Simulizi: Miss Tanzania Sehemu Ya 05.

ADMIN
0

 


ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA


Happy akaikata simu na kumpa Patrick ambaye aliizima kabisa.Patrick alikwisha ng’amua kuwa mambo katu hayakuwa mazuri kwa Happy .


“Happy my baby” Akasema Patrick huku amemshika Happy mkono


“Calm down my sweet love.This is just the beginning .You have to be strong”


Kikapita kimya kifupi halafu Patrick akauliza


“Mama alikuwa anasemaje?


“Alihitaji kufahamu nitarudi lini na ni kwa nini siwasiliani na Mike.Patrick nilikubali kumpa moyo wangu Mike kwa sababu kwa wakati huo nilijua tayari umeshafariki.Laiti ningelijua kuwa badio upo hai nisingempa moyo wangu Mike.Lakini kwa vile tumeshaonana na wewe ndie mwanaume pekee nikupendaye duniani,basi sina budi kuwa wazi kwa Mike.It hurts lakini sina jinsi ni lazima nimweleze ukweli.Patrick ulinipotea mara ya kwanza lakini safari hii hutaweza kunipotea tena.I’ll fight for you”


ENDELEA........................


“MISS TANZANIA ATOWEKA NYUMBANI,MREMBO WA TANZANIA ATOROKA,HAPPY KIBAHO HAJULIKANI ALIPO,WASI WASI WATANDA JUU YA MAISHA YA HAPPY KIBAHO,MASKINI MISS TANZANIA…Hivi ni baadhi tu ya vichwa vya habari ambayo vilikuwa vikipamba kurasa za mbele za magazeti hasa yale ya udaku.Magazeti mengi yaliandika habari nyingi zinazohusiana na kutoonekana hadharani kwa mrembo mpya wa Tanzania,Happy kibaho lakini karibu magazeti yote hakuna hata moja ambalo lilikuwa na taarifa za ukweli juu ya wapi alipo Happy kibaho.


Wakiwa bado Arusha Patrick na Happy waliyasoma magazeti yote na kila kilichoandikwa ,wakacheka sana.


“Umekuwa maarufu sana kwa sasa” Patrick akasema


“mhh yaani wanavyonifuatilia !!’


“Na huu ni mwanzo tu Happy bado watakufuatilia sana katika kila jambo unalolifanya.Kila utakachokifanya itakuwa ni biashara kwao.Unatakiwa uwe jasiri sana na hasa katika hiki kizungumkuti kilichoko mbele yetu,mengi yatasemwa na mengi yataandikwa.Ningependa sana uwe mrembo mwenye sifa nzuri kama Nancy sumari,kama Hoyce Temu.Katika vipindi vyao vya kuvaa taji la miss Tanzania hawakuwa na kashfa yoyote ile iliyoyachafua majina yao.Nitafurahi ikiwa utafuata nyendo zao.”


“Nakuunga mkono Patrick ,unajua Nancy ndiye aliyenivutia mimi mpaka nikaingia katika fani hii ya urembo.Nampenda na nitafurahi sana kama nitafanikiwa kuwa kama yeye yaani kumaliza kipindi cha kulivaa taji hili bila kuwa na skendo yoyote mbaya katika jamii”


Wakakumbatiana na kucheka.


“Happy darl kuwa nawe hapa najiona ni kama vile ninaishi mbingu ya saba mbali na matatizo lukukiya dunia hii.Ninasikitika sana kwamba inatubidi turejee Dar.Nina imani kila mmoja wetu anafurahia sana kuwepo hapa lakini hatwezi kukaa hapa kwa muda mrefu kwa sababu bado tuna majukumu mengine ya kufanya huko tulikotoka na kubwa zaidi ni hili suala letu.Kikao cha mwisho cha harusi yangu kinakaribia hivyo inanibidi niwepo kabla ya kikao hicho na kuweka kila kitu bayana na hatimaye kuuvunja rasmi uchumba wangu na Vero kisha niufungue ukurasa mpya wa maisha yangu ya furaha.Halikadhalika wewe pia unatakiwa uende nyumbani kabla Mike hajaondoka na kufanya kama tulivyokubaliana.”


“ Kweli kabisa Patrick hata mimi nilikuwa na wazo hilo hilo.Hatuwezi kukaa hapa kwa muda mrefu sana wakati kuna jukumu zito linatukabili mbeleni.Ni wazi tunatakiwa kurudi dar”


“Ouh Gosh! Kumbe tulikuwa na wazo moja? Kwa nini sasa hukunieleza kama na wewe ulikuwa ukiwaza hivyo hivyo?Kuhusu usafiri usihofu,nitaongea na Andrew atatutumia gari la kuja kutuchukua hapo kesho.”


***************************CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/


Saa kumi na dakika saba gari aina ya Toyota Surf yenye vioo vyeusi ilifunga breki mbele ya lango la nyumba ya akina Happy .Mlango wa kulia ukafunguliwa akashuka Patrick kijana mtanashati akazunguka na kuufungua mlango mwingine akashuka mrembo mpya wa Tanzania Happy kibaho,tayari walikwisha fika Dar wakitokea Arusha.Kwa takribani dakika tano hivi walizitumia kuagana kisha Patrick akaingia garini na kuondoka.Happy alibaki amesimama pale huku mkono wake ukiwa katika hali ya kupungwa,hadi gari lilipopotea kabisa machoni pake


“I looo…..oove…uuuuuu….Pa…aaa.tri…ck…..”Alisema Happy huku machozi yakimlenga ,mara geti likafunguliwa akatoka mtumishi wa ndani.


“wow! Dada Happy !!!!!!!!!!!!!!”


Happy akastuliwa na sauti ile kugeuka akakuta ni Christina .


‘wow Tina”


Wakakumbatiana kwa furaha .Tina akamshika Happy mkono na kumuongoza mpaka ndani.Huko ndani ilikuwa ni furaha isiyo na kifani ,kila mtu aliruka ruka na kushangilia kwa nguvu Happy kurudi tena.


“Karibu sana mwanangu”Akasema mama yake


“Ahsante mama nimeshakaribia”


“habari za huko utokako”


“huko kwema mama,sijui nyie hapa”


“Sie huku wote wazima kabisa ila hofu yetu kubwa ilikuwa kwako.Tunashukuru Mungu umerudi salama.”


“Hata mimi nashukuru sana mama kama nyote mu wazima.I missed you so much”


Kisha salimiana Happy akaenda kuoga halafu akajifungia chumbani kwake akaanza kutafakari jinsi atakavyoweza kuutekeleza mpango wake wa kuachana na mchumba wake Mike cambell.kabla hajaanza kuwazua ni nini afanye simu yake inalia.Akaichukua na kuangalia ni nani mpigaji akakuta ni Patrick,Happy akatabasamu .


“Haloo my sweet love”


“Haloo darling vipi umepumzika?


“Yes Patrick nimejipumzisha kitandani”


“Ouh I’ve already missed you”


“mhh Patrick jamani hata masaa mawili hayajapita!!!


“Yeah I miss u a lot already.I miss you each second Happy ”


“Hahahahahaa….Mwaaaaaaa.I love you Patrick”


“I love you too Happy ”


“Ok my baby boy ngoja mi nipumzike tutawasiliana baadae.”


“Ok Happy hata mimi ndo najiandaa niende kwa andrew kisha nitapita nyumbani nikamuone mama”


“Ok bye love”


Baada ya kukata simu Happy akaendelea kuitazama simu ile huku akitabasamu.


“Mhh ! kila ninapoisikia sauti ya Patrick nahisi mwili wote unanichemka.I love him so much,and I’ll do anything for him”


Wakati akimuwaza Patrick mara sura ya Mike ikamjia akilini Happy akashindwa kujizuia akaangusha machozi.


“I’m sorry Mike but I have to do this.”


Akachukua simu yake tena na kuzitafuta namba ambazo Mike huwa anazitumia pindi awapo Tanzania akapiga.


“Hallow baby”ilikuwa ni sauti ya upole ya Mike cambell.


“Hallow Mike how are you”


“wow Happy unajisikiaje sasa hivi?


“Najisikia vizuri Mike,nashukuru sana kwa kuja kunitazama”


“Nashukuru hata mimi kama umerudi salama.Nilipata taarifa za ushindi wako na ghafla nikapata taarifa nyingine kuwa ulipoteza fahamu baada ya kutangazwa mshindi.Pole sana haya ni mambo ya kawaida.Nililazimika kuomba dharura ya wiki mbili ili nije kukaa nawe kwa kipindi hiki ambacho najua unanihitaji sana,lakini nilipofika mama akaniambia kuwa haupo umesafiri kidogo nje ya Dar es salaam .Sikutaka kukusumbua kwani nilijua unahitaji kuwa peke yako kwa kipindi hicho.Nafurahi umerudi salama” Mike akasema


“Mike naomba unisamehe kwa kutowasiliana nawe .Mambo mengi yalinitokea hapa kati kati hivyo nlihitaji kuwa peke yangu.Samahani sana kwa hilo”


“Usijali Happy nalitambua hilo na kuyaheshimu maamuzi yako.dont worry I’ll always be there for you my sweet baby.All I want is you to be happy.Happy I want to remind you that anytime you need a shoulder to cry on just count on me.I’m here for you”


Maneno haya yanamchoma sana Happy na kujikuta akitokwa na machozi ,alishindwa ajibu nini ,mara akastuliwa na sauti ya Mike.


“Happy niko njiani nakuja nina hamu sana ya kukuona na kukupa pongezi zangu na kama utakuwa unajisikia vizuri basi tunaweza kutoka out kwa ajili ya dinner.


“Thanx Mike,nashukuru sana lakini najisikia kichwa kinaniuma mno.Nadhani nahitaji kupumzika Hivi kwa nini tusionane kesho?


“Ok Happy kama umeamua hivyo basi vizuri.Jiandae kesho tutoke kwa chakula cha mchana .”Mike alisema kwa sauti ambayo ilionyesha dhahiri kuwa hakuwa ameridhika na maamuzi yale ya Happy .


“sawa Mike nashukuru sana ,tuonane hiyo kesho”


“Ok Happy have a nice rest.I love you………………..”


Happy akashindwa atamke nini ,midomo ikawa mizito machozi yakimtoka.Akakata simu na kujitupa kitandani.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/


“Mike I’m sorry I didn’t want this to happen to our relation but its already happened.I’m sorry……….”


*****************


“Hello Komrade” Andrew akasema huku akimkumbatIa rafikiye Patrick kwa furaha mara baada ya kufungua mlango na kumkuta amesimama mlangoni


“Hello Andrew” Patick akasema huku akitabasamu


Andrew akaushika mkono wa patrick akauinua kidogo na kuuminya halafu akacheka kicheko kikubwa.


“Brother naona mambo ya Arusha hayakuwa madogo.Siku hizi chache tu naona hata mwili umeongezeka. “


Wote wakacheka kicheko kikubwa na kuketi sofani.Andrew ambaye ndiyo kwanza alikuwa amerejea toka katika shughuli zake,akaelekea chumba cha chakula kisha akarejea sebuileni na chupa kubwa ya mvinyo.


“Nashukuru umerudi salama.Hamkupata tatizo lolote njiani?”


Akasema Andrew huku akiweka chupa ile mezani na kuumimina mvinyo katika glasi akampatia Patrick glasi moja.


“hatukupata tatizo lolote njiani.Nashukur yule dereva uliyemtuna ni mahiri mno.” Patrick akasema


“Kaka nipe habari za Arusha.Mambo yamekwendaje? Happy hajambo? Andrew akauliza huku akitabasamu baada ya kupiga funda la mvinyo.Patrick naye akainua glasi yake akapiga funda moja halafu akalegeza tai yake na kusema


“Andrew namshukuru Mungu kwa sababu mambo yaliyotokea Arusha sikuyategemea kabisa.Ndugu yangu sikufichi nilikuwa najihisi kama niko peponi kwa raha nilizokuwa napata .Kama isingekuwa ni masuala haya ya harusi nisingerejea mapema hivi.” Patrick akanyamaza na kunywa tena funda la mvinyo halafu akaendelea


“Happy alifika Arusha kama tulivyokuwa tumepanga.Mara tulipokutanisha macho nilihisi kama ninapaa kwa furaha niliyoipata.Sikuwa nimetegemea kama ningekuja kuonana tena na Happy maishani.Tulikuwa na maongezi marefu sana siku hiyo.Tulikumbushana toka siku ya kwanza tulipokutana ,mambo yote yaliyotokea hadi siku niliyoingia gerezani.Happy alilia sana.Tulikumbuka mambo mengi mno.Tulikumbuka nyakati zetu za furaha na hata nyakati zile tulizokuwa katika wakati mgumu na hasa wakati ule tuliposimamishwa shule kwa kosa la kupigana darasani halafu tukaenda kujificha Bagamoyo ambako ndiko penzi letu lilikoanzia.” Patrick akanyamaza akanywa tena funda la mvinyo halafu akaendelea na maongezi.Andrew alikuwa kimya akimsikiliza.


“Andrew mambo yaliyotokea huko ni makubwa na ya kushangaza sana”


“Patrick hebu niambie ,mambo gani hayo yaliyotokea huko? Nina hamu ya kutaka kufahamu kilichoendelea huko Arusha” Andrew akasema huku akiifungua tai yake na kuitupa pembeni.


“we real had a great time”


“Usiku wa siku ile ya kwanza happy aliniuliza kitu ambacho kilinistua na kunishangaza sana.Aliniuliza eti ni kwa nini niliamua kumdanganya kwamba nimefariki dunia wakati ningali hai? “


“Etu ulifanya nini? Andrew akauliza kwa mshangao


“Anadai nilidanganya kwamba nimefariki dunia”


“Enhee wewe ukamjibuje?


