy kwa nini umepanga safari ya ghafla namna hii? Hutaki kuonana na Mike? Unamkwepa mwenzio? Hebu niambie bila kunificha kitu kwa sababu mwenzio anakuja usiku wa leo na ameacha shughuli zake huko Marekani kwa dhumuni moja tu la kuwa na wewe .Endapo hatakukuta hapa nyumbani ni wazi atahitaji maelezo ya kina na hakuna mwingine atakayempa maelezo juu yako zaidi yangu.Naomba usinifiche kitu mwanangu.Mike anakupenda na sisi tunampenda “ Happy akakaa kimya kidogo halafu akasema
“Mama naomba unielewe.Sifanyi hivi kwa ajili ya kumkimbia Mike.Ninampenda Mike kupita maelezo lakini ninafanya hivi kwa ajili yangu.I need to be ok mother.After all that happened I need sometime alone.Please understand me mother” Happy akasema kwa msisitizo
Mama yake hakuona sababu ya kumkatalia binti yake.
“Happy mwanangu mimi siwezi kukukatalia kwenda huko unakotaka kwenda.Wewe ni mtu mzima kwa sasa na nina imani kuwa kila unachokiamua hakina madhara kwako.Ila mwanangu nataka tu unihakikishie kuwa huko uendako utakuwa salama.”
“mama nitakuwa salama na wala usihofu kitu chochote.Simu yangu itakuwa wazi muda wote”
“Sawa mwanangu hakuna shida baba yako nitamalizana naye mimi.Kwa hiyo saa ngapi unaondoka?
“Saa kumi na moja jioni.Sitaki kusafiri mapema sana kwa sababu watu hasa waandishi wa habari wananifuatilia na wanaweza wakaniharibia safari yangu.margreth atatumia gari lako kunipeleka uwanja wa ndege.Halafu mama naomba usimwambie mtu yeyote zaidi ya baba na Mike ni wapi nimekwenda.Kwa sasa mimi ni mtu maarufu hivyo habari zangu zinauzika sana katika vyombo vya habari.Sitaki watu waniharibie mapumziko yangu.”
“sawa Happy .Twende ukajiandae.Nitakupeleka uwanjani mimi mwenyewe “ mama yake akasema huku akitabasamu .
*************
Ni kengele ya simu ya chumbani ndiyo iliyomstua Patrick toka katika jinamizi la mawazo.Tangu amefika katika hoteli hii ya Kobe Village amekuwa ni mwingi wa mawazo .Kutokana na wasi wasi mwingi aliokuwa nao aliamua kujiliwaza kwa kunywa mvinyo laini.
Aliweka chini glasi yake ya mvinyo na kuiendea simu ile ya chumbani.
“Haloo” Aliita kwa kitetemeshi
“Haloo mapokezi hapa.Samahani kaka mgeni wako uliyesema atawasili tayari amefika.Je utakuja kumchukua au tumlete moja kwa moja chumbani?
Patrick akapumua kwa nguvu ,mapigo ya moyo yakabadilika.
“Mleteni chumbani “Patrick akasema,akaurudisha mkono wa simu kisha akapumua kwa nguvu,kijasho chembamba kilimtoka .Wakati akitafakari na kuuona huu ni kama muujiza kukutana tena na Happy mara kengele ya mlangoni inalia.Taratibu akajivuta na kwenda kuufungua.
Kwa takribani dakika moja nzima wote wawili walipigwa na butwaa kila mmoja akimshangaa mwenzake.Halafu wakakumbatiana kwa nguvu huku wote wawili machozi yakiwatoka..Muhudumu aliyekuwa ameongozana na Happy akapigwa na mshangao kwa hali ile aliyoina.Hisia za penzi la kweli zilijidhihirisha wazi wazi baina ya wawili hawa..Tukio hili linaamsha kumbukumbu kubwa na ya pekee maishani mwao.Hakuna aliyetaka kumwachia mwenzake.
Patrick akamshika Happy taratibu na kumkalisha katika sofa lililokuwamo humo chumbani.Uso wake wote ulikuwa umejaa machozi.
“I cant believe this”Patrick akanong’ona.Happy hakujibu kitu midomo yake ilikuwa ikimtetemeka.Kila alilotaka kuongea lilikwama.
“Is that you Patrick? Happy akajitahidi kusema huku akifuta machozi
“Its me Happy.Its real me” Patrick akajibu
“Its like I’m dreaming…Ni kama ninaota.bado siamini kama nimekuona tena” happy akalalama.
“Ouh Patrick I real love you my angel” Aliwaza Happy huku ameikunja mikono yake kifuani kwake.Patrick alikuwa amesimama akimkodolea macho Happy asiamini alichokuwa akikiona mbele yake..
Baada ya kama dakika kumi hivi za ukimya ,tafakari na hisia nzito kwa kila mmoja ,hatimaye Patrick akaufungua mdomo na kusema
“Welcome back my sunshine”
“Welcome back to my heart Patrick” Happy akanong’ona kwa sauti laini sana.
“Huu ni muujiza mkubwa sikutegemea katika maisha yangu kama nitakuja kukuona tena.,lakini Mungu ni mkubwa na ameweza kutukutanisha tena.” Akasema patrick na kauli ile inaamsha kilio kwa Happy
“Happy nyamaza usilie.Umelia vya kutosha uliponipoteza ,I’m here now.”
“Patrick ninaumia sana kwa kila nikikumbuka mateso niliyoyapata kwa kukupoteza.Awali ya yote naomba unisamehe kwa yote yaliyotokea kipindi cha nyuma.Najua bado una kinyongo moyoni na hata mimi nilikuwa na fundo kubwa moyoni kwa kitendo ulichonifanyia lakini tayari nimekusamehe.Naomba na wewe utafute ndani ya moyo wako jinsi ya kunisamehe.Patrick najua ulifungwa kwa ajili yangu.Mapenzi yako makubwa kwangu ndiyo yaliyosababisha ukafungwa.Uliua kwa kuniokoa mimi nisidhalilishwe.”
Happy akaangusha kilio tena.Patrick katoa kitambaa na kumfuta machozi .
“Patrick halikuwa kusudio langu mimi kwenda kusoma Ulaya na kukuacha peke yako.Nilikuwa nimekataa kwenda lakini ukanishauri niende kusoma kwa ajili ya kutengeneza maisha bora kwangu na kwako.Ni…….”
Kabla hajaendelea simu yake inalia.Akafuta machozi haraka haraka na kuitoa katika mkoba wake.mdogo.Aliangalia namba za mpigaji na kukuta ni Mike mchumba wake.Kwa hasira akakata simu na kuizima kabisa.
Patrick akakiangalia kitendo kile lakini hakukitilia maanani .
“Patrick”Happy aliita huku akimwangalia machoni.
“Yes” Patrick akaitika
“Ninajua itakuwia ngumu sana kwa wewe kama binadamu kunisamehe kwa kile kilichotokea,japokuwa tayari mimi nimekwisha kusamehe….”
“Please Happy “Patrick akadakia.
“Naomba usiseme maneno hayo tena.Yanaumiza sana.Ni kweli nilikuwa na hasira sana lakini huu si muda wake kuyaongelea hayo.”
Happy akamvuta Patrick karibu akamkumbatia na kumpiga mabusu mfululizo.Patrick akahisi kitu kama chaji za umeme zimepita mwilini mwake.
******************
Saa moja na nusu jioni Andrew akiwa nyumbani kwake na mpenzi wake Vick mara simu yake inalia.Akaichukua na kuangalia mpigaji ,alikuwa ni mama yake Patrick.Moyo ukaanza kuenda mbio.
“Du! Kazi imeanza”Alisema kwa sauti ndogo ambayo Vick aliisikia.
“Haloo mama”
“andrew mwanangu hivi huyu mwenzako ana kitu gani jamani kinachomsumbua?Unajua mpaka sasa hivi siamuona hapa nyumbani na wala hajanipigia simu na simu yake ameizima kabisa.Nimekwenda nyumbani kwake hayupo,Veronika amekaa hapa mpaka ameamua kuondoka mtoto wa watu .Sielewi ni kwa nini anaanza kutuweka roho juu juu dakika hizi za mwisho.Maandalizi ya harusi yake yanaelekea ukingoni lakini yeye haonyeshi kujali.sasa hebu niambie baba ulifanikiwa kumuona?”
