Posts

Showing posts from August, 2024

RIWAYA: MUAFAKA - 7

  MTUNZI: AMRI BAWJI SEHEMU YA SABA “Ujuzi wangu kama upi Onespot?!” Aliuliza. “Wewe u mpiga picha mzoefu na mwenye ujuzi na umekwisha fanya kazi hiyo na wanamitindo wengi wenye uzoefu, kwa hiyo utamuonesha Vicky staili zitakikanazo. Picha zake tutazihitaji kwa ajili ya matangazo ya biashara vile vile. Jambo hili ni muhimu kwa faida ya kampuni.” “Una uhakika kuwa sio kwa faida yako binafsi bosi Onespot?!” Edo aliuliza kwa dhihaka huku kimoyomoyo akiwa ni kweli analouliza. Onespot alicheka kwa nguvu huku akitikisa kichwa kukataa, “Hapana… hapana Edo… Oh no! sio kwa faida yangu binafsi… You must believe me Mr. Oloi.” Edo alielezwa nguo hiyo ambayo ataivaa Vicky ni lini italetwa na mara ifikapo zoezi lianze. * * * Wafanyakazi kwa ujumla, wake kwa waume walikuwa wameshughulika na mazoezi ya onesho la mavazi, ndani ya vyumba mbalimbali vya jengo la ofisi za kampuni ya ADFC. Wanamitindo, wavulana na wasichana, wabunifu wa mavazi, wapiga picha za kawaida na za video, waongozaji filamu za ...

.RIWAYA: MUAFAKA - 6

Image
MTUNZI: AMRI BAWJI SEHEMU YA SITA “Lulu, je upo tayari kuolewa na mimi?!” Lulu anampenda sana Edo, lakini katika akili zake bado ana wasiwasi na chaguo lake. Alifikiri ‘Je Edo ni mwanamme alie sawa kabisa kuwa mume wangu?! Je ataonekanaje mbele ya wazazi wangu?! Je sifa zake zinashinda za yule mchumba niliechaguliwa kule nyumbani?!’ Ilimradi maswali mengi yaliyojaa ndani ya kichwa chake, yalimfanya Lulu asiwe na jibu la haraka kwa swali aliloulizwa na Edo, ingawa, alifahamu fika kuwa kwa sasa yu mapenzini na Edo. Aliamua aombe muda kwanza wa kufikiria hivyo, akatamka, “Edo, tafadhali naomba unipe muda kidogo kwa swali lako hilo. Ninaomba usinielewe vibaya, kwani ni kweli ninakupenda, bali suala la ndoa, naomba muda kidogo wa kufikiria.” “Nami pia nisingependa jibu la haraka haraka lisilokuwa na uhakika. Ninachotaka ufahamu ni kuwa nimekwisha kukuuliza swali hilo. Sasa nami nakuomba uchukue muda wa kunipa jawabu litokalo moyoni mwako.” * * * lngawa Lulu na Edo wamezoeana, wanafanya kazi...

RIWAYA: MUAFAKA - 5

Image
MTUNZI: Amri Bawji SEHEMU YA TANO “Tutaonana Edo, hakuna msichana, anaeweza kusema ‘Hapana’ kama mimi Onespot ninamtaka.” Edo alimuangalia kwa jicho la dharau na kutabasamu kidogo. Onespot aliendelea kusema, “Kwa asili mimi Onespot nimezaliwa ‘mshindi’ kwahiyo siwezi kushindwa na vita ndogo kama hii ya kumpata msichana kama Lulu.” “Fahamu mkataa kushindwa si mshindani. Ni kweli Onespot umezaliwa ‘mshindi’ kwa asili, lakini kwa hakika si ‘mpiganaji’. Wewe ni mshindi katika vita vilivyokwisha piganwa na wenzio!” “Hivi vita vya kumgombania Lulu, nitapigana mwenyewe, na ndio maana sitaki hata kukufukuza kazi ili nikutowe ‘knockout’ bwana Edo.” Kama kawaida ya Onespot, pamoja na udhaifu wote aliokuwa nao, lakini alikuwa ni mtu mwenye kujiamini kupita kiasi, “Kunifukuza kazi huwezi bwana Onespot kutokana na mikataba yetu, bali ninaweza niache kazi mwenyewe nikitaka kufanya hivyo. Lakini na mimi sitaki kuwacha kazi sababu ninataka nione ni jinsi gani unaweza kumgombania Lulu dhidi yangu mimi...

RIWAYA: MUAFAKA - 4

Image
RIWAYA: MUAFAKA MTUNZI: Amri BAWJI SEHEMU YA NNE “Sawa iwapo unadhani hivyo. Lakini watu wanasema ‘vichwa viwili ni bora kuliko kimoja.’’ “Kama ni hivyo basi niwache nifikirie peke yangu, nitakapojiona ninahitaji msaada wa mtu mwengine nitakwambia wewe Edo unisaidie.” “Tafadhali usiwache kufanya hivyo Lulu. Pale unapoona ninaweza kusaidia, basi wakati wowote, saa yeyote, pahali popote nieleze nitakuwa tayari kusaidia.’’ “Natanguliza shukrani, Ahsante Edo.’’ Lulu alianza kupendezewa na mazungumzo kati yake na Edo. Yalikuwa yakimfarijii na kumliwaza. Mazungumzo kati yao yalikuwa rahisi yasiyokuwa na majivuno wala kujitapa. Hali kama hiyo iliendelea kwa muda kiasi kumfanya Lulu aanze kuvutika taratibu kwa Edo. * * * Hisia za Vicky juu ya Onespot zilifika kiwango ambacho alishindwa kujikaza kwa kukaa kimya na kuonesha ishara kuwa anampenda kijana huyo. Aliamua asema kwa namna moja au nyingine huku damu ikimwenda mbio mwilini mwake Vicky alitamka kumuuliza Onespot aliekuwa amekaa juu ya kit...