“Kwanza swali lile lilinistua sana japokuwa hata Margreth alikwisha nidokeza kuhusu kuwepo kwa jambo hilo la mimi kudai nimefariki dunia.Nilimtuliza na taratibu nikamuomba anielezee kwa undani kuhusiana na mkasa ule kwa sababu mimi ndiyo kwanza niliusikia.Alianza kunieleza kwamba akiwa chuoni alipokea barua toka kwa mtu ambaye alijitambulisha kwamba ni mtu anayenifahamu mimi na familia yangu na kwa kuwa anaufahamu uhasiano wetu aliamua kumpa taarifa ambazo hazikuwa nzuri hata kidogo.Mtu huyo aliyemuandikia barua hiyo alidai kwamba Patrick yaani mimi ,nilifariki kwa ugonjwa wa kuhara nikiwa gerezani.Nikinukuu maelezo yake anasema kwamba almanusura ajitoe uhaibaada ya kuipata taarifa ile kwa sababu hakuona ni namna gani angeweza kuishi bila mimi.Ilimchukua muda mrefu sana kuja kukubaliana na ukweli kwamba nimefariki.Baada tu ya kumaliza masomo yake alirudi nchini na kitu cha kwanza alichokifanya ni kuanza kutafuta mahala nilipokuwa nimezikwa.Alikwenda hadi Sumbawanga ,mahala tulikokuwa tukiishi kabla ya baba hajastaafu utumishi serikalini akambiwa kwamba familia yangu ilihama kitambo baada ya baba kustaafu kazi.Toka Sumbawanga akaenda hadi Iringa katika gereza nililoanza kutumikia kifungo akaambiwa kwamba nilihamishwa pale gerezani na kwenda Songea nikiwa mzima wa afya.Hakukata tamaa akaenda tena hadi Songea ambako taarifa aliyoipata ilisema kwamba nilimaliza kifungo changu na kufanikiwa kutoka gerezani salama salimini.Majibu haya yalimpa wakati mgumu sana na kumfanya azidi kuchanganyikiwa kwani aligundua sikuwa nimekufa.Kwa mujibu wa maelezo yake,siku ile aliposhinda taji la Miss tanzania alipoteza fahamu baada ya kuiona sura yangu.Hakuamini kama kweli ni mimi au ni mzuka anaouona” Patrick akanyamaza ,akamtazama rafiki yake aliyekuwa kimya akimsikiliza


“Enhee ikawaje baada ya hapo? Andrew akauliza


“baada ya hapo ikanibidi na mimi nimweleze ukweli kwamba nilipokea taarifa toka kwa Vero niliyekuwa nikimtumia kama kiungo cha mawasiliano baina yangu na Happy .Taarifa hiyo ilisema kwamba yeye Happy amepata mchumba wa kizungu na tayari ana ujauzito na kwa sasa wanaishi pamoja kama mume na mke.Nilimweleza ni jinsi gani nilivyoumizwa na taarifa ile.Happy alilia sana hadi nikamuonea huruma.Alinilaumu sana kwa kuwa mwepesi wa kuamini taarifa kama ile hali nikijua kwamba alikuwa akinipenda kwa moyo wake wote.” Patrick akatulia akanywa tena mvinyo halafu akakohoa kidogo.Andrew akainuka na kuwasha feni alianza kuhisi joto.


“Enhee ikawaje tena? Akauliza Andrew huku akiongeza mvinyo katika glasi yake.


“Kilichofuata ikatubidi tukae kwa pamoja na kutafakari ni kwa nini mambo haya yalitokea.Tuligundua kwamba taarifa zile mbili zilikuwa na lengo la kuuvunja kabisa uhusiano wetu.Swali likaja ni nani ambaye aliamua kutufanyia ukatili wa namna ile? Ni nani ambaye alihitaji mimi na Happy tutengane? Happy akanionyesha ile barua aliyotumiwa ambayo ameitunza hadi hivi sasa.Nilistuka mno baada ya kuutambua mwandiko .Ulikuwa ni mwandiko wa Vero.Andrew nilihisi kuishiwa nguvu baada ya kuligundua hilo” Patrick akatulia kidogo na kuinama chini.Andrew akastuka na kusema kwa sauti ndogo


“Ouh My God ! ..Hii sasa ni hadithi mpya”


Pamoja na feni iliyokuwa ikipuliza mle sebuleni na kuipooza hali ya hwea iliyokuwa ya joto,Andrew alikuwa akitoka jasho jingi.


“Pat..patri..Patrick ngoja nikachukue barafu katika friji naona imeisha hapa” Andrew akasema kwa sauti yenye kitetemeshi huku akiinuka na kuelekea chumba cha kulia chakula.Alipofika katika friji akahisi kama mikono yake imeisha nguvu ,akaeliegemea friji.


“Ee Mungu naomba unipe nguvu ya kustahimii kipindi kigumu kinachokwenda kuanza muda si mrefu.” Andrew akaomba kimoyo moyo akiwa bado ameliinamia kabati.


“Nimestuka sana kusikia kwamba Vero ndiye aliyewatenganisha Patrick na Happy.Pamoja na kwamba ni muda mrefu wametengana na Patrick kwa sasa anakamilisha maandalizi ya harusi yake na Vero lakini bado hajaacha kumzungumzia Happy.Kila tukikaa huwa anamkumbuka .Kwa jinsi Patrick anavyompenda Happy ,sina haja ya kuuliza kwani jibu liko wazi,hapa hakuna ndoa tena.Nahisi kuishiwa nguvu…….”


Andrew akachukua barafu na kurejea sebuleni.Patrick alikuwa ameegemeza kichwa katika ukingo wa sofa huku mkono wake mmoja ukiwa umelishika shavu lake.


“Enhee endelea kunipa michapo ya Arusha.Ikawaje baada ya kugundua kwamba ni Veronika ndiye aliyesababisha mambo haya yote? Andrew akauliza


“kwanza Happy alilia sana.Mimi kwa upande wangu nilipandwa na hasira za ajabu .Sikuamini kama Vero anaweza akafanya kitendo cha namna ile.Niliumia sana Andrew.”


“Du ! haya mambo ni makubwa sasa” Andrew akasema


“Ilituchukua muda mrefu sana kuliongelea jambo hilo lakini kuna kitu kiliibuka ambacho kiliniuma sana”


“Kitu gani hicho?


“Happy alikuwa na pete ya uchumba kidoleni”


“Ina maana tayari Happy ana mchumba? Andrew akauliza huku akishusha pumzi


“kweli Andrew.Tayari Happy ana mchumba.Baada ya kukaa muda mrefu bila kuniona aliamua kumpa nafasi mtu mwingine.”


“Too bad.” Andrew akasikitika


“Na wewe ulimweleza kuhusu harusi yako na Vero? Andrew akauliza tena


“Ndiyo Andrew.Hatukutaka kufichana chochote.Tuliweka bayana kila kitu bila kuficha chochote” Patrick akasema


“Baada ya hapo nini kiliendelea? Andrew akauliza huku akitabasamu


“Kilichofuata baada ya hapo tuliiweka dunia yote na matatizo yake kando, tukaingia katika ulimwengu mwingine kabisa wenye raha zisizoelezeka.Andrew nilihisi raha ambayo sijawahi kuipata toka nimezaliwa.Nilijiona ni mwenye bahati kubwa kuwa na mrembo kama yule”


“wow ! maelezo yako yananifanya nijenge picha ya jinsi mambo yalivyokuwa.Tell me about that first night ? Akasema Andrew


“Andrew ,ule ulikuwa ni usiku wangu wa kwanza kuhisi kama niko peponi.Nilihisi kama siko katika dunia hii iliyojaa shida na mahangaiko.Sijawahi kuwa na usiku kama ule.Sikufichi Andrew,Happy ni msichana aliyebarikiwa mno.She’s so sweet” Patrick akasema na kumfanaya Andrew acheke wakagonganisha mikono.


“You had sex with her? Andrew akauliza.Huku akicheka Patrick akasema


“Yes we had .and one thing that you cant agree is that she was still a virgin.I was her first man” Patrick akasema na kumfanya Andrew asimame huku akiwa na tabasamu la mshangao.


“ wuuuh ! Its unbelievable “ Andrew akashangaa


“Yes Andrew.hata mimi nilishangaa sana .Kwa mujibu w a maelezo yake anasema kwamba japokuwa aliamua kuwa na mpenzi mwingne lakini bado moyo wake ulikuwa kwangu.Aliamini siku zote kwamba mimi ndiye mwanaume wake a pekee kwa hiyo alikuwa mzito sana kumpa mwili wake huyo mpenzi wake mpya”


Andrew akamimina mvinyo katika glasi yake akaiinua juu,wakagonganisha glasi


“Patrick nakupa hongera zako” Andrew akasema huku akitabasamu halafu wote wakacheka kwa nguvu.


“Andrew kwa siku hizi chace nilizokaa na Happy kule Arusha nimeonja utamu wa maisha.Sikujua hapo awali kama kuna nyakati maisha huwa matamu namna ile.Kila nikiamka niko na malaika wangu pembeni ilimradi raha na furaha kila wakati.”


Patrick akasema na kuchukua glasi yake ya mvinyo akapiga funda kubwa.Andrew akamtazama na kusema


“Patrick naomba nikuulize jambo moja”


“Uliza Andrew”


“Ni muda mrefu hamjaonana na happy .baada ya kukutana naye safari hii umeuonaje mtazamo wake kuhusu mahusiano yenu?


“Andrew wewe ni mtu wangu wa karibu na siwezi kukuficha kitu.Pamoja na yote yaliyotokea lakini bado mimi ni mtu wa pekee kwake.Bado nafasi yangu iko pale pale ndani ya moyo wake.”


“na vipi kuhusu wewe? Pamoja na yote yaliyotokea,bado unaamini kwamba Happy ana nafasi moyoni mwako? Andrew akaulizaCHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/


Swali lile likamfanya Parick anyamaze kidogo ,akachukua glasi ya mvinyo na kupiga funda moja,akakohoa kidogo na kusema


“Andrew ,pamoja na yote yaliyotokea bado Happy ndiye namba moja wangu .Yeye ndiye furaha yangu.Samahani Andrew kama kwa kusema hivi nimekukera.”


“hapana hujanikera Patrick.Nafurahi kwa sababu siku zote umekuwa mkweli kuhusu hisia zako.Kwa hiyo baada hisia za kila mmoja wenu kuwa wazi kwamba bado mnapendana nini kilifuata?


“Tulikuwa na wakati mgumu mno kwa sababu sote tayari tuko katika mahusiano mapya ambayo yamekwisha piga hatua kubwa,lakini hii haikuwa sababu ya kutufanya tusiendelee na urafiki wetu hata kama tuko katika mahusiano mengine.Tulikubaliana kuendelea na urafiki wetu wa kawaida lakini tukajiuliza tena,sisi tunapendana kwa dhati,je tutakuwa tunajitendea haki sisi wenyewe ? Huko tuliko tutakuwa na furaha? Majibu ya maswali haya yote yalikuwa ni hapana.Hatutakuwa tumejitendea haki sisi wenyewe ,vile vile huko tuliko hatutaweza kuishi kwa furaha na amani.Tukajiuliza tena tufanye nini basi? Jibu likawa kwamba tunalazimika kuifanya maamuzi magumu.”


“maamuzi magumu yapi tena? Andrew akauliza


“Kuachana na wapenzi wetu wa sasa ! Patrick akasema na kumfanya Andrew asimame


“No ! you are kidding me” Akasema Andrew


“Andrew,Happy ndiye furaha ya maisha yangu.Nilimpenda Happy muda mrefu na hata nikafungwa kwa ajili yake.Pamoja na yote yaliyotokea lakini bado Happy amekuwa ni mtu wa pekee kabisa ndani ya moyo wangu .Ninampenda na nitaendelea kumpenda hadi kufa kwangu.Kwa sababu ya upendo huo mkubwa nilionao kwa Happy ,nimeamua kuachana na Vero.Nimeona uwe mtu wa kwanza kufahamu kabla sijaliweka wazi jambo hili kwa ndugu .Ndoa kati yangu na Vero haipo tena.Its over.Happy naye ameamua kuachana na mpenzi wake ili tuweze kuwa pamoja.Nafahamu si jambo rahisi lakini siku zote nguvu ya penzi ni kubwa na hushinda kila kikwazo“ Patrick akasema na kumfanya Andrew ainame na kuzama katika mawazo ghafla.


“Nilijua tu ,hapa hakuna ndoa tena.Masikini Vero” Andrew akawaza.


“Andrew nafahamu umekuwa mtu wangu wa karibu mno na umenisaidia katika mambo mengi lakini tafadhali naomba usinishauri chochote kuhusu jambo hili.Nimekwisha fanya maamuzi na siwezi kurudi nyuma tena.Kwa ajili ya Happy nitafanya kila kitu ili niwe naye maishani..Ahsante sana Andrew kwa kunisaidia katika mambo mengi lakini nakuomba katika suala hili usijihusishe kwa sababu ninafahamu kinachokwenda kutokea si kitu kizuri.Please don’t be part of this” Patrick akasisitiza.Andrew akamtazama na kusema


“Patrick wewe ni zaidi ya rafiki yangu.Tumeshauriana na tumesaidiana katika kila jambo.Mpaka sasa hivi kati ya ndugu zako wote hakuna mtu yeyote anayefahamu kitu gani kinaendelea zaidi yangu.Kusema kwamba nisikushauri au nisijihusishe kwa namna yoyote na suala hili ni jambo lisilowezekana kwa sababu I’m too involved now.Tumetoka mbali na jambo hili kwa hiyo siwezi kuishia hapa.Kama nilikubali toka mwanzo kwamba nitakuwa nawe,siwezi kamwe kukuacha peke yako hasa katika kipindi hiki kitakachokuwa kigumu zaidi kwako.Patrick utake usitake mimi nitakuwa pamoja nawe katika suala hili hata kama umekataa nisikushauri chochote lakini nitakuwa nawe hatua kwa hatua na hata ikibidi kukushauri pale itakaponilazimu japokuwa sintakushauri ubadili mawazo yako kuhusu yupi ni msichana unayemtaka maishani.”


Patrick akamtazama Andrew na kusema


“Andrew narudia tena ,kinachokwenda kutokea si kitu kizuri.Ninaomba kila kitu nikibebe mimi mwenyewe.Umenisaidia sana lakini kwa hili naomba uniache mwenyewe.Nimekwisha jitolea kuubeba mzigo huu mkubwa ,ninajua nitaumia na wengi pia wataumia lakini sina namna nyingine ya kufanya .Lazima nifanye hivyo.Lazima niachane na Vero”


“Patrik nimekuelewa vizuri naomba ufahamu kwamba hata kama hupendi bado nitaendelea kuwa nyuma yako.Naomba tafadhali tusiongelee suala hili tena.Fahamu kwamba tuko pamoja na siku zote tutaendelea kuwa pamoja.” Andrew akasema huku akimpa Patrick mkono.