“Mama kwa kweli nimehangaika sana na hata ofisini sijakaa kwa ajili ya kumtafuta Patrick na katu siwezi kukuficha mama Patrick sijui alipo kwa sasa.Hata mimi alinieleza kuwa ana dharura leo lakini hakunifafanulia ni dharura gani hiyo.Hata mimi nimemtafuta sana katika simu hapatikani nadhani lile tatizo la simu yake bado linaendelea” Andrew akasema
“andrew na wewe usitake kuniudhi kama huyu mwenzio,usinieleze kabisa upuuzi huo wa simu.Patrick si mtu wa kushindwa kununua simu nyingine,angenieleza hata mimi ningemnunulia mpya.Hivi kwa nini mnataka kuzichezea akili zetu nyie watoto?
“Mama naomba unipe muda zaidi mpaka kesho asubuhi nitakuwa nimepata jibu wapi alipo Patrick na nitakujulisha ikiwezekana nimlete nyumbani mimi mwenyewe”
“Sawa baba jitahidi umpate kwa sababu anatuweka roho juu juu kweli huyu mwenzio.”
“Ok mama nitajitahidi”
“Haya Andrew usiku mwema”
“Ahsante mama”
Uuuuuuphhh!!!!!! Andrew alipumua kwa nguvu baada ya kumaliza kuongea na mama yake Patrick
“:Kuna nini andrew? Vick akauliza
“Patrick haonekani”
“etiii!!!!!!! ???” Vick akauliza kwa mshangao,akainuka akashika kichwa kwa mikono yake yote miwili.
“Mungu wangu ! yuko wapi sasa jamani”
“hata mimi sielewi Vick .Mama ndio kanipigia simu sasa hivi anaulizia kama nimemuona”
“Ina maana hujaonana naye leo?” Vick akauliza huku amemkazia macho Andrew
“Nilionana naye asubuhi ya leo na toka hapo sijaonana naye tena na simu yake haipatikani.”
“Hakukueleza kuwa anakwenda wapi?
“alinidokeza kuwa ana dharura ila hakunifafanuia zaidi”
Vick akafikiri kidogo kisha akasema
“andrew ,wewe ndiye rafiki mkubwa wa Patrick.Hakuna kitu ambacho huwa mnafichana.Hainiingii akilini eti Patrick awe na dharura halafu ashindwe kukueleza ni dharura gani hiyo?
“Please Vick nimesema sijui Patrick alipo!Mimi kaniambia hivyo kuwa ana dharura sasa siwezi kuingilia masuala yake binafsi.Umenielewa?
Vick akamwangalia Andrew kwa sekunde kadhaa kisha akaketi sofani.
Baada ya kutafakari kwa muda Andrew akaamua kumpigia simu Veronika
“Haloo shemeji” Andrew akasema baada ya Vick kupokea simu
“andrew I’m confused.Ni kwa nini lakini Patrick ananifanyia hivi?Nimemkosea kitu gani hadi ananitenda hivi? Vick akatamka kwa hasira
“Vero,shemeji yangu hebu tuliza hasira kidogo.” Andrew akamsihi
“andrew I’ll go crazy if I cant see Patrick tonight.maandalizi ya safari yamekwisha kamilika.Ni yeye tu ndiye anayesubiriwa.What am I going to do?? !!! Please Andrew help me to know where Patrick is.Hapatikani hata katika simu…”Vero akashindwa kujizuia akaangua kilio
“Vero please naomba unisikilize.Mama naye kanipigia simu sasa hivi akimuulizia Patrick.Mimi nilionana naye asubuhi ya leo.mama alinipigia simu na kuniagiza niende kwake nikamueleze kuwa anahitajika nyumbani.Nilimkuta akijiandaa kutoka na akanieleza kuwa amepata dharura asubuhi hiyo hivyo angekuja nyumbani mchana.Toka hapo sijaonana naye tena.”
“Oooh My God! Sasa nitafanya nini mimi? Vero akasema
“Usijali Vero bado naendelea kumtafuta na mpaka kesho nitapata jibu yuko wapi”
“Jitahidi Andrew “
“Yes Vero najitahidi sana kuwasiliana na rafiki zetu mbali mbali ili nijue yuko wapi.Kama hatatokea hadi kesho kwa nini basi nisikusindikize badala yake?
“Unasemaje????!!! Vero akauliza
“Nasema hivi kama Patrick hajatokea mpaka kesho unaonaje kama nikakusindikiza katika safari hiyo mliyopanga kwenda wote?CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Nilikuwa nakuamini sana Andrew lakini kumbe nyie wote ni kitu kimoja tu”Vero akajibu kwa hasira na kukata na kukata simu.
Andrew alichanganyikiwa kwa kitendo cha Vero kukata simu.Ni wazi alikuwa amekasirika.Alijilaumu sana kwa kujiingiza katika matatizo makubwa kama haya.Kwa takribani dakika mbili nzima alibaki ameduwaa ameishikilia simu yake.
“andrew kuna nini?
Sauti ile ya Vick inamstua toka katika jinamizi la mawazo lililomkumba ghafla.
“Hakuna kitu Vick,nilikuwa nikongea na Vero”
“Kuhusu nini?
“Kuhusu safari yao ya kwenda London kufanya shopping ya harusi yao”
“Yeye anasemaje ?
“Hana la kufanya kwani Patrick haonekani.Mimi nilijitolea kumsindikiza”
“Yeye amejibuje?
“Amekasirika na kukata simu halafu ameizima kabisa”
“Huna haya Andrew,eti umsindikize mchumba wa mtu London.Hivi unatumia akili kweli Andrew?We ndie mchumba wake?Hata ningekuwa mimi nisingekujibu.Tena amekuheshimu sana hakukutukana.Hebu achana na mambo ya watu tuangalie ya kwetu.”
Andrew hakujibu kitu.Akainamisha kichwa chini kwa sekunde kadhaa.
“Vick I’m confused”
“Na nini?
“na hali nzima ya mambo jinsi yanavyokwenda”
Vick akamsogelea Andrew akamkumbatia na kukilaza kichwa chake katika kifua kipana cha andrew .
“Usijali Mpenzi Patrick atarejea tu muda si mrefu.”Vick akasema huku akiipitisha mikono yake laini mwilini mwa andrew kiuchokozi.Andrew alielewa alichokuwa akihitaji mpenzi wake.
Saa kumi na moja za jioni dege la shirika la ndege la British airways lilitua katika uwanja wa kimataifa wa Julius Nyerere Dare s salaam.Lango la ndege lilifumguliwa na abiria wakaanza kushuka.Miongoni mwa abiria waliokuwamo katika dege hili ni Mike cambell,kijana mtanashati mwenye kila sifa ya uzuri,ambaye kila binti amuonaye angetamani awe naye.Leo hii alivaa suruali ya jeans iliyofifia na shati zuri la mikono mifupi.Kwa ujumla alikuwa amependeza vilivyo.Mike Cambell mchumba wa Happy alikuwa akitokea Marekani .Lengo kuu la safari yake hii ya tanzania lilikuwa ni kuja kumfariji mpenzi wake Happy katika maradhi yanayomsumbua pamoja na kumpongeza kwa kufanikiwa kulitwaa taji la Miss Tanzania.
Baada ya kukamilisha taratibu za uwanjani kama uhamiaji n.k Mike akatoka na kulakiwa na dereva wake aliyetoka katika ubalozi wa Marekani.Alitegemea pengine angeweza kumuona Margreth mdogo wake Happy pale uwanjani kwa kuwa alikwisha mtaarifu juu ya ujio wake lakini mpaka anamuamuru dereva aondoe gari hakumuona mtu yeyote.
Toka uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere ,safari ilikuwa ya moja kwa moja mpaka nyumbani kwa akina Happy .Anapafahamu vizuri mahala pale kwani si mara yake ya kwanza kwenda Moyoni alikuwa akiomba Mungu amsaidie aweze kukuta hali ya Happy inaendelea vizuri.Walifika nyumbani kwa akina Happy geti likafunguliwa wakaingia ndani.baada ya kushuka ndani ya gari akakutana na mama yake Happy .
“wow ! Mike karibu sana”
Alimkumbatia na kumkaribisha ndani.
Mike akaomba maji ya kunywa ya baridi sana ili aweze kulipooza joto kubwa alilokuwa analisikia.
Baada ya kunywa glasi mbili za maji akauliza aliko Happy na Margreth.Mama yake Happy akapatwa na kigugumizi cha ghafla.
“Margreth amekwenda katika mizunguko yake lakini Happy yeye amesafiri kidogo”
“amesafiri?? Mike akauliza kwa mshangao
“Ndio kasafiri” mama Happy akajibu huku akijitahidi kuuficha wasi wasi aliokuwa nao
“Kasafiri toka lini” Mike akauliza
“kasafiri leo mchana”
Mike akashika kichwa akapumua kwa nguvu.
‘Mbona umestuka Mike Ina maana hamkuwasiliana akakwambia kuwa atasafiri” mama Happy akamuuliza Mike ambaye alionyesha kuchanganyikiwa baada ya kusikia Happy amesafiri.
“Hapana mama sikuwasiliana naye. Kama niivyokuwa nimekueleza katika simu sikutaka afahamu kuhusu ujio wangu.Nilitaka nimfanyie mshangao.Lakini Margreth pia nilimtaarifu juu ya safari yangu.Happy alisema anakwenda wapi?” Mike akauliza
“Hakuniambia ni wapi anakwenda .Baada ya kujisikia nafuu aliniambia kwamba amepata safari ya dharura ya kwenda nje ya Dar es salaam.Hakuniambia safarii hiyo inahusu kitu gani.Ujumbe aliouacha ni kwamba kama ukija umsubiri hadi atakaporejea nadhani mdogo wake atakuwa alimdokezea kwamba unakuja”
Mike hakujibu kitu akatoa simu yake na na haraka haraka akazitafuta namba za Happy akapiga.Simu ilikuwa inaita ,akatabasamu.
“Yuko hewani lakini anachelewa kupokea” alisema mike
Simu iliita bila kupokelewa.Akapiga tena mara ya pili na ya tatu na ikakatika.Akapiga tena na mara hii ikawa haipatikani .Mike akapiga tena na tena lakini jibu likawa lile lile simu haipatikani tena.
“amezima simu”
Mike akaishiwa nguvu akakaa sofani.Baada ya dakika kadhaa za ukimya Mike akaomba aondoke akapumzike kwa sababu tayari kichwa chake kilikuwa kimevurugika.
Dakika kama kumi hivi toka Mike aondoke pale nyumbani Margreth akawasili.Alimkuta mama yake akiwa amekaa sebuleni akiwa mwingi wa mawazo.
“mama unaumwa? Margreth akauliza
Mama yake hakujibu kitu,alimwangalia usoni kwa makini na kumuomba aketi.
“Margreth hebu nieleze Happy kaenda wapi?Najua ni lazima unafahamu alikoenda dada yako”
“mama mimi sijui kitu chochote.Kwani wewe alikuaga anakwenda wapi?
“Hakutaka kuniambia anakwenda kupumzika wapi.Lakini wewe ni lazima utakuwa unajua kwa sababu toka ametoka hospitali ni wewe tu ambaye unaongea naye.”
“Hapana mama sijui kitu chochote kile,alivyokwambia wewe na ndivyo alivyoniambia mimi”
“Na vipi kuhuisu shemeji yako Mike?Ina maana hukujua kama anawasili leo ili uende kumpokea?
“Du! Yaani mama nimeshasahau kabisa kama Mike anakuja leo.Vipi ameshafika?
“Saa nyingi sana.Ila nyie watoto!!!Yaani mwenzenu anakuja hamtaki hata kwenda kumpokea.Halafu kitu kingine cha ajabu,amempigia simu Happy mbele yangu na Happy kakataa kupokea na mwishowe akazima simu kabisa.Hivi kuna kitu gani kinaendelea?
“Mhhhh” Margreth akaguna.Akamwacha mama yake hapo sebuleni na kuingia chumbani kwake.akajifungia na kujaribu kumpigia Happy lakini simu yake ilikuwa tayari imezimwa.akajitupa kitandani.
****************
Ni saa tatu za usiku katika hoteli ya Kobe Village chumba namba 68 kilikuwa na mwanga hafifu wa bluu.Sauti ya muziki laini ilisikika kwa mbali.Chumba chote kilikuwa kikinukia uturi mzuri wenye harufu ya ajabu.Chumba hiki kwa sasa kilikuwa katika mkao wa mahaba mazito.
Juu ya kitanda kikubwa watu wawili walikuwa wamekumbatiana wakiwa katika mahaba mazito.
“Patrick” Happy akaita kwa sauti laini,nyororo ya kimahaba huku akimchezea chezea nywele za kifuani.
“Yes darling “ Patrick akaitikia
Happy ambaye tayari macho yake mazuri meupe yalikuwa yamelegea kama amekula kungu akasema
“Patrick najilaumu sana kwa kuamua kuondoka na kukuacha peke yako.Narudia tena kuomba msamaha kwa kitendo hiki cha kukuacha peke yako na wala sintachoka kufanya hivyo tena na tena kwa sababu ni kitendo ambacho kilisababisha mimi na wewe tukatengana.Kama nisingeondoka tungekuwa na maisha yetu ya raha mstarehe.Leo hii nahisi amani na raha ya ajabu.Raha ambayo nimeikosa kwa miaka mingi.Leo hii najisikia raha ya aina yake kama niliyokuwa nikiipata kipindi tukiwa shuleni.Msisimko niliokuwa nao kipindi kile pindi nikiwa karibu nawe bado haujapotea.Nikiwa nawe sihisi tatizo lolote.Nahisi raha kila mahali”
Patrick akatabasamu akausogeza mkono wake usoni na kurudisha nyuma nywele ndefu za binti huyu mrembo ambazo tayari zilikuwa zimevurugika kutokana na kuzichezea.
“Happy hata mimi ninajisikia hivyo hivyo.Sikutaka kuamini moja kwa moja kuwa hauko tena maishani kwangu.Nilimuomba Mungu anisaidie ili kabla siku zangu hazijaisha hapa duniani niwe nimekuona walau kwa mara ya mwisho.Mungu amesikia sala yangu na tayari amenijibu.Leo hii niko nawe tena.”
Patrick akamvuta Happy karibu zaidi na kumpiga busu zito mdomoni.
‘Patrick naomba nikuulize kitu na tafadhali naomba uwe wazi kwangu.usinifiche kitu hata kidogo”
“C’mon baby uliza chochote usihofu ,kwako hata siri za baba yangu nitakupa”
Wote wawili wakacheka.
“Umeshaanza utani wako nawe”
“Usijali mama uliza”
Happy akatulia kidogo kana kwamba anakumbuka kitu kisha akauliza.
“Hivi Patrick ni kwa nini uliamua kunidangaya kuwa umekufa?
Patrick akastuka,akainuka na kukaa kitandani jasho likaanza kumchuruzika.
“What !!! ….me?…Dead?…..why ? Patrick alijikuta akitamka maneno mfululizo huku akimtazama Happy..
“Happy nashindwa kuelewa ,eti nilifanya nini??!!……..
Happy aliuona mstuko mkubwa wa wazi katika sura ya Patrick akaanza kuogopa kwani alisikia Patrick ana matatizo ya moyo.akamsogelea akamkumbatia na kumbusu akamsugua sugua shingo na kuhakikisha ile hamaki aliyokuwa nayo Patrick imekwisha halafu akaendelea
“Kama unakumbuka kipindi nimeondoka kwenda kusoma tulikuwa tunawasiliana vizuri sana.Hii ilinipa faraja na kuupunguza umbali uliokuwapo kati yetu.Lakini ilitokea siku moja ambayo kwa kweli ni vigumu sana kuisahau katika maisha yangu.Ni siku hii ndiyo iliyobadili kabisa maisha yangu,siku niliyopokea barua toka kwa dada ambaye alijifahamiha kuwa alikuwa ni jirani yenu mlikokuwa mkiishi Sumbawanga.Katika barua hiyo alisema kuwa anasikitika kunitaarifu kuwa eti umefariki dunia ukiwa gerezani kwa maradhi ya kuhara”
Patrick akasimama na kushika kiuno.