“Andrew nashukuru kama kwa moyo wako umekubali kuungana nami katika suala hili.Nitakuja kukuona kesho asubuhi na kukufahamisha kwa kina mpango mzima .Naomba nikuache na tuonane kesho.”


Wakaagana na Patrick akaondoka zake na kumuacha Andrew akiwa na mawazo mengi




“Du ! mambo yanazidi kujikoroga.Sipati piha ni kitu gani kitakachotokea baada ya Patrick kutamka kwamba amevunja mahusiano yake na Vero.Sikutegemea kama suala hili lingefika hapa lilipofika.Hatua waliyokwishaifikia ni kubwa sana na umebaki muda mchache tu wafunge ndoa.Kitendo cha kusitisha masuala ya ndoa yao kimeniumiza sana japokuwa sina uwezo wa kulizuia jambo hilo lisitokee, kwani tayari Patrick amekwisha fanya maamuzi na hakuna mtu anayeweza kuyabadili.Ninamfahamu Patrick vizuri akisha amua kitu huwa hapendi kupingwa Nimemuona machoni ,alikuwa akimaanisha kile alichokisema.Sijui Happy amempa kitu gani Patrick mpaka ameshindwa kumsahau hata baada ya miaka mingi kupita.Hadi kufikia hatua ya kusitisha mipango ya harusi yake kwa ajili tu ya Happy basi hakuna kitu ninachoweza kukifanya kwa ajili ya kuinusuru ndoa hii ya Patrick na Vero.Patrick na Happy wanapendana na hilo halina ubishi.Ukijiuliza ni kwa nini Happy ajitokeze katika kipindi hiki baada ya kupotea kwa miaka hii yote utapata jibu kwamba ilipangwa wawe pamoja.Nakubaliana na ukweli huo japokuwa ninamuhurumia sana Vero kwa jinsi anavyompenda Patrick.Kosa moja ambalo alilifanya ni kutumia uongo kuwatenganisha wawili hawa.Uongo wake leo hii umekuja kujulikana na hivyo kumgharimu .Kama walivyoumia wenzake kipindi kile alipowatumia taarifa za uongo zilizowafanya wakatengana basi hata yeye atasikia uchungu kama walioupata wenzake kwa miaka hii yote.Roho inaniuma sana lakini sina namna nyingine ya kuweza kumsaidia..Kingine kinachoniumiza ni gharama kubwa tuliyoitumia katika maandalizi ya harusi hii.Nimetumia fedha zangu nyingi kama mchango kwa rafiki yangu katika kuiandaa harusi hii lakini kila kitu kimepotea bure……” Andrew akawaza huku akiketi sofani akakishika kichwa chake alikuwa na mwazo mengi.


“Ngoja nimpigie mama yake Patrick ili afahamu kama mwanae amesharudi.Kwa jinsi Patrick alivyochanganyikiwa na Happy sidhani kama amekumbuka hata kumtaarifu mama yake kama amesharudi Dar es salaam.” Akawaza Andrew huku akichukua simu na kuzitafuta namba za mama yake Patrick.


“Lakini simlaumu sana Patrick kwa sababu kwa uzuri wa Happy hata mimi ningechanganyikiwa.Mtoto ameumbika mithili ya malaika.Mtoto anastahili kabisa kutwaa taji la mrembo wa dunia” Akawaza Andrew wakati akisubiri simu yake ipokelewe na mama Patrick.


“Hallo Andrew habari yako mwanangu” Akasema mama Patrick baada ya kupokea simu


“Habari nzuri mama ,pole na mihangaiko ya kutwa nzima ” Andrew akasema


“Tumeshapoa baba yangu.Kutwa nzima tumekuwa tukizunguka hapa na pale katika kuhakikisha maandalizi yanakamilika.Japokuwa kuna kamati inayoshughulikia kila kitu lakini hata mimi kuna mambo ambayo inanilazimu kuyafuatilia na kuhakikisha yamekaa sawa.Si unajua siku zimebaki kidogo sana na jiji hili lina sherehe nyingi kwa hiyo inabidi kufanya maandalizi ya mapema.”


“ Pole sana .Mama nimekupigia kukufahamisha kwamba Patick amerejea Dar es salaam jioni ya leo .Umefanikiwa kuonana naye?


“Hapana Andrew.Habari hizi wewe ndiyo wa kwanza kuniambia.Hajanitaarifu kama amerejea japokuwa alinipigia simu jana akaniambia kwamba atarejea Dar es salaam siku yoyote.Andrew huyu mwenzio amepatwa na kitu gani ? mbona amebadilika namna hii?Nimeona kuna mabadiliko makubwa sana katika siku hizi chache toka apatwe na yale matatizo ya kupoteza fahamu.Kitu gani kinamsumbua mwenzio? Mama yake Patrick akauliza


“mama siwezi kujua kitu gani kinamsumbua ,japokuwa mimi na yeye ni marafiki wakubwa lakini kuna masuala ya ndani kabisa ambayo hatuwezi kuambiana.Mimi naona tumpe muda wa kutosha ili atulie kwa sababu ninahisi hali hi inaweza kuwa inachangiwa na mambo mengi aliyonayo na hasa hili suala la harusi yake”


“Sawa Andrew.nashukuru kwa kunifahamisha kwa sababu rafiki yako haoni hata umuhimu wa kuwataarifu wazazi wake kama amerejea salama.Tena imekuwa vizuri amerejea kwa sababu mwenzake alinipigia simu kunitaarifu kwamba atarejea leo saa nane za usiku.Kwa hiyo itakuwa vizuri kama atakuwepo uwanja wa ndege na kumpokea mwenzake kwani aliondoka akiwa hana amani kwa hiyo litakuwa jambo la faraja kama akimkuta Patrick uwanjani akimsubiri .Ngoja nimpigie simu nimfahamishe kuhusu hilo.”


“Ok Ahsante mama.Usiku mwema” Andrew akasema na kukata simu kisha akaitupa sofani.


“Damn you Patrick!! Kila siku nimekuwa nikidanganya watu wazima.Umeniweka katika matatizo makubwa sana na siku mama yako akigundua kama mambo yote niliyokuwa nikimwambia yalikuwa ya uongo atatamani hata kunitoa roho.Hatatamani anione tena katika macho yake…” Andrew akatikisa kichwa kwa masikitiko.


“masikini Vero leo usiku anarejea akiwa na matumaini kwamba ndani ya wiki chache zijazo atakuwa mwanamke mwenye furaha kwani atakuwa ameolewa na mwanaume anayempenda sana.laiti angejua ..nadhani asngekubali kurudi tena Tanzania.Namuonea huruma lakini yote haya aliyataka mwenyewe.Palipo na penzi la kweli hakuna awezaye kulitenganisha.Na tusubiri tuone kitakachotokea….” Andrew akawaza akachukua glasi yake iliyokuwa na mvinyo akapiga funda kubwa.


**********************


Akiwa katika kona ya kuingilia nyumbani kwake smu yake inaita.Akapunguza mwendo wa gari na kutazama mpigaji.Alikuwa ni mama yake.Akasita kuipokea simu ile.


“Ukiona hivi ujue tayari amekwisha pata taarifa kuwa nimerudi.” Akawaza Patrick


“Hallo mama shikamoo” Akasema Patrick baada ya kuipokea simu ile.


“Marahaba hujambo? “ Akaitika mama yake. Patrick akaguna kidogo kwa muitikio ule kwa sababu kuna kitu alihisi hakikuwa sawa katika sauti ya mama yake.Anamfahamu mama yake vyema.


“Sijambo mama.habari za hapo nyumbani? Patrick akauliza


“Hivi wewe mwanangu naomba nikuulize kitu.Sisi wazazi wako unatuweka katika kundi gani? Mama yake akauliza kwa sauti yenye ukali.


“Kazi imeanza” akawaza Patrick


“mama samahani naomba nikupigie baada ya muda mfupi .Nataka kupaki gari.”Akasema Patrick na mama yake akakata simu bila kusema chochote.Baada ya kuliingiza gari ndani akaelekea sebuleni kisha akaketi sofani akaishika simu yake na kumpigia mama yake.


“Samahani mama kwa kukatisha maongezi yetu mida ile.”


“hakuna hata haja ya samahani kwa sababu siku hizi sisi wazazi wako hatuna tena thamani kwako.”


“kwa nini uansema hivyo mama?


“Kwani si kitu kilicho wazi.Hutaki kutusikiliza chochote tunachokwambia.Hutaki ushauri wetu tena.”


“ Si kweli mama.” Patick akajibu


“Kama si kweli unawezaje kurudi bila kututaarifu kwamba umerudi salama?


“Mama ni kweli nimerudi jioni hii na nilikuwa na mpango wa kuja hapo nyumbani lakini nikiwa njiani nilijsikia hali kubadilika ghafla ikanibidi nirudi nyumbani mara moja.Nimetumia dawa na ninajisikia safi kwa sasa.”


“Mh ! Haya bwana.Sasa sikiliza.Mwenzako alinipigia simu na kunitaarifu kwamba anarudi leo saa nane za usiku.”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/


“Mwenzangu !! Patrick akauliza


“Ndiyo mwenzako.Kwani una wenzako wangapi? Ina maana Vero si mwenzako?


“Ouh kumbe unasema Vero”


“Ndiyo anarejea leo saa nane za usiku akitokea London alikoenda kwa ajili ya kufanya manunuzi ya harusi yenu.Kwa kuwa umerudi,litakuwa jembo kama ukienda kumpokea uwanja wa ndege.Patrick mwenzako aliondoka hapa akilia machozi na alikubali kwenda London baada ya mimi kumbembeleza afanye hivyo.Tafadhali mfurahishe mwenzako.Nenda ukampokee usiku huu arudipo.Atajiskia mwenye furaha sana pindi akishuka ndegeni na kukuona pale ukimsubiri.Atasahau kila kitu kilichopita” mama yake akasema .


Patrick akafikiri kidogo na kusema


“Sawa mama nitajitahidi kwenda huko uwanjani.Vipi kuhusu kile kikao?


“Kikao kitafannyika kesho na kila mwanamakati ana taarifa.Katika kikao cha kesho tutafanya majumuisho ya kila kitu na kuangalia kama kuna kitu kilichobaki na kisha jumatatu ndoa ikaandikishwe na kuanza kutangazwa kanisani.Kwa ujumla kila kitu kipo tayari.”


“Sawa mama .Nitafika katika kikao hicho Kuna mambo nataka kuongea na wanakamati wote kwa ndugu wa karibu kwa ujumla.Jitahidi wewe na baba muwepo na umtaarifu pia mama yake Vero naye awepo.Ni muhimu sana..”


“Patrick unataka kutueleza kitu gani? Mama yake akauliza


“Ni masuala madogo madogo tu ya kuwekana sawa kuhusu mambo haya ya harusi” Patrick akasema kisha akaagana na mama yake akaegemeza kichwa sofani na kuvuta pumzi ndefu.


“ Hatua kubwa imeshapigwa mpaka sasa.Kila kitu kiko tayari .Fedha nyingi imeshatumika katika maandalizi ya harusi hii.Ndugu jamaa na marafiki wote wana taarifa juu ya harusi yangu na wanaisubiri kwa hamu kubwa na wengi wametoa michango yao kwa ajili ya maandalizi ya harusi hii.Mambo hayatakuwa rahisi kama nilivyotegemea.Hakuna atakayekubali uhusiano huu uvunjike.hakuna atakayekubali ndoa hii isitishwe.Hakuna atakayenielewa.Hawatanielewa kwa sababu hakuna anayefahamu wapi nimetoka na Happy zaidi ya Andrew .Wazazi wangu walimchukia Happy hasa kwa kitendo chake cha kwenda kusoma Ulaya na kuniacha gerezani.Sipati picha nini kitatokea wakisikia kwamba ninaachana na Vero kwa ajili ya kuwa na Happy.Nafahamu sintaeleweka katika jamii lakini siwezi kurudi nyuma.Lazima niachane na Vero.Nafahamu ni jisni gani Vero anavyonipenda lakini alifanya kosa kubwa sana kuamua kunitenganisha na furaha ya moyo wangu.namuonea huruma sana.Atateseka sana lakini sina namna nyingine ya kufanya .Kwa ajili ya Happy chochote kile nitafanya.Kwa upande wa Happy jambo hili linaweza kumletea picha mbaya katika jamii.Ninafahamu kwa sasa yeye ni mrembo wa Tanzania na ni mtu maarufu.Kila akifanyacho kinatengeneza kichwa cha habari.Kama waandishi wa habari wakilipata jambo hili litasababisha heshima ya Happy kuporomoka ghafla.Nitakuwa nimemsababishia matatizo makubwa mtoto mzuri kama huyu ambaye taifa linamtazama kama mrembo ambaye anaweza akaliletea taifa hili sifa kubwa sana kupitia taji lake hili” Akawaza Patrick akiwa ameketi sofani.Akainuka akawasha luninga akarudi tena kuketi sofani.


“Nilimuahidi mama kwamba nitakwenda kumpokea Vero usiku huu.No ! siwezi kufanya hivyo.Sijisikii kuonana na Vero kwa sasa.Ninaweza nikajaribu mambo bado mapema.Nataka kila kitu kiishe kesho mbele ya ndugu na jamaa.Nataka kila mmoja afahamu nini Vero alinifanyia.Kwa sababu nilikwisha muahidi mama kwamba nitakwenda kumpokea Vero,ngoja niwasiliane na Andrew ili nimuombe akampokee Vero uwanja wa ndege.”


**********************


Honi ya gari ikamstua Andrew akiwa jikoni akijiandalia chakula cha jioni.Akazima jiko na kutoka mle jikoni akaelekea getini .Akafungua na kukutana na gari jipya kabisa aina ya BMW jeusi.Akastuka na kujiuliza ni nani yule kwa sababu hajawahi kuliona gari lile pale kwake.Akalisogelea na mara kioo cha gari kikashushwa taratibu akakutana na sura yenye tabasamu ya mpenzi wake Vick.


“wow ! Vicky” Andrew akasema kwa mshangao huku akilifungua geti lote na gari likaingia ndani.


“Naona kama ndoto .Ni wewe kweli? Andrew akauliza


“Ni mimi Andrew.Kwani kuna kitu gani cha ajabu? Vick akauliza huku akishuka garini.


“wow ! umeazima wapi gari la thamani kubwa namna hii?