“Happy please tell me it’s a joke”
Happy akamtazama kisha akasema.
“Its not a joke Patrick.Baada ya kupata taarifa ile nilipatwa na mstuko,sikutaka kusoma tena,na wala sikuona tena faida ya kushi.You were my everything.Kwa bahati nzuri baba na mama walisafiri haraka sana na kuja kunifariji na kunifanya niendelee kuishi kwani vinginevyo ningekwisha jiua muda mrefu.Patrick ,ilipita miaka mingi bila ya kuwa na furaha na amani moyoni mwangu.Furaha yangu ulikuwa ni wewe pekee.Nilikuwa nikiomba usiku na mchana kwamba taarifa ile isiwe ya kweli na kwamba siku moja ungejitokeza lakini siku zikaenda na hukutokea.Taratibu baada ya miaka kadhaa kupita nikakubaliana na matokeo kuwa tayari umekwisha fariki.Hatimaye baada ya kumaliza masomo nikarudi nyumbani na kitu chja kwanza kukifanya ilikuwa ni kutafuta mahala ulipozikwa.Nilienda mpaka Sumbawanga nikauliza nikaambiwa kuwa familia yako ilikwisha hama muda mrefu sana.Nikaenda tena kule Iringa ulikokuwa umefungwa nikaambiwa kuwa ulihamishwa gereza na kupelekwa Songea.Nikachapa mguu hadi Songea katika gereza ulilohamishiwa pale ndipo niipoufahamu ukweli.Niliwekwa wazi kuwa ulimaliza kifungo chako na ukaachiwa huru.Pale ndipo nilifahamau kwamba hukufa gerezani na kwamba kuna uwezekano mkubwa ukawa mzima.Pamoja na kuufahamu ukweli huo nilikonda kwa kujiuliza swali moja nililokosa mtu wa kunipa jibu,kwa nini unifanyie vile?.Sikujua sababu yaw ewe kuamua kunifanyia vile yaani kusingizia umekufa na kunifanya mimi niishi maisha ya kuteseka miaka yote hii.Nimekuwa nikimuomba Mungu anikutanishe nawe ili walau nifahamu sababu iliyopelekea unifanyie vile.Patrick you were the only man I real loved and trust.I gave myself to you .Please tell me why you did that ,I’ll understand.” Happy aliongea katika hali ya uchungu sana huku ameiweka mikonoyake kifuani kuonyesha machungu aliyokuwa akiyapata
Patrick jasho lilikuwa likimtiririka kama mtu aliyemaliza mbio ndefu.Ingawa chumbani mle mlikuwa na kiyoyozi lakini hakikusaidia kulipunguza joto alilokuwa akilisikia baada ya kuipata taarifa ile.Alisimama na kuzunguka zunguka humo chumbani.
“Happy ! sijui hata nianzie wapi.I’m confused”
Happy akamsogelea akachukua kitambaa na kumfuta jasho lililokuwa likitiririka kwa fujo.
“Please tell me Patrick.Tell me everything.I’ll understand” Happy akasema kwa sautiya upole sana
“Happy sina hakika kama utaniamini na kunielewa.Ukweli ni kwamba haya yote uliyoyasema wewe kwangu mimi ni mageni kabisa.Hakuna ninachoweza kukisema au kukitolea maelezo..Niliyatoa maisha yangu kwa ajili yako ,iweje leo nijifanye nimekufa?bado hainiingii akilini . Happy kumbuka nilikuwa radhi hata kuua japo sikukusudia kwa ajili ya upendo niliokuwa nao kwako iweje leo niamue kutunga kitu ambacho kimetutenganisha?Nashindwa kupata jibu.Katika maisha yangu hakuna kitu ambacho sikupenda kukiona kama kuona ukiumia na hilo unalifahamu fika.Sasa kwa nini basi niamue kuumiza moyo ako kwa kujifanya nimekufa?
Akatulia akafuta jasho.Happy akalifungua sanduku lake dogo akatoa bahasha ambayo ilikwisha anza kuchakaa pengine ni kutokana na kushikwa mara nyingi sana.akatoa karatasi iliyokuwamo ndani ya ile bahasha na kumkabidhi Patrick.
“Barua yenyewe hii hapa hebu isome”
Patrick akatumia dakika kadhaa kuisoma barua ile.Alipomaliza kuisoma akarudia tena na tena.Uso wake wote ukajaa machozi.Midomo ikawa ikimtetemeka kwa hasira,akashindwa kitu cha kuongea.
“Umeona Patrick? Hivyo ndivyo ilivyokuwa” akasema Happy
Kikapita kimya cha dakika kadhaa hapo ndani,kila mmoja akiwaza lake.Patrick akakumbuka toka siku ya kwanza alipokutana na Happy katika kituo cha basi Mbalamaziwa Iringa na hapo ndipo ulipoanzia urafiki wao.Picha za uhusiano wao wakiwa shuleni zikamjia mpaka siku ile alipomuokoa Happy toka katika mikono ya wabakaji .Akakumbuka pia siku alipohukumiwa kifungo cha miaka mitano gerezani na mpaka siku Happy aliyokuja kumuaga kuwa anakwenda Ulaya kusoma.Ghafla akakumbuka siku alipopata taarifa toka kwa Veronika kuwa Happy ameolewa na hatarudi tena Tanzania.Alikumbuka jinsi alivyozimia kutokana na taarifa ile.Machozi yakamtoka.
Patrick akakohoa kidogo kisha kwa sauti yenye kitetemeshi akasema
“Happy nimekusikia na nimekuelewa naomba sasa na mimi nikupe hadithi yangu.Naomba unisikilize kwa makini na unielewe”
“Baada ya wewe kwenda kusoma Ulaya,huku nyuma nilihamishwa gereza na kupelekwa Songea katika gereza jipya kabisa.Siku moja nilikuwa nimepangiwa kutengeneza mazingira katika nyumba ya mkuu wa gereza.Siku hiyo mkuu wa gereza hakuwepo.Nikiwa naendelea na kazi alitokea dada mmoja ambaye alionyesha kuwa na roho ya huruma sana.Alinikaribisha chai nzuri mchana huo aaknikaribisha chakula.Ni dada mcheshi,mchangamfu,na mwenye huruma.Kwa mujibu wa maelezo yake ni kuwa pale alikuwa amekuja kumsalimu mjomba wake ambaye ndiye yule mkuu wa gereza.Baadae alijitambulisha kwangu kuwa anaitwa Veronika.Taratibu mimi na Veronika tukawa marafiki.Nilimhadithia mkasa mzima wa maisha yangu kwa sababu nilitokea kumwamini.Ukiacha wazazi wangu Veronika ndiye mtu pekee aliyekuwa akinipa moyo,kunifariji na kunipa ushirikiano wa kutosha.Muda wake ulipoisha alirudi Dar es salaam kuendelea na shughuli zake aliahidi kuwa angekuwa anakuja mara kwa mara kunitazama.Kwa hiyo nikamuomba yeye awe ni kiungo baina yetu yaani mimi na wewe.Kwa kuwa yeye aliahidi kuja mara kwa mara kuniona nikaona ni bora mawasiliano yetu yaliyokuwa yameanza kufififa yawe yakipitia kwa Veronika.Nikaandika barua na kumkabidhi ili aende akaiposti afikapo Dar es salaam.Siku moja ambayo sintakuja kuisahau alikuja Vero na kuniambia kuwa alikuwa na taarifa ambazo si njema sana.Nilijikaza kiume na kumuomba anieleze.Vero aliniambia kuwa Barua aliyokutumia imerudishwa kwa kuwa haupo tena katika chuo kile ulichokuw ukisoma.Akaendelea kusema kuwa alielekezwa mahala ulipoamia na akakupigia simu lakini ukamjibu kwa kejeli kuwa huanmuda na mimi tena, na wala huna mategemeo ya kurudi tena Tanzania.Alizidi kudai kuwa alimtumia binamu yake aishiye huko huko marekani kufanya uchunguzi na akagundua kuwa tayari ulikuwa umeolewa na tayari ulikuwa ni mjamzito.Nilianguka na kuzimia Sikutaka kuamini moja kwa moja taarifa zile lakini kwa kuwa nilikuwa kifungoni sikua na la kufanya ili kuupata ukweli.Niliwaomba wazazi wangu wanisaidie kufanya uchunguzi juu ya jambo hili lakini wao ndio hawakutaka kabisa hata kunisikia nikilitamka jina lako tena.Siku zilikwenda bila ya mawasiliano yoyote baina yetu na taratibu nikaanza kuukubali ukweli kuwa haupo tena na mimi.Mpaka siku namaliza kifungo changu sikuwa nimepata barua yoyote toka kwako.Nilimaliza kifungo na nikaanza upya tena kuyatengeneza maisha yangu.Nikasoma ,nikamaliza na hatimaye nikaanza maisha yangu ya kujitegemea.Siku moja nikiwa natazama luninga ,warembo waliokuwa wakishiriki fainali za kumtafuta mrembo wa Tanzania walikuwa wakijinadi nilikuona ukipita.Sikuamini nikaanguka na kupoteza fahamu.Na ni hapo ndipo matatizo ya moyo yalipoanza.Hakuna mtu yeyote anayefahamu nini chanzo cha maradhi yangu zaidi ya rafiki yangu wa pekee Andrew.Nilijitahidi ili niweze kukuona siku ile ya shindano lakini kwa bahati mbaya mara tu uliponiona na wewe ukapatwa na mstuko ukaanguka na kupoteza fahamu.”