“Ina maana mimi siwezi kumiliki gari la namna hii?” Vick akauliza


“Kwa maana hiyo gari hili ni lako? Andrew akauliza


“Ndiyo ni gari langu.Kuna tatizo lolote mimi kuwa na gari kama hili?


“hakuna tatizo lakini unapokuwa na kitu cha thamanai kama hiki,kuna tatizo gani mwenzio akifahamu umekipataje pataje? Andrew akauliza


“Kwa maana hiyo unahofia kwamba ninaweza kuwa nimenunuliwa na mwanaume mwingine? Vick akauliza huku akimkazia macho Andrew


“Hata kama umenunuliwa na mwanaume mwingine unaweza ukaniambia?


“Hakuna kitu nilichowahi kukuficha mpenzi wangu na kwa hili ninataka kukueleza ukweli kwamba nimenunuliwa na bosi wangu ambaye mimi ni kimada wake.” Vick akasema na ghafla Andrew akageuza macho akaanguka chini


Vick akamuinamia akambusu na wote wakaangua kicheko kikubwa.


“Usirudie tena kusema hivyo.Unajua sisi wengine hatukawii kuanguka kwa presha” Andrew akasema huku akicheka


“kama ingekuwa ni kweli ningemkata kichwa huyo bosi wako” Andrew akasema na kumfanya Vick acheke kwa nguvu.


“Kweli Andrew unaweza ukakata mtu kichwa kwa ajili yangu?


“Nakwambia ukweli Vick.Niko tayari kukata mtu kichwa kwa ajili yako” Akasema Andrew na kumfanya Vick aendelee kucheka.


“Inuka twende ndani darling.Hili ni gari la mama ametumiwa na dada kwa hiyo ameniachia nilitumie” Vick akasema wakati wakiinuka na kuelekea ndani.


Mara tu baada ya kuingia sebuleni simu yake inaita.Akaichukua na kuangalia mpigaji.Alikuwa ni Patrick.


“halo Patrick” akasema Andrew baada ya kuipokea simu ile.Vick ambaye alikuwa karibu akastuka na kugeuka.


“Patrick ! ina maana Parick amerudi? Akauliza na Andrew akamfanyia ishara kwamba anyamaze


“Andrew kuna jambo limejitokeza ninaomba msaada wako” Akasema Patrick


“jambo gani hilo? Andrew akauliza


“Nimeongea na mama muda mfupi uliopita.Amenitaarifu kwamba Vero anarejea leo saa nane za usiku na akanitaka kwenda kumpokea uwanja wa ndege.Kwa kuwa sikutaka mabishano na mama ikanilazimu kumkubalia kwamba nitakwenda huko uwanja wa ndege kumpokea Vero.Andrew sikufichi kwamba pamoja na kumkubalia mama lakini siko tayari bado kuonana na Vero kwa sasa.Ninaogopa mambo yanaweza yakaharibika mapema.kwa hiyo ninaomba kama hutajali unisaidie kwenda kumpokea Vero.Najua hili ni suala gumu kwako lakini sina mwingine ambaye ninaweza nikamkimbilia kwa msaada.naomba unisaidie kwa hilo” Patrick akasema na kumfanya Andrew akae kimya kwa muda.


“Andrew upo? Akauliza


“Nipo Patrick nilikuwa natafakari kidogo.Anyway nitakwenda huko uwanjani.Nitumie namba ya ndege atakayopanda.”


“nashukuru sana Andrew .Umenisaidia sana ndugu yangu.Hilo ni deni kubwa kwangu.Ngoja niwasiliane na mama anipe namba ya ndege atakayokuja nayo Vero” Patrick akasema na kukata simu.Andrew akabaki katika mawazo mengi,na mara akastuliwa na Vick


“Andrew hebu nieleze.Patrick amerudi?


“Ndiyo amerudi jioni ya leo”


“Alikuwa amekwenda wapi?


“Hakuniambia alikuwa wapi ila alichoniambia ni kwamba alikuwa nje ya mkoa kwa dharura”


“Nimesikia mkiongea kuhusu namba ya ndege.Nani anakuja na dege? Vick akauliza na kumfanya Andrew asite kujibu.


“Andrew niambie tafahdali nani anayekuja na ndege?


“Vero anarudi leo toka London kwa hiyo Patrick ameniomba niende nikampokee badala yake” Andrew akasema


“ Andrew are you out of your mind? Kwa nini yeye ambaye ndiye mpenzi wake asiende na akutume wewe? Vick akauliza


“Patrick hajisikii vizuri na ndiyo maana ameniomba nikampokee Vero badala yake.”


“No Andrew you are not going “ Vick akasema uso wake ukiwa umebadilika


“Unasemaje? Andrew akauliza


“You are not going. Andrew wakati umefika sasa wa kuyaacha mambo ya Patrick na Vero na kuangalia mambo yetu. Sisi tuna mambo mengi ya kukaa na kuongea kuhusu maisha yetu ya baadae. Leo hii nimekuja ili niwe na mpenzi wangu na mimi nifurahi lakini badala yake the whole night unakwenda kumpokea mpenzi wa rafiki yako.Is that fair? Vick akauliza. Andrew akamtazama mpenzi wake halafu akamsogelea karibu akamshika mabegani.


“Vick nimekuelewa. Hata mimi si kwamba ninapenda kuwa mstari wa mbele katika masuala ya Patrick na Vero na kusahau mambo yetu. You are always my everything. You are my breath and my life. Ninamshukuru Mungu kila siku kwa zawadi hii kubwa aliyonipa ya kuwa nawe.Nakupenda sana malaika wangu na niko tayari kufanya chochote kile kwa ajili ya kukufanya uwe ni mwenye furaha daima.Nafahamu umuhimu wako kwangu lakini Patrick he is my best friend.Mimi ni rafiki yake pekee anayeniamini kwa sasa.Sina namna ya kuweza kumkatalia kwa jambo aliloniomba kwa sababu yuko katika wakati mgumu mno kwa sasa na anahitaji msaada.Please let me do this for him and after this, I’m done.Mambo yake atayafanya yeye mwenyewe lakini kwa usiku wa leo naomba uniruhusu niende nikampokee Vero.”


Vick akamtazama Andrew kwa makini akasogea karibu akamkumbatia na kumbusu kisha akasema


“Usihofu baby nimekuelewa. Nitakusindikiza huko uwanja wa ndege siwezi kukuacha uende huko peke yako.lakini naomba uniahidi kwamba baada ya hili utaachana na mambo ya Patrick na kuelekeza nguvu katika mipango yetu”


Huku akitabasamu Andrew akasema


“I promise “


Vick akambusu tena na kusema


“Ok kabla hatujakwenda huko uwanja wa ndege twende kwanza chumbani.Nafasi yangu mimi ni ya kwanza kabla ya hao rafiki zako.” Vick akasema na taratibu wakaelekea chumbani


******************


Ni saa tano za usiku sasa lakini hakuhisi dalili zozote za kuonyesha kupata usingizi.Kila alipojaribu kufumba macho ni picha moja tu iliyokuwa ikimjia .Picha ya Patrick.Happy alishindwa kulala akaamka na kuketi kitandani.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/


“Am I going crazy? Mbona najihisi kama vile siko kawaida? Patrick amenipa nini hadi nishindwe kupata usingizi kwa ajili yake? Kwa siku hizi chache nilizokaa naye Arusha amenifanya niwe kama chizi kwa ajili yake.Siku hizi chache nilizokuwa naye Arusha ndizo zilikuwa siku pekee zenye furaha katika maisha yangu.I lived my whole life in those few days.Sidhani kama nitarudi katika hali yangu ya kawaida bila ya kuwa na Patrick.Ni yeye tu ndiye atakayeweza kuniondolea uchizi huu ulionipanda kichwani .This is too much .This is beyond love.Nitafanya kila kitu kwa ajili ya kuwa naye.I swear I’m going to do anything to get him.He’s all mine.” Akawaza Happy ,akainuka akachukua glasi ya maji akanywa,akaichukua picha ya Patrick akaitazama akaibusu .


“Siwezi kupata usingizi bila kuisikia sauti ya Patrick.Sielewi ni kitu gani kimemfanya asinipigie simu wakati aliniahidi kwamba atanipigia usiku..” akawaza Happy huku akichukua simu na kupiga


“Hallo my angel” akasema Patrick


“Patrick my love, nimeshindwa kulala bila kuisikia sauti yako. Tafadhali usichelewe tena kunipigia simu mpenzi wangu. Kwa sasa siwezi kukaa muda mrefu bila kukuona na kuisikia sauti yako tamu.Its shame to say this but I’m crazy for you Patrick.” Happy akasema


“Ouh my angel,samahani sana kwa kuchelewa kukupigia simu hata hivyo nilikuwa katika maandalizi ya kukupigia simu muda si mrefu.Toka nimefika hapa nilikuwa katika shughuli za usafi kuiweka nyumba katika hali nzuri.”


“Pole sana Patrick.Kuanzia sasa fahamu kwamba siwezi kumaliza siku moja bila kukuona au kuisikia sauti yako nzuri.” Happy akasema


“nalifahamu hilo Happy na ndiyo maana nimekuahidi kufanya kila niwezalo ili kuhakikisha kwamba tunakuwa pamoja daima.Ni wewe tu ambaye unanifanya nijione kama malaika wa peponi.Ni wewe tu uliyeibeba furaha ya moyo wangu” Akasema Patrick


“ Vipi umeshaongea na Vero? Happy akauliza


“Vero alikuwa safarini ulaya na anarejea usiku wa leo.Nimeitisha kikao kesho na katika kikao hicho nitawaeleza kila kitu na kuuvunjilia mbali uchumba wangu na Vero.Nafahamu halitakuwa jambo rahisi lakini nimekwisha jiandaa kukabiliana nalolote litakalojitokeza.Usiumize kichwa kuhusu hilo.Muda si mrefu ile ndoto yetu itatimia”


“nafurahi kusikia hivyo Patick.Hata mimi kesho ndiyo nitaonana na Mike na nitamueleza ukweli.Mike ananipenda kwa hilo siwezi kuficha lakini sina namna nyingine yua kufanya zaidi ya kuachana naye.Ni mtu mwelewa na ninatumai atanielewa “ Happy akasema.


“Kwa hiyo mpaka kesho jioni tutakuwa na jibu lenye uhakika zaidi kuhusiana na suala hili gumu.Happy naomba uwe jasiri kwa sababu hii ni kwa ajili ya maisha yetu,kwa ajili ya furaha yetu.Kwa lolote litakalotokea,naomba uniahidi kwamba hautarudi nyuma.Tutashikamana pamoja hadi mwisho.”


“Kwa penzi zito nililonalo kwako ambalo haliwezi kulinganishwa na kitu chochote,kwa kuwa wewe ndiye mwanaume pekee niliyekukabidhi moyo wangu uutunze hadi mwisho wa maisha yangu,ninakuahidi kwamba sintarudi nyuma.Niko tayari kukabiliana na lolote lile ambalo linaweza kuwa kikwazo cha sisi kutimiza ndoto yetu ya kuwa pamoja.”


Happy akasema huku macho yake yakilengwa na machozi


“Nimekuelewa mpenzi wangu.naomba sasa ulale tutaonana kesho.Nitakupigia simu kesho asubuhi na mapema kukupa busu la asubuhi” Patrick akasema


“nashukuru sana malaika wangu .Sasa ninaweza kulala baada ya kuisikia sauti yako.Ah kabla sijasahu naomba uniimbie ule wimbo uliopenda kuniimbia kila siku kule Arusha” Happy akasema


“Wimbo upi? Patrick akauliza


“Ule wa Diamond Platinum..Lala salama”


Patrick akacheka na kuanza kumuimbia Happy wimbo ule mzuri luiomfanya Happy ahisi kama vile yuko na Patrick karibu yake..




Mlio wa simu ulimstua Patrick toka usingizini.Kitu cha kwanza alichokiangalia ni saa yake ya ukutani ambayo ilimuonyesha kwamba ilipata saa tisa na dakika nane za usiku.Akafikicha macho na kunyoosha mkono akaichukua simu yake iliyokuwa juu ya droo ya kitanda akatazama ni nani aliyempigia simu usiku ule mkubwa .Ilikuwa ni namba ya simu ya Vero.Patrick akakunja uso


“tayari ameshafika.Sijui anataka kuniambia kitu gani.Ngoja nipokee nimsikilize”


“Hallo “ akaita Patrick baada ya kubonyeza sehemu ya kupokelea


“Hallo my love.Unaendeleaje? Vero akauliza


“Naendelea vizuri Vero.Umeshatua?


“Nimeshatua niko kitandani hapa” akasema Vero kwa sauti laini


“Pole na safari” akasema Patrick


“Nimekwishapoa mpenzi wangu.Pole sana kwa kutojisikia vizuri.Nilitegemea kukuona uwanja wa ndege lakini nikamkuta Andrew na Vick peke yao nikaambiwa kwamba umeshindwa kufika kunipokea kwa sababu hukuwa unajisikia vizuri.Vipi maendeleo yako kwa sasa? Vero akauliza


“Naendelea vizuri Vero.” Patrick akajibu.


“nashukuru kama unaendelea vizuri.safari yangu ilikuwa nzuri.Dada na shemeji wanakupa salamu nyingi na wanakutakia uponaji wa haraka.Wameahidi watakuwepo siku ya harusi yetu.”


“Ahsante sana” Patick akajibu kwa ufupi


“Darling are you ok? Vero akauliza


“I’m ok Vero.Kwani vipi? Patrick akajibu


“Ninaona sauti yako haiko kawaida.Naona kama bado hauko sawa.Nini kinakusumbua mpenzi wangu? Nilitaka nije moja kwa moja kwako ili niwe nawe usiku huu lakini Andrew akanikataza akaniambia nikuache upumzike.Baby najisikia vibaya sana kuwa mbali nawe hasa katika kipindi hiki ambacho haujisikii vyema” akasema Vero


Patrick akavuta pumzi akafikir kidogo na kusema


“Usjali Vero.Mimi ninaendelea vizuri .Usihofu kitu”


“najua unaniambia hivyo ili kunitoa wasi wasi .Ngoja nikuache ulale upumzike.Nilitaka kukufahamisha kwamba tayari nimesharudi .Nitakuja kukuona kesho asubuhi kabla sijafanya kitu chochote kile.Sintakuwa na amani ya moyo bila kukuona.Niliondoka bila kukuona na siku zote nimekuwa roho juu juu nikikuwaza wewe mpenzi wangu.Patrick nakupenda sana na sintaweza kuishi bila kuwa nawe.Usiku mwema mpenzi.I love you”Vero akasema


“Bye baby” akajibu Patrick na kuitupa simu pembeni.


“Laiti angejua ninavyomchukia asingethubutu hata kunipigia simu.Angeniogopa kama ziraeli.” Akawaza Patrick wakati akijifunika vizuri


“vero ni mwanamke mzuri,ana roho nzuri ya ukarimu, ni mrembo,msomi na ana kila sifa ya kuwa mke.Sikutegemea kama kuna siku itanitokea nikamchukia kama ilivyonitokea sasa.Kitendo cha kunitenganisha na mtu niliyeyatoa maisha yangu kwake kimeniuma sana.Maumivu niliyoyapata wakati ule sitaki kuyakumbuka.Niliumia sana.Niliteseka kupita kiasi kwa kuamini kwamba ni kweli Happy amenisaliti.Ilinichukua muda mrefu maumivu yale kunitoka moyoni mwangu .Happy naye aliteseka kiasi kikubwa sana baada ya kusikia kwamba mtu pekee ambaye alikuwa akimpenda amefariki dunia.Mateso na maumivu aliyotusababishia Vero ni makubwa sana na kwa hili sidhani kama nitamsamehe.Dunia nzima haitanielewa ni kwa nini nimechukua maamuzi haya lakini sintajali mtu yeyote.Maamuzi niliyoyachukua hakuna mtu anayeweza kuyabadili.Lazima niachane na Vero na kuendelea na mtu ninayempenda maishani.Happy ndiye mwaname pekee mabaye nimepangiwa niwe naye katika maisha yangu na si huyu mlaghai Vero.” Patrick akawaza akiwa amejilaza pale kitandani.Akasikia hasira nyingi akaamka na kwenda kuchukua glasi ya maji akanywa na kurudi tena kitandani.


*********************CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/


Kengele ya mlangoni ndiyo iliyomstua Patrick toka usingizini.Akaangalia saa ya ukutani ilioyesha ni saa tatu za asubuhi.Akajinyoosha na kwa uchovu akatoka mle chumbani na kuelekea mlangoni.Akafungua mlango mdogo wa geti na kukutana na sura yenye tabasamu pana sana ya Vero ambaye alimrukia na kumpa mabusu mengi


“Ouh my love nimefurahi sana kukuona tena mpenzi wangu” akasema Vero kwa furaha huku akimkumbatia Patrick kwa nguvu.


“karibu sana Vero” Patrick akasema .Akalifungua geti na Vero akaingiza gari lake. Na kisha akatoa begi kubwa na kulivuta kuelekea ndani.


“Darling hizi zote ni zawadi nilizokuletea toka uingereza.” Akasema Vero na kumfanya Patrick atabasamu


“nashukuru sana Vero” Patrick akajibu na kwenda kukaa pembeni ya Vero.Wakatazamana kwa sekunde kadhaa.


“Unajisikiaje leo mpenzi wangu? Vero akauliza akiwa ameiweka mikono yake shingoni kwa Patrick


“Najisikia vizuri sana leo.Unajua wewe ndiye dawa yangu.Umekuja na nimepona kabisa” akasema Patrick na kumfanya vero atabasamu na kumkumbatia kwa nguvu.


“Nimekwambia hivyo kukupa moyo tu lakini siku ya leo haitaisha kabla hujalia machozi ya damu” akawaza Patrick.


Wakiwa bado wamekumbatiana ,simu ya Patrick ikaita.Akaichukua na kutazama mpigaji.Alikuwa ni mama yake.


“mama shikamoo”


“marahaba mwanangu hujambo?


“sijambo mama”


“Unaendeleaje? ” akauliza mama Patrick kwa sauti ya upole isivyo kawaida yake.


“mama ninaendelea vizuri sana”


“sasa mwanangu mbona jana hukwenda kumpokea mwenzio? Kwa nini unamfanyia hivyo mwenzako?


“mama nilishindwa kwenda kule uwanjani kwa sababu sikuwa najisikia vyema na ndiyo maana nikamuomba Andrew aende akampokee Vero badala yangu”


“yaani kwenda kumpokea mwenzako hapo uwanjani hujisikii vizuri .mbona kwenye dharura zako husemei kwamba hujisikii vizuri? Mama Patrick akauliza huku sauti ikianza kubadilika na kuwa ile ya ukali iliyozoeleka.


“mama si kwamba nilifanya makusudi kutokwenda kumpokea Vero.Nilikuwa naumwa na ndiyo maana nikamuomba Andrew aende badala yangu.” Patrick akajibu


“Sawa baba nimeshakuelwa manake ukiendelea utaanza kuzungumza vingereza vyako halafu tukashindwa kuelewana.Usichelewe leo kwenye kikao .Tayari kila mtu nimeshampa taarifa na nimewasisitiza kwamba wasikose.”


“haya mama tutaonana mida hiyo.Msalimu baba” Patrick akasema na kukata simu


Wakati Patrick akiongea na mama yake vero alikuwa ameingia bafuni.Aliposikia tayari Patrick amemaliza kuzungumza na simu akatoka mle bafuni akiwa amejifunga taulo na kumfuata Patick pale kitandani akaanza kumtoa zile nguo za kulalia ambazo bado Patrick alikuwa amezivaa.


“Ratiba ya leo itakuwa kama ifuatavyo.Kitu cha kwanza tunatakiwa tukaoge pamoja halafu tupate stafstahi halafu tutajifungia chumbani kwetu siku nzima ya leo” akasema vero akilivua shati la Patrick na kuliweka pembeni.


“Ulimtaarifu mama kwamba sikufika kukupokea uwanja wa ndege? Patrick akauliza


“Nilimpigia simu usiku kumtaarifu kwamba nimeshatua kwa sababu aliniomba nikishafika salama nimfahamishe.Aliniuliza kama ulikuwepo uwanjani nikamwambia kwamba hukuweza kufika kutokana na kutokujisikia vizuri.Samahani kama nilikosea kwa hilo” Akasema Vero huku akimshika Patrick mkono na kumuongza kuelekea bafuni.


“Patrick nilipokuwa safari nilikuwa nikiweweseka kila usiku nikilitaja jina lako mpaka watu wakashangaa umenipa kitu gani cha kunifanya nikupende kiasi kikubwa namna hii.Naomba nikiri kwamba sintaweza kuishi bila kuwa nawe.Wewe ndiye pumzi yangu,wewe ndiye maisha yangu,wewe ndiye kila kitu kwangu.Bila wewe siwezi kitu.” Akasema Vero huku akiutembeza mkono wake taratibu katika kifua cha Patrick wakiwa katika jakuzi.Patrick akamuangalia Vero kwa sekunde kadhaa akataka kusema kitu lakini Vero akamuwahi na kumuwekea kidole mdomoni.


“shhhhhhhh…..Don’t say anything” akasema vero na kutoa kidola kile na taratibu akakisogeza kichwa chake karibu na kuigusanisha midomo na kutoa busu moja zito ,halafu akatoa ulimi na kuilamba midomo ya Patrick.Wakari akifanya hivyo alikuwa akilisugua sikio la kushoto kwa mkono wake wa kulia kwa ufundi mkubwa.Sehemu hii ndiyo ambayo huwa inayaamsha mashetani ya Patrick.Kama Vero alivyokuwa amekusudia Patrick akaanza kuhema mfululizo huku akitoa mguno Fulani kwa raha aliyokuwa akiisikia.Akashindwa kuvumilia na kumvuta Vero karibu zaidi.Wakati wakiendelea kunyonyana ndimi simu ya Patrick ikaanza kuita kule chumbani.Mlango wa bafuni haukuwa umefungwa hivyo aliweza kuisikia simu yake vizuri ikiita


“Vero ngoja kwanza nikapokee simu.Anaweza akawa ni mtu muhimu ananipigia”


“No Patrick.No phone calls at this time.Its only me and you” akasema Vero huku akiendelea na mautundu juu ya mwili wa Patrick.


“Anaweza akawa ni Happy ndiye anapiga.Nisipoipokea simu yake atajiuliza maswali mengi “ akawaza Patrick.


Simu ile ikaita na kukata.Ikaita na kukata tena .Ikaanza kuita kwa mara ya tatu.Patrick akamsukuma Vero pembeni akainuka na kukimbia huku akichuruzika maji kuelekea chumbani .Kabla hajaifikia simu ikakatika.Akachuka na kutazama mpigaji alikuwa ni Happy.Akaishikilia simu ile kwa dakika nzima akijiuliza kama ampigie Happy ama la.


“Nitampigia baadae.Siwezi kumpigia wakati Vero yupo.Hii inaweza ikaharibu kila kitu.Nataka nikamalize mambo yote mbele ya wazee” akawaza Patrick na kuiweka simu yake mezani akarudi bafuni.


“Nani aliyekusumbua namna hiyo kwa kukupigia simu wakati kama huu na kuharibu starehe zetu? Akauliza Vero


“Foregt about it…Kuna jamaa mmoja nilikuwa na miadi ya kuonana naye leo jioni lakini sintaweza kuonana naye kutokana na kikao tutakachokihudhuria ”


“Kikao !! “ Vero akauliza kwa mshangao


“Ina maana hauna taarifa kwamba kikao cha mwisho kinakaa leo ? Saa tisa za alasiri itatubidi tuelekee sote katika kikaohiki.Taarifa zimekwisha sambazwa kwa kila mhusika awepo katika sherehe hii”


“Ouh basi hiyo ni habari nzuri .Hakuna shaka tutahudhuria ili tuweze kuona mpaka sasa maandalizi ya harusi yamefikia wapi.” Akaseam Vero huku akimshika mkono Patrick na kuimvutia katika jakuzi ili waendelee kuoga.


“Vero No! Siwezi kufanya hivyo tena.Sina hamu tena.Tumalizie kuoga tukapate kifungua kinywa.”


Vero akamuangalai Patrick kwa jicho kali lakini hakuwa na la kufanya.wakamaliza kuoga na kuelekea chumbani .


***************************


Mlango wa chumba cha Happy ukagongwa na kumfanya astuke toka usingizini.Akajiinua kitandani na kutembea taratibu huku akifikicha macho na kwenda kuufungua.Alikuwa ni mdogo wake Margreth.


“Wow ! Margreth “ Happy akasema huku akitabasamu


“Ouh Happy…” Magreth akaruka ruka kwa furaha na kumkumbatia dada yake.


“habari za Arusha? Yaani Happy unarudi hutaki hata kunijulisha kama umesharudi” akasema Margreth


“Samahani kwa hilo mdogo wangu.Nilirudi jana jioni na mama akanieleza kwamba umepata kazi katika kampuni ya mtandao wa simu na umeingia zamu ya usiku.Sikutaka kukusumbua kwa sababu nilifahamu lazima tutaonana asubuhi..Kwanza hongera kwa kupata kazi nzuri “ Happy akamwambia mdogo wake.


“nashukuru Happy.Niko upande wa huduma kwa wateja.kazi yangu ni kupokea simu za wateja,kupokea malalamiko ya wateja na kuyawasilisha sehemu husika.Nipe habari za Arusha..naona mambo yalikwenda vizuri kiasi kwamba ukasahau hata kunitaarifu kinachoendelea”


“Margeth ,kwanza kabisa napenda nikushukuru sana kwa kazi kubwa uliyoifanya ya kuniunganisha tena na Patrick.Sikutegema kama ningeweza kumuona tena Patrick maishani mwangu .Mara tu nilipofika katika hoteli ile ya Kobe Village nilikuta tayari Patrick amekwisha fika muda mrefu akinisubiri.Nilipomtia machoni sikuamini kama kweli ni yeye.Nilishindwa kujizuia nikaanza kulia.Nililia sana kwa sababu tayari nilikwisha poteza matumaini ya kuonana naye tena.Kwangu mimi ilikuwa ni kama muujiza mkubwa .Kwa ufupi kwa siku hizi chache nilizokaa na Patrick Arusha nilihisi kama niko peponi kwa raha ya ajabu niliyokuwa nayo.”


Margreth akamtazama dada yake huku akitabasamu na kisha akasema


“Ulimuuliza ni kwa nini aliamua kutangaza amekufa kumbe sivyo?


“Ndiyo nilimuuliza kuhusu jambo hilo na akashangaa sana kwani hakuwahi kufanya jambo kama hilo.Yeye pia aliniuliza ni kwani nini niliamua kumuacha gerezani na kuolewa na mzungu ambaye nilizaa naye mtoto mmoja.Nilistuka sana baada ya kusikia kitu kama hiki.Nilimuuliza alipata wapi taarifa kama hizo.Nilimuonyesha barua niliyotumiwa ikinieleza kwamba amefariki dunia.Akaisoma barua ile na kwa bahati nzuri akafanikiwa kuutambua mwandiko wa mtu aliyetuma ile barua.Kwa mujibu wa maelezo yake ni kwamba baada ya kuhamishwa gereza alikutana na dada mmoja aitwaye Vero ambaye alifika hapo gerezani kumsalimu mjomba wake aliyekuwa mkuu wa gereza jipya alilohamishiwa Patrick.Kwa kuwa kila siku Patrick alipangiwa kwenda kufanya shughuli za usafi nyumbani kwa mkuu wa gereza alijikuta akizoeana na Verona wakawa marafki.Muda wa Vero kuwepo pale ulipokwisha ilimlazimu kurejea jijini Dar es salaam na hivyo Patrick akamuomba amtumie kama kiungo baina yangu na yeye.Vero akakubali lakini kumbe alikuwana lake moyoni.Akatunga uongo ule kwa kunitaarifu kwamba Patrick amefariki dunia na halafu akamweleza Patrick kwamba mimi nimemsaliti kwa kuamua kuolewa na mzungu na kumuacha yeye akiozea gerezani.Margreth niliumia sana baada ya kusikia hivyo. Siwezi kuelezea ni maumivu gani aliyoyapata Patrick baada ya kusikia eti nimemsaliti na kuolewa na mwanaume mwingine.Patrick alifungwa gerezani kwa sababu ya upendo wake kwangu.Alifungwa baada ya kuua bila kukusudia kwa kuniokoa mimi nisidhalilishwe na wale wahuni sasa iweje leo niamue kumtelekeza gerezani na kuolewa na mwanaume mwingine? Ni jambo ambalo haliingii akilini lakini Vero alilifanya likaonekana ni kweli “ Happy akasema na kumtazama mdogo wake.