Patrick akanyamaza akamwangalia Happy usoni.Macho yake yalijaa machozi.Hadithi ya Patrick ilimchoma moyo sana.Donge kubwa likamkaba kooni.Hakuwa na la kufanya zaidi ya kulia.Patrick akamuonea huruma ,akamkaribia na kumfuta machozi kwa kitambaa chance.
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“nyamaza Happy .Nyamaza mrembo wangu.Usilie tena.Hayo yameshapita”
Ilikuwa vigumu kwa Happy kunyamaza kutokana na hasira alizokuwa nazo.
“Nashindwa Patrick kunyamaza kutokana na ukatili niliofanyiwa .Ni bora mt aliyenifanyia hivi angeniua kabisa kuliko kuniacha nikiteseka kwa muda mrefu namna hii.”
Kimya kikapita .Patrick akasema
“Happy nafikiri mpaka hapa hakuna wa kumlaumu mwenzake kwa yaliyotokea.Kila mmoja amekwishapata picha halisi ya nini kilichotokea.Sisiti kusema kuwa Veronika ndiye chanzo kikubwa cha sisi kutengana.Nina imani kubwa kuwa ni yeye tu ndiye aliyeuvuruga uhusiano wetu kwa kutunga uongo huu mkubwa.Hakuna mwingine anayeweza kufanya kitu kama hiki zaidi yake.”
Patrick akainuka na kuelekea mezani huku akiwa amefura kwa hasira.
“I hate you Vero.I hate you..!!”
Alitamka maneno haya kwa hasira sana huku akitokwa na machozi.Happy aliyekuwa amekaa kitandani akaogopa.Hakuwahi kumuona Patrick akiwa katika hasira namna ile.Taratibu akamsogelea na kumshika mkono.
“Calm down Patrick.Its ok.”
“Happy I hate this woman so much.Ametutesa kwa kwa kipindi kirefu sana.Kwa nini? she must pay for this”
Happy akamwacha Patrick atulie kwanza na baada ya dakika kadhaa akasema.
“Patrick”
Patrick akastuka na kumwangalia Happy .
“Patrick” Happy akaita tena.
“Yes Happy nakusikiliza”
“After all that happened do you still love me?
Patrick akastuka kwa swali lile,akainuka na kumsogelea zaidi Happy ,akamshika mikono yake yote miwili akamtazama usoni.
“Happy ” akatulia kidogo halafu akaendelea.
“World do change,weather and climate do change,people do change,everything do change but Patrick never change.I’m the same Patrick you know,who loves you that much.Nothing has changed.Pamoja na yote yaliyotokea lakini I’ve never stoped loving you not for a second.Now that I’ve known the truth I love you even more.Do you still love me?
Kauli ile inamfanya Happy atoe machozi.Midomo inamtetemeka anashindwa kuomgea.Patrick akamuangalia machoni na kumuuliza tena.
“Happy am I still have a place in your heart ?
Happy akajikakamua na kusema
“Patrick you were the first man ever happened in my life.You were my first man I loved.You were the fisrt man to win my heart.I gave you my heart,my body,soul and everything.You were my angel,my Hero.No body will ever win my heart than u did.I’m everything I am because you loved me Patrick.Possibly there could be no Miss Tanzania Happy Kibaho now if its not for your love and sacrifices.Pamoja na yote yaliyotokea Patrick I still love you more and more.U still have chance in my heart,but I’m sorry Patrick….”
Happy akashindwa kujizuia kulia kwa sauti.
“Sorry? Sorry for what Happy ? Patrick akauliza
“Its complicated”
Patrick taratibu akahisi kama nguvu zinamuisha
“Complicated?How”
“Patrick baada ya kuamini kuwa tayari umekwisha kufa basi nikaamua kuwa na mpenzi mwingine.Mike cambell ndiye mpenzi wangu niliyenaye kwa sasa na tayari amekwisha nivisha pete ya uchumba.I’m so sorry Patrick”
Patrick alihisi kama vile kila kitu mle ndani kilikuwa kikizunguka.hakuamini kama ni kweli anaweza kumkosa Happy kirahisi rahisi namna ile.akaunyoosha mkono wa Happy na kuangalia kidoleni.Ni kweli Happy alikuwa na pete ya uchumba kidoleni.Patrick akaingalia huku machozi yakimlenga lenga.wakati Patrick akiwa ameduwaa akiiangalia ile pete ya uchumba kidoleni mwa Happy akashangaa Happy akikinyoosha kiganja chake na kukishika kidole kilichokuwa na pete ya uchumba.
“I’m right.Its complicated.Hata wewe hii si ni pete ya uchumba? Kila mmoja tayari amekwisha amua kuendelea na maisha yake.Kutokana na hali ilivyokuwa hakukuwa na matumaini ya kuonana tena.Hivyo hakuna mtu wa Kulaumiwa kwa maamuzi haya kati yetu sisi wawili.Kila mmoja hakuwa na njia nyingine zaidi ya kuamua kusahau yaliyopita na kusonga mbele na maisha yake.Kwa hiyo Patrick veronica ndiye mchumba wako?
Patrick akakabwa na donge kubwa kooni.akababaika ajibu nini.
“Happy ” Patrick akaita
“Happy nasikitika sana.Halikuwa kusudio langu kufanya hivi lakini kwa kipindi hicho sikuwa na jinsi ya kufanya niliamini kuwa tayari ndoto yetu ya kuwa pamoja imeshapotea .Niliamini moja kwa moja taarifa za vero na nikawa na hasira sana juu yako kwa kuamini kuwa ulikuwa umevunja ahadi yetu.Kweli kwa wakati huo ni Veronika pekee ndiye aliyekuwa ni mfariji wangu mkubwa.Ukaribu wetu ukaongezeka na taratibu tukajikuta tukihama toka katika urafiki wa kawaida na kuwa wapenzi.Kwa kiasi kikubwa alinisaidia kusahau mateso na maumivu niliyoyapata juu yako.Uhusiano wetu umedumu kwa muda mrefu sasa na tukaona ni bora tufunge ndoa kabisa.Hivi sasa tunavyoongea tayari maandalizi ya harusi yetu yako katika hatua zake za mwisho.Nafikiri mwezi ujao tarehe za kati kati nitafunga ndoa na vero.”
Happy alishindwa kujizuia kutoa kilio kikubwa.Patrick akamkumbatia.