“Pole sana Happy.Kumbe hivyo ndivyo mambo yalivyokuwa !! “ Margreth akashangaa.


“Siamini kama dunia hii kuna watu wenye ukatili wa namna hii.Jambo alilolifanya huyu Vero ni baya sana ambalo lingeweza kusababiosha hata mmoja wenu akajitoa uhai.Hebu niambie Vero alifanya ubaya huu kwa sababu ya nini? manake hata mimi nimesikia uchungu sana kwa ukatili huu alioufanya Vero.” Margerth akaulizaCHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/


“ sababu kubwa ni kwamba alimpenda Patrick na akautumia umbali uliokuwepo baina yetu kututenganisha.Kweli alifanikiwa alichokuwa akikihitaji.Amefanikiwa kuwa na Patrick na kikubwa ni kwamba mwezi ujao wanafunga ndoa.” Happy akasema na kumfanya Margerth astuke.


“Ama kweli siku hizi binadamu ni wakatili kuliko hata wanyama.Kumbe uongo wote huu mkubwa ni kwa ajili ya kumpata Patrick ! loh ! “ margerth akasikitika sana.


“lakini siku zote kitu alichokipanga Mungu binadamu hawezi kukipangua.” Happy akasema


“kwa nini unasema hivyo Happy? Margreth akauliza


“Si unaona mambo yalivyojitokeza. Nimekutana na Patrick katika mazingira ambayo sikutegemea.Uongo wa Vero umegundulika muda mfupi kabla ya ndoa yake.Hii ina maana kwamba Mungu hakupendezwa na kitu alichokifanya Vero.Baada ya kuonana na Patrick kwa mara nyingine tena imenibidi nikubaliane na ukweli kwamba sina uwezo wa kumtoa Patrick moyoni mwangu.Yeye ndiye mwanaume pekee anayestahili nafasi katika moyo huu”


“Happy unamaanisha nini unaposema hivyo? Margreth akauliza. Happy akamshika bega na kumtazama machoni kwa makini.


“Nimeamua kuachana na Mike.”


“What !! Margreth akastuka


“Toka moyoni mwangu nimeamua kuachana na Mike na kuendelea na Patrick.”


“Happy sidhani kama inawezekana.Mike tayari amekwisha kuvisha pete ya uchumba.Itawezekana vipi umwambie kwamba umekusudia kuachana naye? Kingine kinacholifanya suala hili kuwa gumu zaidi ni kama ulivyosema kwamba Patrick na Vero wako katika maandalizi ya mwisho ya kufunga ndoa.Unadhani itawezekana vipi kuwatenganisha ?


Happy akatabasamu na kusema


“Itawezekana Margreth.Baada ya kugundua kilichotokea tulijadili suala hii kwa undani na kufikia uamuzi mmoja kwamba hakuna kitu cha kuweza kututenganisha,tukaamua kwa kauli moja kwamba tunaachana na wapenzi wetu wa sasa na kuurudisha uhusiano wetu wa awali.Nitamueleza Mike na nina imani atanielewa.Patrick naye atafanya hivyo hivyo na ataachana na Vero.” Happy akasema na kuichukua simu yake akazitafuta namba za Patrick na kupiga .


“Unampigia nani simu? Margreth akauliza


“Ninampigia Patrick.nataka kufahamu maendeleo yake” akajibu Happy


Simu ikaita na kukata,ikaita tena mara ya pili bila kupokelewa,hakukata tamaa akapiga tena mara ya tatu lakini bado simu haikupokelewa.


“Hapokei simu nadhani atakuwa yuko mbali na simu yake” akasema Happy


“Happy mimi sina tatizo na maamuzi yoyote utakayoyachukua .Najua unahitaji kuwa na furaha maishani na kama Patick ndiye mtu pekee ambaye unaamini atakupa furaha ya maisha ,sina kipingamizi na hilo.lakini ninachokihofia ni kwamba katika maamuzi haya mliyoyachukua watu wengi wataumia.Nina wasi wasi mkuwa na hilo.Mwezi mmoja umebaki Patrick na Vero wafunge ndoa kwa maana hiyo maandalizi yatakuwa yameshafanyika ya kutosha.Kitendo cha Patrick kutangaza kuivunja ndoa kati yake na Vero kitawaumia watu wengi na wengi watakuchukia kwa kuamini kwamba wewe ndiye chanzo cha haya yote.Sitaki uingie katika mtafaruku mwingine dada yangu.Sipendi kukuona ukiw akatika mateso na maumivu.Umekwisha lia kiasi cha kutosha dada yangu” Akasema Margreth.


“Margreth nakubaliana nawe kwamba suala hili ni gumu na litawaumiza watu wengi sana lakini tayari tumeshafanya maamuzi na hakuna kurudi nyuma .Niko tayari kukabiliana na chochote kile .Mambo mengi yatajitokeza lakini nitakabiliana nayo” akasema Happy kwa kujiamini


“Nitakutana na Mike baadae na nitaitumia nafasi hiyo kumweleza ukweli na nina imani atanielewa na kuniacha huru ili niweze kuwa na mtu ninayempenda kuliko wote katika maisha yangu” Happy akasema na Margreth akamtazama dada yake kwa huruma.




Saa sita za mchana gari ndogo nyeupe yenye namna za ubalozi wa Marekani ilisimama mbele ya nyumba ya akina Happy na kijana mmoja mtanashati aliyevalia suti nzuri nyeusi iliyomkaa vyema akashuka.Alikuwa ni kijana mwenye sura nzuri sana na ambaye ni wazi alikuwa akiwasisimua mabinti kila apitapo.Huyu alikuwa ni Mike mchumba wa Happy.kwa uzuri aliokuwa nao happy alistahili kuwa na kijana kama huyu


Margreth ambaye alikuwa amekaa sebuleni akatoka kwa kasi na kwenda kumpokea shemeji yake na kumkaribisha ndani.Mike akasalimiana na familia yote kisha akaletewa kinywaji na kuanza kunywa taratibu wakati akimsubiri Happy aliyekuwa chumbani kwake akijipamba.


“ Mike amekuja yuko sebuleni anakusubiri” Margreth akamwambia Happy baada ya kumfuata chumbani kwake.


Baada ya kupokea taarifa ile toka kwa Margreth Happy akakaa kitandani na kupumua kwa nguvu.Akauweka mkono wake mahala unapokaa moyo .Alipatwa na mawazo mengi ya ghafla.


“happy kulikoni? Margreth akamuuliza dada yake baada ya kuona namna alivyonyong’onyea ghafla


“Maggy nahisi miguu mizito sana kwenda kuonana na Mike.nashindwa nitaanzaje kumweleza kuhusiana na suala la kuachana.Nina wasi wasi mkubwa”


Margreth akamtazama dada yake na kusema


“happy huna sababu ya kuogopa.Hii ni kwa ajili ya furaha ya maisha yako.Kama kweli una nia ya dhati ya kuachana na Mike ili uwe na Patrick usisite kufanya hivyo.Huu ndio wakati wako.Umeipata nafasi naomba uitumie.Usisubri nafasi nyingine ijitokeze.Mueleze Mike ukweli na nina imani ni mtu mwelewa sana na atakuelewa vizuri.Najua ugumu uliopo katika kufanya hivyo hasa kwa mtu ambaye tayari mmeshakuwa wapenzi kwa muda wa miaka mingi na tayari mmeshaingia katika uchumba lakini kama ulivyosema kwamba chaguo lako ni Patrick basi huna budi kuachana na Mike.kwa maana hiyo basi vuta pumzi ndefu inuka hapo kitandani nenda kaonane na Mike,mtoke kwa chakula cha mchana na uitumie nafasi hiyo kumueleza Mike ukweli kuhusiana na msimamo wako huo.Kama kutakuwa na tatizo lolote lile nipigie simu nitakufuata haraka sana.”


Maneno yale ay Margreth yanamfanya Happy atabasamu na kisha akamkumbatia mdogo wake.


“nashukuru sana Maggy kwa kunipa moyo.Ninakwenda kuonana na Mike.” Akasema Happy huku akiichukua pochi yake nogo na kujiangalia kwa mara ya mwisho katika kioo.Akaufungua mlango wa chumba chake akatoka na kuelekea sebuleni.Mara tu alipotokeza sebuleni Mike alishindwa kuvumilia na kwa kasi akainuka na kumkumbatia Happy kwa nguvu.


“Ouh malaika wangu. Nafurahi nimekuona tena.Ningeingiwa na uchizi kama siku aya leo ingekwisha bila kuitia machoni sura yako nzuri” akasema Mike huku akimshika mkono Happy na kumketisha sofani


“habari yako Mike.habari za Marekani? Hajambo Michelle? Happy akauliza


“habari za Marekani ni nzuri.Michelle ni mzima ila mimi ndiye nilikuwa mgonjwa.Nilikuwa nikiumwa ugonjwa wa kutoiona sura yako lakini kwa sasa nimepona baada ya kukutia machoni.” Akasema Mike na wote mle sebuleni wakacheka.Mama yake Happy akainuka na kuondoka kuelekea chumbani kwake na kuwaacha vijana wake pale sebuleni.


“Happy mpenzi wangu vipi maendeleo yako? Mike akauliza huku ameushikilia mkono wa happy


“namshukuru Mungu ninaendelea vizuri sana” Hapy akajibu


“Nashukuru kama unaendelea vizuri.Nilipata taarifa kwamba ulipatwa na maradhi ya ghafla baada ya kulitwaa taji la Miss Tanzania.Niliogopa sana ikanilazimu kuchukua likizo ya ghafla na kuja hapa kuungana nawe katika kipindi hiki ambacho nina imani ulihitaji sana uwepo wangu.Hongera sana kwa kufanikiwa kulitwaa taji hili kubwa la urembo.Nina zawadi nzuri sana kwa ajili ya ushindi wako huo” akasema Mike na kumfanya Happy atabasamu


“ahsante sana Mike kwa kuja kunifariji.Ni kweli nilipata kitu kama mstuko Fulani baada ya kutangazwa mshindi wa taji lile la Miss Tanzania.Sikuwa nimetegemea kama ningeweza kulitwaa taji lile kutokana na ushindani mkubwa uliokuwepo baina ya washiriki.Baada ya hali ile kunitokea ilinilazimu kuchukua siku kadhaa za mapumziko na kuwa mwenyewe kwa ajili ya kuweza kutafakari na kujipanga namna nitakavyoweza kuishi maisha mapya na namna nitakavyoweza kulibeba jukumu hili kubwa nikiwa kama mrembo wa Tanzania.Nashukuru kwamba ninaendelea vizuri kwa sasa .ahsante kwa zawadi yako” Happy akasema na kisha kikapita kimya kifupi


“vipi uko tayari kwa kutoka? Tulikubaliana kwamba leo tutatoka kwa ajili ya chakula cha mchana .” Mike aksema


“Niko tayari Mike tunaweza kutoka” Happy akajibu na kisha Mike akamshika mkono Hapyy wakatoka wakaingia garini na kuelekea mahala ambako Mike alitaka waende wakapate chakula


“Happy nimefurahi sana kwa kukuona tena.Huwezi kujua ni furaha ya namna gani ambayo ninayo kwa kuwa nawe tena .Kwa mahala nilipofika sasa sintaweza kuishi bila kuwa nawe.Niko tayari kufanya kila kitu ili mradi niwe nawe.Niko tayari kuacha hata kazi ninayoifanya kule Marekani kwa ajili ya kuwa nawe .Ninakupenda sana Happy “ Mike akasema wakiwa garini kuelekea hotelini.Happy akatoa kitambaa katika mkoba wake akafuta jasho lililokuwa likimtoka.Alikuwa akitokwa jasho kutokana na mtihani mgumu aliokuwa nao juu ya kuusitisha uhusiano kati yake na Mike.


“Mungu nisaidie.Niko katika mtihani mgumu sana wa kumueleza Mike ukweli kwamba nimekutana na Patrick na nimeamua kurudiana naye.Mike ananipenda sana na sijui nitaanzaje kumueleza ukweli kwamba hatutaweza kuendelea tena na uhusiano wetu.” Happy alizama katika mawazo na ghafla akastuliwa na sauti ya Mike


“Unawaza nini mpenzi wangu? Halafu mbona jasho linakutoka sana?


“ Ni hili joto la Dar “ happy akasema


“Ni kweli hata mimi ninalisikia joto kali sana.Ningejua ningechukua gari la wazi “ akasema Mike Happy hakujibu kitu akatabasamu.


Walifika hotelini ambako tayari Mike alikwisha weka oda ya meza moja maalum kwa ajili yake na Happy.Wakaonyeshwa meza yao na kwenda kukaa na kisha wakaagiza chakula .Wakati wakisubiri chakula kiwe tayari,walikuwa wakiendela kuburudika kwa vinywaji


“Happy bado naendela kukupa hongera zangu kwa kushinda taji la mrembo wa Tanzania.Siku zote nilikuwa nikiamini kwamba una vigezo vyote ya kuwa mrembo mwenye jina kubwa lakini niliogopa kukwambia kuhusiana na masuala ya urembo kwa sababu toka nimekufahamu sijawahi kusikia hata mara moja ukigusia kwamba unapenda mambo ya urembo.” Akasema Mike


“Mike ni kweli sijawahi kukutamkia kwamba ninapenda urembo lakini toka siku nyingi nilikuwa nipenda sana mambo haya ya urembo japokuwa nilikuwa bado sijaamua kujiingiza rasmi katika fani hii.Kuna mtu aliniona akanishauri nijaribu kushiriki mashindano ya miss Tanzania na kweli nikajaribu na nikashinda.” Happy akasema huku akitabasamu.


Chakula kikaletwa wakala na baada ya kula wakaendelea na maongezi mengine.kadiri muda ulivyokuwa ukisonga na ndivyo Happy alivyozidi kuwa na wasi wasi mwingi hali iliyomfanya Mike kugundua kwamba kuna jambo ambalo haliko sawa.Akamuuliza kama kuna jambo linamsumbua.


“hapana Mike hakuna jambo linalonisumbua.Unajua kwa sasa kila nionekanapo ninakuwa nikipigwa picha na waandishi wa habari.Ndiyo maana ninakuwa sina imani kila mahala ninapokuwa” Happy akajibu


“Suala hilo lisikuumize kichwa mpenzi wangu.Kwa sasa wewe ni mrembo wa taifa na ni kioo cha jamii.Hutakiwi kujificha.Unatakiwa kutoka na kuchangamana na jamii inayokuzunguka.usiwe na wasi wasi kuhusu jambo la kupigwa picha ni suala la kawaida” Mike akasema na kisha wakaendelea na maongezi mengine.