“Patrick my first love.Patrick my angel,siwezi kuuzuia uchungu huu mkubwa ninaousikia moyoni mwangu.Ninaumia mno kwa kitendo hiki alichonifanyia mwanamke mwenzangu.Ni bora hata angeniua kabisa kuliko kunifanyia ukatili huu mkubwa.Patrick you were my life,and my breath.Veronika has taken you from me, my breath.Sikutegemea kama mwisho wetu ungekuwa hivi”
Happy aliongea kwa uchungu mwingi sana huku machozi mengi yakimtiririka.
“Patrick nimefurahi kuufahamu ukweli.Sikulaumu kwa yaliyotokea.Hukuwa na kosa na wala wewe hupaswi kinilaumu mimi.Kwa kuwa kila mmoja tayari amekwisha anza maisha yake mimi naona ni bora iwe hivyo.Kila mmoja atabaki ni historia kwa mwenzake.Ninachokuomba mpende zaidi Veronika.Kamwe usimfanyie jambo lolote lililo baya.Alifanya kosa,alidanganya na hii yote ni katika kulipigania penzi lako la kweli.Nakubali kushindwa.Sitaki kushindana na Vero sipendi na yeye aje aumie kama nilivyoumia mimi.Nafikiri mateso yangu ni makubwa na sidhani kama anaweza kuyavumilia kama mimi.Mimi namwachia Mungu kwani yeye………….”
“Happy ”Patrick akadakia
“No Patrick don’t say anything yet.I’m hurt.”
Chumba kilichokuwa katika hali ya mahaba mazito muda mfupi uliopita ,sasa kilikuwa ni sehemu yenye majonzi makubwa.Vilio vya chini chini ndivyo vilisikika.ILikuwa ni hali yenye kuhuzunisha sana kwa wapenzi hawa wa zamani.
Happy akamvuta Patrick karibu yake akamkumbatia kwa nguvu.Akamwachia na kumtazama usoni.Kwa sauti yenye kukata kata Happy akaimba
“Don’t,don’t go to your heart how feels.
Don’t be afraid of dreams not real,
Close ur eyes,pretend it’s just the two of us again,
Make belief, this moment’s here to stay,
Touch, touch me the way you used to do,
I know, I could be lie right here with you,
From now on ,you will be with someone else instead of me,
So tonight, let’s feel these memories.
So for the last, hold me now don’t cry, don’t say u were just, hold me now………
Time, time will be kind once we’re apart,
And ur tears, tears will no have place in ur heart.
I wish I,I could say how much I’ll miss you when ur gone,
All my love for yoy will go away……………
Happy akashindwa kuvumilia akaangua kilio kikubwa.
“No Happy !! Noo……This cant be”Patrick akasema kwa hasira.
***********************
Ulikuwa ni usiku mrefu sana na mgumu kwa Mike cambell.Kitendo cha Happy kuondoka bila kumuaga anakwenda wapi kilimchanganya akili .Kilichompa wakati mgumu zaidi ni kitendo cha Happy kumkatia simu na kisha kuizima kabisa simu yake.Kitendo hiki kilimuumiza mno.Haijawahi kutokea katika uhusiano wao.
“I real love you Happy no matter what”
Alitamka Mike kwa sauti huku akijimiminia mvinyo katika glasi.Toka amefika chumbani kwake leo hii amekuwa akinywa pombe kali kwa dhumuni la kuupunguza mzigo wa mawazo aliokuwa nao.
Alikaa tena sofani,akawaza,akachukua simu na kubonyeza namba za Happy lakini jibu likawa ni lile lile.Simu ya Happy haikuwa ikipatikana.CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Kwa jinsi ninavyomfahamu Happy lazima kutakuwa na jambo linalomsumbua akili yake.Mara nyingi akiwa na jambo linalomsumbua huwa hapendi usumbufu.Lakini ni bora basi angeongea nami japo hata kidogo tu na kunitoa wasiwasi .”
Mike akapiga funda kadhaa za mvinyo.
“I know u need to be alone for a while Happy .I will wait here for you till you come back.I hope you will be back soon.Be safe there my angel”
Mike alikuwa akiongea maneno haya kwa sauti .Ni wazi alikuwa ameanza kulemewa na kilevi.
Wakati Mike akiwa katika mtihani mgumu na kuamua kupoteza mawazo kwa kunywa mvinyo mkali,mambo yalikuwa magumu zaidi kwa Veronika.Usiku huu alikuwa katika kitanda chake akijigeuza geuza, macho yakiwa makavu na mekundu kwa kulia.Akainuka na kwenda kulifungua dirisha akachungulia nje kana kwamba kuna kitu alikuwa akitegemea kukiona.Alikaa hapo dirishani kwa muda mrefu akiziangalia nyota na mwezi.Machozi hayakuwa yakitoka tena alikuwa Amelia sana mchana kutwa.
Ni mlio wa simu yake ndio uliomstua toka katika mawazo mazito.Taratibu akaichukua simu yake na kutazama mpigaji.Alikuwa ni mama yake Patrick.
“Hallo mama”
“Veronika mwanangu unaendeleaje?
“mama naendelea hivyo hivyo tu.Vipi kuna habari yoyote mpaka sasa hivi?
“Hapana Veronika mpaka sasa sijapata taarifa zozote kuhusu mwenzio.Ila nina wazo moja”
“Ndiyo mama nakusikiliza”
“Yawezekana huyu Patrick akawa katika dharura zake kama anavyodai.Mimi naona sisi kuendelea kumsubiri ni kupoteza wakati wetu.Nionavyo mimi hataki kwenda huko Uingereza ndio maana amekuwa akikimbia kimbia.Kwa hiyo basi Vero mwanangu ili tusiendelee kupoteza muda zaidi wewe itakubidi tu uende peke yako ufanye shopping .Hatuna njia nyingine ya kufanya.Vumilia Vero namfahamu Patrick vizuri atatulia tu muda si mrefu.”
Veronika akatulia akatafakari kwa sekunde kadhaa kisha akasema
“Ok nimekuelewa mama.Nitafanya hivyo.Safari ni kesho saa tano asubuhi.Ila sintachukua muda mrefu sana nadhani baada ya siku tatu au nne nitarejea.siwezi kukaa mbali na Patrick kwa kipindi kirefu na hasa wakati huu anaoumwa umwa”
“Sawa Vero nashukuru sana mwanangu kwa kukubali kufanya hivyo.Nitakuja kukusindikiza kabla hujaondoka”
*******************
“Happy ” Patrick aliita huku akimuangalia usoni binti huyu mwenye uzuri wa kimalaika.
“Yes Patrick”akajibu Happy kwa sauti laini sana huku naye akimwangalia Patrick usoni.
“I can’t let you go.Ulinipotea mara ya kwanza nimefanikiwa kukupata tena.Safari hii hutanipotea tena.siwezi kukuacha kamwe upotee tena mikononi mwangu .Happy I love you so much.You are the only one I truly love.The only one.Please Happy stay with me.dont leave me again.”
Patrick aliongea maneno haya taratibu na kwa hisia.Ni wazi maneno haya yalitoka ndani kabisa mwa moyo wake.
“Patrick hata mimi sitaki kukupoteza tena maishani mwangu.Wewe ndiye pumzi ya maisha yangu.Wewe pekee ambaye unaweza kunifanya mimi niishi kwa furaha maisha yangu yote yaliyobakia hapa duniani.Nilikupoteza mwanzo na nimekuona tena.Nisingependa hata mimi kukupoteza tena lakini…………….”
“Lakini?’ Patrick akadakia
“Hakuna lakini Happy .Hata iweje siwezi kukubali upotee tena .Wewe ndiwe mwanamke pekee niliyekupa moyo wangu.Because I love you Happy , I will make a sacrifice for you.”
“Sacrifice?? Happy akauliza kwa mshangao.
“Yes Happy .Ninaifuta ndoa yangu na Veronika.Sintamuoa Veronika tena”
“Patrick!!!!!!!.......
Happy akapiga ukelele wa mshangao.
“Patrick please usifanye hivyo.Nakuomba Patrick niko chini ya miguu yako usifanye hivyo.Najua unanipenda na penzi lako kweli ni la dhati na kweli lakini Patrick tumekwisha umia vya kutosha.Naomba tuendelee kuumia sisi wenyewe tusiwaumize tena watu wengine zaidi.Kufuta ndoa yako na Vero ni suala rahisi kwako lakini so many people will get hurt.Watu wengi wataumia sana.Vero loves you very much and Mike loves me very much.We cant hurt the people that loves us.Patri…….”
“Happy ”Patrick akadakia.
“Please naomba unisikilize kwa makini sana.Najua kwamba uamuzi huu utaumiza watu wengi sana.Ndiyo ni wengi wataumia na kuhuzunika lakini sina namna nyingine ya kufanya zaidi ya hivyo nilivyokwambia.Siwezi kuendelea kujidanganya kwamba nitaishi kwa furaha na amani na Veronika wakati nikijua kuwa upo na bado unanipenda.Siwezi Happy kuendelea kuwa na Veroika mtu aliyetufanyia ukatili mkubwa sana .Niko tayari kuubeba mzigo wote wa lawama na kila kitu kwa ajili ya kuitafuta furaha ya maisha yangu.Nilifungwa kwa ajili ya kuzuia usidhalilishwe kwa hiyo sioni ajabu leo hii nikivunjilia mbali ndoa yangu na vero chui mwenye ngozi ya binadamu.”
Happy ambaye bado machozi yalikuwa yakimtoka alijikaza na kusema.
“Patrick ninajua una nia nzuri na mimi na uamuzi huo ni wazi umetoka ndani kabisa mwa moyo wako.Hata mimi Patrick ninaumia sana tena zaidi hata ya siku ile nilipopata taarifa zile za kufariki kwako.Ninaumia kwa sababu sijui nifanyeje ili usiende mbali na mimi tena.Lakini Patrick tayari nimempa nafasi Mike .Nilifanya vile kwa sababu nilihitaji kuwa na mtu baada ya kuamini haupo tena duniani.Pamoja na nafasi hiyo lakini nafsi yangu imekuwa nzito katika kumpa moyo wangu wote aumiliki kama nilivyofanya kwako.Bado nafsi yangu inaugulia kwa ajili yako.lakini Patrick…………………”
Happy akashindwa kuendelea kuongea akainama akilia
Patrick akamshika shingoni na kumwambia
“Lakini nini Happy ?
“Patrick tayari hatua kubwa sana zimeshapigwa katika maisha yetu ya kimahusiano.Naomba Patrick tusiendelee kuwamiza watu wengine tena.naomba usimuache Vero kwa aijli yangu.Sijui kama ninatweza kuachana na Mike kwa sababu ananipenda kupita kitu chochote”
Patrick akamtazama Happy kwa sekunde kadhaa kisha akasema
“Happy please look at me.Look at me and tell me that U don’t lome me any more.I will understand and let you go.”
Happy akainua uso wake na kumtazama Patrick .
“ooh Patrick please don’t leave me.I love u so much”
Happy akajikuta akijilaza kifuani kwa Patrick na kumkumbatia kwa nguvu.
“patrick I love you so much.Please Patrick don’t ever leave me again.”
“Its ok Happy it’s ok my angel. I won’t let you out of my hands again”
Happy akamkumbatia kwa nguvu zaidi Patrick .Taratibu Patrick akaanza kuzichezea nywele nzuri na ndefu za Happy .Mkono wa kulia ukashika hadi shingoni na kuisugua taratibu kisha kwa pozi za aina yake ukashuka kuelekea mgongoni ukipita kati kati kabisa ya mgongo kana kwamba anapiga kinanda.Happy akastuka.
“ouh Patrick I love you.”
Wakatazamana na taratibu sana kama inavutwa na sumaku midomo ikaanza kukaribiana na mara ikakutana na zoezi tamu la kunyonyana ndimi likaanza.
‘ouh Patrick my baby don’t ever leave me again” alisema Happy kwa sauti ya kuhema iliyojaa raha.
Patrick hakusema kitu taratibu akaanza kufungua vifungo vya shati alilokuwa amevaa Happy akalitoa na kulitupa pembeni.Moyo ukazidi kumwenda mbio baada ya kukutana na kifua kile cha Happy chenye kusisimua.Hakutaka kuwa na papara kwani tayari alijua kila kitu ni chake kwa usiku huo.Akampiga busu zito mdomoni kisha akaifungua sidiria nyeupe aliyokuwa ameivaa Happy akakutana na chuchu nzuri za mlimbwende huyu ambazo zinazidi kumpa wazimu Patrick.Kwa ufundi wa aina yake akaanza kuzinyonya chuchu zile huku Happy akitoa mguno kwa raha aliyoisikia.Wakati akinyonya chuchu zile mkono wake wa kulia ukawa ukiifungua zipu ya sketi fupi aliyokuwa ameivaa Happy akafanikiwa kuifungua na taratibu akaishusha chini.Happy alikuwa amezidiwa na utamu na hata maneno aliyokuwa akiyatamka yalikuwa hayasikiki vizuri.Taratibu Patrick akaanza kushuka chini mpaka maeneo ya kitovuni na halafu chini yake zaidi.Mambo aliyoyafanya hapo siwezi yaelezea.Happy alikuwa akitoa miguno kana kwamba anataka kufa.
“Patrick I…It’s..my first…time don’t hurt me.”
Happy akasema kwa kukata kata.Happy hakuwahi kukutana na mwanaume yeyote kabla.Patrick alistuka kusikia hivyo.Hakutegemea kama msichana mzuri kama Happy angeweza kuutunza usichana wake mpaka wakati ule.
Kwa kuwa ilikuwa ni mara ya kwanza kwa Happy ,Patrick akapunguza kasi na kwenda taratibu ili mrembo huyu asiumie.
Happy akatoa mguno wa maumivu.Tayari usichana wake ulikuwa umeondolewa.
*****************
Ni saa nne asubuhi wakati Mike Cambell aliposimamisha gari nyumbani kwa akina Happy .Moja kwa moja akafululiza mpaka ndani na kumkuta mama yake Happy .
‘ Mike karibu baba” akasema mama yake Happy
“Ahsante mama shikamoo”
“Marahaba mwanangu,karibu sana”
“Ahsante mama.Kuna taarifa zozote za Happy ?
“Hapana baba mpaka sasa hivi hatuna taarifa zozote za Happy .Bado simu yake haipatikani.Vipi wewe una taarifa zozote ?
“Hapana mama .Bado sijapata hata ujumbe wowote toka kwake”
“Jamani mtoto huyu kwa nini lakini anafanya hivi?
“Mama,nafikiri labda tuwe wavumilivu ,tumwache kidogo pengine ni wazi anahitaji kuwa peke yake kwa kipindi hiki.Nina imani huko aliko yuko salama salimini na ni lazima atarejea salama”Mike akasema lakini ni wazi moyoni alikuwa ameumia sana.
“Nashukuru sana baba kwa kuwa mwelewa.Mimi mara tu nitakapopata taarifa yake nitakutaarifu mara moja”
“Sawa mama nashukuru”
Mike aliaga na kuondoka.Mama yake Happy alilisindikiza gari lile la Mike kwa macho mpaka likapotea kabisa.Alipogeuka akakutana na Margreth.
“ Mike anasemaje? Margreth akauliza
Mama yake akamtazama kwa sekunde kadhaa
“Hivi nyie watoto kwa nini mnamfanyia hivi mwenzenu?
“Mwenzetu yupi mama?
”Si Mike? Hivi hamuoni kuwa mnavyomfanyia si vizuri?Happy hataki kuwasiliana naye ,hata wewe unamkwepa shemeji yako.Kwa nini lakini?
Margreth hakujibu kitu akatazama chini
“mama mi naogopa hata kumwangalia kwa sababu atahisi ni lazima ninajua Happy yuko wapi”
“Mhhh!!!! …….haya” Mama yake akaguna na kuondoka
***************
SIKU NNE BAADAE - ARUSHA
“Happy darl ni siku ya nne leo tangu tumefika hapa Arusha.Najua ni lazima huko tulikoondoka watakuwa na wasi wasi mwingi kwa sababu tangu tumefika hapa simu zetu zote tumezima.Nimefikiria nimeona nimpigie simu mama yangu ili nimtoe wasi wasi.’