*****************************


Saa tisa za alasiri tayari viti vyote vilivyokuwa vimeandaliwa kwa ajili ya wale wote waliokuwa wamealikwa kuhudhuria kikao hiki cha mwisho cha maandalizi ya harusi.ya Patick na Vero vilikuwa vimejaa.Kikao hiki kilichojumuisha kamati nzima ya maandalizi ya harusi hii pamoja na ndugu wengine muhimu ambao Patrick alikuwa amependekeza wawepo katika hiki kikao ambacho yeye alikiita ni muhimu sana .


Saa tisa na dakika ishirini gari la Patrick likawasili katika nyumba ya wazazi wake ambako ndiko kikao hiki cha leo kilikuwa kikifanyikia.Toka ndani ya ile gari wakashuka Patrick na Veronika na kuanza kupiga hatua kuelekea ndani.Ni wao pekee waliokuwa wakisubiriwa.katika kikao kile.


Mara tu walipoingia bustanini ambako ndiko kikao kilikuwa kifanyikia vikasikika vigere gere vingi na watu wakaanza kushangilia.Wote waliamini kwamba muda si mrefu tayari familia hizi mbili zingeungana na kuwa kitu kimoja.Akina mama walipiga vigere gere na kushangilia kwa nguvu baada ya kuwaona Patrick na Vero pamoja.


Moja kwa moja Patrick akaanza kwanza kusalimiana na baba yake ambaye hakuwa ameonana naye kwa muda mrefu kidogo na kisha akamsalimu mama yake Vero na ndugu wengine na baada ya zoezi hilo wakachukua nafasi zao.


Mwenyekiti wa kikao kile ambaye ndiye mwenyekiti wa kamati ya maandalizi akafungua kikao kwa sala fupi na kisha akawakaribisha wote katika kikao kile.Baada ya kufungua kikao kile akatoa taarifa ya kamati kuhusiana na maaandalizi yote ya harusi ile kwa ujumla.Baada ya kuisoma taarifa ile ya jumla ,mwenyekiti akawakaribisha wenyekiti wa kamati ndogo ndogo ili nao waweze kutoa ripoti zao na kisha wote kwa pamoja waweze kuangalia kama kuna sehemu yoyote yenye mapungufu ili waweze kuyafanyia kazi.Kabla hajasimama mtu yeyote kuongea Patrick akasimama na kuomba kuongea machache.


“ Wapendwa sana wazazi wetu,ndugu wote mliohudhuria kikao hiki,ndugu wanakamati wote mabibi na mabwana nilikuwa nimeomba nafasi ya kusema machache katika kikao hiki hivyo kabla mambo mengine hayajaendelea naomba niitumie nafasi hii niseme mambo machache sana kwenu nyie ndugu zangu.Kwanza nawashukuru sana kwa namna mlivyojitolea kwa kila hali kuhakikisha kwamba maandalizi ya harusi yangu yanakamilika.Nawashukuru sana kwa jitihada zenu na ushirikiano wa kila mmoja wenu.Sina kitu chochote cha kuwalipa ni mwenyezi Mungu pekee atakayewalipa.Jambo la pili ninalotaka kulisema hapa ni jambo ambalo linahusu historia yangu kwa ujumla.Ni jambo linalonihusu mimi na maisha yangu.Wengi bado hamjafahamu historiia yangu ,wapi nimetoka hadi leo hii tuko hapa pamoja mkinisaidia kuandaa harusi yangu.Sitaki kuchukua muda mrefu sana ila naomba nitumie dakika chache kuwakumbusha japo kwa muhtasari nimetoka wapi hadi nilipo hivi sasa.” Patrick akasema na kuwafanya watu wote wajiulize nini anataka kuwaambia.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/


“Historia ambayo katu haitaweza kufutika maishani na itaendelea kuwapo kichwani mwangu daima ni siku ile ambayo nilihamia katika shule ya sekondari Malangali Iringa nikitokea shule ya Mazwi sekondari Sumbawanga ambako wazazi wangu walikuwa wakiishi na kufanyakazi kule kama watumishi wa umma.Nakumbuka nikiwa katika kituo cha magari yaendeayo katika kijiji cha malangali nilikutana na msichana mmoja ambaye naye alikuwa akielekea huko.Msichana huyu ambaye kwa jina aliitwa Happy baadae alikuwa rafiki yangu mkubwa sana.”


Wazazi wa Patrick wakatazamana.Kila mmoja alikumbuka mbali sana .Vero alionyesha mstuko wa dhahiri.Patrick akaendelea


“ msichana huyu alitokea kuwa rafiki yangu mkubwa kwa sababu ni mimi pekee ambaye nilimuelewa na kumuamini.Happy alikuwa akisemekana kwamba ni muathirika wa virusi vya ukimwi na hivyo wanafunzi wote wakamtenga.Kati ya wanafuni wote ni mimi pekee ambaye nilimuamini aliyonieleza kwamba hakuwa muathirika kama alivyokuwa amezushiwa bali alikuwa na matatizo ya kiafya.Nilifanya kila nilivyoweza na nikafanikiwa kumfanya Happy asikate tamaa na hivyo akaanza kusoma tena kwa bidii na kuanza kushika nafasi za juu kimasomo.Kitendo hiki hakikuwafurahisha wanafuni wengi na hivyo kuzidisha chuki na uhasama.Sitaki kueleza kila jambo kwa sababu ni mambo mengi yalitokea lakini katika kila jambo nilisimama imara kumtetea na sikuwa tayari kuona Happy akinyanyaswa.” Patrick akanyamaza akameza mate .Kila mtu alikuwa akaishangaa ni kitu gani alichokuwa akikiongea Patrick.


“ Ilitokea siku moja kulikuwa na muziki wa disko pale shuleni.Nikiwa sina hili wala lile kumbe kuna baadhi ya wanafunzi watukutu walikuwa wameunda mpango wa kutaka kumdhalilisha Happy.Tukiwa tumekaa peke yetu tulivamiwa ,nikapigwa na kitu kizito kichwani nikapoteza fahamu baada ya hapo Happy akapelekwa katika kichaka na wahuni wale wakaanza kujiandaa kumfanyia vitendo vya udhalilishaji.kwa bahati nzuri nilipata fahamu haraka na kuwafuata wale jamaa kule kichakani nikampiga kiongozi wao na chuma kichwani akaanguka na kufariki dunia.Baada ya hapo nilikamatwa na kufungwa gerezani “ Patrick akanyamaza tena na mara watu wakaanza kusemezana wao kwa wao.Wengi hawakuwa wakifahamu historia ya Patrick.Vero alikuwa amejikunyata akiwa na mawazo mengi sana.


“Nikiwa gerezani bado Happy ambaye kwa kipindi hicho tayari nilikuwa na mahusiano naye ya kimapenzi aliendelea kuwa nami hadi pale wazazi wake walipomtaka akaendelee na masomo yake nchini marekani.Alikataa kwenda huko na kuniacha peke yangu lakini ni mimi ndiye niliye msisitiza kwamba akubali kwenda huko .Hata baada ya kwenda huko bado tuliendelea kuwasiliana kila mara .Matatizo yalianza baada ya mimi kuhamishwa gereza.Nilihamishiwa katika gereza jipya huko Songea na baada ya hapo mawasilano kati yangu na Happy yakawa magumu sana.Siku moja nilikutana na mtu ambaye baadae nilimtambua kwamba ni Veronika ambaye yeye pamoja na mimi tumewakutanisha nyote hapa leo .Nilimweleza historia yangu na nikamuomba Veronika ili aweze kunisaidia katika kufanya mawasiliano kati yangu na Happy.” Patrick akanyamaza tena.Vero alikuwa akimuangalia kwa macho makali .Watu woe walikuwa kimya wakisikiliza


“Siku moja Vero alikuja na taarifa ambayo ilinitesa kwa miaka mingi.Alinieleza kwamba mpenzi wangu Happy ameamua kuolewa huko Marekani na tayari ni mjamzito.Sitaki kukumbuka mateso na maumivu nililyoyapata siku ile.Niliumia mno .Baada ya miaka mingi kupita niliamini kwamba nikweli Happy aliamua kunisaliti.Niliamua kuendelea na maisha yangu na hivyo mimi na Vero tukawa wapenzi.Siku moja tukiwa nyumbani nilitazama katika luninga na mara nikamuona Happy nikapatwa na mstuko na kuzimia.Sikumueleza mtu yeyote yule sababu ya kuzimia kwangu.Siku ya kinyang’anyiro chakumtafuta mrembo wa Tanzania Happy akafanikiwa kunyakua taji la Miss Tanzania na nilipomkaribia alinitambua na yeye akapoteza fahamu.Baada ya hapo nilifanya juhudi mpaka nikafanikiwa kuonana naye.Nilishangaa sana aliponiuliza ni kwa nini niliamua kudanganya kwamba nimekufa hali niko mzima.Nilishangaa sana na sikuamini hadi aliponikabidhi barua aliyoandikiwa na mtu ambaye alimtaarifu kwamba nimefariki nikiwa gerezani.Niliisoma barua ile nikatoa machozi baada ya kugundua kwamba ilikuwa imeandikwa na Vero.Baua yenyewe hii hapa” Patrick akasema huku akimkabidhi baba yake ile barua ili aisome. Watu wote walibaki vinywa wazi.Vero alikuwa ameinama akilia kwa kwikwi.


“ Ndugu zangu nimewaeleza haya yote ili mtambue ni kwa jinsi gani Vero alivyonifanyia ukatili mkubwa.Ni wazazi wangu pekee ambao wanafahamu ni mateso gani niliyoyapata wakati ule.Nimeumia sana baada ya kuufahamu uongo huu mkubwa alioutunga Vero na kusababisha mimi na Happy tukasambaratika.Mbele yenu wazazi na ndugu wengine wote naomba mnisamehe sana kwa haya nitakayoyasema lakini huu ni uamuzi wangu kutoka moyoni….” Patick akanyamaza kidogo na kisha akasema


“Nimeamua kuachana na Vero na kusitisha kila kitu kuhusiana na ndoa yetu. kuan…………….” Patrick hakumaliza kauli yake mara akina mama watatu akiwemo mama yake na mama yake Vero wakaanguka na kuzirai.Kizaa zaa kikaibuka.Baba yake jasho lilianza kumtiririka ,shinikizo la damu lilimuanza.Kila mtu alihisi kuishiwa nguvu.




Eneo ambalo saa chache zilizopita watu walikuwa wakifurahi na kupongezana , akina mama wakipiga vigere gere kwa furaha kubwa waliyokuwa nayo wakiamini kwamba hakuna kipingamizi chochote cha kuwazuia kuziunganisha familia zao kupitia kwa watoto wao wawili Patrick na Veronika , kwa sasa liligeuka sehemu yenye vilio na mstuko mkubwa sana.Kila mtu aliyekuwepo eneo lile alikuwa amestushwa mno na kilichotokea.Hakuna aliyekuwa ametegemea kama Patrick angeweza kuongea kitu kama kile alichokiongea.Hakuna aliyeota kama ingetokea siku Patrick angeweza kusitisha mipango ya ndoa yake na mchumba wake Veronika.Kila mtu aliona hii ni kama ndoto na si kitu cha kweli..


Haraka haraka wale wote waliozirai kutokana na mstuko walioupata wakaanza kusaidiwa kwa kupatiwa huduma ya kwanza ili waweze kurejewa na fahamu zao .Mahala hapa palionekana kama vile kumetokea msiba.Watu waliokuwa wakiishi jirani na eneo lile wakaanza kujaa katika nyumba hii wakiamnini kuna tatizo limetokea baada ya kusikia vilio vya akina mama.Baba yake Patrick alikuwa katika hali mbaya kutokana na shinikizo la damu .Hali ilikuwa ya kuogopesha sana na kwa haraka Patrick akalisogeza gari na kisha baba yake akapakiwa na kumuomba mtu mwingine aendeshe gari kwa kuwa hakuwa na nguvu za kuweza kulimudu gari kwa wakati huo .Baba yake akakimbizwa hospitali.Patrick jasho lilikuwa likimtoka.Alionekana kama ni mtu aliyechanganyikiwa kutokana na alichokishuhudia kikitokea.


“Ee Mungu naomba unisaidie katika suala hili ambalo limeanza kuwa gumu sana” akaomba kimya kimya wakati wakiwa garini wakimkimbiza baba yake hospitali.Patrick hakuwa akiongea kitu alikuwa ameinamisha kichwa chini akitafakari.


“Sikutegemea kama mambo yangeweza kufika hapa yalipofika .Nilitegemea kungekuwa na ugumu na upinzani mkubwa katika jambo hili lakini sikuwa nimetegemea kama jambo la namna hii lingetokea.Imekuwa ni zaidi ya msiba.Hakuna aliyekuwa ametegemea kama ningeweza kuachana na Vero na hasa katika kipindi hiki cha mwisho cha maandalizi ya harusi yetu.Nimewaumiza watu wengi sana .Kila mtu atakayesikia kuhusu suala hili atanilaani na kuniona mkatili mkubwa.Lakini ni kwa nini basi hakuna hata mtu mmoja ambaye yuko tayari kunisikiliza na kunielewa? Kwa nini hawataki kuupa uzito upande wangu pia? Nimejaribu kuwaelezea kwa ufasaha mkubwa sana ili wanielewe lakini hakuna hata mmoja anayeonekana kunielewa.Hakuna hata mmoja ambaye ameguswa na machungu niliyoyapata kwa uongo huu mkubwa wa Vero“ akawaza Patrick halafu akatoa kitambaa na kujifuta jasho lililokuwa likimtiririka kama maji..


“Litakalo tokea na litokee .Sintaweza kurudi nyuma kamwe.Nilimuahidi Happy kufanya kila niwezalo kwa ajili ya kuwa naye tena.Siwezi kubadili maamuzi yangu.Hata kama nitakabiliana na magumu ya kiasi gani lakini sintarudi nyuma katika azma yangu ya kutaka kuachana na Vero.Kwa sababu ya Happy nitafanya kila litakalowezekana hata kama nikilazimika kuutoa uhai wangu.” Patrick bado alizidi kusongwa na mawazo mengi.