Happy aliyekuwa amejilaza katika kiti kilichokuwa pembezoni mwa bwawa la kuogelea ,alimtazama Patrick kwa sekunde kadhaa kisha akasema.
“Ok baby ,ni wazo zuri ,ingawa mimi sikuhitaji kufanya hivyo kwa sasa lakini kwa vile umeomba basi sawa hata mimi itanibidi nifanye hivyo.”
Wakainuka na kuelekea chumbani kwao.
Patrick akaishika simu yake akaitazama kisha akaiwasha.Jumbe fupi za maneno zikaingia mfululizo .Hakusumbuika nazo moja kwa moja akaandika namba za mama yake na kumpigia.
“Haloo mama shikamoo” Akasema Patrick baada ya mama yake kupokea simu
“ Patrick hujambo? Uko wapi we mtoto,mbona unatuweka roho juu namna hiyo?Hatulali tunakuwaza wewe,Vero anapiga simu usiku na mchana kukuulizia,Uko wapi na unafanya nini wewe mt…..” Patrick hakutaka kumpa mama yake nafasi kubw ya kuongea,ikamlazimu kuingilia kati.
“Mama us……………..”CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Kabla hajaendelea mama yake naye akadakia
“Baba yako kawa mbogo huku ,kila siku tunakwaruzana kwamba mimi na wewe letu moja.Sasa ni lini unarudi we mtoto?
“Mama usijali,mimi ni mtu mzima na ninajua kitu ninachokifanya.Watoe shaka watu wote mimi niko salama salimini na muda wowote ninakuja nyumbani.Ni kama nilivyokueleza nilipatwa na dharura ndo maana nikaondoka ghafla vile.”
“lakini Patrick mwanangu hivi hizo dharura zako ni muhimu kuliko suala la ndoa yako? Hivi hizo dharura zina msaada gani katika ndoa yako?Andglia mwanangu harusi ni mwezi ujaona kikao cha mwisho ni wiki ijayo kisha ndoa ikaandikishwe kanisani na kuanza kutangazwa.Sasa huoni kuwa unahitaji kuwa karibu sana kwa wakati huu?
“Nalielewa hilo mama na mojawapo ya mambo yaliyonileta huku ni kuhusiana moja kwa moja na hiyo harusi yangu,hivyo usijali mama,ila tafadhali naomba kikao cha mwisho kisikae kama nitakuwa sijarudi.nataka niwepo katika kikao hicho nina jambo kubwa la muhimu sana la kuongea na kamati nzima pamoja na nyie wazazi wangu”
Mama yake Patrick akanyamaza kidogo kisha akastuliwa na Patrick.
“Mama naomba nikate simu .wasalimu wote hapo nyumbani ila tafadhali naomba unifikishie ujumbe wangu huo kwa kamati. Bye mama.I love you.”
Patrick akakata simu kisha akapumua kwa nguvu.
“Darling kuna tatizo lolote? Happy akauliza baada ya kumuona Patrick akionekana kuzama katika mawazo ghafla.
“Hapana dear hakuna tatizo lolote,ngoja kwanza niongee na Andrew”
Patrick akazitafuta namba za Andrew na kumpigia.
“Yes Comrade” Aliita Patrick baada ya simu yake kupokelewa na Andrew .
“wow!Patrick how are you?
“I’m great andrew”
“hahahah mambo yanakwendaje hapo Arusha brother kwa sababu naona umekaa kimya kabisa ..”
“Du ! Andrew huku ni burudani kila sekunde,.Tayari tumeshamaliza matatizo yetu na kwa sasa tumeazimia tunaanza upya.”
“Wow! That’s great”Akasema Andrew
“sasa andrew sina muda muda mrefu sana wa kuongea na simu hebu nipe japo kwa muhtasari juu ya hali ya mambo yanavyokwenda hapo Dar.Nimetoka kuongea na mama sasa hivi anapiga kelele huyo hadi nikakata simu”
“Patrick huku mambo ndo yanazidi kupamba moto.maandalizi yanaendelea kwa kasi ya ajabu.Kadi ziko tayari na kinachosubiriwa ni kikao cha mwisho cha kamati ya maandalizi kikae ili kuangalia kama kuna kitu kilichobakia kabla ya kutangaza rasmi tarehe ya kufunga ndoa.Vero alienda Uingereza japo kwa shingo upande na kila siku ananipigia simu kama ninataarifa zozote.Watu wanahaha kutaka kujua uko wapi .Yaani ninapata shida sana manake kila mmoja anajua kuwa ni lazima nitakuwa ninajua mahala ulipo.”
“du ! pole sana Andrew.I’m very sorry to involve you in this issue.Nakuomba uwe mvumilivu rafiki yangu bado yatakuja makubwa zaidi ya hayo.Mimi nitarudi muda wowote kwa sababu nataka niwepo siku kikao cha mwisho kitakapokaa.Nina mambo ya kuongea na wanakamati .Kwa sasa bado ninaendelea kula bata na mrembo wangu”
“Sawa Patrick mimi nitafanya kila linalowezekana kufanyika.”
“Ok andrew nitakuwa nakupigia mara kwa mara ingawa muda mwingi simu yangu itakuwa imezimwa.”
“Ok brother take care”
Patrick akakata simu na kumwangalia Happy .
“Mbona Vero humpigii simu?
“Mhh ! forget about her”Akasema Patrick huku akimpa simu Happy
‘Ongea na mama mtoe wasi wasi najua atakuwa na wasi wasi mwingi juu yako kwani toka umefika hapa hujawasiliana naye na kumjulisha unaendeleaje”
Happy akaandika namba za mama yake na kupiga
“Haloo mama shikamoo”
“wow! Happy .Hujambo mwanangu?
“Sijambo mama vipi hapo nyumbani wazima?
“Huku wote wazima Happy ,roho zetu juu juu kwa sababu yako.Lini utarudi? Na mbona simu yako haipatikani?
“Mama msiwe na wasi wasi mi ni mzima kabisa na muda wowote ninaweza kurudi nyumbani.Simu yangu kwa bahati mbaya haina chaji hata kidogo ndio maana imezima.”
“Sawa Happy mi nafurahi kusikia uko salama.lakini ni kwa nini hutaki kumpigia simu Mike?Hivi unajua ni kwa kiasi gani unavyomtesa mwenzio?.Hebu anagali mwenzio katoka Marekani kuja kukupa hongera kwa ushindi wako lakini wewe ndio kwanza hata kumwona hutaki kwa nini lakini Happy ?
Happy akapatwa na kigugumizi cha ghafla akashindwa ajibu nini akanyamaza kimya kwa sekunde kadhaa.
“Happy nakuuliza kwa nini unamfanyia hivyo mchumba wako?
Mamayake akaendelea kuhoji
“Mom please I have to go,bye”
Happy akaikata simu na kumpa Patrick ambaye aliizima kabisa.Patrick alikwisha ng’amua kuwa mambo katu hayakuwa mazuri kwa Happy .
“Happy my baby” Akasema Patrick huku amemshika Happy mkono
“Calm down my sweet love.This is just the beginning .You have to be strong”
Kikapita kimya kifupi halafu Patrick akauliza
“Mama alikuwa anasemaje?
“Alihitaji kufahamu nitarudi lini na ni kwa nini siwasiliani na Mike.Patrick nilikubali kumpa moyo wangu Mike kwa sababu kwa wakati huo nilijua tayari umeshafariki.Laiti ningelijua kuwa badio upo hai nisingempa moyo wangu Mike.Lakini kwa vile tumeshaonana na wewe ndie mwanaume pekee nikupendaye duniani,basi sina budi kuwa wazi kwa Mike.It hurts lakini sina jinsi ni lazima nimweleze ukweli.Patrick ulinipotea mara ya kwanza lakini safari hii hutaweza kunipotea tena.I’ll fight for you”
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
ITAENDELEA
.jpeg)