* * * *


“Kitu gani cha kwanza umepanga kukifanya ukiwa kama mrembo wa Tanzania? Mike akamuuliza Happy huku wakiendelea kupata vinywaji.Happy akamtazama Mike kisha akatabasamu na kusema


“Kama mrembo wa Tanzania nitakuwa nikipangiwa majukumu ya kufanya na ofisi maalum inayohusika na kuratibu mambo yote ya Miss Tanzania.Lakini pamoja na kufanya kazi hizo nitakazokuwa nikipangiwa ambazo ni kazi za kujitolea katika jamii ninafikiria kuanzisha umoja au taasisi itakayowawezesha watu mbali mbali kuweza kujitolea katika jamii.”


Mike akatabasamu na kuuliza


“Sijakuelewa vizuri mpenzi wangu kuhusiana na taasisi hiyo unayotaka kuianzisha”


Happy akatabasamu kama kawaida yake,tabasamu ambalo linamfanya Mike naye atabasamu.


“Umoja huu ninaotaka kuuanzisha lengo lake ni kujenga ule moyo wa kujitolea miongoni mwa wanajamii.Kila mtu ataruhusiwa kujiunga na umoja huu na kila mwisho wa wiki tutakuwa tukitembea katika sehemu mbali mbali kama vile mahospitali,magerezani ,mashuleni,katika vituo vya kulelelea watoto yatima na wanaoishi katika mazingira magumu na hata kuwatembelea wale watu walioko majumbani wasiojiweza na kisha kila mtu akatoa msaada wake.Sitaki kujikita katika sehemu moja tu kama ilivyozoelekea katika jamii yetu kwamba kila mrembo wa Tanzania malengo na mtazamo wake ni kusaidia mayatima.Mtazamo wangu mimi utakuwa tofauti kidogo na wengine kwa sababu mimi ninataka kuisaidia jamii masikini na yenye uhitaji kwa ujumla wake bila kubagua.Katika suala hili sintahitaji mfadhili bali nitaitumia kofia ya Miss Tanzania kupita kila kona ya nchi hii kutoa elimu na kuwafundisha watu maana ya kujitolea .Kila mtu atakayeguswa atakuwa akijitolea kile kitu alichokuwa nacho kwa ajili ya watu wenye uhitaji.Kama atatokea mtu mwenye ufadhili nitashukuru na tutauelekeza ufadhili wake katika kada maalum yenye uhitaji mkubwa.” Happy akasema na kumtazama Mike ambaye alikuwa kimya akisikiliza.


Mike akatabasamu baada ya kuisikia mipango ile ya mchumba wake Happy.


“Happy siku zote ninamshukuru sana Mungu kwa kunipa mchumba mwenye akili nyingi na mwenye roho ya huruma sana.Nina kila sababu ya kujivuna kuwa nawe na siku zote za maisha yangu nitahakikisha kwamba unakuwa ni mwanamke mwenye furaha kubwa.Ninakuahidi msaada wangu mkubwa katika jambo hili unalolifikiria.Siku zote nitakuwa nyuma yako ili kukupa ushirikiano wangu.Nikiwa Marekani nitakuwa nikifanya kazi ya kuwakusanya watu wenye asili ya afrika na kuwaomba tuuchangie mfuko huu kwa ajili ya maendeleo ya jamii zetu huku afrika.Natumai baada ya muda mfupi mfuko huu utakuwa mkubwa na kuwasaidia watu wengi sana.” Mike akasema na kumfanya Happy atabasamu halafu akainama chini.


“Kila nikimuangalia Mike nashindwa nitaanzaje kumueleza kwamba uhusiano wetu umefikia mwisho.Siwezi kuishi bila Patrick lakini kumweleza Mike ukweli ninashindwa.Nitafanya nini sasa? Happy akawaza.Mike akagundua kwamba mchumba wake Happy alikuwa katika mawazo mengi.


“Happy malaika wangu una matatizo gani? Naona kama bado hauko sawa sawa.Kuna jambo gani linalokusumbua akili yako? Ninakufahamu vizuri sana na ninafahamu kuna kitu kinakuumiza kichwa chako.tafadhali naomba unieleze nini kinakusumbua akili yako.Niko hapa kwa ajili yako Happy” Mike akamweleza HappyCHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/


“Mike ni kweli nina tatizo kubwa na sijui hata nianzie wapi kukueleza” Happy akasema huku moyo wake ukimuenda mbio sana


Mike akalegeza tai yake na kumsogelea karibu zaidi Happy ili aweze kusikia ni tatizo gani hilo alilonalo Happy


“Happy niambie una tatizo gani? Mimi niko hapa kwa ajili yako.Nitakwenda hadi mwisho wa dunia kwa ajili ya kuhakikisha kwamba unakuwa na uso wenye tabasamu daima.Niambie tafadhali una tatizo gani? Mike akasema huku akiupeleka mkono wake katika bega la Happy


Happy akakosa la kusema.Kila alipojitahidi kufumbua midomo yake iligoma kufunguka na kubaki ikicheza.Alikuwa akiogopa.Mara simu yake ikalia.Kwa haraka akafungua mkoba wake akaichukua na kuangalia mpigaji ambaye jina lake lilisomeka kama “My everything”.Hili ni jina alilotaka lisomeke katika namba ya Patrick.Moyo ukamuenda mbio.


“Excuse me “ akasema Happy huku akiinuka na kusogea pembeni akabonyeza kitufe cha kupokelea simu.


“Hallo Patrick “ akasema Happy kwa sauti ndogo


“Happy uko wapi sasa hivi? Patrick akauliza na kumfanya Happy astuke kidogo kutokana na sauti ya Patrick kuwa na mabadiliko


“Patrick mbona sauti yako haiko kawaida? Whats wrong? Happy akauliza kwa sauti na kumfanya Mike astuke baada ya kusikia Happy akitamka jina la Patrick.


“Happy matatizo makubwa yametokea.” Patrick akasema


“Matatizo gani Patrick ? Happy akauliza


“Happy nashindwa hata nianzie wapi kukueleza kwa sababu hapa nilipo nahisi kuchanganyikiwa kutokana na mambo yaliyojitokeza. Kwa sasa niko hapa hospitali kuu ya magonjwa ya moyo kama unaweza ukapata nafasi njoo ili niweze kukueleza kwa undani kilichotokea”


“Patrick umenistua sana nieleze ni kitu gani kimetokea? Happy akauliza kwa wasi wasi


“ Baba amepatwa na shinikizo la damu na tumemleta hapa hospitali hali yake si nzuri hata kidogo”


“Ok Patrick nakuja sasa hivi” akasema Happy huku sura yake ikiwa imebadilika na alionekana kuchanganyikiwa ghafla.


“Happy nini kimetokea mbona umebadilika ghafla? “ Mike akauliza baada ya kugundua mabadiliko katika sura ya Happy


“Mike…it.s….uuhhmm...Its nothing “ Happy akasema kwa kubabaika.


“Niambie ukweli Happy nini kimetokea? Mbona umestuka na kubadilika ghafla? Mike akauliza akiwa amemshika Happy mkono


“Mike its nothing.take me back home” Happy akasema huku akiutoa mkono wake toka katika mkono wa Mike


“Happy don’t say its nothing wakati nafahamu kabisa kwamba kuna kitu umeambiwa na mtu aliyekupigia simu kilichokustua na kukufanya uwe katika hali hii.Halafu nimesikia ukimtaja Patrick..Ni nani huyo Patrick ? Mike akauliza na kumfanya Happy amtazame kwa mshangao uliochanganyika na uoga ndani yake.


“Niambie happy ,Patrick ni nani ? kwa sababu amekufanya ubadilike ghafla “Mike akauliza hali uso wake ukionyesha wasi wasi mkubwa.


“Mike please take me back home” Happy akasema kwa sauti kali.


Mike akamtazama Happy kwa makini halafu akamsogelea akamshika mabega yake kwa mikono yake na kusema


“happy wewe ni mchumba wangu na unafahamu kwamba ninakupenda na siwezi kuishi bila kuwa na wewe.tafadhali naomba uniangalie machoni na uniambie huyo Patrick ni nani? Mike akauliza


Happy akashindwa kumuangalia Mike usoni akainama chini huku machozi yakimdondoka.


“take me home Mike” happy akasisitiza


“happy hapa hatutaondoka mpaka unieleze huyo Patrick uliyekuwa ukiongea naye simuni ni nani? Na amekupa habari gani ambayo imekufanya ustuke namna hii? Mike akauliza na uso wake ulionesha kwamba hakuwa akifanya masihara.


“Mike please..not now…kama hutaki kunirudisha nyumbani I’ll take a taxi” Happy akasema akiwa ameanza kupiga hatua kuondoka.Mike akamkimbilia.


“happy samahani.Sikuwa na nia mbaya kukuuliza vile.Yote hii ni kwa sababu ninakupenda na sipendi kukuona ukiwa katika hali hiyo na ndiyo maana nilihitaji kufahamu kilichokusibu .Naomba unisamehe mpenzi wangu” akasema Mike kwa unyenyekevu.Toka wameanza mapenzi yao haijawahi kutokea hata siku moja wakawa katika hali hii. Mike akamfungulia mlango Happy akaingia garini na kisha wakaondoka kurudi nyumbani.


“Kuna jambo ambalo linamsumbua Happy.Nimeanza kuwa na wasi wasi mwingi kuhusiana na mwenendo wake.Naona kuna mabadiliko makubwa sana.Happy niliyemzoea hakuwa namna hii.Amekuwa ni mwingi wa mawazo na si mchangamfu kama nilivyomzoea.Kuna kitu gani kinachoendelea? Halafu nilisikia akiongea na mtu akamtaja jina la Patrick.Ni nani huyo mtu ? Nakumbuka aliwahi kunisimulia kwamba aliwahi kuwa na mpenzi wake aliyeitwa Patrick ambaye alifariki dunia na ndiyo maana akaamua kunipa mimi nafasi ndani ya moyo wake.Huyu Patrick mwingine ambaye kwa maongezi ya dakika chache ameweza kuibadilisha hali ya Happy ni nani? Kitu gani kimetokea kiasi cha kumfanya Happy astuke namna ile na ghafla tu anaamua kurejea nyumbani? Lazima nifahamu kitu gani kinaendelea.Lazima nifahamu jambo gani lialomsumbua Happy.” Mike alikuwa katika mawazo mengi sana


Baada ya kufika nyumbani kwao Happy akashuka ndani ya gari la Mike na kwa haraka akaingia chumbani kwake,akachukua ufunguo wa gari lake na kutoka kwa kasi.


Mike alikuwa amesimama na Margreth wakijadili jambo wakati Happy alipotoka ndani kwa kasi na kuingia katika gari lake.Margreth akamsogelea na kugonga kioo cha gari kwa mkono wake .Taratibu Happy akashusha kioo na kumtazama


“happy nini kimetokea? Margreth akauliza


“Maggy tutaongea baadae.I need to see Patrick now.Kuna tatizo kubwa limetokea.” Akasema happy huku akiwasha gari na kumfanya mdogo wake azidi kushangaa.


“Happy nini kimetokea? Magreth akajaribu kuuliza lakini tayari Happy alikwisha liwasha gari lake na kuondoka kwa kasi.


“Mike nini kimetokea? Mbona Happy amebadilika ghafla hivi? Margreth akamuuliza Mike ambaye bado alikuwa amesimama asiamini kilichotokea


“hata mimi nilitaka kukuuliza swali kama hilo kwa sababu nimegundua kuna mabadiliko makubwa sana kwa Happy.Si Happy yule niliyemzoea.Kitu gani kinamsumbua? “ Mike akauliza


“Hakuna jambo lolote amekueleza huko mlikokuwa? Margreth akauliza


“hapana Margreth.Happy hajanieleza jambo lolote lile.Kwani kuna nini? Mike akauliza.Margreth akainama chini.


“Ninachokikumbuka ni kwamba kuna wakati nilimuona amezama katika mawazo mengi ikanilazimu kumuuliza ni kitu gani kinachomsumbua .Akaniambia kwamba kuna jambo ambalo limekuwa likimuumiza kichwa na alipotaka kunieleza simu yake ikaita na sielewi aliambiwa kitu gani na huyo aliyempigia simu kwa sababu alibadilika ghafla sana na akaniomba nimrudishe nyumbani.” Mike akasema na kumtazama Margreth.


“Margreth ,kuna jambo ambalo hata mimi limekuwa likiniumiza kichwa sana.” Mike aksema


“Jambo gani hilo Mike? Margreth akauliza


“Happy alipopigiwa simu alisogea pembeni na kwenda kuongelea huko kitu ambacho haikuwa kawaida yake.Wakati akiongea nilisikia akilitaja jina la Patrick,nikastuka sana.Unaweza ukamfahamu huyo Patrick? Mike akauliza na kumfanya Margreth astuke kidogo halafu akatabasamu na kusema .


“…unajua Mike kwa sasa Happy ni mrembo wa Tanzania kwa hiyo atakuwa akipigiwa simu na watu mbali mbali.Usihofu kuhusu huyo Patrick.Huyo ndiye mbunifu wake wa mavazi na ndiye aliyemsaidia sana happy hadi akashinda taji la Miss Tanzania.” Magreth akadanganya huku akitabasamu na kumfanya Mike naye atabasamu.


“Nashukuru sana Margreth kwa kuniondolea huu mzigo niliokuwa nao kichwani kwangu.Tayari nilikwisha anza kuwa na wasi wasi mwingi labda Happy amekutana na Patrick aliyekwisha fariki kwa sababu nakumbuka jinsi Happy alivyokuwa akimpenda.” Mike akasema


“Usiwe na wasi wasi Mike.Jisikie amani.halafu kitu kingine unachotakiwa kukifahamu kwa sasa ni kwamba happy anahitaji kuvumiliwa kwa sababu hakuzoea kuishi maisha haya ya kufuatiliwa kila siku mara na waandishi wa habari n.k.Anahitaji muda ili kuweza kuiweka akili yake sawa sawa kwahiyo kuna mambo ambayo anaweza akayafanya ambayo yanaweza yakakuudhi lakini naomba usichukie na uendelee kumvumilia” Margreth akamweleza Mike

Tags

Post a Comment

0 Comments
Post a Comment (0)

Made with Love by

Pixy Newspaper 11 Template is Designed Theme for Giving Enhanced look Various Features are availabl…
To Top